STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, May 30, 2016

Juanfran wa Atletico Madrid aomba radhi mashabiki

http://www.101greatgoals.com/wp-content/uploads/2016/05/Juanfran-Atletico-Madrid.jpgBAADA ya kukosa penalti katika mechi ya fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya mahasimu wao, Real Madrid, beki wa Atletico Madrid Juanfran Torres amewaomba radhi mashabiki wa klabu hiyo.
Beki huyo wa kulia aliyefunga penati ya ushindi katika hatua ya 16 Bora dhidi ya PSV Eindhoven ndiye aliyekuwa mchezaji pekee wa Atletico aliyekosa penalti kwenye Uwanja wa San Siro, Milan Italia wakati wa mikwaju ya penalti na kusaidia kuipa Real Madrid taji la 11 baada ya Cristiano Ronaldo kufunga ya mwisho.
Real Madrid  ilishinda kwa penalti 5-3 baada ya kumaliza dakika 120 timu zote zikifungana bao 1-1, huku Antonie Griezmann akipoteza penalti ambao ingeweza kuisawazishia Atletico katika kipindi cha kwanza.
Juanfran walitia simanzi akiwashinda wachezaji wenzakwa kwa huzuni kubwa iliyowapata baada ya matokeo hayo na beki huyo amewaomba radhi mashabiki wao kwa kile kilichotokea.
Leo Jumatatu Juanfran ameaandika barua maalum kwa mashabiki wa Atletico Madrid ili kuwaomba radhi kwa kilichotokea. Barua hiyo imetupiwa pia katika akaunti ya klabu hiyo ya Instagram.

Waraka huo  unasomeka hivi;


http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2016/05/Juanfran.jpg
Wakara huo wa Juanfran

 
Hello Atleticos,

Nimeomba klabu kuwafikishia barua juu ya kila kitu ninachojisikia
Kamwe sitasahau moyo wa dhati mlioonesha kwangu wakati nilipokuja kwenu kuomba msamaha. Nikiona machozi yangu yakitiririka mbele ya maelfu ya mashabiki wa Atletico waliofika uwanjani na kunisaidia kuendana na uhalisia wa huzuni kubwa iliyokuwa imejaa kwenye nafsi yangu. Vile vile bila ya kusahau sapoti niliyopata kutoka kwa wachezaji wenzangu, kocha na watu wote wanaounda familia hii ya Atletico.
Pia ningependa kuwashukuru kwa imani kubwa ambayo mara zote mmekuwa mkionesha kwetu na zaidi ya yote ni kutufanya sisi kujiona watu wa tofauti wengine na wenye nafsi ya kipeke kutokana na uwepo wetu hapa Atletico.
Miaka miwili iliyopita, niliwaambia kwamba tungerejea tena fainali na tumefanya hivyo, sasa, nawaambia kwamba, Gabi, nahodha wetu hivi karibuni au baadaye atanyanyua Kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya na kusherehekea sote kwa pamoja.
Nawapenda sana na tusonge mbele Wana-Atletico.

Rashford asaini mkataba mpya mrefu Man United

http://ichef.bbci.co.uk/onesport/cps/800/cpsprodpb/ECD9/production/_89833606_marcus_rashford_cameron_borthwick_jackson.jpg
Rashford kushoto na kinda mwenzake Cameron Borthwick-Jackson wakisaini mikataba yao mipya ndani ya Man United
YAMETIMIA. Straika chipukizi wa Manchester United, Marcus Rashford amesainishwa mkataba mpya utakaoenda hadi Juni 2020.
Mkataba huo umeenda sambamba na kuongezwa kwa mshahara wake kwa wiki ambao sasa atalamba Pauni 20, 000, kitu ambacho kinda huyo ameeleza kufurahishwa nacho.
Rashford amejizolea umaarufu mkubwa katika mechi chache za Man United katika Ligi Kuu ya England na michuano ya UEFA Europa League kwa kuifungia mabao na juzi Jumapili aliandikisha rekodi ya kuwa mchezaji kinda kufunga katika kikosi cha Three Lions akicheza mechi yao ya kwanza kabisa.

Zoezi hilo la kusaini mkataba mpya lilienda sambamba pia kwa chipukizi mwingine, Cameron Borthwick-Jackson ambaye naye atajibanza Man United mpaka 2020.

Rais Magufuli afanya uteuzi mwingine, Anne Makinda aula!

http://i1.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2015/12/REUTERS1083589_Articolo.jpg?resize=640%2C400RAIS wa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli amefanya uteuzi wa viongozi wengine wa tatu.
Rais Magufuli amemteua  Jaji Shabani Ally Lila kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.
Kabla ya uteuzi huo  Jaji Shabani Lila alikuwa Jaji Kiongozi, Uteuzi huu umeanza leo Mei 30, 2016.
Wakati huo huo, Rais Dkt. Magufuli amemteua Spika wa Bunge Mstaafu, Anne Semamba Makinda kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).
Uteuzi wa  Anne Semamba Makinda  umeanza Mei 25, 2016.
Anne Semamba Makinda anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Ali Mchumo. 
Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amemteua Prof. Apollinaria Elikana Pereka kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Teknolojia Dar es salaam (Dar es Salaam Institute of Technology - DIT).
Prof. Apollinaria Elikana Pereka ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) Morogoro.
Prof. Pereka anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Prof. Fredrick Mwanuzi ambaye amemaliza muda wake.Uteuzi huu umeanza leo Mei 30, 2016.

Ngoma? Haendi kokote, uongozi Yanga wasisitiza

Ngoma (kushoto)
TAARIFA hii huenda ikapunguza presha za mashabiki wa Yanga, baada ya uongozi wao kusema kwa herufi kubwa kuwa 'NGOMA HAENDI KOKOTE KULE'.
Uongozi wa Yanga umetoa kauli hiyo kukanusha taarifa zilizoenea mtaani kuwa, straika wao mkali, Donald Ngoma anataka kuihama klabu hiyo.
Kuna taarifa ambazo zimesambaa kupitia baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii zikidai nyota huyo kutoka Zimbabwe aliyefunga mabao 17 katika msimu wake wa kwanza wa Ligi Kuu Bara, alikuwa mbioni kutimkia Afrika Kusini na Misri ambao kuna klabu zinamnyemelea wakati mkataba wake ukiwa umesaliwa na mwaka mmoja kabla ya kuisha.
"Klabu ya bado ina mkataba wa mwaka mmoja na Ngoma baada ya kumalizika kwa msimu huu. Bado hatujapokea ofa kutoka klabu yoyote inayomtaka. Hizo ni taarifa ambazo siyo rasmi na wanachama na mashabiki wanatakiwa kuzipuuza," Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Yanga, Jerry Muro alisema mchana huu.“Ngoma anaipenda Yanga na anafurahia maisha ya Tanzania. Ameshaanza kujifunza Kiswahili na kama mwenzake Kamusoko ambaye tayari anazungumza vizuri Kiswahili, na inaashiria ni kwa kiasi gani anafurahia kuwa hapa”, amesisitiza Muro.
Yanga ilimnyakua Ngoma katikati ya mwaka jana kutoka FC Platinum baada ya mechi yao ya Kombe la Shirikisho ambapo Yanga iliing'oa timu yake kwa mabao 5-2.

