STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 25, 2013

Simba yatoa msimamo kuahirishwa ghafla kwa mechi yao na Ruvu Shooting



Na Ezekiel Kamwaga
UONGOZI wa Simba umekubaliana na hatua ya serikali kuzuia kuchezwa kwa mchezo uliopangwa kuchezwa leo wa Ligi Kuu ya Tanzania baina ya Wekundu wa Msimbazi na Ruvu Shooting Stars.
Hata hivyo, uongozi wa Simba haujafurahishwa na namna uzuiaji huo ulivyofanyika. Taarifa imetolewa leo kwenye siku ya mechi yenyewe wakati maandalizi yote yakiwa yamefanyika na hivyo kusababisha matatizo katika sehemu kubwa tatu.
Mosi, uongozi wa Simba umeingia gharama kubwa ya kuweka timu kambini na kujiandaa na mechi. Pili, benchi la ufundi na wachezaji walikuwa tayari wamejiandaa na mechi kimwili na kiakili na kuahirishwa huku kwa mechi kumesaidia tu kuvuruga programu. Tatu, wapenzi na washabiki wa Simba wamepata usumbufu wa kwenda uwanjani na kukuta hakuna mechi.
Uongozi wa Simba unapenda kutumia nafasi hii, katika namna ya kipekee kabisa, kuwaomba radhi wapenzi na wanachama wake ambao walifika Uwanja wa Taifa kutazama mechi ambayo haikuwapo.
Washabiki ndiyo wanaoifanya Simba na mchezo wa mpira wa miguu nchini uwe na umaarufu ulionao na bila wao ligi yetu inaweza kupoteza nguvu na ushindani ilionao.
Simba SC inapenda kuwe na utaratibu unaojulikana wa kuahirisha mechi wa walau saa 48 kabla ya siku ya mechi. Hii itasaidia pande zote zinazohusika. Kama mechi imeshindikana kwa sababu za nje ya uwezo wa kibinadamau (Force de Majeure) kama vile mafuriko, tetemeko la ardhi na vimbunga, mechi inaweza kuahirishwa ghafla lakini si kwa mechi ambayo uwepo wake ulifahamika miezi kadhaa nyuma.
Tunashauri pia kwamba siku za mechi ambapo Ligi Kuu inachezwa (match days), inatakiwa kuwa zinafahamika na isiwe kila siku mechi zinachezwa. Simba ilikuwa na mechi wikiendi iliyopita na Ruvu ilikuwa na mechi Mbeya zaidi ya wiki moja iliyopita na hivyo mechi hii ingeweza kuchezwa hata jana (Jumatano) ambayo ni siku ya kawaida kwa mechi kuchezwa badala ya leo Alhamisi.
Ni matumaini yetu kwamba kuahirishwa kwa mechi hii kutakuwa fundisho kubwa katika upangaji wa ratiba na uahirishaji wa mechi ambao una faida kwa pande zote husika.


Poppe arejea Simba
MWENYEKITI wa Simba, Mhe, Ismail Aden Rage, amemshukuru aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu, Zacharia Hans Poppe, kwa kukubali kurejea kushikilia nyadhifa zake zote.
Poppe alitangaza kujiuzulu nyadhifa zake za uongozi ndani ya Simba Machi 7 mwaka huu, kutokana na hali ya migogoro iliyokuwapo wakati huo.
Hata hivyo, Rage alikataa kujiuzulu huko kwa Poppe na akasema atamshawishi abadili maamuzi kwa manufaa ya Simba.
“Napenda kutumia nafasi hii kuwaarifu wana Simba popote walipo kwamba Poppe amerejea na yuko tayari kuitumikia Simba kama Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba,” alisema Rage.
Kwa upande wake, Poppe alisema amerejea Simba kutokana na utulivu ulioanza kujitokeza klabuni na kwamba nia yake ni kuhakikisha klabu inafanya usajili mzuri na wa kiwango kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu.

