STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 17, 2014

Si Uchawi! Kiatu chako kinaweza kukujulisha umri wako!!


EBU jaribu mwenyewe uone kisha nicheki kwenye micharazomitupu@yahoo.com au wakuzataboy@yahoo.com
1: Andika namba ya kiatu chako.

2: Zidisha kwa5.

3: Jumlisha 50

4: Zidisha kwa 20 ...

5: Jumlisha 1013 

6: Toa mwaka uliozaliwa....

7: Namba ya kwanza ni size ya kiatu, na namba mbili za mwisho ni miaka yako.

Waliopenya maboresho Taifa Stars kutajwa leo

Rais wa TFF, Jamal Malinzi
MCHAKATO wa ung’amuzi wa vipaji kwa ajili ya maboresho ya timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, ulioshirikisha wang’amuzi wa vipaji zaidi ya 40 umekamilika jana na majina ya nyota hao yataanikwa kesho Jumatatu.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura, wachezaji hao watafanyiwa vipimo vya afya kabla ya kuingia kambini Tukuyu, Mbeya na watakaoingia kambini ni wale watakaokuwa wamefaulu vipimo.
Wang’amuzi wa vipaji waliokuwa Lushoto ni Abdul Mingange, Ayoub Nyenzi, Boniface Pawasa, Charles Mkwassa, Dan Korosso, Dk. Mshindo Msolla, Edward Hiza, Elly Mzozo, Hafidh Badru, Hamimu Mawazo, John Simkoko, Jonas Tiboroha, Juma Mgunda na Juma Mwambusi.
Kanali mstaafu Idd Kipingu, Kenny Mwaisabula, Kidao Wilfred, Madaraka Bendera, Madaraka Selemani, Mbarouk Nyenga, Mohamed Ally, Mussa Kissoky, Nicholas Mihayo, Pelegrinius Rutayuga, Peter Mhina, Salum Mayanga, Salvatory Edward, Salum Madadi, Sebastian Nkoma, Sekilojo Chambua, Selemani Jabir na Shabani Ramadhan.
Wengine ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho hilo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi, Kidao Wilfred na Ayoub Nyenzi ambaye mbali ya kuwa  mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho hilo, pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Vijana.
Yumo pia Kaimu Mkurugenzi wa Ufundi, Salum Madadi na Mshauri wa Rais (Ufundi), Pelegrinius Rutayuga.
Mkakati huo umebuniwa na TFF kwa lengo la kupata nyota wa kujumuishwa katika kikosi cha sasa cha Stars inayokabliwa na kampeni ya kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa Afrika (AFCON), zitakazochezwa mwakani nchini Morocco.

Tusiruhusu ushoga nchini ni kama kumbeep Mungu-Sheikh aonya


http://bloggerimports.files.wordpress.com/2008/12/img_2954-raisidd.jpg?w=640
Sheikh Mohammed Muhenga
SERIKALI imeombwa kufuata nyayo za serikali ya Uganda chini ya Rais Yoweri Museveni kwa kuktaa kuruhusu ushoga.
Serikali imeombwa kufuata nyayo za serikali ya Uganda chini ya Rais Yoweri Museveni kwa kukataa kuruhusu ushoga licha ya kuziudhi nchi za magharibi zinazokingia kifua vitendo hivyo.
Ombi hilo limetolewa na Imamu wa Msikiti wa Mwembechai, Sheikh Mohammed Muhenga, alipokuwa akiwahutubia waumini kabla ya swala ya Ijumaa iliyoswaliwa msikiti hapo, jijini Dar es Salaam.
Imamu Muhenga alisema kitendo cha Watanzania kunyamazia na kukumbatia matendo maovu yanayomchukiza Mungu vinaweza kuzua balaa kwa taifa.
"Tushirikiane kukemea maovu, tusinyamazie matendo yanayomchukiza Mungu kwani hakuna anayeweza kuhimili ghadhabu za Mungu akiamua kutuadhibu,"alisema .
Sheikh huyo alisema vitendo vya ulevi, biashara ya watu kujiuza, ujambazi na matendo mengine kwa kisingizio cha kukabiliana na hali ngumu ya maisha vinapaswa kuepukwa kwa nguvu zote.
"Huku ni sawa na kumbeep Mungu, je akiamua kutupigia tupo tayari kuhimili ghadhabu yake, tukemee maovu na kukemea kwani Mtume Muhammad (Sallallah Aley Wasalam) anasema miongoni mwa dalili 10 za kiama ni umma wake kugeuza pombe kuwa chai, watu kurejea enzi za Kaum Lut," alisema.
Sheikh alisema matendo vya ushoga na maovu mengine ni kuvuka mipaka kwa wanadamu ya uumbaji na humchukiza Mungu, hivyo ni wajibu wa kila mtu kukemea na kuyakataa matendo hayo.
Hivi karibuni Uganda ilipitisha sheria kali dhidi ya vitendo vya ushoga na kukera nchi ya Marekani na washirika kwake ambao wameruhusu vitendo hivyo katika nchi zao licha ya kwenda kinyume na mafundisho ya kidini.

