STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 15, 2012

  MASHALI AMTWANGA MGANDA NA KUTWAA UBINGWA EAC

Mchezaji wa Mpira wa Timu ya Simba na Timu ya Taifa ya Tanzania Juma Nyoso kulia akiwa wakiomba Duwa kwa ajili ya bondia Thomas Mashali katikati wa pili kulia ni msanii Maarufu wa bongo Fleva Josephe Haule Pr. J ambapo walikwenda kumpa kampani bondia huyo na kufanikisha ushindi wake na kumuenzi muhasisi wa taifa hili baba wa taifa picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
bondia Thomas Mashali akiwa na mikanda yake ya ubingwa wa Tanzania pamoja na wa Afrika Mashariki na Kati
Rais wa TPBO Yasini Abdallah akisalimiana na Prof.J kwenye kona ya Mashali
Mchezaji wa Mpira wa Timu ya Simba na Timu ya Taifa ya Tanzania Juma Nyoso kulia akiwa amebeba bendera ya Taifa wakati ukipigwa wimbo wa taifa kwa ajili ya bondia Thomas Mashali katikati wa pili kulia ni msanii Maarufu wa bongo Fleva Josephe Haule Pr. J ambapo walikwenda kumpa kampani bondio huyo na kufanikisha ushindi wake na kumuenzi muhasisi wa taifa hili baba wa taifa picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Baadhi ya Viongozi pamoja na mgeni rasmi wakisimama kwa ajili ya wimbo wa tafa kabla ya mpambano
BONDIA THOMAS MASHALI kushoto akioneshana uwezo wa kutupiana masumbwi na  MEDY SEBYALA wa Uganda wakati wa mpambano wao uliofanyika kwa ajili ya kumbukumbu ya baba wa taifa Mashali alishinda kwa Point picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Medy Sebyala akioneshana ufundi wa kutupiana makonde na bondia Thomas Mashali wakati wa mpambano wao wa kugombea ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati Mashali alishinda kwa point picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

BONDIA THOMAS MASHALI kushoto akioneshana uwezo wa kutupiana masumbwi na  MEDY SEBYALA wa Uganda wakati wa mpambano wao uliofanyika kwa ajili ya kumbukumbu ya baba wa taifa Mashali alishinda kwa Point picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Medy Sebyala akioneshana ufundi wa kutupiana makonde na bondia Thomas Mashali wakati wa mpambano wao wa kugombea ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati Mashali alishinda kwa point picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

KAMANDA wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Charles Kenyela kushoto akiwa amekinga ngumi huku akiwa na furahaa baada ya bondia Thomas Mashali kuibuka na ubigwa kwa kumpiga bondia kutoka Uganda wakati wa maazimisho ya kumbukumbu ya baba wa taifa picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Thomasi Mashali akiwa na mkanda wake wa ubingwa wa Afrika Mashaliki katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com



Mbunge wa Kinondoni Iddy Azani akiwa katika picha na Bondia Thomas Mashali baada ya kuvishwa ubingwa wa Afrika Mashariki picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Medy Sebyala akioneshana ufundi wa kutupiana makonde na bondia Thomas Mashali wakati wa mpambano wao wa kugombea ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati Mashali alishinda kwa point picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Sunday, October 14, 2012

RAIS KIKWETE ATEMBELEA MAKANISA YALIYOHARIBIWA KATIKA VURUGU ZA WAISLAMU MBAGALA



Rais Jakaya Kikwete akiangalia uharibifu mkubwa uliofanywa katika kanisa la Pentekoste la Mbagala jijini Dar es Salaam, wakati wa vurugu za Waislamu jana Ijumaa kufuatia habari kuwa kuna mtoto amekojolea Qur an.
Rais Jakaya Kikwete akioneshwa na Mchungaji Alkwin Mbawi uharibifu uliofanywa kwenye magari yaliyokuwa yameegeshwa ndani ya kanisa la Pentekoste la Mbagala jijini Dar es Salaam wakati wa vurugu za Waislamu jana Ijumaa.
Rais Jakaya Kikwete akioneshwa na Katibu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Dar es salaam M Mkosimonga, uharibifu uliofanywa kwenye kanisa hilo huko Mbagala jijini Dar es Salaam wakati wa vurugu za Waislamu jana Ijumaa.
Rais Kikwete akioneshwa na Katibu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Dar es Salaam M. Mkosimonga  uharibifu uliofanywa kwenye kanisa hilo wakati wa vurugu za Waislamu jana.
Rais Kikwete akioneshwa na Askofu Msaidizi wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheli Dayosisi ya Dar es Salaam na Pwani, Mkosimonga uharibifu uliofanywa kwenye kanisa hilo huko Mbagala wakati wa vurugu za Waislamu jana Ijumaa.
You might also like:

