STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, April 25, 2011

Tamasha la ngumi laanzishwa Dar

MABONDIA mbalimbali wakiwemo wakongwe na chipukizi wanatarajia kujumuika pamoja katika tamasha maalum la ngumi linaloanza rasmi kesho kwenye Manispaa ya Ilala, jijini Dar es Salaam.
Tamasha hilo lililoandaliwa na Taasisi ya Kinyogoli Foundation inayomilikiwa na bondia wa kimataifa wa zamani ambaye ni kocha kwa sasa, Habib Kinyogoli, awali lilipangwa kufanyika leo Jumatatu ya Pasaka, kwenye ukumbi wa Panandipanandi.
Akizungumza na MICHARAZO, mmoja wa waratibu wa tamasha hilo, Rajabu Mhamila 'Super D' alisema katika tamasha hilo, mabondia mbalimbali wakongwe na chipukizi watachuana na lengo ni kuwapa nafasi chipukizi ya kujifunza mbinu kutoka kwa mabondia hao wazoefu.
Super D ambaye pia ni bondia wa zamani na kocha wa klabu ya Ashanti, alisema yeye na Kinyogoli, wameamua kushirikiana kuandaa tamasha hilo ili kuhakikisha mchezo wa ngumi nchini unarejesha heshima yake baada ya kudorora kwa muda mrefu.
"Katika kurejesha hadhi ya ngumi nchini, tumeamua kuandaa tamasha la ngumi ambalo litakuwa likifanyika kila wiki kwenye ukumbi wa Panandi Panandi ambapo wakongwe na mabondia wanachipukia watashirikiana kupigana katika kutoa burudani," alisema Super D.
Aliongeza kuwa, mbali na michezo kadhaa ya ngumi, ikiwahusisha baadhi ya nyota wa mchezo huo kama mabondia wa ukoo wa Matumla, pia tamasha hilo litapambwa na burudani kemkem za muziki kutoka kwa wasanii ambao watakakuwa wakipokeza kwenda kutumbuiza kama njia ya kuwahamasisha watu kuhudhuria kwa wingi.

Sikinde wana mbili mpya



BENDI ya Mlimani Park 'Sikinde' imekamilisha vibao viwili ikiwa ni moja ya mikakati yake ya kujipanga upya baada ya kuondokewa na mwanamuziki wake, Shaaban Dede aliyejiunga na mahasimu wao, Msondo Ngoma.
Katibu wa bendi hiyo, Hamis Milambo, alisema kuwa bendi yao ambayo kwa wiki mbili mfululizo imekuwa kambini ikijifua, ambapo imekamilisha nyimbo mbili zilizotungwa na muimbaji wao mkongwe, Hassani Bitchuka.
"Tumeanza kujipanga upya kwa ajili ya kupakua albamu mpya na tayari tupo kambini kwa wiki ya pili sasa, ambapo tumeshakamilisha nyimbo mbili mpya zilizotungwa na Bitchuka," alisema.
Katibu huyo alisema nyimbo hizo zinazoendelea kufanyiwa mazoezi, hazijapewa majina hadi sasa na zitatambulishwa kwa mashabiki wao katika maonyesho yao ya Sikukuu ya Pasaka.
"Tutazitambulisha kwenye maonyesho yetu ya Pasaka, na hapo ndipo zitakapofahamika majina yake, ila ni kati ya nyimbo zitakazothibitisha kuwa Sikinde ni mabingwa wa muziki wa dansi nchini," alisema Milambo.
Milambo alisema baada ya maonyesho ya Pasaka, bendi yao itarejea kambini kwa ajili ya kumalizia kuzifanyia mazoezi nyimbo nyingine mpya ambazo zimeshaandikwa mashairi na waimbaji wao, Abdallah Hemba na Hassani Kunyata tayari kukamilisha idadiu ya nyimbo zinazotakiwa kwa albamu yao ijayo.
Tangu mwaka juzi, Sikinde ilipotoa albamu yao ya Supu Imetiwa Nazi, bendi hiyo haijaachia albamu nyingine zaidi ya vibao viwili vya Wanawake Wanaweza na Tunu ya Upendo vilivyotungwa na Dede maarufu kwa sasa kama 'Mzee wa Loliondo' ambaye ameenda Msondo Ngoma.

Kitabu cha Assosa chatinga mitaani





KITABU cha mwanamuziki nguli wa muziki wa dansi, Tshimanga Kalala Assosa, kiitwacho 'Jifunze Lingala' kimeingia mitaani, huku mwenyewe akijiandaa kutoa toleo la pili la kitabu hicho kinachofundisha lugha ya Kilingala na Kiswahili.
Akizungumza na MICHARAZO, Assosa, alisema kitabu hicho ambacho mbali na kufunza watu Kilingala, pia kina tafsiri ya nyimbo za wanamuziki maarufu wa Kongo na kiliingia sokoni tangu juzi huku kikigombewa kama njugu.
Assosa, alisema tangu akiingize sokoni kitabu hicho kimeshauza kopi zaidi ya 1000, huku akipokea oda kedekede toka kila pembe ya nchi kwa watu wanaokiulizia.
"Aisee kile kitabu changu nimeshakiingiza sokoni, na huwezi kuamini kimekuwa kikinukuliwa kama njugu tofauti na matarajio yangu, hali inayonifariji mno," alisema Assosa.
Mkongwe huyo aliyewahi kuzipigia bendi za Negro Succes, Orchestre Lipualipua, Fukafuka, Le Kamalee, Marquiz du Zaire, Marquiz Original, Mambo Bado, Legho Stars na sasa Bana Marquiz, alisema hakutaraji kama kingegombewa.
Alisema hakuwa na tumaini la kugombewa kwa kitabu chake kutokana na ukweli ndicho cha kwanza kwake kukitoa tangu aamue kujikita kwenye uandikaji wa vitabu, nje ya shughuli zake za muziki anaoendelea nao hadi sasa.
Aliongeza kuwa, hali hiyo unamfanya afikirie kuongeza idadi ya nakala zake, ili kukidhi mahitaji ya mashabiki wanaokiulizia ambacho ndani yake pia kina picha za wasanii wakongwe wa Kongo pamoja na yeye na familia yake.
"Kama watakuwa wanavihitaji pia wanaweza kwenda pale Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, kuna wakala anaviuza pale, au wanaweza kunipigia simu namba 0713-240735, watakipata." alisema Assosa.

