STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 30, 2013

Simon Mberwa kuzihukumu Yanga, Coastal Union

Wachezaji wa Yanga wataendelea kushangilia ushindi kama hivbi kesho kwa Coastal Union?

Na Boniface Wambura
MWAMUZI Simon Mberwa ndiye atakayezichezesha timu za Yanga na Coastal Union katika pambano lao namba 172 la Ligi Kuu Tanzania Bara inayoingia raundi ya 25 kesho kwa michezo mitano tofauti katika miji ya Dar es Salaam, Turiani, Morogoro na Mlandizi.

Licha ya kuwa tayari Yanga imetawazwa kuwa mabingwa wa VPL msimu huu (2012/2013), mechi dhidi ya Coastal Union itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni moja kati ya zitakazovuta macho na masikio ya washabiki wa mpira wa miguu nchini.

Mechi hiyo namba 172 itachezeshwa na mwamuzi Simon Mberwa kutoka Pwani akisaidiwa na Said Mnonga na Charles Chambea wote wa Mtwara wakati mwamuzi wa mezani atakiwa Hashim Abdallah wa Dar es Salaam. Kamishna wa mechi hiyo ni David Lugenge kutoka Iringa.

Viingilio katik mechi hiyo itakayoanza saa 10.15 jioni ni sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, sh. 8,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 kwa VIP C na B wakati VIP A itakuwa sh. 20,000. Tiketi zitauzwa uwanjani siku ya mchezo.

Mtibwa Sugar itakuwa mwenyeji wa African Lyon katika mechi namba 170 itakayochezeshwa na mwamuzi Dominic Nyamisana wa Dodoma kwenye Uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro. Nayo Kagera Sugar iliyo katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi hiyo itakuwa mgeni wa Polisi Morogoro kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Uwanja wa Azam Complex ulioko Chamazi, Dar es Salaam na wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 7,000 uko tayari kwa mechi kati ya JKT Ruvu na Tanzania Prisons. Nayo Ruvu Shooting itakuwa nyumbani kwenye uwanja wake Mabatini ulioko Mlandizi, Pwani kuikabili Oljoro JKT kutoka Arusha.

Mtanzania apewe ITC ya kucheza Msumbiji


Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetoa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa mchezaji Yusuf Kunasa kucheza nchini Msumbiji.

Shirikisho la Mpira wa Miguu cha Msumbiji (FMF) lilituma maombi TFF kumuombea hati hiyo Kunasa anayekwenda kujiunga na timu ya Estrela Vermelha da Beira inayocheza Ligi Kuu nchini humo.

Kunasa ambaye msimu huu hakuwa na timu (free agent) amejiunga na timu hiyo akiwa mchezaji wa ridhaa (amateur). Zaidi ya wachezaji kumi kutoka Tanzania hivi sasa wanacheza katika klabu mbalimbali nchini Msumbiji.

Simba na Polisi Moro wavuna Mil 18 tu!


 
Na Boniface Wambura
PAMBANO namba 163 la Ligi Kuu ya Vodacom lililochezwa juzi (Aprili 28 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa Simba kuibuka ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Polisi Morogoro limeingiza sh. 18,014,000.

Watazamaji 3,145 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo ambayo viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 3,564,252.45 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 2,747,898.31.

Kiingilio cha sh. 5,000 ndicho kilichovutia watazamaji wengi ambapo waliokata tiketi hizo walikuwa 2,841 na kuingiza sh. 14,205,000 wakati idadi ndogo ya washabiki ilikuwa ya kiingilio cha sh. 20,000 kilichovutia washabiki 36 na kuingiza sh. 720,000.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 1,812,331.75, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 1,087,399.05, Kamati ya Ligi sh. 1,087,399.05, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 543,699.53 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 422,877.41.

Coastal Unioni kutibua sherehe za ubingwa Jangwani kesho?




