STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, September 7, 2014

Malawi yapigwa 2-0 na Mali ugenini Afrika

http://www.malawidemocrat.com/wp-content/uploads/2012/06/Flames-e1339493490888.jpg
Kikosi cha Malawi kilichonyolewa 2-0 ugenini leo
TIMU ya taifa ya Malawi imekumbana na kipigo cha mabao 2-0 ugenini mbele ya wenyeji wao Mali katika mechi ya kiporo cha mechi za makundi za kuwania kucheza Fainali za Afrika mwakani nchini Morocco.
Mechi hiyo ya kundi B ilishindwa kufanyika jana kama ratiba ilivyokuwa ikionyesha kutokana na mvua kubwa iliyopiga katika mji wa Bamako na kusogezwa mpaka leo.
WEnyeji walitumia vyema uwanja wa nyumbani kwa kuwanyoosha The Flames kwa mabao 2-0 na hivyo kuongoza kundi hilo kwa pointi tatu sawa na Algeria iliyoinyoa Ethiopia kwa mabao 2-1, ila Mali wanaongoza kwa uwiano wa mabao ya kufungwa na kufungwa.

DRFA yafanya madudu, mechi ya Big Bullets Yanga yaota mbawa

http://news.maraviexpress.com/wp-content/uploads/2014/05/Bullets.jpg
Big Bullets iliyokwama kuja jijini kucheza na Yanga
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhJWEafFWYmtnV6WN3aGK6c4cEcsUAkpPLwbwR46wREXcdd1Zfcm2eRU2wTnXME4uvkevK-oPUMrMc3l-KEB1QIb6KrzEzGw2cH4DOuwZTF9iijFJXxstz8yfAH2Jk-Bi4qd217JLnyzNQ/s1600/Yanga+express+2.jpg
Yanga walioikosa Big Bullets
PAMBANO la kirafiki la kimataifa baina ya Yanga na Big Bullets ya Malawi, limeota mbawa baada ya timu hiyo iliyokuwa ikielezwa ilikuwa Mbeya kushindwa kutua nchini na kusababisha usumbufu mkubwa kwa mashabiki wa kandanda waliofurika uwanja wa Taifa kwenda kushuhudia mechi hiyo.
Inaelezwa kuwa timu hiyo wala haikuwa nchini kama ilivyokuwa imetangazwa awali na kwamba ujio wake chini ya ufadhili wa Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) na badala yake ilikuwa kwao Malawi ikishuka dimbani leo kucheza mechi ya ligi ya nchi yao.
Yanga ilikuwa imeupania mchezo huo ambao ungekuwa wa mwisho kwao kabla ya kuivaa Azam kwenye mechi ya Ngao ya Hisani Jumapili ijayo kwenye uwanja huo huo wa Taifa kuashiria kuanza kwa msimu mpya wa ligi kuu Tanzania Bara 2014-2015.
Viongozi wa DRFA hawakupatikana kueleza kilichotokea katima ujio wa Big Bullets inayoshika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ya nchi yao, huku viongozi wa Chama cha Soka Mkoa wa Mbeya wakidai timu hiyo haikuwa mjini humo na waliitegemea baada ya kucheza na Yanga ndiyo ingetua jijini humo kucheaa mechi na Mbeya City.

Okwi aigaragaza Yanga, ryksa kukipiga Msimbazi, Banda naye...

http://in2eastafrica.net/wp-content/uploads/2014/03/Emmanuel-Okwi.jpg
Yanga ndiyo basi tena
Ruksa kukipiga Msimbazi kama alivyofanya jana kwenye uwanja wa Taifa dhidi ya Gor Mahia
YANGA Chalii ndivyo tunavyoweza kusema baada ya Kamati ya Sheria Maadili na Hadhi za Wachezaji kubaini kuwa klabu hiyo ilikuwa imekiuka mkataba wake na mchezaji Emmanuel Okwi na kwa msingi huo Mganda huyo yupo Huru kujiunga na timu yoyote.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TFF jioni hii imesema kuwa Kamati hiyo iliyokyutana asubuhi imegundua, Yanga SC ilikiuka masharti mengi ya mkataba na mchezaji huyo na kimsingi tangu Januari amekuwa akicheza bila mkataba. Hii ina maana kwamba mipango yake ya kuichezea Simba njia nyeupe kama mwenyewe alivyokuwa akitamba.
Ebu soma taarifa hiyo rasmi ya TFF


