STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 14, 2013

Arsenal yang'oka Ulaya, Malaga yaisulubu Porto

Mfungaji wa bao la pili la Arsenal, Laurent Koscielny (kulia) akiwa haamini kama wametoka michuano ya UIaya
 LICHA ya kupata ushindi uliotarajiwa wa mabao 2-0 ugenini nchini Ujerumani, Arsenal ya Uingereza imejikuta ikishindwa kutinga robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa jana.
Arsenal ilikuwa nchini humo kukabiliana na wenyeji wao Bayern Munich ikiwa nyuma ya mabao 3-1 iliyonyukwa katika pambano lao la awali lililochezwa mjini Londoni mwishoni mwa mwezi uliopita.
Ushindi huo uliotokana na mabao ya Olivier Giroud aliyefunga dakika ya tatu tu ya kuanza kwa mchezo huo na lile la kipindi cha pili lililotumbukizwa wavuni na Laurent Kocsielny, ulifanya matokeo ya mwisho kuwa sare ya mabao 3-3, lakini vijana hao wa Arsene Wenger kung'oka kwa faida ya bao ya ugenini.
Tofauti na mechi yao ya London, Arsenal jana walionyesha uhai na kuwafunika wenyeji wao na kuwashutukiza kwa bao hilo la mapema la Giroud lililodumu hadi wakati wa mapumziko.
Arsenal ilisubiri hadi dakika nne kabla ya kumalizika kwa pambano hilo kuongeza bao la pili kupitia kwa Laurent Koscielny aliyefunga kwa kichwa ambalo hata hivyo halikusaidia kusonga mbele ili kukaribia ndoto zao za kumaliza ukame wa mataji klabuni hapo.
Michuano hiyo ndiyo iliyokuwa tumaini pekee la Arsenal kumaliza ukame huo wa mataji kwani ilishatolewa kwenye michuano ya Kombe la Ligi, Kombe la FA na ndoto za kutwaa ubingwa wa Ligi ya England ni finyu kutokana na ukweli imeachwa mbali kipointi na vinara wa ligi hiyo, Manchester United.
Katiika mechi nyingine ya usiku wa jana katika michuano hiyo ya Ulaya, Malaga ya Hispania ikiwa nyumbani ililipa kisasi cha kunyukwa na Porto ya Ureno bao 1-0 kwa kuilaza wageni wao hao mabao 2-0 na kutinga robo fainali.
Malaga ilipata mabao yake kila kipindi kupitia kwa nyota wake, Isco aliyefunga la kwanza dakika ya 43 na Roque Santa Cruz kuonyesha la pili katika dakika ya 77 na kuifanya timu hiyo sasa kuungana na timu za Barcelona na Real Madrid kutoka Hispania, Borussia Dotmund na Bayern Munich za Ujerumani, PSG ya Ufaransa na Galatasaray ya Uturuki kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo.

Wednesday, March 13, 2013

Silaha 23 za Kim Poulsen kwa Morocco hizi hapa

Kipa wa Mtibwa Husseni Sharrif 'Casillas' akiwajibika uwanjani




Na Boniface Wambura

KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametaja wachezaji 23 watakaoingia kambini Jumamosi  jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mechi ya mashindano dhidi ya Morocco, akimjumuisha kipa wa Mtibwa Hussei Sharrif 'Casillas'.

Mechi hiyo ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Brazil itachezwa Machi 24 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Kocha Kim, wachezaji wa Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager wanatakiwa kuripoti kambini katika hoteli ya Tansoma, Machi 17 mwaka huu.

Wachezaji walioitwa ni makipa Juma Kaseja kutoka Simba ambaye pia ndiye nahodha wa Stars, Aishi Manula (Azam), Hussein Shariff (Mtibwa Sugar) na Mwadini Ally (Azam). Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Issa Rashid (Mtibwa Sugar), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Nassoro Masoud Cholo (Simba) na Shomari Kapombe (Simba).

Viungo ni Salum Abubakar (Azam), Athuman Idd (Yanga), Amri Kiemba (Simba), Khamis Mcha (Azam), Frank Domayo (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Simba) na Shabani Nditi (Mtibwa Sugar).

Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Mrisho Ngasa (Simba), Simon Msuva (Yanga), na Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC).

Mbali ya Kim, benchi la ufundi la Taifa Stars linaundwa na Sylvester Marsh (Kocha Msaidizi), Juma Pondamali (Kocha wa makipa), Leopold Tasso (Meneja), Dk. Mwanandi Mwankemwa (Daktari wa timu), Frank Mhonda (Mtaalamu wa tibamaungo) na Alfred Chimela (Mtunza vifaa).

SEMINA ELEKEZI COPA COCA COLA KUFANYIKA MACHI 19


Na Boniface Wambura

SEMINA elekezi kwa ajili ya michuano ya Copa Coca-Cola 2013 itafanyika Machi 19 mwaka huu jijini Dar es Salaam. Washiriki wa semina hiyo wanatakiwa kuripoti Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) siku moja kabla (Machi 18 mwaka huu).

