STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 20, 2013

Waraka namba 2 wa Zola D kwa Watanzania

Zola D katika pozi
BARUA MAALUM KUTOKA KWA DAVID MICHAEL MLOPE,aka ZOLA D KWENDA KWA WATANZANIA WOTE WALIOSHIRIKI KATIKA MSIBA WA MANGWEAR.pamoJa na LANGA KILEO.

DAVID MICHAEL MLOPE BOX 70098 DAR ES LAAM TANZANIA.
PHONE +255715296889.
barua no 2.

naendelea pale nilipoishia kwenye barua ya mwanzo namba 1 ...... habari zenu ndugu zangu watanzania hope wote ni wazima na mnaendelea na mishe za maisha mimi mzima siJambo Japo nina stress nyingi sana mpaka nimepungua kg 3,kutokana na mawazo na kuto kulala tokea msiba wa arbert mangwear pia tumepata pigo Jingine la mdogo wetu langa kileo,siJui niseme nini kwa Jinsi inavyo niuma ila nina mwachia Mungu maana ndio kazi yake pia pole sana wazazi wa langa kileo baba na mama pamoJa na familia yote kwa uJumla pia asante sana watanzania wote walioJitokeza kwenye safari ya kumsindikiza ndugu yetu msanii mwenzetu langa kileo leo nataka kugusia sana upande wa maisha yetu na dini kama binadamu tunaopita tu kwenye hii dunia maana kila mtu atakufa vitabu vya dini vimeandika.Ndugu zangu wapendwa watanzania dunia imekwisha ndugu zangu tuanze kufanya ibada na kutenda yaliyo mema coz free masons wanawatumia ndugu zetu kwenye big brother na seemu mbali mbali kuwaonyesha wakiwa watupu uchi na kuwadanganya kwa pesa,na sasa wameingia africa mashariki kwa kishindo sana hawa free masons Juzi tu nimepigiwa simu na watu kampuni Jina siri yangu wanataka nikacheze video ya ngono na mwanamke kwa kitita cha milion 70 nikawaeleza siwezi kufanya uchafu kama huo,na leo tena wamenipigia wakisema watanipa milion 100 bado nimekataa Je unaelewa kwa nini nimekataa? free masons wanataka viJana shupavu na wenye akili na vipaJi ili waweze kuwatumia kuitangaza dini yao na wanaweza kukupa maisha ya Juu kwa gharama yoyote ile, Mungu atuepushe nao na Mungu atulindie watoto wetu inshallah wasiingie kwenye dini ya kishetani,wahi kuwapeleka madrasa watoto mapema waitambue dini mapema na kuwapeleka kwenye mafunzo ya dini kwenye makanisa tuliyoyazoea tokea kitambo na tuachane na makanisa mapya yanayoanzishwa kila kukicha na wachungaJi wao wanaJiita miungu watu,ndugu zangu naelewa watu wanaweza kuniona kama nilie changanyikiwa hapana ila nimeamua kupoteza muda wangu kukaa chini na kuandika machache ninayoyaona kwa upeo wangu na vipaJi alivyonipa Mungu kuelimisha na kuburudisha,siwezi kukaa kimya pale ninapo tizama taifa langu lina teketea kwa maovu,na tunapelekeshwa kishetani na dini feki na makampuni ya kigeni katika nchi yetu tuna acha utamaduni wetu na tunaingia kwenye utamaduni wa watu wa kishetani kwa upeo wetu mdogo na umasikini tumetekwa na pesa na starehe kiasi kama sisi wasanii ukitizama storia ya msanii mwanzo kabla aJawa super star alikuwa ni mtu wa kufanya ibada ila sasa amekuwa super star awezi tena kufanya ibada wala kutoa dhaka au kuwasaidia wazazi wake kisa yeye ni star na yupo bussy Je swali huyu star msanii ni kioo cha Jamii au amegeuka kuwa moto wa Jamii? kila kukicha kwenye magazeti utaskia story za sifa mbaya na picha chafu za wasanii sehemu flani wakifanya ngono na mambo mengine ya kumchafua Mungu wetu,ndugu zangu wasanii naomba tubadilike na tuwe mfano ili tuweze kuliongoza taifa letu salama na tuwafundishe wadogo zetu waige mfano mzuri wa tabia zetu nJema na sio uchafu wetu,ndugu zangu watanzania mimi sitaki kuwachosha maana nina MAMBO MENGI SANA YA KUANDIKA ILA NAONA KWA LEO NISHIE HAPA,NACHUKUA NAFASI HII KUAMBIA NAWAPENDA SANA WATANZANIA WENZANGU PIA NAWAPENDA VIONGOZI WANGU WA TANZANIA PIA NAIPENDA NCHI YANGU YA TANZANIA NIPO TAYARI KUFA KUITETEA NCHI YANGU NA WANACHI WANGU NAWATAKIA MAISHA MEMA NA FAMILIA ZENU NI MIMI MTIIFU WENU KATIKA UjENZI WA TAIFA LETU TUKUFU, DAVID MICHAEL MLOPE AKA ZOLA D.ITAENDELEA!!!!!

