STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 15, 2014

Hiki ndicvho kikosi kitakachowavaa magwiji wa Real Madrid

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi0PgyWbjR3xJl_pDRCaNGU3l8dtB2GOqTNf-JSpWlJu49gUt4n2uHIvOpPfV4Z9ddGl5h2g4yTsGK0Jhe_a8dPZrYOqWD9xeWlJLMBfnXfCK8BDTQtWuRA_uILS5LNfN6gPltqdA6sRYA/s1600/Simba+SC+2002.jpg
Baadhi ya nyota wa zamani wa Simba walioitwa katika timu ya Tanzania All Stars
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh1b2UD-fxCvuq6yPPbyH6hYAbnGbxw_AX1a_UUScixb7mZXk_whqMf7JuV-NzIgxAw6F42KBQ6yXvgJjwDP6uRwCsWw5tH5B9AeEgertpkEAM8sAl-lPITOVknWRfcUH4ihF5M3RkNjOE/s400/IMG_1860.jpg
Wengine wametoka katika kikosi hiki cha Yanga
MAKIPA wa zamani maarufu waliowahi kutamba na timu za Simba, Yanga na Taifa Stars, Mohammed Mwameja na Manyika Peter ni miongoni mwa wachezaji wa kikosi cha Tanzania All Stars kitakachovaana na magwiji wa Real Madrid ya Hispania, Agosti 23, mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana jana jijini Dar es Salaam zinasema kuwa kikosi hicho kitakuwa chini ya Kocha Charles Boniface akisaidiwa na Fred Felix 'Minziro' na Jamhuri Kihwelo ‘Julio’.
Mbali na Mwameja na Manyika wachezaji wengine wanaounda kikosi hicho ni mabeki; Nsajigwa Shadrack, Mecky Mexime, Boniface Pawasa, John Mwansasu, Abubakar Kombo, George Masatu na Habib Kondo,
Viungo Suleiman Matola, Shaaban Ramadhani, Salvatory Edward, Sabri Ramadhani ‘China’, Yussuf Macho, Abdul Mashine, Abdul Maneno, Mao Mkami, Steven Nyenge, Madaraka Suleiman, Akida Makunda na Mtwa Kihwelo.
Washambuliaji ni Monja Liseki, Iddi Moshi, Dua Said, Emmanuel Gabriel, Said Maulid, Thomas Kipese, Nasor Mwinyi ‘Bwanga’, Edibilly Lunyamila, Mohamed Hussein ‘Mmachinga’, Clement Kahabuka, Madaraka Suleiman na Akida Makunda.
Safu ya uongozi ya timu hiyo ya Tanzania ni pamoja na Mtemi Ramadhani, Hasannai Mnyenye, Omar Gumbo na Hamis Kisiwa na daktari wake ni Dk Mwanandi Mkwankemwa.
Wachezaji magwiji wa Real Madrid waliotamba kuanzia La Liga, wakacheza ligi nyingine za Ulaya, Kombe la Ulaya, Ligi ya Mabingwa na Kombe la Dunia waliowahi kuchezea Real Madrid watakuja nchini Agosti 22 kwa ziara maalum pamoja na kucheza mchezo wa kirafiki na kikosi maalum cha wachezaji nyota wa Tanzania Agosti 23, kabla ya kufanya ziara ya kitalii katika vivutio mbalimbali, ikiwemo kupanda mlima Kilimanjaro.
Real Madrid inakuja nchini kwa mwaliko wa kampuni ya Tanzania Sisi ni Nyumbani (TSN), chini ya Mkurugenzi wake Mkuu, Farough Baghozah.
Miongoni mwa nyota wanaotarajiwa kuja na Real nchini ni pamoja na Wanasoka Bora wa zamani wa Dunia, Mfaransa Zinadine Zidane, Mreno Luis Figo na Mbrazil, Ronaldo Lima.
Magwiji hao wa Real tayari wamekwishafanya matangazo ya ziara yao nchini wakisema wana hamu mno ya kukanyaga ardhi ya Tanzania.
Kampuni ya Vodacom Tanzania ni miongoni mwa makampuni yaliyojitokeza kudhamini ziara pamoja na Fastjet, Tropical, Pembe Flower, Lake Gas, EFM Radio na Ladger Plaza Bahari Beach.
Wito umetolewa kwa makampuni zaidi kujitokeza kudhamini ziara hiyo ya kihostoria nchini.

