STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 7, 2013

Juventus, PSG nazo zapenya robo fainali Ulaya



KIkosi cha Juve kilichopenya robo fainali Ligi ya Ulaya
  
MABINGWA wa Italia Juventus jana walifanikiwa kuingia robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuilaza Celtic mabao 2-0 na kufuzu kwa jumla ya mabao 5-0, huku PSG ya Ufaransa nayo ikipenya hatua hiyo kwa sare ya 1-1.
Juventus iliyokuwa uwanja wake wa nyumbani mjini Turin, ilipata mabao yake katika kila kipindi bao la kwanza likifungwa dakika ya 24 na Alessandro Matri na kufanya hadi mapumziko matokeo yawe 1-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kushambuliana, lakini ni Juventus walioendelea kutamba kwa kujipatia bao la pili lilitumbukizwa kimiani na Fabio Quagiarella.
Katika mechi nyingine iliyochezwa jana usiku, PSG ilifanikiwa kuungana na timu za Real Madrid, Borrusia Dotmund na Juventus hatua ya robo fainali baada ya kulazimishwa sare kwenye uwanja wake wa nyumbani na Valencia ya Hispania.
Hadi mapumziko timu hizo mbili zilikuwa nguvu sawa kwa kutofungana licha ya kushambiuliana na kufaya kosa kosa kadhaa.
Kipindi cha pili kilianza kwa Jonas wa Valencia kuipatia wageni bao la kuungoza katika dakika ya 55 na kuwafanya wenyeji kucharuka wakisaka bao.
Juhudi zao zilikuja kufanilkiwa katika dakika ya 66 kupitia nyota wake, Ezequiel Lavezzi na kuifanya timu hiyo iliyomchezesha nyota wa zamani wa England, David Beckham kusonga mbele kwa jumla ya mabao 3-2 baada ya mechi ya awali kumalizika kwa PSG kushinda mabao 2-1 ugenini.

Kagera Sugar, JKT Ruvu vitani leo Chamazi

Kikosi cha JKT Ruvu

Kikosi cha Kagera Sugar


BAADA ya kupoteza mechi yake ya mwisho dhidi ya Yanga, timu ya Kagera Sugar jioni ya leo itashuka dimbani kujaribu bahati yake kwa kuumana na maafande wa JKT Ruvu katika mechi ya mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Kagera wanaonolewa na nyota wa zamani wa Simba, King Abdallah Kibadeni na Mrange Kabange wakavaana na vijana wa winga wa zamani wa Yanga, Charles Kilinda ambao mechi yao ya mwisho walipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Toto Afrika.
Kila upande umejinafasi kufanya vema katika poambano hilo la leo litakjalochezwa kwenye uwanja wa Chamazi, nje kidogo ya Dar es Salaam.
Kibadeni alisema kiu yao ni kusaka pointi muhimu ugenini kabla ya kurejea nyumbani kwao Kagera kwa mechi nyingine zijazo.
Kocha huyo alisema kikosi chake kipo tayari kwa pambano hilo na ana imani kubwa ya kupata ushindi licha ya kukiri pambano litakuwa gumu kwa vile JKT Ruvu sio timu ya kubeza hasa ikizingatiwa msimuu huu hawajawa na matokeo ya kuvutia kama misimu miwili iliyopita.
Kwa upande wa JKT Ruvu baadhi ya nyota wake wamedai kama walivyofanya kwa Toto ndiyo itakavyokuwa kwa Kagera katika mechi hiyo kwa nia ya kuipa timu yao ushindi na kuondoka eneo la mkiani wanakochuana na timu nyingine tatu kuwania kuepuka kushuka daraja.
 

