STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, November 3, 2014

Beki Azam chupuchupu kuuwawa na waendesha Bodaboda

http://www.fifa.com/mm/photo/tournament/competition/02/10/49/70/2104970_full-lnd.jpg
Erasto Nyoni (kushoto) akiitumikia Taifa Stars
BEKI wa Azam FC, Erasto Nyoni amekutwa na mkasa mkubwa baada ya kumgonga dereva bodaboda katika eneo la Tip Top Manzese lakini akaendelea kukimbia akiyagonga baadhi ya magari hadi katika eneo la Kijitonyama jijini Dar ambako alikwama baada ya kuligonga gari la Global Publishers.
Baada ya tukio hilo, Nyoni, beki wa Taifa Stars alitoka kwenye gari lake aina ya Toyota Grande Mark 11 GX 110, akaanza kujitahidi kukimbia kutokana na lundo la bodaboda kuanza kumfukuza wakitaka kuchukua sheria mkononi, hali iliyomtia hofu.
Walimfukuza hadi kufika eneo la Kijitonyama ambako alikwama baada ya kuligonga gari hilo la GPL na alipoteremka kwenye gari, wakaanza kumshambulia kama mwizi.
Nyoni alishambuliwa na lundo la madereva Bodaboda, lakini akafanikiwa kukimbia huku wakiendelea kumpiga na hata watu walipojitokeza kumsaidia, waliendelea kumpiga bila huruma.
Kwa mujibu wa walioshuhudia, Nyoni alishambuliwa kama mwizi katika eneo la tukio huku zaidi ya watu 30 wakimpiga. Beki huyo wa Azam FC alionekana kama anakimbilia kituo cha Polisi cha Kijitonyama Mabatini, lakini hakufanya hivyo na madereva hao wa Bodaboda walipomnasa walikuwa wakimshambulia kama mwizi naye alijaribu kujitetea na alipozidiwa, alitokomea kusikojulikana.
SALEH JEMBE

Newz Alert!Kocha wa Azam abwaga manyanga

http://api.ning.com/files/48iT*YTr0YPxYDj01AABZ-Y57HHUz7JiImtjHwmW0--mhgcMrli822GVzy*y9cV27GDkxgov6Sq8O5kkeg7xXw__/13.azam.jpg
Kally Ongalla aliyetangaza kuitema Azam
KOCHA Msaidizi wa Azam, Kally Ongalla ametangaza kubwaga manyanga kuendelea kuinoa timu hiyo.
Taarifa zilizopatikana mapema jioni ya leo zinasema Ongalla ameachana na Azam ikiwa imetoka kupokea kipigo cha pili mfululizo katika mechi za Ligi Kuu Tanzania Bara.
Inadokezwa kuwa kilichomfanya Ongalla mchezaji wa zamani wa Yanga kuachana na Azam imetokana na kutaka kwenda kuongeza taaluma yake ya ukocha nchini Uingereza.
"Kocha Msaidizi ameomba kujiuzulu kuifundisha timu ili aende Uingereza kuongeza ujuzi" chanzo cha habari kiliiambia MICHARAZO.