Serikali yawatoa hofu wananchi kuhusu Ebola

Screen Shot 2014-08-15 at 10.47.21 AM

SERIKALI imewatoa hofu wananchi wake baada ya kutoa ufafanuzi huu ya taarifa za kuingia kwa ugonjwa huo jijini Dar es Salaam na kuibua kizaazaa.
Ugonjwa wa Ebola ambao kwa sasa umeingia kwenye headlines za dunia kutokana na kuripotiwa kwenye nchi mbalimbali za Afrika sasa umeingia kugusa vichwa vya habari na kuihusisha Tanzania.
Waziri wa Afya wa Seif Rashid amesema wagonjwa waliohisiwa kupata maambukizo hayo kutokana na dalili za awali ni kutoka Benin na Mtanzania lakini baada ya vipimo wameonekana hawana maambukizo hayo.
Waziri Seif Rashid amesema kuwa tayari eneo maalumu limetengwa kwa ajili ya kufanyia uchunguzi wagonjwa wanaotiliwa shaka kuwa na ugonjwa huo ikiwa ni kauli iliyotoka baada ya kufanyiwa uchunguzi kwa wagonjwa wawili waliohisiwa.
Kupitia ukurasa wake wa facebook, Waziri Seif amesema vifaa maalumu vitakavyotumiwa na watoa huduma katika kuhudumia wagonjwa vimewekwa pia huku wizara ya afya ikiongeza uwezo wa kufanya uchunguzi katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere ambao wasafiri wengi kutoka nje huutumia.

Tanzania yaporomoka FIFA, yashindwa hata na Sierra Leone

Kikosi cha Stars ambacho kiling'olewa michuanoni na Msumbiji na kuporomoka kwenye viwango vipya vya FIFA
TANZANIA imeporomoka kwa nafasi nne katika viwango vya soka vilivyotolewa na Shirikikisho la Soka duniani, Fifa.
Katika viwango hivyo ambavyo Ujerumani imeendelea kuongoza kwa ubora duniani ikifuatiwa na Argentina na Uholanzi, Tanzania imeshika nafasi ya 110 huku Msumbiji ambayo iliitoa kwenye kinyang'anyiro cha kuwania tiketi ya kucheza fainali za Mataifa ya Afrika mwakani nchini Morocco ikipanda kwa nafasi saba na kuwa ya 107.
Kwa upande wa Afrika Mashariki na Kati, Uganda imeendelea kuwa kinara ikipanda nafasi sita na kuwa ya 81 duniani ikifuatiwa na Rwanda ambayo ni ya 101 baada ya kupanda nafasi nane, Kenya inafuata ikiwa ni 104 licha ya kushuka nafasi tisa mwezi huu, huku Burundi ikiburuza mkia ikiwa ni ya 129 baada ya kushuka nafasi tatu.
Barani Afrika kwa ujumla, Algeria inaongoza huku kidunia ikishika nafasi ya 24 ikifuatiwa na Ivory Coast (25), Nigeria (33), Ghana (36) na Misri (38).
Chini ni 20 Bora ya Dunia safari hii ambayo inafungwa dimba na England;
1. Ujerumani,
2. Argentina
3. Uholanzi
4. Colombia
5. Ubelgiji
6. Uruguay 
7. Hispania
7. Brazil
9. Uswisi
10. Ufaransa
11. Ureno
12. Chile
13. Ugiriki
14. Italia
15. Costa Rica
16. Croatia
17. Mexico
18. Marekani
19. Bosnia and Herzegovina
20. England
AFRIKA 20 Ipo hivi:
    
1. Algeria
2. Ivory Coast
3. Nigeria
4. Ghana
5. Misri
6. Tunisia
7. Sierra Leone
8. Cameroon
9. Burkina Faso
10.Senegal
11.Mali
12.Libya
13.Guinea
14. Afrika Kusini
15.Cape Verde
16.Angola
17.Benin 
18. Kongo
19. Morocco
20. Uganda

Snura kukirudia Kigoda chake cha zamani!

