STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 30, 2012

More 120,000 US Dollars from UAE Embassy for iftar and Zakatul fitr in Tanzania

The Embassy of the United Arab Emirates(UAE)in the country through Sheikh Khalifa bin Zayed Al Hahyan, Sharjah Charity Internation and Red Cresent organizations will use more $120,000 to provide Itfal and Zakatul Fitr to seven regions of the country during this holly months of Ramadan. Speaking in Dar es Salaam on behalf of UEA ambassador in the country H.E Ambassador Mallalla Mubarak Al Ameir and his second secretary, Mohammed Obaid Salem AlZaabi,the embassy accountant Abdallah Ahmedina said the money will benefit seven regions of the country, he named the regions as Dar es Salaam, Iringa, Kilimanjaro, Arusha, Pwani, Dodoma and Morogoro . Ahmedina was speaking this when he donated Iftal at Al Makbool Mosque in Msasani, Dar es Salaam. He explained that his embassy gave the money to the mentioned regions and that the remaining money will be given to, widows, orphans , disabled and other less privileged people during Zakatul Fitr cerebrations. Ahmedina said this is not the first time for his embassy to provide Iftal and Zakatul Fitr and promised that his embassy is committed to continue providing Iftal and Zakatul Fitr to all Muslims in the country during the period of Ramadan . "Its our tradition to give people Iftal and also zakatufitr,and this year we will use $122,000 for that purpose , this money has come from organizations which are Sheikh Khalifa ($80,000), Red Cresent ($36,000)and Sharjah Charity (6,000),"he said On his speech , Al Makbool mosque clergy, Sheikh Mussa Abdallah,thanked the embassy for the donation which he said will help fasting Muslims during this holly months of Ramadan. "There are some muslims who are fasting but do not have food for iftal , we thanked the Embassy of United Arab Emirates (UAE)and the other three organizations for the donation which we strong believe will help many Muslims” he said

UAE's Embassy gave iftar to Moslims in Dar

Al Rahman Mosque Sheikh, Abdullah Salim Bahssany has asked companies , organizations and individuals to provide free Iftal to Muslims during fast breaking time in this months of Ramadan. The sheikh said there are some Muslims who are lacking iftal and its good to help them with food, he was speaking this on Saturday in Dar es Salaam when the Embassy of the United Arab Emirate (UEA)in the country through Khalifa Bin Zaayid Al Nahyaan group gave iftal to Muslims during fast breaking at his mosque. The embassy and the group will provide the food to members of Al Rahman Mosque and other surrounding areas the whole months of Ramadan. He thanked the Embassy and the group for the iftal and he asked other people to emulate the gesture shown by the embassy and the group . “Am asking all Muslims in Kinondoni District who are observing the holly months of Ramadan but are not sure of getting the iftal to come here for the food and also prayers , we are very happy and thank the Embassy of United Arab Emirates(UAE) is giving us the iftal, am asking others to emirate this welcome gesture” he said Some members of the mosque thanked the embassy for the iftal saying it will ease some of the problems which they face to get the iftal at selling points. “This is good as it helps us to get the iftal within the mosque premises , buying this at some selling points is very tiresome as there are queues and also some people may lack money to buy Iftal ” said one member of the church who identified himself as Mustafa Ali .

Kipemba sasa vitani na Waanchari, Warenchoka

MUIGIZAJ
MUIGIZAJI mkongwe nchini, Issa Kipemba anajipanga kufyatua filamu mpya inaozungumzia uhasama wa makabila mawili makuu ya mkoani Mara ya Warenchoka na Waanchari. Nyota huyo wiki iliyopita alikuwa mkoani humo kuonana na 'machifu' wa koo hizo ili kujua chanzo vita vyao na pia kupata baraka za kuicheza filamu hiyo. Akizungumza na NIPASHE juzi siku moja baada ya kurejea toka safarini, Kipemba aliyewahi kutamba na Kaole Sanaa, alisema safari yake ilikuwa na mafanikio tofauti na alivyofikiri. Kipemba alisema amejifunza mengi katika safari yake hiyo na kwa sasa anajipanga ili kufyatua filamu hiyo itakayokuja baada ya kazi yake ya 'Injinia' kuingiza sokoni. Alisema hajajua filamu hiyo itawashirikisha wasanii wapi kutokana na ukweli inahitaji umakini wa hali ya juu kama alivyofanya katika kazi yake ambayo inakaribia kutoka hewani ya 'Injinia'. "Unajua sitaki kulipua kazi, nataka kuonyesha mfano kwa wadau wengine wa filamu, kwamba kazi hii si ya kulipuliwa kwa nia ya kujipatia fedha tu," alisema.

