STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, June 5, 2013

Busara Agro Machinery kutambulisha magari mapya mbio za PUMA Rally Juni 14

Wadhamini wa mbio hizo za magari za Juni 14
Na Seleman Msuya
KAMPUNI ya Busara Agro Machinery Tanzania imesema itafungua mashindano ya mbio za magari za jijini Dar es Salaam kwa kutumia magari yao ya Polaris Range RZR ili kuweza kuyatambulisha magari hayo hapa Tanzania.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo Mhandisi Oded Kit wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi huyo alisema lengo lao ni kuhakikisha kuwa magari hayo yanatambulika katika mashindano ambapo watakuwa wakifanya maandalizi ya kushiriki mashindano mbalimbali ambayo yatakuwa yakiandaliwa hapa nchini.
Alisema wameshashiriki katika mashindano yaliyopita hivi karibuni ya Arusha Enduro ambapo pia walikuwa kama wafunguzi wa njia ya mashindano lengo likiwa ni kutambulisha magari yao ambayo yamekuwa yakishiriki mashindano ya kimataifa.
Mhandisi Kit alisema Polaris Range RZR ni magari ambayo yanakimbia na imara hivyo wana uhakika kuwa yatafanya vizuri kwa siku za karibuni.
Alisema kampuni yao imedhamiria kuwawezesha madereva ambao wanahitaji kushiriki mashindano ambapo wametoa punguzo la asilimia 30% ya bei ya magari hayo ambayo yanatoka nchini Marekani.
Kit alisema mashindano ya magari yanahitaji maandalizi ya kutosha kuanzia dereva mwenyewe gari, na mahitaji mengine kutokana na ukweli kuwa ni kazi ngumu na ya kuhatarisha maisha.
“Tumesikia kilio chao hivyo tunawaomba waje ili waweze kupata magari imara kwa bei ndogo ambayo tumetoa punguzo la asilimia 30% hivyo tunaamini mtu yoyote akitaka anaweza kununua”, alisema.
Kwa upande wake Fundi Mkuu wa Busara Agro Machinery Denis Gastelleir alisema katika kuonyesha ubora wa magari yao wanatarajia kuwa na magari matatu ambayo yatashiriki katika mashindano ya magari ya PUMA ambayo yatafanyika kuanzia 14 hadi16 mwezi huu kwa kulometa 400 hapa jijini Dar es Salaam.
Alisema magari hayo ambayo yanatokea nchini Marekani yamekuwa yakishiriki katika mashindano mbalimbali kama Dakar Rally na mengine mengi yanayofanyika hapa duniani.
Katika hatua nyingine Kampuni ya mafuta ya PUMA Tanzania imejitolea kudhamini mashindano yam bio za  magari zitakazofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Juni 14 hadi 16.
Hayo yamesemwa na Rais wa Chama Cha Magari Tanzania Nizar Jivan wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii jijini Dar es Salaam.
Alisema pamoja na kampuni hiyo ya mafuta ya PUMA pia zipo kampuni zingine ambazo zimejitokeza kudhamini mashindano hayo ambayo yatashirikisha madereva kutoka katika nchi mbalimbali za Afrika.
Rais huyo alizitaja kampuni tanzu katika kudhamini mashindano hayo kuwa ni pamoja na SUNVIC Express, D.B Shapriya , A TO Z, NIC, CMC, Automobile Ltd, Knight Support, M/S Busara Agro Machinery, New Africa Hotel, Monster Energy Drink, Hari Singh and Sons Ltd, Waljis Travel Bureau and Tazara Reailway.
Jivan alisema hadi sasa ni madereva 25 ambao wamethibitisha kushiriki katika mashindano hayo ambapo 18 ni Watanzania na 7 wanatoka nje ya nchi ambapo amewataka madereva wengine wenye sifa wajitokeze ila.
“Tarehe 14 hadi 16 tunatarajia kuwa na mashindano ya kukimbiza magari ambayo yatakuwa ni ya kilometa 400 na yatafanyika hapa Dar es Salaam ambapo tutatumia barabara mbalimbali tukianzia Tazara”, alisema.
Rais huyo alisema katika mashindano hayo kutakuwa na magari mbalimbali kama Subaru Impreza R14, Mistubish Evolution X, Subaru Impreza N12, Mistubishiu Evolution 8, Subaru Impreza MY04, Subaru Impreza MY03, Mistubish Evolution IX, Subaru Impreza MY06, Subaru LEGACY, Mistubish Galant VR4, Toyota CelicaGT-4, Mistubish EvolutionIV, Subaru Impreza GC8, Range Rover, Toyota Land Cruser, VW Beetle, Nissan 240Z na Toyota Spinter.
Naye Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Mafuta ya PUMA ambao ndio wadhamini wa kuu wa  mashindano hayo Philippe Consaletti alisema wao wamejipanga kuendelea kudhamini mashindano hayo kama moja ya sehemu ya faida yao ambayo wanaipata hapa nchini.
Consaletti alisema katika kutekeleza hilo wanatarajia kudhamini mashindano ya mwaka ujao ambapo wameahidi kuwa yatafanyika mkoani Arusha wakati ukifika.
Kwa upande wake Kamanda wa Usalama Barabarani Kamishna Mohammed Mpinga amewahakikishia madereva na raia ambao watakuwa katika maeneo ambayo magari yatapita kuwa usalama utakuwepo.
Mpinga aliwataka raia kuzingatia na kufuata utaratibu ambao utakuwa unatumika ili kuepusha kero mbalimbali ambazo zinaweza kutokea.