Coastal Union
KIVUMBI cha Ligi Kuu Tanzania Bara kinatarajiwa kuendelea tena kesho kwa michezo sita, likiwamo la Mabingwa wapya wa ligi hiyol, Yanga dhidi ya wagosi wa Kaya, Coastal Union walioapa kuwatibulia wana Jangwani sherehe zao za ubingwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Yanga ilitawazwa kuwa mabingwa Ijumaa iliyopita baada ya wapinzani wao wa karibu Azam kulazimishwa sare ya bao 1-1 na wagosi hao wa kaya waliokuwa kwenye uwanja wao wa Mkwakwani-Tanga.
Uongozi wa Yanga na benchi la ufundi la timu hiyo, liemsisitiza kuwa kunyakua kwao ubingwa hakuwafanyi walegeze makali yao ambapo tangu kuanza kwa duru la pili hawajapoteza mechi yoyote.
Hata hivyo kocha wa Coastal, Hemed Morocco amenukuliwa juzi akisema kuwa wamekuja Dar kwa ajili ya kutibua furaha ya ubingwa ya Yanga na kwamba mabingwa hao wasitarajie mteremko kwani lengo lao kuona wakimaliza ligi wakiwa kwenye Tatu au Nne Bora.
Wakati Yanga na Coastal zikitambiana hivyo kabla ya kuvaana kesho Dar, michezo mingine itakayochezwa kesho ni pamoja na lile la Mtibwa Sugar dhidi ya 'vibonde' Agfrican Lyon ambayo imeshashuka daraja, japo bado hawajatangazwa rasmi na TFF kama desturi.
Timu hizo zitaumana kwenye uwanja wa Manungu Complex, Turiani, ambapo Mtibwa itakuwa ikisaka pointi za kuwafukuzia ndugu zao, Kagera Sugar waliopo nafasi ya tatu katika msimamo.
Kagera wenyewe watakuwa ugenini mjini Morogoro kuvaana na Polisi Moro ambayo kama ilivyo kwa Lyona na Toto ni kama zimeshajikatia tiketi ya kurudi Ligi Daraja la Kwanza ilikoicheza msimu uliopita kabla ya kupanda Ligi Kuu msimu huu.
Polisi na Lyon zote zina pointi 19 kila moja na hata zikishinda mechi zao za mwisho zitafikisha pointi 25 ambazo zimerukwa na asilimia kubwa ya timu zinazoshiriki ligi hiyo itakayofikia tamati yake Mei 18.
Pambano jingine la kesho litazikutanisha timu za maafande za Ruvu Shooting itakayokuwa nyumbani kuwakabili wageni wao JKT Oljoro kwenye uwanja wa Mabatini-Mlandizi Pwani.
Tayari Afisa Habari wa Ruvu, Masau Bwire alemchimba mkwara kwamba vijana wao wapo tayari kutoa dozi kwa Oljoro kabla ya kuwakabilia Simba Jumapili kwenye uwanja wa Taifa, baada ya mechi yao ya awali kusogezwa mbele kitatanishi dakika za lala salama kabla ya kuanza kwake.
Bwire alisema lengo lao ni kuhakikisha mechi zao nne zilizosalia wanazishinda zote na kuwa fanya wamalize msimu wakiwa na pointi 42 zinazoweza kuwaweka katyika nafasi ya Tatu Bora au Nne msimu huu.
Mchezo wa mwisho kwa kesho utachezwa kwenye uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam kwa maafande wa JKT Ruvu watakapowakaribisha askari wenzao wa Magereza, Prisons-Mbeya ambazo hazina cha kupoteza kwenye msimamo wa ligi hiyo kutokana na kwamba zote hazina nafasi ya ubingwa wala kushuka daraja.
Msimamo wa Ligi hiyo kwa sasa ni kama ifuatayvyo:


                             P      W     D     L     F      A     D     Pts
Young Africans      24    17     5     2     44     13    31    56
Azam                    24    14     6     4     42     20    22    48    
Kagera Sugar        23    11     7     5     26     18     8     40     
Simba                   23    10     9     4     34     22    12     39
Mtibwa Sugar       24     9      9     6     27     24     3      36   
Coastal Union       24     8    10     6     24     21     3      34    
Ruvu Shooting      23     8     6      9     21     22     -1     30     
JKT Oljoro FC    24     7     7     10    22     28     -6     28     
Tanzania Prisons   24     6     8     10    14     21     -7     26    
Ruvu Stars           24      7     5     12    20     37     -17   26
JKT Mgambo       23     7     4     12    15     23     -8     25
Toto Africans       25      4     10   11    22     33     -11    22
African Lyon        24      5     4     15     16    36     -20     19
Polisi Morogoro   24      3    10    11     12    23     -11     19    
             

Mourinho na vijana wake kuvuna nini leo Ulaya?

http://www.footballtarget.com/wp-content/uploads/2012/11/real-madrid-vs-borussia-dortmund-match-preview-champions-league.jpg
KOCHA Jose Mourinho na vijana wake wa Real Madrid leo wana kibarua kizito cha kuudhibitishia dunia kwamba soka lina maajabu yake watakapowakaribisha Borussia Dortmund nyumbani kwao, Santiago Bernabeu katika nusu fainali ya marudiano wakiwa na deni la kipigo cha mabao 4-1 walichopewa ugenini.
Mourinho na vijana wake walichezea kichapo cha mabao 4-1 ugenini nchini Ujerumani katika pambano la kwanza la Nusu Fainali ya michuano hiyo na hivyo leo watalazimika kulipa kisasi ili  kutinga fainali na kusaka taji la 10 na la kwanza tangu mwaka 2002.

Madrid watahitajika kushinda mabao 3-0 ili kutinga fainali za Ulaya baada ya misimu kadhaa ya ukame wa taji hilo tangu ilipotwa mara ya mwisho mwaka 2002.
Hata hivyo huenda isiwe kazi rahisi kwa vijana wa Santiago Bernabeu kutokana na ukweli wapinzani wao wapo vyema msimu huu licha ya kutemeshwa taji la ubingwa wa Bundesliga na Bayern Munich.
Dortmund wanasaka heshima baada ya kutwaa taji hilo mara ya mwisho mwaka 1997, hivyo huenda hawatakubali kuipoteza nafasi waliyopata safari hii kwa mabao manne ya Robert Lewandowski aliyefunga katika pambano la awali wiki iliyopita.
Wakati hatma ya Madrid na Dortmund ikitarajiwa kufahamika usiku wa leo, mabingwa wengine wa zamani wa Ulaya, Barcelona na Bayern Munich zenyewe zitakuwa na kibarua kingine kesho nchini Hispania.
Barcelona iliyocheze kichapo cha aibu wiki iliyopita ugenini kwa kulala kwa mabao 4-0 itakuwa nyumbani kujaribu kutupa karata yake kwa wageni wao ambao msimu huu wanatisha kisoka barani Ulaya.
Ikiwategemea nyota wake kama Xavi, Iniesta, Cesc Fabregas na Lionel Messi, Barca itakuwa na kazi pevu kulipiza kisasi na kutaka kupenya katika pambano hilo ili kucheza fainali Mei 25 itakayochezwa kwenye uwanja wa Wembley, Uingereza.
Je, ni Wahispania au Wajerumani watakaoenda London kwenye fainali hizo? Tusubiri tuone maana soka lina maajabu yake.

