STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, November 2, 2014

Kombe la Chalenji lakwama Ethiopia, sasa huhamishiwa Sudan

RAIS wa CECAFA, Leodgar Tenga akiwa na Katibu wake, Nicolaus Musonye
Baraza la vyama vya soka Afrika mashariki na kati (CECAFA) kwa sasa linaangalia uwezekano wa kupata muandaaji mpya wa michuano ya mwaka huu 2014 ya chalenji kufuatia Ethiopia kujitoa.
Katibu mkuu wa Cecafa Nicholas Musonye amenukuliwa toka Nairobi, Kenya kuwa Ethiopia imejitoa kuandaa michuano hiyo.
“Ethiopia imetuandikia na kusema hawako katika nafasi ya kuandaa michuano hiyo,” Musonye amesema na kuongeza kuwa CECAFA imekubali kujitoa kwao
“Hatuna la kufanya zaidi ya kukubali ombi la lakini tayari tumeanza kazi ya kusaka mwenyeji mpya.”
Musonye amethibtisha hilo licha ya shirikisho la soka la Ethiopia EFF kuwaandikia wakiwa wamechelewa, lakini amesema kuwa michuano hiyo itafanyika kwa tarehe iliyotajwa kati ya Novemba na Desemba na kwamba mwenyeji mpya atatangazwa wiki iyayo.
"Sudan yuko tayari akingojea hivyo michuano inaweza kuelekea Khartoum, lakini tutatangaza baadaye wiki ijayo"
Mwaka uliopita 2013 michuano hiyo ilifanyika nchini Kenya ambapo wenyeji walitwaa taji hilo baada ya kuifunga Sudan katika mchezo wa fainali uliopigwa katika dimba la Nyayo jijini Nairobi.

Hatimaye Senzo Meyiwa akiwa kwa heshima zote Afrika Kusini

South African police officers salute the coffin of Senzo Meyiwa as thousands of members of the public watch the proceedings
Maafisa wa polisi nchini Afrika kusini wakipiga saluti jeneza la marehemu Senzo Meyiwa wakati umati wa wananchi wa Afrika kusini wakifuatilia.
Police officers place his coffin, draped in the South African national flag, at the centre of the pitch
Maafisa wa pilisi wakiwa wamebeba jeneza lililofunikwa kwa bendera ya taifa ya Afrika kusini katikati ya uwanja.
Meyiwa's widow Mandisa Meyiwa (right), his father Sam Meyiwa (second from left) and mother Ntombifuthi (third from lef, attend Senzo Meyiwa's funeral in Durban South Africa, Saturday, Nov. 1, 2014. Meyiwa, captain of the national soccer team was gunned down at his girlfriend's home, east of Johannesburg, last Sunday night. (AP Photo)
Pichani anaonekana mjane wa Meyiwa Mandisa Meyiwa (kulia), baba yake Sam (wapili kutoka kushoto) na mama yake Ntombifuthi (watatu kutoka kushoto)
Meyiwa, pictured playing for his country against Congo on October 15. The goalkeeper was adored by his teammates and fans
Meyiwa, akiwa katika picha wakati akiitumikia timu ya taifa dhidi ya Congo Oktoba 15. Mlinda mlango huyo ameagwa na wachezaji wenzake na mshabikiA picture taken in January 2013 shows South Africa President Jacob Zuma (left) posing with Senzo Meyiwa during his visit to the national team in Soweto