Rapa wa Levent atua TOT-Plus

BENDI ya TOT-Plus ambayo sasa inaendelea na kambi yake ya mazoezi, Mwananyamala, jijini Dar es Salaam, imempata rapa mpya Dokta Steve 'Sauti ya Ng'ombe' kutoka bendi ya Levent Musica ya mjini Morogoro.
Kiongozi wa TOT-Plus, Badi Bakule, alisema rapa huyo alijiunga na tangu wiki iliyopita na anaendelea
na mazoezi kama kawaida akisubiri kutambulishwa rasmi.
"Tumemchukua rapa huyu ili kuziba nafasi ilioachwa na Jua Kali ambaye ameachana na TOT-Plus na kwenda kufanya kazi kwingine, Dokta Steve ameonyesha uwezo mkubwa hivyo anatufaa," alisema Bakule.
Bakule alisema bendi hiyo ambayo imekuwa na mazoezi kwa zaidi ya mwezi mmoja, inatarajia kutoka kambini Ijumaa Aprili 29 na kisha itajitambulisha rasmi Mei Mosi.
Alisema, rapa huyo kwa sasa amekuwa akijifua katika mazoezi makali kwenye kambi ya bendi hiyo iliopo eneo la Ujiji Mwananymala, jijini Dar es Salaam ili kuhakikisha kwamba anaibuka na vitu vipya.
"Pia tunataka azijue nyimbo zote mpya ambazo tayari tumezikalimisha na hata zile za zamani ambazo wanamuziki karibu wote wamezifanyia mazoezi kabla rapa huyu mpya hajajiunga na bendi yetu," alisema.
Kiongozi huyo alizitaja nyimbo hizo mpya kuwa ni 'Kilio cha Linda', 'Zai' 'Maisha Duni', Liwalo na Liwe','Dakika Tisa' na 'Riziki na Zengwe' ambazo baadhi yake tayari zimesharekodiwa.
Aliongeza kuwa 'Sauti ya Ng'ombe' atatoka kambini akiwa pia amemaliza kuzifanyia mazoezi baadhi ya nyimbo za zamani zilizochangia kuiweka TOT-Plus kwenye matawi ya juu.
"Kuna nyimbo kama Masimango, Mtaji wa Masikini, Elimu ya Mjinga, Mtoto Yatima, Mnyonge Mnyongeni na nyingine nyingi ambazo anatakiwa azifahamu vizuri kabla hatujatoka kambini," alisema.
Tangu imalize kampeni za Uchaguzi Mkuu mwishoni mwa mwaka jana, bendi hiyo bado haijafanya maonyesho na badala yake imeingia kambini ili kujipanga vizuri kwa ajili ya kuibuka kwa kishindo.

Stone Mayiyasika wanasa watano

BENDI ya Stone Mayiyasika 'Vijana wa Kazi' imeimarisha safu ya ushambuliaji wa jukwaa kwa kunasa wanenguaji watano akiwemo mnenguaji mahiri aliyewahi kutamba na bendi ya Twanga Pepeta, Juma Mohamed (Super Danger).
Mratibu wa bendi hiyo, Pascal Mahollelo, alisema wanenguaji hao watano wameanza mazoezi na katika maonyesho yao yote ya kusheherekea sikukuu ya Pasaka wataanza kuwatambulisha kwa mashabiki.
Alisema, mbali ya Super Danger ambaye ni mkongwe, wanenguaji wengine wapya ni wa kike na kwamba ni chipukizi ambao wameonyesha uwezo mkubwa wa kazi.
Aliwataja wanenguaji hao wa kike kuwa ni Zawadi Seif, Joselina Ngatunga (Happy), Shania Malimba na Mwanahamisi Ramadhan.
"Sisi hatuhitaji kugombana na watu ndiyo maana tumeona tuwatengeneze wetu wenyewe na nina imani mashabiki watawakubali kutokana na umahiri wao jukwaani" , alisema Mahollelo.
Alisema, utambulisho wa wanenguaji hao ungeanza kwenye maonyesho yao Sikukuu ya Pasaka.

Cloud atambia Basilisa




MSANII nyota wa filamu nchini, Issa Mussa 'Cloud', amedai filamu yake mpya ya 'Basilisa' ni funika bovu, miongoni mwa kazi zake alizowahi kuzitoa kwa hivi karibuni.
Cloud, alisema filamu hiyo iliowashirikisha wasanii kadhaa mahiri nchini, akiwemo mrembo Wema Sepetu na Ummy Wenslaunce 'Dokii', inaweza kuwa kazi bomba kwa mwaka huu wa 2011 kwa jinsi ilivyoandaliwa kwa ustadi mkubwa.
Mkali huyo aliyetamba na michezo ya kuigiza kupitia runinga kabla ya kuibukia filamu, alisema 'Basilisa' ambayo itasambazwa na kampuni ya Steps Entertainment ni bora kati ya zote alizowahi kuzitoa tangu aiingie kwenye fani hiyo.
Alisema kinachomfanya aamini hivyo ni kwa jinsi hadhithi yake ilivyo, namna alivyoshiriki na umahiri ulioonyeshwa na wasanii wenzake, acha upigaji picha wa kiwango cha hali juu na mandhari iliyotumika kurekodiwa kazi hiyo.
"Sio vibaya mtu kujisifia kwa jinsi anavyofanya kazi yake, nami naiona 'Basilisa' ni moja ya kati niliyoumiza kichwa na kushiriki kwa kiwango kikubwa, nadhani itakuwa miongoni mwa kazi bora kwa mwaka," alisema Cloud.
Msanii huyo, ambaye hushirikishwa kazi mbalimbali, alisema ndani ya filamu hiyo ameigiza katika nafasi tatu tofauti kama alivyowahi kufanya muigizaji wa Kimarekani, Eddy Murphy katika filamu yake ya 'Nutty Professor'.
Tofauti na Murphy aliyeigiza kikomedi zaidi, Cloud ndani ya filamu yake ameigiza 'siriazi' akiwa kama chizi, kiumbe wa kutisha na hali yake ya kawaida, kiasi ni vigumu kubaini kama nafasi hizo tatu tofauti zimechezwa na mtu mmoja.
Mbali na yeye (Cloud) wengine walioshiriki filamu hiyo itakayoingia sokoni mwezi ujao ni Adam Kuambiana, Dokii, Wema Sepetu, Selemani Barafu 'Mzee wa Land Rover', Single Mtambalike 'Richie', Kajala Masanja na wengineo.

Friday, April 15, 2011

Mbio za usajili zaanza Bara * Mastaa wa vigogo matumbo joto * Zilizopanda zawanyemelea







PAZIA la usajili wa wachezaji kwa timu za Ligi Kuu Tanzania Bara kwa ajili ya msimu ujao wa limefunguka kwa klabu mbalimbali kupigana vikumbo kupata saini za nyota inayowahitaji.
Ingawa, Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, halijatangaza zoezi ya usajili litaanza lini, tayari vilabu kadhaa vimeshaanza kujinadi kuwanasa wachezaji wapya na kuwafungulia milango ya kutoka wasiowahitaji kwa msimu ujao, huku Simba, Yanga na Azam zikiongoza kwenye mbio hizo.
Simba ambayo ilipoteza ubingwa kama utani kwa watani zao, imedaiwa imeshawatangazia baadhi ya wachezaji wake kuwa waangalie ustaarabu wake, huku ikiwa imeshawasainisha wachezaji kama Mwinyi Kazimoto toka JKT Ruvu, Patrick Mafisango na wengine wakiendelea kuwafukuzia.
Walioachiwa milango ya kutokea hadi sasa, ingawa haijatangazwa rasmi ni pamoja na kipa Juma Kaseja, kiungo Mohammed Banka, Mussa Hassani Mgosi, Joseph Owino, Hillary Echessa, Salum Kanoni, Anthony Matangalu, Mohammed Kijuso na David Naftal waliokuwa kwa mkopoa klabu za AFC Arusha na Majimaji Songea.
Pia katima orodha hiyo anatajwa beki Kelvin Yondan, ambaye inadaiwa yu mbioni kutua kwa mahasimu wa Simba, Yanga iliyokuwa ikimwinda kwa muda mrefu.
Inaelezwa Yanga inamtaka Kelvin kutokana na kuwepo kwa taarifa kwamba beki wake, Nadir Haroub 'Cannavaro' yu mbioni kutua Azam iliyoanza kumnyemelea tangu msimu ulioisha karibuni.
Yanga wenyewe tayari imeshawapoteza wachezaji wao wawili 'mapro', Mghana Ernest Boakye na Ivan Knezevic wanaodaiwa watakipiga msimu ujao ndani ya Azam Fc.
Ingawa, Yanga imesema inasubiri mapendekezo ya kocha wake, Sam Timbe kuimarisha kikosi chao, baadhi ya wachezaji wanaodaiwa hawatakuwa na timu hiyo msimu ujao ni pamoja na Issac Boakye wa Ghana, Nsa Job, Shamte Ally, Nelson Kimath na wengine walioonekana kuwa 'mizigo'.
Baadhi ya klabu zilizopanda daraja msimu huu zenyewe zinatajwa kuwavizia baadhi ya nyota watakaoachwa katika klabu hizo kubwa ili kuimarisha vikosi vyao kabla ya kushiriki ligi hiyo ngumu na kubwa kwa Tanzania.
Timu zilizopanda daraja toka Ligi Daraja la Kwanza ni pamoja na Villa Squad na Moro United za Dar, JKT Oljoro ya Arusha na Coastal Union ya Tanga inayorejea tena kwenye ligi hiyo.

