STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 20, 2015

Michael Olunga aipeleka Gor Mahia robo fainali Kagame Cup

http://www.standardmedia.co.ke/images/saturday/stdrclwhqpq.jpg
Michael Olunga
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgKxRDIwrjKq6PNP8GUEXC5s6MqT9DpyWecXpY324qzrHOoXoIVRN1JTFo2JKNATy2Jsgaq2axLJ8TZAjWy9G7sdYv_QZSQK4XJBmlJA8gqO93Qfu2HMbmhFDE2Tvc2HSUBSkRfgJDIcrg/s1600/IMG_3285.JPG
Olunga (kulia) alipoikimbiza Yanga katika mechi yao ya kwanza ya Kombe la Kagame ambapo alifunga moja kuisaidia Gor Mahia kushinda 2-1
MSHAMBULIAJI nyota wa Gor Mahia, Michael Olunga ameendelea kuonyesha dhamira yake ya kunyakua kiatu cha dhahabu katika michuano ya Kombe la Kagame baada ya jioni hii kutupia mabao mawili kambani wakati timu yake ikiizamisha KMKM kwa mabao 3-1.
Olunga alifunga mabao hayo katika kipindi cha pili na kuiwezesha Gor Mahia kuwa timu ya kwanza kukata tiketi ya kucheza robo fainali ikitokea Kundi A kwa kukusanya pointi sita na mabao matano baada ya mechi yao ya awali kuitoa nishai Yanga kwa mabao 2-1.
Katika mechi huo wa kwanaa Olunga anayewindwa na Simba, ingawa ni ngumu kumpata kwani ana mkataba wa miaka miwili, alifunga bao moja.
Kwa kufunga mabao hayo mawili jana, imemfanya kuongoza orodha ya wafungaji wa michuano hiyo akiwa na magoli matatu akimzidi kete Sallah Bilal wa Al Khartoum ambaye alikuwa akiongoza kwa mabao mawili baada ya mchana wa leo kuingoza timu yake kuilaza Telecom kwa mabao 5-0.
Mara baada ya mechi yake ya Yanga, Olunga alinukuliwa akisema kuwa amekuja Tanzania akiwa na nia moja ya kuwa Mfungaji Bora wa michuano hiyo, kitu kinachoonyesha ni kweli baada ya kufanikiwa kufunga mabao hayo mawili.
Kabla ya Olonga kufunga mabao hayo, Meddie Kagere mkali mwingine wa Gor Mahia aliifungia timu hiyo bao la mapema akimalizia pande la Olunga kabla ya KMKM kusawazisha na kwenda mapumziki timu zikiwa sare ya 1-1 mpaka kwenye dakika ya 65 Olunga alipoanza kufanya yake na kuwazamisha Wazanzibar.

FIFA yatangaza tarehe ya uchaguzi wake mpya

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/04/Sepp-Blatter.jpg
Rais wa Fifa, Sep Blatter aliyetangaza kujiuzulu mrithi wake atapatika February
SHIRIKISHO  la Soka Duniani, FIFA limetangaza kwamba uchaguzi mkuu wa Rais utafanyika Februari 26 mwakani.
Maamuzi haya yamefanyika leo katika kikao cha kamati ya utendaji ya Shirikisho hilo kilichofanyika mjini Zurich, Uswisi.
Sepp Blatter aliyejiuzulu siku nne baada ya kuchaguliwa amethibitisha kuwa ataendelea kukaa madarakani mpaka uchaguzi mkuu utapofanyika kupata mrithi wake.
Wakati huo, kundi la watu wanaoshinikiza  kufanyika kwa mageuzi wamekutana leo mjini humo wakimuomba katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan kuongoza mapinduzi hayo.
Kundi hilo limesema Annan ni mtu makini ambaye anapaswa kuongoza tume ya mageuzi wakati  huu Dunia ikielekea kupata mrithi wa Sepp Blatter aliyejiuzulu Urais kutokana na kashfa nzito ya rushwa iliyokumba FIFA.
Shirika la Ujasusi la Marekani, FBI liliwatia mbaroni Maafisa saba wa ngazi za juu wa FIFA kwa tuhuma za rushwa.

Stewart afungka mbinu walizoizamisha KCCA

Stewart Hall akiteta na Migi
KOCHA Stewart Hall ni mjanja sana, baada ya kufichua siri ya kuwaanzisha viungo wengi na kucheza soka la kujihami na kushambulia kwa kutumia mipira mirefu. Akizungumzia mbinu zake, Hall alisema alilazimika kutumia mbinu hiyo kwa sababu wachezaji wake wengi bado hawapo fiti. “Tupo katika kipindi cha maandalizi ya mwanzo wa msimu, wachezaji wangu Kipre Tchetche, Didier Kavumbagu na Ramadhani Singano bado hawajawa fiti kwa asilimia mia, lakini naamini tutafika fainali.” alisema Hall Hall aliongeza kuwa timu inayomtisha zaidi ni Gor Mahia kwa sababu wamekuja wakati ligi ya Kenya inaendelea hivyo wachezaji wao wapo fiti.