Bi Hindu ashirikishwa Fungate la Kifo



MTUNZI wa riwaya na simulizi za kusisimua anayezidi kuja juu nchini, Ramadhan Yahya, ameamua kugeukia fani ya filamu akifyatua kazi iitwayo 'Fungate la Kifo', iliyowashirikisha wasanii mbalimbali akiwemo nyota wa Kaole Sanaa, Chuma Suleiman 'Bi Hindu'.
Akizungumza na MICHARAZO jana, Yahya aliyewahi kutamba na vitabu kama 'Uchawi Uliosumbua Maisha Yangu, 'Bibi Yangu Mchawi', na 'Katikati ya penzi' alisema filamu hiyo mpya imekamilika na inafanyiwa mipango ya kuanza kuisambaza.
Yahya alisema hiyo ni filamu yake ya pili baada ya ile ya 'Uchawi Uliotesa Maisha Yangu' iliyotokana na kitabu chake cha awali na imewashirikisha wasanii mchanganyiko wazoefu na chipukizi.
Aliwataja baadhi ya wasanii hao ni Chuma Suleiman maarufu kama 'Bi Hindu', Maua Mbwana na wasanii wengine wanaoibukiwa kwenye fani hiyo.
"Baada ya filamu yangu ya kwanza kufanya vyema kwa sasa natarajia kuja na filamu ya 'Fungate la Kifo' ambayo imeshirikisha wasanii mchanganyiko," alisema Yahya.
Aliongeza kuwa, tofauti na filamu ya awali 'Fungate la Kifo' ataisambaza mwenyewe kwa kile alichodai filamu ya awali hakuambulia cha maana cha kujivunia.
"Nitaisambaza mwenyewe, maana watu tunaowaamini wanatuumiza mno, tunatumia gharama kubwa kuzalisha filamu, lakini malipo tunayoambulia ni mkia wa mbuzi, tunawanufaisha wao, najaribu mwenyewe nione inakuwaje," alisema.
Aidha mtunzi huyo wa hadhithi na mchora katuni, alisema kwa sasa anafanya mipango ya kusaka mfadhili wa kusimamia kazi zake ili fedha zitakazopatikana katika sanaa yake aziwekeze kwa kuanzisha asasi ya kuwasaidia yatima, wajane na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu.

MAZOEZI YA MISS KIBAHA 2013 YAZIDI KUPAMBA MOTO

Mkufunzi wa Warembo wa Miss Kibaha Rehema Uzuwiya akizungumza na warembo hawo wakati wa mazoezi yao yanayo endelea katika ukumbi wa Vijana Kinondoni

Warembo wa miss kibaha wakiwa katika pozi wakati wa mazoezi yao

Warembo watakao wania taji la Miss Kibaha wakiwa katika pozi wakati wa mazoezi yao yanayoendelea katika ukumbi wa vijana Kinondoni Dar es salaam

Saturday, April 27, 2013

HIVI NDIVYO GOLDEN BUSH WALIPOITOA NISHAI WAHENGA FC

Kikosi cha Golden Bush kilichoitambia Wahen ga Fc jana jijini Dar es Salaam

Kikosi cha Wahenga Fc kilichoendeleza uteja kwa Golden Bush jana
Mchezaji wa Wahenga akitafuta mbinu za kuwatoka wachezaji wa Golden Bush

Abuu Ntiro akiwahi pasi ya Athuman Machuppa huku Yusuf (9) wa Wahenga akiwanyemelea


HATARI! Lango la Wahenga Fc likiwa kwenye msukosuko

Ntiro akiwa akitafuta mbinu za kumnyanganya mpira Yusuf wa Wahenga madhara

Kama zamani Ntiro akitiririka pembeni kuelekea lango wa Wahenga, huku Kisiga akiwa tayari kumpa  msaada



Steven Marash na Wisdom Ndlovu wakiuza sura kabla ya kuanza kwa pambano la jana

Athuman Machuppa akiwania mpira na Wanchope wa Wahenga Fc

Machuppa (11) wa Golden Bush akiwania mpira wa Hamza (13) na Mcaremoon wa Wahenga katika pambano lao la jana

Wakati wa mapumziko mashabiki waq Wahenga wakifyeka nyasi ili kuwapa nafasi wachezaji wafanye vitu vyao na kuwarahishia Golden Bush kupata ushindi wa mabao 2-1

Wachezaji wa Golden Bush wakipasha kabla ya pambano hilo




Shaaban Kisiga akiwatoka wachezaji wa Wahenga

Macocha Tembele akiwafungisha tela Athuman Machupa na Godfrey Bonny, huku Kapeta akiwa tayari kumsaidia

HAPA HUPITI: Ni kama Ntiro (12) wa Golden Bush akimwambia Yusuf (9)  wa Wahenga



Kikosi cha Golden Bush Veterani kabla ya kuivaa Wahenga FC

HILI NDILO GARI LITAKAPIGANIWA NA MABONDIA CHEKA, MASHALI


Msemaji wa mbambano wa Thomasi Mashali na Fransic Cheka akiwa nyuma ya gari kuwaonesha wana habari gari hilo litagombaniwa kama zawadi na mabondia hawo

Yanga wanyakuta taji bila jasho, waapa hawabweteki

Wachezaji wa Yanga wakishangilia moja ya mabao yao katika ligi kuu msimu huu, ambapo jana kikosi chao kilitawazwa kuwa mabingwa bila kushuka dimbani baada ya Azam kung'ang'aniwa Mkwakwani.

