STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 20, 2014

Hatma ya Miss Tanzania 2014 kufahamika kesho! Kuvuliwa taji?



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjs8LfgqeGCLMPD0l_OzCE83e65tFC3XKtcF5RNtChqmmXnSLtnzivIr_yKWVCRr_SiQI8wCA8kjbJBrDOzGZV47nLF2NfhTJ-rWQMggqpMXhYafJ_MS5mS970iGseJepVRkhBM4jAvnR5S/s1600/Sitti+1.jpgHATMA ya Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Mtemvu kuendelea kutambuliwa kama Mshindi wa Shindano la Urembo la mwaka huu au la inatarajiwa kufahamika kesho.
Sitti alitangazwa mshindi wa Miss Tanzania 2014 wiki iliyopita na kuvishwa taji la mtangulizi wake Happyness Watimanywa, Miss Tanzania 2013.



Hata hivyo tangu atangazwe mshindi kumekuwa na tuhuma kwamba mrembo huyo ambaye ni mtoto wa Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu alidanganya kuhusu umri wake halisi.
Inadaiwa kuwa mrembo huyo ni 'bibi' akiwa na miaka 25 na siyo 23 kama inayosisitizwa na Kamati ya Miss Tanzania ambayo imetuhumiwa 'kumpa' taji Sitti, huku mwenyewe akinukuliwa awali akisema ana miaka 18 tu.
Mpaka kufikia kutwaa taji hilo na kuwa mrembo wa 21 wa shindano hilo tangu liliporejeshwa tena mwaka 1994 na Aina Maeda kukata utepe, Sitti alishinda mataji mawili likiwemo la Miss Chang'ombe na Miss Temeke yote ya mwaka 2014.


Pia ataiwakilisha Tanzania katika shindano la Miss World 2015.


Warembo 30 waliingia katika kinyang'anyiro cha Miss Tanzania 2014.


Wengi wanahoji umri halisi wa Bi Sitti Mtemvu wakisema alidanganya

Lillian Kamazima alikuwa mshindi wa pili, ambapo Jihhan Dimachk alishika nafasi ya tatu.


Mara baada ya kutwaa taji hilo kumeibuka utata juu ya umri wa Miss Tanzania 2014.


Habari zimezagaa katika mitandao ya kijamii, ambapo anatuhumiwa kudanganya umri wake. Kuna taarifa zinasema Bi Sitti alitaja kuwa ana umri wa miaka 18, jambo linalobishaniwa.


Lakini ukweli utajulikana Jumanne tarehe 21 Oktoba 2014, ambapo waandaji rasmi wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania, Lino International wameahidi kulitolea ufafanuzi suala hilo.
Mratibu wa shindano hilo, Hashim Lundenga 'Uncle' alinukuliwa na kituo kimoja cha Radio kwamba wao wanajua mrembo huyo ana miaka 23 na siyo 25 inayotajwa, japo alishindwa kubainisha miaka 18 aliyotaja mrembo huyo siku ya fainali hizo.

Ghana, Afrika Kusini 'zaichomolea' CAF AFCON 2015

 
NCHI za Ghana na Afrika Kusini zimeichomolea kiaina Shirikisho la Soka Barani Afrika, CAF juu ya kubeba jukumu la kuandaa Fainali za Kombe la Mataifa Afrika, AFCON 2015 baada ya Morocco kukwepa uenyeji kisa ugonjwa wa Ebola.
Wakati Waziri wa wa michezo wa Afrika Kusini, Fikile Mbalula amesema leo kuwa nchi hiyo haiku tayari kuandaa michuano ya Mataifa ya Afrika Januari mwakani kama Morocco watajivua uenyeji kwasababu ya mlipuko wa ugonjwa wa Ebola, Ghana wenyewe wameweka bayana kuwa haikupanga kubeba jukumu hilo.
Inaelezwa kuwa CAF ilizifuata Afrika Kusini, Ghana na nchi zingine tano kuelekea katika mkutano wao wa Novemba 2 kuamua mustakabali wa michuano hiyo. Lakini Waziri huyo wa Afrika Kusini aliviambia vyombo vya habari vya nchi hiyo kuwa hawako tayari kuwa wenyeji wa michuano hiyo kwani wana majukumu ya kuhakikisha wanasaidia kupambana na kuutokomeza ugonjwa huo ambao mpaka sasa umeshaua zaidi ya watu 4,500. 
Mbalula amesema hata wakati kabla suala hilo halijapelekwa katika bunge la nchi hiyo kujadiliwa jibu lilikuwa ni hapana kwani walikuwa hawana uwezo wa kutosha kwa sasa kuandaa michuano hiyo. 
Afrika Kusini imeweza kuandaa michuano hiyo mara mbili kwa dharura, baada ya kuchukua nafasi ya Kenya mwaka 1996 walioshindwa kwa kukosa fedha na Libya mwaka jana kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Naye Rais wa Ghana, John Mahama amesema nchi bado haijafanya maamuzi kama wakubalia kuwa wenyeji wa michuano ya Mataifa ya Afrika mwakani au la. 
Waziri wa michezo wa Ghana Mahama Ayariga ameeleza kuwa nchi hiyo ambayo imewahi kunyakuwa taji la michuano hiyo mara nne ina miundo mbinu ya kutosha kuwa mwenyeji huku kukiwa kumebakiwa miezi mitatu na wanafikiria ombi hilo la CAF. 
Kauli yake hiyo imekosolewa vikali na Chama cha Madaktari wa nchi hiyo na asasi zingine za kiraia ambao wamedai kuwa kuwa mwenyeji wa michuano hiyo kunaifanya nchi nzima kuwa katika hatari ya kulipukiwa na ugonjwa huo ambao tayari umeshaua watu 4,500 mpaka sasa. 
Katika mkutano wake Mahama alipoza hofu za wananchi wa Ghana na kudai kuwa hakuna uamuzi wowote uliofikiwa mpaka sasa kuhusu kuandaa michuano hiyo inayoshirikisha nchi 16.

