STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 8, 2013

YANGA, TOTO AFRICANS HAPATOSHI TAIFA


Kikosi cha Toto African

Vinara wa Ligi Kuu Yanga

Na Boniface Wambura
MICHUANO ya Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaendelea kesho (Machi 9 mwaka huu) kwa mechi mbili ambapo vinara Yanga watakuwa wenyeji wa Toto Africans kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mwamuzi wa mechi hiyo namba 135 atakuwa Andrew Shamba kutoka Pwani akisaidiwa na Abdallah Mkomwa na Abdallah Rashid pia wote kutoka Pwani. Kamishna ni Salim Singano kutoka Tanga wakati Mtathmini wa waamuzi ni Alfred Lwiza.
Nayo Polisi Morogoro itakuwa mgeni wa Azam kwenye Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi, Dar es Salaam. Azam katika mechi hiyo namba 136 na nyingine mbili zinazofuata itakuwa bila kocha wake Steward John Hall ambaye Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imemfungia mechi tatu.
Charles Komba kutoka Dodoma ndiye atakayekuwa Kamishna wa mechi hiyo namba 136 itakayochezeshwa na mwamuzi Simon Mberwa kutoka mkoani Pwani.
Ligi hiyo itaendelea tena keshokutwa (Machi 10 mwaka huu) ambapo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam utashuhudia mechi kati ya Simba na Coastal Union ya Tanga. Waamuzi wa mechi hiyo ni Martin Saanya akisaidiwa na Jesse Erasmo na Vicent Mlabu wote kutoka Morogoro.

TFF bado yaikomalia serikali yasisitiza kuonana na Waziri Mukangara


Rais wa TFF, Leodger Tenga

Na Boniface Wambura
RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga amemshukuru Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenela Mukangara kwa kukubali ombi la Shirikisho la kutaka kukutana naye kwa mazungumzo na kumsihi asitishe hatua anazodhamiria kuchukua hadi hapo kikao hicho kitakapofanyika.
Waziri Mukangara ameiagiza TFF kuitisha Mkutano Mkuu wa marekebisho ya katiba ifikapo tarehe 15 Aprili 2013 na Mkutano Mkuu wa Uchaguzi ifikapo tarehe 25 Mei 2013 na kwamba tamko la TFF kutekeleza maagizo hayo liwe limetolewa katika muda wa siku tano zinazoishia Jumatatu (Machi 11, 2013).
Katika barua pepe ambayo amemuandikia Waziri ambaye kwa sasa yuko nje ya nchi, Rais Tenga ameeleza kuwa alikwenda ofisini kwake tarehe 7 Machi 2013 kujaribu kumuona lakini akaambiwa amesafiri, hivyo kuomba kukutana na Katibu Mkuu wa Wizara, ambaye pia hakuwepo ofisini na hatimaye akakutana na Naibu Katibu Mkuu.
Katika barua hiyo pepe, Rais Tenga ameeleza madhumuni ya kutaka kuonana na Waziri Mukangara kuwa ni kwanza “kukushukuru kwa kukubali kuonana na ujumbe wa TFF ulioongozwa na mjumbe wetu wa Kamati ya Utendaji, Bw. Alex Mgongolwa, akiongozana na Katibu Mkuu wa TFF, Bw. Angetile Osiah, jana tarehe 6 Machi 2013.
“Kukushukuru kwa kukubali kukutana nasi tena siku ya tarehe 19 Machi, kwa ajili ya mazungumzo juu ya maagizo yako.
“Kukuarifu kuwa nimepokea maagizo yako uliyoyatoa jana kupitia kwa Mjumbe wetu wa Kamati ya Utendaji na kwa njia ya barua; na
“Kwa heshima na taadhima, kukuomba usitishe hatua yoyote ile unayodhamiria kuchukua hadi hapo tutakapokutana na kupata maelezo yetu, TFF, juu ya maamuzi na maagizo uliyoyatoa.”
Tenga, ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu la Afrika (CAF) aliondoka jana (Machi 7 mwaka huu) kwenda Marrakech, Morocco kuhudhuria kikao cha kamati hiyo na pia Mkutano Mkuu wa CAF ambao umepangwa kufanyika Machi 10 mwaka huu ukihusisha pia ajenda ya uchaguzi wa rais.