GHANA KUWAKA MOTO KWA MASUMBWI


By Onesmo Ngowi
GHANA, one of the boxing powerhouses in African continent is edging towards three biggest IBF tournaments next week on May 3rd, 2013 at the Accra Sports Arena in Ghana
Princess Hellen Joseph

GoldeMike Boxing Promotion Syndicate is at it again and this time Ghanaian boxing stakeholders and the whole of West Africa region will enjoy a thrilling moment which they all have been carving for.

This is one of the major IBF tournaments in Sub Sahara Africa and nothing is being left to chance as the promoters “Henry Many-Spain and Michael Tetteh” painstakingly deal with all the final details for this epic duel!
Albert Mensah (right)
Drawing the line of this epic boxing tournament is none other than two of the Ghanaian’s most fiercest opponents in Jr. Middleweight, Albert Mensah when he confront his archenemy Ben Odemattey.
 
The duo is battling for the “IBF Continental Africa Jr. Middle Weight Crown”. Came sun, come rain one of them would be the King of the Jr, Middleweight in Africa.
 
Following this epic bout, will be the Princessfrom Nigerian boxing royal family, Princess Helen Joseph when she goes toe to toe with another Princess from Austro-Hungarian Boxing Empire, Princess Marianna Gulyas.

The two beautiful Princesses who would pass in a beauty-parget are battling for the “IBF vacant Intercontinental Featherweight Female Crown”.

"We are definately going to get the crown" said Koffi Dakku-Ricketts,the man who is behind Princess Helen's success as a trainer. Ricketts boast of many similar success stories and make him one of the best trainers Ghana has ever had in years!
 
This has been “a seek and hide game” for the past two years but, this time around, no ground can hide any of the two as the moment of truth is about to come.
 
The man of the moment is none other than the Ghanaian ups and comings boxing star and Olympiad boxer “Issa Samir” in a duel of his life when he host the handsome Georgian true-nan and flamboyant “Robison Omshashavili” for the vacant “IBF World Jr. Middleweight Crown” in a 12 rounds epic battle.
 
The bout christened“The Battle of the Gold Coast” would rekindle the memory when one of the Ghanaian boxing king, Professor Azumah Nelson when hosted Sidnei Dal Rovere in a similar battle at the Accra Sports Stadium in 1988.
 
The ground can be “quicksand” for the two as they crave to prove to the whole world that they are indeed “pound for pound” gladiators and future world champions on the rise!
 
This is; in a matter of fact “a thumb up” for Ghana as it makes African continent proud once again after shining out during the last “World Cup tournament” in South Africa.

Hii kali! Sherehe za Muungano zakwamisha pambano la Simba na Ruvu Shooting Taifa

 
Viongozi wakuu wa TFF, Leodger Tenga na Angetile Osiah
Na Boniface Wambura
PAMBANO la Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Ruvu Shooting na Simba iliyokuwa ichezwe leo (Aprili 25 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeahirishwa mpaka Mei 5 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.

Kisa cha kufanyika ghafla kwa mabadiliko ya pambano hilo imetokana na Serikali kuutumia uwanja kwa ajili ya maandalizi ya sherehe za Muungano ambazo kitaifa zitafanyika kesho (Aprili 26 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawaomba radhi washabiki kwa usumbufu uliojitokeza kutokana na mabadiliko hayo na ghafla. Ratiba ya mechi nyingine za VPL zinabaki kama zilivyo.

Kitendo hicho cha mechi hiyo kuahirishwa ghafla kinauonyesha umuhimu wa klabu na hata FA kumiliki uwanja wake ili kuondokana na matatizo kama hayo yanayolitia doa soka la Tanzania.

Hata hivyo pamoja na pambano hilo kupigwa 'dochi' hadi Mei 5, TFF imesisitiza kuwa ratiba nyingine za ligi hiyo inayopelekea ukingoni itaendelea kama ilivyo, ambapo kesho (Aprili 26 mwaka huu) Coastal Union na Azam itakayochezwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Jumapili 'Mnyama' Simba itaikaribisha Polisi Moro kwenye pambano litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa siku ya Jumapili (Aprili 28 mwaka huu).