Gareth Bale aiweka Real Madrid njia panda Ulaya

http://cf.c.ooyala.com/1jcHI5bzoAOzj81t6e3WBQ9IKBHMte3P/promo230718654
Gareth Bale
KLABU ya Real Madrid bado haina hakika kama nyota wake kutola Wales, Gareth Bale kama atacheza katika mechi dhidi ya Liverpool katika Ligi ya Mabingwa Ulaya siku ya Jumatano.
Bale, 25 anauguza jeraha la misuli ya paja, jeraha lililomfanya ashindwe kushiriki mechi ya La Liga dhidi ya Levante juzi Jumamosi ambapo timu yake ilishinda mabao 5-0, licha ya kuwa benchi kama mchezaji wa akiba.
Taarifa ya klabu hiyo haikufafanua muda ambao Bale atakuwa nje ya uwanja, hata hivyo walisema atazidi kukaguliwa jinsi anavyopata nafuu.
Baada ya mechi yao ya Kundi B itakayochezewa kwenye uwanja wa Anfield, Real Madrid inatarajiwa kukabana koo na mahasimu wao wa jadi Barcelona katika ligi ya El Clasico hapo jumamosi.
Bale aliichezea timu yake ya taifa ya Wales kwa vipindi vyote viwili dhidi ya Bosnia Hercegovina Oktoba 10 kisha akaichezea tena dhidi ya Cyprus siku tatu zilizofuata katika michuano ya kufuzu kwa Fainali za Uero 2016.
Bale ambaye alihamia Real Madrid kutoka Tottenham mwaka uliopita kwa kitita cha pauni milioni 85.3, ameichezea real Madrid mechi 12 huku akiwa amefunga mabao matano.

Mchezaji India afa akibinuka samasoti kushangilia bao

Hapa akiwa bado katika uangalizi wa madaktari hospitali
Hapa wakati akipiga samasoti yaani sarakasi

Hapa ni wakati wa kuugwa mwili wa marehemu
MCHEZAJI wa soka nchini India, Peter Biaksangzuala amefariki kutokana na majeraha aliyoyapata baada ya kuanguka vibaya uwanjani akisherehekea bao lake.
Mchezaji huyo alikuwa na umri wa miaka 23 alijeruhi uti wake wa mgongo baada ya kupiga 'samasoti' uwanjani akisherehekea bao lake la kusawazisha kwa timu yake Bethlehem Vengthlang FC dhidi ya Chanmari West FC.
Biaksangzuala alikimbizwa hospitalini na kufanyiwa upasuaji lakini baadaye alifariki.
Mechi hiyo ambapo alipata jeraha la mgongo, ilikuwa mechi muhimu katika ligi ya nchi hiyo.
Taarifa kutoka kwa ligi hiyo kpitia kwa mtandao wa Facebook, ilisema : 
"imekuwa siku yenye huzuni mkubwa kwa ligi ya Mizoram na kifo cha mchezaji wetu kimetushtua sana pamoja na wachezaji wenzake, wachezaji wa soka na mashabiki wa Mizoram. "
"Peter alikuwa mchezaji mzuri na milizni mzuri sana, na pia alikuwa mchapa kazi.''

Ndanda Fc yakwanza kutimua kocha Ligi KUU 2014-2015

https://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/05/KITAMBI-FILEminimizer.jpg
Kocha Dennis Kitambi aliyetimuliwa kazi Ndanda
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi2Mk1UuFIpUjrvqer3FRmkr0S9KpHVOZtcEZkDIB-piLWMTxJh_u7LApO6hTU6HBJmK3e1B8aa33Lp63lTs1mYA2GG26SxNIfCFhb99_h5Mm7HA5RcyrgEsz-MwSrgwbHTq9ekAsz07Zk/s1600/PICT0123.JPG
Dennis Kitambo katika moja ya mafunzo ya taaluma yake ya ukocha
WAKATI Ligi Kuu ikizidi kuchanja mbuga, klabu ya iliyopanda ligi hiyo, Ndanda ya Mtwara imekuwa klabu ya kwanza msimu huu kumtimua kocha wake baada ya kusitisha mkataba wake na Dennis Kitambi aliyeipandisha baada ya timu hiyo kupokea vipigo vitatu mfululizo.
Kitambi, aliyeitoa timu hiyo katika madaraja ya chini hadi kufikia kucheza ligi kuu kwa mara ya kwanza, alikumbana na kadhia hiyo baada ya Ndanda kupokea kipigoi cha mabao 3-1 nyumbani mbele ya Ruvu Shooting huku ikiwa imepoteza mechi mbili nyingine za nyuma dhidi ya Mtibwa Sugar waliowafunga mabao 3-1 na Cpastal Union waliowanyoosha mabao 2-1 katika mechi za ugenini.
Timu hiyo ilianza ligi kwa kishindo kwa kuilaza wageni wenzsao wa ligi hiyo Stand United kwa mabao 4-1 kabla ya kubainika kumbe ilikuwa nguvu ya soda kwa kugawa pointi hata nyumbani, huku wakielekea kuvaana na Azam katika mechi ijayo ambayo inatarajiwa kuwa kali na yenye upinzani.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo, uongozi umeona ni vema kusitisha mkataba na kocha huyo licha ya kumshukuru kwa mchango wake na wanafanya mipango ya kusaka kocha mwingine ambaye ataipeleka mbali zaidi klabu hiyo.

Simba, Yanga wavuna zaidi ya Shs.Milioni 400

PAMBANO la watani wa jadi wa soka nchini Yanga na Simba lililochezwa juzi (Oktoba 18 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeingiza sh. 427,271,000.
Washabiki 49,542 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo ambapo viingilio vilikuwa sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 20,000 na sh. 30,000. Asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 65,176,932 wakati asilimia 5 ya gharama ya tiketi kwa CRDB ni sh. 21,363,550.
Kwa upande wa Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) ambayo ni sh. 1,000 kwa kila tiketi, timu mwenyeji Yanga imepata sh. 17,339,700, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 7,431,300 na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) sh. 24,771,000.
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni Uwanja sh. 43,678,277.67, gharama za mchezo sh. 24,751,024.01, Bodi ya Ligi sh. 23,295,081.42, TFF sh. 17,471,311.07, DRFA sh. 10,191,598.12, timu mwenyeji Yanga sh. 100,460,038.64 na timu ngeni Simba sh. 71,341,186.86.

