STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, August 26, 2014

TFF yaja na sheria kali kwa wauza, wanunua mechi

http://tff.or.tz/wp-content/uploads/2014/08/TFF-voda-Logo.jpg 
KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imeamua kuanzia sasa adhabu kwa watu wanaotoa rushwa au kupanga matokeo katika mchezo huo itakuwa ni kufungiwa maisha kujishughulisha na mchezo huo. Taarifa katika tovuti ya TFF imesema kwamba hayo yamefikiwa katika kikao cha Kamati ya Utendaji ya shirikisho hilo juzi. Kwa muda sasa, kumekuwa na tuhuma nyingi za wachezaji na marefa kuhongwa ili kupanga matokeo- lakini hakukuwa na sheria madhubuti ya kupambana na hali hiyo- lakini kwa hatua hii mpya ya TFF dhahiri itasaidia kupunguza mchezo huo mchafu.  
  Aidha, baada ya Libya kujitoa kuwa mwenyeji wa Fainali za Afrika (AFCON) za 2017, Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limealika nchi wanachama kuomba uenyeji wa fainali hizo.
Kamati ya Utendaji ya TFF iliyokutana Agosti 24, mwaka huu imeamua Tanzania kuomba uenyeji wa fainali hizo.
“Tunatambua kuwa moja ya masharti ya kuandaa fainali hizo ni pamoja na nchi kuwa imeandaa moja ya mashindano ya vijana. Lakini kwa kuwa suala hili liko katika mazingira maalumu (exceptional circumstances) tunaamini CAF watafikiria ombi letu kwa msingi huo,”.
Awali Libya ilipewa uenyeji wa fainali hizo 2015, lakini zikahamishiwa Afrika Kusini kutokana na sababu za kiusalama. Hivyo, Libya ikapewa fainali za 2017 ambapo sasa imejitoa yenyewe kuandaa fainali hizo.
Wakati huo huo: Kamati ya Utendaji ya TFF imemteua Boniface Wambura kuwa Mkurugenzi mpya wa Mashindano kuanzia Septemba 1 mwaka huu.
Kabla ya uteuzi huo, Wambura alikuwa Ofisa Habari na Mawasiliano wa TFF kuanzia Januari 1, 2011. Nafasi hiyo sasa iko wazi na itajazwa baadaye na Kamati ya Utendaji.

26 waitwa Stars kuivaa Morocco



KOCHA mkuu wa timu ya soka ya Taifa, Mart Nooirj ametangaza kikosi cha wachezaji 26 kitakachocheza mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Morocco.
Mechi hiyo, ambayo imo kwenye kalenda ya Shirikisho la Soka la Dunia (FIFA), imepangwa kuchezwa Septemba 5 mwaka huu nchini Morocco.
Wachezaji wapya waliomo kwenye kikosi hicho ni kiungo Said Ndemla wa Simba SC na washambuliaji Mwagane Yeya wa Mbeya City na Juma Luizio wa ZESCO United ya Zambia.
Kikosi kamili ni makipa; Deogratias Munishi (Yanga) na Mwadini Ali (Azam). Mabeki ni Said Morad (Azam), Oscar Joshua (Yanga), Shomari Kapombe (Azam), Nadir Haroub (Yanga), Kelvin Yondani (Azam), Aggrey Morris (Azam), Joram Mgeveke (Simba) na Charles Edward (Yanga).
Viungo; Erasto Nyoni (Azam), Mwinyi Kazimoto (Al Markhiya, Qatar), Amri Kiemba (Simba), Himid Mao (Azam), Salum Abubakar (Azam), Said Ndemla (Simba), Said Juma (Yanga) na Haruna Chanongo (Simba).
Washambuliaji; John Bocco (Azam), Khamis Mcha (Azam), Simon Msuva (Yanga), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, DRC), Mbwana Samata (TP Mazembe, DRC), Mrisho Ngassa (Yanga), Mwegane Yeya (Mbeya City) na Juma Liuzio ZESCO, Zambia).
Kikosi hicho kinatarajiwa kuingia kambini Jumapili (Agosti 31 mwaka huu) mchana katika hoteli ya Accomondia mjini Dar es Salaam na kitakuwa kikifanya mazoezi Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

BASI LA HOOD LAGONGANA NA LORI ARUSHA

Basi la Hood lililopata ajali asubuhi ya leo eneo la Kikatiti, Arusha.
Raia wakishuhudia ajali ya basi la Hood ilivyotokea.
BASI la kampuni ya Hood lililokuwa likitoka Arusha kwenda Iringa llimepata ajali asubuhi ya leo eneo la Kikatiti, Arusha. Basi hilo lilitaka kugongana uso kwa uso na lori la mizigo, ndipo katika kukwepana ikatokea ajali hiyo. Abiria wa basi wamenusurika , ila lori lilidumbukia darajani na hakukuwa na mtu aliyepoteza maisha.