Ligi ya Kick Boxing sasa Juni





MICHUANO ya Ligi ya Ubingwa kwa Mchezo wa Kick Boxing iliyokuwa ichezwe mwishoni mwa Machi, imesogezwa mbele hadi Juni mwaka huu.
Mratibu wa michuano hiyo, Japhet Kaseba, alisema ligi hiyo imekwama kufanyika kutokana na kutingwa na mazoezi ya maandalizi ya pambano lake la Ngumi za Kulipwa kati yake na bondia Mada Maugo.
Kaseba atapigana na Maugo, wiki ijayo kwenye ukumbi wa PTA, Dar es Salaam katika pambano lisilo na mkanda la uzito wa kilo 72 kuwania nafasi ya kupigana na bingwa wa dunia, Francis Cheka wa Morogoro.
Akizungumza na MICHARAZO, Kaseba, alisema kubanwa na mazoezi kumemfanya ashindwe kuratibu ligi hiyo na kusema, mara baada ya pambano lake atatangaza tarehe rasmi ya ligi hiyo ingawa alisema kuna uwezekano ikafanyika mwezi Juni.
"Nimeshindwa kuratibu ligi kama nilivyopanga ifanyike Machi na sasa natarajia ifanyike Juni, ingawa tarehe nitaitangaza baada ya kumaliza pambano langu dhidi ya Maugo ambalo ndilo lililonifanya niwe 'bize', nataka kumpiga nikapigane na Cheka," alisema.
Kuhusu maandalizi ya pambano hilo, Kaseba alisema anaendelea vema na ana matumaini makubwa ya kushinda pambano hilo, la raundi 10 lililoandaliwa na Double K Entertainment, litakalosimamiwa na TPBO inayoongoza na Rais wake, Yasin 'Ustaadh' Abdalla.
"Kwa kweli naendelea vema, najifua usiku na mchana kuhakikisha nakuwa fiti nimpige Maugo, ili nikavaane na Cheka kuthibitishia mashabiki wangu kuwa, sikupigwa kihalali na Cheka kwenye pambano letu la uwanja wa Uhuru," alisema Kaseba.


Mwisho

Matumla kuzichapa Dodoma




BINGWA wa zamani wa Dunia wa Ngumi za Kulipwa nchini, Rashid Matumla 'Snake Man' anatarajiwa kupanda ulingoni siku ya Pasaka kuzipiga na Mkenya, Joseph Odhiambo katika pambano litakalofanyika mjini Dodoma.
Rais wa Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania, TPBO, Yasin Abdallah 'Ustaadh', alisema pambano lisilo la ubingwa la uzani wa Middle, litakuwa la raundi 10.
Ustaadh, alisema lengo la pambano hilo ni kusaidia kuinua mchezo wa ngumi mkoani humo sambamba na kuwapelekea burudani wakazi wa mji huo ambao watakuwa wakisherehekea sikukuu ya Pasaka.
"Dodoma imekuwa ikipelekewa burudani za muziki, mpira na kadhalika, lakini mchezo wa ngumi kwa muda mrefu haujafanyika mjini humo na TPBO tumeamua kuwapelekea pambano hilo kubwa kama njia ya kuhamasisha mchezo huo na kuwaburudisha wakati wa sikukuu," alisema.
Alisema maandalizi ya pambano hilo litakalodhaminiwa na mfanyabiashara maarufu wa mjini humo, Moshi Semayu yamekamilika na watautangazia umma pambano hilo litafanyikia wapi, ingawa alikuwa na hamu lifanyike uwanja wa Jamhuri, mjini humo.
Aliongeza, baada ya pambano hilo la Dodoma, TPBO ilikuwa itafanya mipango ya kuandaa michezo mingine ya ngumi za kulipwa katika mikoa ya Mbeya, Iringa, Singida na kadhalika kwa lengo la kuuhamasisha mchezo huo katika mikoa hiyo.
Matumla, aliyewahi kuwa bingwa wa dunia wa WBU, alisema yupo fiti kumchapa Odhiambo, ili kudhihirisha kuwa yeye bado wamo katikia mchezo huo uliomjengea sifa ndani na nje ya nchi.

Wakazi wa Udzungwa kufunzwa namna ya kutunza Mbega

SHIRIKA lisilo la kiserikali la STR8 UP Vibes imeandaa warsha maalum kwa wakazi wanaoizunguka hifadhi ya Udzungwa juu ya kuwatunza wanyama aina ya Mbega wekundu wanaopatikana kwenye hifadhi hiyo.
Warsha hiyo imepangwa kufanyika hivi karibuni, mkoani Morogoro, ambapo mbali ya kuwatunza wanyama hao lakini pia itakuwa na lengo la kutoa elimu ya kuvitunza vyanzo vya maji.
Akizungumza na Mtandao huu, mratibu wa warsha hiyo, Salum Kondo alisema kuwa, wameamua kuandaa warsha hiyo ili kuwapa elimu ya kutosha watu wote wanaoishi kando kando ya hifadhi za taifa kujua jinsi ya kuwatunza wanyama na vyanzo vya maji.
Kondo, alieleza kuwa kwa kuanzia wamemua kuanza na mkoa wa Morogoro, ambapo baadaye wataaendelea kwenye mikoa mingine iliyo na hifadhi za Taifa.
"Dhumuni letu ni kuwapa elimu watu wote wanaishi karibu na hifadhi za Taifa, lakini kutokana na umuhimu wa hifadhi za Udzungwa, tumekubaliana tuanzie huko" alisema.
Aliongeza kuwa kumekuwa na ongezeko kubwa la kuwauwa Mbega Wekundu, hali ambayo inaweza kusababisha wanyama hao kutoweka kabisa Duniani.
Kondo aliongeza kuwa kwa kuwa wanyama hao hupatikana, Udzungwa pekee, wameona kuna haja ya kuwalinda kwa gharama yeyote.
"Kama wakazi wa wanaizunguka hiafdhi ya Udzungwa watapatiwa elimu ya kutosha juu ya kuwatunza wanyama hao na namna ya kuwatumia kuwaingizia kipato, bila shaka wataacha kuwaua," alisema.
Kondo alisema katika Kongamano hilo litakalofanyika mkoani Morogoro linatarajia kuwashirikisha wadau mbali ikiwa ni pamoja na wanavijiji, wataalam kutoka wizara ya Maliasili na Utalii, ambapo pia kutakuwa na burudani mbalimbali zitakazowakilisha mila na tamaduni za mkoa huo.