KAIJAGE KOCHA MPYA TWIGA STARS



Na Boniface Wambura

 ROGASIAN Kaijage ameteuliwa kuwa kocha mpya wa timu ya taifa ya mpira wa miguu ya wanawake, Twiga Stars baada ya kocha wa zamani, Charles Boniface Mkwasa kujiuzulu katikati ya mwaka jana.
Mkwasa, ambaye alikuwa nyota wa Yanga na Taifa Stars, alijiengua kufundisha timu hiyo aliyoiongoza kwa muda mrefu, baada ya Twiga Stars kuondolewa katika kinyang’anyiro cha kuwania tiketi ya kucheza fainali za Afrika kwa Wanawake (AWC) zilizofanyika nchini Equatorial Guinea.
Twiga ilipata bao muhimu la ugenini jijini Addis Ababa ilipofungwa na wenyeji wao Ethiopia mabao 2-1, lakini ikiwa na matumaini ya kutumia vyema bao la ugenini ilijikuta ikilala bao 1-0 kwenye Uwanja wa Taifa katika mchezo wa marudiano na hivyo kukosa tiketi ya kurudi tena kwenye fainali hizo.
Kaijage ambaye kwa sasa anajihusisha na mradi wa vijana (grassroots) pamoja na programu nyingine za kukuza vipaji zilizo chini ya TFF, aliteuliwa na Kamati ya Ufundi ya TFF kufanya kazi hiyo na ameita kikosi cha Twiga Stars kwa mazoezi ya siku kumi kuanzia Machi 10 hadi 23 mwaka huu Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam.
Wachezaji walioitwa ni Amina Ally (Lord Barden), Asha Rashid (Mburahati Queens), Aziza Mwadini (Zanzibar), Esther Chabruma (Sayari), Esther Mayalla (TSC Academy), Etoe Mlenzi (JKT), Evelyn Sekikubo (Mbarahati Queens), Fatuma Bushiri (Simba Queens), Fatuma Mustafa (Sayari) na Fatuma Omari (Sayari).
Flora Kayanda (Tanzanite), Hamisa Athuman (Marsh Academy), Hellen Maduka (Bujora), Hellen Peter (JKT), Irene Ndibalema (TSC Academy), Maimuna Said (JKT), Mwajuma Abdallah (Tanzanite), Mwanaidi Tamba (Mburahati Queens), Mwanahamis Omari (Mburahati Queens) na Mwapewa Mtumwa (Sayari).
Nabila Ahmed (Marsh Academy), Nasiria Hashim (Zanzibar), Pulkeria Charaji (Sayari), Rukia Khamis (Sayari), Semeni Abeid (Tanzanite), Sharida Boniface (Makongo Sekondari), Sophia Mwasikili (Luleburgaz Gucu Spor, Uturuki), Theresa Yona (TSC Academy), Vumilia Maarifa (Evergreen) na Zena Khamis (Mburahati Queens).

RHINO, KANEMBWA ZASAKA TIKETI VPL

Mmoja wa wachezaji wa Rhino Rangers (kushoto) akichuana ligi ya msimu uliopita iliyoipandisha daraja Polisi Moro