Mtibwa yatakata yazikamata Simba, Coastal Union

Kocha wa Mtibwa, Mecky Mexime

BAO lililofungwa dakika za lala salama kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga, imeiwezesha mabingwa wa zamani wa soika nchini, Mtibwa Sugar kuzikamata timu za Simba na Coastal Union kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Mtibwa iliibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mgambo JKT na kuifanya ifikishe jumla ya poiinti 31 sawa na wapinzani wake hao watakaovaana Jumapili jijini Dar japo wabakia nafasi tano.
Bao hilo pekee la Mtibwa lilifungwa na 'muuaji' wa Simba, Salvatory Ntebe katika dakika ya 90 na kuwafanya vijana wa Mecky Mexime kupumua baada ya kuanza duru la pili vibaya.
Katika mechi nyingine zilizochezwa jana kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid wenyeji JKT Oljoro iliibuka na ushindi wa bao 1-0 lililofungwa katika kipindi cha pili na Paul Nonga na kuilaza Prisons ya Mbeya ambapo kocha wake Jumanne Chale alilalamikia mchezo huo.
Kocha huyo alidai wenyeji walibebwa kutokana na kukataliwa bao lao safi lililofungwa na mchezaji wake, huku akidai kulikuwa na maamuzi yasiyomvutia kwenye pambano hilo.
Nao maafande wa Ruvu Shooting ya Pwani waliendelea kuizamisha Aficna Lyon kwa kuilaza baio 1-0 na kuifanya timu hiyo kubakia mkiani mwa msimamo wa lihi hiyo itakayoendelea tena leo.
Bao lililoiweka pabaya Lyon katika kuwepo kwake katika Ligi Kuu msimu ujao lilifungwa na Abdulrahman Mussa katika dakika ya 29 katika mechi kali iliyochezwa kwenye uwanja wa Chamazi, jijini Dar.

TFF yabanwa na serikali, hofu yatanda


Waziri Dk Mukangara

WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara ameliagiza Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuhakikisha kuwa linaitisha uchaguzi wake mkuu kabla ya Mei 25 mwaka huu; amri ambayo inazidi kuiweka Tanzania katika hatari ya kufungiwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) ambalo haliruhusu masuala ya soka kuingiliwa na serikali.
Amri hiyo ni moja kati ya maagizo matatu yaliyotolewa na serikali katika kikao cha pamoja kilichofanyika jana baina ya viongozi wa wizara, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na TFF.
Kikao hicho kilichofanyika jana asubuhi badala ya leo kama TFF walivyokuwa wameomba katika barua yao ya Jumatatu Februari 4 kilihudhuriwa na Dk. Mukangara, naibu wake Amos Makalla, katibu mkuu wa wizara Seth Kamuhanda, mkurugenzi wa michezo Leonard Thadeo, mwenyekiti wa BMT, Dioniz Malinzi na katibu wa BMT, Henry Lihaya.
TFF iliwakilishwa na katibu mkuu Angetile Osiah, mjumbe wa kamati ya utendaji Alex Mgongolwa na mkurugenzi wa ufundi, Sunday Kayuni.
Baada ya kikao hicho, Dk. Mukangara aliwaambia waandishi wa habari kuwa amewaandikia barua TFF kuwapa maagizo matatu aliyoyataja kuwa ni; kuhakikisha shirikisho hilo la soka linatangaza hadharani kuwa limekubaliana na maelekezo yaliyotolewa na wizara na kwamba tamko hilo litolewe kabla ya Machi 11 mwaka huu.
Barua hiyo ambayo ilionwa nakala yake jana imeitaka TFF katika agizo la pili kuitisha mkutano mkuu wa marekebisho ya katiba ndani ya siku 40 kuanzia jana (kabla ya Aprili 15, 2013).
Katika agizo la tatu, serikali imeitaka TFF iitishe mkutano mkuu kwa kuzingatia katiba ya mwaka 2006 na kwamba, kwenye mkutano huo wajumbe wapitishe marekebisho yaliyofanywa hadi mwaka 2008.
Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alikaririwa akisema jana kuwa hawezi kuzungumzia lolote kuhusiana na matokeo ya kikao chao cha jana na serikali kwa sababu mwenye mamlaka ya kuzungumzia suala hilo ni Rais wa TFF, Leodger Tenga ambaye hakuwapo nchini.
Maagizo hayo ya serikali yametolewa katika kipindi ambacho tayari serikali imeshatangaza kuifuta katiba mpya ya TFF (ya mwaka 2012) na kuamuru itumike ya 2006, bila kujali ahadi ya FIFA kutuma ujumbe wake katikati ya mwezi huu kujaribu kutatua mgogoro wa uchaguzi mkuu wa shirikisho hilo.
Hata hivyo, kwa mujibu katiba ya TFF ambayo inazingatia maelekezo ya FIFA, ibara ya 25(1) na (2), mwenye mamlaka ya kuitisha mkutano mkuu wa TFF ni kamati ya utendaji ya shirikisho hilo au theluthi mbili ya wajumbe wa mkutano mkuu ambao hutakiwa kuomba kuitishwa mkutano mkuu kwa maandishi.
Katiba hiyo ya TFF haitoi nafasi kwa serikali kuamuru kuitishwa mkutano mkuu.