Msondo Ngoma yapeleka mpya Magereza

Waimbaji nyota wa Msondo Ngoma, Shaaban Dede 'Kamchape' na Juma Katundu 'JK wa Msondo'
BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Msondo Ngoma,  inatarajiwa kuwapelekea burudani mashabiki wao wa maeneo ya Mtoni kwa Aziz Ali na Magereza Ukonga.
Msemaji wa Msondo, Rajabu Mhamila 'Super D' aliiambia MICHARAZO kuwa, bendi yao imeongeza ratiba ya kutoa burudani wiki hii kwa mashabiki wa maeneo hayo.
Alisema Msondo inayojiandaa kupakua albamu mpya ya 'Suluhu' leo itatoa burudani Mtoni kwa Aziz Ali kabla ya kesho kwenda Magereza Ukonga.
"Jumatano na Alhamisi tutakuwa tukitoa burudani katika maeno hayo, na Ijumaa hadi Jumapili ratiba inabaki kama ilivyo," alisema.
Alisema kwa kuwakumbusha mashabiki wao, Ijumaa hufanya vitu vyao Leaders na Jumamosi  huwa TCC Chang'ombe na Jumapili watavuka bahari hadi Kigamboni.
"Jumapili tutakuwa G-Five Kigamboni, ambapo Msondo itapiga nyimbo za zamani na mpya zilizoifanya iitwe Baba ya Muziki," alisema.

CATHERINE FOUNDATION YATOA MSAADA DODOMA


Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda na Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Catherine Magige wakiwakikabidhi zawadi mbalimbali kwa watoto wanaolelewa kwenye kituo cha Matumaini cha mjini Dodoma.

ASASI ya Kijamii ya Catherine Foundation jana imetembelea kituo cha kulelea wa watoto cha Matumaini Village kilichopo mkoani Dodoma ambapo walikwenda kutoa misaada mbalimbali wakiongozwa na Mkurugenzi wa Asasi hiyo, Catherine Magige.
Katika Hafla hiyo Mgeni Rasmi alikuwa Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda ambapo asasi hiyo ilitoa vitu mbalimbali vikiwemo, Madaftari, Mafuta, Sabuni, Juice, miswaki na dawa zake, mchele, sukari, nguo za watoto, kanga za wakinadada wanaowalea watoto hao na vingine vingi.

 
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda akihutubia katika hafla hiyo.
Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Catherine Magige akihutubia katika hafla hiyo jana.
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda akiwakikabidhi zawadi mbalimbali kwa watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho.
Mkurugenzi wa Catherine Foundation, Catherine Magige akiwakiwapa zawadi mbalimbali kwa watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho.

Sikinde kutambulisha mpya wakielekea Mbeya kwenye Mei Day

Waimbaji wa Mlimani Park 'Sikinde' Hassani Kunyata, Abdallah Hemba na Hassani Bitchuka 'Stereo' watakaotoa burudani kwa wakazi wa jijini la Mbeya na vitiongoji vyake kuanzia kesho wakienda kwenye Mei Day

BENDI kongwe ya muziki wa dansi nchini, Mlimani Park 'Sikinde' inatarajiwa kutambulisha nyimbo zake mpya katika miji kadhaa wakati wakielekea Mbeya katika sherehe za Mei Day.
Sikinde imealikwa kutumbuiza katika sherehe hizo ambazo kitaifa zitafanyikia kwenye mkoa huo wa Mbeya wiki ijayo.
Katibu wa bendi hiyo, Hamis Milambo alisema wakati wakiwa njiani kuelekea Mbeya watafanya maonyesho kadhaa katika maeneo mbalimbali na nje na ndani ya mkoa huo.
Milambo alisema maonyesho hayo yataanza kesho Ijumaa watakapotambulisha nyimbo zao kwenye ukunbi wa Comfort Chamazi, kabla ya Jumamosi kuwa City Pub uliopo Mwanjelwa.