Snura katika pozi
STAA wa nyimbo za 'Majanga', 'Umevurugwa' na 'Umeshaharibu', Snura Mushi, amesema yupo katika mipango ya kuurudia wimbo wake wa zamani uitwao 'Kigoda'.
Wimbo huo wa 'Kigoda', ulirekodiwa na Snura miaka zaidi ya 15 iliyopita wakati akianza kuibukia kwenye sanaa, lakini haukupata nafasi ya kumtambulisha kama kazi zake za sasa.
Akizungumza na MICHARAZO, Snura alisema ataurudia wimbo huo kwa kuuweka kwenye miondoko ya mduara akiamini utakubalika kwa vile ni wimbo uliokuwa na mistari iliyoshiba na yenye ujumbe mzuri.
Snura alisema kazi hiyo itafanywa mara baada ya kutengeneza video za nyimbo zake mbili zilizokamilika kwa sasa za 'Ime-expire' na 'Mtaka Basi' ambazo bado hazijaachiwa hewani.
"Nipo katika mpango wa kuurudia wimbo wangu kwa kwanza kabisa katika fani ya muziki uitwao 'Kigoda', ila kazi hiyo itafanywa baada ya kukamilisha video ya nyimbo zangu mpya za sasa," alisema Snura.
Msanii huyo ambaye pia  ni muigizaji wa filamu alisema kila uchao yeye huwaza namna ya kuwashushia mashabiki wake burudani kama njia ya kuwashukuru kwa kumpokea vyema katika fani hiyo.

Coast Modern kuwatoa watatu wapya

Omar Tego
KUNDI la muziki wa taarab la Coast Modern 'Watafiti wa Mipasho' limefanikiwa kuwapata wasanii watatu wapya chipukizi wanaiotarajia kuwatambulisha na kazi zao mpya wanazotarajia kuzirekodi hivi karibuni.
Chipukizi hao walionyakuliwa na kundi hilo linaliotamba kwa sasa na wimbo wa 'Katiba Mpya' ni Mwajuma Othman, Aisha Abdallah na Dualla Ally ambao wameanza mazoezi ya nyimbo zao kabla ya wiki mbili zijazo kuingia studio kuzirekodi.
Mkurugenzi wa kundi hilo, Omar Tego 'Special One' aliiambia MICHARAZO kuwa, wasanii hao wapya wana vipaji vikubwa vya kuimba na kuwatabiria kuja kufunika mbeleni mara baada ya kazi zao wanazoziandaa kurekodi kuanza kurushwa hewani.
Tego alisema tayari kila msanii ameshatungiwa wimbo wake na kuufanyia mazoezi kwa sasa na wataingia kuzirekodi kabla ya kuachiwa hewani wakati akijipanga kutengeneza video zake.
"Tuna vijana watatu wakali achaa...wawili wa kike na mmoja wa kiume na kwa sasa wapo katika mazoezi makali ya nyimbo zao kabla ya kuingia studio kuzirekodi," alisema Tego.
Kundi hilo limejipatia umaarufu mkubwa katika miondoko ya taarab kutokana na nyimbo kadhaa kama 'I'm Crazy for U', 'Kupenda Isiwe Tabu', Chongeni Fenicha', Mwanamke Kujiamini', 'Damu Nzito', 'Gubu la Mume' na nyingine.

Ribery hatimaye atundika daluga, kisa...!