Rais wa TFF, Leodger Tenga

HATARI YA KUFUNGIWA
Ingawa hadi kufika jana haikufahamika kama TFF watatekeleza maagizo hayo ya serikali,
lakini uzoefu katika maeneo mengine unaonyesha kuwa utekelezaji wa amri hiyo utaiweka Tanzania katika hatari kubwa ya kufungiwa na FIFA ambayo inapinga vikali serikali kuingilia masuala ya soka.
Novemba 2006, Kenya ilifungiwa na FIFA kutokana na serikali kuingilia masuala ya soka na kushindwa kufuata taratibu za chombo hicho cha kusimamia mchezo wa soka duniani.
FIFA waliiondolea Kenya kifungo hicho Machi 9, 2007 baada ya Waziri Kamanda 'kuinua mikono' kwa kutangaza hadharani kuwa kamwe hawataingilia tena masuala ya KFF kufuatia 'mashinikizo' makubwa kutoka ndani na nje ya taifa hilo.
Ujumbe wa FIFA ulienda Kenya kutoa mwongozo wa kurejesha soka la Kenya katika hali ya kawaida ikiwamo kumtaka waziri wa michezo akiri kutoingilia tena uendeshaji wa KFF.
Rais wa Nigeria, Jonathan Goodluck aliamuru nchi yake isishiriki tena michuano yoyote ya soka ya kimataifa kwa nia ya kujipanga upya baada ya timu yao ya taifa ya soka kuondoshwa kwa aibu kwenye fainali za Kombe la Dunia mwaka 2010.
Hata hivyo, ilifahamika baadaye kuwa maamuzi hayo ya rais yalikuwa na nia ya kumdhibiti mmoja wa viongozi wa juu wa shirikisho la soka la nchi hiyo (NFF), Amos Adam aliyekuwa mbioni kuwania tena uongozi.
Kutokana na kitendo hicho cha serikali kuingilia soka, FIFA iliipa serikali ya Nigeria saa 48 kufuta agizo lake na kwamba, vinginevyo ingefungiwa. Saa chache baadaye, serikali ya Nigeria ilisalimu amri kwa kutangaza kufuta agizo lake baada ya rais Jonathan kuteta ikulu na Adam.

MGOGORO TFF
Chanzo cha mgogoro wa uchaguzi wa TFF ni kuenguliwa kwa baadhi ya wagombea, wakiwamo Jamal Malinzi anayewania kugombea urais na Michael Wambura anayeutaka umakamu wa rais.