Samatta aweka rekodi Ulaya aibeba Genk

Samatta-ushindi 
We're going to Europe!STRAIKA Mbwana Samatta amweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kuiwezesha timu yake kucheza michuano ya Ligi Ndogo ya Ulaya (UEFA Europa League) baada ya kuisaidia Genk ya Ubelgiji kufuzu hatua hiyo kwa kuilaza Charleroi.
Genk iliyopoteza mchezo wa kwanza katikati ya wiki iliyopita kwa mabao 2-0 ugenini iliikandika Sporting Charleroi kwa mabao 5-1.
Samatta aliyeanza kwenye kikosi cha kwanza cha Genk ikiwa mechi yake ya 18 tangu alipojiunga na timu hiyo kutoka TP Mazembe ya DR Congo, aliibeba timu yake hiyo katika mechi hiyo ya Uwanja wa nyumbani wa Cristal Arena.
Mkali huyo na nahodha wa Taifa Stars, alifunga bao moja ambalo lilikuwa ni goli la pili kwenye mchezo huo, huku Mgiriki Nikolaos Karelis akifunga hat-trick akianza na Mkwaju wa penalti dakika ya 17, kisha Samatta akazamisha bao la pili dakika ya 27 kabla ya Sandy Walsh kupiga bao la tatu dakika ya 45.
Kipindi cha pili Genk waliongeza mabao mengine mawili kupitia Karelis aliyefunga bao la nne dakika ya 56 kisha kukamilisha hat-trick yake dakika ya 71 kwa kufunga bao la tano.
Genk imefuzu kucheza michuano ya Europa ligi kwa matokeo ya jumla 5-3 na itaanzia hatua ya awali ya mtoano kabla ya kuingia makundi iwapo itaing'oa timu itakayocheza nao hatua hiyo ya awali ya mtoano.

Huyu dogo, Rashford acha kabisa Man United

KINDA wa Manchester United, Marcus Rashford aliyeibuka msimu huu na kuwa Staa amezawadiwa mkataba mpya ulioboreshwa.
Straika huyo, 18 alisaliwa na mwaka mmoja tu kwenye mkataba wake wa sasa, lakini sasa atapewa mkataba mpya wa muda mrefu na kuzoa Pauni 20,000 kwa wiki.
Wikiendi Rashford, akiichezea England kwa mara ya kwanza kabisa, alifunga bao katika sekunde 138 tu tangu mpira wakati England inaichapa Australia 2-1 na kuweka rekodi kuwa kijana mdogo kabisa kuifungia England katika mechi yake ya kwanza.
Rashford aliibuka Msimu huu kuchezea Man United alipochezeshwa kwa mara ya kwanza Timu ya kwanza dhidi ya FC Midtjylland kwenye Europa Ligi na kupiga Bao 2 na kisha tena kupiga Bao 2 walipocheza na Arsenal kwenye Ligi Kuu England.

Tangu wakati huo, katika Mechi 18 za Man United, Rashford amepiga Bao 8.
Mbali ya Rashford, Kijana mwingine wa Man United ambae nae amebakisha Mwaka mmoja na atapewa Mktaba mpya bora na mrefu ni Cameron Borthwick-Jackson.

JT amuunga mkono Mourinho Man United

NAHODHA wa Chelsea John Terry amemuunga mkono Jose Mourinho kufanikiwa kwenye Klabu yake mpya Manchester United huku akimueleza kuwa Meneja huyo ndie bora kupita yeyote aliewahi kucheza chini yake.
Terry alikaribia kuondoka Chelsea mwishoni mwa Msuimu huu baada ya Mkataba wake kumalizika lakini sasa ameongezewa Mwaka Mmoja na Msimu ujao atakuwa chini ya Meneja mpya wa Chelsea Antonio Conte ambae ni Meneja wa sasa wa Timu ya Taifa ya Italy.

Terry, ambae aliteuliwa na Mourinho kuwa Kepteni wa Chelsea wakati Mourinho alipotua Chelsea kwa mara ya kwanza Mwaka 2004, ameeleza: “Ni habari njema kwa Manchester United. Hii itawafurahisha Mashabiki na Wachezaji wa Man United kwani mara nyingi nimesema Mourinho ndie Meneja Bora niliyewahi kufanya nae kazi!”

Straika wa JKT Ruvu amfunika Ngoma VPL

https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AMd2imIABKJxV0HhggwR2EZOfOM&midoffset=2_0_0_1_8003251&partid=2&f=1214&fid=Inbox&ymreqid=64fe4ec4-e6bf-e94e-012e-44001c010000&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000
Mussa akiwa amebebwa na wachezaji wenzake baada ya kuidungua Simba katika mechi ya kufungia msimu ambapo Simba ilalala mabao 2-1
STRAIKA mkali wa mabao wa JKT Ruvu, Abdulrahman Mussa amembwaga mkali wa Yanga, Donald Ngoma baada ya kuibuka mshindi wa tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu Bara kwa mwezi Mei.
Mussa amewazidi ujanja Ngoma na Ally Nassor 'Ufudu' wa Mgambo JKT aliokuwa akichuana nao katika kinyang'anyiro hicho.
Katika mwezi huo uliokuwa na raundi tatu na uliofungia msimu wa 2015-2016, Mussa alicheza mechi zote tatu za timu yake na kufunga jumla mabao manne, mawili katika kila mechi kati ya michezo hiyo mitatu.
Kwa kufanikiwa kunyakua tuzo hiyo ya Mei straika huyo atazawadiwa kitita cha Sh. 1,000,000 (milioni moja) kutoka kwa wadhamini wa Ligi hiyo, kampuni ya mtandao wa simu za mkononi ya Vodacom.
Washindi wengine wa tuzo hiyo ya mwezi kwa msimu huu ambao mechi zake za mwisho zilichezwa Mei 22 ni; Hamisi Kiiza-Simba (Septemba), Elias Maguli-Stand United (Oktoba), Thabani Kamusoko- Yanga (Desemba), Shomari Kapombe-Azam (Januari), Mohammed Mkopi- Prisons (Februari), Shiza Kichuya-Mtibwa Sugar (Machi) na Juma Abdul wa Yanga (Aprili).

Mkwasa aishtukia Misri, Stars ikiibana Harambee kwao


NA ALFRED LUCAS, NAIROBI
KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya Tanzania, Charles Boniface Mkwasa amesema kwamba mchezo ujao kati ya Mapharao wa Misri na Taifa Stars, utakuwa ni fainali ya kuamua taifa litakalofuzu katika fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika AFCON hapo mwakani kutoka kundi G.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mchezo kati ya Harambee Stars ya Kenya na Taifa Stars ya Tanzania Mei 29, 2016, uliofanyika Uwanja wa Moi Kasarani, Mkwasa maarufu kama Master anasema kwa msimamo na hali ilivyo kwa sasa, “Najua Misri wanatufuatilia. Na hata Kenya kwa siku zote tatu walikuwako. Najua  Misri wanahitaji sare ili wafuzu kwa fainali hizi, lakini hawataipata Tanzania.”