NYOTA wa klabu ya Yanga jana wangeweza kuwa katika jumba la starehe wakinywa juice kupooza makoo, lakini wamerefusha rekodi ya kutwaa mara nyingi zaidi ubingwa wa Bara, baada ya sare ya 1-1 kati ya Coastal Union na Azam kwenye Uwanja wa Mkwakwani kuipa taji la 23 la ligi kuu bila jasho.
Kwa matokeo hayo, Azam iliyokuwa na matumaini ya mbali ya kuikatili Yanga katika kuwania ubingwa uliotemwa na Simba msimu huu, sasa itaweza kufikisha pointi 54 kama itashinda michezo yake mwili iliyobaki.
Idadi hiyo ni pointi mbili pungufu ya jumla ya alama za sasa za mabingwa wapya hao ambao pia wana michezo miwili kabla ya kumaliza msimu.
Kocha wa Azam ambayo mwishoni mwa wiki itakuwa Morocco kujaribu kuingia hatua ya 16 bora ya Kombe la Shirikisho la klabu za Afrika dhidi ya RAF, Stewart Hall alilaumu ubovu wa uwanja wa Mkwakwani kuwa ndiyo sababu ya kushindwa kuweka hai ndoto ya timu yake Bara.
Mwalimu wa Coastal ambayo sasa imefikisha pointi 34 na kujiimarisha katika nafasi za katikati ya msimamo wa ligi kuu, Hemed Morocco alimlaumu muamuzi Andrew Shamba kwa kuwapendelea wageni, kwa upande wake.
Agrey Moris aliipatia Azam bao la kuongoza kwa penalti katika dakika ya 59, baada ya muamuzi kuamuri adhabu hiyo kufuatia Gaudance Mwaikimba kuangushwa ndani ya eneo la hatari na Yusuf Chuma.
Ilimchukua Dany Lihanga wa Coastal Union dakika moja tu tangu kuingia kutoka benchini kusawazisha bao hilo katika robo ya mwisho ya mchezo, baada ya kumalizia wavuni pasi ya Ibrahim Twaha.
Lihanga aliingia kuchukua nafasi ya Selemani Kassim katika dakika ya 71.
Mbali na mwaka huu, tangu ligi kuu ya Bara (zamani ligi daraja la kwanza) ianze mwaka 1965 Yanga imetwaa ubingwa katika miaka ya 1968-1972, 1974, 1981, 1983, 1985, 1987, 1989, 1991-1993, 1996-1998, 2002, 2005, 2008-2009 na 2011 kwa tofauti ya magoli.

Makamu Mwenyekiti wa timu hiyo ya Yanga, Clement Sanga alisema pamoja na kufurahai kupata ubingwa mapema wakiwa na mechi mbili mkononi, hawatabweteka na badala yake watahakikisha wanashinda mechi hizo ili kuunogesha ubingwa wao.
Sanga alinukuliwa na kituo kimoja akisema furaha yao na sherehe zao za ubingwa zitanoga kama watawafunga Simba na hasa kurejesha kipigo cha aibu walichopewa msimu uliopita wa kunyukwa mabao 5-0.
Hata hivyo Kaimu Makamu Mwenyekiti wa Simba, Joseph Itang'are  'Mzee Kinesi' amepuuza ndoto hizo za Yanga na kudai wasitarajie kitu kama hicho kwani Msimbazi wanataka kuivuruga furaha ya wanajangwani.
"Tunataka kuivuruga furaha ya mtani kwa kuwanyuka Mei 18 ili asherehekee kimya kimya ndani wakiwa na maumivu, tunajua hatuna ubingwa lakini tunataka kulinda heshima yetu," alisema Kinesi.

Ruvu Shooting walalamikia gharama, lakini yaionya Simba

Kikosi cha Ruvu Shooting Stars
UONGOZI wa Ruvu Shooting umesikitishwa na gharama ulizobebeshwa na serikali na shirikisho la soka, TFF, kufuatia kuahirishwa kwa pambano la ligi kuu ya Bara dhidi ya Simba juzi.
Lakini uongozi huo umesisitiza kuwa kipigo kwa 'mnyama' kipo palepale timu hizo zitakapokutana katika tarehe mpya - Mei 5.
TFF ilitangaza kuahirisha pambano hilo lililokuwa lichezwe kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam saa chache kabla ya kufanyika kwake na kupanga lifanyike Mei 5.
Msemaji wa Ruvu Shooting, Masau Bwire aliimbia MICHARAZO jana kuwa wamekerwa na kusikitishwa na kitendo hicho kilichowatia hasara kubwa ya kuweka kambi, kufanya maandalizi na kusafiri kutoka Mlandizi mpaka Dar Es Salaam na kukaa siku kadhaa kisha kuahirishwa mechi.
Bwire alisema licha ya TFF kuwaomba radhi na kujitetea kuwa haihusiki na kuzuiwa kutumiwa kwa Uwanja wa Taifa kutokana na kupisha maandalizi ya sherehe za Muungano, lakini inastahili lawama kwa kitendo hicho kwani walipaswa kulifahamu hilo mapema na kuzipunguzia gharama timu husika.
"Tumeumizwa sana na kilichofanyika, tulifanya maandalizi yenye gharama kwa ajili ya mechi hiyo, hata hivyo hatuna mpango wa kudai fidia yoyote kwani TFF imeshajitetea kwetu na sasa tunafikiria mechi yetu ya Mei Mosi dhidi ya JKT Oljoro," alisema.
Bwire alisema pamoja na kuiwaza mechi hiyo ya Oljoro, lakini Simba wasifikirie tayari wameshaepuka kipigo kutoka kwao, kwani hata Mei 5 wakikutana lazima wakutane nacho kwa maandalizi waliyofanya na kiu yao ya kumaliza kwenye 'Nne Bora'.
"Kipigo kwa Simba kipo pale pale wameahirishiwa tu, tunataka kuonyesha kuwa Ruvu ni timu nzuri na tunataka tumalize katika Tatu au Nne Bora msimu huu, kwani kwa mechi zilizosalia tuna uwezo wa kufikisha pointi 42," alitamba Bwire.
Timu hiyo ipo katika nafasi ya saba ikiwa na pointi 30 ikiwa na michezo minne kabla ya kumaliza msimu wa 2012-2013.