Wednesday, March 6, 2013

Ronaldo aizamisha Manchester United na kuing'oa Ulaya

Kocha wa Real Madrid, Jose Morinho akimtuliza Nani baada ya kulimwa kadi nyekundu
Luca Modric akisawazisha bao la Real Madrid jana


 

'Muuaji' Real Madrid akiwajibika uwanjani jana OT

MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa Manchester United, Cristiano Ronaldo usiku wa kuamkia leo alikuwa mwiba mbali kwa vinara hao wa Ligi Kuu ya England baada ya kufunga bao la ushindi na kuiondosha Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Ronaldo aliyepata mafanikio makubwa akiwa na klabu hiyo ya Old Trafford, jana alirejea kivingine kwa kuifungia Real Madrid bao la pili na la ushindi na kuifanya timu yake kufuzu robo fainali za Ulaya kwa jumla ya mabao 3-2.
Katika mechi ya awali iliyoisha kwa sare ya bao 1-1 mjini Madrid, Ronaldo ndiye alifunga bao la kuasawazisha na jana alionyesha alivyo muhimu kwa kikosi hicho cha Morinho kwa kufunga bao lililoipa Real ushindi wa 2-1 uwanja wa Old Trafford.
Madrid waliwapa matumaini vijana wa Sir Alex Ferguson alimuanzishia benchi Wayne Rooney, baada ya Sergio Ramos kujifunga bao baada ya kipindi cha pili kabla ya kurekebisha kosa lake kwa kusaidia kupatikana kwa bao la kusawazisha lililofuingwa na Luca Modric aliyetokea benchi.
Manchester United iliyomuanzisha benchi nyota wake, Wayne Rooney ilijikuta ikimpoteza winga wake mahiri, Luis Nani aliyemchezea rafu Alvaro Albeloa kadi iliyolalamikiwa na Sir Ferguson kabla ya Ronaldo kuja kuwazamisha.
Katika mechi nyingine iliyochezwa jana mabingwa wa Ujerumani, Borussia Dotmund iliungana na Real baada ya kuing'oa Shakhtar Donetsk kwa jumla ya mabao 5-2 baada ya kupata ushindi nyumbani wa mabao 3-0 wiki mbili tangu walipolazimisha sare ya mabao 2-2 ugenini.
Michuano hiyo itaendelea tena usiku wa leo kwa mechi nyingine mbili, Juventus ya Italia itakuwa nyumbani kuialika Celtic walioitungia kwao mabao 3-0 na Valencia itaifuata PSG nchini Ufaransa wakiwa nyuma ya mabao 2-1 iliyofungwa ilipocheza nyumbani Hispania.

 

 

Tuesday, March 5, 2013

ZFA yaridhia Aman Makungu kujiuzulu Urais

Aman Ibrahim Makungu; Si rais tena ZFA

Na Ally Mohamed, Zanzibar
HATIMAYE Kamati ya Utendaji ya Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), imekubali ombi la Rais wake, Aman Ibrahim Makungu kujiuzulu nafasi hiyo.
Katika Barua iliyoandikwa na ZFA Machi 4, mwaka huu, yaani jana, ikisainiwa na Makamu wa Rais Kisiwani Unguja, ambaye pia ni Kaimu Rais wa ZFA kikatiba, Alhaj Haji Ameir, ikiwa na Kumbukumbu namba. ZFA/PRESIDENT/VOL.11/05, ombi hilo limekubaliwa.
Barua hiyo imesema Kamati ya Utendaji ya ZFA Taifa, imekaa na kujadili kwa kina ombi la kujiuzulu kwa Makungu, na kutafakari kwa makini na hatimaye kufikia uamuzi wa kulikubali ombi hilo.
Aidha katika barua hiyo, ZFA Taifa wamemshukuru Aman Makungu kwa msaada wake alioutoa huku wakimuomba aendelee kuwa na chama hicho wakati wowote atakapohitajika.
Nakala za barua hiyo zimetumwa kwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Michezo la Zanzibar pamoja na Msaidizi Katibu ZFA Kisiwani Pemba.
Kwa mujibu wa Katiba ya ZFA, sasa ni wazi kuwa kunalazimika kufanyika uchaguzi mwingine ndani ya siku 90.
Itakumbukwa kuwa miezi miwili iliyopita, Rais wa ZFA, Aman Ibrahim Makungu aliandika barua ya kuomba kujiuzulu nafasi hiyo kwa kile kilichoelezwa katika barua hiyo kuwa ni kuchoshwa na baadhi ya viongozi wa chama hicho wasiotaka mabadiliko huku wakionekana kuwagawa baadhi ya wajumbe wa ZFA kwa kisingizio cha U-Unguja na U-Upemba, ambapo Kamati ya Utendaji ya ZFA Taifa walilikataa ombi hilo kwa madai kuwa litachangia kurejesha nyuma soka la Zanzibar.