Zola D awashukuru Watz msiba wa Ngwair, Langa, lakini...!


Mwili wa Ngwair ukiingizwa kaburini, ambapo Zola D (mwenye miwani) naye alikuwa mmoja wa walioshiriki mazishi hayo mjini Morogoro.

BARUA MAALUM KUTOKA KWA DAVID MICHAEL MLOPE,ZOLA D KWENDA KWA WATANZANIA WOTE WALIOSHIRIKI KATIKA MSIBA WA MANGWEAR...

DAVID MICHAEL MLOPE BOX 70098 DAR ES LAAM TANZANIA.
PHONE +255715296889.

habari za leo watanzania wote ,nachukua nafasi hii kwa niaba ya wasanii wa kundi la chemba sqward east zoo,kuwashukuru watanzania wote walioshiriki katika msiba wa ndugu yetu mpendwa mangwear hakika nimeona upendo wenu kwa kumzika ndugu yetu Arbert k mangwear kwa upendo wenu mkubwa sana,mimi binafsi sina cha kuwalipa ila nina imani kubwa sana Mungu atawalipa,na sio kwa mangwear tu naomba mzidi kushilikiana na sisi wasanii wenu hata siku nikifa mimi au msanii mwingine naomba mtuzike KWA UPENDO msituache maana sie sote ni binadamu tunapita tu hapa kwenye hii dunia kila mtu atakufa muhimu ni kupendana na kushirikiana kwa upendo,pia kama tunagombana hapa duniani ni bora tupatane kabla ya kifo kutukumba siku yetu ya kufa hakuna anaetambua itakuwa lini, maana Mungu alisema ukisamehe na yeye atakusamehe siku yako ya kihama,kuna mambo mengi nimejifunza kwenye hii dunia,kwamba tujitahidi kufanya yaliyo mema kutengeneza njia bora siku tukifa,napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru sana wana kamati wote waliojitolea tokea mwanzo kuandaa safari kutoka south africa mpaka tanzania asante sana BRO P FUNK MAjANI , BONGO RECORDS kwa upendo wako na mchango wako kwetu sie wadogo zako Mungu ATAKULIPA ZAIDI NA ZAIDI ,ASANTE SANA RADIO CLOUDS FM KWA KUSHIRIKI KWA UPENDO WENU MKUBWA ,na wafanyakazi wake wote walioshiriki kwa upendo katika kukamilisha safari ya mpendwa wetu MANGWEAR,asante sana BRO ADAMU jUMA VISUAL LAB NIMEONA KAZI KUBWA ULIYOIFANYA MUNGU AKUBARIKI SANA ENDELEA KUWA NA MOYO HUO HUO , ASANTE SANA, BRO MIRAD AYO,BRO MAjIZO,BRO TC TIMOTH CHERULA,ADAMU MCHOMVU,RADIO TIMES FM,RADIO EAST AFRICA NA EAST AFRICA TV,ITV,CHANEL TEN BRO RIZ 1 KIKWETE,BRO SUGU,SIST j DEE,Dj CHOKA, PUSH NA WENGINE WENGI,AMBAO NIMEWASAHAU MAjINA YENU ASANTENI SANA SANA WOTE WALIOTOA MAGARI YAO KWENDA MOROGORO KUZIKA,PIA ASANTE SANA WANAKAMATI WA MOROGORO,ASANTE SANA VIONGOZI WA POLICE DAR ES SALAAM NA VIONGOZI WA POLICE MOROGORO KWA KUIMALISHA ULINZI KATIKA MSAFARA WA MANGWEAR KUANZIA DAR MPAKA MOROGORO NINA MAMBO MENGI SANA YA KUANDIKA ILA NAONA KWA LEO NISHIE HAPA,NACHUKUA NAFASI HII KUAMBIA NAWAPENDA SANA WATANZANIA WENZANGU PIA NAWAPENDA VIONGOZI WANGU WA TANZANIA PIA NAIPENDA NCHI YANGU YA TANZANIA NIPO TAYARI KUFA KUITETEA NCHI YANGU NA WANACHI WANGU NAWATAKIA MAISHA MEMA NA FAMILIA ZENU NI MIMI MTIIFU WENU KATIKA UjENZI WA TAIFA LETU TUKUFU, DAVID MICHAEL MLOPE AKA ZOLA D.ITAENDELEA!!!!!

