STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 9, 2013

Aisha Bui akana kukamatwa na 'unga' Brazili, adai yu salama Afrika Kusini


MWANADADA anayetamba kwenye filamu nchini, Aisha Bui amekanusha taarifa kwamba amekamatwa na dawa za kulevya na kufungwa kifungo cha miaka mitano nchini Brazil.

Akizungumza na MICHARAZO kutoka Afrika Kusini, Aisha Bui alisema ameshtushwa na taarifa hizo za kunaswa na 'bwimbwi' Brazili, ilihali yeye yupo Afrika Kusini salama wa salimini.
Aisha alisema angependa kuwafahamisha watanzania kwamba yu salama na wazichukulie taarifa hizo kama uzushi kwa sababu hajawahi na wala hajishughulishi na biashara hiyo ya 'unga'.
Pia mwanadada huyo alitupia ujumbe katika 'wall' yake Facebook akisisitiza suala hilo kwa kuandika;
Dear Friends, Fans n Family Naskia kuna habari flani mbaya zimetolewa na baadhi ya vyombo vya habari, napenda kuwajulisha wote kua hiyo si kweli Mimi ndio kweli niko safari lkn niko salama salmin Hakuna kitu Kama Hicho n namuomba mungu aniepushe na mambo hayo. Niko poa Kabisa n nawapenda wote.
Alipoulizwa kama kuna hatua zozote atakazochukua kwa kuzushiwa tuhuma hizo, Aisha aliyewahi kung'ara katika filamu mbalimbali, alisema hana mpango wa kufanya lolote kwa sababu hataki kugombana na vyombo vya habari, inagwa hakupendezwa na kilichoripotiwa ambacho alidai alikisoma mapema leo.
"Nawapotezea tu sina mda wa kugombana na vyombo vya habari," alisema Aisha Bui, mwanadada aliyewahi kuripotiwa kuolewa na aliyekuwa mfanyabiashara na mdau mkubwa wa muziki nchini, Marehemu Mohammed Mpakanjia.

MSAIDIE MWANAHABARI HUYU MUNGU ATAKULIPA INSHALLAH


 Zuberi Mussa  katika mwonekano wa picha tofauti 
tofauti nje ya Ofisi ya Mtendaji Kata ya Mazinde.

Zuberi Mussa (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Mwandishi Dotto Mwaibale (kushoto), Mashaka Kibaya (kulia) wote wa Gazeti la Jambo Leo na Mashaka Mhando wa Gazeti la Majira, walipokwenda kumjulia hali kijjiini kwao.

Na Dotto Mwaibale, Tanga
Zuberi Mussa ambaye ni mpiga picha mkongwe katika vyombo mbalimbali vya habari nchini ambaye kwa sasa anafanyakazi Kampuni ya New Habari ni mgonjwa anayehitaji msaada wa hali na mali.
Kikubwa kinacho msumbua mwandishi mwenzetu huyu ni ugonjwa ambao bado haujafahamika ambapo kwa mtu anayemfahamu ni rahisi kumgundua kuwa ana matatizo ya kiafya kwani katika kila sentesi yake ya pili wakati wa kuongea naye hautaelewana naye kutokana na matamushi yake ambayo hayafahamiki yanayoonesha  kama mtu aliyechanganyikiwa.
Kutokana na kukosekana kwa fedha za kumsaidia katika matibabu hasa Hospitalini, Zuberi Mussa amelazimika kwenda kupata matibabu yake kwa waganga wa jadi.
Wakati Zuberi akiwa kijijini kwao Kata ya Mazinde wilayani Korogwe mkoani Tanga bila ya kuwa na msaada wowote mke wa mwenzetu huyo aitwaye Rehema Amir kwa kipindi cha mwaka mzima yupo hoi kitandani kutokana na maradhi ya kupooza yaliyompata mwanzoni mwa mwaka jana akiwa jijini Dar es Salaam, hawezi kufanya chochote ikiwa ni pamoja na kuongea hakika inaumiza na kusikitisha.
Ndugu wanahabari kila mmoja wetu kwa imani yake na utamaduni tulionao wa kusaidiana tujitokeze kumsaidia mwenzetu huyu ambaye anapita katika kipindi kigumu.
Binafsi nilipofika kumuona kwa mara ya kwanza wiki iliyopita nilishitushwa na hali aliyokuwa nayo ingawa kaka yake aitwaye Waziri Mussa anayemuuguza alidai kuwa alikuwa amepata nafuu.
Zuberi alifika katika eneo nililokuwepo akiwa katika hali ambayo si ya kawaida zaidi ya kusalimiana na kunitambua mengine yote nilioongea naye hatukuweza kuelewana. Kwa mtu yeyote atakayependa kumsaidia Zuberi pamoja na mke wake kipenzi  Rehema Amir anaweza kuwasiliana na Dotto Mwaibale kwa namba 0712-727062 ambaye atakuunganisha na kaka yake.
Ndugu wanahabari wenzangu  na mtu mmoja mmoja, Taasisi yoyote, shirika lolote, Mfuko wa Taifa wa  Bima ya Afya, Wafanyabiashara, Makampuni mbalimbali na vyama vya michezo  hima tujitoe kimasomaso kumsaidia mpiga naji mwenzetu Zuberi Mussa na mke wake waondoke katika matibabu ya jadi wanayopata badala yake wapelekwe hospitali kwa uchunguzi zaidi wa afya zao kwani kutoa ni moyo na si utajiri.
 