Simba yatishiwa Polisi, Machaku aapa Mnyama lazima akae


Kikosi cha Simba
Machaku Salum 'Balotelli' wa Polisi Moro
LICHA ya kuhitaji miujiza ili kubaki kwenye ligi kuu ya Bara msimu ujao, wachezaji wa Polisi Morogoro wana imani ya kujikwamua na janga hilo kwa kuanzia na kuifunga Simba katika mchezo baina ya timu hizo kwenye Uwanja wa Taifa kesho.
Polisi Morogoro ni ya pili toka mkiani katika ligi ambayo zitashuka timu tatu za mwisho, ikiwa na pointi 19.
Ili kubaki kwenye daraja hilo la juu zaidi Polisii nahitaji kushinda mechi zake tatu zilizobaki ili kufikisha pointi 25 na kupunguza tofauti ya magoli ya -10 iliyonayo.
Bahati mbaya kwa Polisi, hata hivyo, jumla hiyo imeshafikiwa na ama kupitwa na timu zote zilizo katika eneo la salama la kubaki kwenye ligi kuu na zikiwa si tu na michezo iliyobaki bali pia uwiano bora wa magoli.
African Lyon na Toto Africa nazo zina uwezo wa kufikisha pointi 25 lakini kwa kubakiwa na michezo miwili na mmoja, kwa mpangilio huo, zipo katika mazingira magumu zaidi ya Polisi Morogoro.
Mmoja wa wachezaji wa Polisi Salum Machaku alisema licha ya timu yao kuwa katika eneo la hatari, lakini hawajakata tamaa.
Amedai wachezaji wote wamejipanga kufanya kweli katika mechi zilizosalia dhidi ya Simba, Kagera Sugar na Coastal Union.
"Hatujakata tamaa na wala hatuamini kama Polisi itarudi daraja la kwanza," alisema na kueleza zaidi, "tumejipanga kupigana kiume katika mechi zilizosalia ili kubaki na Simba wakae chonjo kwani tutakufa nao Uwanja wa Taifa."
Mshambuliaji huyo aliyewahi kuichezea Simba na timu za Pan Africans, Azam na Mtibwa Sugar, alisema hakuna mchezaji wala mwana Polisi Moro anayetaka kusikia habari za kushuka daraja japo wamechelewa mno kuzinduka.
Machaku alisema ugeni wao katika ligi wakati wa duru la kwanza lililosababisha wapoteze mechi na pointi nyingi ndiyo iliyowagharimu kabla ya kuzinduka katika duru la pili wakiwa wamechelewa.

Machupa, Kisiga waibeba Golden Bush wakiipa kichapo Wahenga Fc

Shaaban Kisiga (Katikati) akiwatoka wachezaji wa Wahenga Fc

Nyota wa Wahenga Fc, Macocha Tembele akiwatok wachezaji wa Golden Bush

Yusuf (9) wa Wahenga, akitafuta mbinu za kumtoka Abuu Ntiro huku wachezaji wenzake wakiwa tayari kumpa msaada katika pambano lao lililochezwa jana na Wahenga kunyukwa mabao 2-1

Abuu Ntiro akimtoka Yusuf

Heka heka katika lango la Wahenga Fc

NYOTA wa zamani wa Simba na taifa Stars, Athuman Idd Machuppa na Shaaban Kisiga 'Marlon' jana waliisaidia Golden Bush Veterani kupata ushindi muhimu  wa mabao 2-1 dhidi ya wapinzani wao wa jadi Wahenga Fc katika pambano maalum la kusherehekea  Miaka 49 ya Muungano.
Timu hizo zilipambana katika mchezo mkali na uliosisimua uliochezwa kwenye uwanja wa TP Afrika, Sinza Darajani, ambapo Machuppa, Kisiga wakisaidiwa na nyota wa zamani wa Simba na Yanga walifunga mabao hayo katika muda wa dakika tano tu mara baada ya kurejea toka mapumziko timu zikiwa hazijafungana.
Machuppa ndiye aliyeanza kuifungia Golden Bush bao tamu katika dakika ya 68 akimalizia kazi nzuri ya Herry Morris kabla ya Kisiga kuongeza jingine dakika tano baadaye na kuzima matumaini na Wahenga Fc waliokuwa uwanja wa nyumbani kulipa kisasi ilichokutana nacho mwezi uliopita kwenye uwanja wa Kinesi.
Katika pambano hilo la Kinesi, Wahenga walinyukwa pia mabao 2-1 huku mvua ikiwanyeshea timu zote mbele ya aliyekuwa mgeni rasmi, Kamanda wa Polisi, Thobias Andengenye.
Golden Bush na kikosi kilichosheheni nyota waliowahi na wanaendelea kutamba nchini kama kipa Aman Simba, Abuu Ntiro, Godfrey Bonny 'Ndanje', Wisdom Ndlovu, Herry Morris, Said Sued, Salum Sued, Kisiga, Machuppa na wengine waliifanya Wahenga ishindwe kufuruka licha ya mara kadhaa kubisha hodi langoni mwa mwao.
Dakika chache kabla ya pambano hilo kumalizika huku kiza kikiwa kimeshaanza kutamba uwanjani, Wahenga walipata bao la kufutia machozi lililofungwa kwa mkwaju wa penati na nyota wa kikosi hicho, Macocha Tembele aliyekuwa akihaha uwanja mzima kuibeba timu yake.
Licha ya Wahenga kuendelea kushambulia lango la Golden Bush, mpaka kipyenga cha mwamuzi, Pondamali kulia walijikuta wakiendelea kuwa 'wateja' wa Wakali wa soka Dar es Salaam kwa kukubali kipigo kingine cha mabao 2-1.