KITABU CHA ASSOSA CHATOKA HADHARANI




Na Badru Kimwaga
MWANAMUZIKI mkongwe wa muziki wa dansi, Tshimanga Kalala Assosa, amekamilisha kitabu chake cha tafsiri ya Lugha ya Kilingala na Kiswahili kiitwacho 'Jifunze Lingala', ambapo licha ya kufunza lugha hizo mbili pia ina nyimbo kadhaa za wanamuziki wa zamani wa DR Congo (Zaire).
Kitabu hicho kilichoanza kuandaliwa tangu mwishoni mwa mwaka jana, tayari kimeshachapishwa na mwanamuziki huyo anayemiliki bendi ya Bana Marquiz anafanya mipango ya kuanza kuvisambaza ili wadau wa muziki wa lingala na wengineo waanze kukipata.
Akizungumza na MICHARAZO, Assosa, aliyewahi kutamba na bendi mbalimbali kama 'Negro Succes', 'Le Kamalee', 'Lipualipua' na 'Fukafuka', alisema kitabu hicho ni mwanzo wa kujitosa kwenye kazi ya uandikaji vitabu wenye lengo la kufundisha lugha ya Kilingala, moja ya lugha maarufu ya Congo.
Assosa, alisema msukumo wa kuandika kitabu hicho alichochapisha nakala 50,000 za awali kama majaribio ni kutokana na simu na maombi ya mashabiki wa muziki wanaofuatilia fasiri zake katika kituo cha TBC! kinachohusu miziki ya Kavasha.
"Nilikuwa napokea simu nyingi za kuwatafsiria watu baadhi ya nyimbo za nyota wa zamani wa Zaire (sasa DR Congo) na kupata wazo la kuandaa kitabu kwa mfumo wa kamusi ambao pia una nyimbo za wakali hao na tafsiri mbalimbali za maneno ya lugha hiyo," alisema Assosa.
Mtunzi na muimbaji huyo aliyefanyia kazi bendi nyingine za 'Mambo Bado', 'Legho Stars', 'DDC Mlimani Park', 'Marquiz du Zaire' na ile ya Original, alisema mafanikio ya mauzo ya kitabu hicho kitamfanya aweze kutoa muendelezo wake siku za baadae.
Assosa, alisema shukrani pekee katika maandalizi ya kitabu hicho 'toleo la kwanza' ni kwa wanachama wa klabu ya Dar Family Kavasha na Mhariri, Joseph Kulangwa aliyekihariri hadi kuweza kuchapishwa na kuandaliwa kuachiwa mtaani wakati wowote kuanzia sasa.
Mwanamuziki huyo aliyetamba kwa utunzi wa nyimbo kama 'Minou', 'Salama', 'Huba', 'Promotion' 'Masua' na 'Abisina' alizoimba kwa kushirikiana na Nyboma Mwandido, alisema pamoja na kutaka kujitosa jumla kwenye utunzi wa vitabu, bado hajaachana na kazi ya muziki akiwa na bendi yake ya Bana Marquiz ambayo inaendeela kutumbuiza kuanzia Alhamis hadi Jumapili kila wiki.

Mwisho

KASEBA, MAUGO WAPIMA UZITO KUZIPIGA KESHO PTA






MABONDIA Japhet Kaseba na Mada Maugo pamoja na watakaowasindikiza kwenye pambano lao litakalofanyika Jumamosi, wanatarajiwa kupima uzito wao leo jijini Dar es Salaam.
Upimaji huo wa uzito utafanyika kwenye ukumbi wa Idara ya Habari-MAELEZO saa 5 asubuhi, ukihusisha pia upimaji wa afya kama moja ya kampeni ya kupambana na ukimwi michezoni.
Akizungumza na MICHARAZO asubuhi ya leo, Mratibu wa pambano hilo, Kaike Siraju, alisema mabondia wote watakaopigana Jumamosi watapimwa leo tayari kwa michezo hiyo itakayofanyika kwenye ukumbi wa PTA, jijini Dar es salaam.
Siraju, alisema mbali na Kaseba na Maugo watakaopogana kwenye pambano la kusaka mkali kati yao ili kupata tiketi ya kwenda kupigana na Francis Cheka, mabondia wengine watakaopimwa ni wale watakaosindikiza pambano hilo.
"Mabondia wanaotarajiwa kucheza siku ya Jumamosi kwenye pambano la kusaka mkali kati ya Kaseba na Maugo, watapimwa uzito na afya yao siku ya Ijumaa majira ya saa 5 asubuhi kwenye ukumbi wa Idara ya Habari-Maelezo," alisema Siraju.
Siraju, alisema maandalizi ya michezo yote ikihusisha pambano hilo la Nani Mkali la uzani wa Middle raundi 10, yamekamilika na kinachosubiriwa ni mashabiki kwenda ukumbini kupata burudani.
Michezo itakayosindikiza pambano hilo la Kaseba na Maugo, ni lile la Bingwa wa Kick Boxing wa Afrika, Kanda Kabondo atakayezipiga na Maneno Osward 'Mtambo wa Gongo', nahodha wa zamani wa ngumi za ridhaa, Joseph Martin dhidi ya George Dimoso.
Mapambano mengine ni la Yohana Robert dhidi ya Saidi Zungu, Deo Njiku atakayepigana na Issa Sewa, Fadhili Awadh atapigana na Bakari Dunda na Hassan Mandula atatwangana na Uwesu Said, Mohammed Matumla 'Snake Boy Junior' atakayeonyeshana kazi na Sadiki Momba.

Mwisho

Mafisango ambadili Humud Simba






KIUNGO aliyetua Msimbazi kwa mbwembwe na kuishia kushindwa kutamba katika timu ya Simba kutokana na majeruhi ya mara kwa mara, Abdulhalim Humoud, ametua Azam akipishana na beki Mnyarwanda Patrick Mafisango.
Humoud aliyesajiliwa na Simba msimu uliopita akitokea Mtibwa Sugar, ikiwa ni siku chache tangu ang'are kwenye pambano la kihistoria la kimataifa kati ya Tanzania na Brazil, ni miongoni mwa wachezaji wapya waliotua Azam kwa ajili ya msimu ujao.
Kwa mujibu wa taarifa za mtandao wa klabu hiyo, kiungo huyo anayependa kufananishwa na Ronaldinho Gaucho, ametua Azam akibadilishana na beki Mafisango aliyeenda Msimbazi kuimarisha kikosi chao kilichopoteza ubingwa kwa Yanga.
Wachezaji wengine wapya waliotuma Azam, ikiwa ni kati ya wachezaji 20 waliopendekezwa na kocha wao, Stewart Hall ni pamoja na aliyekuwa kipa wa Yanga,
Obren Cuckovic toka Serbia na Mwadini Ally aliyekuwa Mafunzo ya Zanzibar.
Pia wamo Waziri Salum toka Mafunzo, Ghulam Abdallah wa Chuoni Zanzibar, Zahor Pazi wa African Lyon na nyota wa Ocean View, Khamis Mcha 'Viali'.
Habari hizo zinasema kuwa hao ni sehemu ya wachezaji wapya wanaotua Azam kuungana na wachezaji wengine walioisaidia klabu hiyo kushika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara ambao wameshasainishwa mikataba mipya.
Wachezaji hao kwa mujibu wa mtandao huo ni Manahodha Ibrahim Shikanda na Aggrey Moris, Malika Ndeule, Lackson Kakolaki, Erasto Nyoni, Ibrahim Mwaipopo, Seleman Kasim Selembe, Kalimangonga Ongala, Jamal Mnyate, Mrisho Ngassa na John Bocco.
Wachezaji vijana waliokuwa wamepandishwa kwenye kikosi hicho toka timu ya vijana na kubakishwa ni Himid Mao, Salum Aboubakar na Jamal Mnyate, wakiongezewa nguvu na kipa Daudi Mwasongwe aliyepandishwa toka Azam Academy.
Makipa Vladmir Nhyonkulu na Jackson Chove pamoja na wachezaji wengine kama saba walioichezea timu hiyo wapo katika hatihati ya kuendelea kubaki katika kikosi hicho kinachosukwa kwa ajili ya kuongeza upinzani kwa msimu ujao wa ligi kuu nchini.