Barabara ya Kimara King'ongo yafungwa mwezi mzima kisa....!




HIVI ndivyo wakazi wa Kimara King'ongo Kata ya Kimara na Samanga wanavyohenyeka majira ya asubuhi kwa kutembea kwa miguu kupandisha kilima sumbufu cha Peter's School ambacho kinatengenezwa kwa kuwekewa zege ili kuruhusu magari kupita bila usumbufu .
Matengenezo ya barabara hiyo yanayoendelea kwa sasa yamefanya njia hiyo ifungwe kwa mwezi mzima tangu Juni 1-30, ili ikiachiwa wakazi wa eneo hilo wafurahie huduma ya usafiri baada ya sasa kila siku asubuhi magari ushusha abiria darajani badala ya kuzunguka njia ya kutokea Stop Over au Kimara Temboni.

Hatimaye mhanga wa bomu la Arusha azikwa

HATIMAYE aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA) Kata ya Sokoni I, Judith William Moshi, aliyefariki kwa mlipuko wa bomu kwenye viwanja vya Soweto jijini Arusha siku ya Jumamosi (Juni 15, 2013) wakati wa ufungwaji wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani umezikwa leo jijini humo.
Chini baadhi ya picha za msafara wa mazishi wa mwanadada huyo ambaye alikuwa miongoni mwa watu watatu waliokufa katika mlipuko huo ambao al manusura ungewakumba viongozi wa kuu wa chama hicho akiwamo Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe (Mbunge).

Hapa ni Sugu akiwa na Peter Msigwa wakiongoza msafara.
Viongozi  wa chadema watua Arusha kwa ajili ya kutoa heshima zao za mwisho kwa wale waliofariki katika mkutano wa Chadema wakati wa mripuko wa bomu. Huku wakishirikiana na wananchi wa Arusha, John Mnyika ataongoza shughuli hizo.
Hili ndilo jeneza lililolobeba mwili wa marehemu ukipelekwa sokon 1


 

Mbowe, Lema wajisalimisha Polisi

Mwenyekiti wa CHADEMA  Fremaan Mbowe pamoja na mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema leo wamejisalimisha Polisi  baada ya jeshi hilo kutangaza linawasaka baada ya vurugu ziliztokea jana mjini Arusha.
Akiongea na waandishi wa habari,  Fremaan Mbowe alisema kuwa wao wamejisalimisha kama polisi walivyosema wanawatafuta na walipofika waliandika maelezo ambapo alisema kuwa polisi waliwaita kwa mambo mawili, moja likiwa ni kwa kuwahoji kwanini walifanya mkutano usio wa halali ambapo alisema kuwa;
"Jambo la kufanya mkutano pasipo kuwa halali sio kweli kwani polisi walituruhusu tukafanye mkutano katika sehemu hile lakini kinachotushangaza tumefanya wamekuja kutupiga mabomu na kusema sio wa halali na kuhusiana na ushahidi msimamo wangu upo pale pale tunao ushahidi wa kutosha na tunamjua aliyerusha bomu Jumamosi, lakini hatutautaoa hadi  Rais atakapounda Tume Huru ya majaji ili wafuatilie suala hili. Hao ndiyo tutawaonyesha ushahidi huo, lakini siyo Polisi hatuwezi kuwapa," alisema Mbowe.
Afande Chagonja akiongea na waandishi wa habari
Kwa upande wa Polisi kupitia Kamishna wa Mafunzo na Operesheni za Kijeshi,  Paul Chagonja akiongea na wanahabari alisema waliwahoji wabunge hao na kuwaomba ushahidi waliokuwa nao kama wanavyodai, lakini waheshimiwa hao hawakutoa ushirikiano.
"Mbowe alisema kuwa ana ushahidi na hata katika vyombo vya habari ametangaza lakini nashangaa tulivyomuuliza hapa amesema kuwa hana ushahidi wowote na wala hajawahi kutamka hivyo sasa sisi kwa kuwa kasema hivyo nitakaa na makachero wangu na tutaangalia jinsi ya kufanya"alisema Chagonja
Aidha alisema kuwa alimuliza mbunge wa Arusha mjini kwanini awali alikuja kuwasifia Polisi baadae akawageuka ilihali alishasema katu hawezi kusema uongo na kuwajibu kuwa, yeye anafuata mwenyekiti wake anachosema.