Machejo wa ITV ana Ngekewa

MSANII nyota wa maigizo aliyepo kundi la Jakaya Theatre linaloonyesha michezo yake kupitia kutuo cha ITV, Halid Chihame maarufu kama 'Alex Machejo' au 'Mzee wa Rivasi', amefyatua wimbo mpya uitwao 'Ngekewa' ikiwa ni maandalizi yake ya kupakua albamu kamili. Akizungumza na MICHARAZO, Machejo, alisema wimbo huo ameurekodia katika studio za Kili Records chini ya mtayarishaji wake mahiri, C9 na tayari ameshakisambaza kwenye vituo vya redio na kuanza kuchezwa hewani. Machejo alisema kibao hicho amekiimba peke yake na kipo katika miondoko aliyoipa jina la 'Flava Champlin', huku akiwa tayari ameshakamilisha nyimbo nyingine tano kwa ajili ya kuzirekodi kuwapa burudani mashabiki wake. "Kaka nimeanza kusambaza kibao changu kipya kiitwacho 'Ngekewa' wakati huo huo nikiwa na nyimbo nyimbo tano zilizokamilika ambazo natarajia kuzifyatua wakati wowote kuanza wiki ijayo," alisema. Alizitaja nyimbo hizo nyingine zitakazofuatia baada ya 'Ngekewa' ni 'Wa Kwalu', 'Mtoto kwa Mama Hakui', 'Tanzania', 'Nasubiri' na Kimanzichana'. Msanii huyo aliyetamba na michezo kama 'Kovu la Siri', 'Kivuli', 'Utelezi', 'Riziki' na 'Bakora', alisema mipango yake ni kufyatua albamu kamili hapo baadae, ingawa alisema itategemeana na maamuzi ya menejimenti inayomsimamia kazi zake.

Simba, Yanga zatishia Super8

USHIRIKI wa Simba na Yanga katika michuano mipya inayotarajiwa kujumuisha timu nane za Tanzania Bara na Visiwaniinayokwenda kwa jina la "BancABC Super 8" uko katika hatikati kutokana na timu hizo kutoiweka ligi hiyo kwenye kalenda zao, imefahamika. Ligi hiyo inayofanana na Ligi ya Muungano inatarajiwa kufanyika kuanzia Agosti 4 hadi 18 mwaka huu chini ya udhamini wa benki ABC na itajumuisha timu nane. Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, alisema jana kwamba ligi hiyo ni nzuri kwa lengo la kuiandaa timu lakini klabu yake itakuwa radhi kushiriki endapo mgawanyo wa mapato ya mlangoni utabadilishwa na kuwa zaidi ya yale yanayopatikana kwenye mechi za Ligi Kuu ya Tanzania Bara. Rage alisema kwamba klabu zimechoka kunyonywa na hivyo Simba itakuwa tayari kushiriki endapo klabu zitapata mgao wa zaidi ya asilimia 60 ya mapato ya mlangoni. "Ni lazima kwanza tukae na kukubaliana tunapata nini sisi klabu, wakati wa kuona klabu zinanyonywa umepita na sasa kila mkataba ambao TFF watakuwa wameingia wanatakiwa kutushirikisha vilabu ili tujue maslahi yetu," alisema Rage. Katibu Mkuu wa Yanga, Mwesigwa Selestine aliliambia gazeti hili jana kwamba klabu yake inaona ligi hiyo imeingiliana na programu zao za maandalizi ya msimu ujao wa ligi kuu hivyo maamuzi ya kushiriki au kutoshiriki yatajulikana baada ya kufanyika kwa kikao cha pamoja na benchi la ufundi la timu hiyo. Mwesigwa alisema kwamba mara baada ya kocha mpya, Tom Saintfiet kutua, alipewa ratiba ya michuano iliyopo na hivyo kocha huyo aliandaa programu yake ambayo itaanza kutekelezwa hivi karibuni baada ya mapumziko ya wachezaji kumalizika. "Uwezekano wa timu yetu kushiriki ni mdogo, haikuwa kwenye programu na hivyo inabidi uongozi na benchi la ufundi tujadiliane na kufanya maamuzi yatakayoisaidia timu," alisema katibu huyo. Shirikisho la Soka Nchini (TFF) lilitangaza kusaini mkataba wa miaka mitatu na benki ABC ambayo itadhamini ligi hiyo mpya yenye lengo la kuziandaa klabu kwa ajili ya msimu mpya wa ligi. CHANZO:NIPASHE