Sunday, September 8, 2013

Narietha Boniface ndiye Redd's Miss Tanzania Top Model 2013

Mshindi wa taji la Redd’s Miss Tanzania Top Model 2013, Narietha Boniface katika picha ya kwanza hapo chini akiwa amepozi mara baada ya kushinda taji hilo jana na kuwa mrembo wa pili kuingia katika nusu fainali za Miss Tanania 2013 baada ya kuwashinda warembo wenzake 29. Shindano la Miss Tanzania Top Mode lilifanyika katika Hoteli ya Snow View Arusha na kuwashirikisha warembo 30. 
Mshindi wa taji la Redd’s Miss Tanzania Top Model 2013, Narietha Boniface (katikati) akipozi kwa picha na mshindi wa pili Elizabeth Pert (wapili kushoto), mshindi wa tatu Svetlana Nyameyo (wapili kulia), mshindi wanne Happiness Watimanywa ambaye pia ni Miss Tanzania Photogenic 2013 na Mshindo wa tano Latifa Mohamed, mara baada ya kushinda taji hilo jana ambapo Narietha amekuwa mrembo wa pili kuingia katika nusu fainali za Miss Tanania 2013 baada ya Miss Photogenic. Shindano la Miss Tanzania Top Mode lilifanyika katika Hoteli ya Snow View Arusha na kuwashirikisha warembo 30.

Warembo walipo jinadi kwa pozi kali na miondoko ya kufa mtu katika kuwania taji hilo la Redd's Miss Tanzania Top Model 2013 ndani ya Snow View Hotel Arusha.
Wadau kutoka TAN MEDIA ambao ni waendeshaji wa Radio Gwala (Radio 5) ya jijini Arusha wakifuatilia kwa ukaribu shindano hilo wakiongozwa na Fransic
Emma Mroso kutoka JAZZ Collection ya jijini Arusha akipozi na warembo waliovaa mavazi kutoka kampuni hiyo.
Wadau mbalimbali wakifuatilia shindano hilo.



STARS YAMALIZA VIBAYA MECHI ZA KOMBE LA DUNIA


Na Boniface Wambura
TIMU ya soka ya taifa, Taifa Stars imemaliza vibaya mechi za mchujo za Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika baada ya kufungwa na Gambia huku Kocha Kim Poulsen akisema timu yake imefungwa mabao mepesi.

Wenyeji Gambia walishinda mabao 2-0 katika mechi hiyo iliyochezwa jana (Septemba 7 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Independence ulioko hapa jijini Banjul ukiwa ni ushindi wake wa kwanza katika kundi hilo la C ambapo imemaliza ikiwa ya mwisho ikiwa na pointi nne.

Akizungumza baada ya mechi hiyo, Kocha Poulsen amesema Gambia ilistahili kushinda kwa vile ilitengeneza nafasi nyingi kuliko timu yake, na kuongeza kuwa mabao iliyopata Gambia yalikuwa mepesi.

“Hatukutengeneza nafasi nyingi za kufunga, lakini tukaruhusu mabao mapesi. Nawapongeza Gambia kwani walistahili ushindi. Unapofanya makosa unaadhibiwa. Gambia ilikuwa timu nzuri leo, kwani ilitengeneza nafasi nyingi za kufunga, sisi tukatoa mabao mepesi,” amesema Kim.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imemaliza katika nafasi ya tatu katika kundi hilo lililokuwa na timu nne ikiwa na pointi sita ilizozipata nyumbani kwa kuzifunga Morocco na Gambia.

Hata hivyo, Kim amesema sababu nyingine ya kutofanya vizuri ni kuwakosa wachezaji wanaocheza nje ya nchi na wengine wa kikosi cha kwanza ambao ni majeruhi.

Mabao yote ya Gambia katika mechi hiyo iliyochezeshwa na Munyemana Hudu kutoka Rwanda yalifungwa na nahodha wa timu hiyo Mustapha Jarjue. Alifunga la kwanza dakika ya 44 na kupachika lingine dakika ya 51, mabao yaliyotokana na wachezaji wa Stars kutokuwa makini.
Katika mechi hiyo Stars iliwakilishwa na Juma Kaseja, Vincent Barnabas, Erasto Nyoni/David Luhende, Nadir Haroub, Henry Joseph, Frank Domayo, Haruni Chanongo, Amri Kiemba, Mrisho Ngasa, Simon Msuva na Khamis Mcha/Juma Liuzio.

Taifa Stars inaondoka Banjul leo (Septemba 8 mwaka huu) saa 6 mchana kwa ndege ya Arik hadi Dakar, Senegal ambapo itaunganisha kwa ndege ya Kenya Airways kupitia Nairobi ambapo itawasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) kesho (Septemba 9 mwaka huu) saa 8.05 mchana.

Saturday, September 7, 2013

Mark Band, Pembe wafyatua nne wakienda kurudia za zamani Ulaya

Rashid Pembe akionyesha makeke yake kwa mashabiki ughaibuni
Rashid Pembe (kulia)
 BENDI iliyojikita kwenye muziki wa asilia ya Mark Band, imekamilisha nyimbo nne kwa ajili ya albamu yao ya pili mpya walioyopanga kuitoa Desemba mwaka huu, wakati wakiwa katika maandalizi ya kurudia nyimbo za albamu yao ya kwanza barani Ulaya.
Mkurugenzi wa bendi hiyo, Rashid Pembe 'Professa', aliiambia MICHARAZO kuwa, nyimbo mbili za mwisho za albamu hiyo mpya zinatarajiwa kutenmgenezwa nchini Chile na kurekodiwa Ufaransa kabla ya kufanyiwa uzinduzi jijini Dar.
Pembe, nyopta wa zamani wa bendi ya Vijana Jazz, alizitaja nyimbo hizo nne zilizokamilika kuwa ni Tanzania Yetu na Kibule zilizotungwa na yeye (Pembe), Amani wa Balusi Kitembo na Nasoma Namba wa Noel Msuya.
"Nyimbo mbili za mwisho tutaenda kuzimalizia tukiwa kwenye ziara yetu nchini Chile na kuzirekodia Ufaransa, lakini pia tumepanga kurudia upya nyimbo za albamu yetu ya kwanza ambayo imechangia kutupatia mialiko Ulaya na Amerika," alisema.
Alisema wamelazimika kuzirudia upya nyimbo hizo kwa ushauri wa wadhamini wao barani Ulaya ili kuzifanya ziwe na kiwango za kimataifa na kuzidi kujizolea soko nje ya nchi.
Pembe, mkali wa kupuliza 'domo la bata' alizitaja nyimbo zitakazorudiwa Ulaya ambazo ziliitambulisha bendi hiyo iliyoanzishwa mwaka 2006 ni 'Matukio', 'Baba Kaleta Panya', 'Slow Puncture', 'The Girl from Tanzania', 'Amani Tanzania' na 'Angela'.