Messi aing'arisha Argentina

Lionel Messi wa Argentina


MENDOZA, Argentina
Lionel Messi aliiongoza Argentina kuilaza timu ngumu ya Uruguay katika nusu saa ya mwisho ya mchezo kwa mabao mawili ya kifundi katika ushindi wa 3-0 jana ambao umeibakiza kileleni mwa msimamo wa kundi la Amerika Kusini la michuano ya awali ya Kombe la Dunia.
Argentina inaongoza kundi la timu tisa la Amerika Kusini ikiwa na pointi 17 katika mechi nane ambazo ni nusu ya kampeni. Colombia na Ecuador zipo pointi moja nyuma, Uruguay na Chile tano nyuma yake.
Messi alitengeneza na kumalizia goli lake la kwanza katika dakika ya 66, alipotoa pasi kwa Angel Di Maria kabla ya kukimbia kwenda kuusukumizia wavuni mpira huo uliompita Fernando Muslera.
Argentina ilipata bao la pili dakika tisa baadaye kwa muvu nyingine kwenye wingi ya kushoto, Messi akimpa pasi tena Di Maria ambaye alirudisha mpira huo kwa 'tachi' ya kwanza ambapo Sergio Aguero aliugusa na kutumbukia nyavuni.
Goli la tatu katika dakika ya 80 lilitokana na mpira wa kijanja wa adhabu ndogo wa Messi, ambaye aliudanganya ukuta wa Uruguay kwa kupitisha mpira huo chini yao na kufunga wakati wenyewe wakiruka wakitaraji atalenga lango kwa juu.
Kilikuwa kisasi kizuri kwa Messi, ambaye sasa amefunga magoli 12 katika mechi saab zilizopita za timu ya taifa, na Argentina ambayo ilitolewa na Uruguay kwa penalti katika fainali za mwaka 2011 za Copa America ambazo washiriki hao wa nusufainali ya Kombe la Dunia mwaka 2010 walikuja kutwaa ubingwa.
Reuters

Simba hawashikiki Bara licha ya kunasa kwa Coastal Union


Mabingwa wa ligi kuu ya Bara Simba jana walipunguzwa kasi na Coastal Union hapa Tanga, lakini angalau wakamudu kuendeleza rekodi ya kutopoteza mchezo mpaka robo ya msimu, kufuatia sare ya 0-0 kwenye Uwanja wa Mkwakwani.
Kwa sare hiyo dhidi ya Coastal iliyokuwa na wachezaji 10 uwanjani kwa zaidi ya dakika 20, Simba imeendelea kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya Bara baada ya kufikisha pointi 17 kutokana na michezo saba. Wenyeji wamefikisha pointi 10.
Azam imejichimbia katika nafasi ya pili, pointi moja nyuma ya Simba baada ya jana kuifunga Polisi Morogoro bao 1-0 kwenye Uwanja wa Jamhuri, huku ikiwa na mechi moja mkononi.
Simba ambayo ilishinda michezo minne mfululizo kabla ya kutoka sare ya 1-1 na Yanga na kurejea kushinda katika mchezo uliopita dhidi ya JKT Oljoro, ingeweza kuwa imepoteza mechi yake ya kwanza jana kama Coastal iliyoonyesha soka maridadi ingekuwa makini.
Hemedi Morocco, kocha wa Coastal Union, alisema anashukuru kupata pointi moja licha ya timu yake kushindwa kutumia vizuri nafasi nyingi za kufunga ilizotengeneza.
Kocha wa Simba Milovan Cirkovic aliwaambia waandishi wa habari baada ya mchezo huo kuwa Coastal ilicheza vizuri, lakini pia hakufurahishwa na uchezaji wa mshambuliaji wake wa kulipwa kutoka Ghana Daniel Akuffor.
Chipukizi Haruna Chanongo alikaribia kuipatia Simba bao la kuongoza katika dakika ya 12 baada ya shuti lake kugonga mwamba wa juu na kutoka nje.
Kama Chanongo angefunga, Nsa Job angeweza kuwa ameisawazishia Coastal Union katika dakika ya 39 wakati shuti lake lililopotoka nje akiwa katika nafasi nzuri, kutokana na krosi ya Selemani Kassim ambaye alikuwa amemtoka beki Pascal Ochieng.
Siku ya mshambuliaji wa kati Job ilimalizika vibaya dakika 20 hivi kabla ya filimbi ya mwisho hata hivyo, baada ya kutolewa uwanjani na muamuzi Haji Mbelwa kutokana na kosa la pili la kadi ya njano dhidi ya mabeki wawili wa kati wa Simba.
Katika kosa la kwanza, Job ambaye ni mchezaji wa zamani wa Simba, alimchezea vibaya Shomari Kapombe kabla ya kumfanyia madhambi Ochieng katika kipindi cha pili.  
Timu zilikuwa:
COASTAL: Jackson Chove, Said Sued, Juma Jabu, Mbwana Hamisi, Jamal Machelenga, Jerry Santo, Mohammed Athumani, Selemani Kassim, Green Atupele, Nsa Job, Razak Khalfani (Lameck Dayton dk.45).
SIMBA: Juma Kaseja, Said Nasoro, Amiri Maftah, Pascal Ochieng, Shomari Kapombe, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba, Haruna Moshi (Uhuru Selemani dk.58), Felix Sunzu, Daniel Akuffor (Salum Kinje dk.72), Haruna Chonongo.
Kutoka Morogoro Idda Mushi anaripoti kwamba bao la Azam lilifungwa na Kipre Tchetche katika dakika ya 54 hivyo kuiweka timu hiyo katika nafasi nzuri ya kukaa kileleni kama itashinda mechi yake ya mkononi.
Kocha wa Azam Boris Bunjak alielezea kutoridhishwa na ukubwa wa ushindi huo kutokana na Polisi kuwa timu ya mkiani.
John Simkoko, mwalimu wa Polisi alisema makosa madogo madogo ya mchezaji mmoja mmoja na si timu, ndiyo yaliyowagharimu.