Mwisho

Tundaman ni Bora Tuachane tu



MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya toka kundi la Tip Top Connection, Khaleed Ramadhan 'Tundaman', ameachia kibao kipya kiitwacho 'Bora Tuachane', akiwa mbioni kufyatua wimbo mwingine akiwashirikisha Mapacha wa kundi la P Square la Nigeria.
Nyimbo hizo mbili ni maandalizi ya kufyatuliwa kwa albamu yake mpya itakayokuwa ya nne kwa msanii huyo aliyetumbukia kwenye sanaa ya muziki mwaka 2007 akitokea kwenye soka.
Akizungumza na MICHARAZO, Tundaman, alisema kibao hicho cha 'Bora Tuachane' ambacho kinatarajiwa kusambazwa hivi karibuni ni simulizi la kweli linalomhusu yeye.
"Wakati albamu yangu ya Hali Yangu Mbaya ikitamba sokoni, nimeanza maandalizi ya kufyatua albamu mpya ya nne, ambapo nimeachia ngoma inakwenda kwa jina la 'Bora Tuachane' ambao ni simulizi la kweli linalonihusu mimi mwenyewe," alisema Tundaman.
Msanii huyo, mwenye mtoto mmoja wa kike aitwae Khairat, alisema kama zilivyo nyimbo zake za nyuma, kibao hicho kipo katika mahadhi ya 'kulalamika' na kutamba kitabamba kutokana na ujumbe uliopo na midundo yake inayovutia.
Aliongeza mbali na kibao hicho, pia ana wimbo mwingine mpya ambao ataimba kwa kushirikiana na wasanii wawili mapacha wa Nigeria, P Square.
"Kibao kingine ninachokiandaa ni The All One, ambacho nimewatumia mistari P Square ili waweke sauti zao, kabla ya kuja kuchanganywa, mie nitaimba kiswahili na wao wataimba kwa lugha ya Kiingereza, lengo likiwa ni kusaka hadhi ya kimataifa," alisema.
Tundaman, aliyewahi kuzichezea timu za Friends Rangers na Yanga kabla ya kuhamia kwenye muziki, hadi sasa ana albamu tatu, ambazo ni Neila iliyomtambulisha rasmi kwenye ulimwengu wa muziki huo, Nipe Ripoti alioshirikiana na Spark na Hali Yangu Mbaya, aliyoachia hivi karibuni.

Coast Modern wapika albamu ya nne



BAADA ya kutamba na albamu yao ya 'Damu Nzito', kundi mahiri la muziki wa taarab la Coast Modern 'Watafiti wa Mipasho', limeanza maandalizi ya albamu yao mpya ya nne ikiwa imeshakamilisha nyimbo zipatazo tatu hadi sasa.
Mkurugenzi wa kundi hilo, Omar Tego 'Special One' aliiambia MICHARAZO kuwa, nyimbo tatu kati ya nne zinazolengwa kuwepo kwenye albamu hiyo ijayo zimeshakamilika kutungwa na kufanyiwa mazoezi tayari kupelekwa studio kurekodiwa.
Hata hivuo Tego alikataa kuzitaja nyimbo hizo kwa madai ni mapema mno na pia kuhofia asiibiwe 'idea' na wapinzani wake katika muziki huo wa taarab nchini.
"Tupo katika maandalizi ya kufyatua albamu yetu mpya itakayokuwa ya nne kwa Coast Modern, tayari tumekamilisha nyimbo tatu na tumesaliwa na mmoja, kuhitimisha nyimbo zitazotakiwa kabla ya kuzipeleka studio kurekodiwa," alisema Tego.
Tego alisema kwa jinsi walivyojipanga, huenda albamu hiyo ikakamilika na kuwa mitaani kabla ya Julai, kwani karibu kila kitu kimekamilisha wanachosubiri ni kuingia studio.
Alisema wataichelewesha kidogo albamu hiyo kutoka hadi Julai kwa nia ya kutoa nafasi ya albamu yao ya sasa ya 'Damu Nzito' kuendelea kutamba kwenye soko la muziki huo.
"Unajua tumeachia 'Damu Nzito' muda mfupi tu uliopita, hivyo ili kuipa nafasi ya kufanya vema sokoni, ndio maana tumepanga kuitoa albamu yetu ya nne kabla ya Julai," alisema Tego.
Kabla ya albamu hiyo ya 'Damu Nzito' kundi hilo la Coast Modern, liliachia albamu mbili zilizotikisa muziki wa mwambao nchini za 'I'm Crazy For You' na 'Kupendwa Isiwe Tabu' iliyokuwa na kibao kilichotamba cha 'Chongeni Fenicha Sio Maneno' ulioimbwa na Tego.
Aidha Tego, alisema kundi lao linaendelea kuzitambulisha nyimbo zao mpya na zile za albamu zao zilizopita katika maonyesho yao, ambapo kila Ijumaa huwa kwenye ukumbi wa Kiburugwa Inn, Mbagala na Jumamosi ufanya makamuzi yao Bashnet Hall, Mtoni Mtongani, jijini Dar es Salaam.

Mwisho

Katundu ana Nadhiri ya Mapenzi Msondo






MTUNZI na muimbaji mahiri wa bendi ya Msondo Ngoma 'Baba ya Muziki', Juma Katundu ameibuka na kibao kipya kiitwacho 'Nadhiri ya Mapenzi', ambacho kimekamilisha idadi ya nyimbo sita za albamu mpya ya bendi hiyo inayoandaliwa kwa sasa.
Akizungumza na MICHARAZO, Shaaban Dede 'Mzee wa Loliondo', alisema Msondo imeongeza nyimbo mbili mpya ambazo zinakamilisha idadi ya nyimbo za albamu yao ijayo, kikiwemo kibao chake kiitwacho 'Suluhu' na hicho cha Katundu ambacho kinaendelea kufanyiwa mazoezi.
Dede, alisema kibao chake kingine kinachokemea Dawa za Kulevya, nacho kipo tayari isipokuwa hana hakika kama kitakuwa kwenye albamu hiyo ijayo ya Msondo Ngoma, moja ya bendi kongwe ya muziki wa dansi nchini.
"Kwa kifupi ni kwamba Msondo imekamilisha nyimbo nyingine mbili mpya, moja ukiwa ni wangu uitwao 'Suluhu' na kingine kimetungwa na Juma Katundu, kinaitwa 'Nadhiri ya Mapenzi'," alisema.
Dede, aliyetua hivi karibuni katika bendi hiyo akitokea Mlimani Park 'Sikinde' alisema pamoja na kukamilika kwa nyimbo hizo sita za albamu yao ijayo, bado wanamuziki wa bendi hiyo wanaendelea kutunga vibao vingine vinavyoendelea kufanyiwa mazoezi ili vipigwe ukumbini.
"Wanamuziki tunaendelea kutunga nyimbo nyingine kwa ajili ya kudhihirisha kuwa Msondo ni Baba ya Muziki kutokana na kuundwa na wanamuziki wanaojua majukumu yao, vibao hivyo vitakuwa vikipigwa kwenye maonyesho yetu ya ndani na nje ya jijini la Dar," alisema Dede.
Msondo, iliyokuwa na desturi ya kufyatua albamu mpya kila mwaka, kwa mwaka uliopita ilishindwa kufanya hivyo kwa kile kilichoelezwa na meneja wake, Said Kibiriti, maelekezo ya wasambazaji wa kazi zao waliotaka watoe nafasi kwa albamu yao ya 'Huna Shukrani' ifanye vema sokoni.
Albamu zilizofuatana pamoja kwa miaka karibu 10 mfululizo ni 'Cheusi Mangala', 'Demokrasi ya Mapenzi', 'Ndoa Ndoana', 'Kilio cha Mtu Mzima', 'Piga Ua Talaka Utatoa', 'Kaza Moyo', 'Ajali', 'Kicheko kwa Jirani' na 'Huna Shukrani' inayoendelea kutamba iliyoachiwa mwaka juzi.