Zola D 'kuparii in da house' Mombasa

Mkali Zola D katika pozi
NYOTA wa muziki wa Hip hop nchini, David Mlope 'Zola D' amekamilisha wimbo wake mpya uitwao 'Party in da House' na kwa sasa amekimbilia Mombasa Kenya kwa ajili ya kurekodi video yake.
Akizungumza na MICHARAZO, Zola D staa wa nyimbo za 'Moto wa Tipper', 'Rap Gangester', 'Msela Sana' na Jana Siyo Leo', alisema ameamua kwenda kurekodi video hiyo Mombasa kwa lengo la kuipa mandhari tofauti.
Alisema, ndani ya wimbo huo ameimba na 'dogo' aitwaye Man DVD ambaye pia ndiye mzalishaji wa wimbo huo ambao alidai video yake itaachiwa hadharani ndani ya mwezi mmoja ujao baada ya kukamilika kwake.
"Natarajia kuachia 'ngoma' yangu mpya ya 'Party in da House' ambayo nimpigiwa 'chorus' (kibwagizo) na Man DVD na video yake naenda kuirekodia Mombasa Kenya kwa nia ya kuipa ladha na mandhari tofauti na kazi zangu za nyuma," alisema Zola D.
Msanii huyo mwenye 'mwili jumba' na anayejishughulisha pia na mchezo wa ngumi, alisema kazi hiyo mpya ni kati nyimbo zitakazokuwa katika albamu yake ijyao itakayofahamiaka kama 'Swahili Hip Hop'.

Friday, September 6, 2013

Aishi Manula achekelea ushindani Ligi Kuu

Kipa Aishi Manula
KIPA mahiri anayedakia timu ya Azam FC na timu ya soka ya Tanzania (Taifa Stars), Aisha Manula, amesema anafurahishwa na hali ya ushindani uliojitokeza mapema kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu.
Manula, miongoni mwa wachezaji chipukizi waliopo kikosi cha Kim Poulsen kinachojiandaa na mechi ya kukamilisha ratiba kati ya Tanzania na Gambia, alisema kwa mwendo ulianza kwenye ligi hiyo ni wazi msimu huu ni mgumu.
Kipa huyo aliyewahi kuwa kipa bora wa michuano ya Uhai Cup 2011, alisema matokeo ya kustaajabisha yaliyojitokeza katika mechi za raundi mbili za awali ni dalili za kuwa na msimu mgumu ulioweza kutabirika kirahisi.
"Nafurahishwa na namna ligi ilivyoanza, inaonyesha itakuwa ya aina yake msimu huu kwani timu zinaonyesha kupania kufanya vyema na ndiyo maana mechi mbili za awali za kila timu kumekuwa na matokeo yaliyostaajabisha, " alisema. Manula, alisema kwa upande wa klabu yake ya Azam anaamini huu utakuwa ni msimu wake wa kuweka rekodi kwa kunyakua ubingwa kwa mara ya kwanza baada ya miaka nenda taji hilo kuzunguka klabu za Simba na Yanga.
Kipa huyo aliyekuwa dimbani wakati Azam ikizamishwa bao 1-0 na Yanga katika mechi ya Ngao ya Hisani, alisema haoni kitakachoizuia Azam isitimize ndoto ya kutwaa taji la Ligi Kuu mwaka 2013-2014.
Azam washindi wa pili wa misimu miwili mfululizo, ilianza ligi hiyo kwa mechi za ugenini ikipata sare ya 1-1 kwa Mtibwa Sugar kabla ya kuilaza Rhino Rangers  2-0 mjini Tabora na mechi ijayo itakuwa Kagera kuvaana na Kagera Sugar.

Mauaji ya kinyama! Waendesha Bodaboda wazidi kuuwawa Iringa

Edger Lalika akiwa  wodini kabla ya  kufariki dunia
 Francis Godwin na  Kayanda Mnyanya,Iringa 
 
ZIKIWA  zimepita  siku  chache  toka  mmoja kati ya madereva boda boda mjini Iringa kutekwa kisha  kujeruhiwa vibaya kabla ya kuporwa  pikipiki  yake ,unyama huo dhidi ya madereva  boda boda  umeendelea kutikisa mji wa Iringa baada kijana mmoja mkazi wa kihodombi kutekwa kisha kuuwawa kinyama.
Tukio hilo la kinyama  limetokea  usiku  wa  leo baada ya kijana  huyo aliyetambulika kwa  jina la Edger Lalika kukutwa ameuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani .
Mashuhuda  wa  tukio hilo  wameueleza mtandao  huu wa matukio daima .com kuwa tukio la kuuwawa  kwa  dereva  boda  boda  huyo liletokea eneo la  Tosamaganga wilaya ya Iringa mkoani Iringa.
Hata  hivyo kijana  huyo anayekadiliwa  kuwa na umri wa miaka 20,ameuwa akiwa anafanya shughuli zake za bodaboda baada  ya  kukodiwa na mteja  wake huyo ambae aliamua  kuitoa roho yake kabla ya kumpokonya boda boda.
Kutokana na tukio  hilo  baadhi ya madereva bodaboda wamelaani vikali kitendo hicho na kuwataka madereva bodaboda wengine kuungana na kushirikiana na jeshi la polisi kufichua vitendo hivyo  vya utekaji na mauwaji  dhidi ya madereva  boda boda.
Mazishi ya kijana huyo yanafanyika leo katika makaburi ya mlolo Iringa mjini
Jeshi la  polisi mkoa  wa Iringa  limethibitisha  kutokea kwa mauwaji  hayo.