Mabondia Francis Miyeyusho,Mashali kupamba usiku wa matumaini Taifa


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEinRhjpHSbCg9922iuKEu7yRGuZPivlZYKf5raXPv4zYh46zFQoJQ0-1Sh6iLAKEVHIbv3u3aFQ0lHTdlr_OU9lIuCGjNoDBHEDotXfejWXg0vtj6VvPMB_uhMfTLKiCj0cwmyJUrBGp-GB/s640/miyeyusho3.JPG
Francis Miyeyusho

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgtcm3L7pzcbja7bSnx_bJy-ImxGoBHRqZqfw5QUsg3g5ocnIaLOkRpz-LEPJGDUySKvqg1G_zJ11McXXzRECzzEm3xIIYxJrvk0zRrkugyCJ2Hx9PHrLbn-wMfi2SGRUeXMUb8SU9J0cg/s1600/IMG_5146.JPG
Thomas Mashali

MABONDIA nyota nchini Francis Miyeyusho na Thomas Mashali wanatarajiwa kupigana na mabondia kutoa nchi jirani za Kenya na Uganda katika kulinogesha Tamasha la Usiku wa Matumaini linalotarajiwa kufanyika Julai 7 mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Tamasha hilo litakalofanyika kwa mara ya pili tangu kuanzishwa kwake linaratibiwa na kampuni ya Global Publishers na litasimamiwa na Oganaizesheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO).
Akizungumza na MICHARAZO, Rais wa TPBO-Limited, Yassin Abdallah 'Ustaadh' alisema  Miyeyusho bingwa wa Afrika wa uzani wa Bantam na Mashali bingwa wa Afrika Mashariki na Kati uzito wa Kati ndiyo watakaopamba usiku huoi utakaokuwa na burudani mbalimbali siku hiyo.
Ustaadh alisema mabondia hao wa Tanzania watapanda ulingoni siku hiyo kwenye uwanja wa Taifa kuzipigana na mabondia kutoka Kenya na Uganda ambao majina yao yatarajaiwa kuanikwa hivi karibuni.,
"Tumewateua mabondia Francis Miyeyusho na Thomas Mashali ili waweze kupambana na mabondia toka nje ya nchi kati ya Kenya na Uganda na kwa sasa tunaendelea na mawasiliano na vyama vya mchezao huo vya nchi hizo ili kupata majina ya wapinzani wa mabondia wetu," alisema Ustaadh.
Ustaadh alisema mabondia hao wa Tanzania hawatawaangusha Watanzania siku ya tamasha hilo ambalo mwaka jana lilishuhudiwa bondia Francis Cheka akimkimbia kwenye ulingo, bingwa wa Taifa wa PST, Japhet Kaseba.
Kama ilivyokuwa mwaka jana tamasha hilo la 'Night of Hope', lina lengo la kusaka fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni kwa wanafunzi wa kike nchini.

FM Academia kupamba Miss Kigamboni Ijumaa


Katika harakati za kumpata mrembo wa taifa atakayewakilisha nchi katika mashindano ya urembo ya dunia, baadhi ya vitongoji vya DSM vinaendelea na maandalizi ya kupata warembo wake ambapo vitongozi wa SINZA na KIGAMBONI vitapata warembo wake Ijumaa wiki hii yaani Juni 7, ambapo kwa shindano la Kigamboni bendi ya FM Academia 'Wazee wa Ngwasuma' wanatarajiwa kupamba kwa kutoa burudani. Shindano hilo la Redds' Miss Kigamboni 2013 linaratibiwa na mwanadada Somoe Ng'itu anayeoonekana hapo pichani juu.

Uchaguzi Mkuu wa BFT sasa Julai 7


Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga
UCHAGUZI Mkuu wa Shirikisho la Ngumi za Ridhaa Tanzania (BFT) ambao awali ulitangazwa ungefanyika mwishoni mwa Mei, sasa umepangwa kufanyika Julai 7, jijini Mwanza.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolea na BFT ikisainiwa na Katibu Mkuu wake, Makore Mashaga uchaguzi huo ufanyika sambamba na michuano ya Majiji ambayo nayo iliahirishwa mpaka Julai badala ya Mei kama ilivyokuwa imepangwa.
Taarifa hiyo inasema kuwa nafasi zitakazowaniwa katika kinyang'anyiro hicho ni Urais, Makamu wake, Katibu Mkuu, Mhazini na Wajumbe 9 wa Kamati ya Utendaji wa shirikisho hilo zitakazohusisha Kamati za Mipango na Fedha, Waamuzi na Majaji, Mashindano na Vifaa, Walimu, Ufundi na Utafiti, Kamati ya Uhusiano, Habari na Masoko,  Wanawake, Kamati ya Maendeleo ya Mikoa na Taasisi za Umma.
Kamati ya Tiba na Kamati za Maendeleo ya Vijana na Wachezaji.
Fomu za uchaguzi huo zimeshaanza kutolewa tangu leo Jumanne (04/06/2013) katika Ofisi za Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na zoezi litaendelea hadi Julai 7, ambapo ada za fomu hizo zimepangwa kulingana na nafasi ambayo mgombea atajitokeza kuiwania.
Kwa fomu ya kuwania nafasi ya Rais, ada yake ni Tsh. 150,000/=, Makamu wa Rais, Katibu Mkuu na Mweka Hazina kila moja ni Tsh. 100,000/=, wakati kwa nafasi ya Ujumbe kila fomu itauzwa kwa Tsh. 50,000/=
BFT imetoa wito kwa  watanzania wenye uwezo wa kuongoza michezo kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu za kugombea nafasi kama zilivyoelezwa hapo juu.