Mkwasa anasema mchezo dhidi ya Misri, ana uhakika vijana wake watajitahidi ili kupata matokeo mazuri baada ya Jumapili kufanya vema dhidi ya Harambee Stars waliocheza mechi hiyo mbele ya mashabiki wao wachache ambao pia hawakuchangamka kama wale wa Tanzania ambao licha ya kuwa ugenini walichangamsha mji na uwanja.

Wakati Misri wana pointi saba, Taifa Stars ina pointi moja na hivyo wa kuibania au kupindua matokeo ya Misri isiende AFCON mwakani, basi ni Tanzania hasa kama itawafunga Mapharao Jumamosi kabla ya kwenda Nigeria Septemba, mwaka huu kucheza na Nigeria.

“Kama nilivyosema, Misri wanakujawanahitaji pointi moja. Lakini sisi tunahitaji pointi tatu. Mchezo wa leo unatosha kuona mapungufu (upungufu). Maana ilikuwa mechi ngumu iliuyojaa nyota wote wa Kenya ambao ni professionals, lakini mimi nilikuwa na local based players na matokeo yamekuwa hayo.

“Tilianza kufunga bao, lakini wakarudisha. Bora mchezo umeishia hivi maana najua Wakenya hawana uvumilivu, tungewafunga hapa sijui kama tungetoka salama,” amesema Mkwasa ambaye baadhi ya waandishi, hususani wale wa Kenya walianguka kicheko kuashiria kuwa kuna matatizo katika utawala wa soka.

Mkwasa anasema ana taarifa namna ambavyo Misri wanaifuatilia Taifa Star hususani ukusanyaji wa video kwa ajili ya kuona aina ya soka la Tanzania, huku akisema: “Hawatafanikiwa kwa sababu soccer is the game of different approach (Soka ni mchezo wenye mifumo tofauti). Hivyo tulivyocheza na Kenya sivyo nitakavyocheza na Misri, nitakuwa na approach yake.”

Anasema ushindi wa Jumamosi ijayo ni wa kuvuna pointi tatu ili kupata kasi ya kushinda mchezo dhidi ya Nigeria na kufungua ukurasa mpya wa Taifa Stars kutengeneza mazingira mazuri ya kuwashinda Nigeria katika mchezo wa mwisho hatua ya makundi utakaofanyika Septemba, mwaka huu.

“Tunaomba Wakenya mtuombee. Nasi tunawaombea ili kama wote inatokea mwaka huu tunakosa mafasi, basi iwe kheri kwa kipindi kijacho. Sisi tumekuja kucheza kwenu katika mji wenu wenye baridi basi nanyi karibuni siku moja dar es Salaam, Tanzania katika mji wetu wetu wenye joto, huenda mkaambulia sare vile vile,” anasema.

Mkwasa alipongeza Shirikisho la Soka Tanzania (FKF), kwa kuandaa mchezo huo angalau kwa asilimia 70 kwa kushirikiana na Tanzania iliyojazia gharama za juu sambamba vijana wake kwa kucheza kwa kujituma licha ya kuwakosa nyota wake wa kulipwa na hivyo kupata picha na mbinu sahihi za kuivaa Misri Jumamosi ijayo.

“Bado tunaendele kujenga timu yetu, wengi ni vijana kama mlivyoona na wengine ni mara ya kwanza wanacheza. Nimewapa nafasi na mmeona uwezo wao, bila shaka tutafanya vema maana wengine ni under 21 wako kwenye kikosi. Huko mbele tutakuwa na timu nzuri,” anasema Mkwasa akimtolea mfano Shiza Ramadhani ambaye alipewa nafasi kwa mara ya kanza katika kikosi cha kwanza akichukua winga ya kulia.


VICTOR WANYAMA
“Kwa hiyo tayari tumeona kitu gani cha kuongeza,” anasema Mkwasa hoja yake iliyoungwa mkono na Nahodha wa Harambee Stars, Victor Wanyama ambaye kwa dakika chache, alizungumza na Ofisa Habari na Mawasiliano wa Shirikisho la Soka Tanzania na kuhoji: “Unasema leo hamkuwa na professional pale uwanjani?” alipohakikishiwa ukweli huo, akasema:

“Basi mna kikosi kizuri. Wengi ni vijana, wanaweza kama mkicheza kwa kutubana kama mlivyobana hapa, Misri mnaifunga na hata hao Nigeria, si ajabu nikasikia mnakwenda AFCON mwakani. Ninaitakia kila la khetri timu hii, nawatakiwa kila la kheri Watanzania katika harakati zao. Sisi mwaka huu tumepotea kabisa, hatuna matumaini tena, tunajipanga ndiyo maana nimekuja kutetea taifa langu, hata kama tumekosa nafasi,” alisema Wanyama anayekipiga Southampton ya England.

Katika mchezo huo, Taifa Stars iliwakosa nyota wake Mbwana Samatta anayechezea Genk ya Ubelgiji kwa kuwa alikuwa na mchezo muhimu wa kupa nafasi timu yake ama icheze Ligi ya Uropa au ibaki nje katika michezo ya kimataifa ngazi ya klabu Ulaya. Shirikisho la Soka Tanzania na Kocha Mkwasa walimruhusu kama ilivyo kwa Thomas Ulimwengu anayekipiga TP Mazembe waliokuwa na mchezo mkali dhidi ya AS Vita ambao wana utani na ushindani mkali wa soka huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).


MWINYI KAZI MOTO
Naye Nahodha wa Taifa Stars katika mchezo huo, Mwinyi Kazimoto amesema kwamba mchezo dhidi ya Kenya, umeonesha picha ya kinachotakiwa kufanyika katika michezo ijayo inayoikabili timu hiyo baada ya kusifu maandalizi, mapokezi mazuri na sapoti nzuri kutoka kwa mashabiki wa Kitanzania, hasa wale waliosafiri umbali mrefu kutoka Dar es Salaam kwenda Nairobi, Kenya kuishangilia Stars. Nahodha wa Taifa Stars ni Mbwana Samatta anayesaidiwa na John Bocco ambao katika mchezo huo, hawakucheza. Bocco ni Majeruhi.

 MCHEZO WA HARAMBEE STARS, TAIFA STARS
Katika mchezo huo, kipindi cha kwanza mashabiki walishuhudia mabao 1-1 kwa kila upande na ndiyo yaliyokuwa matokeo ya mwisho katika dakika 90, lakini kipindi cha pili wadau wa soka walishuhudia mabadiliko ya kila timu kujaribu nyota wake kwa mujibu wa sheria na taratibu za Shirikisho la soka la Kimataifa (FIFA), linaloruhusu kubadili wachezaji hadi wachezaji sita. Lakini hakukuwa na mabadiliko ya matokeo.

