STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, May 27, 2013

Coastal Union kusajili kimyakimya


baadhi ya viongozi wa Coastal Union

WAKATI klabu za Simba na Yanga zikipigana vikumbo na kutambiana kwenye vcyombo vya habari juu ya wachezaji inayowanasa kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, uongozi wa Coastal Union ya Tanga umesema utafanya usajili wao kimyakimya bila makeke kama vigogo hivyo vya soka nchini.
Coastal iliyorejea kwenye Ligi Kuu msimu wa 2011-2012, imesema kitu cha muhimu na watakachozingatia ni kusajili kwa umakini mkubwa na kwa kiwango cha kimataifa, ili kuiwezesha timu yao kufanya vyema kwa ligi ijayo sambamba na kutimiza malengo waliyojiweka mabyo msimu huu wameshindwa kuyafikia.
Mkurugenzi wa Ufundi wa klabu hiyo, Nassor Binslum, aliiambia MICHARAZO kuwa, hawatafanya usajili wa mbwembwe na makeke badala yake ifanya mambo yao kimyakimya bila kuwashtua watu hadi mwishoni watakapokianika kikosi chao.
Binslum, alisema watakachozingatia ni kusajili wachezaji watakaoiwezesha Coastal ifanye vyema katika ligi hiyo tofauti na msimu huu waliomaliza wakiwa kwenye Sita Bora, kinyume na msimu uliopita walipomaliza nafasi ya Tano.
"Coastal Union hatuna mbwembwe tutafanya usajili wetu kimyakimya na kwa umakini mkubwa ili msimu ujao tutishe na tutakitangaza kikosi mara baada ya mambo yote kukamilika," alisema Binslum.
Mabingwa hao wa zamani wa soka nchini, walimaliza katika nafasi ya sita kwa kujikusanyia pointi 35 kutokana na michezo 26 iliyocheza na ilimaliza msimu vibaya kwa kupewa kichapo cha mabao 2-0 na Polisi Morogoro.

Mtoto wa miaka 7 anusurika kuchomwa moto, kisa...!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiRYGNK4P0cFIyKRqOFynOrQq3EIcCP4FHCqYF9HopGj2yWE0li5U95QShB5g6C5tyfVNd6rQZix8eewbtSTxRe5-c3My82W5tXZIy2_4U5Ugq8tTUcyyGuAgGc9nDbHRECNaAQ2qXPtLU/s1600/Waalimu.JPG
Mwenyekiti wa Mtaa wa Kimara King'ongo, Bw Mapesi (kushoto) anayedaiwa kumuokoa mtoto na kijana aliyetaka kumchoma moto mtoto huyo kwa tuhuma za kuiba viatu.