Matukio Daima

Mhe. Ndugai atupiwa lawama vurugu za jana bungeni

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgbR2CeEeeh8aIgUAxVg23rr5e1DG0s7zx41yhCH6ZY0ziYoTLNSlZ-GP5_9Ea0yd37vWfoS1hBkiDketxjf3x7RCdF75YebSxZRnTJ2pZrrF6f6fURo2Bm3aA0BXX6bHz5R5_eUhGDKMDI/s400/_MG_0724+MBILI.JPG

Wanabodi, 
Mwaka mmoja uliopita niliwahi kuleta hoja hii humu Wito: Wabunge Badilini Kanuni Kuondoa Udikteta wa Spika/N.Spika!
Leo nimeikumbuka kufuatia vurugu za jana bungeni!.
Chanzo cha vurugu zile ni "Ukosefu wa Busara Ndogo Tuu toka kwa Naibu Spika!".
Tangu tumepata uhuru, Tanzania imekuwa nchi ya chama kimoja kwa kipindi kirefu, tulipoingia mfumo wa vyama vingi ile 1992, tulifanya marekebisho tuu ya kanuni, ila hatukuweza kufanya mabadiliko ya "mind set" toka mfumo wa chama kimoja hadi mfumo wa vyama vingi, hivyo hali hii imeendelea mpaka sasa kwa CCM ambayo ndio chama tawala, kuendelea kuonekana ni chama dola kwa sababu ndiyo inayoongoza dola, na nafasi ya vyama vya upinzani kuonekana vipo vipo tuu kwa vile vimeanzishwa kwa mujibu wa sheria!.
Kufuatia hali hii ya "CCM Supremacy" kunapelekea viongozi wa mihimili mikuu ya nchi, Bunge, Mahakama na Serikali, kutimiza wajibu wake kwa mlengo wa heshima kwa CCM kwa sababu M/Kiti wa chama tawala ndie head of Executive, ambaye ndiye rais wa nchi anaeteua kila mtu!.
Huku kujikomba komba kwa CCM, kumepelekea hata Spika na Naibu Spika ambao walipaswa kutimiza majukumu yao independently, wanajikuta wakiifavour CCM, kwa lengo la kujikomba komba huku wakiliangamiza taifa bila wao kujijua kwa kisingizio kuwa kwa vile CCM ndio chama tawala!.
Kwa mujibu wa uendeshaji wa mabunge ya vyama vingi, Mkuu wa shughuli za serikali bungeni, ambaye ni Waziri Mkuu, na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, KUB, ambaye ni Mhe. Freeman Mbowe, wana hadhi sawa kabisa ndani ya bunge!. Hakuna mmoja ambaye ni mkubwa zaidi ya mwingine wala hakuna aliyebora zaidi ya mwenzake!. Wako sawa sawa kabisa!.
Vivyo hivyo, hadhi za mawaziri na mawaziri vivuli ndani ya bunge ni sawa kabisa, tofauti pekee ni mawaziri wana means zaidi kutokana na uwezeshaji kiliko hawa vivuli!. Mfano Waziri Magufuli, akishakagua barabara au kuizindua, waziri kivuli alipaswa aifanyie ukaguzi na kutoa mawazo yake kama ni chini ya kiwango etc, etc.
Haki zote za Waziri Mkuu bungeni ndizo pia haki za KUB!. 
Japo haijaandikwa kwenye kanuni yoyote kuwa Waziri Mkuu akisimama, "ni lazima spika ampe ruhusa ya kusikilizwa" no matter what!. Spika hana mamlaka yoyote ya kuamua kutomsikiliza Waziri Mkuu anaposimama kwa hoja yoyote!. Vivyo hivyo, spika au naibu spika, "hana mamlaka!" ya kumzuia KUB kuzungumza!. 
Naomba wale wenye mapenzi mema na nchi hii, hebu tuwe wakweli toka ndani ya nafsi zetu, hivi kweli pale bungeni jana, angesimama Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda, hivi kweli Naibu Spika angemwambia "Kaa Chini?!". Angeendelea kusimama hivi Naibu Spika angewaamuru askari wa bunge kumtoa nje?!.
Hadhi ya KUB ni sawa kabisa na Waziri Mkuu, kitendo cha Naibu Spika kumzuia KUB asizungumze, kumuamuru akae chini na kisha kuamuru atolewe nje, "that was provocation kwa wapinzani wote wa kweli!", kiliwatia hasira, na kilichofuata ni actions in provocation!. Chanzo ni ukosefu wa busara ndogo tuu wa Naibu Spika!.
Laiti Mhe. Naibu Spika, angelimruhusu KUB kuzungumza na kuisikiliza hoja yake!, naamini 100% kwa 100%, yote yaliyofuatia yasingetokea!.
Bungu letu lina mapungufu makubwa na ya msingi ya kikanuni za uendeshaji mabunge ya vyama vingi!. Kiukweli kila kunapotokea vurugu bungeni, mimi huwa namkumbuka sana Mhe. Samuel Sitta!.
Kiukweli huko nyuma nimewahi kulalamikia sana uendeshaji wa bunge wa Madam Spika, Mhe. Anna Makinda, lakini sasa sasa nakiri, pamoja na mapungufu yake yote ya kibinaadamu, Mhe. Anna Makinda is better of 100 times than Mhe. Job Ndugai!. This man is a disaster!. 
Wabunge tumieni kanuni namba 135-(1) Kutuondolea mtu huyu, japo najua wabunge wa CCM watautumia wingi wao vibaya kutoipitisha hoja hiyo, ile tuu process ya "kukataliwa!" ni funzo tosha!.
Mwaka mmoja uliopita nilitoa angalizo hili, na leo nalitoa tena! Wito: Wabunge Badilini Kanuni Kuondoa Udikteta wa Spika/N.Spika!

