STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 15, 2017

Manchester City aibu tupu, wapigwa 4-0

Picha zote kwa hisani ya Mirror
AIBU tupu. MANCHESTER City jioni hii imekumbana na aibu kubwa baada ya kutandikwa mabao 4-0 na Everton kwenye uwanja wa Goodson Park, mjini Liverpool.
City inayonolewa na Kocha Pep Guardioala kwa kipigo hicho imesalia nafasi ya tano ya msimamo na ikiwa katika hati hati ya kuzidiwa maarifa na watani zao wa Jiji la Manchester, Man United iwapo itafanikiwa kuifunga Liverpool kwa idadi kubwa ya mabao, kwani zinaweza kulingana na kuzidiana uwiano wa mabao.
United ina pointi 39 na mabao 31 ya kufunga na kufungwa 19 wakati City kwa kipigo cha jioni hii imesaliwa na pointi 42 na mabao 41 ya kufunga na kufungwa 26, ikiwa na maana wana uwiano tofauti na mabao matatu tu mpaka sasa.
Mabao yaliyoiangamiza City leo ikiwa kiigo chao cha tano msimu huu yalitumbukizwa na Romelu Lukaku dakika ya 34, Kevin Mirallas dakika 47', Tom Davies dakia ya 79 na chipukizi Ademola Lookman aliyefunga dakika za nyingeza za mpambano huo mkali ambao umemfanya Guardiola kujikuta kwenye simanzi kubwa.
Muda mchache ujao Man United itakuwa wenyeji wa Liverpool kwenye Uwanja wa Old Trafford, kwenye mchezo wao wa kwanza wa Ligi Kuu msimu huu timu hizo zilishindwa kutambiana kwa kutofungana. Mechi ilichezwa Oktoba 17, 2016.

Mbao, Lyon zashindwa kutambiana kesho zamu ya Toto v Prisons

Mbao FC
Lyon
Na Mwandishi Wetu
KLABU za Mbao FC na wageni wao African Lyon zimeshindwa kutambia kwenye mfululizo wa mechi za Ligi Kuu Bara baada ya kutoka suluhu.
Timu hizo zimeshindwa kufunga kwenye mchezo uliopigwa Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na kuzifanya zigawane pointi moja moja.
Kwa matokeo hayo zimezifanya timu hizo kuendelea kusalia katika nafasi zao walizokuwa kabla ya mchezo huo uliomalizika hivi punde.
Lyon imefikisha pointi 21 na Mbao imekusanya alama 20, lakini zimeshindwa kusogea katika maeneo waliyokuwapo.
Ligi hiyo itaendelea tena kesho Jumatatu kwa mchezo mmoja kati ya Toto African na Prisons jijini Mwanza na Jumanne Yanga itakuwa wageni wa Majimaji Songea na Jumatano Simba na Azam zitashuka viwanja tofauti vya mjini Morogoro na Dar es Salaam.
Simba itakuwa mgeni wa Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri, Morogoro wakati usiku wa saa 1 jioni, Azam itakuwa wenyeji wa Mbeya City kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi pembezoni mwa jiji la Dar es Salaam.
Simba ndio vinara wa Ligi Kuu mpaka sasa ikiwa na pointi 44 baada ya kushuka uwanjani mara 18, ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 40 na Kagera Sugar kushika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 31 ikiiengua Azam iliyoshuka nafasi ya nne na pointi zao 30.

Msimamo wa Ligi Kuu Bara

                                P  W   D  L   F   A  Pts
1. Simba                   18 14  2   2  30  6  44
2. Yanga                   18  12  4   2  39  9  40
3. Kagera Sugar        19  9   4   6   21 18 31
4. Azam                    18  8   6   4  23  15 30
5. Mtibwa Sugar        18  8   6   4  22  19 30
6. Stand Utd             19  6   7   6  18  16  25
7. Mbeya City            18  6   6   6  16  16  24
8. Ruvu                    19   5   9   5  18  20  24
9. Prisons                 18   5   7   6  10  13  22
10.Mwadui                19   6   4   9  16  24  22
11.African Lyon         19   4   9   6  11  16  21
12.Mbao                   19   5   5   9  17  24  20
13.Ndanda                19  5   4  10  15  26  19
14.Majimaji               18  5   2  11  13  26  17
15.Toto Africans         18  4   4  10  11  20  16
16.JKT Ruvu              19  3   9   7   7   17   15

Wafungaji:   

9- Shiza Kichuya                             (Simba)
     Simon Msuva                             (Yanga)   
     Amissi Tambwe                         (Yanga)
8- Abdulrahman Mussa  (Ruvu Shooting)
    Mbaraka Yusuf              (Kagera Sugar)
7- Rashid Mandawa         (Mtibwa Sugar)
    Donald Ngoma                           (Yanga)
    John Bocco                               (Azam)
6- Mzamiru Yasin                           (Simba)
    Haruna Chanongo        (Mtibwa Sugar)
5- Omar Mponda                         (Ndanda)
    Obrey Chirwa                             (Yanga)
    Riffat Khamis                           (Ndanda)
    Victor Hangaya                        (Prisons)
    Rafael Daud                      (Mbeya City)
    Venance Joseph              (African Lyon)
4-Peter Mapunda                      (Majimaji)
    Kelvin Sabato                (Stand United) 
    Laudit Mavugo                          (Simba)
    Marcel Boniventure             (Majimaji)
    Boniface Maganga                     (Mbao)
    Deus Kaseke                              (Yanga)
    Shaaban Kisiga            (Ruvu Shooting)
    Mohammed Ibrahim 'MO'        (Simba)   
    Tito Okello                       (Mbeya City)
3- Hood Mayanja                (African Lyon)
    Ibrahim Ajib                               (Simba)
    Abdalla Mfuko                        (Mwadui)
    Subianka Lambert                   (Prisons)
    Ditram Nchimbi                (Mbeya City)
    Wazir Junior                    (Toto African)
    Issa Kanduru               (Ruvu Shooting)
    Ally Nassor 'Ufudu'       (Kagera Sugar)
    Kelvin Friday                 (Mtibwa Sugar)
    Mfanyeje                                 (Majimaji)
    Francisco Zukumbawira             (Azam)
    Shaaban Idd                                 (Azam)
    Jamal Mnyate                             (Simba)
   Jamal Soud                  (Toto Africans)
    Adeyum Saleh               (Stand United)
    Jacob Massawe             (Stand United)
2- Adam Kingwande          (Stand United)
    Samuel Kamuntu                  (JKT Ruvu)
    Vincent Philipo                            (Mbao)
    Mcha Khamis                               (Azam)
    Danny Mrwanda            (Kagera Sugar)
    Pastory Athanas           (Stand United)
    Paul Nonga                             (Mwadui)
    Fully Maganga           (Ruvu Shooting)        
    Themi Felix                  (Kagera Sugar)
    Mudathir Yahya                        (Azam)
    Atupele Green                    (JKT Ruvu)
    Jerry Tegete                          (Mwadui)
    Jamal  Mwambeleko               (Mbao)
    Vincent Barnabas     (Mtibwa Sugar)
    Adam Salamba            (Stand United)
    Jaffar Salum             (Mtibwa Sugar)

Mbaraka Yusuf aibeba Kagera Sugar kwa Ndanda FC

Kagera Sugar wakishangilia moja ya mabao yao ya Ligi Kuu Bara
Na Rahim Junior
MABAO mawili moja kila kipindi yamemfanya Mbaraka Yusuf wa Kagera Sugar kuwasogelea vinara wa mabao wa Ligi Kuu Bara, Simon Msuva, Amissi Tambwe wote wa Yanga na Shiza Kichuya wa Simba.
Yusuf aliyeisaidia Kagera kupata ushindi muhimu nyumbani wa mabao 2-0 dhidi ya Ndanda katika mechi iliyopigwa jana, amefikisha jumla ya mabao nane, moja pungufu na waliyonayo kina Msuva.
Straika huyo wa zamani wa Simba, amelingana sasa kwa ufungaji mabao nane na mkali mwingine wa Ruvu Shooting, Abdulrahman Mussa aliyeisawazishia timu yake juzi isiadhiriwe na JKT Ruvu katika mechi iliyoisha kwa sare ya 1-1.
Katika mechi nyingine ya jana Mwadui ikiwa ugenini Uwanja wa Kambarage, mjini Shinyanga ilikumbana na kipigo cha kushtukiza cha mabao 2-0 toka kwa Chama la Wana, Stand United.
Hicho kilikuwa kipigo cha kwanza kwa Mwadui mbele ya wapinzani wao hao wa jadi wa mkoa huo na kuwafanya isalie na pointi zao 22 katika nafasi ya 10, huku Stand ikichupa toka nafasi ya saba hadi ya sita kwa kufikisha pointi 25.
Mabao ya beki Adeyum Saleh dakika ya 16 na lingine la penalti la Nahodha Jacob Massawe dakika nne baadaye yaliyotosha kuipa Stand ushindi wake wa kwanza tangu ilipokimbiwa na kocha wake, Mfaransa Patrick Liewig.
Kabla ya ushindi huo Chama la Wana ilikuwa imecheza mechi 11 bila kupata ushindi wowote, huku mitatu kati ya hiyo ikiwa chini ya Kocha Mkuu mpya, Hemed Morocco, ambaye ni Kocha Msaidizi wa timu ya taifa, Taifa Stars.
Ligi hiyo jioni hii kuna mchezo mmoja unaoelekea ukingoni kati ya Mbao FC ya Mwanza dhidi ya African Lyon ya Dar es Salaam na kesho Toto Africans itaikaribisha Prisons Mbeya kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.