UTAMU WA KOMBE LA KAGAME WAZIDI KUNOGA DAR

https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AKh2imIAABZpVaY5ZwsQCBMD2%2BU&midoffset=2_0_0_1_4350124&partid=2&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000http://rushyashya.net/IMG/jpg/apr_fc_team_-_rwanda_-_kigalitoday-2-2.jpg
APR Rwanda
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/07/Yanga-leo-14.jpg
Yanga na Gor Mahia
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgU-pwUoReK1Inoqwa-tv9F7B4FsQQHzQW9GaG7wzubvb9SCAbF6zgGuLW0T-HTTo2ede7ls9zqJuGTrYNNSoghMV8GO4-5kfnAbuNX1yjWmHghK_qRzBu2MQ1YkUVYSo-N7z6p23PgLzs/s640/426464_358635040821389_1508036080_n.jpg
Al Shend
http://kabumbu.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/kikosi-azam-fc.jpg
Azam ya Tanznaia Bara
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiYr-ePKerYIvN49hCZ9IJI-ICEdPieA86ey85RJHvQ131iGA6GEbCXWWbDogjLkjX3y6u7CQrhi07Wnmkj3cDy2Drr-O8hj23no_e0NxN6qDxt_0KSgzSb0084QpabXSEI7dIMJoRXD4bc/s1600/1385637_526389100785782_1638137288_n.jpg
Telecom ya Djibout
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg3v7qvqTyHyaPiHb4iJPQ2UjF7MIw0nVpNbqWGraZLfn3zrJ6t9J4bGJ0Ok268cn_goKj9RqzWVvhzIbNvWOTsBfGmrrJGfaTXfZfAcFez2kVA97hfblC6PDlqUiHoUIKjm5SeoML2U9q_/s1600/IMG_9898.JPG
KMKM ya Zanzibar
http://entebbenews.com/wp-content/uploads/2014/09/KCCA-Mulindwa-9.jpg
KCCA ya Uganda
Kikosi cha Yanga

Kikosi cha Gor-Mahia

Mchezaji wa Yanga, Amis Tambwe akiwa chini huku wachezaji Collins Okoth (kulia) na Harun Shakava (kushoto) wa Gor Mahia ya Kenya wakiwania mpira wakati wa mchezo wa ufunguzi wa mashindano ya Kombe la Kagame uliochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo. Yanga imefungwa mabao 2-1.
Mashabiki wa Yanga

MICHUANO ya Kombe la Kagame imezidi kushika kasi ikiwa inaingia siku yake ya tatu leo tangu yalipofunguliwa rasmi siku ya Jumamosi, huku Al Khartoum ya Sudan ikitoa onyo kwa kuopata ushindi wa kishindi mchana huu dhidi ya Telecom ya Djibout.
Wawakilishi hao wa Sudan waliokuwa sambamba na Al Shandy kuchukua nafasi za mabingwa watetezi Al Merreikh na Al Hilal waliitandika bila huruma Telecom kwa mabao 5-0 na kukwea kileleni mwa Kundi A, ingawa kwa sasa Gor Mahia inayokamata nafasi ya pili na KMKM waliopo nafasi ya tatu wakiendelea kutifuana kwenye Uwanja wa Taifa.
KMKM ambayo ilichukuliwa poa katika kundi hilo, inaendelea kuonyesha kuwa haisindikizi mtu kwani ilitanguliwa kufungwa bao la kwanza na Gor Mahia iliyowazamisha Yanga kwa mabao 2-1 katika pambano la ufunguzi juzi, lakini ikakomaa na kulirejesha dakika tisa baadaye.
Wakenya walipata bao la mapema dakika ya tatu kupitia Meddie Kagere aliyemaliza pande tamu la Michael Olunga ambao ulimbabatiza beki mmoja wa KMKM na kumpoteza kipa wao, lakini Simon Mateo alifunga bao dakika ya 12 tu ya mchezo na muda huu wametoka kukosa bao la wazi.
Mpaka sasa wakati karibu timu zote zikiwa zimeshacheza mechi moja moja, Yanga na Telecom ndio wanaoburuza mkia katika kundi A zikiwa hazina pointi, ingawa Yanga wanakamata nafasi ya nne.
Katika Kundi B, APR ya Rwanda inaongoza msimamo baada ya kuishinda Al Shandy kwa bao 1-0 katioka mchezo wa kwanza, huku timu za Heggan ya Somalia na LLB AFC ya Burundi zinafuatia baada ya jana kutoka suluhu ya kutofungana.
Malakia ya Sudan Kusini inaongoza kundi C ikiwa na pointi tatu sawa na Azam iliyoitambia KCCA ya Uganda jana, lakini wanatofautiana kwa mabao ya kufunga na kufungwa. Malakia iliitambia Adama City ya Ethiopia kwa bao 2-1, wakati Azam yenyewe iliishinda KCCA bao 1-0.
Mpaka muda huu unaosoma blogu hii jumla ya mabao 18 yameshatinga wavuni kwa mechi 8 zilizokwisha kucheza mpaka sasa baada ya jioni hii Gor Mahia kuitambia KMKM kwa mabao 3-1.