Nnyota wa Simba, Yanga washindwa kutambiana 'mchangani'

Onesmo Waziri 'Ticotico' (4) wa Golden Bush akitafuta mbinu za kumtoka mchezaji wa wahenga Fc (kulia) huku Abdallah Msheli akiwa tayari kumsaidia

Katina George (14) wa Golden Bush akijaribu kufunga bao mbele ya msitu wa mabeki wa Wahenga Fc katika pambano lao lililochezwa jana Sinza, Dar es Salaam.

NYOTA wa zamani wa klabu za Simba na Yanga jana walishindwa kutambiana baada ya timu walizokuwa wakizichezea za Golden Bush na Wahenga Fc kutoshana nguvu ya kutoka sare ya 1-1 katika pambano la kirafiki.
Wazir Mahadhi, Abdul Ntiro, Ally Yusuf  'Tigana', Abdallah Msheli na Steven Marashi walioichezea Golden Bush ya Mabibo walishindwa kuwazidi ujanja wenzao Mengi Matunda na Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio' wa Wahenga ya Sinza katika mchezo huo uliochezwa uwanja wa TP, Sinza.
Nyota hao walionyesha bado wamo katika usakataji soka kwa jinsi walivyokuwa wakikimbiza dimbani ili kuzisaidia timu zao, lakini mpaka wakati wa mapumziko Wahenga ndio waliokuwa wakiongoza kwa bao 1-0.
Bao lao lilifungwa na Mohammed Ibrahim katika dakika ya 38 baada ya kufanikiwa kuihadaa ngome ya Golden Bush iliyokuwa chini ya Msheli na kumchambua kipa Steven Marashi kwa shuti la karibu.
Kipindi cha pili Golden Bush chini ya nahodha wake Onesmo Wazir 'Ticotico', iliingia kwa kasi baada ya kufanya mabadiliko kadhaa na kufanikiwa kurejesha bao hilo katika dakika ya 64 kupitia Dau 'Messi' aliyemegewa pande zuri Ally Yusuf  'Tigana'.
Licha ya timu zote kushambuliana kwa zamu na kufanya kosa kosa nyingi, mpaka kipyenga kilichokuwa kikipulizwa na Ally Mayay Tembele kilipolia matokeo yalikuwa yamesalia kama awali kwa timu hizo kutoka sare ya bao 1-1.

Mwisho

Waliovamia maeneo ya shule Ilala kukiona

Afisa Mipango Miji wa Ilala, Paul Mbembela akisisitiza jambo alipozungumza na wakazi za Kitunda

Baadhi ya watu waliohudhuria mkutano huo

Mmoja wa wakazi wa Kitunda akiuliza swali ili apate ufafanuzi juu ya hatma ya makazi yao katika eneo wanaloishi
WAKAZI wote waliovamia na kujenga ndani ya maeneo ya shule wilayani Ilala, jijini Dar es Salaam wametahadharishwa kuanza kuondoka wenyewe kabla ya kuchukuliwa hatua za kuondolewa kwa lazima katika maeneo hayo.
Aidha serikali na Manispaa hiyo ya Ilala imeweka bayana kwamba haitakuwa na huruma wala kuwaonea haya wavamizi wa maeneo hayo ya shuleni wakati wa zoezi la kuwaondoa kwa lazima.
Afisa Mipango Miji wa Ilala, Paul Mbembela, ndiye aliyeyasema hayo juzi katika mkutano wa pamoja kati ya ofisi yake na wakazi wa Kitunda, nje kidogo ya Dar es Salaam.
Mbembela alisema Manispaa haitakuwa na huruma na wale wote waliovamia na kujenga ndani ya maeneo ya shule kwa madai waliofanya hivyo wamevunja sheria na hawapaswi kuchekewa.
"Tutakuwa wakali kwa wale wote waliovamia na kujenga katika maeneo ya shule, kuchekea jambo hilo ni kutaka kuwafanya vijana na watoto wete wawe mbumbumbu kwa kushindwa kusoma katika mazingira mazuri," alisema.
Aliongeza kuwa, wananchi wote wanaojitambua kuwa wamefanya hivyo waanze mapema kuchukua uamuzi wa kuondoka wenyewe kwa hiari katika maeneo hayto kabla ya Manispaa ya Ilala haijaenda kuwatoa kwa nguvu.
Afisa huyo, alisema kumekuwa na desturi ya watu kuvamia maeneo ya shule ya kuweka makazi au sehemu za biashara na kusababisha wanafunzi kushindwa kusoma kwa utulivu, kitu ambacho Manispaa yao haipo tayari kuvumilia.
Alisema wananchi wanapaswa kutambua kuwa shule ni moja ya vitu muhimu vinavyopaswa kutochezewa kwani ndiko kunakozalisha viongozi na wataalam kwa baadaye wa taifa hivyo kila mmoja ana jukumu la kuzilinda shule.