Carzola majanga matupu Arsenal, nje wiki 10 zaidi

MAJANGA. Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger anahofu kiungo wake nyota Santi Cazorla anaweza kukaa nje ya uwanja kwa wiki 10 zaidi kutokana na majeruhi ya kifundo cha mguu yanayomsumbua.
Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania amekuwa nje ya uwanja toka Oktoba baada ya kucheza mechi 11 katika mashindano yote msimu huu. Lakini Cazorla mwenye umri wa miaka 32 sasa anategemewa kuendelea kukaa nje zaidi kutokana na majeruhi kupona taratibu kuliko ilivyotegemewa awali.
Wenger alisema Cazorla bado hajaanza hata kukimbia hivyo hadhani kama atarejea uwanjani hivi karibuni.

Imeelezwa huenda Wenger akafanya mpango wa kusajili mbadala wake.
Klabu hiyo jana Jumamosi ilivaana na Swansea City na kupata ushindi wa mabao 4-0 ugenini katika mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya England.

PSG yaingia vita ya kumnasa Depay wa Man United

Memphis Depay
PSG nayo imoooo! Klabu ya Paris Saint-Germain ya Ufaransa, imedaiwa nayo kuingia kwenye mbio za kumwania winga wa Manchester United, Mholanzi Memphis Depay.
Meneja wa United Jose Mourinho tayari ameshamwambia winga huyo kutafuta timu nyingine, huku Everton na Olympique Lyon zote zikitajwa kumtaka.
PSG walikaribia kumsajili Depay kabla hajakwenda Old Trafford kwa kitita cha Pauni milioni 25 mwaka 2015, lakini sasa wanaonekana kumhitaji tena mchezaji huyo ambaye hajacheza katika kikosi cha United toka Novemba mwaka jana. United inataka kitita cha Paundi milioni 15 kwa Depay baada ya kukataa ofa ya Paundi milioni 10 iliyotolewa na Everton inayoshiriki Ligi Kuu ya England.

Breaking News: Mwili wa Amina kuletwa, kuagwa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu

HABARI zilizotufikia muda huu, zinasema kuwa mwili wa Mwandishi wa Habari wa Kampuni ya Uhuru Publications Limited, inayochapisha magazeti ya Uhuru, Uhuru Wikiendi, Burudani na Mzalendo, Amina Athuman unatarajiwa kurejeshwa Dar es Salaam kesho asubuhi kwa boti kutoka Zanzibar. Msemaji wa Familia ya Marehemu, Athumani Kazukamwe, amesema jioni hii kuwa, mwili wa Amina utasafirishwa kutoka Zanzibar saa moja asubuhi kwa boti na unatarajiwa kuwasili Dar es Salaam kati ya saa tatu na saa nne asubuhi.
Kazukamwe, ambaye ni baba mkubwa wa mume wa marehemu, amesema mazishi ya Amina yamepangwa kufanyika keshokutwa Jumanne katika makaburi ya Soni, nje kidogo ya mji wa Tanga.
Amesema awali, upande wa mume wa marehemu ulitaka mazishi hayo yafanyike kesho Dar es Salaam, lakini baada ya majadiliano na familia ya marehemu, waliafikiana mazishi yakafanyika Tanga.
Kwa mujibu wa msemaji huyo wa familia ya marehemu, taratibu za kuuaga mwili wa Amina zitafanyika papo hapo bandarini na mara baada ya kumalizika, utasafirishwa kwa basi maalumu la kukodi kupelekwa Tanga.
Kaimu Mhariri Mtendaji wa UPL, Ramadhani Mkoma, amethibitisha mazishi ya marehemu Amina kufanyika Tanga.
Ramadhani amesema amepokea taarifa za kifo hicho kwa mshtuko mkubwa kwa sababu hakutarajia iwapo Amina angetangulia kuondoka duniani katika umri mdogo.
Amesema Amina ameacha pengo kubwa kwa sababu alikuwa mmoja wa wanahabari wa UPL waliokuwa wakifanyakazi kwa kujituma, aliipenda kazi yake na ilikuwa mwiko kwake kusukumwa kutimiza wajibu wake.
Amesema kazi aliyoifanya wakati wa michuano ya Kombe la Mapinduzi, ambayo alitumwa kuandika habari zake, ni uthibitisha wa wazi wa utendaji mzuri aliokuwa nao.
Amesema hawana la kufanya isipokuwa kumshukuru Mungu kwa kuwa kila alipangalo, hakuna anayeweza kulipangua. Amewataka wafanyakazi wa UPL kumuenzi Amina kwa kuiga utendaji wake wa kazi.

Mwanariadha wa Tanzania, Alphonce Simbu ang'ara India Marathon

Simbu (wa pili kushoto) akipozi na washindani wake baada ya kutwaa nafasi ya kwanza wa Mbio za kimataifa za India Marathon 2017
Na Lasteck Alfred
MWANARIADHA wa kimataifa wa Tanzania, Alphonce Simbu, ameibuka mshindi kwenye mbio ndefu za Mumbai Marathon  2017, akifanikiwa kumpiku Mkenya Joshua Kipkorir na wakimbiaji wengine wazoefu kutoka mabara mbalimbali.
Mashindano hayo yajulikanayo kama Standard Chartered Mumbai Marathon huwa yanafanyika kila Jumapili ya tatu ya Januari katika jiji la Mumbai, India na yanaaminika kuwa ni mbio kubwa kabisa barani Asia kwa idadi ya washiriki.
Simbu, aliyedhaminiwa na kampuni ya Multichoice Tanzania, aliibuka mshindi kwa kutumia muda wa dakika 2:09:28 muda ambao ni mzuri sana kwa mbio za aina hiyo.
Akizungumzia ushindi wake, Simbu alisema ushindi huo umesababishwa na maandalizi mazuri aliyoyafanya.
Alisema anauchukulia ushindi huo kama changamoto kwa mashindano mengine makubwa na kwamba huo ni mwanzo tu. Amesisitiza kuwa ushindi huo sio wake pekee yake au Multichoice ambao ndio wathamini wake, bali ni ushindi wa Taifa zima.
Kwa upande wa Serikali,  Waziri wa Habari, Utamaduni , Sanaa na Michezo, Nape Nnauye alimpongeza kupitia kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter akisema: "Tumefanikiwa tena, hongera Simbu, hongera RT (Chama cha Riadha Tanzania), asanteni Multichoice Tanzania kwa kumsapoti. Mungu ibariki Tanzania."
Kwa upande wake Mkuu wa Mahusiano wa Multichoice Tanzania, Johnson Mshana alisema Multichoice imefurahishwa sana na matokeo hayo na kwamba wataendela kumdhamini Simbu kwa mujibu wa makubaliano yao, ili kuhakikisha anaendelea kufanya vyema na kuliletea taifa sifa kubwa.
“Tulichukua jukumu la kumdhamini simbu katika mazoezi na maandalizi yake kwa kipindi cha mwaka mzima, kwani tunafahamu fika kuwa mazoezi na maandalizi ndiyo siri kubwa ya mafanikio katika mchezo wowote.
Alisema Mshana na kuongeza “Dhamira yetu kubwa ni kuinua vipaji na kulirejesha taifa letu kwenye ramani ya dunia katika ulingo wa michezo na burudani”
Katika mbio hizo, waigizaji maarufu wa Bollywood John Abraham and Neha Dhupia walikuwepo kuleta amsha amsha kwa washiriki. Alphonce anatarajiwa kurejea nyumbani leo Jumatatu.

