STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, February 10, 2014

Abdallah Juma aililia TFF, alia na Nkongo

Abdallah Juma enzi akiwa Simba
MSHAMBULIAJI nyota wa Mtibwa Sugar, Abdallah Juma ameliomba Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kuwafuatilia kwa ukaribu marefa wanaochezesha Ligi Kuu ili kuepusha 'maafa' yanayoweza kutoka uwanjani kutokana na maamuzi yao mabovu na yenye upendeleo.
Pia ameliomba shirikisho hilo kuweka chini ya uangalizi uwanja wa Sokoine-Mbeya ambao kwa msimu huu umekuwa ukilalamikiwa na baadhi ya klabu kukithiri kwa vitendo vya hujuma kwa timu wageni.
Mshambuliaji huyo pekee mzawa aliyefunga hat-trick kati ya tatu zilizofungwa msimu huu, alisema waamuzi wamekuwa wakifanya maamuzi mabovu yanayowatia hasira wachezaji na mashabiki.
Mchezaji huyo alisema ni vyema TFF wakawa wanafuatilia waamuzi hasa kwenye mechi hizi za duru la pili ambalo klabu huwa zikitafuta nafasi za kuwania ubingwa na kuepuka kushuka daraja.
"Mimi huwa siyo mlalamishi kwa waamuzi, lakini tulichofanywa jana kwenye uwanja wa Sokoine kwa kunyimwa mabao mawili ya wazi moja nikilifunga mimi kwa shuti kali la mbali inaumiza," alisema.
Alisema mbaya alienda kumuuliza mwamuzi, Israel Nkongo sababu ya kulikataa bao lake lililokuwa la kusawazisha na kuishi kutupiwa maneno machafu na kejeli.
"Sidhani kama huyu mwamuzi anastahili kuendelea kuchezesha ligi kwa alichokifanya kwetu na hasa kwangu kwa kunitusi baada ya kwenda kumuuliza," alisema mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba.
Strika huyo alisema mbali na TFF kuwafuatilia kwa makini waamuzi walioteuliwa kuchgeza mechi za lala salama za ligi hiyo, pia waumulike uwanja wa Sokoine kwa kukithiri vitendo vya uzalendo.
"Majuzi wenzetu wa Ruvu Shooting walifanyiwa vitendo kama hivyo, jana tumefanyiwa sisi na hata Yanga, Ashanti walishakuja hapa na kulalamika, ni vyema TFF wakaufuiatilia uwanja huu," alisema.
Juma alisema kunyamazia vitendo vya kizalendo siyo tu vinatrudisha nyuma soka, lakini pia vinahatarisha usalama na amani uwanjani kwa sababu zipi timu ambazo mashabiki wao siyo wavumilivu.
"Fikiria jana tu imetokea rasbha kubwa uwanjani baada ya mechi kwa kuharibiwa kwa viti sababu ya maamuzi ya upendeleo yaliyofanywa je kwa mashabiki wahuni hali inakuwaje," alihoji mchezaji huyo wa zamani wa AFC Arusha.
Mtibwa Sugar ilikuwa uwanja wa Sokoine kuumana na Mbeya City na kulazwa mabao 2-1, huku viongozi wake wakilalamika kunyimwa mabao mawili ya wazi na mwamuzi Nkongo ambaye MICHARAZO halikufanikiwa kumpata kujibu tuhuma alizotupiwa na Juma.