Mbeya City majanga, Mgambo JKT yatuma salam Jangwani


Mbeya City walipopigwa Mkwakwani jioni ya leo
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2014/05/273f8-63.jpg
Mgambo JKT iliyotuma salamu Jangwani
TIMU ya soka ya Mbeya City imeendelea kupata majanga baada ya jioni ya leo kutandikwa mabao 2-1 na Mgambo JKT katika pambano la kiporo cha Ligi Kuu Tanzania Bara lililokwama kuchezwa jana kwa sababu ya mvua kubwa iliyonyesha jijini Tanga.
Mbeya City ambayo ilikuwa inauguza kipigo toka kwa mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Azam ilijikuta ikienda mapumziko ikiwa nyuma kwa mabao 2-0. 
Mabao yaliyofungwa na Malimi Busungu kwa mkwaju wa Penati dakika ya 11 na Ally Nassor kuongeza la pili dakika ya 24 kabla ya Steven Mazanda kuwapa Mbeya bao la kufutia machozi dakika ya 76.
Ushindi huo imeifanya Mgambo kufikisha jumla ya pointi 9 wakati Mbeya City imesalia mkiani ikiwa na pointi 5.
Mgambo JKT inajiandaa kufunga safari kuja Dar kwa ajili ya pambano lake dhidi ya Yanga litakalopigwa siku ya Jumamosi.
MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA
                               P   W    D    L    F    A   GD   Pts
01. Mtibwa Sugar    06  04  02  00  09  02  07   14
02.  Coastal Union   06  03  02   01  08   05 03  11
03.  Azam               06  03  01  02  06  03  03   10
04. Yanga               06  03  01  02  07   05  02  10
05. Kagera Sugar    06  02  03   01  05   03 02   09
06.  Mgambo JKT    06  03  00  03   04    05  -1  09
07. JKT Ruvu          06  02  01  03   05   07   -2  07
08. Ruvu Shooting  06  02  01   03  04   06   -2  07
09. Prisons             06  01  03   02  06   06  00   06
10. Simba              06  00  06   00  06    06  00  06
11. Ndanda Fc        06  02  00   04  08    10  -2  06
12. Polisi Moro       06  01  03  02   05    07   -2  06
13. Stand Utd         06  01  03   02  04   09  -5   06
14. Mbeya City       06   01  02   03  02   05  -3   05

Bastia yamtema kocha wao Claude Makelele

http://cdn.sports.fr//images/media/football/ligue-1/articles/un-nouveau-cycle-a-bastia/claude-makelele-a-pris-le-relais-de-frederic-hantz/12064163-1-fre-FR/Claude-Makelele-a-pris-le-relais-de-Frederic-Hantz_w484.jpg 

KLABU ya Bastia inayoshiriki Ligi Kuu ya Ufaransa (Ligue 1) imethibitisha kuachana na aliyekuwa kocha wao, kiungo wa zamani wa kimataifa wa The Blues, Claude Makelele.

Taarifa ya klabu hiyo inayokamata nafasi ya pili toka mkiani, imesema Makelele ameondoka katika klabu hiyo leo Jumagtatu kutokana na mwenendo mbaya wa timu yao ikiwa imeshinda mechi mbili kati ya 12 za ligi.

Makelele aliyetamba na klabu mbalimbali zikiwamo Real Madrid na Chelsea, alipewa mikoba ya kuinoa timu hiyo mwishoni mwa msimu uliopita akitokea PSG.

Miezi sita tangu awe na kikosi hicho, Bastia imeweka bayana kuwa inasaka kocha mpya baada ya kuwa na Makelele kutemwa.

"Kamati ya Wakurugenzi ya SCB inapenda kuwataarifu wote wanaoiunga mkono klabu yetu kuwa kuanzia leo Claude Makelele  siyo tena kocha mkuu wa SC Bastia," taarifa hiyo ya klabu imesomeka hivyo.

"Mazoezi kwa sasa yatakuwa mikononi mwa Ghislain Printant na Herve Sekli mpaka atakapoteuliwa kocha mkuu mpya," taarifa ya klabu hiyo iliongeza.

Makelele alikiongoza mara ya mwisho kikosi cha timu hiyo siku ya Jumamosi wakati waliponyukwa bao 1-0 na Guingamp kwa goli lililofungwa na Sambou Yatabare.

