STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 21, 2015

Chelsea wabanwa, Man Utd yafa, Arsenal raha

Ben Mee rises above the Chelsea defence to equalise for Burnley against Premier League leaders Chelsea at Stamford Bridge
Ben Mee akiisawazishia Burnley bao kwa kichwa
Mee wheels away in celebration after finding the target with a header to level proceedings at Stamford bridge with 10 minutes left
Oyooooooooooo!
Manchester United must get used to their new style of play under Louis van Gaal, according to Gary Neville
hoi
Cazorla is congratulated by his team-mates as Arsenal looked to pick up an eighth win in nine games
Arsenal kwa raha zao
Wilfried Zaha skips past Nacho Monreal in the opening moments, and the England winger caused his full back plenty of problems
ilikuwa vita
QPR walip[okuwa wakizamishwa ugenini
WAKATI vinara wa Ligi Kuu ya England, Chelsea wakingángániwa nyumbani kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1, Mashetani Wekundu, Manchester United wamenyukwa mabao 2-1 na Swansea City, huku Arsenal ikingára ugenini kwa kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Crystal Palace.
Chelsea wakiwa kwenye uwanja wao wa Stanford Bridge walitangulia kuandika bao la kuongoza lililofungwa na beki wake Branslav Ivanovic katika ya 14 na wageni Burnley kuchomoa bao hilo dakika tisa kabla ya mchezo kumalizika kupitia kwa Ben Mee.
Chelsea itajilaulumu kwa kushindwa kuibuka na ushindi nyumbani kutokana na kutawala mchezo huo na washambuliaji wake Eden Hazard na Diego Costa wakikosa mabao ya wazi.
Sare hiyo imeifanya Chelsea kufikisha pointi 60 na kutoa fursa kwa wapinzani wao mabingwa watetezi Manchester City kupunguza pointi zilizokuwapo kwani mpaka muda huu wa mapumziko City wanaoongozxa mabao 3-0 dhidi ya Newcastle United.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Arsenal ikiwa ugenini imeshinda mabao 2-1, Manchester Utd ikipigwa 2-1 na Swansea City, wakati Aston Villa wameendelea kutetepa kwa kukubali kichapo cha 2-1 wakiwa nyumbani toka kwa Stoke City huku QPR wakilala ugenini 2-1 mbele ya Hully City na timu za Sunderland na West Bromwich wakitoka suluhu ya kutofungana.

Barcelona yazamishwa nyumbani na Malaga

Barcelona 0-1t Bat BA Malaga
Juanmi akiitungua Barcelona leo
Barcelona forward Lionel Messi (left) vies with Malaga's forward Samuel Castillejo (right) on Saturday
Messi hakufua dafu leo kwa Malaga siku chache kabla ya Barcelona kuvaana na Manchester City kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya
KLABU ya Barcelona ikiwa dimba la nyumbani la Camp Nou imekubali kipigo cha bao 1-0 mbele ya Malaga katika mfululizo wa Ligi ya Hispania, La Liga.
Kipigo hicho cha nne kwa Barcelona msimu huu katika ligi hiyo kimezidi kuongeza ushindani wa mbio za ubingwa dhidi ya watetezi Real Madrid ambayo watashuka dimbani kesho wakiwa ugenini.
Bao pekee la wageni Malaga mbele ya Barcelona liliwekwa kimiani na  Juanmi katika dakika ya saba ya mchezo huo na kungángánia hadi mwisho na kuwaacha Barcelona wakiwa hoi nyumbani.
Mechi nyingine inayochezwa hivi sasa Valencia wakiwa ugenini waongoza bao 1-0 dhidi ya wenyeji wao Cardoba.

Jahazi la Mtibwa lazidi kuzama, Coastal hoi, Kagera yaua

Mtibwa Sugar iliyoipokea kichapo cha nne mfululizo leo kwa Mgambo JKT
http://api.ning.com/files/cPakA0chAEyfyqjZRP3k2djpZ9GyxNW23W69D7FY4fYhsuNz2vmH6gr7yEITcci18IdnTvIgOej4xydmYu8LtJiXW0uQDhCL/16.jpg
Kagera Sugar waliongára Kambarage kwa kuilaza Polisi Moro
Polisi Moro wliopoteza mchezo wa pili leo mbele ya Kagera Sugar baada ya wiki iliyopita kulala kwa Simba 2-0
Ndanda iliyotakata nyumbani Mtwara kwa kuilaza Coastal Union 1-0
JAHAZI la Mtibwa Sugar linazidi kuzama baada ya kufungwa 1-0 na Mgambo JKT ikiwa ni mechi ya nne mfululizo kupoteza katika Ligi kuu Tanzania Bara.
Kipigo hicho cha Mtibwa kimeifanya timu hiyo kuzidi kuporomoka kwenye msimamo wa ligi hiyo wakisaliwa na pointi zao 19 baad ya mechi 15.
Bao lililoizamisha Mtibwa katika pambano hilo lililochezwa katika uwanja wa Mkwakwani Tanga, liliwekwa kimiani na Malimi Busungu katika dakika ya 36 na kuifanya timu yao kufikisha pointi 17.
Katika mchezo mwingine ul;iochezwa Nangwanda Sijaona, wenyeji Ndanda waliinyuka Coastal Union kwa bao 1-0 lililowekwa kimiani na Jacob Massawe katika dakika ya 79.
Aidha Kagera Sugar wakwia uwanja wa Kambarage Shinyanga wanaoutumia kama uwanja wao wa nyumbani, iliendelea kutakata baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Polisi Moro.
Bao hilo pekee lililowapa ushindi Kagera na kuzidi kujikita nafasi ya tatu ikifikisha pointi 24 liliwekwa kimiani na Rashid Mandawa ambaye anafikisha bao lake la saba katika ligi hiyo, bao moja nyuma dhidi ya kinara wa mabao kwa sasa wa ligi hiyo Didier Kavumbagu wa Azam.
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa michezo mitatu, Yanga wakiwa uwanja wa Sokoine Mbeya kupapetana na Mbeya City, Simba watakuwa wageni wa Stand Utd mjini Shinyanga na Azam watauamana na Prisons Mbeya uwanja wa Chamazi.
Mechi hiyo ya Azam na maafande itachezwa saa 2 usiku na kila timu imetamba kujiandikishia ushindi katika pambano hilo.