Mario Balotelli akabidhiwa namba ile ile 45

MSHAMBULIAJI nyota wa Italia, Super Mario Balotelli amekamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Liverpool kwa pauni milioni £16 akitokea AC Milan kwa mkataba wa miaka mitatu na kukabidhiwa jezi namba 45.
Balotelli, 25 alitua mchana wa jana Melwood na kumalizana na uongozi wa Liverpool kabla ya kusaini mkataba huo na kukabidhiwa jezi yenye namba hiyo ambayo amekuwa akitumia kuanzia Manchester City na AC Milan alikotokea kwa sasa.
Alifanyiwa ukaguzi wa afya na mtaalamu wa mambo ya utabibu wa Liverpool Ryland Morgans.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester City atakuwa akilipwa kwa wiki kiasi cha pauni £125,000 ndani ya uga wa Anfield, alihudhuria pambano la usiku wa jana dhidi ya Manchester City, ambapo klabu yake mpoya ilinyukwa na ile aliyoichezea kabla ya kwenda Milan.
History makers: Italian striker Balotelli poses with the European Cup, which Liverpool have won five times, most recently in 2005
Mshambuliaji wa kimataifa wa Italia Balotelli akiweka pozi mbele ya kikombe cha Ulaya ambacho Liverpool imetwaa mara tano huku mara ya mwisho ikiwa ni 2005
Ready for business: The 24-year-old arrived at Melwood on Monday afternoon to put the finishing touches to the transfer
Balotelli  akiwa amepozi pembeni ya nembo ya klabu yake mpya ya Liverpool.
Signing up: Balotelli returns to England after an 18-month absence having scored 30 goals with AC Milan
Balotelli akisaini mkataba wa kuichezea Liverpool akiwa anarejea England baada ya miezi 18 kupita tangu aondoke Manchester City kwenda AC Milan na kuifungia mabao 30.
Raring to go: Balotelli poses in the boot room at Melwood, and will be in attendance for Liverpool's clash with Manchester City on Monday
'A great team with young players': Balotelli, who left Manchester City in 2013, said Liverpool are one of the best teams in England

Hivi ndivyo Di Maria alipotua Manchester United

On the look out: Di Maria peers out of his United car as he arrives for the completion of his trasferKIUNGO Angel di Maria amewasili viwanja vya mazoezi vya Manchester United, Carrington kwa ajili ya kukamilisha uhamisho wa Pauni 60 kutoka Real Madrid ya Hispania.
Nyota huyo wa Argentina aliyeng'ara kwenye Kombe a Dunia amewasili England huku viongozi wa Old Trafford wakiendelea na mazungumzo na Real Madrid juu ya kukamilisha uhamisho wa dau la rekodi Uingereza.
Di Maria, mwenye umri wa miaka 26, anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake usiku huu ambao utamfanya alipwe Pauni 200,000 kwa wiki kwa zaidi ya miaka mitano, mshahara ambao pia utamfanya awe mchezaji wa pili kulipwa zaidi katika klabu hiyo baada ya Nahodha, Wayne Rooney. 
Uhamisho wote utaigharimu United zaidi ya Pauni Milioni 90 na mchezaji huyo ataingia moja kwa moja katika kikosi kilichojeruhiwa cha Louis van Gaal kwa ajili ya mchezo dhidi ya timu iliyopanda Ligi Kuu, Burnley.

Liverpool yamkaribisha Balotelli kwa kichapo


Balotelli akiishuhudia Liverpool ikilala Etihad kwa mabao 3-1
http://img.theepochtimes.com/n3/eet-content/uploads/2014/08/22/453741350-676x450.jpg
Kun Aguerro akishangilia bao lake walipoifumua Liverpool mabao 3-1
VIJANA wa Brendan Rogers, Liverpool wamemtambulisha mshambuliaji wao nyota kutoka AC Milan , mario Balotelli, wamejikuta wakipata kipigo cha mabao 3-1 ugenini mbele ya mabingwa watetezi Manchester City katika mfululizo wa Ligi Kuu ya England.
Machester City ni kama ilimkaribisha tena Balotelli kwenye dimba la Etihad kwa kuwaonyesha kuwa wao ni zaidi kwa ushindi huo ambao umeifanya timu hiyo kujogea kwenye nafasi za juu za msimamo wa ligi hiyo iliyomaliza raunid mbili za awali.
Mabao mawili ya Stevan Jovetic na jingine la Sergio 'Kun' Aguerro yalitosha kuwazima vijogoo vya Anfield ambao wanahaha kusaka mbadala wa mshambuliaji wao nyota waliyemuuza Barcelona, Luis Suarez.
Liverpool ingeondoka patupu Etihad kama siyo beki wa City Zabaleta kujifunga na kuwaoa bao la kufutia machozi na kuwapa wakati mgumu kujiandaa kuwakabili Tottenham Hotspur ambao wanaoongoza msimamo kwa sasa japo wanalinda pointi na Chelsea na City walioruhusu nyavu zao kufungwa bao moja tofauti na Spurs ingawa zote zina pointi 6 na mabao matano ya kufunga.