Mwisho

Wakazi Kitunda wahakikishiwa makazi ya kudumu mradi wa viwanda



Afisa Mipango Miji wa Manispaa ya Ilala, Paul Mbembela akifafanua jambo katika mkutano wake na wakazi wa Kitunda waliojenga makazi yao ndani ya mradi wa viwanda uliotengwa na serikali miaka kadhaa iliyopita

Prisca Bassu mmoja wa wakazi wa Kitunda akiuliza swali katika mkutano huo

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kipunguni B, Novatus Nyiratu akifafanua jambo katika mkutano huo wa jana

Mkazi mwingine wa eneo la Kitunda akiuliza swali

Sehemu ya umma uliohudhuria mkutano huo wa jana kujua mustakabali wa waliojenga ndani ya mradi wa viwanda

Nataka kujua tusiokuwa na leseni za makazi inajuwaje hatma yetu? Ndivyo mmoja wa wakazi hao alihoji katika mkutano huo

Ibrahim Ismail naye alisimama na kuuliza swali

Hata kinamama nasi tumo kwa maswali

Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Kitunda Kati, Seleman Abdallah Mtama akieleza jambo kabla ya kuufunga mkutano huo







UONGOZI wa Manispaa ya Ilala, umewatoa hofu na kuwahakikishia wakazi wa eneo la Kitunda, waliojenga na kuweka makazi ndani ya eneo lililotengwa kwa ajili ya mradi wa viwanda kwamba kamwe hawataondolewa.
Pia uongozi huo umewahakikishia wakazi hao kuwa maeneo yao yatapimwa upya na kumilikishwa ardhi ili yawe makazi yao ya kudumu mara taratibu za kubadilisha matumizi ya eneo hilo zilizoanza zitakapokamilika.
Akizungumza na wakazi hao katika mkutano wa hadhara ulioitishwa na uongozi wa serikali za mitaa ya Kipunguni B na Kitunda Kati, uliofanyika juzi kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Kipunguni, Afisa Mipango Miji Manispaa ya Ilala, Paul Mbembela alisema wakazi hao hawapaswi kuwa na hofu.
Mbembela alisema licha ya kwamba wakazi wa eneo hilo wapo ndani ya ardhi iliyotengwa kwa miaka mingi na serikali kwa ajili ya mradi wa viwanda, bado hawana hofu kwa vile unafanyika mchakato wa kubadilishwa matumizi yake.
Alisema katika mabadiliko hayo ya matumizi, wakazi waliojenga na kumiliki viwanja katika eneo hilo watafanyiwa utaratibu wa kupimwa maeneo yao na kisha kumilikishwa upya kihalali na mradi huo wa viwanda utahamishiwa maeneo mengine ya viwanja vya serikali vilivyopimwa tayari.
Afisa huyo aliyataja baadhi ya maeneo ambayo mradi huo unaweza kuhamia ni pamoja na Buyuni, Chanika na kwingineko katika manispaa ya Ilala ambayo tayari yameshapimwa na kutengwa.
Aliwasisitiza wakazi hao waliowatuma viongozi wa serikali zao za mitaa katika ofisi za manispaa kuhakikisha wanaipa ushirikiano kamati hiyo katika zoezi la kuwatambua wamiliki halali wa sasa waliopo katika eneo hilo ili kurahisisha mchakato wa kuyapima na kuwamilikisha upya.
Kabla ya ufafanuzi huo wananchi wa maeneo hayo kupitia serikali zao za mitaa walikuwa na hofu kubwa ya kubomolewa na kupoteza mali zao katika eneo hilo baada ya kubainika eneo hilo lilitengwa kwa mradi wa viwanda.
Baadhi ya wananchi katika mkutano huo uliohudhuriwa na Mwenyekiti wa Serikali ya Kitunda Kati, Seleman Mtama na ile ya Kipunguni B, Novatus Nyiratu walitaka kujua hatma yao iwapo watatimuliwa katika eneo  hilo.
Miongoni mwa wakazi hao, Ibrahim Ismail, Prisca Bassu walitaka kufahamu iwapo wananchi ambao hawana hati au leseni ya makazi katika eneo hilo hatma yao itakuwaje na kuelezwa watasaidiwa  kumilikishwa bila ya tatizo mradi wahakikiwe na kamati yao.

Saturday, October 13, 2012

Mashali, Sebyala wapima uzito kuvaana kesho Friends Cornerupimwa uzito kesho


BONDIA Thomas Mashali wa Tanzania na Mganda Medi Sebyala wamepima uzito leo kwenye ukumbi uliopo Manzese jijini Dar es Salaam tayari kwa ajili ya pambano lao la ubingwa wa Afrika Mashariiki na Kati litakaofanyika Jumapili kwenye ukumbi wa Friend's Corner, Manzese jijini Dar es Salaam.
Mabondia hao walipimwa uzito na afya hizo asubuhi ya leo tayari kwa pambano hilo lililoandaliwa na mratibu Regina Gwae chini ya TPBO.
Mbali na mabondia hao wengine waliopimwa leo ni  Abdul Awilo atakayepanda ulingoni kuchuana na Shedrack Juma, Selemani shaaban atakayechapana na Hamis Mohamed,  Jonas Segu atakayemkabili Ibrahim Class  na  Charles Mashali atakayevaana na Teacher Aaron.
Regina alisema maandalizi yote yamekamilika ikiwamo waamuzi wenye sifa za kuchezesha mapambano ya kimataifa anbao tayari wameshapatikana na mgeni rasmi katika pambano hilo atakuwa Kamanda wa  Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela ambaye anatarajiwa kuambatana na wageni wengine maalum akiwamo Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Mhe. Idd Azzan.
---