Sikinde itaendeleza makamuzi yake siku ya Jumapili eneo la Tunduma kabla ya siku ya Mei Mosi kutumbuiza kwenye sherehe za Mei Daya asubuhi kwenye uwanja wa Sokoine kabla ya usiku kufanya vitu vyao ukumbi wa Benjamini Mkapa mjini humo.
"Siku ya Mei Mosi tukishatoka kutumbuiza uwanja wa Sokoine tutafanya onyesho katika ukumbi maarufu mjini humo kisha kuanza safari ya kurejea Dar kuendelea na mengine," alisema.
Milambo anasema katika maonyesho yote watatambulisha nyimbo zao wanazoziandaa kwa ajili ya albamu mpya kama 'Jinamizi la Talaka', 'Kuvunjika kwa Dole Gumba', 'Nundule' na nyingine.
"Pia tutawapa burudani mashabiki kwa kuwakumbusha vibao vyetui vya zamani vilivyotufanya Sikinde kutambuliwa kama 'Mabingwa wa Muziki wa Dansi Tanzania," alisema Milambo.

Ally Mustafa 'Barthez' afichua siri nzito Yanga

Kipa Ally Mustafa 'Barthez' akiwa mazoezini

KIPA tegemeo wa vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Ally Mustafa 'Barthez' amefichua siri akidai kung'ara kwake katika msimu wa kwanza ndani ya Yanga kumetokana na kuaminiwa na makocha pamoja na kuungwa mkono na wachezaji wenzake, wanachama na mashabiki wa klabu hiyo.
Barthez aliyeitwa kwenye kikosi cha pili cha timu ya taifa 'Young Taifa Stars', alisema pia kiu kubwa ya mafanikio aliyokuwa nayo na kutaka kuwadhihirishia Watanzania kwamba yeye ni mkali ndiyo iliyomfanya kujituma zaidi na kuipigania Yanga kufanya ilivyofanya msimu huu.
Akizungumza na MICHARAZO, Barthez aliyetua Yanga akitokea Simba alikokuwa akisugua benchi nyuma ya kipa Juma Kaseja, alisema ameweza kung'ara kwa sababu makocha aliokutana nao Jangwani walimuamini na kumpa nafasi ya kuonyesha kipaji alichonacho.
Barthez, alisema ni vigumu kwa mchezaji yeyeote kuweza kuonyesha ubora wake kama hapewi nafasi na hata yeye hakuonekana bora mahali alipotoka kwa vile hakuamini na kupewa nafasi ya kucheza tofauti na tangu atue Yanga.
"Najisikia faraja kufanikiwa kuisaidia Yanga, pia kurejesha heshima yangu, lakini hii haikuja kimiujiza bali ni kutokana na makocha wangu kuniamini na kunipa nafasi sambamba na ushirikiano mzuri ninaopata kwa wachezaji wenzangu na sapoti kubwa ya wanachama na mashabiki," alisema.
Kipa huyo aliyewahi kutamba na timu mbalimbali za wilayani Ilala kabla ya kupanda daraja na Ashanti United kisha kunyakuliwa na Simba mwaka 2005, alisema bado hajaridhika na mafanikio aliyonayo akiota kuisaidia zaidi Yanga na hasa kwenye michuano ya kimataifa.
Barthez aliyetua Yanga na mguu mzuri kwa kuiwezesha kuibebesha taji la Kombe la Kagame kwa mara ya pili mfululizo Julai mwaka huu kisha kukaribia kuipa taji la 23 la Ligi Kuu Tanzania Bara, alisema anatambua changamoto inayomkabili kuendelea kubaki kuwa bora na atajituma zaidi.