Warembo 16 watemwa Miss Tabata



Warembo wa watakaoshiriki shindano la Miss Tabata 2013 wakiwa katika pozi tofauti kambi yao ya mazoezi Da West Park
 
JUMLA ya warembo 16 wametemwa katika kinyang’anyiro cha kumtafuta Redds Miss Tabata ambao utafanyika Mei 31 Dar West Park.
Mratibu wa shindano hilo, Godfrey Kalinga, alisema jana kuwa warembo hao wametemwa kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo utoro, kukosa sifa za kushiriki na utovu wa nidhamu.
Kalinga aliwataja warembo waliyotemwa kuwa ni Sophia Claud (21), Lilian Mpakani (19), Lilian Msanchu (19), Rita Frank (20), Pasilida Mandali (21), Rachel Mussa (19), Jasmin Damian (18), Angelina Mkinga (19), Mercy Mwakasungu (20), Tunu Hamis (19), Ray Issa (22), Shamim Abass (22), Shan Abass (22), Amina Ally (18), Magdalena Bhoke (21)  na Zilpha Christopher (19)
Kalinga aliwataja warembo wanoendelea na mazoezi katika umbumbi wa Dar West Park, Tabata kila siku kuwa ni Hidaya David (22), Aneth Ndumbalo (19), Dorice Mollel (22), Eunice Nkoha (19), Kazunde Kitereja (19),  Angela Fradius (19), Domina Soka (21), Rehema Kihinja (20) and  Glory Jigge (18).
Wengine ni Rachel Mushi (20), Caroline Sadiki (20), Kabula Juma Kibogoti (20), Blath Chambia (23), Suzzane Daniel Gingo (18), Upendo Lema (22), Pasilida Mandari (21) na Martha Gewe (19).
Washindi watano kutoka Tabata watafuzu kushiriki Redds Miss Ilala baadaye mwaka huu.
Anayeshikilia taji la Miss Tabata ni Noela Michael ambaye pia ni Miss Ilala.
Redds Miss Tabata inaandaliwa na  Bob Entertainment na Keen Arts na chini ya Udhamini wa Redds, CXC Africa, Fredito Entertainment, Brake Points na Saluti5.
 

Cheka, Mashali patachimbika Mei Mosi


Reeling from the recent defeat in the hands of the German strongman Uensal Arik , TEAM Francis Cheka is back on the drawing board as it attempts to defuse negative impact of the loss in their forthcoming rumble against the man of the people and dreadlock Thomas MashaliThe duo is competing for the “IBF Continental Africa Super Middleweight Title” as optional defense for Cheka.
 
 
The tournament slated for 1st May, 2013 (May Day) has elicited a lot of excitements from thousands of boxing stakeholders in Tanzania and the whole of East African region. Thomas Mashali is the East & Central African Middleweight Champion and the biggest crowd puller in the region todate.

                                                                      Francis Cheka (right) and Uensal Arik (left)
 

Cheka’s recent defeat was kind of embarrassment as he took the fight as a warm up but alas, things turned bitter as the Germany strongman Uensal Arik sent him reeling to the floor before Thomas Mtua threw out the towel as SOS for the Tanzanian slugger! It was a defeat from “Manna”as this kind of taught Cheka a lesson or two about taking boxing serious as there is nothing as a small fight in boxing.


Adam Tanaka of Mumask Investment and Gebby Presure LTD, the man of the hour promoting this fight has been working over drive to have all the details finalized. Of the top priority is the arrival of the ring officials (all coming outside Tanzania) who have been summoned to preside over the rumble. This is so because Adam want to avoid complaints from either boxer should the decision goes against their expectations.

"The poster in Kiswahili language tells it all"

 
The man who has been charged with the responsibility to stand in as “the third man in the ring” is no other than the Zambian Army Officer, John Shipanuka who himself looks like a heavyweight boxer in refereeing uniform. Shipanuka’s body language and impatiality with boxers in the ring has illuminated his CV and make him one of the most sort-out ring officials in Sub Sahara Africa.

Arusha Mayor (left) and IBF/AFRICA' Onesmo Ngowi(right) crowing Cheka after his last defense 12/26/12

To assist him would be two Sedentary Generals of; Uganda Professional Boxing Commission (UPBC), master Simon Katogole and Daudi Chikwanje of Malawi Boxing Association (MBA). These two gentlemen would be in the company of one of the most experienced judges in East Africa Alhaj Ismail Sekisambu also from Uganda.


So, “the chickens have finally come home to roost" as any of the two has to face the consequences of his mistakes in the ring on that particular day.


So, as the clock ticks to the morning hours of May Day 2013, Dar Es Salaam landscape may turn into a “quicksand” for the two gladiators as fans from all walks of life jams the PTS Social Hall to witness yet another rumble of the year!
 
 
 Nothing has been left to chances as the World's premier professional boxing “top dog” the IBF has already given its blessing by sanctioning for the title!
 