Kiemba akana kuziba pengo la Mafisango Simba

Amri Kiamba akishangilia bao moja ya mabao yake katika Ligi Kuu msimu huu

KIUNGO nyota wa Simba, Amri Kiemba, licha ya kuwashukuru mashabiki wa klabu hiyo kumfananisha na kiungo wa kimataifa wa timu hiyo Patrick Mafisango, aliyefariki kwa ajali ya gari Mei mwaka huu, amekiri hajaliziba pengo la kiungo huyo.
Akizungumza na MICHARAZOE muda mchache kabla ya kuondoka jijini na kikosi cha timu yake kuelekea Tanga kuwahi pambano lao dhidi ya Coastal Union, Kiemba alisema licha ya kuanza msimu kwa kung'ara, bado anajiona hajaliziba pengo la Mafisango hata kama watu wanaridhika na kiwango chake.
Kiemba, alisema ni vigumu pengo la kiungo huyo aliyefariki Mei 17 kuzibika kirahisi na kwa ukamilifu kutokana na uwezo na kipaji kikubwa alichokuwa nacho nyota huyo kutoka nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.
"Nashukuru mashabiki kuridhika na juhudi zangu uwanjani kiasi cha kuona kama nimeziba pengo la Mafisango, ila ukweli ni vigumu pengo la kiungo huyo kuzibika kirahisi hata mie mwenyewe najiona sijaliziba hata kidogo, " alisema
Kiemba aliongeza, binafsi alikuwa akimkubali Mafisango kwa umahiri wake hivyo anajisikia vibaya kufananishwa naye japo anafurahia kuona mashabiki wanakikubali kiwango chake kwa mechi chache zilizoanza za msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Kiungo huyo wa zamani wa Yanga, aliyeigomea Simba msimu uliopita kumtoa kwa mkopo kwenda kuichezea timu iliyokuja kushuka daraja ya Polisi Dodoma ameanza  msimu kwa kuonyesha kiwango cha hali ya juu akiifungia Simba mabao yaliyoiweka kileleni mwa msimamo huku mwenyewe akiongoza orodha ya wafungaji mpasa sasa.
Mchezaji huyo ameifungia Simba jumla ya mabao manne mpaka sasa, matatu akiyafunga katika mechi mbili zilizopita dhidi ya Yanga waliotoka nao sare ya bao 1-1 na ile ya ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya JKT Oljoro, jingine alifunga walipilaza JKT Ruvu.

Mwisho

Miyeyusho, Nassib kuvaana Uhuru Day


MABONDIA wanaozidi kupanda chati nchini, Francis Miyeyusho na Nassib
Ramadhani wanatarajia kuvaana jijini Dar es Salaam siku ya Desemba 9 katika pambano la kuwania ubingwa wa Mabara unaotambuliwa na WB-Forum.
Pambano hilo linatarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa PTA na limeandaliwa na promota Mohammed Bawazir wa kampuni ya Dar World Link chini ya usimamizi wa Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania, PST.
Hilo litakuwa pambano la kwanza kwa mabondia hao wenye rekodi ya kuwapiga wapinzani wao kukutana.
Akizungumza kwenye utambulisho wa mabondia hao, promota wa pambano hilo la uzani wa Bantam (kilo 53.5), Mohammed Bawazir, alisema maandalizi ya mchezo huo yamekamilika ikiwemo kumalizana na mabondia hao.
Bawazir alisema ana imani litakuwa la aina yake kulingana na rekodi za mabondia hao.
Kwa mujibu wa rekodi za Miyeyusho mwenye umri wa miaka 32 amecheza jumla ya mapambano 44 akishinda michezo 32, 19 ikiwa ya KO amepigwa 10 na kutoka sare michezo miwili.
Kwa upande wa rekodi za Nassib inaonyesha amecheza mapambano 12 akishinda 10 na kupoteza mawili.
Kabla ya kuvaana na Miyeyusho bondia huyo anatarajiwa kuvaana na Mkenya Nick Otieno atakayepigana nae Novemba 30 kwenye pambano la kuwania ubingwa wa IBF Afrika na Ghuba ya Uajemi.

GOLDEN BUSH WALIPOPIMANA UBAVU NA WAHENGA FC UWANJA WA TP-SINZA


BAADHI YA PICHA ZA MATUKIO YA PAMBANO LA TIMU YA SOKA YA GOLDEN BUSH ILIYOKUWA IKIUNDWA NA NYOTA WA ZAMANI WA YANGA KAMA AKINA ALLY YUSUF 'TIGANA', ABDALLA MSHELI, WAZIR MAHADH 'MANDIETA' CHINI YA UNAHODHA WA ONESMO WAZIR 'TICOTICO' DHIDI YA WAHENGA FC ILIYOKUWA IKIONGOZWA NA MKONGWE MADARAKA SELEMAN 'MZEE WA KIMINYIO'.
Patashika dimbani kati ya Golden Bush na Wahenga FC

Onesmo Wazir 'Ticotico' wa Golden Bush (kushoto), akitafuta mbinu za kumpotoka China wa Wahenga Fc, huku mchezaji wenzake akiwa tayari kumsaidia.