Na Boniface Wambura
KINDUMBWENDUMBWE cha Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kinaendelea kesho (Machi 9 mwaka huu) katika makundi yote matatu, lakini macho na masikio ya washabiki wa mpira wa miguu yakiwa kwenye mechi za Rhino Rangers ya Tabora na Kanembwa JKT ya Kigoma.
Timu hizo ndizo ziko katika nafasi nzuri ya kupata tiketi ya kucheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao kutoka kundi hilo la C. Tayari Mbeya City ya Mbeya na Ashanti United ya Dar es Salaam zimeshapata tiketi za kucheza VPL msimu ujao kutoka kundi A na B.
Rhino Rangers itaikaribisha Polisi Dodoma kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora, wakati Kanembwa JKT itakuwa mgeni wa Pamba kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Mechi nyingine za kundi C ni Mwadui vs Polisi Tabora (Kambarage, Shinyanga), na Morani vs Polisi Mara (Kiteto, Manyara). Mechi za kundi A ni Majimaji vs JKT Mlale (Majimaji, Songea), Mkamba Rangers vs Mbeya City (Sokoine, Mbeya) na Polisi Iringa vs Burkina Faso (Samora, Iringa).
Mshikeshike ya kundi B ni Ndanda vs Ashanti United (Nangwanda Sijaona, Mtwara), Villa Squad vs Green Warriors (Karume, Dar es Salaam), Polisi Dar vs Transit Camp (Mabatini, Mlandizi) wakati Tessema na Moro United zitacheza Machi 10 mwaka huu Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

 

TWFA YAANIKA MIKAKATI YAKE SOKA LA WANAWAKE



Mwenyekiti wa TWFA, Lina Kessy
MIKAKATI YA KUENDELEZA MPIRA WA MIGUU KWA WANAWAKE

Utangulizi:
Awali ya yote napenda kuchukua nafasi hii kwa niaba ya kamati ya utendaji ya TWFA kuwashukuru wajumbe wa mkutano mkuu kwa kutupa ridhaa ya kuongoza chama kwa kipindi cha miaka minne.

Pia napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru wadau wote wa mpira wa miguu kwa kutuwezesha kufika hapa tulipo. Napenda niwashukuru wadau wote kwa ujumla wao na pia kuishukuru serikali kwa namna ya pekee zaidi kwa mchango wake ,na mashirika na makampuni ambayo yamekuwa karibu sana nasi NMB, SERENGETI, NSSF, PPF, na Bakheresa Group of Companies.

Tunaamini kabisa kuwa vyombo vya habari ni washirika wetu wakubwa katika kuendeleza mpira wa miguu wanawake. Napenda kuvishukuru vyombo vyote vya habari hapa nchini na hata vile vya nje vilivyoweza kutoa nafasi katika ujenzi wa mpira wa miguu wanawake.

 Maendeleo ya mpira
 Kutekeleza na kuendeleza mpango wa grassroot.

Kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira wa miguu Tanzania,Chama cha Mpira  wa Miguu wanawake  na vyama vya mikoa na wadau mbalimbali  tutaendelea kuendeleza mradi wa mpira wa miguu kwa watoto wa kike na wa kiume Grassroot programme.(umri wa miaka 06-12).kwa mwaka 2013 mradi huu utatekelezwa katika mikoa  mitano (5) mikoa hiyo ni  Tanga,Pwani.Mwanza,Mtwara na Lindi. Mradi huu unaendeshwa kupitia shule za msingi.Kwa mwaka 2012 Mradi huu umeendeshwa katika mkoa wa Dar es Salaam na  watoto wapatao 8766 (wasichana 4909 na wavulana 3857 ) na walimu 26 wameshirikishwa.

Mafunzo ,semina na makongamano
Kwa mwaka 2013 tunatengemea kuendesha mafunzo mbalimbali katika nyanja kuu nne za maendeleo ya mpira wa miguu yaani Utawala na uongozi,Ualimu(Ukocha)  Uamuzi na utabibu katika mpira wa miguu .Katika mwaka mwaka 2013 mafunzo yatafanyika zaidi katika nyanja ya uongozi ili kuwajengea stadi za uongozi viongozi wengi ambao wameingia madarakani katika chaguzi zilizofanyika kwa mwaka 2012/2013.Mafunzo ya utawala na uongozi yatafanyika katika mikoa nane:Dar es Salaam,Pwani,Morogoro,Mwanza,Musoma,Shinyanga,Kilimanjaro na Tanga.Katika mafunzo hayo baadhi ya washiriki watateuliwa kutokana na uwezo wao kwa kuzingatia vigezo vitakavyowekwa na watahudhuria semina itakayo andaliwa kwa kushirikiana na shirikisho la mpira wa miguu Tanzania.