Picha iliyochukuliwa January 2013 ikionyesha Rais wa Afrika kusininPresident Jacob Zuma (kushoto) akipiga picha na Senzo Meyiwa wakati alipotembelea timu ya taifa mjini Soweto
Mjane wa Meyiwa
MAELFU ya waombolezaji waliofurika kwenye mazishi ya aliyekuwa Nahodha na Kipa tegemeo wa timu za Orlando Pirates na ile ya taifa, Bafana Bafana walionekana wakibubujikwa na machozi huku macho yao yakiwa na rangi nyekundu wakiwa wamevalia jezi nyeusi na wengine nyekundu wakisema buriani Senzo Meyiwa katika mji wa Durban.
Huzuni ilitawala watu wakilia kwa uchungu wakimlilia mlinda mlango huyo aliye uwawa akiwa na umri wa miaka 27 ambapo jeneza lake lilizungushwa uwanjani huku watu wakipuliza vuvuzela na kuimba nyimbo za kisoka.
Wengi waliohudhuria mazishi hayo waliungana kwa pamoja ndani ya uwanja wa Moses Mabhida akiwemo mjane wa Meyiwa, wanasiasa,wachezaji wa mpira wa miguu, watu mashuhuri na maarufu na kutoa salamu zao za mwisho kwa mpendwa wao.
Meyiwa, alipigwa risasi Jumapili iliyopita, baada ya majambazi kuingia nyumbani mwa mpenzi wake karibu na Johannesburg.
Mtuhumiwa wa mauaji ya Meyiwa alifikishwa mahakamani Ijumaa na alishitakiwa kwa mauaji dhidi ya mlinda mlango huyo maarufu nchini Afrika Kusini.
Kifo cha Meyiwa kilisababisha mshituko mkubwa nchini Afrika Kusini na yameonyesha kiwango cha juu cha uahlifu wa kutumia nguvu nchini humo.
Mazishi yanafanyika katika uwanja wa mpira wa miguu wa Moses Mabhida Stadium katika mji wa Durban nyumbani kwa Meyiwa.
Senzo Meyiwa alionekana kama kivutio katika mchezo wa mpira miongoni mwa wananchi wa Afrika Kusini.
Wengi wa waombolezaji wamevaa fulana zenye picha ya Meyiwa, mtu ambaye alikuwa kivutio kikubwa kimichezo.
Mazishi ya mwanamichezo mwingine shujaa wa Afrika Kusini, bingwa wa zamani wa dunia wa mbio za mita 800 Mbulaeni Mulaudzi, pia yatafanyika Jumamosi.
Mulaudzi aliuawa katika ajali ya gari kabla ya kifo cha Meyiwa.
Rais Zuma ameamuru bendera ya taifa ipepee nusu mlingoti siku ya Jumamosi ili kumuenzi mlinda mlango huyo wa timu ya taifa.
Mechi kati ya timu za Orlando Pirates na Kaiser Chiefs katika ligi ya Afrika Kusini imeahirishwa baada ya kifo cha Meyiwa.
Senzo Meyiwa alikuwa nahodha na mlinda mlango wa timu ya Afrika Kusini, Bafana Bafana.
Mamlaka ya soka nchini humo wametangaza mchezo wa timu ya taifa ya Afrika Kusini wa kufuzu fainali za kombe la mataifa ya Afrika dhidi ya Sudan ifanyike Durban.
Polisi wamesema Ijumaa kuwa mtuhumiwa wa mauaji ya Meyiwa alitambuliwa katika gwaride la utambuzi.
Mtuhumiwa huyo, Zanokuhle Mbatha, mwenye umri wa miaka 25, anakabiliwa na mashitaka ya mauaji na ujambazi wa kutumia silaha na anatarajiwa kufikishwa tena mbele ya mahakama Novemba 11.Polisi wametangaza zawadi kwa mtu atakayewezesha kupatikana kwa taarifa zaidi kuhusu shambulio hilo ili kuwanasa watuhumiwa wengine.
Meyiwa alipigwa risasi akiwa nyumbani kwa mchumba wake huko kusini mashariki ya jiji la Johannesburg Jumapili iliyopita
Mwanamke akibubujikwa na machozi wakati wa sherehe ya kuuaga mwili wa mpendwa wao Meyiwa.

Wasichana 6000 Mtwara kunufaika mradi wa 'Hakuna Wasichoweza'