Twende sasa kama 'Ronaldo'

Ticotico akitafuta mbinu za kumtoka mchezaji wa Wahenga Fc

China wa Wahenga Fc akiambaa na mpira dimbani katika mechi yao leo dhidi ya Golden Bush ambapo mpaka tunaondoka uwanjani matokeo yalikuwa bao 1-1. Wahenga wakitangulia kupata bao dakika ya 38 kupitia Moahmmed Ibrahim kabla ya Golden Bush kurejesha katika kipindi cha pili kupitia kwa Dau 'Messi'

China wa Wahenga akimtokea beki wa Golden Bush (14) huku wachezaji wengine wakiwa tayari kutoa msaada.

Machota wa Golden Bush akimiliki mpira mbele ya mchezaji wa Wahenga Fc

Sunday, September 30, 2012

MASHETANI WEKUNDU HOI KWA SPURS, YALALA OLD TRAFFORD




Jan Vertonghen akishangilia bao aliloifungia timu yake ya Tottenham dhidi ya Manchester United jana. Picha:Reuters


TIMU ya soka ya Tottenham Hotspurs chini ya kocha wake Andre Villa Boas jana walivunja mwiko wa kutoifunga Manchester United kwa muda mrefu baada ya kuwalaza Mashetani Wekundu hao kwenye dimba lao la nyumbani la Old Frafford kwa mabao 3-2.
Bao la mapema lililofungwa na Vertonghen liliwachanganya Man United kabla ya kukujikuta wakifungwa jingine nusu saa baadae na Garret Bale na kuwafanya Spurs kwenda mapumziko wakiongoza mabao 2-0.
Katika mechi nyingine, vinara wa ligi hiyo Chelsea wameendelea kung'ara kwa kuilaza Arsenal mabao 2-1, huku Liverpool ikitoa kisango cha 'mbwa mwizi' kwa Norwich City kwa kuilaza mabao 5-2, huku jahazi la Swansea City likiendelea kuzama kwa kulazwa mabao 2-0 na Stoke City mabao yote yakitupiwa kambani na Peter Crouch.
Matokeo mengine ya mechi za Ligi Kuu ya England kwa jana ni kama iofuatavyo:


29 September
Man Utd2 - 3Tottenham
LCAdC Nani (50)
S Kagawa (53)

J Vertonghen (1)
G Bale (31)
CD Dempsey (51)
Old TraffordAttendance (75566)
Teams | Report
29 September
Stoke2 - 0Swansea
P Crouch (11)
P Crouch (35)

Britannia StadiumAttendance (27330)
Teams | Report

29 September
Norwich2 - 5Liverpool
S Morison (60)
G Holt (86)

L Suarez (1)
L Suarez (37)
N Sahin (46)
L Suarez (56)
S Gerrard (67)
Carrow RoadAttendance (26831)
Teams | Report
29 September
Sunderland1 - 0Wigan
S Fletcher (50)
Stadium of LightAttendance (37742)
Teams

29 September
Fulham1 - 2Man City
M Petric (pen 9)
SL Aguero (42)
E Dzeko (86)
Craven CottageAttendance (25698)
Teams
29 September
Everton3 - 1Southampton
L Osman (24)
N Jelavic (31)
N Jelavic (37)

G Ramirez (5)
Goodison ParkAttendance (37922)
Teams

29 September
Reading2 - 2Newcastle
JB Kebe (57)
N Hunt (61)

D Ba (57)
D Ba (82)
Madejski StadiumAttendance (24097)
Teams | Report
29 September
Arsenal1 - 2Chelsea
YK Gervinho (41)
FJS Torres (19)
JMG Mata (52)
Emirates StadiumAttendance (60101)
Teams | Report

Yanga, Lyon kujiuliza leo Taifa

MABINGWA wa Kombe la Kagame, Yanga leo ikiwa chini ya kocha wake mpya, Ernstus Brandts inatarajiwa kuivaa Africna Lyon katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara pambano litakalofanyika kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Yanga ambayo imemsainisha mkataba wa mwaka mmoja kocha huyo kutoka Uholanzi, itaikaribisha Lyon ikiwa bado inachekelea ushindi mnono wa mabao 4-1 iliyopata dhidi ya JKT Ruvu.
Pambano hilo ambalo litarushwa hewani na kituo cha Super Sport katika ule muendelezo wa Tanzania Weekend Soccer, linatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na wapinzani wa Yanga kutoka kupokea kichapo cha mabao 2-1 toka kwa Prisons ya Mbeya.
Yanga itahitajika ishinde ili kujiweka pazuri kabla ya kuvaana na watani zao keshokutwa kwenye pambano lao la kwanza ambapo wana Jangwani wana deni kubwa la kulipa kisasi cha kufungwa mabao 5-0 katika mechi ya kufungia msimu uliopita.
Mbali na deni hilo la karibuni, pia Yanga ina deni la miaka 37 la kipigo cha mabao 6-0 ilichopewa mwaka 1977 ambacho imekuwa ikihangaika kukirudisha bila ya mafanikio.
Bila shaka pambano hilo litakuwa kipimo kizuri kwa makocha wa timu hizo mbili, Brandts wa Yanga na Muargentina anayeinoa Lyon, iliyoshinda mechi moja tu kama wapinzani wao hao wanaovaana wakiwategemea mshambiliaji wake nyota, Adam Kingwande na wengineo.