Kuhusu mabao ni Elias Maguli ndiye aliyetangulia kuifungia Taifa Stars bao katika dakika ya 30 kwa kichwa baada ya kupokea krosi murua kutoka kwa Juma Abdul kutoka Mashariki ya Uwanja wa Moi Kasarani kabla ya dakika saba baadaye kumfanyia madhambi Winga Ayub Masika ndani ya eneo la hatari hivyo Mwamuzi, Brian Nsubuga kutoka Uganda, kuamuru penalti iliyokwamishwa wavuni na Victor Wanyama.

Katika mchezo huo ambao wakati wote ulikuwa ni wa kushambuliana kwa timu zote mbili, Taifa Stars iliwapumzisha kipa Deogratius Munishi na nafasi yake ikachukuliwa na Aishi Manula na kwa wakati mmoja kuwatoa Jonas Mkude na Shiza Ramadhani na nafasi zao kuchukuliwa na Farid Mussa na Mohammed Ibrahim baadaye Kocha Mkwasa alimwingiza Jeremiah Juma kuchukua nafasi ya Maguli.


Kenya wao waliwatoa Humphrey Ochieng kwa kuingia Cliford Miheso; akatolewa tena Jesse Were kwa Wyclif Ochomo; Ayub Masika akapumzishwa na John Makwata akapewa nafasi kama alivyopumzishwa Anthony Agay na nafasi yake kuchukuliwa na Mayeko Mohammed. Pamoja na mabadiliko hayo, matokeo yalibaki vilevile 1-1 hadi dakika ya 90 katika mchezo ambao Wanyama alipewa kadi ya njano kwa kumfanyia madhambi Kazimoto.

VIKOSI VYA TIMU ZOTE
Vikosi vya kwanza katika mchezo, Kenya: 1. Boniface Oluoch, 9. Joakins Otieno Atudo, 5. Abud Omar Khamis, 12. Eugene Ambuchi Asike, 8. David Owino Odhiambo, 14. Anthony Akumu Agay, 15. Victor Mugubi Wanyama, 23. Ayub Timbe Masika, 19. Humphrey Mieno Ochieng’ 16. Eric Johanna Omondi, 29. Jesse Jackson Were
Wachezaji wa akiba: 3. David Okello Abongo, 10. Eric Ouma Otieno, 6. Mayeko Musa Mohammed, 24. Victor Ali Abondo, 27, Wycliff Okello Ochomo, 20. John Mark Makwata, 21. Clifford Miheso Ayisi

Tanzania XI: 1. Deo Munishi, 6. Juma Abdul Jafari, 2. Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, 13. Aggrey Morris, 15. Erasto Edward Nyoni, 17. Jonas Gellard Mkude, 7. Himid Mao Mkami, 16. Shiza Ramadhan Yahya, 12. Mwinyi Kazimoto Mwitula, 10. Elias Mrugao Maguli, 4. Deus David Kaseke

Wachezaji wa akiba walikuwa: 18. Aishi Salum Manula, 5. David John Mwantika, 9. Farid Mussa Shah, 11. Jeremiah Juma Ally, 8. Abrahim Hajibu Migomba, 3. Mwinyi Haji Mngwali, 14. Mohammed Ally Ibrahim

 WAAMUZI


Brian Nsubuga (Mwamuzi wa kati), Hussein Bugembe (Msaidizi wa Kwanza), Ronald Katenya (Msaidizi wa Pili), Amir Abdi Hassan (Kamishna wa mchezo) and  Davies Omweno (Mwamuzi wa Akiba, Mezani.)

Sunday, May 29, 2016

Waganda kuziamua Taifa Stars v Harambee Stars

NA ALFRED LUCAS, NAIROBI
WAAMUZI watatu wa soka kutoka Uganda, ndio wakaochezesha mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya Taifa Stars ya Tanzania na Harambee Stars ya Kenya utakaofanyika leo Jumapili kwenye  Uwanja wa Moi Kasarani jijini Nairobi, Kenya.
Waamuzi hao watakaochezesha mchezo huo utakaoanza saa 10.00 jioni na kurushwa moja kwa moja na Kituo cha Televisheni cha Azam Tv kwa kushirikishi na Shirika la Utangazaji la Kenya (KBC) ni Brian Nsubuga atakayepuliza kipenga na wasaidizi wake ni Bugembe Hussein upande wa kulia (line 1) na Katenya Ronald kwa upande wa kushoto (line 2).


Kamishna wa mchezo atakuwa Amir Hassan kutoka Somalia ambako Meneja wa Uwanja wa Moi Kasarani, Lilian Nzile amesema kwamba mazingira uwanja ni mazuri na mipango yote ya mchezo huo imekaa vema ikiwa ni pamoja na usalama uliothibitishwa pia na Kanali wa Jeshi la Polisi, Muchemi Kiruhi OCS wa Kasarani.

Kwa upande wa Kocha Mkuu Taifa Stars inayodhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro inayozalishwa na Kiwanda cha Bia Tanzania (TBL), Charles Boniface Mkwasa atawakosa washambuliaji wake watatu katika kikosi ambacho kitaivaa Harambee Stars.

Washambuliaji hao ni Mbwana Samatta kutoka Genk ya Ubelgiji, Thomas Ulimwengu anayechezea TP Mazembe ya Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC) na John Bocco ambaye ni majeruhi wa mguu aliumia wakati wa fainali za Kombe la FA kati ya Yanga na Azam Jumatano wiki hii.

“Madaktari wamempa Bocco saa 72 za mapumziko. Bila shaka kabla ya kucheza na Misri atakuwa amepona,” alisema Mkwasa leo Mei 28, 2016 asubuhi na kuongeza kuwa Samatta ametuma taarifa kukosa mchezo dhidi ya Kenya kwa kuwa ana ratiba ya kucheza mchezo muhimu Mei 30, mwaka huu na matarajio ni kujiunga na timu Juni 1, 2016 kabla ya kuivaa Misri Juni 4, mwaka huu.

Kwa upande wa Ulimwengu, uongozi wa TP Mazembe nao waliomba kumtumia Ulimwengu katika mchezo wa ushindani wa mpinzani wake AS Vita. TP Mazembe na AS Vita ni timu pinzani huko DRC Congo na uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ukaridhia na Mkwasa sasa amejipanga kukiandaa kikosi bila nyota hao mahiri.

“Katika mchezo huu sitakuwa na professionals (wachezaji wa kulipwa),” alisema Mkwasa ambaye jioni ya leo ameahidi kutoa kikosi cha nyota 11 watakaonza dhidi ya Kenya kesho.

Kwa sasa anaangalia namna ya kuipanga vema safu yake ya ulinzi baada ya kumkosa Kelvin Yondani anayetumikia adhabu ya kuonywa mara mbili kwa kadi ya njano hivyo kutojumuishwa kwenye mipango mchezo dhidi ya Misri. Mabeki anaotarajiwa kuanza nao ni Juma Abdul upande wa kulia na Mohammed Hussein upande wa kushoto.