Bale arejea dimbani Madrid ikiikaribisha Liverpool kesho Ulaya

Gareth Bale akiwa mazoezini
KLABU ya Real Madrid inayojiandaa kurudiana na Liverpool katika Ligi ya Mabingwa Ulaya imeongezewa nguvu baada ya nyota wake Gareth Bale kuanza mazoezi na wenzake.
Bale aliyekuwa majeruhi alikuwa akifanya mazoezi ya kujitegemea kabla ya jana kuanza kufanya pamoja na wenzake.
Bale raia wa Wales ni mmoja wa washambuliaji nyota na hatari wa kikosi cha Madrid.
Vinara hao wa La Liga itarudiana na Liverpool kesho mjini Madrid baada ya kuwanyoosha kwa mabao 3-0 katika mechi yao iliyopita kwenye uwanja wao wa Anfield.
Mechi nyingine za kesho ni Kundi A litashuhudia Juventus ikiumana na Olympiakos mjini Turin, Italia wakati Malmo itajiuliza upya kwa Atletico Madrid wakiwa kwao Sweden.
Kundi B mbali na Real Madrid na Liverpool kuwa kesho kutakuwa na mtanange kati ya  Basel dhidi ya  Ludogorets wakati Kundi C litashuhudia timu za Zenit ikiumana na Bayer Leverkusen na Benfica kuikaribisha Monaco.
Michezo mingine ni ile ya kundi D kati ya Arsenal dhidi ya Anderlecht na Borussia Dortmund ambayo inachechemea katika Bundesliga, itapoialika Galatasaray.

Silas Mwakibinga amaliza mkataba TPBL

https://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/11/DSCN3060.jpgOFISA Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), Silas Mwakibinga amemaliza mkataba wake tangu Oktoba 31 mwaka huu.
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na TPLB wanamshukuru Mwakibinga kwa mchango wake kwa kipindi ambacho ameitumikia Bodi, na kumtakia kila la kheri katika majukumu yake mapya huko aendako.
TPLB hivi sasa iko katika mchakato wa kupata Ofisa Mtendaji Mkuu mpya kwa ajili ya kuziba nafasi hiyo iliyoachwa wazi na Mwakibinga baada ya muda wa mkataba wake kumalizika.

Mart Nooij kutaja kikosi cha Stars cha kuifuata Swaziland

https://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/08/DSCN2670.jpg
Kocha wa Taifa Stars, Mart Nooij
 KOCHA Mkuu wa Taifa Stars, Mart Nooij keshokutwa (Novemba 5 mwaka huu) atatangaza kikosi cha timu hiyo kwa ajili ya mechi ya kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) itakayochezwa ugenini Novemba 16 mwaka huu.
Nooij atatangaza kikosi hicho mbele ya waandishi wa habari katika mkutano utakaofanyika saa 4.30 asubuhi kwenye ofisi za TFF zilizoko ghorofa ya tatu, Jengo la PPF Tower jijini Dar es Salaam.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itacheza na Swaziland, mechi itakayopigwa kwenye Uwanja wa Taifa wa Somhlolo jijini Mbabane.
Mwezi uliopita Stars ilicheza mechi ya kirafiki na Benin na kuicharaza mabao 4-1 ikiwa ni wiki chache tangu wakung'utwe mabao 2-0 na Burundi mjini Bunjumbura.

Sitta 'amng'ong'a' Jaji Warioba vurugu za jana

Samuel Sitta, Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh6YLIzt5yxM8bGdMOOt4NZ7sOY_QCkcA60TVGri9nIvQHC_VMnTvoDja22z1RugAn-oF2QnW7FV5SRtaVkjFrSKYDcipeS2QhhWNrpQXfNU6L0K5mSZn6K7BAxRgIvq3nhXT-tBHp1pzc/s1600/05WARIOBAAFANYIWAFUJO5.jpg
Jaji Warioba jana kabla ya kufanyiwa vurugu na watu wanaodaiwa kupangwa na watu wasiofurahishwa na msimamo wake wa kutetea wananchi baada ya kuchakachuliwa kwa maoni yao kupitia Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliyoiongoza.
ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samwel Sitta amesema kilichomkuta aliyekuwa Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya Katiba jana ni sawa na kujitakia mwenyewe.
Akihojiwa na Redio Voice of Tabora, inayomilikiwa na Mbunge wa Jimbo la Tabora, Ismail Aden Rage kuhusu maoni yake kwa vurugu kubwa iliyoongozwa na Paul Makonda jana, Mzee Sitta amesema kimsingi wananchi walio wengi wanaunga mkono Katiba pendekezwa.


