STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, September 3, 2013

Hatimaye Arsenal 'yavunja' benki

* Ozil asaini miaka mitano Arsenal

http://www.independent.co.uk/incoming/article8794558.ece/ALTERNATES/w460/mesut-ozil-getty.jpg
Kifaa kipya kilichotua Arsenal, hatimaye
LONDON, Uingereza
MESUT Ozil amekamilisha uhamisho uliogharimu paundi milioni 42 wa kutua Arsenal baada ya kusaini mkataba wa miaka mitano.
Arsenal wamevunja rekodi yao ya uhamisho katika kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani, ambaye alifanyiwa vipimo kwa mara ya pili jana baada ya kuafiki malipo binafsi na klabu hiyo.
Ozil amesaini mkataba utakaomfanya alipwe paundi mshahara wa 130,000 kwa wiki utakaomweka Emirates hadi mwaka 2018 baada ya Real Madrid kumruhusu kuondoka.
Atakuwa mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa zaidi Arsenal, wakati kocha Arsene Wenger akitoa paundi zaidi ya 20,000 katika kusajili mchezaji mmoja kwa mara ya kwanza katika historia ya klabu hiyo.
Zoezi la usajili barani Ulaya ulikamilika usiku wa kuamkia leo ambapo wachezaji kadhaa wamehama na kutua katika klabu mbalimbali.
Baadhi ya wachezaji waliohama ni Marouane Fellaini aliyetua Manchester United kumfuata kocha wake wa zamani, David Moyes kutoka Everton kwa kitita cha pauni Milioni 27, Victor Moses aliyetoka Chelsea kwenda Liverpool kwa mkopo, Romelu Lukaku aliyetoka Chelsea kwenda West Brom kwa mkopo.
Orodha kamili ya nani katoka wapi na kaenda wapi itawajia baadaye kidogo hapa hapa MICHARAZO.

No comments:

Post a Comment