Beki Mholanzi akichonganisha Chelsea na Man United

Beki Stefan De Vrij
LAZIMA kieleweke. Klabu za Chelsea na Manchester United zimedaiwa kuingia vitani kwa ajili ya kusaka saini ya beki wa Lazio, Stefan De Vrij.
Duru za kisoka zinasema kuwa, Chelsea imejipanga kupambana na Man United katika kipindi cha kiangazi kwa ajili ya kumwania beki huyo wa kimataifa wa Uholanzi ambaye kwa muda mrefu amekuwa akiwindwa na Mashetani Wekundu.
Chelsea inadaiwa nao wako tayari kuingia katika kinyang’anyiro hicho, huku klabu yake ya Lazia imeondoa uwezekano wa kumuuza beki huyo katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo.
Hatua hiyo imetoa mwanya kwa klabu hiyo kuweka kitita cha Euro milioni 40 kwa timu itakayomhitaji majira ya kiangazi, ambapo klabu yoyote kati ya Man United ama Chelsea wakituliza kichwa inaweza kueleweka kwao kwa beki huyo.

Simanzi! Mwandishi Amina Athuman hatunaye, Malinzi amlilia

Amina Athuman enzi za uhai wake
Na Alfred Lucas
SIMANZI. Mwandishi wa habari wa michezo wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo, Amina Athuman amefariki dunia asubuhi ya leo Jumapili na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ametuma salamu za rambirambi.
Malinzi ametuma salamu hizo kwa Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya Uhuru, Mzalendo na Burudani kutokana na kifo hicho cha Amina, aliyekuwa visiwani Zanzibar kuripoti michuano ya Kombe la Mapinduzi iliyomalizika juzi Ijumaa.
Katika salamu hizo ambazo pia zimeenda kwa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), Juma Pinto; Rais Malinzi ameelezea kushtushwa kwake kwa taarifa za kifo cha ghafla cha Amina.
“Niseme tu wazi kuwa tangu kuanza kwa michuano ya Mapinduzi, nimekuwa nikifuatilia taarifa mbalimbali zinazotolewa na wanahabari. Huwa pia sikosi magazeti ya Uhuru na Mzalendo na kuona byline (jina la mwandishi) ya Amina. Mpaka matokeo ya fainali zilizofanyika Januari 13, mwaka huu.
“Sasa asubuhi hii nimepata taarifa za kifo chake, ama kwa hakika zinasikitisha. Ni kifo cha ghafla, ninavyomfahamu binti huyo ni mchapakazi hodari na mfano uko wazi kwani katika hali ya ujauzito alikuwa hakosi kufuatilia habari,” amesema Rais Malinzi.
Kadhalika, Rais Malinzi ametuma salamu hizo za rambirambi kwa familia ya marehemu Amina, ndugu, jamaa na marafiki na kuwataka kuwa na moyo wa subira wakati huu mgumu wa msiba wa mpendwa wao.
“Binafsi naona ni kama askari aliyefia vitani. Naweza kumwita ni shujaa, lakini ndivyo hivyo tena, huwezi kupingana na mipango ya Mungu, nimepokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa, naomba wenzangu pia muwe na subira wakati huu mgumu ambao tasnia na Kampuni ya Uhuru Publications imepoteza mwanahabari mahiri.
Taarifa zinasema Amina alifariki dunia leo Jumapili Januari 15, 2017 akiwa anapatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Mnazimmoja, iliyoko Zanzibar mara baada ya kujifungua jana kwa mtoto ambaye pia alifariki muda mfupi baada ya kuzaliwa.
Hadi mauti yanamkuta alikuwa Mwandishi wa magazeti ya Uhuru na Mzalendo pamoja na gazeti la Burudani linalochapisha mahsusi habari za michezo na sanaa kabla ya hapo aliwahi pia kufanya kazi kampuni na Business Times Limited. Mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya marehemu Amina Athuman Mahala Pema Peponi. Inna Lillah wa Innaa Ilaihi Rajaajiuun.

Friday, January 13, 2017

Msuva, Manula, Mwanjali noma sana Ma[pinduzi 2017


Add caption
Na Rahma White
SIMON Msuva amefanikiwa kunyakua tena tuzo ya Mfungaji Bora wa michuano ya Kombe la Mapinduzi baada ya mabao yake manne aliyofunga kwenye mechi mbili za awali za Yanga kushindwa kufikiwa na mchezaji yeyote.
Mwaka 2014 winga huyo alinyakua pia tuzo hiyo kwa idadi kama hiyo wakati Yanga ikiwa imeaga mashindano hatua ya robo fainali kwa kuchapwa bao 1-0 na JKU.
Kipa Aishi Manula wa Azam ambaye hakuruhusu wavu wake kuguswa hata mara moja kama alivyofanya kwenye michuano ya Kombe la Kagame mwaka 2015, alitangazwa kuwa Kipa Bora wa michuano ya mwaka huu ya Mapinduzi, huku beki wa Simba, Method Mwanjali akitwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa mashindano na Said Mohammed wa Taifa akitangazwa Mchezaji Bora Chipukizi.
Mwamuzi Mfaume Ali alitwaa tuzo ya Mwamuzi Bora na kila mmoja kati ya walionyakua tuzo hizo alitwaa kitiota cha Sh 1 milioni moja.
Tuzo hizo na zawadi kwa washindi wote wa michuano ya msimu huu wa 11 ya Kombe la Mapinduzi walikabidhiwa zawadi zao na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein aliyekuwa mgeni rasmi.
Azam ndio mabingwa wapya wa michuano hiyo iliyoanza Desemba 30 mwaka jana kwa kuilaza Simba kwa bao 1-0.

AZAM NDIO MABINGWA WAPYA WA KOMBE LA MAPINDUZI 2017

PAMBANO la fainali ya Kombe la Mapinduzi 2017 limeisha kwa Azam kutwaa taji kwa mara ya tatu bila kupoteza pambano lolote wala kufungwa bao hata moja baada ya usiku huu kuichapa Simba kwa bao 1-0.
Bao pekee la Azam liliwekwa kimiani dakika ya 13 na Himid Mao 'Ninja' na kuifanya Azam kuweka rekodi ya aina yake katika michuano hiyo ikifanikiwa kuzilaza Simba na Yanga kwa hatua tofauti na kubwa kutoruhusu bao lolote katika michuano hii ya 11 iliyochezwa Uwanja wa Amaan.
Azam ilionekana tangu mapema kuibana Simba ambayo ilicharuka dakika za mwishoni mwa washambuliaji wake Juma Liuzio, Pastory Athanas na Laudit Mavugo wakikosa mabao ya wazi.

Zimeongezwa dakika nne

ZIMEONGEZWA dakika nne kabla ya pambano la fainali tya Kombe la Mapinduzi 2017 kati ya Simba na Azam kumalizika na Azam inaelekea kuweka rekodi ya kutwaa taji lao la tatu katika fainali tatu ilizowahi kucheza katika michuano hiyo.
Kama itatwaa itakuwa inalingana na Simba ambayo ilikuwa imetwaa mataji matatu katika fainali zao tano za mwanzo kabla ya leo inayoelekea mwishoni. Azam 1 Simba 0.

Mudathir Yahya kabadili mchezo

KUINGIA kwa Mudathir Yahya kwa upande wa Azam kumefanya timu hiyo kubadilika kabisa, tofauti na kipindi cha pili kilipoanza ambapo Simba walitawala kwa sehemu kubwa ya mchezo na kuonekana kama itasawazisha bao. Bao bado 1-0 Azam ikiwa mbele.

Dakika ya 75 bado 1-0 Azam ikiongoza

DAKIKA ni ya 75 matokeo bao ni 1-0, Azam ikiongoza na timu zimefanya mabadiliko, Joseph Mahundi katoka kumpisha Frank Domayo, Mudathjiri Yahya kampokea Yahya Mohammed, huku Simba ikimtoa Mzamiru Yahya na kumuingiza Pastory Athanas. 

Pambano limeanza tena kule Amaan

PAMBANO la Simba na Azam, limeanza tena kwa ngwe ya dakika 45 za mwisho, matokeo yakiwa bado ni bao 1-0, azam wakiwa mbele.

Kocha Antonio Conte atwaa tuzo nyingine England

Kocha Conte

Zlatan na tuzo yake
KOCHA wa Chelsea, Mtaliano Antonio Conte ametwaa tuzo kwa mara nyingine ya kuwa Kocha Bora katika Ligi Kuu ya England kwa mwezi Desemba.
Hiyo ni tuzo ya tatu mfululizo ambayo Kocha hjuyo ameitwaa ikiwa ni rekodi katika ligi hiyo. Conte alipewa tuzo hiyo leo ikiwa ni mara ya tatu baada ya Oktoba na Novemba pia kuibeba.
Wakati huo huo, straika wa Man United, Zlatan Ibrahimovic amenyakua tuzo ya Mchezaji Bora wa mwezi huo wa Desemba mwaka jana.

