STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, October 6, 2014

Jahazi la QPR lazidi kutota, wapigwa 2-0 na West Ham

QPR  defender Rio Ferdinand
Rio Ferdinand akiwajibika na QPR akifikisha mechi ya 500 katika miaka ya 18 ya kucheza kwake
West Ham United v QPR
Ooh kitu! Wachezaji wa QPR hawaamini wakitunguliwa bao na West Ham
West Ham v QPR
Yebaaa! Wachezaji wa West Ham wakipongeza kwa kupata ushindi wa mabao 2-0 kwa vibonde QPR
JAHAZI la timu ya QPR linaloongozwa na kocha Harry Redknapp limezidi kuzama baada ya jana kucharazwa mabao 2-0 na West Ham United katika mfululizo wa Ligi Kuu ya England.
QPR wenye pointi na kuburuza mkia walianza vibaya mchezao huo baada ya beki wake kutoka Nigeria Chinedum Onuoha, aliyewahi kuichezea Mancjester City kujifunga bao dakika ya tano tu ya mchezo huo uliochezwa Uptown Park.
Kipindi chja pili kilikuwa majanga zaidi kwa wageni baada ya Diafra Sakho kuongeza bao la pili kwa West Ham kwa kuunganisha mpira wa kichwa katika dakika ya 55 na kuifanya West Ham kuchupa toka nafasi ya tisa katika msimamo wa ligi hiyo hadi ya saba, wakati QPR wakiendelea kung'ang'ania mkiani.
QPR haijawahi kushinda mechi yoyote ya uwanja wa ugenini tangu Machi 2, 2013.

No comments:

Post a Comment