Wasalaam.
Pasco.

Chanzo : JamiiForums

Msikiti wa Answar Sunna wateketea kwa moto, kisa...!

 
MSIKITI mkubwa wa Answar Sunna  uliopo  barabara ya Saba mjini Dodoma  umewaka  moto  mchana  huu  ikiwa  ni  muda  mfupi  baada  ya  swala  ya  mchana  kumalizika.

Akiongea  kwa  njia  ya  simu  mmoja  wa  mashuhuda  walioshuhudia  tukio  hilo  amedai  kuwa  chanzo  cha  moto  huo  ni  moto wa  JIKO  la  wakazi  wa    ghorofa ya  juu  ya  jengo  la  msikiti  huo...

Hata  hivyo, shuhuda  mwingine  aliyeongea  na  mtandao  huu  amedai    kuwa  chanzo  cha  moto  huo  ni  hitilafu  ya  umeme  iliyoanzia  ghorofa  ya  juu  ya  jengo  hilo.

 
Kwa  mujibu  wa  mashuhuda  hao, moto  huo  umefanikiwa  kudhibitiwa  na  jeshi  la  zima  moto  na  kwamba  hakuna  mtu  aliyepoteza  maisha  kutokana  na  moto  huo.


  
MPEKUZI

Anko Kitime, Shigongo, Msama waula BASATA

Profesa Penina Mlama
Na Veronica Kazimoto – MAELEZO, Dar es Salaam
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Profesa Penina Mlama kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo.  
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Idara ya Habari - MAELEZO, Uteuzi huo wa Profesa Mlama unaanzia mwaka 2013 na unatarajia kumalizika mwaka 2016.
Prof. Mlama ni Profesa wa Sanaa na Sanaa za Maonyesho Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.  
Aidha Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara ameteua jumla watu 12 kuwa wajumbe wa BASATA kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo kuanzia mwaka huu.
Walioteuliwa ni pamoja na wawakilishi wa Vyama na Asasi mbalimbali wa Baraza hilo ambao ni Dkt. Vincensia Shule, John Kitime, Angela Ngowi, Dkt. Herbert Makoye, Erick Shigongo na Alex Msama.
Alex Msama
Wawakilishi wengine ni pamoja na Juma Adam Bakari, Daniel Ndagala, Michael Kadinde na Joyce Fisoo.
Wanaoingia kwa mujibu wa nyadhifa zao ni Prof. Hermas Mwansoko na Katibu Mtendaji wa BASATA.
http://www.bongocelebrity.com/wp-content/uploads/2012/06/John-Kitime.jpg
John Kitime 'Anko'
 
Katika hatua nyingine Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara amemteua Bwana Ghonche Materego kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa). 
Kabla ya uteuzi huo Materego alikuwa amemaliza muda wake kama Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa.
Wajumbe wa Bodi hiyo walioteuliwa na Waziri Mukangara ni Dkt. Herbert Makoye, Prof. Emanuel Mbogo, Dkt. Lucy Mboma, Prof. Hermas Mwansoko pamoja na Katibu Mtendaji wa BASATA.
Wakati huo huo Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara ameteua jumla ya watu 21 kuwa wajumbe wa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia mwaka 2013 hadi 2015. 
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjoeAYpD19CUAPAApd52dHguEu911uTkpaFXAq9066MauQU5HEOi7C5LkQMpYFJQ0CXHPoiVJTGw5pvzB3-YujazwtVwQPuZQWhh4elz789G570CD39Q2Vvf-E15sj7DMO2jURIUcZW5jJy/s1600/eric.jpg
Eric Shigongo
Wajumbe hao ni Dkt. Shani Omari, Prof. Yohana Msangila, Ester Riwa, Dkt. Issa Zidi, Khadija Juma na Dkt. Martha Qorro.
Wengine ni Mmanga Mjawiri, Razia Yahaya, Richard Mbaruku, Selina Lyimo, Keneth Konga, Amour Khamis, John Kiango, na Shani Kitogo. 
Wajumbe wengine ni Ally Kasinge, Ahmed Mzee, Rose Lukindo, Shabani Kisu pamoja na Edwin Mgendera.
Taarifa hiyo imefafanua kuwa Mwenyekiti wa Baraza hilo la BAKITA atachaguliwa na wajumbe watakapokutana kwenye kikao chao cha kwanza.

Zantel yamleta Azonto, kuwasha moto kesho Dar

Mwanamuziki anayetamba na wimbo wa Azonto kutoka Ghana, Fuse ODG (katikati), akionesha manjonjo yake  wakati wa mkutano na waandishi wa habari, kuhusiana na onesho lake litakalofanyika Jumamosi katika viwanja vya Posta jijini Dar es Salaam. Katikati ni Ofisa Biashara Mkuu wa Zantel, Sajid Khan. Mwanamuziki huyo ameletwa na Kampuni ya Simu za mkononi ya Zantel kwa kushirikiana na Times FM. (Picha na Francis Dande)
Mwanamuziki anayetamba na wimbo wa Azonto kutoka Ghana, Fuse ODG akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kuhusiana na onesho lake litakalofanyika leo katika viwanja vya Posta jijini Dar es Salaam. Wa pili kushoto ni Ofisa Biashara Mkuu wa Zantel, Sajid Khan.

Wanaombeza bondia Francis Cheka someni hapa!