TFF, Klabu zakutana kuteta kuboresha Soka

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) wamekutana mwishoni mwa wiki na kujadili masuala mbalimbali ya kuboresha maendeleo ya mchezo huo nchini.
Mkutano huo uliofanyika Dar es Salaam uliongozwa na Rais wa TFF, Jamal Malinzi na kuhudhuriwa na wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF pamoja na wanyeviti wa klabu za VPL.
Masuala yaliyozungumzwa ni leseni za klabu (club licensing), maboresho ya Taifa Stars, Kanuni za Ligi Kuu, Kombe la FA (Shirikisho) na mchango wa klabu hizo katika kuendeleza mpira wa miguu kwa vijana.
Uwasilishaji katika mkutano huo kuhusu maboresho ya Taifa Stars ulifanywa na Kocha Mkuu wa timu hiyo Mart Nooij wakati leseni kwa klabu ulifanywa na Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF, Boniface Wambura.
Kuhusu Kombe la FA, klabu zilifahamishwa kuwa mazungumzo kati ya TFF na mdhamini yanaendelea, ambapo zilikaribisha wazo hilo kwa vile michuano hiyo itatoa fursa kwa timu zao kucheza mechi nyingi za mashindano, hivyo kutoa nafasi ya kucheza kwa wachezaji wengi zaidi.
Bingwa wa michuano ya FA ndiye atakayeiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.
Rais Malinzi aliziomba klabu kukutana na kuwasilisha mapendekezo yao ya jinsi ya kuchangia/kuboresha maendeleo ya mpira wa miguu kwa vijana, kuboresha Kanuni za Ligi Kuu na kuboresha Kanuni za Bodi ya Ligi ili yaweze kufanyiwa kazi

Polisi yaua wanayedai kuwa ni 'Mlipuaji' mabomu ya Arusha

HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Jeshi la polisi mkoani Arusha limemuua kwa kumpiga risasi mtu wanayedai kuwa ni mtuhumiwa namba moja wa milipuko ya mabomu katika mikusanyiko na mmwagiajie tindikali viongozi wa kidini.
Inaelezwa kuwa mtuhumiwa huyo aliuwawa kwa risasi wakati akijaribu kutoroka akiwa chini ya ulinzi akiwa njiani kuelekea Kondoa, Dodoma kuonyesha bomu alilokuwa amelificha maeneo hayo.
Taarifa zinamtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Yahya Hassan Omar na Polisi wamedai ndiye aliyekuwa mtuhumiwa namba moja wa kesi ya ulipuaji mabomu jijini Arusha, akiwa amewahi kukiri mwenyewe kuhusiana na matukio hayo.

Mada Maugo, Nyilawila wapigwa KO za Hatari Russia

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiBcwlX3-lyDkZhobrSthUDTyr1mGFUNxkqFjKh3n7cgksSBo3UVI63lUcKYQKrRGf8TYKIMMFzCnbOmWQApSTlFQimrbHokODaKYmqjoFNezsa2MiV6IQVOgLDwuQsf5Z-ef3R6aOxplhO/s1600/maugo.JPG
Mada Maugo aliyekung'utwa Ko ya raundi ya 5
http://www.ibn-tv.com/wp-content/uploads/2012/02/Nyilawila.jpg
Karama Nyilawila aliyepigwa KO ya raundi ya 6
http://api.ning.com/files/R3T6T9I24RSa6NUyNcEyQXNbk7D*VkxN7XK3Lq5FfN0guD9GCvxKmjrOjcP0cQz19llJSudNgL3Rw5InTNIeIfQqBUpr0E0h/RamdhaniShauri.jpg
Ramadhani Shauri aliyepigwa KO ya raundi ya kwanza
MABONDIA kutoka Tanzania wamendelea kuwa wanyonge wanapoenda kucheza nje ya Tanzanioa baada ya Mada Maugo, Ramadhani Shauri na Karama Nyilawila wamejikuta wakiendeleza 'aibu' kwa kupigwa kwa KO kila mmoja nchini Russia mwishoni mwa wiki.
Mabondia hao walikumbana na vipigo hivyo katika michezo yao ya kimataifa ya kuwania mataji ya Dunia ya UBO na WBC iliyochezwa siku ya Jumamosi kwenye ukumbi wa Express, mjini Rostov-na-Donu nchini Russia.
Bondia Mada Maugo aliyekuwa akiwania ubingwa wa Dunia wa UBO katika uzani wa Middle dhidi ya Aliklych Kanbolatov wa Russia na kupigwa kwa KO ya raundi ya tano kati ya 12 alizokuwa akipigane.
Maugo alipigwa katika pambano lililofanyika kwenye ukumbi wa Express, katika mji wa Rostov-na-Donu, kuwania taji hilo lililokuwa wazi, ukumbi ambao pia ulishuhudia wenzake wawili wakipigwa.
Bondia Ramadhani Shauri aliyekuwa akiwania ubingwa wa Mabara Dunia wa WBC kwa Vijana alipigwa na Viskhan Murzabekov kwa KO ya raundi ya kwanza kati ya 12 za pambano hilo la uzani wa Welter.
Kama ilivyokuwa kwa watanzania hao wawili, pia Karama Nyilawila alikumbana na kipigo cha KO ya raundi ya sita ya pambano la raundi 12 dhidi ya Varazdat Chernikov.
Bingwa huyo wa zamani wa WBF alikuwa akiwania taji la Mabara la UBO la uzito wa Super Middle lililokuwa pia wazi na kuendeleza rekodi za mabondia wa Tanzania kushindwa kutamba nje ya nchi.