Mafunzo kwa walimu katika ngazi mbalimbali na uratibu wa utekelezaji wa mafunzo yaliyofanyika yatapewa kipau mbele.

Mafunzo kwa waamuzi yatalenga zaidi kuibua vipaji vya watoto wa kike walioko mashuleni na wachezaji wanaomaliza/waliomaliza muda wao.Mafunzo yatafanyika kwa awamu mbili katika mkoa wa Dar es Salaam.

Madaktari  wa michezo  ni muhimu sana katika maendeleo ya mpira na afya za wachezaji kwa kushirikiana na vyombo husika mafunzo kwa mwaka 2013 yatafanyika kwa awamu mbili na yatafanyika katika mkoa wa Dar es Salaam. 
Wanahabari wenye uweledi katika mpira wa miguu wa wanawake ni chachu ya maendeleo ya mpira huo.Nafasi ya wanahabari ni kubwa katika kuendeleza mpira wa miguu ili kuwajengea ujuzi zaidi kutakuwa na mafunzo kwa wanahabari yatakayofanyika Dar es Salaam.

Uongozi na utawala bora
Maendeleo ya mpira wa miguu kwa wanawake yanahitaji viongozi bora na waliopewa ridhaa na vyombo husika.Chaguzi zimefanyika katika  mikoa 16 kati 25  ya mikoa ya Tanzania Bara. Pia tunahimiza mikoa ambayo haijafanya uchaguzi ifanye chaguzi mapema.  Mikoa hiyo ni: Dar es salaam, Mwanza, Kilimanjaro, Rukwa, Arusha, Geita, Simiyu, Njombe, Katavi na Mbeya.

Katika chaguzi hizo kuna baadhi nafasi zote hazikujazwa ni matumaini yetu kuwa  zitajazwa katika mikutano ijayo ya vyama husika.
Pia nichukue nafasi hii kuwahamasisha kina mama wengi wenye sifa kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali katika vyama vya mikoa na taifa pale uchaguzi utakapoitishwa.

Mashindano
Mashindano mbalimbali ndio moyo wa mpira wa miguu bila mashindano  hakuna anayeweza kutambua  ubora na kiwango chakena pia ni kipimo cha maendeleo.
Kutakuwa na mashindano mbalimbali katika ngazi ya  mikoa,taifa na kimataifa.
Mashindano hayo pia yatahusisha shule za msingi na sekondari  na vyuo mbalimbali.Kwa kushirikiana na vyombo husika kutakuwa na ufuatiliaji wa karibu wa michezo ya UMISSETA toka ngazi ya mkoa hadi Taifa na kuwa na mpango endelevu wa kuwaendeleza wale wenye vipaji ambao wamechaguliwa /wanaweza kuchaguliwa kwenye timu za taifa.

Ligi itachezwa katika ngazi za mikoa na baadaye kuunda kombaini ya mkoa itakayoshiriki mashindano ya taifa.

Kwa mwaka 2013 tunatengemea mikoa kuchezesha ligi isiyopungua timu tano kwa mikoa 15 itakuwa na timu  10 na timu itaruhusiwa kusajili wachezaji 25 kwa mwaka 2013 tunatengemea watoto/wasichana  3750 kushiriki katika mpira wa miguu. Idadi hii ukizidisha mara nne unapata jumla ya wachezaji 15,000.Endapo tutakuwa na benki ya wachezaji hawa tutaweza kuunda timu bora za umri tofauti na zenye kiwango cha juu.

Pia mikoa inahimizwa kuanzisha mashindano mbalimbali yatakayoamsha ari kwa watoto wa kike na wasichana kushiriki katika mpira wa miguu.