Polisi waua raia kwa risasi Mbeya, RPC afafanua kilichotokea




 Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya  Diwani Athuman
---

MAUAJI YA MTU MMOJA KUFUATIA VURUGU YA WANANCHI WA KIJIJI CHA LUMBILA WILAYA YA MBOZI KUWASHAMBULIA ASKARI WALIOKUWA WANAFANYA OPERESHENI.
--
MNAMO TAREHE 19.06.2013 MAJIRA YA SAA 13:00HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA LUMBILA KATA YA RUANDA WILAYA YA MBOZI MKOA WA MBEYA. RAJABU S/O WILSON MWASHITETE, MIAKA 25, MNYIHA, MKULIMA, MKAZI WA KIJIJI CHA LUMBILA ALIUAWA KWA KUPIGWA RISASI NA ASKARI POLISI WALIOKUWA KATIKA MSAKO DHIDI YA WAHALIFU/WAPORAJI KATIKA ENEO LA MLIMA SENJELE.

CHANZO NI BAADA YA ASKARI POLISI WAKIWA KATIKA OPERESHENI ENEO HILO KUZINGIRWA NA KUNDI LA WANANCHI ZAIDI YA 150 WA KIJIJI HICHO WAKIWA NA SILAHA ZA JADI MAPANGA, MARUNGU, SHOKA NA MAWE WAKIWAZUIA ASKARI HAO KUKAMATA WAHALIFU NA KUANZA KUFANYA VURUGU BAADA YA KUWA WAMEKAMATA MALI INAYODHANIWA KUWA YA WIZI AMBAYO NI MAFUTA  AINA YA DIESEL MADUMU ZAIDI YA 100.

HATA HIVYO KUFUATANA NA VURUGU ZILIZOJITOKEZA WALIFANIKIWA KUCHUKUA MADUMU MACHACHE AMBAYO NI MADUMU MATATU YENYE UJAZO WA LITA 60, MADUMU MAWILI YENYE UJAZO WA LITA 20 NA 
MADUMU NANE LITA 30 HIVYO UVAMIZI HUO WA WANANCHI NDIO ULIOWAFANYA ASKARI POLISI WASHINDWE KUCHUKUA VIELELEZO VYOTE.


MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA WILAYA YA MBOZI.  AIDHA KATIKA TUKIO HILI CHARLES  S/O JOSE  MWAWALO,MIAKA 27,MNYIHA,MKULIMA MKAZI WA KIJIJI CHA LUMBILA ALIJERUHIWA KWA KUPATA MICHUBUKO TUMBONI AMBAPO UCHUNGUZI UNAFANYWA KUBAINI NI KITU GANI KILICHOMJERUHI.

PIA WANANCHI WALIFUNGA BARABARA KUU YA MBEYA/TUNDUMA KWA KUWEKA MAWE NA MAGOGO NA KUSABABISHA MSONGAMANO MKUBWA WA MAGARI BARABARANI. 

HALI ILIKUWA SHWARI BAADA YA KAMANDA WA POLISI KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI KUFIKA ENEO LA TUKIO NA KUZUNGUMZA NA WANANCHI PAMOJA NA VIONGOZI WA ENEO HILO KISHA KUFUNGUA BARABARA .

ASKARI POLISI WANNE WALIJERUHIWA KATIKA TUKIO HILO KATI YAO WATATU WALIPATIWA MATIBABU NA KURUHUSIWA NA ASKARI MMOJA  AMELAZWA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA KWA MATIBABU ZAIDI . 

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA TABIA YA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI KWANI NI KINYUME CHA SHERIA BADALA YAKE KUWA NA UTAMADUNI WA KUTATUA KERO/MALALAMIKO YAO KWA NJIA YA MAZUNGUMZO KWA KUYAWASILISHA KATIKA MAMLAKA HUSIKA. AIDHA ANAWATAARIFU WALE WOTE WALIOWAHI KUIBIWA/KUPORWA MALI MBALIMBALI YAKIWEMO MAFUTA WAJITOKEZE POLISI KWA AJILI YA HATUA ZINAZOSTAHILI.