Farid Mussa apata leseni, ila apelekwa timu B Hispania

Na Mahmoud Zubeiry
HATIMAYE winga chipukizi wa kimataifa wa Tanzania, Farid Malik Mussa amepewa leseni ya Mamlaka ya Shirikisho la Soka Hispania (RFEF) aanze kuchezea nchini humo na klabu yake, Deportivo Tenerife imempangia kuanza kuchezea kikosi cha vijana chini ya umri wa miaka 23.
Akizungumza na Bin Zubeiry Sports - Online leo kwa simu kutoka Tenerife, Farid amesema kwamba amepangiwa kuanza kuchezea kikosi cha U23 ili kupata uzoefu kabla ya kupandishwa kikosi cha kwanza kinachocheza Ligi Daraja la Kwanza nchini humo, maarufu kama Segunda.

Farid Mussa na mmoja ya wachezaji wenzake wa timu yake mpya
“Nimepatiwa leseni na tayari nimepelekewa Tenerife B ili nikapate uzoefu kwanza na Jumamosi (leo) natarajia kucheza mechi yangu ya kwanza dhidi ya timu inaitwa Vera,”alisema Farid.
Farid amejiunga na klabu hiyo ya Santa Cruz de Tenerife, Tenerife, visiwa vya Canary Desemba kwa mkopo wa muda mrefu wa msimu kutoka Azam FC ya Dar es Salaam.
Azam FC imemtoa kwa mkopo Farid kwenda CD Tenerife kwa makubaliano maalum baada ya winga huyo kufuzu majaribio katika klabu hiyo Aprili mwaka jana alipokwenda na Mkurugenzi wa klabu yake, Yussuf Bakhresa.
Farid alitua Hispania Aprili 21 baada ya kuichezea Azam FC katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Esperance mjini Tunis, Tunisia ikifungwa 3-0 na kutolewa kwa jumla ya mabao 4-2 baada ya awali kushinda 2-1 Dar es Salaam.
Na ilimchukua wiki moja tu Farid kuwakuna kwa kipaji chake makocha wa Tenerife na kutaka kumnunua, lakini Azam ikakataa na kuamua kumtoa kwa mkopo.
Bin Zubeiry

Sasa ni mapumziko Azam 1, Simba 0

Kotei akithibitiwa na mabeki wa Azam wakiongozwa na Gadiel Michael (2)
Mashabiki wa Azam
DAKIKA 45 za kwanza za fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi, ni mapumziko wakati Azam ikiwa mbele kwa bao 1-0 dhidi ya Simba. Kwa wastani pambano lilikuwa fifte fifte, licha ya Azam kukosa bao la pili baada ya kichwa cha Bocco kushindwa kuingia kimiani dakika moja kabla ya mapumziko.

Kazimoto katoka, Mavugo achukua nafasi yake

DAKIKA tatu kabla ya mapumziko, Simba inamtoa Mwinyi Kazimoto na kumuingiza Laudit Mavugo. Kazimoto kajitonesha enka yake ya mguu na benchi la Msimbazi limeamua kumtoa.
Azam wakikosa bao muda mfupi uliopita. Sure Boy akishirikiana na John Bocco. Azam 1 Simba 0.

Dak 33, Azam bado ipo mbele kwa bao 1-0

SIMBA wanafanya kosa kosa nyingi langoni mwa Azam, ikiwa dakika ya 33 sasa matokeo yakiwa bado 1-0 Azam ikiongoza.

Dakika 21, Azam 1 Simba O

PAMBANO bado kali kwelikweli kila timu ikishambulia, ikiwa dakika ya 21 sasa mabao bado 1-0. Azam ikiongoza.

Himid Mao anaiandikia Azam bao tamu la

HIMID Mao 'Ninja' anaiandikia Azam bao dakika ya 13 kwa shuti kali la Dar mpaka Moro, lililomuacha Kipa Agyei ashindwe kuokoa.
Azam 1 Simba 0

Pambano la Simba na Azam limeanza

PAMBANO la fainali za Kombe la Mapinduzi kati ya Simba na Azam limeanza kama dakika 10 zilizopita na Wekundu wa Msimbazi wanafanya mashambulizi makali langoni mwa Azam.
Kichuya ameonekana msumbufu kwa mabeki wa Azam, lakini bado Simba wamekosa plan ya kupata bao mapema.
Azam wameonekana kuimarika na wamejaribu kama mara mbili kumpima Daniel Agyei, lakini milango imekuwa migumu. Micharazo itaendelea kukuwaletea dondoo za mchezo huu.

Azam yaivaa Simba kuitemi, Himid Mao ndani, Domayo anasubiri

Kikosi cha Azam, hapo Domayo tu ndio yupo nje kumpisha Himis Mao 'Ninja'
Na Rahma White
MABINGWA wa Kombe la Kagame, Azam imemjumuisha kikosi Himid Mao 'Ninja', wakati wakijiandaa kuvaana na Simba muda mchache kwenye pambano la fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi 2017 litakalochezwa Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Sehemu kubwa ya kikosi hicho ni kile kile kilichoizamisha Yanga na Taifa Jang'ombe kwenye nusu fainali kwani golini atasimama Aishi Manula, akisaidiwa na Shomari Kapombe na Gadiel Michael, huku kati wakiwamo Aggrey Morris na Yakubu Mohammed, wakati kati kuna majembe kama Himid Mao na Shephan Kingue, huku pemeni wakicheza Salum Abubakar 'Sure Boy' na Joseph Mahundi wakati safu ya ushambuliaji itaongozwa na Nahodha, John Bocco 'Adebayopr' akisaidiana na Yahya Mohammed.

Akiba: Mwadini Ali, David Mwantika, Frank Domayo, Mudathir Yahya, Enock Atta-Agyei, Samuel Afful na Shaaban Idd.

Majembe ya Simba yatakayoivaa Azam usiku huu, Kazimoto ndani

Na Rahma Junior
KOCHA wa Simba amekitoa hadharani kikosi chake kitakachoivaa Azam muda mchache kwenye pambano la fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi 2017 litakalochezwa Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Sehemu kubwa ya kikosi hicho ni kile kile kilichoizamisha Yanga kwenye nusu fainali kwani golini yupo, Mghana Daniel Agyei kama kawa akilindwa na mabeki wa pembeni Janvier Bokungu na Mohammed Hussein 'Tshabalala' huku kati wakiwamo Abdi Banda na Method Mwanjali.
Jonas Mkude, Muzamir Yassin na James Kotei wakisimama kati, huku mshambuliaji akiwa Juma Liuzio 'Ndanda' na mawinga wakiwa ni Shiza Kichuya na Mkongwe, Mwinyi Kazimoto.


Akiba: Manyika Peter, Hamad Juma, Novaty Lufunga, Said Ndemla, Jamal MNyate, Pastory Athanas na Laudit Mavugo.

Kocha Lyon anamtaka Depay hata leo hii

Depay
KOCHA wa klabu ya Olympique Lyon, Bruno Genesio amefichua kuwa straika wa Man United, Memphis Depay ni moja ya vipaumbele vyake katika usajili wa Januari.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uholanzi inaelezwa kuwa, huenda akaondoka klabu hapo mwezi juu kwenda katika klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Ufaransa, ingawa inadaiwa kikwazo ni dau la Pauni 13 milioni lililotajwa kutaka kulipwa na Lyon.
Mabosi wa Mashetani Wekundu wanataka kumuuza mchezaji huyo kwa Pauni milioni 15.
Hata hivyo, Kocha Genesio amefichua juu ya kumhitaji mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 kwa kusema; "Depay ni kipaumbele changu."
"Ni mchezaji aliyekamilika kwa kila kitu na atatufaa kuziba nafasui ya (Rachid) Ghezzal, iwapo mchezaji huyo ataamua kuondoka Lyon," aliongeza Genesio.
Depay amekuwa hana nafasi ndani ya kikosi cha Kocha Jose Mourinho, huku ikielezwa 'ubishoo' ndio unaomponza, hivyo njia pekee ya kuokoa kipaji chake ni lazima apate timu ya kuichezea na Lyon inasisitiza inamtaka.

Nani kubeba taji la Mapinduzi Cup 2017?