Azam yakana kuchunguza kipigo cha Yanga

WAKATI taarifa zilizagaa jana kwamba Azam imewasimamisha wachezaji wake wawili Mrisho Ngassa na Salum Aboubakar 'Sure Boy' kwa tuhuma za kucheza chini ya kiwango dhidi ya Yanga katika fainali ya Kombe la Kagame waliyolala 2-0 Jumamosi na kwamba nyota wengine watatu Aggrey Morris, Said Morad na kipa Deogratius Munishi 'Dida' wanachunguzwa, uongozi wa klabu hiyo ya Chamazi umesema walifungwa kihalali na hakuna mchezaji wa wanayemtuhumu kwa chochote. Afisa Habari wa Azam FC, Jaffer Idd alisema Yanga walitumia makosa machache yaliyofanywa na mabeki wa Azam na kupachika mabao yaliyowapa ushindi wana Jangwani hao. "Timu yetu ilicheza vizuri kwenye mechi ya fainali lakini Yanga ilituzidi ujanja na kutumia vizuri nafasi chache walizopata," alisema Jaffer. Alisema hawawezi kumlaumu mchezaji yeyote kwa kipigo hicho kwa sababu wachezaji walioifikisha fainali timu hiyo ndio waliocheza mechi hiyo ya fainali na akawasifu wachezaji wa timu hiyo kwa ushujaa wa kuifikisha Azam fainali licha ya kwamba ilikuwa ikishiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza. Jaffer alisema uongozi wa Azam umeridhika na matokeo hayo na kwamba sasa wanaelekeza nguvu zao katika maandalizi ya Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho Afrika. Akizungumza na gazeti hili jana, Ngassa alisema kuwa timu yake juzi haikuwa na bahati ya kutwaa ubingwa huo lakini wanamshukuru Mungu kwa kufika fainali. Ngassa alisema kwa dakika chache alizopewa kucheza, zikiwemo za mechi ya fainali alijituma na kuisaidia timu yake. "Sidhani kama kuna aliyecheza chini ya kiwango, tumejituma na tumefika mbali licha ya kutochukua ubingwa," alisema Ngassa na kuongeza kwamba hajasimamishwa na uongozi wa timu yake kama ambavyo ilikuwa inazungumzwa jana. Ilidaiwa pia kwamba uongozi wa Azam haukufurahishwa na kitendo cha Ngassa kwenda upande wa mashabiki wa Yanga na kushangilia baada ya kufunga goli kwenye mechi ya nusu fainali ya Kombe la Kagame dhidi ya Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Wachezaji wa Azam wamepewa mapumziko ya siku mbili ambapo kesho wataanza mazoezi ya kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

Kidunda adundwa Olimpiki

BONDIA pekee wa Tanzania katika mashindano ya Olimpiki, Seleman Kidunda jana alipigwa kwa pointi 20-7 na bondia Vasilli Beraus toka Jamhuri ya Moldova.