Mwalubadu: Kujituma kumenipa tuzo 2010







ANAFAHAMIKA zaidi kama 'Mwalubadu', ingawa jina lake halisi ni Athuman Mussa Masangula, mmoja wa wachekeshaji mahiri nchini ambaye kipaji chake kilianza kuonekana tangu akiwa darasa la nne katika Shule ya Msingi Mgulani, jijini Dar es Salaam.
Mwalubadu alisema alianza kushiriki maigizo shuleni kwa kuigiza sauti za walimu wake na baadhi ya viongozi maarufu, huku akishiriki pia katika uchezaji ngoma na michezo mbalimbali.
Alikiendeleza kipaji chake hata alipokuwa Shule ya Sekondari Mzalendo, iliyopo Moshi, Kilimanjaro ambapo alikuwa akikodishwa kwa ajili ya kunogesha sherehe mbalimbali za harusi na kipaimara na kuzidi kupata umaarufu zaidi hadi alipomaliza masomo yake na kurejea Dar.
Alijiendeleza kielimu kwa kusomea masomo ya IT ngazi ya cheti pale Chuo Kikuu Mlimani, kitengo cha Kompyuta, huku akijishughulisha na masuala ya sanaa kupitia kundi la Katavi lililowahi kutamba na michezo ya kuigiza kiup[itia kituo cha ITV.
Baadhi ya michezo aliyoshiriki akiwa na kundi hilo yaliyomtambulisha kwa mashabiki ni 'Jabali', 'Miale' na 'Tunduni' kabla ya kuangukia kwenye filamu akiigiza 'Copy' mwaka 2007 na kufuatiwa na nyingine zikiwemo za vichekesho zilizomjengea jina kubwa nchini.
Mwalubadu ambaye kwa sasa ni mtangazaji wa kituo cha Radio cha Ebony FM iliyopo, Iringa, alisema alijikuta akipenda sanaa ya uigizaji na hasa vichekesho kwa kuvutiwa na Steve Urkel, aliyetamba na 'Family Matters' na Brian Deacon, aliyeigiza filamu kadhaa ya Yesu.
Alisema kujibidiisha na kujifunza kwa waliomtangulia kwenye fani ndiko kulikomfanya anyakue tuzo ya Mchekeshaji Bora wa mwaka 2010, kupitia mtandao wa Filamu Central.
Mkali huyo anayependa kucheza soka, muziki na kuangalia filamu za vichekesho, alisema pamoja na mafanikio aliyoyapata kwenye fani hiyo, bado hajaridhika na anajibidiisha zaidi ili zweze kuwa msanii wa kimataifa, akimiliki kampuni yake mwenyewe sambamba na kujiendeleza kielimu.
Baadhi ya kazi za filamu alizoshiriki na kumjengea jina kubwa katika fani hiyo nchini ni pamoja na 'Sheria', 'Lango la Jiji', 'Inye' na 'Kaka Ben' za vichekesho, huku filamu za kawaida ni 'The Strangers', 'Swahiba', 'Solomba' na nyinginezo.
Mbali na kuchekesha, Mwalubadu pia ni mtunzi na mwandishi wa filamu hizo, moja ya kazi yake binafsi ni 'King Mwalubadu'.
Mkali huyo aliyezaliwa Januari 10, miaka kadhaa iliyopita akiwa mtoto wa tatu wa familia ya Mzee Mussa Masangula, alisema hakuna jambo la furaha kwake kama siku alipoanza kutangaza katika kituo cha Ebony Fm, huku tukio la huzuni ni kufiwa na baba yake mzazi, kitu alichodai akisahau.

Mwisho

Jahazi, Manchester Musica kuonyeshana kazi 'Usiku wa Naksh'

ONYESHO la 'Usiku wa Naksh Naksh wa Mwambao na Mastaa wa Muziki na Filamu', litakuwa ni pambano lisilo rasmi la kundi la Jahazi Modern Taarab na bendi ya Manchester Musica.
Kwa mujibu wa mraribu wa onyesho hilo litakalofanyika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Travertine, Abdallah Mensah, makundi hayo mawili yataonyeshana umwamba mbele ya mashabiki watakoenda kulishuhudia.
Mensah, alisema tayari makundi hayo yameshaanza kutoleana tambo juu ya kufunikana siku ya onyesho hilo, ambalo litahusisha mastaa wengine kibao wa muziki akiwemo Prince Mwinjuma Muumin, aliyepo Africana Stars 'Twanga Pepeta'.
"Japo ni onyesho la kutoa burudani kwa kushirikisha wasanii mbalimbali nyota wa muziki na filamu, lakini ni kama mpambano wa Jahazi Modern Taarab na Manchester Musica, moja ya bendi zinazokuja juu kwa sasa nchini kwenye muziki wa dansi," alisema Mensah.
Wengine watakaopamba onyesho hilo litakalofanyika Mei 8 ni pamoja na Malkia wa Mipasho nchini, Khadija Kopa, Mwanaidi Shaaban, Hassani Ally, Maua Tego, Thabit Abdul na kundi la Kanga Moja 'Ndembendembe.'
Pia wasanii wa kundi la TMK Wanaume Family, Said Fella, Said Chegge pamoja na wakali wa filamu ambao bado wameweka kapuni kwa sasa nao watajumuika pamoja kuwapa wakazi wa jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake burudani ya aina yake kwa wakati mmoja.
"Unaweza kuona mchanganyiko uliopo siku ya onyesho hilo, utakavyoweza kuwapa burudani zaidi ya moja kwa wakati mmoja, maana mbali ya taarab na dansi, pia wasanii mbalimbali wa filamu na muziki wa kizazi kipya watakuwepo kutoa burudani kabambe," alisema Mensah.
Mensah, alisema kwa sasa anahaha kusaka wadhamini wa onyesho hilo, ili kulizidishia manjonjo kabla ya kufanyika kwake.