SIMBA YAREJEA KILELENI, YAITUNGUA PRISONS 2-1

 
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu, Simba jana waliendelea kutakata kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuitandika Prisons ya Mbeya mabao 2-0 na kurejea kileleni wakiiondosha Azam Fc iliyowaengua kwa saa kadhaa.
Bao la kwanza la Mrisho Ngassa kwa timu hiyo ndilo lililoipa Simba ushindi iliyomaliza mechi hiyo iliyochezwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ikiwa wachezaji tisa uwanjani.
Kwa ushindi huo, Simba imeendelea kuwa timu pekee yenye matokeo ya asilimia 100 baada ya raundi nne, ikiwa na pointi 12, mbili juu ya Azam, katika pambano lililohudhuriwa na watazamaji wachache kuliko kawaida ya mechi za mabingwa watetezi hao.
Coastal Union ni ya tatu ikiwa na pointi nane, tatu juu ya Prisons ambayo imeshuka kwa nafasi moja mpaka kuwa timu ya tano nyuma ya JKT Oljoro kwa uwiano wa mabao, zote zikiwa na pointi tano baada ya michezo minne.
Siku iliisha vibaya kwa Simba baaada ya beki wake Amiri Maftaha kuonyeshwa kadi nyekundu na muamuzi Paul Soleji dakika mbili kabla ya filimbi ya miwsho, baada ya kumchezea rafu mbaya Khalid Fupi.
Siku ilianza vibaya pia kwa Simba baada ya Lugano Mwangama kuipatia Prisons bao la kuongoza katika dakika ya saba tu ya mchezo kwa shuti kali ambalo lilimbabatiza beki Juma Nyoso wa Simba kabla ya kutinga wavuni, kwenye Uwanja wa Taifa.
Iliichukua Simba kipindi kizima cha kwanza kupata bao la kusawazisha lililofungwa na Felix Sunzu katika dakika ya 45 akiunganisha krosi ya Mwinyi Kazimoto.
Kama alivyomalizia ngwe ya kwanza, Sunzu angeweza kuongeza idadi ya mabao ya Simba dakika tatu tangu kuanza kwa kipindi cha pili lakini shuti lake kutokana na pasi ya Mrisho Ngassa lilipaa juu.
Ndipo Ngassa alipochukua jukumu la kusahihisha kosa hilo mwenyewe dakika saba baadaye kwa shuti lililomshinda David Abdallah kuzuia katika lango la Prisons, akiunganisha krosi ya Said Nassoro.  
Simba iliwatoa Amri Kiemba na nafasi yake kuchukuliwa na Salim Kinje, Ramadhani Chombo aliyempisha Jonas Mkude na Edward Christopher kwa Daniel Akuffor baada ya goli la Ngassa ikiwa ni jitihada za kutawala zaidi mechi hiyo, lakini hapakuwa na goli la ziada.
Kocha wa Simba Milovan Circovic alisema timu yake ilipata ushindi kutokana na kucheza vizuri, na akasikitikia athari za kadi nyekundu ya Maftah ingawa alisema kuna wachezaji wa kuziba pengo lake.
Timu zilikuwa:
SIMBA: Juma Kaseja, Nassoro Masoud, Amir Maftah, Shomari Kapombe, Juma Nyoso, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba (Salim Kinje dk.74), Ramadhani Chombo (Jonas Mkude dk.67), Edward Christopher (Daniel Akuffor dk.76), Felix Sunzu, Mrisho Ngassa.
PRISONS: David Abdallah, Aziz Sibo, Laurian Mpalile, Lugano Mwangama, David Mwantika, Khalid Fupi, Misango Magai, Fred Chudu, Elias Maguri, Peter Michael (Sino Agustino dk.67), John Matei.

 

 Wachezaji wa Simba wakishangilia bao la kwanza lililofungwa na Felix Sunzu (kulia)
 Mashabiki wa Simba wakishangilia
 Mshambuliaji wa Simba, mrisho Ngasa akichuana na nahodha wa Tanzania Prisons, Lugano Mwangama
 Golikipa wa Prisons, David Abdallah akiokoa hatari langoni mwake
Wachezahi wa Prisons ya Mbeya wakiongozwa na kipa wao kuomba dua wakati wa mapumziko





CHEKA AMCHAPA TENA NYILAWILA SAFARI HII KWA KO

Bondia Fransic Cheka akinyooshwa mkono juu na mmoja wa mashabiki wa Kigeni waliokuja kuangalia mpambano wake dhidi ya Karama Nyilawila Cheka alishinda katika raundi ya sita baada ya karama kusalimu amri kushoto ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa na wa pili kulia ni mgeni rasmi Kamanda wa polisi wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es salaam Suleiman Kova.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Refarii wa mpambano akiwaelekeza mabondia wasicheze kwa kukumbatiana