Wiki 2 ngumu kwa Simba na Yanga VPL, kipimo cha Maximo, Phiri

Simba na Yanga zilipokuatana zenyewe siku ya Jumamosi na kushindwa kutambiana uwanja wa Taifa
Makipa wa Simba na Yanga, Peter Manyika na Deo Munishi 'Dida' wakipongezana
Kazi tumeimaliza kati yetu sasa tuangalie mechi zetu zijazo, makocha Marcio Maximo na Patrick Phiri wakisalimiana
BAADA ya kumalizana wenyewe kwa wenyewe, Watani wa Jadi wa Soka Tanzania, Simba na Yanga zinaanza wiki mbili ngumu kwao katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara wakati wakatapokabiliwa na mechi ngumu ambazo zinaweza kubadili muelekeo wa klabu hizo.
Yanga wanaokamata nafasi ya nne kwa sasa katika msimamo itakuwa na mechi ngumu mbili mfululizo kuanzia Jumamosi hii kwa kuumana na Stand United mjini Shinyanga kabla ya kuvaana tena na Kagera Sugar ambao wamekuwa wakiwatesa mara kadhaa wakiwafuata uwanja wa Kaitaba.
Iwapo Yanga itashinda mechi hizo za ugenini au kumaliza salama bila kupoteza itakuwa imevuka kikwazo cha mbio zake za ubingwa msimu huu.
Stand United licha ya kuwa ni timu ngeni katika ligi baada ya kupata msimu huu, lakini haitabiriki kwani iliwabania Simba uwanja wa Taifa kwa kutoka nao sare ya 1-1, kadhalika Kagera Sugar haitabiriki kabisa.
Wakati Yanga wakiwa na kibarua hicho, watani zao wenyewe wataanza wiki hii kwa kucheza ugenini kama Yanga kwa kuwafuata Prisons-Mbeya ambayo imekuwa ikisumbua kwenye uwanja wa Sokoine.
Baada ya kibarua hicho Simba itasafiri hadi Morogoro kuwafuata Mtibwa Sugar ambao wamekuwa wakiwajeruhi kwenye uwanja wa Jamhuri kila wakikutana.
Simba yenye pointi nne kama Prisons haijaonja ushindi katika ligi ya msimu huu, hivyo watakuwa na kazi ngumu kuhakikisha wanavunja mwiko wa kucheza mechi 10 za ligi tangu msimu uliopita bila kushinda.
Hata hivyo tayari benchi la ufundi na viongozi wa klabu hiyo ya Msimbazi imekuwa ikisisitiza kuwa mambo yanaelekea kutengemaa na kwamba mashabiki wao watarajie faraja ya kuonja ushindi katika mechi zijazo
Baada ya mechi za mwishoni mwa wiki MICHARAZO inakuletea msimamo kamili wa sasa wa ligi hiyo sambamba na mechi zitakazofuata katika ligi hiyo inayozidi kuchanja mbuga.

MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                              P   W    D    L    F    A   GD   Pts
01. Azam               04  03  01  00  06  01  +5   10
02. Mtibwa Sugar   04  03  01  00  06  01  +5   10
03.Coastal Union    04  02  01  01  06  04  02    07
04.Yanga                04  02   01  01  04  04  00   07
05. Kagera Sugar   04  01  02   01  03  02 +1   05
06. Mbeya City       04  01  02  01  01   01  00   05
07.Stand Utd         04  01  02   01  03   05  -2   05
08.Prisons             04  01  01   02  04   04  00   04
09.Simba               04  00  04   00  04    04  00  04
10. JKT Ruvu         04  01  01  02   03   05   -2  04
11. Ruvu Shooting 04  01  01   02  03   05   -2  04
12. Ndanda Fc       04  01  00   03  07    09  -2  03
13. Polisi Moro       04  00  03  01   03    05   -2  03
14. Mgambo JKT    04  01  00  03   01    04  -3  03
RATIBA

Okt 25, 2004
Stand United v Yanga (Kambarage-Shinyanga)
Azam  v JKT Ruvu (Chamazi-Dar es Salaam)
Prisons-Mbeya vs Simba (Sokoine-Mbeya)
Ndanda v Mgambo JKT (Nangwanda Sijaona-Mtwara)
Kagera Sugar v Coastal Union (Kaitaba-Bukoba)
Ruvu Shooting v Polisi Moro (Mabatini-Mlandizi)

Okt 26, 2014
Mbeya City v Mtibwa Sugar (Sokoine-Mbeya)
 

Nov 1, 2014 
Kagera Sugar v Yanga (Kaitaba-Bukoba)
Coastal Union v Ruvu Shooting (Mkwakwani-Tanga)
JKT Ruvu vs Polisi Moro (Chamazi-Dar es Salaam)
Ndanda Fc Azam (Nangwanda Sijaona-Mtwara)
Stand Utd v Prisons-Mbeya (Kambarage-Shinyanga)
Mtibwa Sugar v Simba (Jamhuri-Morogoro)
 

Nov 2, 2014
Mgambo JKT vs Mbeya City (Mkwakwani-Tanga)

Juve yang'ang'aniwa, AC Milan ikishinda ugenini Italia

http://forzaitalianfootball.com/wp-content/uploads/2014/10/Honda-Hellas-Verona-v-AC-Milan.jpg
Kaisuke Honda kipongeza na wachezaji wenzake wa Ac MIlan baada ya kuifungia timu yake mabao mawili jana
http://hoofoot.com/images/pics/5320.jpg
http://images.cdn.fourfourtwo.com/sites/fourfourtwo.com/files/styles/main-image-landscape-small/public/paulpogba_vk8n8jqtapnz173kuqh1is5x3.jpg?itok=9INmTWtt
Paul Pogba aliyeifungia Juventus bao lililowapa pointi moja ugenini baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 dhidi ya Sassuolo
MABINGWA watetezi wa Serie A, Juventus iking'ang'aniwa ugenini na Sassuolo kwa kulazimishwa sare ya 1-1, AC Milan imeendeleza libeneke kwa kupata ushindi wa pili mfululizo katika ligi hiyo wakiwa ugenini na kuwapandisha hadi kwenye nafasi ya Nne.
Milan wanaonolewa na Phillip Inzaghi 'Pippo' ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Hellas Verona na kuwafanya wafikishe pointi 14, tano pungufu na ilizonazo Juventus iliyolazimishwa sare  siku ya Jumamosi.
Mabao ya washindi katika mchezo huo yalifungwa na Raphael Marques aliyejifunga katika dakika ya 21 wakati akiwa katika harakati za kuokoa shambulizi la Milan, kabla ya Kaisuke Honda kufunga mabao mawili dakika ya 27 na 56 na wenyeji kupata la kufutia machozi dakika tatu kabla ya pambano hilo kumalizika kupoita kwa Lopez.
Katika mechi nyingine za Ligi ya Serie A kwa siku ya jana Fiorentina ilikubali kukung'utwa nyumbani mabao 2-0 na Lazio, Atalanta ikatakata nyumbani kwa kushinda kiduchu kwa bao 1-0 dhidi ya Parma, huku Cagliari ililazimishwa sare ya 2-2 nyumbani na Sampdoria.
Palermo wakang'ara nyumbani kwa kuifumua Cesena kwa mabao 2-1, huku Udinese ikilala ugenini mbele ya wenyeji wao Torino kwa bao 1-0 na Inter Milan iking'ang'aniwa nyumbani kwa sare ya 2-2 na Napoli.
Ligi hiyo itaendelea tena kwa mchezo mmoja kati ya Genoa itakayoikaribisha Empoli.