http://www.soccerroomtoday.com/wp-content/uploads/2012/06/franck-ribery-p12.jpg
KIUNGO Mshambuliaji wa Ufaransa, Franck Ribery ametangaza rasmi kustaafu mechi za kimataifa.
Ribery (31), anayeitumikia Klabu ya Bayern Munich amekuwa mchezaji bora wa mwaka mara tatu nchini Ufaransa huku akiichezea timu ya taifa mechi 81 na kufunga mabao 16.
"Ninataka kujikita zaidi katika kuiangalia familia yangu na kuitumikia vema Bayern Munich na kutoa njia timu ya taifa kwa wachezaji wengi makinda," Ribery ambaye ameichezea Ufaransa katika fainali za Kombe la Dunia za 2006 na 2010 aliliambia Jarida la Ujerumani la Kicker.
Ribery ambaye alizikosa fainali za Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil kutokana na kuwa majeruhi, amekuwa mmoja wa nyota wenye vipaji tangu ametua Bayern kwa dau la paundi milioni 20 akitokea Marseille mwaka 2007, ametwaa ubingwa wa Bundesliga mara nne na mara moja Kombe la Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Kadhalika Ribery alishika namba tatu katika kinyang'anyiro cha tuzo ya Mchezaji Bora wa Dunia wa Mwaka 2013 (Fifa Ballon d'Or 2013), akimaliza nyuma ya Lionel Messi na mshindi Cristiano Ronaldo.
Uamuzi huo unamaana Ribery hatajumuishwa katika kikosi kitakachoshiriki michuano ya Euro 2016, ambayo itafanyika Ufaransa.

Ronaldo, Manuel Neuer kuwania tuzo Mchezaji Bora Ulaya

KWA muda wa miaka minne mfululizo Cristiano Ronaldo amekuwa katika orodha ya mwisho ya wachezaji bora wa UEFA ambao wamekuwa wakiwania tuzo ya Ulaya na mara hii pia yumo katika orodha hiyo akiwa pamoja na Arjen Robben na Manuel Neuer.

Mshambuliaji huyo wa Madrid Ronaldo atakuwa akitegemea kutwaa tuzo hiyo kwa mara ya kwanza baada ya kuingia katika kinyang'anyiro hicho tangu kuanza kuteuliwa mwaka 2011 lakini akishindwa kutwaa tuzo hiyo katika kila igizo.

Mshindi huyo wa Ballon D'Or alikuwa na msimu mzuri uliopita akishinda tuzo ya Copa del Rey pamoja na taji la 10 kwa Madrid la michuano ya European Cup - La Decima.

Cristiano Ronaldo akifunga goli la rekodi la 17 katika michuano ya vilabu bingwa Ulaya
Strike: Robben won the league and cup double for Bayern Munich and scored three World Cup goals for Holland
Robben alishinda mataji mawili ya ligi na kikapu kwa Bayern Munich na alifunga na aliifungia magoli matatu Uholanzi katika kombe la dunia
Glory: Manuel Neuer (centre) won the league and cup double with Bayern and the World Cup with Germany
Furaha: Manuel Neuer (katikati) alishinda Ligi na vikapu mara mbili akiwa na Bayern na kombe la dunia 
Saba waliokwama kutinga hatua ya mwisho




4) Thomas Muller (Germany, Bayern Munich) - 39 points 
5)Philipp Lahm (Germany, Bayern Munich) - 24 points
=) Lionel Messi (Argentina, Barcelona) - 24 points
7) James Rodriguez (Colombia, AS Monaco, now at Real Madrid) - 16 points 
8) Luis Suarez (Uruguay, Liverpool, now at Barcelona) - 13 points
9) Angel Di Maria (Argentina, Real Madrid) - 12 points
10) Diego Costa (Spain, Atletico Madrid, now at Chelsea) - 8 points

EBOLA YALETA KIZAAZAA CAF YAZUIA MECHI AFRIKA

http://tv360nigeria.com/wp-content/uploads/2014/03/Ebola-virus1.jpg.pagespeed.ic_.b7XBqLSN9I1.jpg 
SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limezuia mechi zake kuchezwa Guinea, Liberia na Sierra Leone kutokana na kuripotiwa kuwepo kwa wagonjwa wengi wa Ebola katika nchi hizo.
Ikiwa ni njia mojawapo ya kuzuia kusambaa kwa virusi vya ugonjwa huo kupitia mkusanyiko wa watu, CAF imevitaka vyama vya mpira wa miguu vya nchi hizo kuchagua viwanja vingine huru kwa ajili ya timu zao zinazoshiriki michuano yake kwa kipindi hiki hadi katikati ya mwezi ujao.