Na Rahma White
LIMEBAKI kama saa moja na ushei tu kabla ya Simba na Azam kumaliza ubishi kwenye pambano la fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi 2017 litakalopigwa kwenye Uwanja wa Amaan, visiwani Zanzibar.
Simba inacheza fainali yake ya sita katika msimu huu wa 11 wa michuano hiyo, ilihali Azam itakuwa ni ya tatu, lakini ikiwa na rekodi ya kusisimua ya kuingia fainali chache lakini haijawahi kuacha taji.
Iliingia mwaka 2012 na 2013 na mara zote likabeba taji mbele ya Jamhuri ya Pemba na KCCA, wakati Simba katika fainali zake tano za awali imetwaa mara tatu ikiwa klabu yenye historia ya kutwaa mara nyingi taji hilo.
Licha ya rekodi hizo za kusisimua kwa wababe hao wa Ligi Kuu Bara, bado timu yoyote itakayocheza vema na kutumia kwa ufanisi dakika 90 inaweza kubeba taji na kuhitimisha siku 15 za michuano hiyo iliyoanza Desemba 30, 2016.
Makocha na wachezaji wa timu zote wamekuwa wakitambiana tangu walipofahamu watakutana kwenye mchezo huo utakaoanza majira ya Saa 2:15, lakini ukweli ni kwamba lolote linaweza kutokea usiku huu visiwani humo.
Simba inayotarajiwa kupanga kikosi karibu chote kilichoitoa nishai Yanga kwa kuifunga kwenye nusu fainali, inaivaa Azam ikiwa haijkapoteza mechi yoyote ila imeruhusu bao moja wavuni wake, tofauti na Azam ambayo haijafungwa kabisa.
Mbali na mashabiki usiku kutaka kushuhudia timu ipi itakuwa bingwa mpya wa michuano ya mwaka huu, pia fainali hizo zitakuwa na utamu mwingine wa kujua wachezaji gani watakaonyakua tuzo za Ufungaji Bora, Kipa Bora, Mchezaji Bora Chjipukizi na Mchezaji Bora wa michuano.
Mpaka sasa tuzo ya Mfungaji Bora ni kama inarudi tena kwa Simon Msuva aliyetwaa mwaka 2014 akiwa na mabao manne sawa na aliyonayo msimu huu, licha ya timu yake ya Yanga kutolewa.
Wachezaji waliokuwa wakimfukuzia winga huyo mchachari, Bokota Labama wa URA Uganda ma Abdulsamad Kassim wa Jang'ombe Boys timu zao zimeaga michuano, japo Laudi Mavugo mwenye mabao mawili anaweza kumvurugia.
Kipa Bora nafasi ipo wazi kwa Aishi Manula wa Azam ambayo mpaka timu yake ikiivaa Simba, hajaruhusu bao lolote na akiwa ameonyesha kiwango cha hali ya juu, huku Daniel Agyei wa Simba naye aliyeibuka shujaa katika mechi ya nusu fainali dhidi ya Yanga kwa kuokoa penalti mbili za Deo Munishi 'Dida' na ile ya Haji Mwinyi anaweza kujikuta akibeba, iwapo Simba itafanya yake usiku huu.
Kwenye tuzo ya Mchezaji Bora Chipukizi ni vigumu kufahamu kwa sasa kwa sababu kuna vijana wengi walioonyesha makali akiwamo Enock Atta-Agyei wa Azam ambaye ndio kwanza anamiaka 18, lakini amepiga soka la nguvu Zanzibar.
Bila shaka ni suala la kusubiri kujua mambo yatakuwaje na MICHARAZO MITUPU litakuletea hatua kwa hatua ya pambano hilo mpaka mwisho wa fainali hiyo, usiache kuperuzi blog yako makini upate uhondo.

Kijeba cha Congo chazingua, CAF chapigwa mkwara

Na Alfred Lucas, TFF
BADO hakijaeleweka. Lile sakata la kijeba cha timu ya taifa ya vijana ya Congo, Langa Lesse Bercy, halijatafutiwa ufumbuzi mpaka sasa, ila safari hii Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF), limetoa nafasi ya mwisho kwa Shirikisho la Soka la Jamhuri ya Congo (FECOFOOT) kumpeleka mchezaji huyo  jijini Libreville, Gabon ili apimwe kipimo kipya cha MRI ili kutambua umri wake.
CAF limetaka FECOFOOT kumpeleka mchezaji huyo huko Libreville, Gabon ndani ya siku 10 zijazo kuanzia jana Januari 12, 2017.
CAF limepata kumwita mchezaji huyo mara mbili mwaka jana, na FECOFOOT imeshindwa kumpeleka kwa sababu mbalimbali wanazozijua FECOFOOT.
Kwa mujibu wa kanuni za mashindano ya kimataifa ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17, vijana waliohitajika kucheza ni wale wenye umri wa chini ya miaka 17.
Langa Lesse Bercy, amelalamikiwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwamba amezidi umri hivyo kuhitajika kumpeleka kwani hakustahili kucheza hatua ya kufuzu kwa michuano hiyo ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana.
Fainali za vijana zinatarajiwa kufanyika katika nchi nyingine itakayotangazwa hapo baadaye baada ya Madagascar kuondolewa kuandaa fainali hizo baada ya kubainika kutokamilisha baadhi ya taratibu.
Hii inatokana na ripoti ambayo CAF wameipata kutoka kwa wakaguzi wa maandalizi ya fainali hizo. CAF imefungua kandarasi ya kwa nchi wanachama wengine kuandaa fainali hizo. Mwisho wa kupokea maombi ni Januari 30, mwaka huu.
Kadhalika Kamati ya Utendaji ya CAF, imemteua Rais wa zamani wa TFF, Leodegar Chilla Tenga kuwania nafasi ya uwakilishi katika Shirikisho la Kimataifa la Soka (FIFA).
Katika nafasi hiyo kutoka nchi za Afrika zinazozungumza Kiingereza, Tenga atachuana na Rais wa zamani wa Shirikisho la Soka la Zambia, Kalusha Bwalya na Kwesi Nyantakyi wa Ghana.
Wengine waliopitishwa kuwania nafasi ya uwakilishi katika Kamati ya Utendaji ya FIFA kutoka nchi za Afrika ni Tarek Bouchamaoui wa Tunisia ambaye anaingia kwenye kundi la nchi zinazozungumza lugha za Kiarabu, Kireno na Kihispaniola.
Kwa nchi zinazozungumza lugha ya Kifaransa wamo Constant Omari Selemani wa DR Congo na Augustin Sidy Diallo wa Cote d’Ivoire wakati nafasi nyingine za wazi ihuhusisha mwanamke mmoja, wamo Almamy Kabele Camara (Guinea), Chabur Goc (South Sudan), Danny Jordaan (Afrika Kusini), Hani Abo Rida (Misri)  na Lydia Sekera (Burundi).

Maafande wa Ruvu washindwa kutambiana Mabatini

JKT Ruvu
Ruvu Shooting
Na Rahim Junior
MAAFANDE wa JKT Ruvu na Ruvu Shooting zimeshindwa kutambiana jioni ya leo baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika muendelezo wa Ligi Kuu Bara iliyoanza tena baada ya kusimama kwa wiki mbili.
Timu hizo zimevaana kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi na JKT imeshindwa kulipa kisasi cha kipigo cha bao 1-0 ilichopewa na ndugu zao hao kwenye mchezo wa duru la kwanza.
JKT ndio waliojkuwa wa kwanza kuandika bao la kuongoza lililopatikana mapema dakika ya tatu tu, kupitia Renatus Morris, lakini Ruvu Shooting ilichomoa dakika sita baadaye kupitia mfumania nyavu wao mahiri, Abdulrahman Mussa.
Bao la Mussa limemfanya kufikisha jumla ya mabao nane na kubakisha moja tu kuwanasa vinara wa magoli, Shiza Kichuya wa Simba, Amissi Tambwe na Simon Msuva wa Yanga wenye mabao tisa kila mmoja.
Sare hiyo haijabadilisha lolote katika nafasi kwa timu hizo, kwani Ruvu imeongeza pointi na kufikisha 24, lakini imesalia nafasi iliyokuwapo sawa na JKT ambayo inasalia mkiani ikiwa na pointi 15 tu,  ikiwa imecheza mechi 19.
Ligi hiyo itaendelea tena kesho Jumamosi kwa mechi mbili ambapo mjinio Shinyanga, Chama la Wana, Stand United itavaana na Mwadui kwenye Uwanja wa Kambarage, huku Ndanda itakaribishwa na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Kaitaba, mjini Bukoba mkoani Kagera.
Msimamo wa Ligi Kuu Bara
                               P  W   D  L   F   A  Pts

1. Simba                 18 14  2   2  30  6  44
2. Yanga                 18  12  4   2  39  9  40
3. Azam                  18  8   6   4  23  15 30
4. Mtibwa Sugar      18  8    6   4  22  19 30
5. Kagera Sugar      18  8   4   6   19  18 28
6. Mbeya City          18  6   6   6   16  16 24
7. Ruvu                   19  5   9   5   18  20  24
8. Stand Utd            18  5   7   6   16  16  22
9. Prisons                18  5   7   6   10  13  22
10.Mwadui               18  6   4   8   16  22 22
11.African Lyon        18  4   8   6   11   16  20
12.Mbao                  18  5   4   9   17  24  19
13.Ndanda               18  5   4   9   15  24  19
14.Majimaji              18  5   2  11  13  26  17
15.Toto Africans        18  4   4  10  11  20  16
16.JKT Ruvu            19   3   9   7    7  17   15