Mwisho

Madee kudondosha nyingine



MSANII mahiri wa muziki wa kizazi kipya nchini, Hamad Ally 'Madee', anatarajia kuachia hewani ngoma nyingine mpya baada ya wiki mbili zilizopita 'kudondosha' audio na video ya kibao kipya cha 'Napeleka Benki'.
Ingawa Madee hakuweza kuweka bayana kibao kipi kitakachofuata baada ya 'Napeleka Benki', lakini alisema wiki ijayo ataachia kazi nyingine mpya wakati akiendelea na maandalizi ya kupakua albamu yake mpya na ya nne.
Kiongozi huyo wa kundi la Tip Top Connection, alisema moja kati ya nyimbo zake saba alizokamilisha itaachiwa kuzidi kuitambulisha albamu hiyo mpya itakayokuwa na nyimbo nane.
"Natarajia kuachia wimbo mwingine mpya baada ya 'Napeleka Benki', sijui itakuwa ipi kati ya 'Nisikilize', 'Siku ya Mwisho', 'Mtasubiri', 'Pendo', 'Hifla', 'Amka' au 'Siri Zote Ninazo Mimi'," alisema Madee.
Madee alisema nyimbo zote za albamu hiyo ya nne tangu alipoingia kwenye fani ya muziki zimerekodiwa katika studio mbili tofauti za MJ Production na Bongo Records chini ya watayarishaji Makochali, Master J na P Funk.
Ingawa bado hajaipa jina albamu yake ijayo iitwe vipi, lakini hiyo itakuwa ni albamu ya nne kwa Madee baada ya awali kutamba na 'Kazi ya Mola', 'Hip Hop Haiuzi' na 'Pesa'.Msanii huyo aliyesherehekea siku yake ya kuzaliwa mwanzoni mwa wiki hii, aliwahi kutangaza kutaka kustaafu muziki, ili apumzike na kujiendeleza kimasomo, lakini kwa ushauri wa watu wake wa karibu pamoja na mashabiki wa muziki aliamua kufuta wazo hilo lililokuwa alifanye mwaka juzi.

Ray kumbe ni 'Handsome wa Kijiji'

WAKATI filamu yake ya 'Second Wife' ikiendelea kutesa mitaani kwa sasa, msanii mkali wa filamu nchini, Vincent Kigosi 'Ray' amekamilisha kazi yake nyingine mpya iitwayo 'Handsome wa Kijiji', ambayo kwa mara ya kwanza ameigiza kama mtu dhalili aishie kijijini tofauti na alivyozoeleka.
Filamu hiyo iliyokamilika wiki iliyopita imerekodiwa maeneo ya Bagamoyo, mkoani Pwani, baada ya ushauri wa mashabiki wake waliodai wamechoshwa kila mara kumuoa akiigiza kama mtu tajiri anayeishia kifahari mjini, na hivyo kumlazimisha kutekeleza wazo hilo na kwenda 'bush'.
Kazi hiyo mpya ambayo imewashirikisha wakali kadhaa wa fani hiyo nchini kama Ben Blanco, Mzee Magali, Tash, Hashim Kambi, Irene Paul na wengine ipo kwenye uhariri tayari kupelekewa sokoni.
Katima ujumbe kwa mashabiki wake, Ray, amewataka amewataka wadau wa filamu kukaa mkao wa kula kushuhudia picha ya aina yake ambayo, ndani yake ameigiza kwa jina la Hamza.
"Wadau wa kiwanda cha filamu Tanzania napenda kuwafahamisha kuwa filamu yenu mpya ya kipekee na yenye manjonjo mengi sasa yakamilika," sehemu ya ujumbe wa Ray kupitia mtandao wake unasomeka hivyo.
Pia unaongeza; Nawashukuru sana kwa kuweza kufuatilia mchakato mzima wa sinema yenu ya Handsome wa Kijiji subirini sana wadau mzigo huu maana kampuni ya Rj Company imekuja tofauti kabisa na watu walivyozoea."
Filamu hiyo ni ya tatu kwa Ray ndani ya mwaka huu, baada ya awali kuachia 'Family Disaster' na kisha 'Second Wife' iliyopo sokoni kwa sasa ikiendelea kufanya vema kati ya kazi zilizotoka mwezi uliopita.

Cloud aibuka na Basilisa



MSANII nyota na mkongwe wa fani ya uigizaji nchini, Issa Mussa 'Cloud' ameibuka na kazi mpya iitwayo 'Basilisa', akitamba kuwa ni moja ya kazi itakayoziba midomo wote wanaoziponda filamu za Kitanzania.
Cloud, aliyeanza kufahamika kupitia michezo ya kuigiza iliyokuwa ikirushwa na kituo cha ITV alipokuwa na kundi la Splended, alisema filamu hiyo iliyowashirikisha wasanii kadhaa nyota nchini imeshakamilika na kwa sasa ipo foleni kabla ya kuanza kuwa mitaani.
Filamu hiyo ambayo Cloud kaigiza katika nafasi tatu tofauti imekuja wiki kadhaa tangu mkali huyo kutamba na kazi kama Ukiwa, Pigo na Suria.
Cloud alisema ndani ya filamu hiyo amefanya mambo makubwa akishirikiana na wakali wenzake kama Adam Kuambiana, Wema Sepetu, Single Mtambalike 'Richie', Ummy Weslaunce 'Dokii', Suleiman Said 'Barafu', Kajala Masanja na wengineo.
"Sitaki kujisifu, lakini naamini Basilisa ni moja ya kazi makini itakayoleta mapinduzi katika sanaa ya filamu nchini, hii inatokana na vichwa vilivyoshirikishwa ndani yake na jinsi kazi yenyewe ilivyo na ubora wake kuanzia hadithi, upigaji picha, mandhari na mengineyo," alisema Cloud.
Alisema kitu cha muhimu ni mashabiki wa filamu kukaa mkao wa kula kuishuhudia kazi hiyo mpya itakayosambazwa na kampuni ya Steps Entertainment ambayo ilivutiwa na filamu hiyo.
"Kazi yangu inatarajiwa kusambazwa na Steps na itakuwa mitaani kabla ya mwisho wa mwezi huu, hivyo wadau wa filamu wakae mkao wa kula kupata kitu roho inapenda," alisema Cloud.
Ndani ya filamu hiyo, Cloud, ameshiriki baadhi ya vipande akiwa kama kichaa, jitu la kutisha na muonekano wake wa kawaida, huku simulizi kuu la kazi hiyo mpya ni kuiasa jamii juu ya kutodharau viumbe wengine kwa jinsi ya muonekano wao.