Atletico Madrid yaendeleza rekodi Vicente Calderon, Barca yaua tena

Atletico Madrid
Wasiofungika nyumbani, Atletico Madrid wakishangilia moja ya mabao yao jana dhidi ya Espanol
WAKATI Barcelona wakiendeleza rekodi yake ya kutopoteza mchezo wowote atika La Liga, mabingwa watetezi, Atletico Madrid yenyewe imeendeleza rekodi yake ya kutokufungwa katika uwanja wake wa nyumbani wa Vincent Calderon katika Ligi hiyo.
Watetezi hao jana walipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi Espanol na kufikisha mechi ya 24 katika uwanjani huo bila kuonja kipigo.

Tiago Mendes aliiandikia timu yake bao la uongozi baada ya kupokea pasi ya Gabi Fernandez na kupiga kichwa mpira ulimshinda mlinda mlango Kiko Casilla.

Mabingwa hao walifanikiwa kuongeza bao la pili katika kipindi cha pili kupitia kwa Mario Suarez aliyeupata mpira wa kichwa ulipigwa na Gimenez kutoka katika eneo la kona.


Ushindi huu una maana kuwa kikosi cha Diego Simeone kinasalia na nyuma kwa alama tano dhidi ya Barcelona ambao walipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Elber kwa mabao ya Xavi, Neymar na Lionel Messi lakini wakikamata nafasi ya tano baada ya Sevilla kuopata ushindi ugenini wa mabao 2-0 dhidi ya Elche.
Timu hiyo Atletico itashuka tena dimba lake la nyumbani keshokutwa wakati watakapoikaribisha Malmo ya Sweden katika mchezo wa ligi ya mabingwa Ulaya mchezo wa kundi A.
Katika mechi nyingine za La Liga kwa wikiendi Córdoba ililala nyumbani kwa mabao 2-1 dhidi ya wageni wao Malaga, Deportivo La Coruna ikiwa nyumbani iliibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Valencia, huku Villarreal ikishinda nyumbani 2-0 dhidi ya Almeria na leo kutakuwa na pambano moja kati ya Real Sociedad itakayoikaribisha Getafe.

Mourinho 'amchongea' Wenger kwa FA

http://www.independent.co.uk/incoming/article9775470.ece/alternates/w620/Wenger-1.jpg
Makocha Jose Mourinho (kulia) na Arsene Wenger (kushoto) katika mzozo wao uliokaribia kuchapana makonde kabla ya kuamuliwa kama inavyoonekana pichani.
KOCHA wa Chelsea, Jose Mourinho anaamini kushindwa kwa Chama cha Soka cha Uingereza-FA kumuadhibu Arsene Wenger kwa kumsukuma kinawaacha katika hatia na kusisitiza kama ingekuwa yeye ndiye aliyefanya tukio hilo wangemuadhibu.
Kufuatia kuchezewa vibaya Alexis Sanchez na Gary Cahill wakati wa mchezo Chelsea walioshinda mabao 2-0 dhidi ya Arsenal mapema mwezi huu, Wenger alivamia eneo la Mourinho kulalamikia faulo hiyo na kumsukuma Mreno huyo wakati akimwambia arejee eneo lake. 
Akihojiwa Mourinho amesema ameshangazwa kwa Wenger kutoadhibiwa na FA kwa kitendo chake hicho kwani anaamini ingekuwa yeye lazima angechukuliwa hatua. 
Wenger mwenyewe tayari aliomba radhi kwa tukio hilo na kudai kuwa alichokuwa akilalamikia ni kuchezewa faulo mchezaji wake na sio vinginevyo.
Makocha hao wawili wamekuwa kwenye 'bifu' kwa muda mrefu hasa zinapokutana timu zao na wakati mwingine kupigana vijembe hata kama hawana mchezo wowote.

Liverpool yashinda ugenini, Stoke yaua, Man U kazi leo






KLABU ya Liverpool imepata ushindi wa kushangaza ugenini baada ya kuilaza QPR mabao 3-2, huku mabao yake mawili yakitokana na kujifungwa kwa mabeki wa timu wenyeji.
Vijana hao wa Brendan Rodgers, walianza kutangulia kufunga baada ya beki wa QPR Richard Dunne kujifunga katika dakika ya 67 kabla ya mtokea benchi  Vargas kuisawazishia wenyeji katika dakika ya 87 na kuongeza la pili dakika 90.
Hata hivyo Coutinho wa Liverpool aliiandika timu yake bao la pili na Steven Caulker akajifunga kwenye dakika za nyongeza na kuwapa LIverpool ushindi huo muhimu.
Katika pambano jingine la ligi hiyo timu ya Stoke City ikiwa nyumbani iliinyoosha Swansea City kwa kuilaza mabao 2-1. Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea leo Jumatatu wakati Manchester United wastakapokuwa ugenini kuwakabiliWest Bromwich Albion kusaka pointi tatu zitakazowaingiza kwenye Nne Bora kwa mara ya kwanza msimu huu.