Wafungaji:   

9- Shiza Kichuya                           (Simba)
     Simon Msuva                            (Yanga)   
     Amissi Tambwe                         (Yanga)
8- Abdulrahman Mussa      (Ruvu Shooting)
7- Rashid Mandawa             (Mtibwa Sugar)
    Donald Ngoma                           (Yanga)
    John Bocco                                 (Azam)
6- Mzamiru Yasin                           (Simba)
    Haruna Chanongo            (Mtibwa Sugar)
5- Omar Mponda                          (Ndanda)
    Obrey Chirwa                             (Yanga)
    Riffat Khamis                           (Ndanda)
    Victor Hangaya                         (Prisons)
    Mbaraka Yusuf                 (Kagera Sugar)
    Rafael Daud                        (Mbeya City)
    Venance Joseph                 (African Lyon)
4-Peter Mapunda                         (Majimaji)
    Kelvin Sabato                   (Stand United) 
    Laudit Mavugo                           (Simba)
    Marcel Boniventure                 (Majimaji)
    Boniface Maganga                       (Mbao)
    Deus Kaseke                              (Yanga)
    Shaaban Kisiga              (Ruvu Shooting)
    Mohammed Ibrahim 'MO'            (Simba)   
    Tito Okello                          (Mbeya City)
3- Hood Mayanja                   (African Lyon)
    Ibrahim Ajib                              (Simba)
    Abdalla Mfuko                         (Mwadui)
    Subianka Lambert                    (Prisons)
    Ditram Nchimbi                  (Mbeya City)
    Wazir Junior                      (Toto African)
    Issa Kanduru                 (Ruvu Shooting)
    Ally Nassor 'Ufudu'          (Kagera Sugar)
    Kelvin Friday                   (Mtibwa Sugar)
    Mfanyeje                                (Majimaji)
    Francisco Zukumbawira                (Azam)
    Shaaban Idd                               (Azam)
    Jamal Mnyate                             (Simba)
    Jamal Soud                       (Toto Africans)
2- Adam Kingwande              (Stand United)
    Samuel Kamuntu                    (JKT Ruvu)
    Vincent Philipo                             (Mbao)
    Mcha Khamis                               (Azam)
    Danny Mrwanda                (Kagera Sugar)
    Pastory Athanas                 (Stand United)
    Paul Nonga                                (Mwadui)
    Adeyum Saleh                    (Stand United)
    Jacob Massawe                   (Stand United)
    Fully Maganga                  (Ruvu Shooting)        
    Themi Felix                       (Kagera Sugar)
    Mudathir Yahya                             (Azam)
    Atupele Green                         (JKT Ruvu)
    Jerry Tegete                              (Mwadui)
    Jamal  Mwambeleko                      (Mbao)
    Vincent Barnabas              (Mtibwa Sugar)
    Adam Salamba                  (Stand United)
    Jaffar Salum                     (Mtibwa Sugar)

Diamond akikinukisha Gabon, Vita ya Afcon 2017 imeiva

Zimbabwe
Guinea Bissau

Senegal

Watetezi Ivory Coast
Taji linalowaniwa
Ghana
Uganda

LIBREVILLE, GABON
KUMEKUCHA. Kesho Jumamosi pazia la michuano ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon 2017), kusaka bingwa wa bara la Afrikalitafunguliwa.
Wenyeji wa michuano hiyo Gabon, itakata utepe kwa kuvaana na Guinea Bissau kabla kabla ya wababe Cameroon kukwaruzana na Burkina Faso katika pambano jingine tamu linalosubiriwa kwa hapo kwenye ufunguzi wa michauno hiyo.
Tanzania ambayo ina miaka karibu 37 inajifariji kwa kuwakilishwa na mwimbaji wa muziki wa kizazi kipya, Naseeb Abdul 'Diamond Platinumz' atakayepamba sherehe za ufunguzi sambamba na wakali wa Nigeria akiwamo Mr Flavor.
Tanzania ilishiriki mara ya kwanza na mwisho mwaka 1980 ilipofanyikia Nigeria, lakini pamoja na kukosekana kwao bado mashabiki wa soka watazitumia runinga zao kufuatilia michuano hiyo itakayofikia tamati Februari 5 wakati Bingwa atakapofahamika.
MICHARAZO MITUPU inakuletea orodha ya vikosi vitakavyochuana kwenye michuano hiyo pamoja na ratiba nzima ya Afcon 2017.

ALGERIA
Makipa: Malik Asselah (JS Kabylie), Rais M’Bolhi (Antalyaspor/TUR), Chemseddine Rahmani (Mouloudia Bejaia)
Mabeki: Mohamed Benyahia, Mohamed Meftah (both USM Alger), Hichem Belkaroui (Esperance/TUN), Mokhtar Belkhiter (Club Africain/TUN), Ramy Bensebaini (Rennes/FRA), Liassine Cadamuro (Servette/SUI), Faouzi Ghoulam (Napoli/ITA), Aissa Mandi (Real Betis/ESP), Djamel Mesbah (Crotone/ITA)
Viungo: Mehdi Abeid (Dijon/FRA), Nabil Bentaleb (Schalke/GER), Yacine Brahimi (Porto/POR), Rachid Ghezzal (Lyon/FRA), Adlene Guedioura (Watford/ENG), Riyad Mahrez (Leicester City/ENG), Saphir Taider (Bologna/ITA)
Mastraika: Baghdad Bounedjah (Al Sadd/QAT), Sofiane Hanni (Anderlecht/BEL), Islam Slimani (Leicester/ENG), El Arabi Hillel Soudani (Dinamo Zagreb/CRO)
Kocha: George Leekens (Ubelgiji)

BURKINA FASO
Makipa: Herve Koffi (ASEC/CIV), Moussa Germain Sanou (Beauvais/FRA), Aboubacar Sawadogo (Kadiogo)
Mabeki: Yacouba Coulibaly (Bobo), Issoufou Dayo (Berkane/MAR), Bakary Kone (Malaga/ESP), Souleymane Kouanda (ASEC/CIV), Patrick Malo (Smouha/EGY), Issouf Paro (Santos/RSA), Steeve Yago (Toulouse/FRA)
Viungo: Prejuce Nacoulma, Alain Traore (both Kayserispor/TUR),Cyrille Bayala (Sheriff Tiraspol/MDA), Adama Guira (Lens/FRA), Charles Kabore (Krasnodar/RUS, capt), Bakary Sare (Moreirense/POR), Blati Toure (Omonia Nicosia/CYP), Abdoul Razack Traore (Karabuspor/TUR), Bertrand Traore (Ajax Amsterdam/NED), Jonathan Zongo (Almeria/ESP)
Mastraika: Aristide Bance (ASEC/CIV), Banou Diawara (Smouha/EGY), Jonathan Pitroipa (Al Nasr/UAE)
Kocha: Paulo Duarte (Ureno)

CAMEROON
Makipa: Jules Goda (Ajaccio/FRA), Georges Mbokwe (Coton Sport), Fabrice Ondoa (Sevilla/ESP)
Mabeki: Fai Collins (Standard Liege/BEL), Mohamed Djeitei (Nastic Tarragone/ESP), Ernest Mabouka (Zilina/SVK), Michael Ngadeu Ngadjui (Slavia Prague/CZE), Jonathan Ngwem (Progresso Sambizanga/ANG), Nicolas Nkoulou (Lyon/FRA), Ambroise Oyongo (Impact Montreal/CAN), Adolphe Teikeu (Sochaux/FRA)
Viungo: Franck Boya (Apejes Academy), Arnaud Djoum (Hearts/SCO), Georges Mandjeck (Metz/FRA), Edgar Salli (Saint-Gallen/SUI), Sebastien Siani (Ostend/BEL)
Mastraika: Vincent Aboubakar (Besiktas/TUR), Christian Bassogog (Aalborg/DEN), Benjamin Moukandjo (Lorient/FRA), Clinton Njie (Marseille/FRA), Robert Ndip Tambe (Spartak Trnava/SVK), Karl Toko-Ekambi (Angers/FRA), Jacques Zoua (Kaiserslautern/GER)
Kocha: Hugo Broos (Ubelgiji)
 