Batungi: Mkali wa Kikapu achekeleaye ajira jeshini

LICHA ya mchezo wa kikapu kumpatia rafiki wengi na kufahamika ndani na nje ya nchi, nyota wa klabu ya ABC, Gilbert Batungi 'B10' amesema kitu kikubwa anachojivunia kupitia mchezo huo ni elimu na ajira aliyopata jeshini. Batungi, aliyeingia kwenye kikapu kwa ushawishi wa kaka yake aitwaye Jerome, alisema ajira hiyo aliipata mwaka 2006 kutokana na umahiri wake dimbani. Alisema anaifurahia ajira hiyo kwa vile hakuwahi kuiota kuja kuipata maishani mwake. Batungi, anayemudu nafasi ya kati, alisema pia kikapu kilimwezesha kupata nafasi ya kusoma Shule ya Sekondari Jitegemee baada ya kung'ara katika UMISSETA mwaka 2000 iliyofanyikwa jijini Mwanza. Alisema wakati akishiriki michuano hiyo alikuwa mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Binza, kwa jinsi alivyong'ara aliuvutia uongozi wa Jitegemee iliyomchukua akiwa kidato cha pili na kusoma hadi alipohitimu kidato cha nne. Alisema kutua kwake Jitegemee kulimwezesha kuonwa na kuitwa timu ya mkoa wa Dar tangu mwaka 2001 na ile ya taifa 2005 na kuzichezea mpaka sasa bila kutarajia. Juu ya pambano gumu alilowahi kukutana nalo, Batungi apendae kula ugali kwa dagaa na mboga za majani na kunywa juisi ya embe, alitaja mchezo wa mwaka 2005 kati ya Tanzania na Kenya wa kuwania ubingwa wa Afrika Mashariki. "Naikumbuka mechi hii kwa vile ilikuwa mara yangu ya kwanza kuichezea timu ya taifa, pia licha ya ugumu wake niliisaidia Tanzania kuilaza Kenya kwa mara ya kwanza." Alisema mchezo huo uliochezwa Nairobi na kuisha kwa Tanzania kuiduwaza Kenya kwa vikapu 61-60. "Hakika mafanikio niliyopata katika mechi hiyo hasa kuaminiwa na makocha na kutiwa moyo na wachezaji wenzangu, ni jambo linalonifanya nisiisahau," alisema. Batungi, aliyekuwa mmoja wa wawaniaji wa Tuzo za TASWA za 2012 kama Mchezaji Bora wa Kikapu kwa mara ya pili mfululizo, alisema safari yake ya michezo kwa kiasi kikubwa imechangiwa na makundi matatu ya watu asiowasahau milele. Alitaja kundi la kwanza ni wazazi wake waliomuunga mkono kwa kumtia moyo tangu utotoni, pili makocha wote waliomfundisha katika timu tofauti, na wachezaji wenzake waliomtia nguvu kwa kukitambua kipaji chake katika mchezo huo. "Nitakuwa mchoyo wa fadhila kama sintowashukuru watu hawa kwa hapa nilipofika," alisema. Batungi, aliyetwaa ubingwa wa Majiji akiwa na timu ya mkoa wa Dar 'The Dream Team', ubingwa wa Taifa wa Kikapu (NBL) na ule wa Muungano akiwa na klabu ABC ni mnazi mkubwa wa soka mchezo alioupenda kabla ya kaka yake kumbadilisha. Ni shabiki mkubwa wa klabu za Chelsea na Simba akivutiwa na kiungo Mwinyi Kazimoto na Didier Drogba. B10 Mkali huyo alitoboa siri ya jina lake la utani la 'B10', akisema ni kifupi cha ubini wake na jezi namba 10 anayopenda kuivaa tangu alipoibukia katika kikapu mwaka 1998. "Naipenda mno jezi namba 10, nimekuwa nikiivaa tangu naanza kucheza kikapu na ndio maana wengi huniita B10, ikimaanisha Batungi Namba 10," alisema Batungi, anayechizishwa na rangi nyekundu na nyeupe akimzimia nyota wa kikapu nchini Abdallah Ramadhani 'Dullah', alisema ndoto zake ni kuiona Tanzania ikitamba kimataifa na kuwasaidia vijana chipukizi kuja kuvaa 'viatu' vyao mara wakistaafu. Nyota huyo anayependa kucheza Pooltable, alisema mchezo wa kikapu umedidimia kwa kukosekana viongozi makini na wenye uchungu na mchezo huo. Alisema wengi wa viongozi wa sasa ni wababaishaji wanaojali masilahi yao na ndio waliochangia hata wadhamini kuukimbia mchezo huo na kutoa rai kwa wadau wenzake kubadilika kwa kuwachagua watu makini. "Tusipozinduka na kuchagua watu wenye mapenzi na uchungu na kikapu, tutarajie mchezo huo kudidimia zaidi," alisema. Alidai kama angekutana na Rais au Waziri wa Michezo, angeomba serikali isaidie michezo yote badala ya kuangalia soka tu, pia angeiomba ishinikize makampuni kuwekeza kwenye michezo kwa kusaidia udhamini. "Pia ningeiomba serikali iwekeze nguvu katika michezo ya vijana ili kusaidia taifa kuwa na nyota wa baadae kwa michezo yote ili itambe kimataifa," alisema. Batungi, ambaye hajaoa ila ana mtoto mmoja, alisema hakuna ujinga anaoujutia kama tabia aliyokuwa nayo enzi akiibuka katika kikapu ya kutega mazoezi magumu kwa kusingizia ugonjwa alipokuwa akisoma Jitegemee. Alisema kitu kinachomhuzunisha ni kifo cha nyota wa Netiboli, Grace Daudi 'Sister' na kudai kitu kimngine anachokifanya nje ya ajira yake jeshini ni biashara ya kuuza nguo. ALIPOTOKA Gilbert Paul Batungi, alizaliwa Januari 5, 1983 mkoani Shinyanga akiwa wa sita kati ya watoto saba wa familia yao. Alisoma Shule ya Msingi Binza ya Maswa-Shinyanga na kuendelea na masomo ya Serkondari Shule ya Binza na baadae Jitegemee. Kimichezo alianza kucheza soka na kutamba katika timu ya shule kabla ya kaka yake kumshawishi kucheza kikapu ambapo aliianza kuucheza rasmi mwaka 1998 katika klabu ya Black Wizard ya Shinyanga. Baada ya kung'ara katika UMISSETA mwaka 2000 iliyofanyika Mwanza na kuonwa na Jitegemee alihamia jijini Dar na kupata fursa ya kuzichezea timu za Mgulani JKT, Chang'ombe Boys na Vijana. Mwaka 2004 akiwa ameshamaliza masomo yake ya Sekondari, aliitwa JKT Mgulani kama mchezaji wa kiraia na miaka miwili baadae akapata fursa ya kuwa miongoni mwa walioajiriwa jeshini na kuhamia timu ya ABC anayoichezea mpaka sasa. Batungi, anayetamani kuwa na watoto wawili pale atakapooa, aliwakumbusha wachezaji wenzake kujibidiisha kufanya mazoezi na kuwa makini na ugonjwa wa Ukimwi aliodaai unapoteza nguvu kazi kubwa ya taaifa. Alisema rai hiyo ya kujikinga Ukimwi sio kwa wachezaji tu bali jamii kwa ujumla kwa kuitaka kuepuka ngono zembe, wawe waaminifu na kutumia kinga, huku akisisitiza kinga sahihi ni kufanya ibada na kufanya mazoezi ili kupunguza mihemko. Aliwasihi wachezaji wenzake kujituma uwanjani na kuwa na nidhamu ili kusaidia kushawishi wadhamini kuwasaidia.
Mwisho