Walinzi wakaoachukua nafasi ya Yondani na Nadir Haroub Cannavaro ambaye hakuongozana na timu katika safari ya Kenya ni Erasto Nyoni, Aggrey Morris na David Mwantika huku viungo wa kati wanaotarajiwa kupangwa ni Mwinyi Kazimoto, Jonas Mkude na pembeni ni Farid Mussa na Shiza Kichuya. Washambuliaji watakaotikisa Kenya katika mchezo wa kesho ni Elisu Maguli na Ibrahim Ajib.

“Kipa anaweza kuanza Dida (Deo Munishi) au Aishi Manula. Lakini hao niliokutajia ni proposed team (kikosi tarajiwa), lakini hasa nani anaaza kesho nitakutajia jioni ya leo mara baada ya mazoezi pale Moi Kasarani,” alisema Mkwasa aliyeonekana kujiamini na mipango yake kama lilivyo jina lake la umaarufu la Master.

“Nimeiandaa timu kucheza mifumo miwili ambayo ni 4-3-3 ambao ni mfumo wa kushambuliaji na pale tutakapokuwa tuna-defense (tunazuia) basi mfumo utakuwa ni 4-5-1,” alisema Mkwasa.

Katika mchezo wa kesho Mkwasa anayesaidia na Hemed Morocco na Manyika Peter anayewanoa makipa atapata nafasi ya kubadili wachezaji hadi sita ambao ni utaratibu wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) kwa mechi za kirafiki za kimataifa kadhalika makubaliano katika mkutano wa kabla ya mchezo wa kesho.

Stars iliwasili Nairobi, Kenya jana asubuhi na kupokewa na wenyeji Shirikisho la Soka Kenya iliyowapeleka hoteli ya Nairobi Safari Club iliyoko mtaa wa Koinange, katikati ya jiji la Nairobi ambako mchana kabla ya kwenda mazoezi ilitembelewa na Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Dk. John Haule aliyewahakikishia usalama  timu hiyo licha ya kuwako kwa taarifa za kuvamiwa.

“Msaada wowote mnaotaka na chochote mnachohitaji tunaomba mtutaarifu tujue namna ya kuwasaidia. Msiwe na wasiwasi kabisa. Hata kama hamjaipenda hoteli, semeni,” alisema Dk. Haule ambaye aliitakia timu mafanikio mazuri katika mchezo wa dhidi ya Harambee na ule wa Mafarao wa Misri.

Viongozi wa msafara wa Taifa Stars, Ahmed Mgoyi na Omar Walii walimweleza Balozi DK. Haule kuridhika na kambi na kwamba hawakupata tatizo lolote hali ilivyo hadi sasa.

Real Madrid vidume Ulaya, yaikandamiza tena Atletico

http://theblogfc.com.au/wp-content/uploads/2014/08/real-madrid-champions-league.jpg KLABU ya Real Madrid usiku wa kuamkia leo Jumapili, imefanikiwa kutwaa taji lake la 11 la Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuilaza kwa mikwaju ya penalti 5-3  mahasimu wao, Atletico Madrid.
Real na Atletico zilimaliza muda wa dakika 120 zikiwa nguvu sawa ya kufungana bao 1-1 katika mchezo mkali wa fainali uliochezwa Uwanja wa San Siro, Milan, Italia.
Kipa Keilor Navas Gamboa alijitanua vizuri langoni na Juan Francisco Torres Belen ‘Juanfarn’ akaona lango dogo na kugongesha nguzo ya pembeni penalti ya nne ya Atletico.
Cristiano Ronaldo akaenda kwa kujiamini kupiga penalti ya mwisho ya Real Madrid na kumtungua kipa Jan Oblak wa Atletico kuwapa Magalactiico taji la 11 la Ligi ya Mabingwa.
Wengine waliofungaa penalti za Real Madrid ni Lucas Vazquez, Marcelo, Gareth Bale na Sergio Ramos, wakati Atletico zimefungwa na  Antonio. Griezmann, Gabi na Saul.
Nahodha wa Reald Madrid, Sergio Ramos akiinua taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuifunga Atletico Madrid kwa penalti 5-3 usiku huu Uwanja wa San Siro PICHA ZAIDI GONGA HAPA   

Mchezo huo uliochezeshwa na marefa wa England, Mark Clattenburg aliyesaidiwa na Simon Beck na Jake Collin, Real Madrid walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa beki wake na Nahodha, Sergio Ramos dakika ya 15 aliyemalizia mpira wa kichwa wa winga Gareth Bale.
Baada ya bao hilo, Real waliuteka mchezo na kupeleka mashambulizi mengi langoni mwa Atletico, lakini bahati haikuwa yao.
Kipindi cha pili, kocha Diego Simeone wa Atletico alianza na mabadiliko, akimpumzisha kiungo Muargentina mwenzake Augusto Matias Fernandez na kumuingiza kiungo Mbelgiji Yannick Ferreira Carrasco.
Mabadiliko hayo yalikuwa msaada kwa kikosi cha Simeone, kwani ni Carrasco aliyekwenda kuisawazishia Atletico dakika ya 79, akimalizia pasi ya Juan Francisco Torres Belen, maarufu kama Juanfran.
Bao hilo ‘likauamsha’ upya mchezo huo, timu zote zikicheza ka nguvu na kasi kusaka bao la ushindi, lakini dakika 90 zikamalizika kwa sare ya 1-1.
Awali ya hapo, mshambuliaji hatari wa Atletico Madrid, Antonio Griezmann alipaisha mkwaju wa penalti dakika ya 48 baada ya Fernando Torres kuangushwa na Pepe kwenye boksi.
Kocha Mfaransa, Zinadine Zidane aliwapumzisha Karim Benzema, Daniel Carvajal na Toni Kroos kipindi cha pili na kuwaingiza Isco, Danilo na Lucas Vazquez.
Katika dakika 30 za nyongeza timu zote zilicheza kwa tahadhari mno na mwishoni mwa mchezo, Simeone akawatoa Filipe Luis na Koke na kuwaingiza Lucas Hernandez na Thomas Teye Partey.
  Kwa ushindi huo Real inafikisha mataji 11 ya Ligi ya Mabingwa, mengine ikitwaa misimu ya 1955–1956, 1956–1957, 1957–1958, 1958–1959, 1959–1960, 1965–1966, 1997–1998, 1999–2000, 2001–2002 na 2013–2014.