Wafanyakazi TTCL wafanya usafi Muhimbili kuadhimisha siku ya Mazingira Duniani

Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya simu nchini TTCL wakijumuika kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo wafanya kazi hawo walikuwa wakiungana na watu wote duniani kuadhimisha siku hiyo ambapo wamewaomba wananchi kuwa na moyo wa kufanya usafi katika maeneo yanayowazunguka na kuto tupa takataka ovyo TTCL ina azimisha siku hiyo kwa kaulimbiu yao ya 'TTCL  huleta watu karibu'


Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya simu nchini TTCL wakijumuika kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo

Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya simu nchini TTCL wakijumuika kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo

Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya simu nchini TTCL wakijumuika kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo

BAADHI YA MAOFISA WA TTCL WAKIWA NA MAFAGIO KWA AJILI YA KUSAFISHA MAZINGIRA YA MAENEO YA HOSPITALI YA TAIFA


BAADHI YA MAOFISA WA TTCL WAKIWA NA MAFAGIO

Maelfu wajitokeza kumuaga Ngwair

Sehemu ya umati uliojitokeza kumuaga Ngwair viwanja vbya leaders
Diamond Platnumz akipita mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu Albert Mangwea kutoa heshima zake za mwisho.


Rais wa Chama cha Wanamuziki Nchini.

Mwili wa marhemu Albert Mangwea ukiwa kwenye jeneza tayari kwa watu kutoa heshima za mwisho



Umati wa watu wakiwa wamepanga mstari tayari kwa kwenda kuaga huku kikosi cha msalaba mwekundu na polisi kikiwa stand by.
Baadhi ya wasanii wa bongo wakiwa kwenye mstari tayari kwa kuaga.








Umati wa waliojitokeza kumuaga Ngwair leo(Picha zote Mpekuzi Huru)



    




Simba, Golden Bush kupimana ubavu Jumamosi

Kikosi cha Golden Bush
Kikosi cha Kikijifua uwanja wa Kinesi
TIMU isiyofungika ya Golden Bush Fc ya jijini Dar es Salaam inayoshiriki Ligi Daraja la Nne Wialaya ya Kinondoni, wikiendi hii itashuka dimbani kupimana ubavu na Simba inayojiandaa na michuano ya Kombe la Kagame itakayofanyika nchini Sudan.
Kwa mujibu wa taarifa ya Mlezi wa Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico' pambano hilo la kirafiki ya kujipima nguvu litafanyika siku ya Jumamosi saa 10:30 jioni kwenye uwanja wa Kinesi.
Ticotico alisema mechi hiyo ni muhimu mno kwa vijana wake, lakini pia amemwagia sifa kocha wa Simba, King Abdallah Kibadeni kwa kukubali ombi la timu hizo kupepetana.

Taarifa rasmi ya Golden Bush iliyotumwa na Ticotico kwa blogu hii ni kama ifuatavyo hapo chini;

Naomba nitoe taarifa kwamba siku ya jumamosi weekend hii pale uwanja wa Kinesi timu yetu ya vijana Golden bush itaumana uso kwa uso na Simba sports club kuanzia saa kumi na nusu jioni. ni game ambayo Simba watatumia kama maandalizi yao ya mwishomwisho kwa ajili mashindano ya Kagame Cup huku Golden bush tukitumia game hiyo kungalia vijana wetu wameiva kiasi gani ajili ya mzunguko wa pili wa ligi daraja la nne Kinondoni. tunawaomba mashabiki, wapenzi, wadau, wakereketwa tufike Kinesi jumamosi jioni ili tushuhudie mpambano wa kutaka na shoka.

Aidha nichukue nafasi hii kumpongeza King Kibadeni kwa kukubali game yetu bila mizengwe, ikumbukwe kwamba King ndiye alifanikisha game yetu na Kagera sugar wakati ule akiwa kocha wao. juzi tena Uongozi umeomba game na bila ajizi King kasema kipigwe siku ya jumamosi.

Najua veterans watakuwa na game weekend hii na kama itakuwa jumamosi basi mkae mkao wa kula maana Golden bush tutao burudani asubuhi na jioni, kwa kiswahili unapiga nyuma na mbele.

naomba kutoa hoja.