Full Maganga alitoa bao lake la Simba kwa mwanae

Full Maganga
MFUNGAJI wa bao pekee lililoiua Simba kwenye uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, Full Maganga wa Mgambo JKT amesema bao hilo ni zawadi maalum kwa mwanae kipenzi, Jamilat (5).
Aidha amesema amejisikia faraja kubwa kuwatungua Simba kutokana na ukweli kwa muda mrefu alikuwa na ndoto za kuzifunga timu kubwa nchini na kuahidi bado zamu ya Yanga watakapoumana nao.
Akizungumza na MICHARAZO kwa njia ya simu mapema leo kutoka jijini Tanga, Maganga alisema bao alilofunga juzi wakati wakiizamisha Simba kwa bao 1-0 analitoa kwa mwanae huyo anayempenda kupita maelezo.
"Bao langu la jana ni zawadi maalum kwa mwanangu kipenzi, Jamilat mwenye miaka mitano, nilijiwekea ahadi kuwa ni lazima niwatungue Simba na Mungu amenisaidia nimefurahi sana," alisema.
Aliongeza kuwa, amekuwa na ndoto za muda mrefu kuwazifunga timu kubwa na bahati imekuwa kwake na kuahidi atafanya hivyo siku timu yao itakakapoumana na Yanga.
"Bado zamu ya Yanga, naamini Mungu atanijalia kutimiza hilo kama nilivyotimiza kwa Simba na furaha zaidi ni kwamba timu yangu imepata pointi tatu muhimu tulizokuwa tunazihitaji," alisema Maganga.
Mgambo ambayo pamoja na ushindi huo bado imesalia mkiani, iliiduwaza Simba kwa kuwalaza bao hilo lililofungwa na Maganga katika dakika 28 za kipindi cha kwanza.
Pamoja na Maganga kufunga bao hilo lililomnyima raha kocha wa Simba, Zdrakov Lugarusic, lakini kazi kubwa iliyofanywa na kipa wao Salehe Tendega aliyeokoa michomo hatari ya nyota wa Simba.
Mgambo JKT itasafiri hadi mjini Tabora kuvaana na Rhino Rangers mechi itakayochezwa Jumamosi ijayo.

Kocha Marsh asubiri vipimo vya mwisho kuanza matibabu

Kocha Msaidizi wa Taifa Stars, Sylvester Marsh (Pichani kushoto) ambaye amelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) anasubiri vipimo vya mwisho ili aweze kuanza matibabu.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemtoa kocha huyo nyumbani kwake jijini Mwanza na kumleta Dar es Salaam kwa lengo la kuhakikisha anapata matibabu zaidi na kwa uangalizi wa karibu.
Tayari majibu ya kipimo cha kwanza yameshapatikana, hivyo yanasubiriwa majibu ya kipimo kingine ili aweze kuanza rasmi matibabu, lengo likiwa ni kubaini kitaalamu ugonjwa unaomsumbua.

Twiga Stars kuagwa Jumatano

TIMU ya Twiga Stars itaagwa rasmi Jumatano (Februari 12 mwaka huu) tayari kwa safari ya Lusaka, Zambia kwa ajili ya mechi ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kwa Wanawake (AWC) ambayo fainali zake zitafanyika Oktoba mwaka huu nchini Namibia. Msafara wa timu hiyo itakayoondoka kwa ndege ya Fastjet utaongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Ahmed Idd Mgoyi.

Hafla ya kuwaaga wachezaji wa timu hiyo itafanyika saa 5 asubuhi kwenye ofisi za TFF. Timu hiyo itaondoka Februari 13 mwaka huu alfajiri tayari kwa mechi hiyo itakayochezeshwa na waamuzi kutoka Rwanda.

CCM yashukuru wananchi kuikataa CHADEMA chaguzi ndogo za udiwani

NAPE NNAUYE
DAR ES SALAAM, Tanzania
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimewashukuru Watanzania kwa kukiamini na kukipatia ushindi wa kishindo katika uchaguzi mdogo wa udiwani uliofanyika jana katika kata 27 na CCM kushinda kata 23. 
Akitoa shukrani hizo, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye amesema leo kwamba siri ya CCM kuimwaga CHADEMA ni uadilifu katika kuwatumikia wananchi na kwamba, kushindwa kwa chama hicho ni ushahidi kwamba hakikubaliki na Watanzania wamewathibitishia kwamba hawajazoea vurugu.
Nape alisema CCM inaahidi kuendelea kuwatumikia Watanzania kwa amani na utulivu kwa kuwa ina uzoefu wa kufanya siasa kistaarabu na ndio siri ya kukubalika kwa wananchi.
Akizungumzia kushindwa kwa CHADEMA alisema wamehukumiwa kutokana na vurugu na kupiga watu kwenye kampeni za uchaguzi na ndio maana wametumia gharama kubwa na helkopta tatu na kuambulia kata tatu.
"CHADEMA wamevuna walichopanda Watanzania hawapenda vurugu, wamezoea amani na utulivu sasa wamewaadhibu kwa kuwanyima kura na huo ni ushahidi kwamba Watanzania hawakiamini," alisema.
Katika uchaguzi huo CCM ilishinda katika kata CCM ilishinda katika kata 23 za Kibindu na Magomeni (Pwani), Kiwalala na Namikage (Lindi), Ubwage (Shinyanga), Ibumu na  Nduli (Iringa), Kiomoni na Mtae (Tanga), Nyasura(Mara), Malindo, Santillya (Mbeya), Partimbo(Arusha, Mkwiti (Mtwara), Tungi na Ludewa (Morogoro) na Mrijo (Dodoma).

