STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, June 20, 2013

NMB, Wabunge walivyoonyeshana kazi Dodoma

KATIKA kuendeleza na kuimarisha uhusiano mzuri baina ya Benki ya NMB na Watunga Sheria wa Bunge la Jamhuri, mwishoni mwa wiki timu hizo zilionyeshana kazi kwa kuumana katiuka pambano lililoandaliwa na Benki hiyo ambao uilihudhuriwa na mashabiki lukuki wa timu hizo wea mjini Dodoma.
 Hiki ndicho kikosi kamili cha timu ya benki ya NMB kilichong’ara katika mechi na timu ya Wabunge kwenye Uwanja wa Jamhuri.
 Kikosi kamili cha timu ya Wabunge.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mh. George Mkuchika ambae alikua ndiye mgeni rasmi akikagua kikosi cha timu ya NMB  kabla ya mpambano huo.
 Naibu waziri wa habari Vijana,Utamaduni na Michezo Mh.Amos Makalla (Jezi ya njano na Bluu) akipigwa chenga na  Afisa mkuu wa fedha NMB  Waziri  Waziri katika mtanange huo uliokuwa wa kukata na shoka.
 Mbunge wa Kinondoni Mh. Iddi Azan ambae ndiye mlinda mlango wa timu ya wabunge  (Jezi ya rangi ya chungwa) akiongoza wachezaji wenzake kufurahia goli moja walilolipata na kuwapa ushindi dhidi ya timu ya NMB
Mashabiki wa timu zote mbili wakifuatilia mtanange huo ambao uliisha kwa Wabunge kuibuka kidedea dhidi ya NMB.

No comments:

Post a Comment