Maafa! Nane wafa mgodini wakichimba dhahabu

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEheVO-yFu1eXU8rBz8T2or-Ju6EDw0WANzohJuqwB-gznjg64LLdt457Xp3Hknvz8ecoigpuV9P6NtgqOga42ZkUv0ap58cBWwGAEyWC2RU0eLeNz3Itb98lPeBA-njALSgerp4-BhmQsOR/s1600/Geita+gold+mine+1.jpg
Picha haihusiani na habari, ila wanaoonekana ni Vijana wakiwa machimboni
WATU wanane wamefariki dunia na moja kunusurika katika machimbo  madogo ya dhahabu yaliyopo vijiji cha Kalole na Nyangalaya kata ya Lunguya  wilayani Kahama, Shinyanga baada ya kuangukiwa na vifusi.
Ofisa Mtendaji wa kijiji cha Kalole, Furaha Mashamba, alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 5:00 usiku wakati wachimbaji hao wakiendelea kuchimba dhahabu.
Alisema katika matukio hayo, watu saba walikufa katika machimbo ya kijiji cha Kalole na mmoja   machimbo ya Nyangalata.
Mashamba alisema kuwa baada ya tukio hilo, wakazi wa kijiji hicho walipewa taarifa na kwenda eneo la tukio kujaribu kuwaokoa, lakini ilishindikana.
Hata hivyo, kwa mujibu wa mtendaji huyo, mmoja wa wachimbaji aliokolewa akiwa hai.
Aliwataja waliofariki ambao ni wakazi wa kijiji cha Kalole kuwa ni Mwadogo Kibasi Kiaka (26), Juma Malingaya (30), Charles Iheyolo (21), Roma Masolwa (26), Juma John (33), Paul James (24), Ngaleba Kacheyekele (24) na Daudi John wa kijiji cha Nyangalata Alimtaja aliyenusurika kuwa ni Michael Pius (43) mkazi wa Morogoro.
Ofisa Mtendaji huyo alisema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mashimo hayo kutokuwa na usalama wa kutosha na maji kuingia kutokana na mvua za masika zinazoendelea kunyesha wilayani Kahama.
Kwa upande wake, Ofisa Madini wilayani Kahama, Amir Chande, alisema kuwa machimbo ya kijiji cha Kalole yalishafungwa muda mrefu, lakini wachimbaji wamekuwa wakiyavamia kuendelea na uchimbaji kinyemela.
Chande alitoa agizo kwa wachimbaji ambao bado wapo eneo hilo kusitisha kazi hiyo haraka hadi hapo serikali itakapotoa maelekezo mengine.
“Mnaoendelea kuchimba mpo hapa kimakosa na kwa sababu hakuna mwenye leseni hapa ya uchimbaji wa madini, ni makosa kufanya kazi hii ya uchimbaji na kuanzia sasa machimbo  tunayafunga kwa usalama wenu,” alisema Chande.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Evarist Mangala, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kueleza kuwa miili ya wachimbaji hao imetambuliwa na kuchukuliwa na ndugu zao kwa mazishi.
CHANZO: NIPASHE

PSG haishikiki Ufaransa, Zlatan nouma!



Cruising: Ibrahimovic scored twice in the first-half to restore PSG's eight point lead at the top of the table
Oyooooooo! Zlatan akishangilia bao
PSG inaelekea kutetea taji lake la ubingwa wa Ligue 1 nchini Ufaransa baada ya usiku wa jana kupata ushindi wa mabao 2-0 nyumbani dhidi ya St Etienne.
Mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic 'Acadabladabla' ndiye aliyefunga mabao hayo na kuipa PSG ushindi wa saba mfululizo kwenye mashindano yote.
Wapinzani wao wa karibu, Monaco nao jana waliendelea kupata ushindi na kuwafukuza wapinzani wao kwa kuizabua Lyon kwa mabao 3-2.
PSG inayotetea taji la ligi hiyo inaendelea kuongoza msimamo kwa tofauti ya pointi nane ikiwa na pointi 70 huku Monaco wakiwafuata kwa mbali wakiwa na 62.

Hii ilitokea Kitonga baada ajali ya malori mawili


Baadhi ya abiria wa kutoka sehemu mabalimbali wakisubiri lori lililoziba barabara kuondolewa baada ya kupata ajali ya kugongana na lori jingine kwenye mlima Kitongo. Ajali hiyo imesababisha magari mengi kuweka kambi kwa muda wa zaidi ya saa nne.

Lori likiwa limetumbukia kwenye korongo mlimani kitonga

Lori la mafuta lililopo upande wa kulia na lori la mizigo lililopo upande wa kulia yaligongana na kuziba barabara kwenye mlima kitonga na kusababisa magari mengine kukwama kwa zaidi ya saa manne



Jana tulilazimika kufanya utalii ndani ya mlima kitonga baada ya kukwama kwa zaidi ya masaa manne