Mzee Sitta amesema Jaji Warioba anapaswa kutulia kwani akiendelea anaweza kuaibishwa kuliko aliyofanyiwa jana pale Ubungo blue pearl.
Mzee Sitta amemtaka Warioba awaachie wananchi Katiba pendekezwa waamue wenyewe kwa njia ya kura.
Sitta ameendelea kusema watanzania wa sasa siyo wajinga na wakikuona unawadanganya watakuvamia hapohapo.
Amedai uelewa wa wananchi kwa sasa ni mkubwa kuliko wakati mwingine wowote.
Alipoulizwa swali kuhusu Uvumi kwamba yeye ndiye anamfadhili na kumtuma Paul Makonda kupambana na yeyote anayempinga Mzee Sitta amecheka na kusema hatajibu hilo swali.
(MALUNDE)
Kuvamiwa kwa Jaji Warioba kuleta hisia kwamba ni 'chuki' dhidi yake katika kueneza ukweli juu ya kilichofanywa na wajumbe wa Bunge la Katiba Maalum katika Katiba Pendekezwa ambayo imeachja baadhi ya maoni ya wananchi na kuwekwa mawazo ya wajumbe hao ambao wengi wao ni wa chama tawala (CCM).
Kadhalika watu wamekuwa wakihoji inakuwaje Waziri Mkuu Mstaafu anaweza kufanyiwa uhuni kama ule uliofanyika Blue Pearl kama HAKUNA NGUVU nyuma ya vijana WALIOHUSIKA?!
MICHARAZO ina HAMU kubwa ya kuisikia SERIKALI itatoa TAMKO gani juu ya UHUNI aliofanyiwa WAZIRI MKUU MSTAAFU, Jaji Joseph Warioba kwani siyo kitu cha kawaida kwa wananchi waliostaarabika na wenye kudumisha udugu, umoja na mshikamano hata kama watu WANATOFAUTIANA mawazo. Ngoja tuone.
Makonda mwenyewe amekanusha taarifa za kuhusika na vurugu hizo za jana akidai hajampinga Jaji Warioba kama mitandao mingine ya kijamii ilivyoripoti na pia amejitetea alikuwa akimsaidia Jaji mstaafu huyo ili asipate madhara na kwamba anamuheshimu kama BABA YAKE MZAZI.

Majeruhi wazidi kumchanganya kocha Luis Van Gaal

http://www.nerdoholic.com/wp-content/uploads/2014/07/Van-Gaalmoyes1.jpg
Kocha Luis Van Gaal
KOCHA Louis Van Gaal wa Manchester United, yupo katika hali tete kufuatia timu yake kukumbwa na balaa la kuwakosa nyota wake tegemeo kutokana na kuwa majeruhi.
Jumla ya wachezaji nane wa Mashetani Wekundu ambao jana walilala ugenini bao 1-0 dhidi ya mahasimu wao Manchester Citym, wapo nje ya dimba  wakiuguza majeraha mbalimbali japo baadhi wakitarajiwa pengine kurudi uwanjani wiki hii.
Radamel Falcao ana jeraha la sehemu ya nyuma 'kigimbi' ya mguu wake wa kulia
Falcao anauguza 'Kigimbi'
Moja ya wachezaji waliokosa mechi mbili zilizopita ni mshambuliaji Radamel Falcao ambaye aliumia sehemu ya nyuma ya mguu wake ambayo inafahamika kama kigimbi au Calf kwa jina la kitaalamu na anatarajiwa kurudi uwanjani tarehe 8 ya mwezi huu .
Marcos Rojo aliteguka bega kwenye mchezo dhidi ya Manchester City.
Marcos Rojo yeye katenguka bega jana wakati wakiumana na Man City
Marcos Rojo akitolewa uwanjani baada ya kuumia bega .
Mlinzi wa kimataifa wa Argentina Marcos Rojo ni jina lingine ambalo limeingia kwenye orodha ya majeruhi wa United baada ya kuteguka bega kwenye mchezo dhidi ya Manchester City .
Bado haijafahamika beki huyo atarudi lini uwanjani lakini hatarajiwi kuonekana kwa angalau siku 21 ambazo ni sawa na wiki tatu ambazo atalazimika kuwa nje ya uwanja .
Jonny Evans naye amekuwa nje kwa jeraha la kifundo cha mguu .
Jonny Evance naye yupo Wodi ya Majeruhi Old Trafford
Beki wa Ireland ya Kaskazini Jonny Evans naye ni miongoni mwa ‘wagonjwa ‘ walioko kwenye wodi ya Manchester United tangu alipoumia ‘enka’ takribani wiki tatu zilizopita .
Beki huyu anakaribia kurudi uwanjani na tarehe aliyopangiwa kuanza mazoezi mepesi ni mwishoni mwa wiki hii .
Phil Jones ana jeraha la ugoko alilopata kwenye mechi dhidi ya Chelsea.
Phil Jones anauguza ugoko
Majeruhi mwingine ni Phil Jones ambaye alipata jeraha kwenye eneo la ugoko kwenye mchezo ambao United ilicheza dhidi ya Chelsea na bado hajapangiwa tarehe ya kurudi uwanjani .
Rafael Da Silva
Rafael Da Silva