Rais Kikwete aifariji familia ya Marehemu Patrick Qorro

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini katika kitabu cha maombelezo ya msiba wa aliyekuwa Mbunge wa Karatu Waziri wa Kilimo na Ushirika Serikali ya awamu ya kwanza, Mhe. Patrick Qorro (72) aliyefariki  dunia usiku wa kuamkia Jumamosi baada ya kuugua kwa muda mfupi na kulazwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha Mifupa ( MOI)  jijini Dar es Salaam. 

Marehemu Qorro ambaye wakati wa Serikali ya awamu ya kwanza aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali, ikiwamo Waziri mdogo wa Kilimo na Ushirika na baadaye kuwa waziri kamili wakati wa awamu ya pili, alikuwa akisumbuliwa na tatizo la kuvuja damu kwenye mzunguko wa kichwa kulikosababishwa na hitilafu ya figo.Kwa mujibu wa msemaji wa familia, Bw. James Bwana, Marehemu anatarajiwa kuagwa rasmi kesho kabla ya kusafirishwa Jumatano hadi Kijiji cha Mbulumbulu, wilayani Karatu, mkoani Arusha kwa ajili ya mazishi.Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji mjane wa marehemu Dkt Martha Qorro na wanafamilia wengine nyumbani kwa  aliyekuwa Mbunge wa Karatu Waziri wa Kilimo na Ushirika Serikali ya awamu ya kwanza, Mhe. Patrick Qorro (72)  aliyefariki  dunia usiku wa kuamkia Jumamosi baada ya kuugua kwa muda mfupi na kulazwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha Mifupa ( MOI)  jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU

TFF yawafungia wachezaji watano JKT Kanembwa


KAMATI ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imewafungia mechi tatu wachezaji watano kati ya tisa wa timu ya Kanembwa JKT waliolalamikiwa na Sekretarieti kwa kumpiga mwamuzi kwenye mechi ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) iliyochezwa Novemba 2 mwaka jana.
Wachezaji hao ni Bariki Abdul, Mrisho Musa, Nkuba Clement, Nteze Raymond na Philo Ndonde. Wachezaji ambao hawakutiwa hatiani kutokana na ushahidi dhidi yao kutojitosheleza ni Abdallah Mgonja, Mbeke Mbeke, Ntilakigwa Hussein na Uhuru Mwambungu.
Mechi hiyo dhidi ya Stand United iliyochezwa Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga ilivunjwa na refa Peter Mujaya dakika ya 87 kutokana na kupigwa na wachezaji hao baada ya kuamuru ipigwe penalti dhidi ya timu yao.
Adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Ibara ya 49 (1)(b) ya Kanuni za Nidhamu za TFF baada ya kupitia vielelezo vilivyowasilishwa na Sekretarieti ya TFF ambavyo ni ripoti ya refa, ripoti ya kamishna wa mechi hiyo na video iliyoonesha tukio hilo.
Pia kabla ya kutoa adhabu baada ya kusikiliza utetezi kutoka kwa walalamikiwa ambao ni wachezaji hao na timu yenyewe ya Kanembwa JKT. Nayo Kanembwa JKT imetiwa hatiani na kupigwa faini ya sh. milioni ambayo inatakiwa kuilipa kabla ya kucheza mechi inayofuata.
Kamati hiyo iliyokutana jana (Februari 9 mwaka huu) chini ya Mwenyekiti wake Tarimba Abbas, kwanza imelaani kitendo cha wachezaji wa timu hiyo kumzonga refa, kwani vitendo vya aina hiyo ndiyo vichocheo vya vurugu viwanjani.
Lakini pia imempongeza nahodha wa Kanembwa JKT, Mbeke Mbeke kwa kuwa mstari wa mbele kuwazuia wachezaji wenzake waliokuwa wakimpiga refa wa mchezo huo.
Vilevile Kamati hiyo imesema aliyesababisha matatizo hayo ni refa Mujaya, na ingawa ilikuwa na uwezo wa kumchukulia hatua lakini haikufanya hivyo kwa vile hakukuwa na mlalamikaji na tayari Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) ilishamwadhibu.
Wakati huo huo: Vyama vya Mpira wa Miguu vya mikoa vimetakiwa kuwasilisha majina ya mabingwa wao kufikia Machi 30 mwaka huu kwa ajili ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL).
Timu zote zitakazofuzu kucheza RCL zinaruhusiwa kusajili wachezaji wapya wasiozidi watano kutoka ndani ya mkoa kwa kufanya taratibu za uhamisho. Kamati imesisitiza kuwa usajili wa RCL ni uleule uliotumika kwenye Ligi ya Mkoa.
Kamati ya Mashindano ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana Februari 6 mwaka huu imekataa ombi la Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA) kuongeza timu za Ligi ya Mkoa kutoka 20 hadi 24.
Ikiwa chini ya Mwenyekiti wake Geofrey Nyange, Kamati hiyo imesema kwa mujibu wa Kanuni ya Ligi ya Mkoa, ligi hiyo inatakiwa kuwa na timu kati ya 16 na 20, hivyo vyama vya mpira wa miguu vya mikoa vinatakiwa kuendesha ligi kwa kufuata kanuni.
Kamati hiyo imeongeza kuwa hata kama ingekubalia ombi la MZFA kiutaratibu lisingewezekana kwa vile kanuni hufanyiwa marekebisho baada ya msimu kumalizika, wakati ombi hilo limewasilishwa katikati ya msimu.

KWA HUDUMA ZA MAFOTO EBU CHEKI HAPA

MAFOTO PRODUCTION & ENTERTINMENT KWA MAHITAJI YAKO YA STILL PICTURE, VIDEO SHOOTING, MUSIC & Mc's KATIKA SHEREHE YA AINA YEYOTE. 

KAZI NYINGINEZO:- VIDEO EDDITING, COVER DISGNING, PPS ZA DK 3, POSTERS ZA AINA MBALIMBALI COVER CD PRINTING, BURNING CD N.K. WASILIANA NASI KWA NO, 0787 200005/0754, 0655-306109/0714 656660 

BARUA PEPE:- muhidinuk@yahoo.co.uk,sufianimafotoblog@gmail.com AMA TEMBELEA www.sufianimafoto.com

OFISI ZETU ZIPO KIJITONYAMA NYUMA YA KITUO CHA POLISI MABATINI, BARABARA YA SPIKA WA BUNGE

Barcelona yarejea kileleni, Messi moto mkali

At the double: Messi (left) scored twice to help Barcelona to a 3-1 win against Sevilla
Messi akishangilia moja ya mabao yake na Pedro
NYOTA wa Argentina, Lionel Messi anayichezea Barcelona jana alidhihirisha bado ni moto wa kuotea mbali baada ya kuisaidia klabu yake kuibuka na ushindi wa mabao 4-1 ugenini dhidi ya Sevilla.
Messi aliifungia Barca magoli mawili moja la kila kipindi huku bao la mapema la Alex Sanchez na lingine la jioni la Cesc Fabregas yalitosha kuirejesha mabingwa hao watetezi kileleni mwa msimamo waking'oa Real Madrid na Atletico Madrid waliokuwa juu yao.
Barcelona wamerejea kileleni wakiwazidi wapinzani wao uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa, licha ya zote kulingana pointi 57.
Wenyeji ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Moreno katika dakika ya 15 kabla ya Sanchez kusawazisha dakika ya 34 na baadaye Messi kufunga bao la pili dakika ya 44.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Messi kuongeza bao la tatu katioka dakika ya 55 kabla ya Fabregas kuhitimisha ushindi huo mnono kwa bao la dakika ya 87.