Signed By,
                          
[DIWANI ATHUMANI  

[DIWANI ATHUMANI   - ACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

NMB, Wabunge walivyoonyeshana kazi Dodoma

KATIKA kuendeleza na kuimarisha uhusiano mzuri baina ya Benki ya NMB na Watunga Sheria wa Bunge la Jamhuri, mwishoni mwa wiki timu hizo zilionyeshana kazi kwa kuumana katiuka pambano lililoandaliwa na Benki hiyo ambao uilihudhuriwa na mashabiki lukuki wa timu hizo wea mjini Dodoma.
 Hiki ndicho kikosi kamili cha timu ya benki ya NMB kilichong’ara katika mechi na timu ya Wabunge kwenye Uwanja wa Jamhuri.
 Kikosi kamili cha timu ya Wabunge.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mh. George Mkuchika ambae alikua ndiye mgeni rasmi akikagua kikosi cha timu ya NMB  kabla ya mpambano huo.
 Naibu waziri wa habari Vijana,Utamaduni na Michezo Mh.Amos Makalla (Jezi ya njano na Bluu) akipigwa chenga na  Afisa mkuu wa fedha NMB  Waziri  Waziri katika mtanange huo uliokuwa wa kukata na shoka.
 Mbunge wa Kinondoni Mh. Iddi Azan ambae ndiye mlinda mlango wa timu ya wabunge  (Jezi ya rangi ya chungwa) akiongoza wachezaji wenzake kufurahia goli moja walilolipata na kuwapa ushindi dhidi ya timu ya NMB
Mashabiki wa timu zote mbili wakifuatilia mtanange huo ambao uliisha kwa Wabunge kuibuka kidedea dhidi ya NMB.

Prof Lipumba mgeni rasmi miaka `13 ya Kikosi cha Mizinga

http://sphotos-a.ak.fbcdn.net/hphotos-ak-ash3/p480x480/712_467874856634160_1616825647_n.jpg
Kiongozi wa Kikosi cha Mizinga, Karama Masoud 'Kalapina'
 MWENYEKITI wa Chama cha CUF, Prof Ibrahim Lipumba anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika onyesho la maadhimisho la miaka 13 ya Kikosi cha Mizinga zinazotarajiwa kufanyika kesho kwenye ukumbi wa Msasani Club, jijini Dar es Salaam.
Kiongozi wa Kikosi, Karama Masoud 'Kalapina' aliiambia MICHARAZO kwamba, Prof Lipumba ndiye atakayekuwa mgeni rasmi baada ya mipango ya awali kumualika Mbunge wa Jimbo la Kinondoni, Idd Azan kushindikana kumpaka kwa kuwaomba udhuru.
Kalapina alisema maandalizi ya onyesho hilo ambalo mashabiki watalazimika kulipa Buku 5 tu mlangoni, yamekamilika ikiwemo kuongezeka kwa idadi ya wasanii na makundi yatakayowasindikiza katika onyesho hilo ambalo litaambatana na maonyesho mbalimbali yenye asili ya utamaduni wa Hip hop.
"Maandalizi ya onyesho la Kikosi cha Mizinga yamekamilika ikiwemo kutarajiwa Mwenyekiti wa Kitaifa wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mgeni rasmi baada ya kumkosa Mhe. Idd Azan, pia burudani zimeongeza zaidi katika kunogesha miaka hiyo 13," alisema Kalapina. 
Mkali huyo ambaye pia ni mwanaharakati na mwanasiasa alisema baadhi ya wasanii watakaoshiriki kupigwa mizinga 21 ya Kikosi kesho ni Afande Sele, Young Killer, Manzese Crew, Stereo, Kala Jeremiah, LWP, Mansu-Lee, Gangwe Mob  wakiwa na Inspekta Harun na wengine wakiwamo Kikosi cha Mizinga chenyewe.
Shughuli nyingine zitakazoambatana na onyesho hilo ni maonyesho ya uchoraji na kupaka rangi, mitindi ya nguo na mavazi, kucheza break dance na utoaji wa tuzo kwa watu na asasi zilizosaidia Kikosi cha Mizinga kufika hapo ilipo ikiwa inatimiza miaka hiyo 13 tangu kuzaliwa kwake.