CAF itafanya tathmini nyingine kuhusiana na ugonjwa huo kuanzia katikati ya Septemba ili kuona kama nchi hizo zinaweza kupokea timu ngeni kwa ajili ya mechi mbalimbali za michuano yake, na baadaye kufanya uamuzi wa kuruhusu au kuendelea kusimamisha.

Pia kutokana na mapendekezo ya Shirika la Afya Duniani (WHO), CAF imesema kwa nchi zenye virusi vya Ebola ni muhimu kwa vyama vyake vya mpira wa miguu kuufanyia vipimo vya afya msafara wa timu zao ili kuhakikisha wenye virusi vya ugonjwa huo hawasafiri.

DENI LAIPONZA TFF, MADALALI WALISHIKILIA BASI LA STARS

BASI la Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limekamatwa na madalali kwa amri ya mahakama kutokana na deni la sh milioni 140 ambalo tunadaiwa hadi litakapolipwa.

Amri hiyo imetokana na deni hilo la kampuni ya Punchline ya Kenya iliyokuwa ikichapa tiketi za kuingilia uwanjani kuanzia mwaka 2007. Hadi sasa tumeshalipa sh. milioni 70 katika deni hilo.

Jitihada zinafanyika ili kumaliza deni hilo. Pia tunachunguza mwenendo mzima uliosababisha kuwepo deni hilo.

YANGA YAIPIGA BAO SIMBA, YAMNASA BEKI WA JKT RUVU

Guu la kushoto; Yanga SC imeizidi kete Simba SC katika saini ya Edward Charles
YANGA SC imefanikiwa kumpata beki chipukizi wa JKT Ruvu, Edward Charles baada ya kukamilisha taratibu zote za usajili wake kutoka timu hiyo ya Jeshi la Kujenga Taifa na kumsainisha Mkataba wa miaka mitatu.
Yanga SC kwa miezi miwili sasa imekuwa ikisotea saini ya mchezaji huyo kwa kuanzia kufuata taratibu za kuvunja mkataba wake jeshini- hadi leo ilipokamilisha. Viongozi wa Yanga SC wakiongozwa na Francis Kifukwe leo walikuwa na kikao cha mwisho na uongozi wa JKT juu ya suala la uhamisho wa mchezaji huyo na mambo yamekwenda vizuri. Beki huyo alikuwa pia anawaniwa na mahasimu Simba SC, ambao jitihada zao ziligonga ukuta mapema, baada ya kuambiwa wapinzani wao Yanga SC, wamepiga hatua kubwa katika kufukuzuia huduma za chipukizi huyo. Edward sasa atajiunga na Yanga SC mara moja chini ya kocha Mbrazil, Marcio Maximo kuanza maandalizi ya msimu mpya. Ni Maximo aliyewasukuma viongozi wa Yanga SC kufukuzia haraka saini ya mchezaji huyo baada ya kutovutiwa na uchezaji wa beki wa sasa wa kushoto wa klabu hiyo, Oscar Joshua.  Edward Charles ni kati ya chipukizi waliopo timu ya taifa ya wakubwa kwa sasa, Taifa Stars chini ya kocha Mholanzi, Mart Nooij ambao wanainukia vizuri.   Ni mkabaji mzuri, ana nguvu, kasi- mbinu za anapokuwa na mpira na asipokuwa nao na pia hupanda vizuri kushambulia na kurudi kwa haraka. Anasifika kwa kupiga krosi nzuri pamoja na mpira iliyokufa.
BIN ZUBEIRY