Washiriki hao ni makatibu wa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa ya Tanzania Bara na Zanzibar. Pia waratibu wa mikoa wa mashindano ya Umoja wa Michezo wa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA).

Barua za mwaliko kwa ajili ya semina hiyo tayari zimetumwa kwa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa.

FIFA yaionya Tanzania kuingiza siasa TFF

Katibu Mkuu wa FIFA, Jerome Velcke
BERNE, (Reuters)
TANZANIA has been warned by soccer's governing body FIFA over alleged government interference in the country's football federation.

"We can confirm that FIFA secretary general Jerome Valcke has sent a letter to the president of the Tanzanian Football Federation, Leodegar Tenga, concerning alleged governmental interference in the internal affairs of the TFF," said FIFA in a statement sent to Reuters.

"FIFA is in contact with the TFF president who is optimistic that the matter can be sorted out between TFF, FIFA and the Tanzanian authorities.

"Furthermore, we can confirm that FIFA is also planning to send a mission to assess the situation with regard to the electoral process as soon as the current matter of alleged interference has been clarified."

Tanzanian media said that the government has declared the TFF's new statutes illegal and told it to use the old ones for upcoming elections.

FIFA statutes state that its member associations must remain independent of their respective national governments and routinely suspends those who break the rules.

Suspension for Tanzania would mean that they would be excluded from the World Cup qualifiers and their clubs would be kicked out of African competitions.

Tanzania, who have never qualified for the World Cup, are second in African qualifying Group C with three points from two games, one behind leaders Ivory Coast.

BARCELONA YAFANYA MAANGAMIZI ULAYA

 

'Mchawi Mweupe' Lionel Messi akishangilia moja ya mabao yake mawili usiku wa jana.

NI Maangamizi! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya vinara wa Ligi Kuu ya Hispania, Barcelona usiku wa kuamkia leo kuifumua bila huruma AC Milan ya Italia na kutinga robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya bila kutarajiwa.
Mabao mawili ya 'Mchawi Mweupe' Lionel Messi na mengi ya David Villa na Jordi Alba, imeifanya Barca kutinga hatua hiyo kwa kuitupa nje AC Milan kwa jumla ya mabao 4-2 baada ya mechi ya awali kuchezea kipigo cha mabao 2-0 ugenini.
Messi aliendelea kuimarisha rekodi yake ya mabao katika michuano ya msimu huu kwa kufunga bao la kwanza dakika ya tano akimalizia kazi nzuri ya Xavi, kabla ya kuiongeza jingine dakika tano kabla ya mapumziko kwa shuti kali kwa pasi murua ya Iniesta na kuifanya Barca iende mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 2-0.
Kipindi cha pili, AC Milan wakiingia wakitafuta mbinu za kuweza kudhibiti mashambulizi ya wenyeji wao, lakini wakajikuta wakitungulia bao la tatu kupitia kwa Villa aliyemegewa pande tamu na Xavi na kufunga dakika ya 55.
Bao lililoikata maini AC Milan ambayo kupitia nyota wake Robinho, Kevin Prince Boateng, Sule Muntari walijaribu kufurukuta bila mafanikio, lilitumbukizwa kimiani na Alba dakika za nyongeza pambano hilo na kuifanya Barca kuweka historia kwa timu iliyonyukwa mabao 2-0 katika mechi ya kwanza kusonga mbele katika michuano hiyo ya Ulaya.
Katika mechi nyingine ya michuano hiyo iliyochezwa usiku wa jana, wenyeji Schalke 04 walijikuta wakinyukwa nyumbani na wageni wao Galatasaray kwa mabao 3-2 na kung'oka kwenye michuano hiyo.

Kikosi cha Galatasaray kilichokuwa na Didier Drogba kilishtukizwa kwa kufungwa bao la dakika ya 18 kupitia Roman Neustadter kabla ya Hamit Altintop kusawazisha katika dakika ya 37 na Burak Yilmaz kuiongezea wageni bao la pili katika dakika ya 42.
Michael Bastos aliipatia Schalke bao la kusawazisha katika kipindi cha pili kwenye dakika ya 63 na wengi kuamini mechi hiyo ingeisha kwa sare hivyo ambapo jumla ya matokeo yalikuwa yakisomeka 3-3 kutokana na sare ya baoa 1-1 waliyopata timu hizo katika mechi ya ya kwanza, Galatasaray walipata bao la tatu.
Bao hilo lililwekwa kiminia kwenye dakika za nyongeza za pambano hilo kupitia kwa Umut Bulut na kuivusha timu yake hadi robo fainali ya michuano hiyo mkubwa kwa ngazi za klabu barani Ulaya.