Francis Cheka (kulia) alipokuwa akimsulubu Mmarekani Phil Williams na kutwaa mkanda wa WBF
HIVI karibuni Mtanzania Francis Cheka ambaye alikuwa  bingwa wa IBF katika bara la Afrika uzito wa kati (Super Middleweight) alimshinda bondia kutoka Marekani Phil William na kutawazwa kuwa bingwa wa dunia anayetambuliwa na Shirikisho la Ngumi la Dunia (WBF). Ushindi wa Cheka sio tu kwa Tanzania bali na kwa bara la Afrika na dunia yote kwa ujumla.
 
Cheka ameungana na mabingwa wengine wa dunia wa uziro wa kati (Super Middleweight) wanaotambuliwa na vyama na mashirikisho kadhaa kama ifuatavyo:
 
IBF    -  Carl Froch kutoka nchini Uingereza
WBC -  Andre Ward kutoka nchini Marekani
WBA -  Andre Ward kutoka nchini Marekani
WBO -  Robert Stieglitz kutoka nchini Ujerumani
WBF -   Francis Cheka kutoka nchini Tanzania
IBO   -  Thomas Oosthuizen kutoka nchini Afrika ya Kusini

Kwa uchache hao ni mabingwa wa uzito wa uzito wa kati (Super Middleweight ) wanaotambuliwa na vyama/mashirikisho hayo niliyoyataja hapo juu. Kati ya mabingwa wa dunia wa mashirikisho/vyama sita vikubwa duniani Afrika imetoa mabindia wawili tu nao ni Francis Cheka kutoka nchini Tanzania na Thomas Oosthuizen kutoka nchini Afrika ya Kusini.
 
Ubingwa alioupata Francis Cheka ni wa dunia na hautakiwi upingwe na mtu yeyote yule nje ya ulingo bali wanaotaka kumpinga na kuukebehi wanatakiwa wapande naye ulingoni au wamtafutie mtu wao apande naye ulingino ili apigane na Francis Cheka.
 
Kwa bahati mbaya, taratibu na sheria za mchezo wa ngumi haziruhusu mtu yeyote ambaye hayuko kwenye viwango vya ubora wa ngumi agombee ubingwa wa aina yeyote ule.
 
Mashirikisho au vyama vya ngumi vimeweka utaratibu maalum wa mabondia watakaoweza kugombea ubingwa wa dunia na mara nyingi ni wale tu walio kwenye viwango vya juu kuanzia namba moja hadi namba tano.
 
Tanzania sasa tuna bingwa wa dunia katika uzito wa kati (Super Middleweight) na ni Francis Cheka. Tunachukua fursa hii kumfagilia na kumpongeza Francis Cheka kwa kulitangaza vyema jina la Tanzania na kuliweka kwenye chati duniani.
Onesmo Ngowi
Rais wa IBF Africa, Ghuba ya Uarabu na Uajemi na mashariuki ya Kati
 

Stars watua salama Banjui, Kaseja kukaa golini kesho

Juma Kaseja
Na Boniface Wambura
KIKOSI cha Taifa Stars kimewasili salama hapa Banjul, Gambia tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya wenyeji itakayochezwa kesho (Septemba 7 mwaka huu).

Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imewasili hapa jana (Septemba 5 mwaka huu) saa 11 jioni ikitokea Dakar, Senegal ambapo ilichelewa kuunganisha ndege, hivyo kuamua kutumia usafiri wa barabara kwa vile ni karibu na baadaye kupanda kivuko kuingia Banjul badala ya kulala na kuchukua ndege nyingine siku inayofuata.

Wachezaji wako katika hali nzuri na leo jioni wanatarajia kufanya mazoezi ya mwisho kwenye Uwanja wa Independence ulioko Bakau ambao utatumika kwa mechi ya kesho. Timu imefikia hoteli ya Seaview iliyoko kandokando ya Bahari ya Atlantic.

Mechi hiyo itaanza saa 10.30 jioni kwa saa za hapa ambapo nyumbani Tanzania itakuwa saa 1.30 usiku, na itachezeshwa na waamuzi kutoka Rwanda Munyemana Hudu. Waamuzi wasaidizi ni Theogene Ndagijimana, Honore Simba na Issa Kagabo. Kamishna ni Andy Quamie kutoka Liberia.

Washabiki na vyombo vya habari vya hapa wanaizungumzia mechi hiyo ambayo ina umuhimu mkubwa kwa pande zote, huku Gambia ikiwa imeita wachezaji tisa wanaocheza barani Ulaya na Marekani. Gambia ambayo imepata uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Gambia (GFA) imepania kuhakikisha haimalizi mechi za mchujo ikiwa na pointi moja tu.

Kwa upande wa Tanzania, Kocha Kim Poulsen amesema nia ni kuona Stars yenye pointi sita inamaliza katika nafasi ya pili nyuma ya Ivory Coast ambayo tayari imechukua tiketi pekee ya kucheza raundi ya mwisho kutoka kundi hili la C.

“Mechi hii ni muhimu kwetu kwa vile tunataka matokeo mazuri ugenini. Lakini kikubwa ni kuwa matokeo mazuri si tu yatatuweka katika nafasi ya kuwa wa pili, lakini vilevile yatatusaidia kuongeza pointi kwenye viwango vya ubora vya FIFA, na kikubwa zaidi hii ni sehemu ya maandalizi ya sisi kucheza Fainali za Afrika za 2015,” amesema Kim.

Stars inatarajiwa kupangwa hivi; Juma Kaseja, Vincent Barnabas, Erasto Nyoni, Nadir Haroub, Henry Joseph, Frank Domayo, Haruni Chanongo, Amri Kiemba, Mrisho Ngasa, Simon Msuva na Khamis Mcha.