Suarez apeta, apungiziwa adhabu na CAS

http://i.smimg.net/13/39/luis-suarez-liverpool.jpgHATIMAYE Mahakama ya Soka ya Kimataifa CAS, imekubali kupunguza adhabu ya kumfungia miezi minne Luis Suarez wa Barcelona baada ya kumuuma Giorgio Chiellini wa Italia wakati wa Kombe la Dunia.
CAS imetoa nafuu kwa Suarez na sasa Barcelona itamtambulisha rasmi Jumatatu na atapewa ruksa ya kufanya mazoezi na wenzake.
Mambo ambayo yamepunguzwa na yale yanayobaki kuwa adhabu ni kama yafuatayo.
Suarez ruhusa:
- Kufanya mazoezi na Barcelona.
- Kutambulishwa na Barcelona.
- Kucheza mechi za kirafiki, si zile za mashindano.
- Kucheza mechi za kirafiki za Uruguay dhidi ya Japan, Korea na Saudi Arabia katika miezi ya Septemba na Oktoba
- Kuhudhuria mechi uwanjani. 
- Kuhudhuria shughuli za matangazo zinazoihusisha Barcelona.
Suarez si ruhusa:
- Kucheza mechi yoyote ya mashindano akiwa na Barca hadi Oktoba 26.
- Kuichezea Uruguay mechi yoyote hadi zifikie mechi nane.

MAMIA WAMZIKA MAMA TUNDA WA AFANDE SELE

 Professor akiwa na Afande Sele Morogoro
 Professor Jay amesafiri hadi mkoani Morogoro kwenda kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa mke wa msanii mwenzake Afande Sele.
Kupitia Instagram, Professor ameshare picha akiwa kwenye mazishi na kuandika: Msibani Morogoro nyumbani kwao marehemu Asha au mama Tunda sasa hivi… tunajiandaa kwenda kumpumzisha kwenye nyumba yake ya milele saa kumi jioni ya leo, bwana alitoa bwana ametwaa, jina la bwana lihimidiwe….Amen
Jeneza la marehemu likiwa nje pamoja na watu mbalimbali waliojitokeza katika mazishi hayo
Awali Afande Sele alisema kifo cha Mama Tunda kimetokana na uzembe wa madaktari. Mama Tunda alifariki baada ya kulazwa kutokana na kuugua Malaria. Akizungumza na Bongo5 leo, Afande alidai kuwa bila uzembe wa madaktari huenda malaria isingechukua uhai wa Mama Tunda.

Afande Sele akilia kwa uchungu
“Mama Tunda ametuachia pengo kubwa sana kwenye familia,” alisema Afande. 
 “Amefariki jana saa tano usiku katika hospitali kubwa hapa Morogoro kutokana na uzembe wa madaktari. Walimpa matibabu akarudi nyumbani, sitaki kulizungumzia kiundani kwa sasa hivi kwa sababu tupo kwenye wakati mgumu. 
Huku mazishi yatafanyika kuanzia kama saa tisa hivi lakini bado hatutajua itakuwa wapi bado tupo kwenye mipango. Malaria ilimchukua sana, kwa familia na watoto kwetu ni msiba mkubwa sana, yaani ni huzuni sana,” aliongeza.
MAMIA ya wakazi wa mkoa wa Morogoro na wasanii wa fani mbalimbali jana walijitokeza katika mazishi ya mke wa nyota wa muziki wa kizazi kipya Seleman Msindi 'Afande Sele' yaliyofanyika katika makaburi ya Kola katika Manispaa ya Morogoro.
Mke wa Afande Sele, Asha Shengo maarufu kama Mama Tunda alifariki usiku wa kuamkia Alhamisi majira ya saa 5.45 katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Morogoro alikokuwa akitibwa baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa malaria iliyomuanza siku ya Jumatatu.
Akizungumza kabla ya mazishi hayo, mmoja wa ndugu wa marehemu, Ally Bushiri alisema Mama Tunda alianza kujisikia vibaya siku ya Jumatatu na kwenda kupimwa na kubainika alikuwa na malaria nne.
Alisema kuwa baadaye Mama Tunda alipatiwa matibabu na siku ya Jumanne hali yake haikuwa nzuri na kupelekwa katika hospitali ya Mtakatifu Mary iliyopo eneo la la kata ya Mafiga na ilipofika Jumatano asubuhi hali yake iliimarika na kuruhusiwa kurudi nyumbani.
Bushiri alisema kuwa siku ya Jumatano jioni hali ya Mama Tunda ilibadilika na hivyo ndugu waliamua kumpeleka katika hospitali ya Mkoa wa Morogoro ambako alianzishiwa matibabu na wakati akiendelea na matibabu ghafla ilipofika majira ya saa 5.45 hali ilibadilika na kufariki dunia.
Akizungumza kwa uchungu, msanii Afande Sele alisema kuwa marehemu Mama Tunda amemuachia pengo kubwa hasa watoto wake wawili Tunda pamoja na Asante, mwenye umri wa miaka mitatu .
Afande Sele ambaye muda wote alionekana kububujikwa na machozi alisema kuwa mpaka sasa anashindwa kuamini kama mzazi mwenzake huyo ametangulia mbele za haki kwakuwa ndiyo alikuwa mmoja wa washauri wa karibu katika mambo yake ya muziki.
Mmoja wa marafiki wa karibu wa Afande Sele, Nickson Mkilanya akimuelezea marehemu Mama Tunda alisema kuwa alikuwa ni miongoni mwa wanawake shupavu, mvulivu na mwenye kupenda ushirikiano katika kila jambo.
Mungu alaze roho ya marehemu Mama Tunda mahali pema poponi Amina.
 