Saturday, May 28, 2016

United? Mawe subiri mshtukizwe na Zlatan Ibrahimovic


http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/photo/2014/0605/fc_ibrahimovic_rh_1296x729.jpg&w=738&site=espnfcMSHAMBULIAJI wa KImataifa wa Sweden, Zlatan Ibrahimovic amekuwa akihusishwa na kutaka kutua Manchester United ili kuungana na Kocha wake wa zamani, Jose Mourinho, lakini wakala wake wamesema klabu atakayojiunga nayo itashangaza wengi.
Wakala wa mchezaji huyo, Mino Raiola, alisema Straika huyo ambaye mkataba wake na PSG imeisha hakuna anayejua atatua wapi na hivyo mashabiki wasubiri kushtukizwa tu.
Nahodha huyo wa Sweden mwenye miaka 34, kwa sasa anaendelea na maandalizi ya kuiongoza timu yake katika michuano ya Fainali za Kombe la Ulaya itakayoanza Juni 10 nchini Ufaransa.
"Sidhani kama atajiunga na United, na wala hakuna anayelala Sweden kwa sasa hakuna anayejua kitakachotokea," alisema Raiola.
Wakala huyo alisema bila shaka mwisho wa yote watu watashangazwa na maamuzi ya mkali huyo kwa klabu atakayojiunga nayo kwa msimu ujao.
"Bado hatuajamua, lakini itashangaza wengi mwishowe. Watu wanazungumza kuhusu United, ila ukweli utafahamika tu na ndio maana hatusemi mengi kwa waandishi wasubiri waone wenyewe," alisema wakala huyo.

Mascherano, Higuain wajipa tumaini kwa Messi Copa America 2016

http://static.dnaindia.com/sites/default/files/styles/half/public/2016/05/28/465312-messi-injury.jpg?itok=WVjhADzW
Messi akisaidiwa kutoka uwanjani jana Ijumaa alipoumia katika mechi yao ya kirafiki dhidi ya Honduras
HOFU tupu. Kuumia kwa nyota wa Argentina, Lionel Messi kumezua hofu miongoni mwa wachezaji wa timu yake ya taifa inayojiandaa na fainali za michuano ya  Copa America zitakazoanza mwezi ujao nchini Marekani.
Javier Mascherano na Gonzalo Higuain kwa nyakati tofauti wamenukuliwa wakisema kuwa wana matumaini nahodha wao huyo, Lionel Messi atakuwa fiti kabla ya kuanza kwa fainali za Copa America 2016.
Messi aliumia jana Ijumaa katika mechi za kirafiki ya kimataifa dhidi ya Honduras na kusababisha hofu kubwa kwa wachezaji, mashabiki wa Argentina.
Mwanasoka huyo bora wa dunia, alitolewa Uwanjani baada ya kudondoka vibaya na kujiumiza mgongo na mbavu zake kwenye mjini San Juan waliposhinda bao 1-0.
Kocha Mkuu wa Argentina, Gerardo Martino alisema yu tayari kupokea taarifa zozote juu ya majeraha ya Messi, wakiwa wanakabiliwa na mchezo wa ufunguzi dhidi ya watetezi Chile Juni 6.
Hata hivyo mchezaji mwezake wa Barcelona Javier  Mascherano amesema anatumaini Messi atapona haraka na kurejesha Uwanja kwa ajili ya michezo ya Copa America.
Kauli kama hiyo ilitolewa pia na mfungaji wa bao pekee katika mchezo huo wa Honduras, Gonzalo Hiuguain, alisema anaamini tatizo lililompata nyota wao halitakuwa kubwa kiasi cha kumkosa kwenye michuano hiyo migumu.

Spurs yakimbilia Wembley kwa Uefa Champion League ijayo

https://static.guim.co.uk/sys-images/Sport/Pix/columnists/2015/1/28/1422488355275/tottenham-010.jpgKLABU YA Tottenham Hotspur imetangaza kuwa itacheza mechi zake za Ligi ya Mabingwa Ulaya mwakani kwenye Uwanja wa Wembley.
Spurs ipo katika maandalizi ya kuukarabati Uwanja wao wa White Hart Lane, hivyo imeona ni vema mechi zake za UEFA ikacheza. katika Uwanja huo wa Taifa wa Uingereza wa Wembley.
Timu hiyo iliyomaliza Ligi Kuu ya England msimu huu kwa kushika nafasi ya tatu imethibitisha taarifa hizo leo Jumamosi kwa sababu ya upishaji wa matengenezo na upanuzi wa uwanja wao.

Chama cha Soka cha Uingereza (FA) kimewapa ofa pia timu hiyo kucheza mechi zao zote za Ligi Kuu za nyumbani na na zile michuano mingine ya makombe ya Uingereza kwenye Uwanja huo wa maarufu wa Wembley.

'Juventus? Hapana Dani Alves hajasaini bhana!'

http://static.pulse.ng/img/football/origs4099488/8810481433-w980-h640/danialves-cropped-nghtlocydwb61j2jec4boxnqp.jpgWAKALA wa beki kisiki wa Barcelona, Dani Alves amekanusha taarifa kuwa mteja wake amesaini mkataba wa awali na Juventus, japo amekiri kuwa mabingwa hao wa Italia na klabu nyingine zinamwinda mchezaji huyo. 
Vyombo vya habari nchini Hispania viliripoti juzi kuwa beki huyo wa Barcelona anatarajiwa kuondoka baada ya kutimukia timu hiyo kwa miaka nane na kwenda Turin kwa mkataba wa miaka mitatu. 
Hata hivyo, wakala wake ambaye pia amewahi kuwa mke wake, Dinorah Santa Ana da Silva alikanusha taarifa hizo akidai hazina ukweli wowote. 
Dinorah aliongeza kuwa hakuna klabu yoyote ambayo Alves aliyosaini nayo mpaka sasa kwani amehamishia nguvu zake zote katika timu ya taifa ya Brazil ambayo inakabiliwa na michuano ya Copa America inayotarajiwa kuanza mapema mwezi ujao. 
Wakala huyo aliendelea kudokeza kuwa, ni kweli amekutana na Juventus lakini sio wao peke yao bali ameshakutana pia na klabu nyingine, ila hakuna dili lolote lililoafikiwa mpaka sasa.

Kocha Benitez akomaa na Newcastle United 'mchangani'

Benitez Akisaini Mkataba huo wa kumweka Newcastle United Miaka 3Wakati wa Mkutano na Waandishi wa habari juu ya kuongeza Miaka 3 kuifundisha Klabu hiyo ya Newcastle UnitedKwenye Mkutano na Waandishi huko St. James Park
KOCHA Rapa Benitez amesaini mkataba wa miaka mitatu wa kuendelea kuinoa Newcastle United licha ya klabu hiyo maarufu England kushuka daraja msimu huu.
Benitez alisaini mkataba huo baada ya mkataba wake wa muda mfupi wakati akipambana kuiokoa Newcastle isizame kumalizika. Kocha huyo ameahidi kuirejesha timu hiyo Ligi Kuu ya England akiamini alicheleweshwa kukabidhiwa timu wakati ikiwa na hali mbaya. VIjana hao wa Benitez walimaliza msimu kwa kutoa kipigo kitakatifu kwa Tottenham Hotspur na kuinyima nafasi ya kumaliza ikiwa ya pili na badala yake kuwaacha mahasimu wao wa London ya Kaskzini, Arsenal wakiibamba nafasi hiyo nyuma ya Leicester City walikuwa mabingwa wapya wa England.

