STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, September 10, 2013

TMK yaifumua Rukwa Copa Coca Cola


TIMU Temeke imejiweka katika nafasi nzuri ya kucheza robo fainali ya michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 baada ya leo (Septemba 10 mwaka huu) asubuhi kuizamisha Rukwa mabao 5-1.

Hadi mapumziko katika mechi hiyo ya kundi B hatua ya Fainali za Taifa iliyochezwa Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam, washindi walikuwa mbele kwa mabao 3-0.

Mabao ya washindi yalitiwa wavuni na Constantine Katepa aliyefunga dakika ya 28, Patrick Ambrose dakika ya 36 huku Hamisi Kajole akipiga mawili dakika ya 43 na 71. Bao la nne lilifungwa dakika ya 46 na Ramadhan Juma.

Rukwa ambayo kwa matokeo hayo imeshatolewa ilipata bao lake dakika ya 51 kupitia kwa Francisco Nkanga. Timu nyingine katika kundi hilo ni Geita na Ilala.

Robo Fainali ya michuano hiyo itaanza keshokutwa (Septemba 12 mwaka huu). Kila kundi linatoa timu mbili kucheza hatua hiyo katika mashindano hayo yanayodhaminiwa na kampuni ya Coca-Cola.

TFF yamfungia Pondamali, refa wa Yanga na Coastal

Juma Pondamali (kushoto) akimlisha ujuzi Kaseja Taifa Stars
Na Boniface Wambura
KAMATIi ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imempiga faini ya sh. milioni moja na kumfungia miezi mitatu kocha wa makipa wa timu ya Coastal Union Juma Pondamali kwa kuwatukana washabiki wanaominika kuwa wa Simba.
Pondamali alifanya kosa hilo katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya timu yake na Yanga iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Mwamuzi Martin Saanya na mwamuzi msaidizi namba moja Jesse Erasmo waliochezesha mechi kati ya Yanga na Coastal Union nao wamefungiwa mwaka mmoja kila mmoja kwa kutoimudu mechi hiyo.

Nayo Yanga imepigwa faini ya sh. milioni moja (sh. 500,000) kwa kila kosa kutokana na washabiki wake kuwarushia waamuzi chupa za maji baada ya Coastal Union kusawazisha bao katika mechi hiyo. Pia waliwarushia chupa waamuzi hao wakati wakirejea vyumbani baada ya pambano hilo.

Vilevile Coastal Union imepigwa faini ya sh. 100,000 baada ya kuchelewa kwenye kikao cha maandalizi ya mechi (pre match meeting). Timu hiyo ilichelewa kwa dakika 23. Kikao kinatakiwa kuanza saa 4 kamili asubuhi.

Kivumbi cha FDL kuanza Jumamosi, Kimondo Kurugenzi kuvaana Mbozi


Na Boniface Wambura
Timu za Kimondo SC ya Mbeya na Kurugenzi ya Mafinga zitatumia viwanja vya Mbozi na Mafinga kwa ajili ya mechi za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inayoanza Jumamosi (Septemba 14 mwaka huu).

Kimondo SC sasa itatumia Uwanja wa CCM Vwava ulioko wilayani Mbozi badala ya Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine wa jijini Mbeya. Nayo Kurugenzi itatumia Uwanja wa Wambi ulioko Mafinga mkoani Iringa badala ya Uwanja wa Makambako ulioko mkoani Njombe.

Mechi za fungua dimba FDL msimu huu zitakuwa kati ya Burkina Faso na Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro, Mkamba Rangers na Lipuli ya Iringa kwenye Uwanja wa CCM Mkamba, Majimaji na Mlale JKT kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea na Kimondo na Kurugenzi kwenye Uwanja wa CCM Vwawa katika mechi za kundi B.

Septemba 14 mwaka huu Tessema na Green Warriors zitaoneshana kazi Uwanja wa Karume, Dar es Salaam. Siku inayofuata (Septemba 15 mwaka huu) Transit Camp na Polisi Dar (Mabatini mjini Mlandizi) wakati mechi nyingine za kundi hilo la A zitakuwa kati ya Villa Squad na African Lyon (Karume) na Ndanda FC na Friends Rangers (Nangwanda Sijaona, Mtwara).