DR CONGO
Makipa: Joel Kiassumbua (Wohlen/SUI), Nicaise Kudimbana (Antwerp/BEL), Ley Matampi (TP Mazembe)
Mabeki: Jordan Ikoko (Guingamp/FRA), Joyce Lomalisa (V Club), Chancel Mbemba (Newcastle/ENG), Issama Mpeko (Mazembe), Fabrice N'Sakala (Alanyaspor/TUR), Marcel Tisserand (Ingolstadt/GER), Gabriel Zakuani (Northampton/ENG, capt)
Viungo: Merveille Bope (Mazembe), Herve Kage (Kortrijk/BEL), Neeskens Kebano (Fulham/ENG), Jacques Maghoma(Birmingham/ENG), Paul-Jose M'Poku (Panathinaikos/GRE), Remy Mulumba (Ajaccio/FRA), Youssouf Mulumbu (Norwich/ENG)
Mastraika: Cedric Bakambu (Villarreal/ESP), Jeremy Bokila (Al Kharitiyat/QAT), Jonathan Bolingi (Mazembe), Jordan Botaka (Charlton/ENG), Dieumerci Mbokani (Hull City/ENG), Firmin Ndombe Mubele (Al Ahly/QAT)
Kocha: Florent Ibenge
EGYPT
Makipa: Sherif Ekramy (Al Ahly), Essam El Hadary (Wadi Degla, capt), Ahmed El Shennawy (Zamalek)
Mabeki: Ahmed Fathy, Ahmed Hegazy, Saad Samir (all Ahly), Ahmed Dwidar, Ali Gabr (both Zamalek), Ahmed Elmohamady (Hull City/ENG), Omar Gaber (Basel/SUI), Karim Hafez (Lens/FRA), Mohamed Abdel-Shafi (Ahly Jeddah/KSA)
Viungo: Tarek Hamed, Ibrahim Salah (both Zamalek), Abdallah El Said (Ahly), Mahmoud Hassan (Mouscron/BEL), Mohamed Elneny (Arsenal/ENG), Amr Warda (Panetolikos/GRE)
Mastraika: Ahmed Hassan (Braga/POR), Marwan Mohsen (Ahly), Mahmoud Abdel-Moneim (Ahly Jeddah/KSA), Mohamed Salah (Roma/ITA), Ramadan Sobhy (Stoke City/ENG)
Kocha: Hector Cuper (Argentina)

GABON
Makipa: Anthony Mfa Mezui (clubless), Yves Stephane Bitseki Moto (Mounana), Didier Ovono (Ostend/BEL)
Mabeki: Aaron Appindangoye (Laval/FRA), Bruno Ecuele Manga (Cardiff City/WAL), Franck Perrin Obambou (Stade Mandji), Johann Serge Obiang (Troyes/FRA), Benjamin Ze Ondo (Mosta/MAL), Lloyd Palun (Red Star/FRA), Andre Biyogho Poko (Karabukspor/TUR), Yoann Wachter (Sedan/FRA)
Viungo: Guelor Kanga Kaku (Red Star/SRB), Mario Lemina (Juventus/ITA), Levy Clement Madinda (Nastic Tarragona/ESP), Didier Ndong (Sunderland/ENG), Junior Serge Martinsson Ngouali (Brommapojkarna/SWE), Merlin Tandjigora (Meixian Hakka/CHN), Samson Mbingui (Raja Casablanca/MAR)
Mastraika: Serge Kevyn Aboue Angoue (Uniao Leiria/POR), Pierre-Emerick Aubameyang (Borussia Dortmund/GER, capt), Cedric Ondo Biyoghe (Mounana), Denis Athanase Bouanga (Tours/FRA), Malick Evouna (Tianjin Teda/CHN)
Kocha: Jose Antonio Camacho (Hispania)

GHANA
Makipa: Razak Braimah (Cordoba/ESP), Adam Kwarasey (Rosenborg/NOR), Richard Ofori (Wa All Stars)
Mabeki: Harrison Afful, Jonathan Mensah (both Columbus Crew/USA), Frank Acheampong (Anderlecht/BEL), Daniel Amartey Leicester City/ENG), John Boye (Sivasspor/TUR), Edwin Gyimah Orlando Pirates/RSA), Baba Rahman (Schalke/GER), Andy Yiadom Barnsley/ENG)
Viungo: Afriyie Acquah (Torino/ITA), Emmanuel Agyemang-Badu (Udinese/ITA), Christian Atsu (Newcastle/ENG), Ebenezer Ofori (AIK Stockholm/SWE), Thomas Partey (Atletico Madrid/ESP), Samuel Tetteh (Leifering/AUT), Mubarak Wakaso (Panathinaikos/GRE)
Mastraika: Ebenezer Assifuah (Sion/SUI), Andre Ayew (West Ham/ENG), Jordan Ayew (Aston Villa/ENG), Asamoah Gyan (Al Ahly/UAE, capt), Bernard Tekpetey (Schalke/GER)
Kocha: Avram Grant (Israeli)

GUINEA-BISSAU
Makipa: Rui Dabo (Cova Piedade/POR), Papa Mbaye (Aguadulce/ESP), Jonas Mendes (Salgueiros/POR)
Mabeki: Mamadu Cande (Tondela/POR), Eridson (Freamunde/POR), Emmanuel Mendy (Ceahlaul Piatra Neamt/ROU), Rudinilson Silva (Lechia Gdansk/POL), Agostinho Soares (Sporting Covilha/POR), Juary Soares (Mafra/POR)
Viungo: Tony Silva Brito, Toni Silva, Zezinho (all Levadiakos/GRE), Bocundji Ca (Paris FC/FRA, capt), Idrissa Camara (Avellino/ITA), Francisco Junior (Stromsgodset/NOR), Jean-Paul Mendy (Quevilly-Rouen/FRA), Piqueti (Sporting Braga/POR), Sana (Academico Viseu/POR), Naní Soares (Falgueiros/POR)
Mastraika: Amido Balde (Maritimo/POR), Abel Camara(Belenenses/POR), Joao Mario (Chaves/POR), Frederic Mendy (Ulsan Hyundai/KOR)
Kocha: Baciro Cande

IVORY COAST
Makipa: Sylvain Gbohouo (TP Mazembe/COD), Ali Badra Sangare (Tanda), Mande Sayouba (Stabaek/NOR)
Mabeki: Serge Aurier (PSG/FRA), Mamadou Bagayoko (Saint-Trond/BEL), Eric Bailly (Manchester Utd/ENG), Simon Deli (Slavia Prague/CZE), Wilfried Kanon (ADO Hague/NED), Lamine Kone (Sunderland/ENG), Adama Traore (Basel/SUI)
Viungo: Victorien Angban (Granada/ESP), Geoffrey Serey Die (Basel/SUI, capt), Cheick Doukoure (Metz/FRA), Franck Kessie (Atalanta Bergamo/ITA), Yao Serge N'Guessan (Nancy/FRA), Jean-Michaël Seri (Nice/FRA)
Mastraika: Wilfried Bony (Stoke City/ENG), Max-Alain Gradel (Bournemouth/ENG), Salomon Kalou (Hertha Berlin/GER), Jonathan Kodjia (Aston Villa/ENG), Nicolas Pepe (Angers/FRA), Giovanni Sio (Rennes/FRA), Wilfried Zaha (Crystal Palace/ENG)
Kocha: Michel Dussuyer (Ufaransa)

MALI
Makipa: Soumaila Diakite, Djigui Diarra (both Stade Malien), Oumar Sissoko (Orleans/FRA)
Mabeki: Mahamadou N'Diaye, Charles Traore (both Troyes/FRA), Ousmane Coulibaly (Panathinaikos/GRE), Salif Coulibaly (TP Mazembe/COD), Mohamed Konate (Berkane/MAR), Youssouf Kone Lille/FRA), Hamari Traore (Reims/FRA), Molla Wague Udinese/ITA)
Viungo: Yves Bissouma (Lille/FRA), Lassana Coulibaly (Bastia/FRA), Moussa Doumbia (Rostov/RUS), Mamoutou N'Diaye (Royal Antwerp/BEL), Samba Sow (Kayserispor/TUR), Yacouba Sylla (Montpellier/FRA, capt), Adama Traore (Monaco/FRA), Sambou Yatabare (Werder Bremen/GER)
Mastraika: Kalifa Coulibaly (Gent/BEL), Moussa Marega (Guimaraes/POR), Bakary Sako (Crystal Palace/ENG), Moustapha Yatabare (Karabukspor/TUR)
Kocha: Alain Giresse (Ufaransa)

MOROCCO
Makipa: Yassine Bounou (Girona/ESP), Yassine El Kharroubi (Lokomotiv Plovdiv/BUL), Munir Mohamedi (Numancia/ESP)
Mabeki: Amine Attouchi (Wydad Casablanca), Mehdi Benatia (Juventus/ITA, capt), Fouad Chafik (Dijon/FRA), Manuel Da Costa (Olympiacos/GRE), Nabil Dirar (Monaco/FRA), Hamza Mendyl (Lille/FRA)
Viungo: Karim El Ahmadi (Feyenoord/NED), Youssef Ait Bennasser (Nancy/FRA), Aziz Bouhaddouz (Saint-Pauli/GER), M’bark Boussoufa (Al Jazira/UAE), Mehdi Carcela (Granada/ESP), Fayçal Fajr (Deportivo Coruna/ESP), Omar El Kaddouri (Napoli/ITA), Mounir Obbadi (Lille/FRA), Romain Saiss (Wolves/ENG)
Mastraika: Rachid Alioui (Nimes/FRA), Youssef El Arabi (Lekhwiya/QAT), Khalid Boutaib (Strasbourg/FRA), Youssef Ennesyri (Malaga/ESP)
Kocha: Herve Renard (Ufaransa)