Yanga yafafanua sakata la Katibu Mkenya

Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Clement Sanga (kati) akifafanua jambo wakati wa mkutano wake na wanahabari leo kufafanua suala la ajira ya Katibu Mkuu wa klabu hiyo uliofanyika leo. (Picha:Francis Dande)
UONGOZI wa klabu ya Yanga kupitia Makamu Mwenyekiti wake, Clement Sanga ametoa ufafanuzi juu ya habari zilizokuwa zimeenea kuhusiana na taarifa za mabadiliko ya kaimu katibu mkuu Lawrence Mwalusako kuondolewa kwenye nafasi yake na kuchukukuliwa na mtu mwingine.
Akiongea na waandishi wa habari leo,  Sanga amesema taarifa hizo hazina ukweli kwamba tayari kuna mtu anachukua nafasi ya Mwalusako, bali kilichotokea ni kutokuwepo kwa mawasiliano mazuri katika suala hilo kati ya viongozi na wazee.
Kilichopo ni kwamba uongozi wa klabu ya Young Africans upo katika mchakato wa kuhakikisha unajaza nafasi zilizopo wazi za mkurugenzi wa ufundi, mkurugenzi wa masoko, mkurugenzi wa fedha na zoezi hilo linaendeshwa na kampuni moja ambayo waliipa nafasi ya kuendesha zoezi hilo.
Zoezi likiwa ndani ya mchakato mmoja wa waombaji wa nafasi hizo Patrick Naggi aliwasili makao makuu ya klabu ya Yanga kwa lengo la kutaka kujua mazingira ya ufanyaji kazi yakoje na kufahamu baadhi ya mambo kuhusiana na klabu ndipo kulipotokea kutokuelewana na baadi ya wanachama wakiwemo wazee waliokuwepo eneo la klabu.
Kwa maana hiyo napenda kutoa taarifa kwa umma na wanachama wa Yanga kuwa uongozi bado haujatoa baraka za ajira kwa mtu yoyote katika nafasi hizo, isipokuwa ni muombaji aliwahi kufika makao makuu kabla ya mchakatao wa usahili kukamilika.
Lawrence Mwalusako anaendelea kuwa kaimu katibu mkuu wa Yanga mpaka hapo kutakapokuwa na taarifa nyingine zozote za mabadiliko kwa nafasi zote zilizopo wazi katika idara mbalimbali.
Uongozi unawaaomba wanachama, wapenzi na washabiki wa soka kuwa kitu kimoja katika kuunga mkono harakati za kimaendeleo ili kuifanya timu iende katika hatua nyingine ya ushindani wa kimatifa.

Fundi Kinyambe fumbafu thana

Kinyambe (kushoto) akiwa na Mzee Jangala

MCHEKESHAJI mahiri nchini James Mohammed 'Kinyambe'  amefyatua filamu tatu binafsi ambazo amepanga kuziachia moja baada ya nyingine hivi karibuni.
Kinyambe anayetamba kwenye kipindi cha vichekesho cha 'Vituko Show' alizitaja filamu hizo kuwa ni 'Fundi Kinyambe', The Twins na ' Fumbafu Thana' kuanzia Novemba mwaka huu.
Akizungumza na MICHARAZO, Kinyambe alisema filamu hizo amepanga kuziachia moja moja kuanzia Novemba mwaka huu.
Kinyambe alisema filamu hizo za vyumba mbavu ameigiza na wasanii mbalimbali nchini wakiwamo wenzake wanaoigiza nao katika kipindi cha 'Vituko Show'.
"Ni kati ya kazi zinavyomfanya mtazamaji ashikilie mbavu zake mwanzo mwisho, nitaanza kuziachia rasmi Novemba nikianza na 'Fundi Kinyambe' kisha 'The Twins' na kumalizia 'Fumbafu Thana'," alisema Kinyambe.

Afande Sele kuzindua Novemba

Afande Sele

MSANII mkongwe wa muziki wa kizazi kipya, Seleman Msindi 'Afande Sele' anatarajia kufanya uzinduzi wa albamu yake mpya iitwayo 'Kingdom wa Amani na Upendo' utakaofanyika Novemba mwaka huu mjini Morogoro na kusindikizwa a  wasanii mbalimbali nyota wa hapa nchini.
Akizungumza na MICHARAZO Afande Sele, alisema kwa sasa ni mapema kuwataja wasanii watakaomsindikiza kwa sababu anaendelea kumalizana na wadhamini wake.
Alisema kwa sasa anajipanga kuitambulisha albamu hiyo kwa kuachia video ya wimbo unaoendelea kutamba wa 'Dini Tumeletewa' alioimba kwa kushirikiana na Belle 9.
Mkongwe huyo alisema albamu hiyo itakuwa na nyimbo 10 na siku za uzinduzi itaachiwa 'audio' na video yake kwa mpigo ili mashabiki wake wapate vitu kamili kwa wakati  mmoja.
Alitaja baadhi ya nyimbo za albamu hiyo ni pamoja na 'Dini Tumelewa', 'Amani na Upendo', 'Soma Ule', 'Mi Sielewi', 'Karibu Moro', 'Sukari na Chai', 'Simba Dume na 'Kingdom'.