Suarez akubali yaishe, aomba msamaha



LONDON, England
Mshmbuliaji wa Liverpool Luis Suarez ameomba msamaha baada ya kukubali adhabu ya kutocheza mechi 10 kwa kumng'ata Branislav Ivanovic wa Chelsea katika mechi ya ligi kuu ya soka ya Uingereza mwishoni mwa wiki iliyopita.
Muuruguay huyo alikuwa na muda mpaka mchana jana kupinga adhabu ya Chama cha Soka ya kuongeza mechi saba katika adhabu ya kawaida ya kukosa michezo mitatu kwa kosa la kufanya ukatili lakini akaamua kutobishia.
"Nataraji kuwa watu niliowaudhi Jumapili iliyopita watanisamehe na narudia tena kumuomba radhi binafsi Branislav," Suarez aliseka katika ukurasa wake wa Twitter.
"Ingawa ni wazi kwamba mechi 10 ni nyngi kuliko vifungo vilivyowahi kutolewa katika kosa kama hili huko nyuma ambapo wachezaji walijeruhiwa, nakubali kuwa kitendo changu kilikuwa hakikubaliki kwenye uwanja wa soka hivyo sitaki kuleta picha mbaya kwa watu kwa kukata rufaa."
Suarez, ambaye alimng'ata Ivanovic mkononi katika sare ya 2-2 kwenye uwanja wa Anfield wiki-endi iliyopita, hatoweza kuichezea Liverpool katika michuano ya ndani mpaka Septemba.
Liverpool, ambayo ilimpiga faini Suarez, ilisisitiza kusikitishwa kwake na uamuzi wa FA wa kumfungia Suarez kwa mechi 10.
"Adhabu dhidi ya Luis ilikuwa yake binafsi kuamua na ni lazima tuheshimu uamuzi wake wa kutokata rufaa kufungiwa mechi 10," mkurugenzi mtendaji Ian Ayre alisema.
Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers aikilaumu chama cha soka kwa ukali wa adhabu ya Suarez na palikuwa na kuungwa mkono na makocha wa timu pinzani jana.
"Katika kesi hii, ukubwa wa adhabu na kosa vinaonekana kupishana mno kulingnaisha na makosa ambayo wachezaji wengine wamewahi kuadhibiwa nayo," kocha wa Arsenal Arsene Wenger aliwaambia waandishi wa habari.
"Nadhani kilichommaliza kabisa Suarez ni historia yake, ambayo ina makosa mengi.
"Ndiyo sababu ameadhiwa vikali sana, ndiyo sababu pekee ambayo naweza kuiona."
Kocha wa Manchester City Roberto Mancini alisema katika mkutano wake wa Ijumaa na waandishi wa habari: "Mechi tano au sita zilitosha, huu ndiyo mtazamo wangu lakini sifanyi kazi FA."
Ni mara ya pili kwa Suarez, 26, kufungiwa kwa kumng'ata mchezaji wa timu pinzani baada ya kumng'ata Otman Bakkal wa PSV Eindhoven kwenye shingo wakati akiichezea Ajax 2010, na kufungiwa mechi saba.
Suarez alifungiwa pia mechi nane msimu uliopita baada ya FA kumuona ana kosa la kumbagua kwa rangi ya ngozi Patrice Evra wa Manchester United Oktoba 2011.
Reuters

Suarez

Thursday, April 25, 2013

Simba yatoa msimamo kuahirishwa ghafla kwa mechi yao na Ruvu Shooting



Na Ezekiel Kamwaga
UONGOZI wa Simba umekubaliana na hatua ya serikali kuzuia kuchezwa kwa mchezo uliopangwa kuchezwa leo wa Ligi Kuu ya Tanzania baina ya Wekundu wa Msimbazi na Ruvu Shooting Stars.
Hata hivyo, uongozi wa Simba haujafurahishwa na namna uzuiaji huo ulivyofanyika. Taarifa imetolewa leo kwenye siku ya mechi yenyewe wakati maandalizi yote yakiwa yamefanyika na hivyo kusababisha matatizo katika sehemu kubwa tatu.
Mosi, uongozi wa Simba umeingia gharama kubwa ya kuweka timu kambini na kujiandaa na mechi. Pili, benchi la ufundi na wachezaji walikuwa tayari wamejiandaa na mechi kimwili na kiakili na kuahirishwa huku kwa mechi kumesaidia tu kuvuruga programu. Tatu, wapenzi na washabiki wa Simba wamepata usumbufu wa kwenda uwanjani na kukuta hakuna mechi.
Uongozi wa Simba unapenda kutumia nafasi hii, katika namna ya kipekee kabisa, kuwaomba radhi wapenzi na wanachama wake ambao walifika Uwanja wa Taifa kutazama mechi ambayo haikuwapo.
Washabiki ndiyo wanaoifanya Simba na mchezo wa mpira wa miguu nchini uwe na umaarufu ulionao na bila wao ligi yetu inaweza kupoteza nguvu na ushindani ilionao.
Simba SC inapenda kuwe na utaratibu unaojulikana wa kuahirisha mechi wa walau saa 48 kabla ya siku ya mechi. Hii itasaidia pande zote zinazohusika. Kama mechi imeshindikana kwa sababu za nje ya uwezo wa kibinadamau (Force de Majeure) kama vile mafuriko, tetemeko la ardhi na vimbunga, mechi inaweza kuahirishwa ghafla lakini si kwa mechi ambayo uwepo wake ulifahamika miezi kadhaa nyuma.
Tunashauri pia kwamba siku za mechi ambapo Ligi Kuu inachezwa (match days), inatakiwa kuwa zinafahamika na isiwe kila siku mechi zinachezwa. Simba ilikuwa na mechi wikiendi iliyopita na Ruvu ilikuwa na mechi Mbeya zaidi ya wiki moja iliyopita na hivyo mechi hii ingeweza kuchezwa hata jana (Jumatano) ambayo ni siku ya kawaida kwa mechi kuchezwa badala ya leo Alhamisi.
Ni matumaini yetu kwamba kuahirishwa kwa mechi hii kutakuwa fundisho kubwa katika upangaji wa ratiba na uahirishaji wa mechi ambao una faida kwa pande zote husika.


