STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, August 15, 2015

Azam wazidi kunoa makali Zanzibar

11846696_1009621735744849_7161429854397873130_n
Kikosi cha Azam kilipopelekea Kombe lao la Kagame Ikulu kwa Rais Jakaya Kikwete
BAADA ya kuikong'ota KMKM ya Zanzibar katika pambano lao la kirafiki, mabingwa wa Kombe la Kagame, Azam jioni ya leo inatarajiwa kushuka Uwanja wa Amaan kucheza mchezo wake wa pili visiwani humo wakiwa wamepiga kambi kujiandaa na mchezo wao wa Ngao ya Hisani dhidi ya Yanga wikiendi ijayo.
Azam chini ya kocha Stewart Hall imejichimbia humo ikiwa na kikosi chake chote isipokuwa Allan Wanga aliyepo Kenya alipoenda kwa matatizo, huku Mganda Brian Majwega akiwa ametemwa rasmi kikosini.
Mabingwa hao wanajaribu kusaka ushindi kwa mara ya kwanza kwenye mechi ya Ngao ya Hisani kwani tangu mwaka 2012 haijawahi kushinda mbele ya Simba na Yanga waliowatungua mara mbili mfululizo ikiwamo mwaka 2013 walipowafunga bao 1-0 na mwaka jana kuwafumua mabao 3-0.
Azam inatarajiwa kurejea jijini Dar es Salaam Jumanne baada ya kuwepo kwa taarifa ya ziara ya TP Mazembe kufutwa rasmi, na kabla ya kutimka visiwani inaelezwa kuwa huenda ikaiita URA ambayo leo inashuka Uwanja wa Taifa kucheza na Simba katika pambano la kirafiki la kimataifa, ili angalau kuwapa makali ya kuikabili Yanga ambayo ina hasira ya kung'olewa kwenye Kombe la Kagame kwa matuta.

Ratiba ya Ligi Kuu ya England wikiendi hii ipo hivi

optimized-premier-league-2015-2016-700x400

BAADA ya Mashetani Wekundu, Manchester United jana kupata ushindi na kukwea kileleni mwa Msimamo, Ligi ya England itaendelea leo na kesho kwa michezo kadhaa na ratiba kamili tunakuwekea kama ifuatavyo:

Jumamosi Agosti 15
14:45 Southampton vs Everton
17:00 Sunderland vs Norwich
17:00 Swansea vs Newcastle
17:00 Tottenham vs Stoke
17:00 Watford vs West Brom
17:00 West Ham vs Leicester
Jumapili Agosti 16
15:30 Crystal Palace vs Arsenal
18:00 Man City vs Chelsea

Jumatatu Agosti 17
22:00 Liverpool vs Bournemouth
 

Huku Simba, kule Yanga Utamu Ulioje!

https://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2015/08/KIKOSI.jpg
Kikosi cha timu ya Simba
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhgBANjTf-2fkrx3RLm5RPaUrUbyBwYcFEdzPN7vo1to9_q2hUECoRKM5sjZMEd6wKlYjM72Itb9JeMgpbevjrJZAmBeXrbFiVN2ohR7iP20AWcyQ7rwfR__s4p6_Gx2dc7gmy0Ivy3BZ6R/s640/DSC_6726.JPG
Mabingwa wa Tanzania Yanga
WAKATI kocha Dylan Kerr akiwa na mtihani mwingine mgumu wa kutaka kuwathibitishia mashabiki wa Simba kwamba kikosi chake kimeiva wakati jioni ya leo Jumamosi watakabiliana na URA ya Uganda, watani zao Yanga wenyewe wataendeleza libeneke lao jijini Mbeya kesho kuwa kuumana na Mbeya City.
Mechi hizo za kirafiki ni maalum kwa maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu, ambapo Simba yenyewe baada ya kuweka kambi ya mwezi mmoja na ushei katika wilaya ya Lusohoto, Tanga na Zanzibar imerudi jijini Dar es Salaam ikijifua Uwanja wa Chuo cha Polisi Kurasini na leo itaumana na URA Uwanja wa Taifa.
Mechi hiyo ni ya sita kwa Kerr tangu apewe jukumu la kuinoa timu hiyo akimpokea Goran Kopunovic, akiwa na rekodi ya kushinda mechi zote, zikiwemo tano na timu za visiwani Zanzibar na moja ya kimataifa walipoumana na SC Villa ya Uganda kwenye tamasha la Simba Day Jumamosi iliyopita.
Simba inatarajiwa kuwatumia nyota wake wale wale iliyowatumia katika mchezo wao na Villa, huku ikiwa imeshamalizana na nyota wao wa kimataifa, Vincent Agban na Justice Majabvi.
Yanga wenyewe ambao wamekimbilia Tukuyu Mbeya baada ya kutolewa Kombe la Kagame, kesho Jumapili itaumana na Mbeya City katika mechi yao ya tatu jijini humo, awali ilianza kwa mkwara kwa kuitandika Kimondo Fc ya Mbozi kwa mabao 4-1 kabla ya bkuizabua Prisons Mbeya kwa mabao 2-0 na baada ya mchezo hio wa kesho itawasubiri Zesco ya Zambia na Bata Bullets ya Malawi kumaliza kazi kabla ya kurudi Dar kuisubiri Azam kwenye pambano la Ngao ya Hisani litakalochezwa Jumamosi ijayo.
Mechi hiyo ya Ngao ya Hisani itakayopigwa Uwanja wa Taifa ni maalum katika kuzindua msimu mpoya wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara amabyo itaanza kutimua vumbi lake, Septemba 22.