Utamu wa michuano hiyo upo hivi kwa mwaka huu wa 2015
MAKUNDI:

KundiA: Yanga-Tanzania, Gor Mahia-Kenya, Khartoum-Sudan, Telecom-Djibout, KMKM-Zanzibar
Kundi B: APR-Rwanda, Al Shandy-Sudan, LLB-Burundi, Heegan-Somalia,
Kundi C: Azam-Tanzania, Malakia-Sudan Kusini,  KCCA- Uganda, Adama City- Ethiopia.

Viwanja:
Taifa- Temeke
Karume-Ilala


MATOKEO:

APR              1-0  Al Shandy
KMKM           1-0  Telecom
Yanga           1-2  Gor Mahia
Adama City   1-2  Al Malakia
LLB              0-0   Heegan
Azam           1-0   KCCA
Telecom        0-5  Al Khartoum
Gor Mahia     3-1  KMKM
 

MSIMAMO:
Kundi A:
                      P  W  D  L   F  A PtsGor Mahia       2   2   0  0   5  2  6Al Khartoum    1   1   0  0   5  0  3
KMKM             2   1   0  1   2  3  3
Yanga             1   0   0  1   1  2  0
Telecom          2   0   0  2   0  6  0

Kundi B:
                     P  W D  L  F  A Pts
APR               1   1  0  0  1  0  3
LLB AFC         1   0  1  0  0  0  1
Heegan          1   0  1  0  0  0  1
Al Shandy      1   0  0  1   0  1  0

Kundi C:

                     P  W D  L  F  A  Pts
Al Malakia       1  1 0  0  2  1   3
Azam              1  1 0  0  1  0   3
Adama City     1  0  0  1  1  2  0
KCCA              1  0  0  1  0  1  0

Wafungaji:

3-Michael Olunga         (Gor Mahia)

2- Salah Bilal               (Al Kahrtoum)
1- Ousmaila Baba         (Al Khartoum)
    Haruna Shakava       (Gor Mahia)
    Michael Olunga         (Gor Mahia)
    Kirkir Glay (og)         (Gor Mahia)
    John Bocco               (Azam)
    Bizimana Djihad        (APR)
    Takele Elemayehu     (Malakia)
    Samuel Ssekamatte  (Malakia)
    Jafar Delil                 (Adama City)
    Juma Mbwana           (KMKM)
    Wagdi Abdallah         (Al Khartoum)
    Murwan Abdallah      (Al Khartoum)
    Meddie Kagere          (Gor Mahia)
    Simon Mateo            (KMKM)
    Meddie Kagere          (Gor Mahia)
RATIBA
KESHO Jumanne

Saa 8 Mchana  Al Shandy vs LLB-Karume
Saa 10 Jioni     Heggan vs APR-Karume
Saa 10 Jioni     Malakia vs Azam-Taifa

Jumatano

Saa 10 Jioni     Khartoum vs KMKM-Karume
Saa 8 Mchana  KCCA vs Adama City-Taifa
Saa 10 Jioni     Telecom vs Yanga-Taifa

Julai 23

Saa 8 Mchana  Hegaan vs Al Shandy-Taifa
Saa 10 Jioni     APR vs LLB-Taifa

Julai 24

Saa 8 Mchana  Khartoum vs Gor Mahia-Taifa
Saa 10 Jioni     KMKM vs Yanga-Taifa

Julai 25

Saa 8 Mchana  KCCA vs Malakia-Taifa
Saa 10 Jioni     Adama City vs Azam-Taifa

Julai 26

Saa 8 Mchana  Gor mahia vs Telecom-Taifa
Saa 10 Jioni     Yanga vs Khartoum-Taifa

Julai 27 Mapumziko
Julai 28-Robo fainali
B1 vs A3
A1 vs Best Looser

Julai 29
B2 vs C2
Ca vs A2

Julai 30-Mapumziko

Julai 31-Nusu Fainali
Winner B2/C2 vs C1/A2
    ""      B1/A3 vs A1/Best Looser
Agosti 01-Mapumziko

Agosti 02-Fainali