Poppe arejea Simba
MWENYEKITI wa Simba, Mhe, Ismail Aden Rage, amemshukuru aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu, Zacharia Hans Poppe, kwa kukubali kurejea kushikilia nyadhifa zake zote.
Poppe alitangaza kujiuzulu nyadhifa zake za uongozi ndani ya Simba Machi 7 mwaka huu, kutokana na hali ya migogoro iliyokuwapo wakati huo.
Hata hivyo, Rage alikataa kujiuzulu huko kwa Poppe na akasema atamshawishi abadili maamuzi kwa manufaa ya Simba.
“Napenda kutumia nafasi hii kuwaarifu wana Simba popote walipo kwamba Poppe amerejea na yuko tayari kuitumikia Simba kama Mjumbe wa Kamati ya Utendaji na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba,” alisema Rage.
Kwa upande wake, Poppe alisema amerejea Simba kutokana na utulivu ulioanza kujitokeza klabuni na kwamba nia yake ni kuhakikisha klabu inafanya usajili mzuri na wa kiwango kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu.

GHANA KUWAKA MOTO KWA MASUMBWI


By Onesmo Ngowi
GHANA, one of the boxing powerhouses in African continent is edging towards three biggest IBF tournaments next week on May 3rd, 2013 at the Accra Sports Arena in Ghana
Princess Hellen Joseph

GoldeMike Boxing Promotion Syndicate is at it again and this time Ghanaian boxing stakeholders and the whole of West Africa region will enjoy a thrilling moment which they all have been carving for.

This is one of the major IBF tournaments in Sub Sahara Africa and nothing is being left to chance as the promoters “Henry Many-Spain and Michael Tetteh” painstakingly deal with all the final details for this epic duel!
Albert Mensah (right)
Drawing the line of this epic boxing tournament is none other than two of the Ghanaian’s most fiercest opponents in Jr. Middleweight, Albert Mensah when he confront his archenemy Ben Odemattey.
 
The duo is battling for the “IBF Continental Africa Jr. Middle Weight Crown”. Came sun, come rain one of them would be the King of the Jr, Middleweight in Africa.
 
Following this epic bout, will be the Princessfrom Nigerian boxing royal family, Princess Helen Joseph when she goes toe to toe with another Princess from Austro-Hungarian Boxing Empire, Princess Marianna Gulyas.

The two beautiful Princesses who would pass in a beauty-parget are battling for the “IBF vacant Intercontinental Featherweight Female Crown”.

"We are definately going to get the crown" said Koffi Dakku-Ricketts,the man who is behind Princess Helen's success as a trainer. Ricketts boast of many similar success stories and make him one of the best trainers Ghana has ever had in years!
 
This has been “a seek and hide game” for the past two years but, this time around, no ground can hide any of the two as the moment of truth is about to come.
 
The man of the moment is none other than the Ghanaian ups and comings boxing star and Olympiad boxer “Issa Samir” in a duel of his life when he host the handsome Georgian true-nan and flamboyant “Robison Omshashavili” for the vacant “IBF World Jr. Middleweight Crown” in a 12 rounds epic battle.
 
The bout christened“The Battle of the Gold Coast” would rekindle the memory when one of the Ghanaian boxing king, Professor Azumah Nelson when hosted Sidnei Dal Rovere in a similar battle at the Accra Sports Stadium in 1988.
 
The ground can be “quicksand” for the two as they crave to prove to the whole world that they are indeed “pound for pound” gladiators and future world champions on the rise!
 
This is; in a matter of fact “a thumb up” for Ghana as it makes African continent proud once again after shining out during the last “World Cup tournament” in South Africa.

Hii kali! Sherehe za Muungano zakwamisha pambano la Simba na Ruvu Shooting Taifa

 
Viongozi wakuu wa TFF, Leodger Tenga na Angetile Osiah
Na Boniface Wambura
PAMBANO la Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Ruvu Shooting na Simba iliyokuwa ichezwe leo (Aprili 25 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam limeahirishwa mpaka Mei 5 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.

Kisa cha kufanyika ghafla kwa mabadiliko ya pambano hilo imetokana na Serikali kuutumia uwanja kwa ajili ya maandalizi ya sherehe za Muungano ambazo kitaifa zitafanyika kesho (Aprili 26 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawaomba radhi washabiki kwa usumbufu uliojitokeza kutokana na mabadiliko hayo na ghafla. Ratiba ya mechi nyingine za VPL zinabaki kama zilivyo.

Kitendo hicho cha mechi hiyo kuahirishwa ghafla kinauonyesha umuhimu wa klabu na hata FA kumiliki uwanja wake ili kuondokana na matatizo kama hayo yanayolitia doa soka la Tanzania.

Hata hivyo pamoja na pambano hilo kupigwa 'dochi' hadi Mei 5, TFF imesisitiza kuwa ratiba nyingine za ligi hiyo inayopelekea ukingoni itaendelea kama ilivyo, ambapo kesho (Aprili 26 mwaka huu) Coastal Union na Azam itakayochezwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Jumapili 'Mnyama' Simba itaikaribisha Polisi Moro kwenye pambano litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa siku ya Jumapili (Aprili 28 mwaka huu).