Simba jeuri bwana, yamlipa Mosoti na kuwaokoa Wakimataifa

http://taarifa.co.tz/wp-content/uploads/2015/02/musoti.jpg
Mosoti
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEijkioCMLTxbWmSc7Or2shgbE674AVVOh8YREydnX4Y5pvner4ydWT610U0c1usyjR8IfbiAf_g6S3i-E4u_ylGIZCrsSr_-gUGX0_JaOfiXiQo9pb9KI0WWeEJyEj_SnYTR4TR7HnQCUGb/s1600/HANS+POPPE.jpg
Zakaria Hanspoppe
YAEPUSHA ugomvi. Klabu ya Simba imemaliza utata baada ya kumlipa chake, aliyekuwa beki wao wa kati, Mkenya Donald Mosoti na kujiepusha kushushwa daraja na pia kuikoa Tanzania isifungiwe na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA).
Simba imemlipa Mosoti fedha zake za malimbikizo ya usajili na fidia nyingine zinazokaribia Sh Milioni 64.2 Mei 19 mwaka huu ikiwa ni wiki moja na ushei kabla ya siku ya mwisho waliyopewa na FIFA kabla ya kuchukuliwa hatua za kukiuka maamuzi ya Baraza la Usuluhishi la klabu Shirikisho hilo la Dunia.
Kabla ya Simba kulipa fedha hizo ambazo Mosoti amethibitisha kupata taarifa mapema wiki hii, Yanga kupitia Msemaji wake, Jerry Muro, ilitaka Simba iwapelekee nyaraka za deni inalodaiwa na Mosoti ili walipe kupitia Mamilioni ya fedha walizovuna kupitia michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika hatua ya makundi.
Siku chache baada ya Muro kutoa kauli hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo, Zakaria Hans Poppe alisema klabu yao ina uwezo wa kulipa fedha hizo na isingehitaji msaada kutoka kokote.
Mosoti aliiburuza Simba FIFA kutokana na kuvunja mkataba wake wa kuichezea klabu hiyo kienyeji na hata ilipotolewa hukumu ya kumlipa Mkenya huyo, Simba ilipuuza ndipo mapema mwezi huu FIFA iliiagiza TFF kuilazimkisha Simba imlipe Mosoti ndani ya mwezi mmoja la sivyo Iishushe Daraja na yenyewe (TFF) itafungiwa kwa michuano ya kimataifa, jambo ambalo lingeizuia Yanga kucheza hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho.

Friday, May 27, 2016

Ratiba nzima ya Yanga na wenzake Kombe la Shirikisho Afrika


Yanga kikosi
Mashabiki

 Round 1

June 17
FUS RabatAl Ahly Tripoli


Kawkab MarrakechEtoile Sahel


MazembeMedeama


MO BejaiaYoung Africans
Round 2

Juni 28 Al Ahly TripoliKawkab Marrakech


Etoile SahelFUS Rabat


MedeamaMO Bejaia


Young AfricansMazembe
Round 3

Julai 15 Etoile SahelAl Ahly Tripoli


Kawkab MarrakechFUS Rabat


MO BejaiaMazembe


Young AfricansMedeama
Round 4

Julai 26 Al Ahly TripoliEtoile Sahel


FUS RabatKawkab Marrakech


MazembeMO Bejaia


MedeamaYoung Africans
Round 5

Agosti 12Al Ahly TripoliFUS Rabat


Etoile SahelKawkab Marrakech


MedeamaMazembe


Young AfricansMO Bejaia
Round 6

Agosti 23FUS RabatEtoile Sahel


Kawkab MarrakechAl Ahly Tripoli


MazembeYoung Africans


MO BejaiaMedeama

Kijana anusurika kufa kwa kujirusha kutoka mnara wa simu

Kijana Mmoja (picha) Jijini Mwanza amenusurika kifo baada ya kujirusha kutoka katikati ya mnara wa simu.
Tukio hilo limetokea hii leo na kuvuta watu wengi waliofika kumshuhudia kijana huo ambae amepanda katika mnara huo tangu majira ya asubuhi na kukatalia mnarani hadi majira ya saa sita mchana.
Mashuhuda wa tukio hilo ambao pia ni marafiki wa karibu na kijana huyo, wamesema huenda kijana huyo amefikia maamuzi hayo kutokana na ugumu wa maisha ambao amekuwa akiulalamikia huku wengine wakisema ni kutokana na kuathiriwa na matumizi ya dawa za kulevya ikiwemo gundi ambayo amekuwa akiyatumia.
Akizungumza kwa niaba ya Kamanda wa jeshi la uokoaji na zima moto mkoani Mwanza, mmoja wa maafisa wa uokoaji Mussa Kaboni, amsetoa rai kwa makampuni yenye minara ya simu kuimarisha ulinzi katika minara hiyo ili kuondoa hatari inayoweza kujitokeza kutoka kwa raia wasio wema.
Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo walionekana kuchukizwa na kitendo cha kijana huyo na kusikika wakifoka kwa hasira na makelele ya hali ya juu "rukaa, ruka sasa, jirushe kama wewe ni mwanaume" hali ambayo ilikuwa ikimuongezea morari kijana huyo na hivyo kujirusha kweli kutoka katikati ya mnara huo.
Baada ya kijana huyo kujirusha kutoka katikati ya mnara hadi chini, alipoteza fahamu na kukimbizwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Mwanza, Sekour Toure kwa ajili ya huduma ya kwanza.
Credit:Mwanaharakati Mzalendo

Fomu za Uchaguzi Yanga zadoda Karume

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgrzE3bbtu7GRPgGN93LhICuCjwQRZE3vqY_pGiWVkAF9jOSdE1Vzs2La-FJH2SHaflrratFARxI8Kpk9nWsIf5KHY24cksHhFC4MeNgvfpBsCC8hqwZR4sJoE1lsIf5F2cNVttMU0iWYcp/s1600/Page+2.JPG
Manji (kati)n akitetea na Cannavaro na Chuji misimu kadhaa ya nyuma ya Ligi Kuu Bara
FOMU za Uchaguzi Mkuu wa Yanga zimesuswa baada ya kushindwa kujitokeza hata mwanachama mmoja wa klabu hiyo kuchukua ili kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.
Kamati ya Uchaguzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ilitangaza leo Ijumaa ndio siku ya kufunguliwa kwa zoezi hilo, lakini mpaka jioni hii hakuna aliyejitokeza, huku kukiwa na taarifa kwamba Yanga wameugomea uchaguzi huo.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Alloyce Komba amedokeza kuwa, hakuna aliyejitokeza kuchukua fomu, lakini akiamini muda bado kwani wana siku 5 za zoezi hilo kufikia tamati.
Hata hivyo MICHARAZO imenasa taarifa kuwa, uchaguzi huo umesuswa na wana Yanga baada ya kutaka usifanyike kipindi hiki ambacho klabu yao itakuwa kwenye pilikapilika za kuelekea kwenye mechi zao za kimataifa ya Kombe la Shirikisho.
Yanga imepangwa Kundi A na timu za MO Bejaia ya Algeria, TP Mazembe ya DR Congo na Medeama ya Ghana na itaanza mechi zao siku mbili kabla ya kuvaana na Bejaia mjini Algiers, Algeria.
Uchaguzi wa Yanga umepangwa kufanyika Juni 15, lakini uongozi wa klabu hiyo ukitaka ufanyike tarehe moja na uchaguzi wao mdogo uliofanyika Julai 15, 2012 na kumuingiza Mwenyekiti na tajiri wao, Yusuf Manji.