Zahoro Pazi ajiandaa kutimkia Celtic ya 'Sauzi'

Zahoro Pazi (kulia) alipokuwa na kikosi cha Azam kabla ya kupelekwa kwa mkopo JKT Ruvu

MSHAMBULIAJI wa Azam FC anayecheza kwa mkopo katika klabu ya JKT Ruvu, Zahoro Pazi anatarajiwa kuondoka nchini kwenda Afrika Kusini kwa mara ya pili kujiunga na klabu ya Bloemfotein Celtic ya nchini humo.
Celtic inayoshiriki Ligi Kuu ya nchi hiyo (PSL), ilimuita na kumfanyia majaribio mchezaji huyo mapema mwaka huu na kuelezwa kuwa alifaulu lakini kwa kuwa nafasi ilikuwa ni ya mchezaji mmoja tu, alichukuliwa Mzimbabwe Roderick Mutuma.
Hata hivyo, mara aliporejea nchini Pazi alisema aliahidiwa na klabu hiyo kuitwa tena mara baada ya msimu huu kumalizika ili kuendelea kujifua na timu hiyo kwa ajili msimu ujao na kwamba safari hiyo ingefanyika mwezi Mei.
Akizungumza na MICHARAZO jana, Pazi alisema mapema wiki hii alipigiwa simu na kocha wa klabu hiyo, Clinton Larsen, na kumfahamisha kuwa ajiandae kwenda nchini humo mwezi Juni wakati mazoezi ya kusaka wachezaji wa msimu ujao utakapoanza.
"Ile safari yangu haitakuwa tena Mei, nimepigiwa simu na kocha wa Celtic na kunieleza kwamba mazoezi yao kwa ajili ya kujiandaa msimu mpya yataanza mwezi Juni, hivyo natakiwa niende wakati huo," alisema Pazi.
Alisema kusogezwa mbele kwa safari yake kumekuwa ni nafuu kwake akiamini kutamfanya ajifue zaidi ili atakapoenda awe katika kiwango kile kile kilichoivutia klabu hiyo iliyomuona kwenye michuano ya Kombe la Kagame na Kombe la Hisani nchini DR Congo.
"Ligi yao kama yetu itaisha mwezi ujao, na kwa vile safari itakuwa Juni naamini nitatumia muda uliosalia kujifua zaidi ili niendapo huko niwe katika kiwango kile kile na kufanya niweze kujiunga nao, naamini Mungu ataniwezesha kutimiza ndoto zangu kucheza soka la kulipwa," alisema Pazi.
Mchezaji mwingine wa Azam, Abdulhalim Humud 'Gaucho' naye amefaulu majaribio yake katika klabu ya Jomo Cosmos na atajiunga nao Julai mwaka huu kwa ajili ya msimu mpya.