Bondia Fransic Cheka kushoto akipepesuka baada ya kupigwa ngumi na Karama Nyilawila wakati wa mpambano wao uliofanyika usiku wa jumamosi cheka alishinda kwa K.O raundi ya sita na kufanikiwa kunyakuwa ubingwa picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Fransic Cheka kushoto akimshambulia Karama Nyilawila kwa masumbwi wakati wa mpambano wao uliofanyika usiku wa jumamosi Cheka alishinda raundi ya sita baada ya kumpiga na kudondoka chini baada ya kuesabiwa akashindwa kuendelea picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Karama Nyilawila  kulia akijitaidi kukwepa makonde ya mpinzani wake Fransic Cheka wakati wa mpambano wao uliofanyika usiku wa jumamosi cheka alishinda kwa K,o raundi ya sita picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Mabondia Karama Nyilawila kushoto akionesheana umwamba wa kutupa masumbwi na Fransic Cheka wakati wa mpambano wao cheka alishinda kwa K,O Raundi ya sitapicha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Fransic Cheka kushoto na Karama Nyilawila wakiwa uringoni kuoneshana uwezo wa kutupiana masumbwi Cheka alishjnda kwa K,O ya Raundi ya sita picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mabondia Karama Nyilawila kushoto na Fransic Cheka wakionesheana umwamba wa kutupiana makonde wakati wa mpambano wao uliofanyika usiku wa jumamosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba Cheka alishinda kwa K,o raundi ya sita picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Fransic Cheka akinyooshwa mkono juu na mmoja wa mashabiki wa Kigeni waliokuja kuangalia mpambano wake dhidi ya Karama Nyilawila Cheka alishinda katika raundi ya sita baada ya karama kusalimu amri kushoto ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa na wa pili kulia ni mgeni rasmi Kamanda wa polisi wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es salaam Suleiman Kova.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Fransic Cheka akinyooshwa mkono juu na mmoja wa mashabiki wa Kigeni waliokuja kuangalia mpambano wake dhidi ya Karama Nyilawila Cheka alishinda katika raundi ya sita baada ya karama kusalimu amri kushoto ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa na wa pili kulia ni mgeni rasmi Kamanda wa polisi wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es salaam Suleiman Kova.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Fransic Cheka akinyooshwa mkono juu na mmoja wa mashabiki wa Kigeni waliokuja kuangalia mpambano wake dhidi ya Karama Nyilawila Cheka alishinda katika raundi ya sita baada ya karama kusalimu amri kushoto ni Rais wa PST Emanuel Mlundwa na wa pili kulia ni mgeni rasmi Kamanda wa polisi wa Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es salaam Suleiman Kova.Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
BINGWA wa ngumi za kulipwa anayetambuliwa na vyama vya ICB, IBF na WBC, Francis Cheka 'SMG' usiku wa kuamkia leo amedhihirisha kwamba hana mpinzani katika ngumi hizo nchini baada ya kumchapa kwa KO mpinzani wake mkubwa, Karama Nyilawila na kuongeza taji jingine.
Cheka alimpiga Nyilawila katika raundi ya sita ya pam,bano hilo lililokuwa la uzani wa Super Middle la raundi 12 lililofanyika kwenye ukumbi wa PTA, Temeke jijini Dar es Salaam na kutwaa ubingwa wa Mabara wa UBO uliokuwa wazi.
Pambano hilo lililohudhuriwa na mashabiki lukuki, lilishuhudia raundi zote tano za kwanza Nyilawila akionyesha kumdhibiti Cheka kwa kumchezea 'kibabe' akitumia nguvu nyingi kujihami na baadhi ya watu ukumbini kuamini mwisho wa tambo za Cheka zilikuwa zimewadia.
Hata hivyo raudni ya sita ilipoanza Cheka alionyesha amebadilika na hasa baada ya kocha wake Abdallahj Saleh 'Komando' kupanda ulingoni na kuzungumza na bondia huyo na kumshushia kipigo Nyilawila, ambapo moja ya makonde matatu ya mfululizo yalimpeleka chini mpinzani wake.
Mwamuzi wa pambano hilo, Jerome Waluza alimhesabia Nyilawila ambaye alijitahidi kuinuka, lakini ghafla akaonyesha ishara kwamba asingeweza kuendelea na pambano hilo na ukumbi mzima kuripuka kwa shangwe akishangiliwa Cheka ambaye hiyo ni mara ya pili kumpiga Nyilawila.
Kabla ya pambano hilo lililoanza majira ya saa 3;40 usiku, kulikuwa na mapambano saba ya utangulizi pamoja na burudani ya muziki toka bendi ya Mashujaa ambao hata hivyo sio wapenzi wengi walioweza kuishuhudia kutokana na kuondoka ukumbini mapema.
Katika pambano la kwanza la utangulizi Said Mbelwa alimpiga kwa pointi Dickson Mwakipesile, Juma Kihiyo alipigwa kwa pointi na Ibrahim Mahokola katika pambano lililovutia kwa namna mabondia hao walivyoonyeshana kazi.
Pia mdogo wa Cheka, Cosmas Cheka alifanikiwa kuibuka na ushindi wa pointi dhidi ya Fadhil Awadh katika pamnbano jingine lililosisimua wengi kwa ufundi uliokuwa ukionyesha na mabondia hao, naye Shaaban Kilumbelumbe alimpiga kwa pointi Anthony Mathias kabla ya Safari Mbiyu kumpiga kwa KO ya raundi ya kwanza Khalfan Jumanne.
Michezo minginme iliwakutanisha Stan Kessy na Seba Temba, pambano lililoisha kwa mabondia hao kutoka sare na Hassani Kidebe alitolewa nishai na Deo Samwel kwa kupigwa kwa pointi.
Mgeni rasmi katika pambano hilo alikuwa Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam ambaye aliutangazia umma kwamba kama Mlezi wa Ngumi za Kulipwa amefanikiwa kuwafuta wafadhili katika mchezo huo na kumtambulisha raia mmoja wa kigeni kwamba ni miongoni mwao.