VITENDO vya watoto wadogo kufanyiwa vitendo vya kikatili vinazidi kushamiri katika jamii ambapo hivi karibuni mtoto mmoja wa miaka saba anayesoma Shule ya Msingi iliyopo Kimara King'ongo kata ya Saranga alinusurika kuuwawa kwa kuchomwa moto na kijana mmoja mshona viatu akimtuhumu mwizi.
Tukio hilo ambalo MICHARAZO imedokezwa lilitokea wiki mbili zilizopita majira ya mchana katika eneo la Kwa Komba, Kimara King'ongo baada ya mshona viatu huyo anayefahamika kwa jina na Ngosha kumpiga na kisha kumwagia dumu zima la mafuta ya taaa mtoto huyo kisha kumburuta hadi dukani ili anunue kiberiti cha kumwashia moto kabla ya wasamaria wema kuingilia kati na kumgeuzia kibao kijana huyo.
Inaelezwa mtoto huyo (jina linahifadhiwa) siku moja kabla alienda kwa fundi huyo na kuviona viatu ambavyo alimuomba ampe akamuonyeshe baba yake ili aweze kumununu kutokana na kuvipenda na Ngosha alimpa bila hiyana akimtaka arejeshe mara baada ya kumaliza haja zake kwa baba yake.
Hata hivyo mmoja wa mashahuda wa tukio hilo alidai mara baada ya mtoto huyo kwenda na viatu hivyo kwa wazazi wake na kueleza shida na mahali alipovipata, baba yake alimchapa fimboa kimtaja kuvirejesha mahali alipovipata akiamini huenda kijana wake aliviiba.
Kwa kuwa ilishafika usiku, mtoto alilala na viatu na kesho aliamua kuvirejesha kwa Ngosha na kumueleza baba yake alimchapa akidhani ameviiba na ghafla kijana huyo (pengine kwa bhangi, anazoelezwa anavuta katika eneo lake la kazi) alimbadilikia kijana huyo na kuanza kumchapa makofi akidaia anawatafuta watoto wengi kama mtoto huyo.
Mtoto huyo aliamua kupiga kelele akijitetea yeye siyo mwizi, lakini Ngosha kama asiyemjua alimpiga tani yake kisha kuchukua dumu la mafuta ya taa alililokuwa nalo katika eneo lake la kazi na kumwagia kijana huyo mdogo bila huruma kisha kujisachi na kukuta hana kiberiti na kumburuta hadi kwenye duka lililokuwa jirani na eneo hilo la kituo cha mabasi cha Kwa Komba.
Hata hivyo baadhi ya waendesha pikipiki waliokuwa katika eneo hilo walioshuhudia tukio hilo na wasamaria wema wengine waliamua kuingilia kati na kumhoji Ngosha kwa nini anampiga mtoto na kutaka kumtenda alichokuwa amekusudia na bila aibu alisema anataka kumwasha mtoto mtoto huyo kwani mwizi.
Ndipo wasamaria wema na waendesha pikipiki hao waliamua kumgeuzia kibao kwa kumpiga kijana huyo kabla ya kuja kuokolewa na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa huyo aliyekuwa amembatana na Polisi na kuondoka na kijana huyo na mtoto aliyekuwa anachuruzika mafuta hadi kituo cha Kidogo cha Polisi cha Kimara.
"Huyo jamaa ni kama aliyechanganyikiwa, alimpa mwenyewe mtoto viatu kisha akamgeuzia kibao baada ya kusikia simulizi lake toka kwa wazazi wake, na kumwagia mafuta yaani kama tusingekuwepo mtoto wa watu angeteketea kibaya wazazi wake wote hakuwepo nyumbani," alisema dereva mmoja wa pikipiki Ally aliyeshuhudia tukio hilo mwanzo mwisho.
Ally alimwagia sifa Mwenyekiti huyo wa serikali ya Mitaa aliyemtaja kwa jina la Demetrius Mapesi, ambaye mbali na kumnusuru mtoto, lakini pia alisaidia Ngosha kufikishwa Polisi kwa usalama bila kudhurika kwani wananchi walutaka wamuunguze yeye wakidai wamemchoka kwa mambo yake yasiyoendana na ustaarabu.
"Kama siyo Mapesi, Ngosha angeiva yeye," alisema Ally.
 MICHARAZO ilimpigia simu mwenyekiti huyo baada ya kupewa namba na dereva huyo, ambapo Mwenyekiti huyo alikiri kutokea kwa tukio hilo na kueleza liliishia Polisi Kimara ambapo mtuhumiwa huyo alifikishwa kwa ajili ya taratibu za kushtakiwa kwa kosa alilotaka kulifanya kwa mtoto huyo mdogo.
"Ni kweli tukio hilo lilitokea wiki mbili zilizopita na tulishamfikisha Ngosha mikononi mwa Polisi kwa taratibu za kufikishwa mahakamani, Ila ilitushtusha mno kijana mzima kaka yeye kumwagia mtoto mafuta ya taa na kutaka kumwasha moto kwa sababu ya viatu ambavyo inadaiwa alimpa mwenyewe," alisema Mapesi.
sikijana mmoja ambaye ni mshona viatu, maarufu kwa jina la Ngosha alikaribia kumlipua kwa moto mwanafunzi wa darasa la kwanza (jina kapuni) akimtuhumu alimuibia viatu.

Vyama vya ngumi vya TPBO, TPBC vyalumbana

http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2012/09/OnesmoNgowi.jpg
Rais wa TPBC, Onesmo Ngowi


http://www.ippmedia.com/media/picture/large/tpboyassinpresidaaa.jpg
Rais wa TPBO, Yasin Abdallah 'Ustaadh'



MASHIRIKISHO ya ngumi za kulipwa nchini yenye heshima kubwa katika mchezo huo, TPBO na TPBC vimeingia kwenye malumbano kila kimoja kikishutumu na kuanika udhaifu wa wenzake kisa ikiwa ni mahojiano aliyoyafanya bondia nyota wa zamani George 'Lister' Sabuni na gazeti moja la kila siku.
Katika habari hiyo Sabuni alinukuliwa akiliponda Oganaiziesheni ya Ngumi za Kulipwa, TPBO kwamba inawakimbiza mapromota kutokana na kuendeshwa kibabaishaji na kuwataka mabondia wapitia Kamisheni ya Ngumi Tanzania, TPBC analofanya nayo kazi.
Hata hivyo kauli hizo zilimfanya Rais wa TPBO, Yasin Abdallah 'Ustaadh' kuwaka na kuanika madudu ya uongozi wa TPBC, ikiwamo kuwakata mabondia asilimia 10 ya fedha kwa safari zao za nje ya nchi badala ya asilimia 1 na mengine ambayo yalijibiwa na Rais wa TPBC, Onesmop Ngowi.
Ngowi alifafanua taarifa kwamba wao TPBC ndiyo waliosababisha promota maarufu nchini wa zamani wa ngumi, DJB Promoters chini ya Jamal na Dioniz Malinzi kuachana na mabondia Rashid Matumla na Mbwana Matumla akidai mabondia hao waliandika wenye barua baada ya kuhamia kwa Kajumulo na Don King Promotions na siyo kweli kama kamisheni yao inahusika.
Kifupi ni kwamba malumbano hayo kwa wadau wa ngumi hayawasaidii na muhimu viongozi hao ambao kwa siku za karibuni walikuwa wakifanya kazi kwa pamoja kukaa chini na kumaliza tofauti zao kwa manufaa ya mchezo huo.
Huu ni mtazamo wa MICHARAZO kama mdau wa michezo nchini.

Ajali tena: Treni yaua mtu Ukonga




Muda mfupi uliopita treni imegongana na gari aina ya RAV4 na dereva (mwanaume)amekufa muda huu na abiria(mwanamke) yu mahututi.