Jesse Lingard aliumia goti kwneye mchezo wa kwanza wa ligi dhidi ya Swansea City.
Jesse Lingard anauguza goti kwa muda mrefu
Ashley Young ana jeraha la paja.
Ashley Young anaugulia maumivu ya paja

Kwa jumla United ina wachezaji saba wa kikosi chake cha kwanza ambao wako nje wakiuguza majeraha mbalimbali japo orodha hiyo inategemea kushuka na kufikia wachezaji watano baada ya kurejea uwanjani kwa Radamel Falcao na Jonny Evans huku Rafael Da Silva naye akiwa hayuko mbali kwani jeraha alilopata kwenye mazoezi ya mwisho kuelekea mchezo dhidi ya Manchester City sio kubwa hivyo huenda akampa afueni LVG.

Ngassa aweka historia Ligi Mabingwa Afrika, aibuka 'Mfungaji Bora'

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjSNrV2Vw9ADjzK0QsqXHv5f-rU5lb1GUa0wq0H0XWXrkF4MeDm2Vo3wyzFJ6qwCh15_1Q3nlimtsnkwdpCU01VERuI95w2AJ53nlR3HJ2u97pQVvO1nyE3s5Z7SyZSYljBWW9J0cFQtmE/s640/ngassa.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhnQpXo6MHALL-ZuJIh9unVMS1kB_h8piBza5z_Q_qp_BvJYLYhnn8mHOEpfBNdIbATYXmjIMuHpJ2660NaZHukVsSbnOApungYQ8ZW4vC9ez0MEVHGHcfF5UVkNahytsAisgQO_wmXAOG-/s1600/DSC_0042.JPG
Ngassa (17) akishangilia na wenzake moja ya mabao yake wakati wakiichakaza Komorozine ya Comoro kwa mabao 70-0 uwanja wa Taifa katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika 2014
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgmHOmnqw2_HrlI8coC359ewdUFnCTH6YyKOkxcdN1K-y2BQXSMPfxZIu72LMR8L7uNNdo5C1kpSBfBxv1bs_A6aioBRMl0L9mWQ7Fw7wKS_b9aubckH3g0j9npx9fiF0i6zIrvs0FXPxU/s1600/ngasa.jpg
Siku ya mechi hiyo dhidi ya Komorozine, Ngassa alikuwa akinyanyasa kama anavyoonekana pichani akimtokea beki wa timu hiyo ya Comoro waliong'olewa kwa jumla ya mabao 12-2
MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Yanga Mrisho Ngassa ameweka historia baranui Afrika baada ya kuwa miongoni mwa wachezaji wanne walioibuka 'Wafungaji Bora' wa michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika iliyomaliza mwishoni mwa wiki kwa timu ya Es Setif ya Algeria kutwaa ubingwa.
ES Setif ilinyakua taji hilo ikiwa ni mara ya kwanza tangu mwaka 1988 baada ya faida ya goli la ugenini kuwabeba kutokana na kufungana jumla ya mabao 3-3 baada ya kufunga 2-2 mjini Kinshasa kabla ya Jumamosi kufunga tena 1-1 Algeria.
Ngassa anayeichezea pia timu ya taifa, Taifa Stars ambaye timu yake ya Yanga ilitolewa katika raundi ya pili amefungana na wachezaji wenzake watatu wakiwa na mabao sita kila mmoja.
Wachezaji wengine waliofungana na Ngassa ni El Hedi Belameiri wa ES Setif ambaye ana nafasi kubwa ya kunyakua Kiatu cha Dhahabu kutokana na kuweza kuifikisha timu yake fainali na kutoa pasi ya mwisho iliyowapa sare nyumbani dhidi ya Vita.
Nyota wengine waliomaliza wakiwa na idadi hiyo ya mabao mbali na Ngassa na Belameiri, ni Ndombe Mubele wa As Vita ya DR Congo na Haythem Jouini wa Esperance ya Tunisia.