Mbio za kinyang'anyiro cha Redd's Miss Tanzania zaanza rasmi


Mshindi wa Redd's Miss Tanzania 2012, Brigitte Alfred

HARAKATI za awali za kumsaka Redd’s Miss Tanzania zinaanza rasmi mwishoni mwa wiki hii wakati kutakapokuwa na kinyang’anyiro cha kuwapata warembo wa vitongoji katika maeneo mbalimbali nchini wakiwamo wa vyuo vya elimu ya juu (Redd’s Miss High Learning), imefahamika.
Taarifa kutoka kwa waandaaji wa shindano la Redd’s Miss High Learning mkoani   Morogoro, zinaeleza kuwa mwakilishi wao atasakwa mkoani humo kesho. Imefahamika vilevile kuwa Jumamosi, pia kutakuwa na kinyang'anyiro cha aina hiyo mkoani Dodoma wakati atakaposakwa mrembo wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), mwakilishi wa vyuo vya elimu ya juu kutoka mikoa ya Kagera na Mwanza.
Mratibu wa shindano la Redd’s Miss Morogoro High Learning, Verdian Kamugisha, alisema kuwa kila kitu kimekamilika na kutakuwa na burudani za kutosha wakati watakapokuwa wakimsaka mwakilishi wao.
“Tumekamilisha kila kitu na warembo wote wako katika hali nzuri na kutakuwa na burudani za kutosha. Wakazi wa Morogoro waje kuwaunga mkono warembo wetu ili hatimaye tupate mwakilishi atakayepeperusha vyema bendera ya mkoa huu," alisema Kamugisha.
Mratibu wa Shindano la Redd’s Miss UDOM, Rachel Matina, alisema vilevile kuwa wamekamilisha maandalizi wanaamini kwamba kazi iliyobaki ni kwa watu wa Dodoma kujitokeza keshokutwa kushuhudia namna washiriki kutoka Chuo Kikuu Dodoma walivyopania kulitwaa taji la Redd’s Miss Tanzania mwaka huu.
Joseph Rwebangira anayeratibu shindano la wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu wa mikoa ya Kagera na Mwanza, alisema mrembo wao atapatikana keshokutwa katika shindano litakalofanyika jijini Mwanza na wanachosubiri sasa ni kwa mashabiki wa mikoa hiyo kujitokeza kwa wingi ili kuwaunga mkono warembo wao na pia kupata burudani mbalimbali.
Katika hatua nyingine, shindano la kumsaka mrembo wa kitongoji cha Hai mkoani Kilimanjaro linatarajiwa pia kufanyika mjini humo mwishoni mwa wiki hii, kama ilivyo kwa kinyang'anyiro cha kuwasaka warembo wa kitongoji cha Tarime mkoani Mara.
Hivi sasa, shindano la Redd’s Miss Tanzania hudhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia kinywaji chake cha Redd’s Original. Mshindi wa shindano hilo ngazi ya taifa huiwakilisha nchi katika shindano la kumsaka mrembo wa dunia.

Lewandowski ainyanyasa Real Madrid Ligi ya Ulaya

Robert Lewandowski aliyeiua Real Madrid jana usiku
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Poland Robert Lewandowski usiku wa jana aliinyanyasa atakavyo Real Madrid baada ya kuwatungua mabao manne na kuiwezesha klabu yake ya Borussia Dortmund kuizabua timu hiyo ya Hispania kwa mabao 4-0 katika pambano la Nusu Fainali Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Lewandowski aliyefunga bao mopja kipindi cha kwanza na mengine kipindi cha pili, ameiweka mabingwa wao zamani wa Ulaya kutoka Ujerumani ambao hivi karibuni walitemesha taji la Bundesliga, katika nafasi nzuri ya kufuzu fainali.
Mkali huyo anayefukuziwa na klabu mbalimbali za Ulaya ikiwamo Manchester United, alifunga bao la kwanza dakika ya nane, kabla ya nyota wa Madrid, Cristiano Ronaldo kusawazisha bao dakika mbili kabla ya mapumziko.
Akiwainyanyasa atakavyo ngome ya Madrid, Lewandowski alifunga mabao mawili ndani ya dakika tano mara baada ya kipindi cha pili kuanza akifunga la pili dakika ya 50 na kuongeza jingine dakika ya 55 kabla yua kumalizia udhia dakika ya 67 kwa bao la penati.
Kipigo hicho kimeiacha Madrid wakiwa hoi wakisubiri miujiza kupitia kocha wao Mreno Jose Mourinho kusaka ushindi katika mechi ya marudianoi itakayochezwa wiki ijayo nyumbani kwao ili kufuzu fainali wakihitajika kushinda mabao 3-0.
Pia kipigo hicho cha Madrid jana kimeongeza machunbgu ya Wahispania ambao walikuwa wakiota kushuhudia fainali ya El Classico Mei 25 kufuatia Barcelona juzi kugaragazwa na mabingwa wa Ujerumani na wanafainali wa mara tatu katika miaka miaka minne Bayern Munich kwea mabao 4-0 na kufifisha matumaini hayo.