STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, December 18, 2010

BREAKING NEWS-ABUU SEMHANDO 'BABA DIANA' IS NO MORE





MWANAMUZIKI Mkongwe wa muziki wa dansi nchini, Abuu Semhando 'Baba Diana' amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo kwa ajali ya gari baada ya kugongwa akiwa kwenye pikipiki eneo la Africana, Mbezi jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana mapema zinasema kifo hicho kilitokea majira ya saa 9 usiku baada ya kugongwa na gari aina ya Benz lililomjeruhi vibaya sehemu ya kichwani.
Abuu aliyetamba miaka ya 1970 akiwa na bendi ya Vijana Jazz, amepatwa na mauti hayo ikiwa ni siku moja tu tangu ashiriki kumziba mkongwe mwenzake, Ramadhani Mtoro Ongalla 'Dk Remmy' aliyefariki Jumatatu na kuzikwa Alhamis.
Kwa hakika ni pigo kwa wanafamilia, ndugu, jamaa na marafiki na wadau wa muziki wa dansi kwa ujumla, ingawa Kazi ya Mola Haina Makosa kwa sababu alishatuambia mapema kwamba KILA NAFSI ITAONJA MAUTI, wametangulia sisi tu nyuma yao tuwadhaike na vifo vyao kwa vile hatujui saa au siku ambayo Malaikat Maut, Izraili atatupitia kuchukua AMANA.
INNALILLAH WAINNA ILAHI RAJIUN!

No comments:

Post a Comment