Tshimanga Kalala Assosa: Mkongwe wa muziki asiyechuja *Ajitosa kwenye utuzi wa vitabu







SI kila wakati mipango yetu inaweza kutimia kama yalivo matarajio. Unaweza kupanga kufanya jambo fulani lakini lisitimie, na badala yake likaja lingine ambalo hukulipanga, lakini likawa na faida pengine kuliko hata lile la awali.
Hivi ndivyo ilivyotokea kwa msanii wa muziki Tshimanga Kalala Assosa, ambaye hakuwahi kufikiria katika maisha yake kama ingetokea siku akawa mwanamuziki.
Malezi kutoka kwa wazazi wake wakati akiwa mdogo, yalimpa mwanga wa siku moja kuja kuwa mtumishi wa kiroho-padri.
Lakini baba yake aliyemlea kwa kipindi chote akiwa mdogo, naye alikuwa na mtazamo tofauti juu nini atakachokuja kukifanya mwanae.
Yeye (mzazi) alipenda sana mtoto wake aje kuwa daktari wa binadamu, lakini kumbe yote hayo hakuna lililotimia. Assosa ametua kwenye sanaa ya muziki.
Assosa ni mmoja wa wakongwe wa muziki wa dansi aliyeng'ara barani Afrika kupitia bendi kadhaa za Kongo (zamani Zaire) kama Negro Succes, Lipualipua, Fukafuka na Marquis du Zaire.
"Nilipokuwa mdogo mjini Kamana, Jimbo la Katanga, nilifanya kazi kanisani na kutamani kuwa Padri, wakati baba mzazi yeye alitaka nisome zaidi ili niwe daktari," alisema.
Assosa, maarufu kama 'Mtoto Mzuri', alisema alivutwa kwenye muziki kwa nyimbo za wakali wa zamani wa Kongo kama Franco, Vicky Longomba na Kabasela Joseph.
Ladha na utamu wa muziki wao ulimfanya asitishe mipango ya kusomea zaidi taaluma na kujiingiza kwenye elimu ya muziki akiwa darasa la 5.
Alianza kuimba kanisani, shuleni na baadaye mitaani akipigia bendi ndogo ndogo za mjini Kamana, kabla ya kuhamia Kinshasa katikati ya 1960 alipokutana na Bavon Marie Marie aliyemchukua katika bendi yake ya Negro Succes.
"Nilipata taabu sana kupata mafanikio ndani ya Negro Success kwa vile sikujua vema lugha ya Lingala. Nashukuru Bavon aliyenisaidia mpaka alipofariki kwa ajali ya gari mwaka 1970, na mimi kuhamia Lipualipua nikiwa na Nyboma Mwandido," alisema.
Makundi mengine aliyopitia mkali huyo aliyejitosa kwenye Uandishi wa Vitabu kwa sasa, akiwa ameachia kitabu kiitwacho 'Jifunze Lingala', ni Le Kamalee, Fukafuka, Marquiz du Zaire kabla ya kuja nchini na kupigia bendi mbalimbali.
Baadhi ya bendi alizopigia nchini ni DDC Mlimani Park, Makassy Band, Mambo Bado, Marquiz Original, Legho Stars kabla ya kuanzisha bendi ya Bana Marquiz inayotamba hadi sasa jijini Dar es Salaam.
Assosa alisema japo anasikitika kushindwa kuwa Padri, bado anashukuru fani ya muziki imemsaidia kwa mengi, ikiwemo kumudu maisha, akisomesha watoto na kuitunza familia yake, mbali na kufahamika na kumiliki mali ambazo hakupendwa zitajwe.
"Sio siri muziki umenisaidia kwa mengi na siwezi kuacha mpaka mwisho wa maisha yangu. Nimejikita kwenye uandishi wa vitabu, lakini haina maana ndio mwisho wangu wa muziki."
Mkali huyo, alizaliwa miaka 60 iliyopita akiwa mtoto wa pili kati ya nane, ameoana na Evangeline Paul Kimiti na kupata naye watoto.
Mkali huyo, alisema ameingia kwenye uandishi wa vitabu baada ya kuona Watanzania wengi wanapenda kujifunza Kilingala kwa kuzipenda nyimbo za Kongo.
"Nimeanza na 'Jifunze Lingala' ili kukidhi maombi ya mashabiki wa nyimbo za Lingala waliotaka tafsiri ya mashairi yake, ila nipo mbioni kutoa vingine ili niwasaidie wale wanaotaka kujifunza lugha hiyo," aliongeza.
Assosa anayependa kula Ugali kwa Kisamvu na Uyoga, aliwahi kucheza soka kama kiungo alipokuwa St Luhanga Seminary.
Assosa ni shabiki wa Manchester United, na mpenzi mkubwa wa mavazi ya rangi nyeupe na nyeusi. Hatumii kilevi.
Assosa, aliyetikisa Afrika na vibao kama Masua, Abisina, alichokitunga na kuimba na Nyboma, kabla ya mwenzake kumuomba akimiliki, alisema tukio la furaha kwake ni siku alipoanza kuwa na familia, huku akihuzunishwa na vifo vya wanamuziki wenzake.
Mtunzi na muimbaji huyo, alisema licha ya kutunga vibao vingi, kibao cha Bomoa Tutajenga Kesho alichotunga akiwa Mambo Bado, ndicho anachokikumbuka zaidi kwa jinsi kilivyomtia misukosuko na serikali ya awamu ya kwanza miaka ya 1980.
Assosa alisema japo alitunga kibao hicho bila ya maana yoyote zaidi ya kutoa burudani mashabiki wao, ulitafsiriwa vibaya na serikali ya Julius Nyerere kiasi cha kufikia kupigwa marufuku kwa kuonekana unachochea 'ufisadi'.
Kibao hicho alichotunga mwaka 1983, kina mistari isemayo 'Bomoa ee Bomoa ee Bomoa aa mamaa tutajenga kesho ooh i maee Oo Beti mayaiee ooh maax2'
Assosa, alisema kama angekutana na Rais angemuomba awe mkali kwa wanaoichezea amani na kutaka kuleta vurugu nchini.
"Rais awe mkali kwa wanaoichezea amani na utulivu wa nchi, machafuko na vita ni mambo mabaya, wanaovishabikia hawajui madhara yake," alisema.
Assosa aliyeitungia DDC Mlimani Park kibao cha 'Gama Nihurumie', alisema muziki wa Tanzania hautambi kama zamani kwa sababu ya uvivu wa wasanii wa sasa na bendi zote kupiga muziki unaofanana wakiiga toka Kongo.
"Zamani ilikuwa rahisi kujua miondoko ya Msondo, Sikinde, Marquiz au OSS, kwa vile zilikuwa zikipiga mirindimo yao, kwa sasa bendi zote zinapiga muziki wa aina moja wakiiga nje, ndio maana muziki wetu hautambi kimataifa," alisema.
Alisema jambo hilo lipo hata Kongo, kwa JB Mpiana, Koffi Olomide, Werrason, Ferre Gora na Fally Ipupa kutojitofautisha kama ilivyokuwa kwa akina Tabu Ley au Franco na African Jazz waliowapagawisha wazungu.

Mwisho

BOB JUNIOR AMCHAMBUA DIAMOND



MWIMBAJI na mtayarishaji wa muziki wa Bongo Fleva kutoka kundi la ‘Masharobaro’, Bob Junior ‘Rais wa Masharobaro amesema kuwa sababu ya msanii, Nasib Abdul ‘Diamond’ kukosa tuzo mwaka huu inasababishwa na kujikweza kwake.
Alisema Dimond baada ya kupata tuzo tatu mwaka jana amekuwa anajisikia na kujiona huku akitafuta wanawake wenye sifa mbaya ili aweze kuandikwa.
Bob Junior ambaye ndiye alitayarisha albamu ya msanii huyo ya kwanza alisema kuwa sifa zinamfanya msanii huyo kushindwa kufanikiwa katika tuzo za mwaka huu.
“Msanii huyo amekuwa akinitafuta hata mimi na kufikia kunilalamikia kuwa namuongezea fedha za kutengenezea nyimbo, kitu ambacho ni maamuzi ya kiofisi.
Alisema kuwa ukiachilia suala la kuchukua jina lake la Rais wa wasafi akibadilisha jina lake la rais wa masharobaro ambalo lina maana hiyo kwa sasa amekusanya genge kwa nia ya kumfanyia kitu kibaya, hali iliyomfanya atoe taarifa kituo cha polisi
http://mamapipiro.blogspot.com/