KUMEKUCHA TAMASHA MIAKA 16 YA HOME GYM

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEglDi10hCTdPFV9XxEqn-1KSWZYuF_sACGfpP12l93qXdf8kdG-xuil-cmSIFlYKe09y6W2DnhzXOcRrsDtyv4EDe4H6FFqQ25J9cHiQ-OX2OzBUxnUpD90byP0kV5t7JkIIYvK5exbhCo/s1600/HPIM1779.jpgKLABU 12 za timu za soka za maveterani zinazooundwa na nyota wa zamani nchini zinatarajiwa kuchuana katika michezo maalum ya Tamasha la Miaka 16 ya Home Gym, itakayofanyika Septemba 6 kwenye uwanja wa Mwenge, Dar es Salaam.
Aidha zaidi ya klabu 30 za Jogging nazo zinatarajiwa kupamba tamasha hilo ambalo litahusisha pia michezo mbalimbali ikiwamo ya netiboli, kuvuta kamba, kukimbia kwenye magunia na kukimbiza kuku.
Kwa mujibu wa mratibu wa tamasha hilo, Andrew Mangomango, klabu za maveterani zilizothibitisha kushiriki tamasha hilo ambalo litapambwa na burudani ya muziki na shoo ya watunisha misuli, wanyanyua vitu vizito, ngumi na karateka ni Mbagala Veterani, Boko, 501, Break Point, Survey, Mwenge na Msasani.
Mangomango alizitaja nyingine kuwa ni Biafra Veterani, Meeda, Mikocheni, Mbezi, Mabenzi, Segerea na Ukonga Veterani ambazo zinaundwa na nyota wa zamani wa kandanda waliowahi kutamba na timu za Simba, Yanga na Taifa Stars.
Juu ya klabu za Jogging mratibu huyo alizitaja kuwa ni pamoja na Temeke Jogging, Mwananyamala, Kingungi, Amani, Magenge, Makuka, 501, Ndiyo Sisi, Wastaarab, Makutanom, Pasada, FBI, Kongowe, Oysterbay Police, Zakheem, Kwa Nyoka, Kawe Beach, Satoji, Kawe Mkwamani na nyingine.
Mangomango aliongeza kuwa baada ya michezo yote wanamichezo washiriki watajumuika pamoja kuwatembelea yatima wanaolelewa kituo cha Chakuhama kwa ajili ya kuwapeleka misaada mbalimbali.
"Ni tamasha ambalo litaambatana na michezo mbalimbali kama ya kuvuta kamba, kukimbiza kuku, kukimbia kwenye magunia, na shoo za watunisha misuli, wanamieleka, mabondia na karateka kisha kwenda kutembelea yatima," alisema.
Mangomango alisema mgeni rasmi wa shughuli zote hizo anatarajiwa kuwa Mkuu wa Kikosi cha Jeshi cha 501, J.B Kapumbe.
Hii ni mara ya pili kwa tamasha hilo kufanyika mwaja jana lilifanyika wakati Home Gym ikiadhimisha miaka 15 tangu kuasisiwa kwake ambapo shughuli zake kuu ni kufanyisha mazoezi na kutoa ushauri juu ya afya ya mwili.