Manchester United yafanya kweli Ligi Kuu ya England

Luke Shaw grabs Januzaj after his opening goal put Manchester United on course for their second consecutive victory
Januzaj akishangilia bao lake la wachezaji wenzake wa Man United
MASHETANI Wekundu, Manchester United usiku wa jana walifanikiwa kukwea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu kwa mara ya kwanza msimu huu baada ya kushinda baoa 1-0 ugenini dhidi ya Aston Villa.
Baoa pekee la dakika ya 29 lililofungwa na Adnan Januzaj limewawezesha vijana wa Louis Van Gaal kushinda mechi ya pili mfululizo katika Ligi Kuu ya England na kukaa kileleni ikiwa na pointi 6.
Pambano hilo lililochezwa Uwanja wa Villa Park, liliwahishwa kuchezwa kutokana na muingiliano wa masuala ya kijamii karibu na mji huo na Mashetani WEkundu wakaona wafanye yao mapema kabla ya kuelekea kwenye pambano lao la mchujo la Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Warusi.
Januzaj alifunga bao hilo akimalizia pasi murua ya Juan Mata. Ligi hiyo itaendelea leo kwa michezo kadhaa, lakini kivumbi kitakuwa kesho kati ya Manchester City dhidi ya mabingwa watetezi Chelsea kwenye Uwanja wa Etihad, mjini Manchester. Tayari makocha wa timu hizo wametoa tambo zaom lakini Manuel Pellegrin amesisitiza ni lazima safari hii ampe mkono Jose Mourinho.

Hapana! Hii ni Barcelona kweli? Yapigwa 4-0 na Bilbao

Athletic Bilbao's defender Mikel San Jose points to the heavens after scoring an incredible goal to put the underdogs ahead
Wachezaji wa Bilbao wakishangilia mabao yao dhidi ya Barcelona
Gorka Iraizoz comes out to deny Luis Suarez as the former Liverpool man tries to round the home keeper and bring his side level
Suarez akijitahidi kuipiugania Barcelona, lakini wapi walilala 4-0
Mikel Balenziaga ushers the ball away from Messi as the home defence looked to minimise the impact of Barcelona's best player
Messi hakufurukuta kabisa
SIKU chache baada ya kufanikiwa kushinda UEFA Super Cup kwa mbinde kwa kushinda mabao 5-4 dhidi ya Sevilla, mabingwa wa Hispania, Barcelona imetoa ishara mbaya ya kwamba msimu huu huenda ikawa urojo baada ya usiku wa jana kupigwa 4-0.
Barca wamekumbana na kipigo hicho kwenye pambano la Super Cup la Hispania kuashiria kuanza kwa msimu mpya wa La Liga na klabu ya Athletico Bilbao waliokuwa uwanja wa nyumbani.
Mabao matatu ya Aritz Aduriz na jingine la Mikel San Jose kwenye Uwnaja wa wa San Mames Barria, yalitosha kuizima Barcelona licha ya kuwa na nyota wake kadhaa akiwamo Messi na Luis Suarez.
San Jose alianza kumtungua kipa Marc-Andre ter Stegen dakika ya 13 kabla ya Aduriz kufunga mabao mawili ya haraka haraka dakika za 53 na 62.
Aduriz akakamilisha hat-trick yake kwa bao la mkwaju wa penalti, baada ya beki Dani Alves kumchezea rafu. 