Ronaldo kwa vijembe hajambo, awakejeli Barcelona kimtindo

http://u.goal.com/2890500/2890552.jpgHEBU msikieni CR7. Straika nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amesema kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya itakuwa na thamani kubwa zaidi kuliko mataji mawili yaliyonyakuliwa na wapinzani wao, Barcelona msimu huu.
Ronaldo aliye na umri wa miaka 31 aliyekuwa majeruhi katika wiki za karibuni na kumfanya akose mechi ya nusu fainali ya mkondo wa kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Manchester City ni kama amewapiga kijembe wapinzani wao hao.
Hata hivyo juzi aliwaondoa hofu mashabiki wa timu hiyo akidai kuwa atakuwa fiti kwa asilimia 100 kwa ajili ya fainali hiyo dhidi ya Atletico Madrid.
Akihojiwa Ronaldo amesema kama wakishinda taji hillo la Ligi ya Mabingwa itakuwa ni thamani kubwa zaidi kwao kuliko mataji mawili ya Barcelona waliyoshinda hivi karibuni, kwani taji la michuano hiyo ya Ulaya liko katika ndoto za kila mchezaji. Klabu hasimu za jiji la Madrid, Real Madrid na Atletico Madrid zitakutana kesho Jumamosi katika fainali ya tatu zilizozikutanisha timu za Hispania na mechi ya fainali ya pili baina yao baada ya mwaka juzi 2014 kukutana na Real kushinda 4-1.

Kaka akumbukwa Brazil, aitwa kuziba pengo la Costa

http://www.fantasista10.co.uk/wp-content/uploads/2015/03/Kaka-orlando1.jpg
Kaka akiwajibika kwa klabu yake ya Orlando
BADO wamo. Straika mkongwe wa Brazil anayeichezea klabu ya Orlando City, Kaka ameitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya nchi yake kwa ajili ya michuano ya Copa America akichukua nafasi ya Douglas Costa.
Costa mwenye umri wa miaka 25, amepata majeraha ya misuli ambayo yatamfanya akose michuano hiyo maalumu ya kuadhimisha miaka 100 toka kuanzishwa kwake. Kaka mwenye umri wa miaka 34 ameichezea Brazil mechi 91 na kufunga mabao 29 katika kikosi hicho.
Costa alikuwa sehemu ya kikosi cha Bayern Munich ambacho kimeshinda taji la Bundesliga na Kombe la Ujerumani katika msimu wa mwisho wa Pep Guardiola na timu hiyo.
Brazil imepangwa kufungua pazia la Copa America kwa kucheza na Ecuador katika Uwanja wa Rose Bowl huko Pasadena, California Juni 4 mwaka huu, huku mechi zao nyingine mbili za kundi B zitakuwa dhidi ya Haiti na Peru.

Yanga yaibania Simba kucheza kimataifa

Yanga
Simba
 MWAKA wa hasara ni wa hasara tu. Baada ya ndoto za kucheza fainali za michuano ya Nile Basin iliyopangwa kufanyika Sudan kupotea hewani, Simba imeikosa tena fursa nyingine ya kushiriki michuano ya kimataifa mwaka huu.
Simba ilikuwa ikijipa matumaini ya kuwemo kwenye michuano ya Kombe la Kagame iliyopangwa kufanyika kuanzia mwezi ujao nchini, lakini michuano hiyo sasa haitafanyika tena Tanzania baada ya TFF kuchomoa kuiandaa.
Shirikisho hilo la Soka Tanzana, limetangaza kutoandaa michuano hiyo  inayohusisha timu za nchi wanachama wa Shirikisho la Soka la Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), maarufu kama Kombe la Kagame kwa mwaka 2016 kama ilivyopendekezwa.
Sababu za TFF ya kutoandaa fainali hizo ni kwa kubanwa na ratiba ya michuano ya kitaifa na kimataifa.
Awali mkutano mkuu wa CECAFA, uliamua Zanzibar iwe mwenyeji wa michuano ya Kagame.
Baadaye kwa sababu zilizo nje ya uwezo wa ilionekana Zanzibar hawataweza kufanya.
Baada ya hapo TFF ilianza kuangalia uwezekano wa mashindano haya kwa kumshirikisha mabingwa wa 2015/16 ambao ni Yanga.
Kutokana na ratiba ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika (CAFCC) iliyotolewa na Shirikisho la Soka la Afrika (CAF), kipindi ch Juni hadi Agosti, 2016 Yanga watakuwa na kwenye michuano ya CAF hatua ya makundi hivyo ushiriki wao CECAFA utakuwa mgumu ilihali michuano ya CECAFA imepangwa kufanyika Juni na Julai, mwaka huu.
Watetezi wa taji hilo ni Azam na tayari Yanga ilikuwa ikisita kushiriki na kutoa nafasi kubwa kwa Simba kubeba jukumu, lakini kwa hali ilivyo watabidi wasubiri sana.

Dani Alves ainyima ubingwa Real Madrid Ulaya

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2016/05/17/16/344C8FAD00000578-0-image-a-60_1463500208098.jpg
Dani Alves
https://cdn2.vox-cdn.com/thumbor/7-e7Hp4ZSgo6fGmgV0DLxHNGWuQ=/0x25:3000x2025/1310x873/cdn0.vox-cdn.com/uploads/chorus_image/image/49093871/GettyImages-515165792.0.jpg
Atletico Madrid
KUELEKEA kwenye Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya itakayochezwa kesho Jumamosi, Beki wa Barcelona, Dani Alves amekiri kuwa angependelea zaidi Atletico Madrid ishinde taji hilo kuliko mahasimu wao Real Madrid.
Atletico na Madrid zitavaana kesho, katika mechi ya kisasi kwea kocha Diego Simeone ambaye alifungwa kwenye fainali ya mwaka juzi na mabingwa hao wa kihistoria wa michuano hiyo ya Ulaya kwa mabao 4-1.
Atletico walio chini Diego Simeone ndio waliowang’oa mabingwa watetezi Barcelona katika hatua ya robo fainali ya michuano hiyo kabla ya kuitoa tena Bayern Munich kwenye hatua ya nusu fainali.
Madrid ndio timu pekee iliyopo mbele ya Atletico kwasasa ikiwa ni kama marudiano baada ya ile fainali ya mwaka 2014 ambapo Madrid waliibuka kidedea kwa kushinda mabao 4-1 katika muda wa nyongeza.
Hata hivyo, Alves ana mawazo tofauti katika fainali hiyo itakayofanyika katika Uwanja wa San Siro jijini Milan nchini Italia kwani anadhani Atletico wanastahili zaidi taji hilo kuliko Madrid. Alves amesema Atletico ni timu ambayo imepambana sana mpaka kufikia hapo walipo hivyo anadhani wanastahili taji hilo