Kundi C ni Polisi Mara na Polisi Dodoma (Uwanja wa Karume, Musoma), Kanembwa JKT na Polisi Tabora (Uwanja wa Lake Tanganyika, Kigoma), Stand United na Mwadui (Kambarage, Shinyanga) wakati Pamba na Toto Africans zitamenyana Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Mademu toka Kenya, Nigeria kuvaana Okt

DAR ES SALAAM, TANZANIA - You can easily liken her with a PIII student or a fresh model who happen to put on gloves but, there is more to this affably pretty and shy Kenyan boxing star Sarah Achieng than you can chew. To start with, she is known as the defender of the underprivileged in her area and she takes no cue from anybody who want to undermine those close to her. The beautiful paid ranked slugger known for her hard hitting ferocity punches. Her fury in the ring is not easily contained.

sarah achieg
The Beautiful Goddess Sarah Achieng from KENYA 
 
Sarah Achieng derive from  the Western Kenyan city of Kisumu. She was raised by a fish mongering family and to her; fish diet is what made her skin health, soft and beautiful. She was once a finalist to the beauty parget. Sarah is BLACK, sweet, warm, soft and strong AFRICAN whose only purpose in the ring is to dispatch her opponents as fast as she can.
 
Now she has to wait until October 4, 2013 when her fury and ferocity punches may be properly utilized but, alas to whom other than the Princess Royal of African boxing Helen Joseph, the one and only "IBF Intercontinental Female Featherweight Champion".
This may be an ominous task for beautiful Sarah who want to emulate her heroines Conjestina Acheing better known as Conje to her friends and Kenyan public at large. Sarah Achieng (not  related to Conje) is an astute beautiful woman who happen to take a different turn in life and embrace boxing. She is the cutest of all the female boxers that Kenyan has ever had and a darling of the media as would the public.
 
Helen Joe 
Princess Royal of African boxing Helen Joseph from NIGERIA
 
Together with Conjestina Achieng they have feminizing Kenyan boxing fraternity with the tonic of their beauties! This is perhaps why most Kenyans identify with the name "Achieng"
 
Sarah's journey and her comfortable life in the SHOW BIZ would be majored by how far she can contain the amazingly punching power of the Ghanaian based Nigerian Princess Royal of African boxing Helen Joseph. Now the duo will meet in October 4, 2013 at the Accra National Sports Stadium. They would join other Ghanaian boxing luminaries the like of Issa Samir and Aryee Ayittey as they hassle each other for the "IBF World Youth Jr. Middleweight Title".
 
The two beautiful sluggers would be inline for the "IBF Intercontinental Female Featherweight Title" which Princess Royal of African boxing Helen Joseph won against the beautiful Hungarian slugger Mariana Guyas on May 3rd, 2013. Helen has promised her fans to spit fires and defend her title with all what she has. She will welcome Sarah with her open arms but, reminded her of the consequences that comes with her heroine attempt!
 
This would be yet another epic battle for Ghana that is reeling from recent breathtaking and star studded IBF competitions and this one would surely give boxing spectators their money worth.
 
Discussing the strategies used to enlist so many star boxers in his stable, Henry Manly-Spain who is the CEO of the Golden Concept Business Group tells the story of nationalism and business acumen. Manly-Spain's only interests is to equip Ghanaian boxing fraternity with several world acclaimed boxers who would promote the great nation of Ghana to the international scene.
 
"Boxing is tourism. It is business. It is economy. It is life."  said Manly-Spain. "We would use boxing to promote this great nation which Osagyfo Kwame Nkrumah made it Paradise for all those who are seeking freedom and prosperity" concluded this major businessman who is known as the Muttest (Godfather) to his friends.
 
The questions in the minds of many boxing fans is who would emerge the winner between these two beautiful sluggers? This one billion dollars question will be answered on October 4, 2013 as the two African beauties KISS the face of "SWEET SCIENCE"
 
Watch this space for more news on Helen Joseph and Sarah Achieng's rumble for October 4, 2013  
 
Congratulations TEAM Helen/Sarah: Henry Manly-Spain, Kofi Dukku-Rackets and Micahel Tetteh. Africa is proud of you!   

"Nothing else like IBF/AFRICA as it advances African interests to the Global professional boxing fraternity"   

They Call it AFRICA...! We Call it HOME. 
 