Ngassa alifunga mabao hayo sita yaliyomfanya kuwa mchezaji wa kwanza wa Tanzania kumaliza Mfungaji Bora Afrika wakati wakiingamiza Komorozine ya Comoro kwa jumla ya mabao 12-2,  yeye akifunga 'hat trick' mbili, moja katika kila mechi  nyumbani na ya ugenini kabla ya Yanga kutupwa nje na Al Ahly ya Misri.
Katika mechi ya kwanza iliyochezwa jijini Dar es Salaam ambapo Yanga ilishinda mabao 7-0, Ngassa alifunga mabao yake dhidi ya Komorozine katika dakika za 14, 65, 68, huku mengine yakifungwa na Nadir Haroub Cannavaro (Dk 20) Didier Kavumbagu (Dk  57 na 80) na Hamis Kiiza (Dk 60)
Walipowafuata wapinzani wao nchini Comoro ambapo Yanga waliigagadua Komorozine mabao 5-2, Ngassa alifunga tena 'hat trick' ya pili kwa mabao ya DK 22, 87 na 90, huku magoli mengine yalifungwa na Hamis Kiiza katika dakika ya 13 na Simon Msuva aliyefunga dakika ya 37 na mabao ya wenyeji yakiwekwa kimiani na Anli  na Ismail katika dakika ya 41 na 77.
Yanga ilikutana na waliokuwa mabingwa watetezi, Al Ahly ya Misri na kuwalaza bao 1-0 nyumbani katika mechi ya raundi ya pili, goli likifungwa na Cannavaro kabla ya kwenda Misri na kulala 1-0 na kulazimisha mechi hiyo kumalizwa kwa mikwaju ya penati na Yanga kutolewa kwa mikwaju 4-3.
Licha ya Al Ahly kuitoa Yanga ilienda kukwama kwa Al Ahly Benghazi ya Libya na kuhamia kwenye Kombe la Shirikisho Afrika ambapo Wamisri hao wamefanikiwa kufika fainali na watavaana na Sewe Sports ya Ivory Coast kuwania taji hilo katika mechi mbili zitakazochezwa Novemba 29 na Desemba 6 mwaka huu.

ES SETIF MABINGWA WAPYA AFRIKA, AS VITA YAKWAMA

KLABU ya ES Setif ya Algeria imeweka historia ya kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa Afrika kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1988 baada ya kuishinda AS Vita ya DR Congo kwa uwiano wa bao la ugenini.
Timu hizo zilitoshana nguvu kwa kufunga bao 1-1 katika mechi ya marudiano mwishoni mwa wiki na kufanya matokeo ya jumla kuwa 3-3 baada ya awali timu hizo kutoka sare ya 2-2 mjini Kinshasa.
Katika mechi iliyochezwa uwanja wa Mustapha Tchaker mjini Blida, wenyeji walianza kutangulia kupata bao dakika ya nne tu ya kipindi cha pili kupitia Sofaine Younes aliyemaliza pasi ya El Hadi Belameiri.
AS Vita iliyokuwa ikiliwinda taji hilo kwa udi na uvumba baada ya kufanikiwa kutinga fainali baada ya miaka mingi kupita, ilirejesha bao hilo dakika tano baadaye kupitia kwa Lema Mabidi kwa mkwaju mkali nje ya penati.
Mabidi ndiye aliyefunga mabao mawili wakati Vita ikilazimishwa sare nyumbani wiki iliyopita.
Kufungwa kwa bao hilo kuwafanya wenyeji kuanza kujiangusha kwa nia ya kupoteza muda na hatimaye kufanikiwa kumaliza dakika 90 wakiwa mabingwa wapya baada ya miaka 26 iliyopita.