Uratibu wa mikoa
Wajumbe wa kamati ya utendaji pamoja na  majukumu yao kama wajumbe watakuwa na jukumu la kuratibu shughuli za  maendeleo ya mpira wa miguu katika mikoa:Uratibu huo utakuwa kama ifuatavyo:
Rose Kissiwa
Makamu Mwenyekiti
Tabora, Dodoma, Rukwa, Kigoma, Pwani
Amina Karuma
Katibu
Lindi, Mtwara, Iringa, Njombe, Ruvuma
Zena Chande
Mjumbe
Dar es Salaam, Morogoro, Katavi, Shinyanga, Mbeya
Triphonia Temba
Mjumbe
Manyara, Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Singida
Sophia Charles
Mjumbe
Mara, Kagera, Simiyu, Geita, Mwanza
Kwa mujibu wa katiba ya TWFA  ibara ya 37  inatoa nafasi kwa kamati ya utendaji kuunda kamati ndogo za kuendeleza mpira wa miguu wanawake kamati hizo ni kamati ya Fedha na mipango,kamati ya Ufundi,kamati ya ngingine itakayoonekana inafaa.Kamati ya utendaji kwa pamoja ilikubaliana kuunda kamati ya habari na masoko.
Kamati ya Fedha na Mipango
1.     Rose Kissiwa       - Mwenyekiti
2.     Evans Aveva
3.     Sophia Tigalyoma
4.     Sophia Mukama
5.     Asha Baraka
Kamati ya Ufundi
1.     Tryphonia Temba – Mwenyekiti
2.     Florence Ambonisye
3.     Miraji Fundi
4.     Dr. Leonia Kaijage
5.     Furaha Francis
6.     Richard Muhotoli
Kamati ya Habari na Masoko
1.     Zena Chande – Mwenyekiti
2.     Beatrice Mgaya
3.     Mohamed Mkangara
4.     Florian Kaijage
5.     Somoe Ng’itu

Masoko na Habari
Mpira wa miguu wanawake hauna udhamini na pia vyanzo rasmi vya kupata mapato.Kwa kupitia kamati ya habari na masoko ,tunaamini kutakuwa na mikakakti mbalimbali ya kuelimisha ,kuhamasisha wadau na watanzania wote kuwiwa na kujitoa kuendeleza mpira wa miguu .

Asanteni
Lina P.Kessy
Mwenyekiti Chama cha Mpira wa miguu wanawake 

Abdi Kassim 'Babi' aendeleza rekodi zake kimataifa

Abdi Kassim 'Babi'

MCHEZAJI Abdi Kassim 'Babi' ameweka rekodi nyingine katika historia ya soka ya kuwa mchezaji wa kwanza wa Azam kufunga bao kwenye mechi ya kimataifa tangu timu hiyo iundwe.
Bao alilofunga dakika ya 14 kwenye mechi ya kwanza dhidi ya Al Nasri ya Juba nchini Sudan ya Kusini limemfanya aingie kwenye rekodi hiyo.
Mechi hiyo ilichezwa uwanja wa Taifa, Azam ilitoka na ushindi wa bao 3-1, kabla ya kwenda kushinda tena ugenini bao 5-0, hivyo kusonga mbele kwa jumla ya bao 8-1.
Kwenye uwanja wa Taifa, mbali na Babi, mabao mengine mawili ya Azam yalifungwa na Kipre Tchetche.
Azam  ilianzishwa mwaka 2007 na kupanda Ligi Kuu Tanzania Bara mwaka 2008, kabla ya kufanikiwa kucheza michuano ya kimataifa mwaka huu na kuziacha .
Mchezaji huyo wa zamani wa Yanga, anayefahamika pia kama 'Barack wa Unguja' amejiongezea rekodi hiyo baada ya ile ya kuwa mfungaji wa bao la kwanza katika uwanja mpya wa Taifa jijini Dar es Salaam mara tu ulipofunguliwa.
Rekodi hiyo aliiweka mwaka 2007 kwenye mechi ya kirafiki kati ya Taifa Stars na Uganda Cranes iliyokuwa ya ufunguzi rasmi ya uwanja huo pamoja na kujiandaa na mechi dhidi ya Msumbuji iliyokuwa ya kusaka kwenda Ghana ilikochezwa fainali ya Afrika mwaka 2010.
Bao hilo alilifungwa dakika ya 54 kwa shuti kali umbali wa mita 18 baada ya gonga vizuri kti ya Said Maulid na Haruna Moshi 'Boban'.