Tuesday, March 12, 2013

Kim Poulsen kuanika silaha za kuivaa Morocco

Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen
Na Boniface Wambura
KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Kim Poulsen kesho anatarajia kuanika kikosi cha timu yake kitakachovaana na Morroco katika pambano la kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2014.
Kim atazungumza na wanahabari kesho majira ya saa 5 asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itacheza na Morocco kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Machi 24 mwaka huu katika mechi ya kundi C ikiwa sambamba na Ivory Coast na Gambia.
Mpaka sasa Stars inashika nafasi ya pili katika msimamo wa kundi lake ikiwa na pointi 3 moja nyuma ya ilizonazo Ivory Coast wanaoongoza msimamo na ambao wikiendi hii nao watashuka dimbani kucheza na Gambia.
Stars inahitaji ushindi katika mechi hiyo ili kuweka hai matumaini yta kufuzu fainali hizo za Kombe la Dunia ambazo zitafanyika mwakani nchini Brazili.
Msimamo wa kundi walilo Stars ni kama ifuatavyo:

                                   P  W  D  L   F  A  GD PTS
1. Ivory Coast             2   1   1   0   4   2    2   4
2. Tanzania                  2   1   0   1   2   3   -1   3
3. Morocco                 2   0   2   0   3   3    0   2
4. Gambia                    2   0   1   1   2   3  -1   1

Pambano la Simba, Coastal laingiza Mil 37



Na Boniface Wambura
PAMBANO la Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya mabingwa watetezi, Simba dhidi ya Coastal Union iliyochezwa juzi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 36,820,000 kutoka na watazamaji 6,284.

Viingilio katika mechi hiyo namba 138 iliyomalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 8,265,752.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 5,616,610.17.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 4,202,924.97, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 2,521,754.98, Kamati ya Ligi sh. 2,521,754.98, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 1,260,877.49 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 980,682.49.

Uchaguzi TAFCA kufanyika Morogoro



Na Boniface Wambura

UCHAGUZI Mkuu wa viongozi wa Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania (TAFCA) utafanyika Jumamosi (Machi 16 mwaka huu) mjini Dodoma ambapo wajumbe wanatakiwa kuripoti siku moja kabla ya uchaguzi.

Wagombea waliopitishwa kuwania uongozi na Kamati ya Uchaguzi ya TAFCA chini ya uenyekiti wa Ramadhan Mambosasa ni Oscar Don Koroso (Mwenyekiti), Lister Manyara (Makamu Mwenyekiti) na Katibu (Michael Bundala).

Wengine ni Gabriel Gunda (Katibu Msaidizi), Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania- TFF (Wilfred Kidao) wakati wagombea ujumbe wa Kamati ya Utendaji ni Jemedali Saidi, George Komba na Magoma Rugora.

Kivumbi cha Ligi Kuu kuendelea J'mosi, Yanga kunusa ubingwa?



Wachezaji wa Yanga wakifurahia moja ya mabao yao ya Ligi kuu

Na Boniface Wambura

KIVUMBI cha Ligi Kuu Tanzania Bara (VPL) kinatarajiwa kuendelea tena Jumamosi kwa mechi tatu kupigwa viwanja vya mikoa mitatu tofauti ya Mwanza, Dar es Salaam na Morogoro.
Timu inayopigana kuepuka kushuka daraja, Toto Africans itakuwa dimba la nyumbani la CCM Kirumba jijini Mwanza kuvaana na Mgambo JKT katika moja ya pambano linalosubiriwa kwa hamu wikiendi hii.
Toto walio nafasi ya pili kutoka mkiani wakiwa na pointi 15 na ikiuguza kipigo cha 'kaka' zao Yanga itakuwa na kiu ya kupata ushindi ili kuweza kujinasua mkiani na kujiweka katika nafasi za kuepuka kushuka daraja.
Pambano jingine la mwishoni mwa wiki ni kati ya vinara wa ligi hiyo, Yanga watakaokuwa dimba la Taifa jijini Dar es Salaam kuwakaribisha maafande wa Ruvu Shooting, mechi ambayo itatoa taswira ya mbio za ubingwa kwa Yanga ambao msimu huu wameonekana wapo tofauti wakiwa na kiu ya kutwaa taji.
Mpaka sasa Yanga inaoongoza msimamo wa Ligi ikiwa na pointi 45 kutokana na mechi 19 ilizocheza ikifuatiwa na Azam waliopo nafasi ya pili na pointi zao 37 kisha Simba wanaokamata nafasi ya tatu wakiwa na pointi 34 wote pia wakiwa wamecheza mechi 19 kila mmoja.
Mtanange mwingine wa Jumamosi utazikutanisha timu zinazolingana pointi na kutofautiana uwiano wa mabo ya kufunga na kufungwa, Coastal Union ya Tanga watakaokuwa wageni wa Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Manungu, Morogoro.
Mshindi yoyote wa mechi hiyo wataweza kufikisha pointi 34 na hivyo kuwakamata mabingwa watetezi ambao wenyewe watashuka dimbani siku ya Jumapili.