Imehamishwa:Bin Zubeiry


TFF yawasilisha barua ya kutaka kuonana na Waziri




NA BONIFACE WAMBURA
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewasilisha rasmi maombi ya kuonana na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara ili kuzungumzia uamuzi wake wa kutengua usajili wa Katiba ya 2012.
Maombi hayo yaliwasilishwa rasmi Wizarani jana (Machi 4 mwaka huu) ambapo TFF imependekeza kikao hicho kifanyike keshokutwa (Machi 7 mwaka huu) au Machi 13 mwaka huu.
Kamati ya Utendaji ya TFF iliyokutana Machi 2 mwaka huu kujadili tamko ya Waziri kutengua matumizi ya Katiba ya 2012 ndiyo iliyopendekeza kikao hicho kwa lengo la kusikiliza upande wa TFF katika suala hilo.
TFF imeamua kuchukua hatua hiyo kufuatia tamko la serikali kutangaza kuifuta katiba mpya ya shirikisho hilo iliyorekebishwa kwa njia ya waraka na iliyotumika kuwaengua baadhi ya wagombea kwenye uchaguzi wake uliokuwa ufanyike Februari 24 mwaka huu.
Hatua ya serikali imekuwa ikielezwa na wadau kama tisho la Tanzania kuadhibiwa na Shirikisho la Soka Duniani, FIFA linalopinga serikali kuingilia vyama wanachama wake.

Hatma ya Lyon kesho Chamazi, Ligi Kuu ikiendelea




NA BONIFACE WAMBURA
HATMA ya African Lyon kuendelea kushika mkia au la kwenye Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inajulikana kesho wakati itakapokuwa mwenyeji wa Ruvu Shooting kwenye Uwanja Azam Complex ulioko Chamazi, Dar es Salaam.
Lyon yenye pointi 13 kutokana na mechi 19 inabidi iifunge Ruvu Shooting kama inataka kuirejesha mkiani Toto African yenye pointi 14. Kama kweli inazitaka pointi zote tatu itabidi ifanye kazi mbele ya Ruvu Shooting inayotiwa makali na Kocha Charles Boniface Mkwasa.
Hiyo itakuwa mechi ya 18 kwa Ruvu Shooting inayoshika nafasi ya saba ikiwa na pointi 26 ikitanguliwa na vinara wa ligi hiyo Yanga, Azam, Simba, Coastal Union, Kagera Sugar na Mtibwa Sugar yenye pointi 28 ikinolewa na nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Mecky Maxime.
Mechi hiyo namba 139 itachezeshwa na mwamuzi Amon Paul kutoka Musoma wakati wasaidizi ni Anold Bugado wa Singida na Milambo Tshikungu kutoka Mbeya. Mwamuzi wa mezani atakuwa Shafii Mohamed wa Dar es Salaam.
Nayo Tanzania Prisons ya Jumanne Chale itakuwa mgeni wa Oljoro JKT katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha wakati Mgambo Shooting itaoneshana kazi na Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
Keshokutwa (Machi 7 mwaka huu) Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya JKT Ruvu ya Kocha Charles Kilinda na Kagera Sugar.
Ligi hiyo itaendelea tena Jumamosi ya Machi 9 mwaka huu kwa mechi mbili; Yanga vs Toto Africans (Uwanja wa Taifa), na Azam vs Polisi Morogoro (Azam Complex, Chamazi).