The United States Boxing Association (USBA) and International Boxing Federation (IBF) continental body to Africa, Middle East & Persian Gulf

Mesut Ozil akandia Real Madrid

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg4ofh6d-gXibmGvc2xSsD8UfdtNJEaoqFh5VR-k8V5ZtbFQkA38OgBh_eW2UhZjNmxZJun5lUreGf6kmv9B3JxAoWcDyI6DqafsqZSqnXRzd4hrsJsA7mPvEmI-S1M0stt-cf073BC4981/s640/Mesut+Ozil+2013_1.jpg
MESUT Ozil amedai kwamba angejiunga Arsenal hata bure  na amebainisha kwamba "uwazi, kuaminiwa na kuheshimiwa" vilipotea Real Madrid.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani alikamilisha uhamisho wake wa siku ya mwisho ya usajili na kutua katika kikosi cha Arsene Wenger kwa dau la uhamisho la paundi milioni 40, akisaini mkataba wa miaka mitano na klabu hiyo.
Ozil alibainisha kuwa mazungumzo na kocha huyo wa Arsenal yalimshawishi kupima hali yake ndani ya Real Madrid na kumvutia kuhamia kwenye Ligi Kuu ya England.
“Kwa namna fulani, mazungumzo yale yalinivutia kuhama na kunifanya nitambue kuwa nilichokipoteza Madrid: uwazi, kuaminiwa, kuheshimiwa," Ozil aliliambia gazeti la Die Welt.
"Yeye (Wenger) aliniambia vile anavyoniona, namna anavyonihitaji, na kile anachotarajia kutoka kwangu.
"Siwezi kufanya chochote kuhusu ada ya uhamisho. Ningeweza kuja hata bure."
Ozil, mchezaji aliyenunuliwa kwa ada iliyovunja rekodi ya uhamisho kwa Arsenal, alifunga ama kutoa pasi za magoli 108 katika mechi 159 katika michuano yote akiwa na Madrid.

Kumekucha tamasha la wanafunzi la Mtakuja J'mosi hii


BAADA ya kimya kirefu tangu kufanyika kwa mara ya mwisho kwa tamasha  wanafunzi hasa wa shule za Sekondari, uongozi wa Mtakuja Secondary School iliyopo Kunduchi kwa kushirikiana na mtangazaji maarufu Allan Lucky 'Rais wa Wanafunzi' wa kipindi maarufu cha Skonga ambacho hurushwa kupitia televisheni ya vijana ya EATV umeandaa tamasha la wanafunzi linalotarajiwa kuhudhuriwa na wanafunzi zaidi ya 3000 kutoka shule zaidi ya 20 za jijini Dar.
 
Tamasha hilo lenye lengo la kuwakutanisha wanafunzi wa shule mbali mbali za Dar-es-salaam kwa pamoja na kupata changamoto kimawazo na kiburudani, pia kuwakutanisha wadau mbali mbali wa elimu katika kufanikisha uboreshwaji wa elimu na kusaidia katika kutekeleza mpango wa 'Matokeo Makubwa Sasa', linatarajiwa kufanyika Jumamosi  katika viwanja vya shule hiyo.

Miongoni mwa shule ambazo zitashiriki ni: Mtakuja, Kondo, Jordan, St. Gasper, Mbezi Beach, Boko, Goba, Twiga, Maendeleo, Mwambao, Kisauke, Kinzudi, londa, Makongo, Kawe Ukwamani, Tegeta, Mbweni, Teta, Hananasif na Mtongani, zote ni za sekondari.

Tamasha hilo linatarajiwa kuhusisha wadau mbali mbali wa elimu watakaokutana katika kubadilishana mawazo na kupata burudani kwa kushuhudia vipaji lukuki walivyo navyo wanafunzi kutoka shule mbali mbali.

Miongoni mwa shughuli zitakazoendeshwa ni pamoja na maswali na majibu, fashion show, uimbaji, ufokaji, na wanafunzi wenye vipaji mbali mbali maalum watapewa nafasi.

Msemaji wa tamasha hilo ambaye pia ni mwalimu wa michezo wa Mtakuja Beach Sekondari Bw Misonji Charles amewataka wadau mbali mbali wa elimu kuhudhuria na kushuhudia vipaji vya wanafunzi mbali mbali na pia amewataka waandishi wa habari kujitokeza kwa wingi katika kuchukua habari na matukio mbali mbali yatakayojitokeza. Pia amewaomba wadau mbali mbali wenye uwezo wa kuchangia katika kufanikisha tamasha hili wajitokeze, kwa kuwa linaandaliwa kwa nguvu za shule na kamati maalum ya maandalizi pekee.

Kwa maelezo na kama unataka kushiriki, tafadhali wasiliana na Msemaji wa Tamasha Bw Misonji Charles kupitia 0714642442.