SENEGAL
Makipa: Abdoulaye Diallo (Caykur Rizespor/TUR), Khadim N'Diaye (Horoya/GUI), Pape Seydou N'Diaye (Niarry Tally)
Mabeki: Saliou Ciss (Valenciennes/FRA), Lamine Gassama (Alanyaspor/TUR), Kalidou Koulibaly (Napoli/ITA), Cheikh M'Bengue (Saint-Etienne/FRA), Kara Mbodj (Anderlecht/BEL), Zargo Toure (Lorient/FRA)
Viungo: Mohamed Diame (Newcastle/ENG), Papakouli Diop (Espanyol/ESP), Idrissa Gueye (Everton/ENG), Cheikhou Kouyate (West Ham/ENG, capt), Papa Alioune Ndiaye (Osmanlispor/TUR), Cheikh N'Doye (Angers/FRA), Henri Saivet (Saint-Etienne/FRA)
Mastraika: Keita Balde (Lazio/ITA), Famara Diedhiou (Angers/FRA), Mame Biram Diouf (Stoke/ENG), Moussa Konate (Sion/SUI), Sadio Mane (Liverpool/ENG), Ismaila Sarr (Metz/FRA), Moussa Sow (Fenerbahce/TUR)
Kocha: Aliou Cisse

TOGO
Makipa: Kossi Agassa (clubless), Cedric Mensah (Le Mans/FRA), Baba Tchagouni (Marmande/FRA)
Mabeki: Serge Akakpo (Trabzonspor/TUR), Vincent Bossou (Young Africans/TAN), Djene Dakonam (Saint-Trond/BEL), Maklibe Kouloun (Dyto), Gafar Mamah (Dacia/MDA), Sadate Ouro-Akoriko (Al Khaleej/KSA), Hakim Ouro-Sama (Port)
Viungo: Lalawele Atakora (Helsingborgs/SWE), Franco Atchou (Dyto), Floyd Ayite (Fulham/ENG), Ihlas Bebou (Fortuna Dusseldorf/GER), Matthieu Dossevi (Standard Liege/BEL), Henritse Eninful (Doxa/GER), Serge Gakpe (Genoa/ITA), Alaixys Romao (Olympiacos/GRE), Prince Segbefia (Goztepe/TUR)
Mastraika: Emmanuel Adebayor (clubless, capt), Komlan Agbeniadan (WAFA/GHA), Razak Boukari (Chateauroux/FRA), Kodjo Fo-Doh Laba(Berkane/MAR)
Kocha: Claude le Roy (Ufaransa)

TUNISIA
Makipa: Moez Ben Chrifia (Esperance), Rami Jeridi (Sfaxien), Aymen Mathlouthi (Etoile Sahel, capt)
Mabeki: Zied Boughattas, Hamdi Nagguez (both Etoile Sahel), Aymen Abdennour (Valencia/ESP), Chamseddine Dhaouadi (Esperance), Slimen Kchok (CA Bizertin), Ali Maaloul (Al-Ahly/EGY), Hamza Mathlouthi (Sfaxien), Mohamed Ali Yaakoubi (Caykur Rizespor/TUR), Syam Ben Youssef (Caen/FRA)
Viungo: Mohamed Amine Ben Amor, Hamza Lahmar (both Etoile Sahel), Larry Azouni (Nimes/FRA), Ahmed Khalil (Club Africain), Wahbi Khazri (Sunderland/ENG), Youssef Msakni (Lekhwiya/QAT), Ferjani Sassi (Esperance), Naim Sliti (Lille/FRA)
Mastraika: Ahmed Akaichi (Ittihad Jeddah/KSA), Saber Khalifa (Club Africain), Taha Yassine Khenissi (Esperance)
Kocha: Henryk Kasperczak (Poland)

UGANDA
Makipa: Salim Jamal (Al Merrikh/SUD), Robert Odongkara (Saint George/ETH), Denis Onyango (Mamelodi Sundowns/RSA)
Mabeki: Timothy Awany, Joseph Ochaya (both KCCA), Shafiq Batambuze (Tusker/KEN), Denis Iguma (Al Ahed/LIB), Isaac Isinde (clubless), Murushid Juuko (Simba/TAN), Nicholas Wadada (Vipers)
Viungo: Khalid Aucho (Baroka/RSA), Mike Azira (Colorado Rapids/USA), Geoffrey Kizito (Than Quang Ninh/VIE), William Kizito (Rio Ave/POR), Tony Mawejje (Throttur/ISL), Hassan Wasswa (Nijmeh/LIB),Moses Oloya (Hanoi T and T/VIE), Godfrey Walusimbi (Gor Mahia/KEN)
Mastraika: Geoffrey Massa (Baroka/RSA, capt), Farouk Miya (Standard Liege/BEL), Yunus Sentamu (Ilves/FIN), Geofrey Sserunkuma (KCCA), Muhammad Shaban (Onduparaka)
Kocha: Milutin Sredojevic (Serbia)

ZIMBABWE
Makipa: Donovan Bernard (How Mine), Takabva Mawaya (ZPC Kariba), Tatenda Mkuruva (Dynamos)
Mabeki: Teenage Hadebe, Lawrence Mhlanga (both Chicken Inn), Onismor Bhasera (SuperSport Utd/RSA), Bruce Kangwa (Azam/TAN), Oscar Machapa (V Club/COD), Elisha Muroiwa (Dynamos), Costa Nhamoinesu (Sparta Prague/CZE), Hardlife Zvirekwi (CAPS Utd)
Viungo: Kudakwashe Mahachi, Danny Phiri (both Golden Arrows/RSA), Khama Billiat (Mamelodi Sundowns/RSA), Willard Katsande (Kaizer Chiefs/RSA, capt), Marvelous Nakamba (Vitesse Arnhem/NED)
Mastraika: Tinotenda Kadewere (Djurgardens/SWE), Cuthbert Malajila (Wits/RSA), Nyasha Mushekwi (Dalian Yifang/CHN), Knowledge Musona (Ostend/BEL), Tendai Ndoro (Orlando Pirates/RSA), Evans Rusike (Maritzburg/RSA), Mathew Rusike (CS Sfaxien/TUN)
Kocha: Kallisto Pasuwa

Makundi yapo hivi:



Ratiba ipo hivi:
Jumamosi 14 Januari 2017


   
Gabon v Guinea-Bissau Stade d'Angondje 18:00
Burkina Faso v Cameroon Stade d'Angondje 21:00
Jumapili 15 Januari 2017
       
Algeria v Zimbabwe Stade de Franceville 18:00
Tunisia v Senegal Stade de Franceville 21:00
Jumatatu  16 Januari 2017
       
Cote d'Ivoire v Togo Stade d'Oyem 18:00
DR Congo v Morocco Stade de Franceville 21:00
Jumanne  17 Januari 2017
       
Ghana v Uganda Stade de Port Gentil 18:00
Mali v Egypt Stade de Port Gentil 21:00
Jumatano 18 Januari 2017
       
Gabon v Burkina Faso Stade d'Angondje 18:00
Cameroon v Guinea-Bissau Stade d'Angondje 21:00
Alhamis  19 Januari 2017
       
Algeria v Tunisia Stade de Franceville 18:00
Senegal v Zimbabwe Stade de Franceville 21:00
Ijumaa  20 Januari 2017
       
Cote d'Ivoire v DR Congo Stade d'Oyem 18:00
Morocco v Togo Stade d'Oyem 21:00
Jumamosi 21 Januari 2017
       
Ghana v Mali Stade de Port Gentil 18:00
Egypt v Uganda Stade de Port Gentil 21:00
Jumapili 22 Januari 2017
       
Guinea-Bissau v Burkina Faso Stade de Franceville 21:00
Cameroon v Gabon Stade d'Angondje 21:00
Jumatatu  23 Januari 2017
       
Senegal v Algeria Stade de Franceville 21:00
Zimbabwe v Tunisia Stade d'Angondje 21:00
Jumanne  24 Januari 2017
       
Togo v DR Congo Stade de Port Gentil 21:00
Morocco v Cote d'Ivoire Stade d'Oyem 21:00
Jumatano 25 Januari 2017
       
Egypt v Ghana Stade de Port Gentil 21:00
Uganda v Mali Stade d'Oyem 21:00