Russian Ambassador pleased efforts to develop Sports


The Russian Embassy Athletic's  team in Kilimanjaro Marathon last week
RUSSIAN Ambassador to the country Alexander Runnikh said he is pleased by the government efforts to develop sports in the country.
In an email response, Runnikh said it’s very good to see the country leadership is doing its best to improve sports in the country, saying sports contribute a lot to social and economic development of any country.
 “I can see many people in Tanzania who are really interested in sport. The events like Kilimanjaro marathon or others prove it. Just have a look how many people participate in it. You should continue to follow this principles of healthy nation, because only with active, strong and positive people is possible to build and develop any country” he said .
The Russian ambassador who said he likes Sambo and received a prize in USSR team competitions in sambo wrestling in 1968 and 1970 competitions said it’s very encouraging that many young people in the country are involved in sporting activities.
According to him Sambo  is a Russian martial art and combat sport. In his native language it means  "self-defense without weapons".he said the sport is relatively modern and  its development began in the early 1920s by the Soviet Red Army to improve their hand-to-hand combat abilities.
He also said  Sambo has roots in Japanese judo, international styles of wrestling, plus traditional folk styles of wrestling such as: Armenian Kokh, Georgian Chidaoba, Romanian Trînta, Tatar Köräs, Uzbek Kurash, Mongolian Khapsagay and Azerbaijani Gulesh
He also said a sport improves discipline among people as they try to uphold the principles of the game.
 Runnikh further said his office encourages its staff to participate at local sporting activities as this helps to build a strong relationship between people.
“Sports improve relationships and understanding and due to this the Team of The Embassy of Russian Federation with close cooperation with The Russian Tanzanian Cultural Centre & Russian School this year also took part in just ended Kilimanjaro Marathon” he said.
According to him on top of  Sambo , he also like horse ridding and as a Sambo player he also  won the USSR Master of Sports in Sambo wrestling in 1969 and 1980 , he also won a  prize winner in sambo world championship veterans in Men category  in 2007and in 2009 he emerged second place in sambo world championship Mens veterans.

DGC to groom Squash players

Akil Hirji

The re elected Dar es Salaam Gymkhana Club (DGC) squash section captain Akil Hirji has  said his second term will be dedicated to improve women and students participation in the sport.
Outlining his 2013 /2014 activities, Hirji said more efforts will be put on development of the game within and outside DGC .
He said he is working closely with members and management of the club to see that Squash is played by many people in the country.
Hirji said soon his club will send invitation letters to Schools within Dar es Salaam to send their students for squash lessons at the Club , saying he had already a greed with management of DGC so that students should not be paying entry fee at the club. 
“ This term we have a greed to dedicate our time to create women team , women tournaments and also  Junior teams for both boys and girls , conduct trainings for our members and also we will be organizing interclub tournaments ” he said .
The Captain said his first year of leadership at the club was dedicated to refurbishment of the DGC squash courts and also organizing tournaments at the facilities.
 He also maintained his plans to have a close working relationship with the National sports council (NSC)so that they are to develop the game in the country together.
“I will try to talk to National Sports Council to see how best we can do to develop the game to all parts of the country, I believe that is the only way we can develop the game in the country” he said.
The captain also discloses that their Zambian coach Nipa Bwaya  is expected in the country any day soon as all procedures for his employment are completed .
The 36 years old  Zambian trainer was in the country last year  for  10 days coaching trails and he  successfully met the satisfaction of both players and leadership of DGC squash section.
According to Hirji the trainer will be contracted for renewable six month.