JKT Ruvu watuma Salamu kwa Azam, yaibanjua Prisons

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiOCmvYXNhX3tkdKNCPqKEV5L44ICPCwveet-N3cYUzti1f903gJ0gVDWtA8IlIXpjSRIequIstXGUXd_w4PZtEiTpSyCnPo9nwdW1tplM_O34AZiGAmJATZNAMMaszczARYCeLEGBIpshM/s1600/1.jpg
Kikosi cha JKT Ruvu
TIMU ya maafande wa JKT Ruvu wamefuata 'nyayo' za ndugu zao Ruvu Shooting kwa kupata ushindi wao wa kwanza katika msimu huu uwanja wa ugenini dhidi ya Prisons-Mbeya na kuonekana kama wanatuma salamu za mapema kwa Azam watakaokutana nao mechi ijayo jijini Dar.
Ruvu Shooting walipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Ndanda Fc Jumamosi kwenye uwanja wa Nangwanda Sijaona, mjini Mtwara na JKT walipata ushindi wao wa mabao 2-1 Jumapili kwenye uwanja wa Sokoine Mbeya.
Mafaande hao wanaonolewa na kocha Fred Minziro walipata ushindi huo wa kwanza kwao baada ya kuanza msimu kwa sare ya bila kufunga dhidi ya Mbeya City, kisha kupoteza mara mbili mfululizo dhidi ya Kagera Sugar na Yanga.
Mabao ya washindi katika mchezo huo ambao Kocha David Mwamaja ameelekeza lawama zake kwa kipa wake, Benno Kakolanya yalifungwa na Najim Magulu na Jabir Aziz wakati la wenyeji liliwekwa kimiani na Amri Omary.
Kwa ushindi huo JKT Ruvu wameondoka mkiani kwa kufikisha pointi nne kawa Ruvu Shooting, isipokuwa wenyewe JKT wanatangulia mbele kwa sababu ya herufi ili wakifunga kila kitu wakiwa nafasi ya 10.
Mgambo JKT kwa sasa ndiyo wanaokamata mkia wa ligi hiyo kwa kuwa na idadi ndogo ya mabao ya kufungwa licha ya kuwa na pointi tatu sawa na timu za Ndanda na Polisi Morogoro wanaofuatana nao mkiani.
Mechi ijayo kwa JKT Ruvu itakuwa uwanja wa Chamazi jijini Dar kuumana na mabingwa watetezi Azam ambayo ipo kileleni mwa msimamo kwa sasa kwa kubebwa na Herufi licha ya kuwa sawa kwa kila kitu na Mtibwa Sugar.
Mara kadhaa Azam imekuwa ikiiotea JKT Ruvu hali inayofanya pambano lijalo kushindwa kutabirika baada ya JKT Ruvu chini na Minziro kuonekana kuanza kuamka tofauti na ilivyoanza, huku pia kikosi chao msimu huu kikiimarishwa na nyota kadhaa waliowahi kukipiga Simba, Yanga na Azam wenyewe kama Jabir Aziz, Jackson Chove na Haruna Shamte aliyekuwa nahodha msaidizi wa Simba msimu uliopita..

Saturday, October 18, 2014

Real Madrid yatuma salamu Liverpool, yaua 5-0 Ronaldo afunga 2

James Rodriguez
'Wauaji' wengine wa Real Madrid leo ni hawa watatu
Cristiano Ronaldo
Ronaldo akishangilia mabao yake
MWANASOKA Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo ameendelea kutupia mabao kambani baada ya jioni ya leo kufunga mabao mawili wakati Real Madrid wakipata ushindi mnono ugenini dhidi ya Levante kwenye Ligi Kuu ya Hispania, La Liga.
Ronaldo aliyefikisha mabao 15 katika mechi  ya nane, alianza kuaiandikia wageni bao kwa mkwaju wa penati dakika ya 13 baada ya Juanfran kufanyiwa madhambi na Javier Hernandez 'Chicharito' kufunga bao la pili katika dakika ya 38 akimalizia kazi nzuri ya James Rodriguez 'James Bond' .
Ronaldo alirudi tena kambani katika dakika ya 61 kwa kuaindikia Real Madrid bao la tatu akimalizia kazi ya Isco na James Bond akafunga bao la nne dakika ya 66 kwa kazi nzuri ya Ton Kroos na isco akamalizia kazi kwa kufunga bao la tano dakika nane kabla ya pambano hilo kumalizika kwa pande la Chicharito.
Ushindi huo wa Madrid uliowafanya wapunguze pengo la pointi na vinara Barcelona ni kama salamu kwa wapinzani wao wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Liverpool ya England watakaoumana nao siku ya Jumatano.
Katika mechi nyingine Athletic Bilbao ikiwa nyumbani ililazimishwa sare ya 1-1 dhidi ya Celta Vigo na kwa sasa Barcelona wapo nyumbani wakiumana na Elber na m atokeo bado ni 0-0.

Bayern yazidi kuchinja Bundesliga yapiga mtu 6-0

Mario GotzeMABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Ujerumani, Bayern MUnich wamezidi kuimarisha uongozi wao kwa kuibamiza bila huruma Werder Bremen kwa mabao 6-0.
Phillip Lahm na Mario Gotze walifunga mara mbili, huku Xabi Alonso na  Thomas Muller wakimalizia udhia kwa kuwekwa mingine kimiani na kuifanya vijana wa Pep Guardiola kufikisha pointi 20 baada ya michezo nane ya ligi hiyo maarufu kama Bundesliga.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Mainz 05 ikiwa nyumbani iliitambia     Augsburg kwa mabao 2-1, Hannover 96 ikalala nyumbani kwa mabao 3-0 dhidi ya Borussia Mönchengladbach, huku Freiburg  nao wakilala nyumbani 2-1 kwa Wolfsburg.
Timu za  Stuttgart na Bayer Leverkusen zilitoshana nguvu kwa kufungana mabao 3-3, huku FC Koln ikishinda nyumbani 2-1 dhidi ya Borussia Dortmund na hivi punde Schalke 04 ikiwa nyumbani iliitambia Hertha Berlin kwa mabao 2-0.

AS Roma yaua Italia, kibabu Totti afunga

http://www2.pictures.zimbio.com/gi/Roma+v+AC+Chievo+Verona+Serie+97hI1zc0UGix.jpg
AS Roma ikiwa uwanja wa nyumbani wameibuka na ushindi wa mabao 3-0, huku mkongwe Francisco Totti akifunga moja ya mabao hayo na kuzidi kuweka rekodi katika Seria A.
Mabao ya washindi yaliwekwa kimiani na Destro katika dakika ya nne,  Ljajić dakika ya  25'na Totti  aliyefunga kwa penati dakika ya 33.

Newcastle United yaona Mwezi England

Gabriel Obertan
Raha ya ushindi kwa Newcastle United
KLABU ya Newcastle United baada ya kushindwa kupata ushindi wowote katika Ligi Kuu ya England tangu Agosti 30 imezinduka kwa kuichapa Leicester City kwa bao 1-0 katika mechi iliyomaliza hivi punde.
Bao pekee lililotoa afueni kwa timu hiyo iliyokuwa nyumbani lilifungwa na Gabriel Obartan katika dakika ya 71 akimalizia kazi nzuri ya Demba Pappis Cisse na kuifanya timu hiyo kufikisha jumla ya saba japo imeshindwa kuchomoka kwenye eneo la hatari la kushuka daraja.