 

Simba kurejea kinyonge nyumbani leo usiku

Na Ezekiel Kamwaga, Kwanza Sul, Angola
TIMU ya Smba inarejea nchini Tanzania kesho usiku ikitokea Angola ambako jana ilitolewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Libolo ya hapa.
Wachezaji wa Simba leo asubuhi wamefanya mazoezi katika Uwanja wa Libolo uliopo hapa ambako mechi hiyo ilichezwa na mchana itasafiri kwenda mji mkuu wa Angola, Luanda, itakapolala kusubiri safari ya kesho.
Hali katika kambi ya Simba iliyopo katika Hoteli ya Ritz, ilikuwa ya huzuni kutokana na kipigo hicho kikubwa zaidi cha ugenini ambacho Simba imewahi kukipata katika kipindi cha miaka minne iliyopita.
Mara ya mwisho Simba kupata kipigo kikubwa ilikuwa mwaka 2009 ilipofungwa mabao 5-1 na Harass Al Hadoud ya Misri katika michuano kama hii kwenye mechi iliyopigwa jijini Alexandria, Misri.
Kwa ujumla, Simba ilicheza vizuri katika mchezo huo isipokuwa katika dakika 10 za mwisho ambazo iliruhusu mabao matatu kati ya manne iliyofungwa.
Hata hivyo, matokeo hayo ya 4-0 hayatoi tathmini halisi ya mechi hiyo kwa vile katika sehemu kubwa ya mchezo huo, Simba na Libolo zilikuwa zimetoshana nguvu.
Libolo walikuwa na faida ya kuwa na wachezaji wenye uzoefu mkubwa wa mechi za kimataifa kama vile kiungo Ruben aliyekuwa nyota wa mchezo huo ambaye pamoja na kufunga bao la tatu, ndiye aliyekuwa akiichezesha timu hiyo.
Ruben ametoka kuichezea klabu ya Braga ya Ureno iliyokuwa ikishiriki katika Ligi ya Mabingwa Ulaya na tofauti za wachezaji kama hao na wale wa Simba ilionekana katika namna ambavyo wenyeji walitumia nafasi zao.
Saa moja kabla ya mechi kuanza, mvua kubwa ilinyesha katika mji wa Calulo na kuathiri hali ya uwanja jambo lililosabisha mpira kuchezwa katika mazingira magumu.
 

TFF YAIPONGEZA AZAM KUSONGA MBELE AFRIKA


NA BONIFACE WAMBURA
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pongezi kwa timu ya Azam ya Tanzania Bara kwa kufanikiwa kusonga mbele katika michuano ya Kombe la Shirikisho iliyo chini ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).
Ushindi wa jumla ya mabao 8-1 ambao Azam imeupata dhidi ya Al Nasir Juba ya Sudan Kusini si fahari kwa timu hiyo tu, bali Tanzania kwa ujumla, na unaonyesha jinsi klabu hiyo ilivyojipanga kiushindani katika michuano hiyo ya Afrika.
Hata hivyo, ni vizuri Bodi ya Wakurugenzi ya klabu hiyo, benchi la ufundi na wachezaji wa timu hiyo wakautazama ushindi huo kama changamoto kwao kuhakikisha wanajipanga vizuri zaidi kwa raundi inayofuata.
Timu ya Azam inayofundishwa na Mwingereza John Stewart Hall ilishinda nyumbani mechi ya kwanza mabao 3-1, na juzi kuibuka na ushindi wa mabao 5-0 ugenini jijini Juba.
Kwa kufanikiwa kuing’oa Al Nasir Juba, Azam sasa watacheza raundi ya kwanza (raundi ya 16 bora) ya michuano dhidi ya Barrack Y.C.II ya Liberia ambayo katika raundi ya awali iliitoa Johansens ya Sierra Leone. Barrack ilishinda bao 1-0 nyumbani katika mechi ya kwanza na kulazimisha suluhu katika mechi ya marudiano jijini Freetown.
 
Azam itaanzia mechi hiyo ugenini kati ya Machi 15,16 na 17 mwaka huu wakati mechi ya marudiano itachezwa Tanzania kati ya Aprili 5,6 na 7 mwaka huu.