http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2014/04/IMG_8023.jpg
Wasuichana kama hawa watanufaika na mradi huo wa Hakuna Wasichoweza unaofanywa baina ya T-MARC, USAID na VODACOM FOPUNDATION
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhN8Loi_EH5sLVBuD3fb3C9loLIysbtQgYt6y-C6B5xcBZstm5QJ68mtNnwHBIUhLxaOp5WazU0UxKqLhnfj_7lpNYEzD5LtL31oaVXUYso0JFg9IlCI4zggXEHChWf6UjyO8D8doHTTW4/s1600/DSC09780.JPG
Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa T-MARC, Maurice Chirimi akizungumza na wanahabari katika shughuli zake ndani ya T MARC hivi karibuni.
JUMLA ya wasichana 6,000 mkoani Mtwara walio umri wa Balehe wapo katika nafasi nzuri ya kujikinga na mimba za umri mdogo zinazowasababishia kuacha shule pamoja na kujikinga na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi.          
Akizungumza na MICHARAZO jijini Dar es Salaam jana, Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa T-Marc Tanzania, Maurice Chirimi alisema mafanikio hayo yametokana na mradi unaojulikiana kama ‘Hakuna Wasichoweza’ unaotekelezwa na T-Marc kwa ufadhili wa Shirika la Misaada la Marekani (USAID) na Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom.
Chirimi alisema kuwa, mradi huo ulianza mwaka 2013 ambapo USAID kwa kushirikiana na Vodacom kupitia mfuko wake wa kusaidia jamii (Vodacom Foundation waliwapa nguvu ili kufanikisha mradi huo.
Alifafanua kuwa, kupitia mradi huo, T-MARC imefanikisha kutoa mafunzo kwa wasichana walio mashuleni na wasi mashuleni ikiwa na lenga la kuwapatia elimu pamoja na kuwapatia pedi wasichana wanatoka katika familia maskini kwa ajili ya kujihifadhi wakati wakiwa hedhi.
Aliongeza mafunzo pamoja na pedi za bure zimewafikia wasichana 5,232 waliopo katika shule 24 za msingi na wengine 552 wasiokuwepo mashuleni katika kata 17 mkoani Mtwara.
“Mafunzo ya namna na kujihifadhi wakati wakiwa hedhi pamoja na afya ya uzazi yanafanyika chini ya uwezeshaji wa walimu waliopewa mafunzo na wauguzi wa jadi. Kitini cha kufundishia juu ya masuala haya kimeweza kuandaliwa na T-Marc kwa kushirikiana Taasisi ya Elimu Tanzania kupitia mradi huu wa ‘Hakuna Wasichoweza’,” alifafanua
Alisema kupitia mafanikio yaliyopatikana kwenye awamu ya kwanza ya mradi, T-MARC kwa msaada wa dola za Kimarekani 166,000 itaupanua mradi na kuwafikia wasichana wengine 4,200 katika shule mpya 10 na kuongeza shirika lake litawapatia mafunzo walimu wengine 20 kwa ajili ya kuwafundisha na kuwaelekeza wasichana
Kwa upande wake, Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Rosalynn Mworia alisema Vodacom Foundation ikitambua mchango wa mwanamke katika jamii inayomzunguka kwani ukimwelimisha mwanamke ni sawasawa na kuelimisha jamii.
Alisema mara nyingi ukosefu wa elimu sahihi juu ya afya ya uzazi umekuwa ukiwafanya wasichana kuanza kuacha kuhudhuria vipindi vyao mashuleni yote hayo pia ni kwa kukosa nguo za kujihifadhi wakiwa katika siku za hedhi na kuwafanya watoto kuanza ngono wakiwa katika umri mdogo bila kujua madhara yake jambo ambalo huwasababishia mimba na kuwafanya washindwe kutimiza ndoto zao za kielimu.

Barcelona yapigwa kidude nyumbani na Celta Virgo


Celta Vigo goal
Wachezaji wa Celta Vigo wakishangilia bao pekee dhidi ya Barca
Neymar
Neymar licha ya kukukuruka kutaka kuendeleza rekodi ya mabao Barca alikwama jana kwa Celta Vigo
Lionel Messi
Messi akisikitika baada ya kukosa bao
BAO pekee lililofungwa dakika ya 55 na JoaquĆ­n Larrivey wa Celta Virgo lilitosha kuizamisha Barceona ikiwa nyumbani kwao katika pambano la La Liga lililochezwa uwanja wa Camp Nou.
Barcelona ikiwa na kikosi chake kamili walishindwa kuhimili vishindo vya wageni wao na kulala huku nyota wake Luis Suarez, Lionel Messi na Neymar wakikosa mabao mengi ya wazi wakiwa lango la wpainzani wao ambao ushindi huo nui wa kwanza kwao kenye uwanja wa Camp Nou.
Kocha Luis Enrique amekuwa akitumia mfumo wa kuwachezesha kwa pamoja washambuliaji hao watatu kwa imani ya kuifanya timu yake itishe, lakini bado mfumo huo haujazaa matunda kwani wiki iliyopita walikumbana na kipigo cha mabao 3-1 kwa Real madrid katika pambano la El Classico mjini Madrid.

Kwa kipigo hicho imeifanya Barcelona kuporomoka hadi nafasi ya tatu ikiachia usukani wa ligi mikononi mwa wapinzani wao Real Madrid yenye pointi 24 na mabingwa watetezi Atletico Madrid waliopo wa pili na pointi 23, moja zaidi ya ilizonazo wakali hao wa 'Cataluna',
Barca wana hatihati ya kuporomoka zaidi iwapo Sevilla itakayokuwa ugenini leo itashinda mechi yake dhidi ya Athletic Bilbao kwani zinalinda pointi 22, ila wenzao wana mchezo mmoja mkononi ambao unachezwa leo ambapo kama itashinda itakwea hadi kileleni ikiiengua Real Madrid.

Celta Vigo goal
Celta Vigo scored with one of only four attempts on target to win the match
Neymar
Brazil striker Neymar could not add to his record of 11 goals in all competitions for Barcelona this season
Lionel Messi
Barcelona's Lionel Messi remains on 250 La Liga goals, one behind Telmo Zarra's all-time record