Kiporo cha Mbeya City, Mgambo JKT leo Mkwakwani Tanga

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg-O1Bsrv7R14eySj51Bdkjnh-ROxWzaAWbez2AwRB4TkE8bBSq51y8jp6dKblzfOsMPwJyQoa1QlRAzF6xuJLTdauDI9Jzq47_2Hv4Wg4cD21PggfvNLVRSLs_YUPoqXcDLEYU-EZNJfxC/s1600/IMG-20140920-WA0053.jpghttp://www.hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/08/MGAMBO.jpgMVUA kubwa iliyonyesha jijini Tanga imekwmaisha pambano la Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya wenyeji Mgambo JKT na Mbeya City kushindwa kufanyika kwenye uwanjka wa Mkwakwani na badala yake kipute hichio kitachezwa leo.
Mchezo huo uliokuwa uchezeshwe na refa Israel Mujuni Nkongo uliamriwa kuharishwa hadi leo kutokana na hali ya uwanja kutoruhusu ambapo hata mashabiki walikosa mahali pa kujikinga dhidi ya mvua kubwa iliyonyesha mapema asubuhi na kukata kabla ya kurudi tena jioni kwa nguvu kubwa.
Kwa mujibu wa msimamizi wa mchezo huo mwamuzi mstaafu Hamisi Kisiwa mara baada ya ukaguzi kufanywa na waamuzi wa mchezo huo iliamuriwa mchezo huo kusogezwa mbele kwa saa 24 kwa mujibu wa kanuni huku taarifa zaidi ikisubiriwa kutoka kwa wasimamizi wa ligi hiyo bodi ya ligi.
Mbeya City inakutana na Mgambo ikiwa imetoka kujeruhiwa nyumbani katika katika mechi dhidi ya Azam, wakati Mgambo bado wanachekelea ushindi wa bao 1-0 iliyopata mjini Mtwara mbele ya Ndanda Fc 

Aguero awaliza Mashetani Wekundu, Spurs yaizima Aston Villa

Ilikuwa ikionekana ni ngumu leo kumfunga David de Gea. Kwa upande wake Sergio Aguero haikuwa hivyo kwani alidhihirisha kuwa yeye ni noma alipoifungia bao pekee kwa timu yake na kuipa ushindi City dhidi ya United.
Tayari dakika 63 zilikwisha kupita wakati Aguero akifunga goli hilo na kudhihirisha kuwa yeye ndiye shujaa wa 'derby' ya Manchester hii leo.
Wasiwasi ulitanda tangu mapema kufuatia United kupungua na kusali kumi kunako dakika ya 39 wakati Chris Smalling alipoondoshwa uwanjani na mwamuzi kwa makosa mawili huku pia Marcos Rojo akiumia bega.
Wakati huo Tottenham Hotspur ilitoka nyuma na kuizima Aston Villa kwa mabao 2-1 katika pambano la ugenini.
Spurs ilitanguliwa kufungwa bao la kipindi cha kwanza na wenyeji kupitia Weimann kabla ya Chadli kusawazisha dakika ya 84 na Harry Kane kufunga bao lake la saba katika mechi saba za Spurs na kuipa ushindi timu yake.
Katika pambano hilo wenyeji walimpoteza nyota wa Christian Benteke aliyelimwa kadi nyekundu dakika ya 65.
Sergio Aguero converts Gael Clichy's low cross from the left to put Manchester City 1-0 ahead in the Manchester derby
Sergio Aguero akiunganisha krosi ya Gael Clichy kutoka kushoto na kuwapa uongozi Manchester City wa bao 1-0 dhidi ya majirani zao Manchester United
Juhudi za Aguero zikionekana katika picha akipiga mpira unaomzidi David de Gea kunako dakika ya 63 uwanja wa Etihad
Aguero (third from left) is mobbed by his team-mates after giving Manchester City the lead against their local rivals United
United players (from left to right) Paddy McNair, Wayne Rooney and Luke Shaw appear dejected following City's goal