STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 3, 2015

'Mauro Icardi hang'oki Inter Milan ng'o'

http://gilabola.com/wp-content/uploads/2015/03/icardi.gifMKURUGENZI wa michezo wa Inter Milan, Piero Ausilio amesisitiza kuwa hata Euro Mil. 40 hazitarajiwa kutosha kumng’oa Mauro Icardi katika klabu hiyo.
Icardi mwenye umri wa miaka 22 amekuwa katika kiwango kizuri msimu huu akiwa amefunga mabao 14 katika mechi 24 za Serie A walizocheza.
Hata hivyo, pamoja na vilabu mbalimbali kuanza kumuwinda nyota huyo, Inter inamuona kama mchezaji muhimu kwao na hawana mpango wowote wakumuuza hivi sasa.
Ausilio amesema kwasasa wanatengeneza timu ambayo itadumu kwa kipindi kirefu hivyo hawana mpango wa kuuza wachezaji wao muhimu wanaochipukia.
Strika huyo wa kimataifa wa Argentina ambaye amewahi pia kucheza katika timu za Sampdoria na Barcelona ana mkataba na Inter unapomalizika Juni mwaka 2018.

Shamsa Ford ataka ubunifu zaidi Bongo Movie

WASANII waigizaji nchini wameaswa kuwa wabunifu na kuumiza vichwa kutengeneza kazi za kipekee ili kujitofautisha na pia kulenga kujitangaza kimataifa.
Wito huo umetolewa na muigizaji nyota nchini Shamsa Ford ambaye amesema bila ubunifu na kutoa kazi za kipekee ni vigumu wasanii watanzania kujitangaza katika anga la kimataifa.
Shamsa alisema hata yeye alifikiria na kujaribu kuibuka kivyake vyake katika simulizi la 'Chausiku' ambayo imemjengea jina hata kwa wale ambao siyo mashabiki wa filamu.
"Ubunifu ndiyo siri ya mafanikio, hata mimi niliumiza kichwa kuja na filamu ya 'Chausiku' kwa nia ya kujitofautisha na ninashukuru kazi ilipokelewa vema kiasi kwamba kwa sasa nimepata changamoto ya kutoa kazi nyingine itakayovutia kama hiyo au zaidi," alisema.
Shamsa alisema kwa kuonyesha hakubahatisha kwa sasa yupo katika maandalizi ya kuja na filamu ya 'Mama Muuza' ambayo imebeba uhalisia wa maisha ya uswahili yaliyozoeleka.
"Hakuna njia ya mkato katika mafanikio na hata soko la kimataifa ni ubunifu na kutoa kazi ya kipekee, ili hata zikishindanishwa ijitofautishe," alisema Shamsa.

Nahodha John Terry kuzeekea Chelsea

http://static.goal.com/87600/87660.jpg
John  Terry
NAHODHA wa Chelsea, John Terry amesisitiza amebakisha miaka michache katika timu hiyo huku akidai hana mpango wa kucheza popote baada ya hapo.
Beki huyo wa kati wa vinara hao wa Ligi Kuu ya England ambaye mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu, alifunga bao la kwanza katika ushindi wa mabao 2-0 waliopata katika mchezo wa fainali ya Kombe la Ligi dhidi ya Tottenham Hotspurs Jumapili iliyopita.
Terry amesema kama huu ndio utakuwa mwaka wake wa mwisho katika soka anataka kuumaliza kwa mafanikio.
Nyota huyo aliendelea kudai kuwa kwasasa klabu ndio itakayoamua juu ya mustakabali wake kama aendelee au la, lakini hana mpango wa kwenda popote kwingine.
Chelsea inayoongoza msimamo wa Ligi Kuu kwa tofauti ya alama tano wanasafiri kuifuata West Ham United kesho katika moja ya mapambano yatakayochezwa leo, ingawa kwa leo kuna michezo mingine mitatu itachezwa usiku katika mfululizo wa ligi hiyo inayozii kushika kasi.

Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin

Staa wa Sunderland matatani kwa ngono

http://www2.pictures.zimbio.com/gi/Adam+Johnson+Sunderland+v+Carlisle+United+ccdTvhuGA5Tl.jpg
MCHEZAJI wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Sunderland, Adam Johnson amekamatwa na polisi kwa tuhuma za kufanya ngono na msichana wa umri wa miaka 15.
Katika taarifa ya polisi , Johnson mwenye umri wa miaka 27 alikamatwa kwa tuhuma hizo za kujihusisha kimapenzi na msichana mwenye umri chini ya miaka 16 lakini ameachiwa kwa dhamana.
Klabu hiyo imedai kuwa kwasasa wamemsimamisha mchezaji huyo ili kupisha uchunguzi wa polisi unaoendelea.
Johnson aliibuka kutoka katka shule ya soka ya klabu ya Middlesbrough akiwa na umri wa miaka 17 mwaka 2005 katika mchezo wa Kombe la UEFA.
Kabla ya kujiunga na Sunderland mwaka 2012 Johnson alikuwa ametokea kwa mabingwa wa Ligi Kuu Manchester City.

Ujenzi Rukwa, Volcano zashushwa daraja

TIMU za Ujenzi Rukwa na Volcano FC ya Morogoro zimeshushwa madaraja mawili hadi ligi za wilaya baada ya kushindwa kufika uwanjani kwenye mechi zao za Ligi Daraja la Pili (SDL).
Uamuzi huo umefanya na Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana jana jijini Dar es Salaam kupitia ripoti za matukio mbalimbali ya ligi hiyo.
Ujenzi Rukwa ilishindwa kwenda Kigoma kuikabili Mvuvumwa FC ya huko wakati Volcano FC haikutokea kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya ambapo ilitakiwa kucheza na Wenda FC.
Uamuzi wa Kamati ya Mashindano umefanywa kwa kuzingatia Kanuni ya 27 ya SDL ambapo mbali ya kushushwa madaraja mawili, lakini pia timu hizo zimepigwa faini ya sh. milioni moja kila moja. Vilevile matokeo yote ya mechi zao kwenye Ligi hiyo yamefutwa.
Nayo Singida United imepewa ushindi wa pointi tatu na mabao matatu baada ya Ujenzi Rukwa kubainika kumchezesha mchezaji asiyestahili (non qualified) kwenye mechi iliofanyika Februari 8 mwaka huu kwenye Uwanja wa Mandela mjini Sumbawanga na timu hizo kutoka sare ya bao 1-1.
Mchezaji Emmanuel Elias Mseja wa Mbao FC amepigwa faini ya sh. 100,000 na kufungiwa mechi tatu baada ya kukojoa uwanjani kwenye mechi dhidi ya AFC iliyochezwa Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha.
Pia viongozi wa Mbao FC, Abdallah Chuma (Daktari) na Meneja Yasin Abdul wamefungiwa miezi sita na faini ya sh. 100,000 kila mmoja kwa kumtukana na kumtishia maisha Kamishna wa mechi hiyo.
Nayo klabu ya AFC imepigwa faini ya sh. 300,000 kutokana na washabiki wake kuifanyia vurugu timu ya Bulyanhulu FC kwenye mechi yao iliyofanyika Februari 7 mwaka huu Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid na kumalizika kwa sare ya bao 1-1.
Timu ya Magereza Iringa imepigwa faini ya jumla ya sh. 200,000 kwa kuchelewa kufika kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (pre match meeting), na uwanjani kwenye mchezo wao na Njombe Mji uliochezwa Februari 21 mwaka huu. 

Naye mchezaji wa timu Amasha Mlowasa amefungiwa mechi tatu na faini ya sh. 100,000 kwa kumtukana mchezaji mwenzake kwenye mechi hiyo.