Huu ndiyo msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjtlvkjDhSlS65-hB-004rsYZJHQE4NobZV403ZyTd0wOSg5y8GsHbLgtIjZMhi54tknwwuuTLLETjNKtUeQgg2XaPMUfzGeIx26H3KEFoxiV0ynG2zxCXwoN3Ms2Tsy19Go4NbKzuhAyk/s1600/HMB_3985.JPG
Coastal Union iliyowaengua Yanga kwenye nafasi ya tatu
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjN3yUookRbw5iagyyNOdXVC2x3bCSKEWnMyE3CdD3ClDJbjRMBjlm46wOFkf2vG3QxuVrysM_bG3S082zNzQ77EZ7WFu1gUXfcaatYEYOkE9Hswh57h_eXGh1G5kvKN9Zq5YUG22jzhdM/s1600/YAA.jpg
Yanga waliosimamishwa na Simbaa
Mbeya waliokubali kipigo cha pili nyumbani dhidi ya Azam
MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                            P   W    D    L    F    A   GD   Pts
01. Azam              04  03  01  00  06  01  +5   10
02. Mtibwa Sugar  04  03  01  00  06  01  +5   10
03.Coastal Union   04  02  01  01  06  04   02   07
04.Yanga              04  02  01  01  04  04   00  07
05. Kagera Sugar  04  01  02   01  03  02  +1   05
06. Mbeya City      04  01  02  01  01   01  00   05
07.Stand Utd        04  01  02   01  03   05  -2   05
08.Prisons            03  01  01   01  03   02  +1   04
09.Simba              04  00  04   00  04    04  00  04
10. Ruvu Shooting 04  01  01   02  03   05   -2  04
11. Ndanda Fc       04  01  00   03  07    09  -2  03
12. Polisi Moro       04  00  03  01   03    05   -2  03
13. Mgambo JKT    04  01  00  03   01    04  -3  03
14.JKT Ruvu          03  00  01  02   01   04   -3  01

Wafungaji Bora:
4-
Didier Kavumbagu(Azam)
3-
Ally Shomari (Mtibwa)
2- Shaaban Kisiga (Simba), Nassor Kapama (Ndanda), Ame Ally (Mtibwa), Rashind Mandawa (Kagera), Rama Salum (Coastal), Aggrey Morris (Azam)


Ratiba:
Kesho JUMAPILI
Prisons-Mbeya vs JKT Ruvu

Arsenal chupuchupu, Chelsea yaua, Southampton nouma

Arsenal walipotungulia mapema mabao kabla ya kuyarejesha
Alexis Sanchez (kushoto) akipongezwa kwa kufunga bao la kuongoza la Arsenal
Cesc Fabregas akishangilia bao lake wakati Chelsea wakishinda ugenini
Southampton celebrate
Southampton wakishangilia karamu yao ya mabao
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiJ8gVj4IzJtst16bFSW_FamQning4RDHnfQOlk3S1lv7CaHgAJvnfydlnLb1oqRZ8Y_RYiOcVgXAYzeQqhG40uG3ylSssbREGAk_Z23vGsZQkGAT29YghLNR-XJbx03NmjYbznx1efM9g/s1600/1413638977348_Image_galleryImage_Manchester_City_s_Argenti.JPG
Kun Aguero akishangilia moja ya mabao yake manne mapema leo walipoiua Spurs
MSHAMBULIAJI Danny Welbeck ameendelea kuonyesha jinsi gani alivyo muhimu ndani ya Arsenal baada ya kuifungia timu hiyo bao katika dakika za lala salama na kuwaepushia wapiga mtutu hao wa Emirates kuambulia sare ya mabao 2-2 ikiwa nyumbani dhidi ya Hull City.
Welbeck aliyekuwa hapewi umuhimu wowote katika kikosi cha Manchester United na hivyo kuuzwa kwa Arsenal, alifunga bao hilo dakika za nyongeza kabla ya pambano kumalizika na kumpa nafuu meneja wake, Arsene Wenger.
Mshambuliaji huyo nyota wa England alifunga bao hilo akimalizia kazi nzuri iliyofanywa na Alexis Sanchez, ambaye alianza kuwafungia wenyeji  bao dakika ya 13 kwa kumalizia kazi ya Per Martesacker.
Wageni walifunga mabao yao katika dakika ya 17 kupitia Mohammed  Diamé kisha kuongeza la pili dakika chache baada ya kipindi cha pili kuanza kupitia kwa Abel Hernandez.
Katika mechi ya mapema leo, Sergio 'kun' Aguero aliisambaratisha Tottenham Hotspur waliowafuata nyumbani kwenye uwanja wa Etihad baa da ya kufunga mabao manne wakati wakiwazisha vijogoo hao wa London ya Kaskazini kwa mabao 4-1. Mabao mawili yakiwa kwa mikwaju ya Penati.
Chelsea ikiwa ugenini ilipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Crystal Palace kwa mabao ya Oscar aliyefunga dakika ya sita kabla ya Cesc Fabrages kuongeza la pili dakika ya 51 na Campbell akaipatia bao la kufutia machozi wanyeji katika dakika ya 90.
Nayo Southampton ikiwa nyumbani iliwasambatarisha Sunderland kwa kuwafunga mabao 8-0 ikiwa ni rekodi ya kipigo kikubwa katika msimu huu wa ligi ya England, huku    Burnley ikiwa nyumbani ilifumuliwa mabao 3-1 na West Ham United na Everton walishinda nyumbani kwa mabao 3-0 dhidi ya Aston Villa.
Ushindi wa Southmpton umeifanya timu hiyo kufikia rekodi mojawapo ya mechi iliyokuwa na ushindi mnono ikienda sambamba na mechi nyingine tano tangu Ligi Kuu ilipoanza kutumika rasmi 1992 toka daraja la kwanza nchini humo..
Mechi nyingine za awali ni;
Manchester United 9-0 Ipswich, March 1995
Newcastle United 8-0 Sheffield Wednesday, September 1999
Tottenham Hotspur 9-1 Wigan Athletic, November 2009
Chelsea 8-0 Wigan Athletic, May 2010
Chelsea 8-0 Aston Villa, December 2012
Southampton 8-0 Sunderland, October  2014