Ubalozi wa UAE kutumia zaidi ya Dola 1200,000 kufuturisha mikoa saba nchini

UBALOZI wa Nchi za Falme za Kiarabu (UAE) nchini, kupitia taasisi za Sheikh Khalifa bin Zayed Al Hahyan, Sharjah Charity Internation na Red Cresent, unatarajia kutumia zaidi ya dola 120,000 za Marekani, kuifadhili mikoa saba nchini kwa ajili ya futari na Zakatul Fitr kipindi chote cha mfungo wa mwezi wa Ramadhani. Akizungumza kwa niaba ya Balozi wa UAE nchini Tanzania, Mallalla Mubarak Al Ameir na msaidizi wake, Mohammed Obaid Salem AlZaabi, baada ya kugawa futari katika msikiti wa Al Makbool, Msasani Dar es Salaam juzi, Mhasibu wa ubalozi huo, Abdallah Ahmedina, alisema baadhi ya msikiti ya mikoa hiyo ndiyo itakayonufaika. Ahmedina, aliitaja mikoa ambayo waumini wake tangu kuanza kwa mfungo wa mwezi wa ramadhani wamekuwa wakifuturishwa na watakuja kupewa Zaka kwa ajili ya Eid El Fitri ni Dar es Salaam, Iringa, Kilimanjaro, Arusha, Pwani, Dodoma na Morogoro. Mhasibu huyo alichangua kuwa kiasi cha dola 80,000 zinatoka asasi ya Khalifa, dola 36,000 kutoka Red Cresent na dola 6,000 zinatoka Sharjah na kusema utaratibu huo wa kusaidia waumini wa misikiti ya mikoa hiyo umeanza tangu ubalozi wao uwe nchini na utaendelea kwa lengo la kuwasaidia waumini kutekeleza ibada yao ya funga bila ya hofu ya kukosa futari au kuisherehea Eid. Alifafanua, kati ya fedha hizo zilizotolewa na asasi hizo tatu zinatumika kwa futari na zilizosalia ni kwa ajili ya kugawa Zakatul fitr ambayo huwalenga waumini wajane, yatima, walemavu, maskini na fukara ili kuisherekea sikukuu kwa furaha na amani. "Miaka yote huwa tunatoa futari na kugawa zakatufitr, mwaka huu tutatumia kama dola 122,000 za Marekani zinazotolewa na asasi zilizopo chini ya ubalozi wetu za Sheikh Khalifa, Red Cresent na Sharjah Charity," alisema. Akitoa shukrani kwa niaba ya waumini wake, Imamu wa msikiti wa Al Makbool, Sheikh Mussa Abdallah, aliushukuru ubalozi huo kwa kile walichosema umewasaidia kutimiza moja ya nguzo za dini yao. "Waumini wengine hawana uwezo wa kupata futari kama hii, tunashukuru ubalozi na asasi zote zilizochangia msaada huu na Inshallah, Mwenyenzi Mungu awazidishie," alisema Imamu Abdallah. Alisema baadhi ya watu waliokuwa hawafungi kwa kutokuwa na hakika ya kupata futari kwa sasa hawana sababu tena kwa vile wamepata uhakika wa kupitia ufadhili huo wa ubalozi wa UAE.