Bayern Munich yatoa onyo mapema Bundesliga

Benatia (left) races away to celebrate following his 27th opener at the Allianz Arena
Wachezaji wa Bayern Munich wakipongezana baada ya kufunga moja ya mabao yao jana katika Bundesliga
Bayern striker Robert Lewandowski jumps for joy after the Poland striker made it 2-0 after the break
Robert Lewandowski akishangilia bao alililoifungia Bavarian usiku wa jana
MTAISOMA namba! Hivyo ndivyo Bayern Munich ilivyojitambulisha baada ya usiku wa jana kuanza vema Ligi Kuu ya Ujerumani wao kama mabingwa watetezi kwa kuikandika Hamberger kwa mabao 5-0.
Bavarians hao walipata ushindi huo kwenye mechi ya ufunguzi wa ligi hiyo katika Uwanja was nyumabi wa Allianz Arena kwa mabao ya Robert Lewandowski, Mehdi Benatia, Thomas Muller aliyefunga mawili na Douglas Costa.

Edin Dzeko atua AS Roma toka Etihad

www.bukobasports.com
MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Manchester City Edin Dzeko amejiunga na klabu ya ligi ya Seria A Roma kwa mkopo.
Roma imetoa kitita cha pauni milioni 2.9, na nyingine pauni 7.9 zikitarajiwa kulipwa iwapo uhamisho huo utabadilika na kuwa wa kudumu.
''Nimekuja hapa kushinda mataji'',alisema Dzeko.
''Ninaweza kuahidi kitu kimoja kwamba nitajitahidi vilivyo katika kilabu hii''.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 alijiunga na kilabu ya Etihad kutoka Wolfsburg mnamo mwaka 2011 kwa pauni milioni 27.
Alikuwa ameweka sahihi ya kandarasi ya miaka minne katika uwanja wa Etihad msimu uliopita.
Hatahivyo,meneja manuel Pelegrini hivi majuzi alikiri kwamba Dzeko alikuwa na uwezo mkubwa kuondoka katika Etihad kufutia usajili wa Raheem Sterling kutoka Liverpool kwa kitita cha pauni milioni 49.

Mtaipendaje Simba? Baada ya Agban kusaini sasa zamu ya Mzenji

Simba Day
Simba wakishangilia ushidni wa mechi yao na SC Villa ya Uganda siku ya Tamasha la Simba Day
KLABU ya Simba kwa hakika imepania msimu huu, kwani baada ya kumlambisha mkataba wa miaka miwili kiungo wake wa Kizimbabwe, Justice Majabvi, iliona haitoshi, ikamsainisha tena kipa Muivory Coast, Vincent Agban. Sasa kama  ulidhani walishamaliza kazi, umekosea kwa sasa klabu hiyo imemuita jijini kipa wa JKU-Zanzibar, Mohammed Abdulrahman ili kumalizana naye.
Kipa huyu ndiye waliyewahi kumtangaza mapema kwamba imemnasa kisha ikabainika kuwa bado ana mkataba mrefu na klabu yake kama ilivyokuwa pia kwa straika wa Vital'O, Laudit Mavugo.
Baada ya kutafakari kwa kina na hasa kutokana na kipa Ivo Mapunda kuwadengulia tangu wampe Sh. Milioni 10 za kusaini mkataba mpya, Simba ilipiga hesabu kumleta kipa Mbrazili, Ricardo Andrade, lakini ikamshtukia ana umri mkubwa mno, hivyo wakaachana naye.
Ndipo wakaamua kurudi kwa Abdulrahaman ambaye leo hii atatua jijini Dar es Salaam kumalizana na viongozi wa Simba tayari kuidakia timu hiyo katika michuano ya Ligi Kuu msimu wa 2015-2016.
Viongozi wa Simba wamekuwa wasiri katika suala la kipa huyo, lakini MICHARAZO inafahamu kuwa Abdulrahaman jana alikuwa Bububu na leo Jumamosi atapata boti kuitikia wito wa viongozi wa Simba ambao wiki sasa wamekuwa wakifanya mazungumzo naye na klabu yake ya JKU itakayoshiriki Kombe la Shirikisho Afrika mwakani,
Simba tayari imeshamshainisha kipa Agban aliyewahi kufanya majaribio timu ya vijana ya Chelsea na kuonekana kijeba na mwezi mmoja uliopita alikuwa akijifua na Azam kusaka nafasi ya kusajiliwa kabla ya kocha Stewart Hall kumpotezea kwa kuamini kazi nzuri ya Aisha Manula na Mwadini Ali.