Simba, Yanga debe tupu, Azam yaua, Mtibwa yabanwa

Mpambano wa watani ulivyokuwa uwanja wa Taifa leo
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgnGI0Fa_A1fReGNq630wAe-HUeAeC3CnzyXNWI0OAPfBgI-aka3Ybg_uU2XVpZaMurdewSapeGfrEvocd18umDQjB5vFdhDmsHEVhTWCSFg3rp4vfk7e-UZaT1IRvH4QtZHSFcKp6a8H7v/s1600/Picha+Simba.JPGhttps://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgNPa5lzs3_DyhJWIBPQ4eR7PVVwEV7kBsmZgbFj2NkFWHudak-xT3RA29hwYq_es9UcaOF5fj0I9w9hmoY_GT4jyCWZ2zMxmOX1zN7vws4XBFeRVRUgqalCm9eoug3LZYGSjq7wMFA9_PP/s1600/Yanga+leo+1.JPGWAPINZANI wa jadi wa soka Tanzania, Simba na Yanga zimeshindwa kutambiana katika pambano lao lililochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa, licha ya tambo za mapema kabla ya mchezo huo, huku Azam wakijikwea kileleni mwa msimamo wakiipiku Mtibwa Sugar waliobanwa mjini Morogoro.
Simba na Yanga ambazo zilikamiana na kutambiana kwa wiki kadhaa sasa, walishindwa kufungana katika pambano lililoshuhudia mtoto wa nyota wa zamani wa Mtibwa, Yanga na Taifa Stars, Manyika Peter, kipa Peter Manyika Jr aking;ara kwa kuinyima Yanga mabao kwenye uwanja huop wa Taifa.
Timu zote ilifanya kosa kosa za hapa na pale na has akwenye kipindi cha pili huku makocha wao, Marcio Maximo wa Yanga na Patrick Phiri wa Simba wakifanya mabadiliko ya wachezaji bila kuleta tija hadi dakika 90 za pambano lililochezeshwa vema na mwamuzi Israel Mujuni Nkongo.
Kwa matokeo hayo Yanga imefikisha pointi 7 na kushuka hadi nafasi ya nne wakiwapisha Coastal Union kukalia nafasi hiyo baada ya jioni ya leo kushinda mabao 2-0 dhidi ya Mgambo na kufikisha idadi kama hiyo ya pointi ila ikiwa na uwiano tofauti ya mabao, huku watani zao hiyo ikiwa ni sare yao ya nne msimu huu na ikifikisha mechi ya 10 katika ligi bila kuonja ushindi imefikisha pointi nne.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Azam waliwafyatua Mbeya City nyumbani kwao kwenye uwanja wa Sokoine kwa bao 1-0 na kufikisha idadi ya mechi 38 bila kupoteza katika Ligi Kuu..
Bao hilo liliwekwa kimiani na beki wake wa kati, Aggrey Morris kwa mkwaju wa adhabu kwenye dakika ya 19 na kuifanya mabingwa watetezi hao kukwea kileleni wakifikisha pointi 10 sawa na Mtibwa Sugar ambao walilazlmishwa suluhu mjini Morogoro na ndugu zao Polisi Moro kwenye uwanja wa Jamhuri.
Azam na Mtibwa zote zimefungana idadi ya pointi zikiwa na 10 kila moja, huku wakiwa na mabao sita kila moja na kufungwa moja, isipokuwa kiherufi Azam inawatangulia Wakata Miwa.
Kutoka Mkwakwani Tanga, Coastal Union imezidi kujiongezea pointi baada ya kuilaza Mgambo JKT kwa mabao 2-0.
Mabao ya washindi yalifungwa na Rama Salim kwa mkwaju wa penati kabla ya Kennedy Masumbuko kuongeleza la pili kwenye kipindi cha pili.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEheu2S3fe_9FoFd7hnk3AwEiXmoOP2ulk9Y13fiRJl12EdBwVuaIaC0y1ulilytUphp2lKiDBXt3tJkB_gfKPzweV4tFKqdIhBe-kGqjPOH6NhkBOCD0sjIxEJ00LhbAeNd57i_xQ_Yrxkh/s1600/20140913_160438.jpg
Ndanda waliopigwa nyumbani na Ruvu Shooting

Nayo timu ya Ruvu Shooting wakiwa ugenini mjini Mtwara wamewatoa nishai wenyeji wao Ndanda Fc kwa kuwalaza mabao 3-1, mabao ya washindi yakiwekwa kimiani na Juma Nade, Abdurahman Mussa na Mathew. ilihali Kagera Sugar wakiwa nyumbani wamelazimishwa suluhu ya kutofungana na Stand United.
Ruvu waliovunja mwiko wa kutofunga bao lolote katika ligi ya msimu huu kwa kuilaza Ndanda mabao 3-1
Mtibwa iliyobanwa mbavu na Polisi na kutoka suluhu

Chelsea katika kibarua kizito England

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/03008/Chelsea4_3008183b.jpgVINARA wa Ligi Kuu ya England, Chelsea wataelekea kwa wapinzani wao jijini London Crystal Palace Jumamosi wakilenga kupanua mwanya wa alama tano walioweka kileleni mwa Ligi hiyo baada ya mapumziko ya kimataifa.
Palace walishangaza Chelsea, na klabu nyingine katika ligi, kwa kushinda dhidi ya Chelsea msimu uliopita na nahodha wa Blues John Terry amepuuzia mbali madai kwamba tayari mshindi wa ligi msimu huu amejulikana.
“Ni wazi (kwamba kinyang’anyiro cha ligi) hakijaisha,” amesema Mourinho.
“Klabu nyingine zimejipata katika nafasi kama hii. Ni vyema kuongoza lakini ukiwa juu, kila mtu hutaka kukuangusha.
“Hilo ndilo jambo zuri kuhusu Ligi ya Premia na ndio maana kila mtu huipenda. Timu zinalenga kutushambulia kwa sababu tuko juu na twacheza vyema.”
Mabingwa watetezi Manchester City, walio wa pili kwa sasa, watakuwa nyumbani dhidi ya Tottenham Hotspur na kiungo wa kati anayeichezea City kwa mkopo Frank Lampard amewaambia wachezaji wenzake wajihadhari dhidi ya Spur ambao wameanza kuamka.
“Huenda wanapitia kipindi cha mpito lakini nilifurahishwa sana na meneja wao (Mauricio Pochettino) alipokuwa Southampton na ikiwa anaweza kufanya hayo Tottenham, ambao bila shaka wana vipaji kwenye kikosi chao, watafana. Ni timu nzuri sana.”