Kinondoni yainyuka Pwani 7-0 Copa Coca Cola


MABINGWA mara mbili wa Copa Coca-Cola timu ya Kinondoni imewapa kipigo kikubwa wenyeji timu ya Pwani cha magoli 7-0 katika mashindano yanayoendelea ya vijana chini ya umri wa miaka 15 ya Copa Coca-Cola ngazi ya kanda kwenye uwanja wa Tumbi, Kibaha juzi jioni.
Kinondoni walipata goli lao la kwanza katika dakika ya 4 kupitia kwa Kidanga Hamadi baada ya kuunganisha krosi kutoka upande wa kulia. Hamadi kwa mara ya pili alitikisa nyavu za wapinzani wao katika dakika ya 11 baada ya kuwapiga chenga mabeki wa timu ya Pwani na kupiga shuti lililotinga moja kwa moja wavuni.
Magoli mengine yalifungwa na Alex Milanzi katika dakika ya sita, Oswin Nungu katika dakika ya 20, Ayubu M. Ayubu katika dakika ya 41, Majid Musa katika dakika ya 66 kwa njia ya penati na Aboubakari Mussa alihitimisha karamu ya magoli katika dakika ya 74.
Katika uwanja wa Chuo cha Ualimu Butimba jijini Mwanza, Geita waliifunga Mara 1-0 katika mechi iliyojaa ushindani.
Kigoma hawakuwa na bahati siku ya Jumatano baada ya kupoteza mchezo dhidi ya wenyeji timu ya Mwanza kwa kufungwa  2-1. Beki wa Kigoma, Hashimu Mussa alijifunga mara mbili katika dakika ya kwanza na ya 72. Kigoma walipata goli lao katika dakika ya 36 kupitia kwa Rashidi Bakari.
Mechi nyingine iliyochezwa katika uwanja huo wa chuo cha ualimu Butimba, Tabora waliilaza Simiyu 2-1. Tabora  walipata goli la kwanza katika dakika ya sita kupitia kwa Selemani Husein kwa njia ya penati kabla ya Rashidi Omary kuhitimisha katika dakika ya 54.
Mechi nyingine katika uwanja wa Butimba juzi iliwakutanisha Shinyanga na Kagera ambapo Shinyanga walishinda 3-0. Magoli ya Shinyanga yalipachikwa wavuni na Anwar Amada katika dakika ya 24, Jahid Nuru dakika ya 60 na Felix Rweyemamu dakika ya 74.
Katika uwanja wa Mkokotoni , Zanzibar , Timu ya Kaskazini Pemba na Kusini Unguja walitoka sare ya 3-3 wakati huo huo Tanga na Temeke nao walitoka sare ya 4-4. Na katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Singida  waliilaza Manyara kwa mabao 2-0.
Fainali za Taifa za Copa Coca-Cola zinahusisha timu 16 ambazo zitaanza kuchuana wiki ijayo jijini Dar es Salaam.

Kaliza wa TRA afagilia masumbwi

Meneja wa Tanzania Revenue Authorithority 'TRA' Mkoa wa Dodoma Bw. Thadeo Kaliza katikati akiwa na promota na mdau wa masumbwi Mohamedi Bawazir kushoto Bondia Fransic Cheka na Fransic Miyeyusho wakati walipokwenda Dodoma kutembelea bunge la jamuhuri ya muhungano wa Tanzania baada ya Cheka kutwaa ubingwa wa Dunia wa WBF na kualikwa chakula cha jioni na meneja huyo mjini Dodoma
Baadhi ya wadau wa masumbwi na mabondia wakigongesheana grass na Meneja wa Tanzania Revenue Authorithority 'TRA' Mkoa wa Dodoma Bw. Thadeo Kaliza wakati wa kutakiana heri baada ya wadau hawo wa masumbwi kupewa heshima ya kutembelea bungeni kwa mara ya kwanza 

Baadhi ya wadau wa masumbwi na mabondia  wakiwa katika picha ya pamoja na  Meneja wa Tanzania Revenue Authorithority 'TRA' Mkoa wa Dodoma Bw. Thadeo Kaliza
Baadhi ya wadau wa masumbwi na mabondia wakigongesheana grass na Meneja wa Tanzania Revenue Authorithority 'TRA' Mkoa wa Dodoma Bw. Thadeo Kaliza wakati wa kutakiana heri baada ya wadau hawo wa masumbwi kupewa heshima ya kutembelea bungeni kwa mara ya kwanza  na kuarikwa kwa chakula cha jioni na meneja huyo
Baadhi ya wadau wa masumbwi na mabondia wakigongesheana grass na Meneja wa Tanzania Revenue Authorithority 'TRA' Mkoa wa Dodoma Bw. Thadeo Kaliza wakati wa kutakiana heri baada ya wadau hawo wa masumbwi kupewa heshima ya kutembelea bungeni kwa mara ya kwanza

Wednesday, September 4, 2013

RUKWA YACHACHAFYA COPA COCA-COLA



Na Boniface Wambura
TIMU ya soka ya Rukwa imeanza vizuri michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 baada ya leo kuichapa Katavi mabao 4-0 katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Shule ya Sekondari Iyunga jijini Mbeya.

Mabao ya washindi yalitiwa wavuni na Tumaini Boniface dakika ya 13 na 65, Francisco Mkanga akipachika la pili dakika ya 29 wakati la mwisho lilifungwa dakika ya 75 na Innocent Ahombile.

Katika kituo cha Zanzibar, wenyeji Mjini Magharibi imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Kaskazini Pemba kwa mabao ya Faisal Salum na Masoud Mohamed.

Mechi ya pili katika kituo hicho ilikuwa kati ya Kusini Pemba na Kusini Unguja. Bao pekee lililofungwa na Othman Abdallah lilitosha kuipa ushindi wa 1-0 timu ya Kusini Pemba.

Tuesday, September 3, 2013

WAFANYAKAZI STRABAG WAFUNGIWA NJE NA UONGOZI KISA....NI WA MRADI WA MABASI YA KWENDA KASI

 Wafanyakazi wa Kampuni ya Ujenzi wa Mradi wa Mabasi yaendayo Kasi Dar es Salaam (DART), ya Strabag, wakiwa nje ya lango kuu la kuingilia makao makuu ya kampuni hiyo, Ubungo, Dar es Salaam asubuhi hii baada ya uongozi wa kampuni hiyo kuwafungia nje, kutokana na mgomo wa kudai maslahi zaidi kufanyika    KAMANDA WA MATUKIO

















KAMANDA WA MATUKIO BLOG