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Septemba 7, 2014

MKATABA WA YANGA, OKWI HAUPO
"Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imekutana leo (Septemba 7 mwaka huu) na kupitia masuala mbalimbali ikiwemo mgogoro wa kimkataba kati ya klabu ya Yanga na mchezaji Emmanuel Okwi.
Mkataba huo ulipitiwa na Kamati ikiwemo kumsikiliza mchezaji mwenyewe pamoja na upande wa Yanga, na kuridhika kuwa mkataba kati ya pande hizo umevunjika.
Ukiwa ni mkataba wa pande mbili, Yanga ilikiuka kipengele namba 8 kuhusu malipo ya ada ya usajili.
Yanga ikiwa mwajiri, haikutekeleza kipengele hicho cha kimkataba hadi kufikia Juni 27 mwaka huu ilipoandika barua TFF kuomba mkataba huo uvunjwe. Kwa maana hiyo Okwi ni mchezaji huru, hivyo yuko huru kujiunga na timu yoyote.
Mkataba ni uhusiano kati ya mwajiri (Yanga) na mwajiriwa (Okwi), ambapo Kamati imebaini kuwa uhusiano huo haupo, hivyo hakuna mazingira ya pande hizo mbili kuendelea kufanya kazi pamoja.
Pamoja na Yanga kuwasilisha pingamizi la kuwepo mmoja wa wajumbe katika kikao kwa sababu za kimaslahi (conflict of interests), walifahamishwa kuwa kilichopo mbele ya kamati ni mgogoro wa kimkataba kati ya Yanga na Okwi, na si usajili.
Pia lilijitokeza suala la Okwi kutakiwa na klabu ya Wadi Degla ya Misri. Kamati imeiagiza Sekretarieti ya TFF kulifanyia uchunguzi suala hilo na kulitolea taarifa katika kikao kijacho.
Hata hivyo mjumbe huyo hakushiriki katika kuchangia hoja na kutoa maamuzi. Uamuzi wa kamati ulifanyika baada ya majadiliano, hivyo hakukuwa na suala la kupiga kura.
Kuhusu pingamizi la Coastal Union kwa Abdi Banda, Kamati imebaini kuwa klabu hiyo imevunja mkataba kati ya pande hizo mbili kwa kushindwa kumlipa mchezaji huyo mshahara wa miezi mitatu mfululizo kama takwa la mkataba.
Klabu ya Coastal Union iliwakilishwa na mmoja wa viongozi wake, wakati Banda aliwakilishwa na mwanasheria wake.
Vilevile Kamati imekubaliana na pingamizi la Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Morogoro (MRFA) kuhusu wachezaji waliofanyiwa uhamisho kutoka katika mkoa wake bila kulipiwa ada za usajili, hivyo klabu husika zinatakiwa kulipa ada hizo.
Pia Kamati imeagiza klabu zote zilizosajili wachezaji bila kuwafanyia uhamisho, kulipa ada za uhamisho kwa pande husika kabla ya kuanza ligi, vinginevyo leseni zao zitazuiwa hadi watakapolipa.
Mashauri mengine ya pingamizi yatasikilizwa baadaye kwa vile klabu husika hazikupata fursa ya kufika mbele ya kamati. Kamati inasisitiza kwa wanachama wa TFF kuheshimu mikataba,".
"BONIFACE WAMBURA, KAIMU KATIBU MKUU
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)."

HAWA NDIYO WALIOTEULIWA KUENDELEA NA MASOMO 2014-2015


WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
WAOMBAJI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA STASHAHADA YA JUU (MIAKA 3) MWAKA WA MASOMO 2014/2015
MAELEKEZO:
Waombaji waliochaguliwa kujiunga na Mafunzo ya Ualimu mwaka wa masomo 2014/2015 wanatakiwa kuripoti katika Vyuo walivyopangiwa tarehe 06/10/2014. Fomu za maelekezo (Joining Instructions) zitatolewa na chuo husika na zitatumwa kwa waliochaguliwa tu. Waliochaguliwa wanatakiwa kufika vyuoni wakiwa na mahitaji yaliyoainishwa kwenye fomu
 ya kujiunga na Chuo. Aidha, fomu hizi zinapatikana pia kwenye Tovuti ya Wizara:www.moe.go.tz; NACTE:www.nacte.go.tz; na TAMISEMI:
 www.pmoralg.go.tz 

Muhimu:

1. Waombaji waliochaguliwa ni wale wenye ufaulu wa Daraja la I hadi III

2. Waliochaguliwa wanatakiwa kuwasilisha Vyeti halisi vya Baraza la Mitihani
la Tanzania Kidato cha NNE na SITA (CSEE na ACSEE) na vyeti vya kuhitimu
Elimu ya Sekondari na Mafunzo ya Ualimu.

3. Ada ya mafunzo Stashahada ya Juu ni 600,000/= kwa mwaka (Muhula wa
 kwanza 300,000/= na muhula wa pili 300,000/=)

4. Wanafunzi watakaosajiliwa Chuoni ni wale waliopo kwenye orodha hii tu na
SIYO vinginevyo, waweza pata orodha hyo kwa kufungua kiunganishi kimoja
wapo hapo chini au kwa kutembelea mfumo wenye majina - bonyeza hapa

MAJINA YA WALICHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAADA YA JUU SAYANSI & HISABATI
MAJINA YA WALICHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAADA YA JUU ELIMU MAALUMU
MAJINA YA WALICHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAADA YA JUU LUGHA (KISWAHILI, ENGLISH & 
FRENCH)
MAJINA YA WALICHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAADA YA KAWAIDA ELIMU YA AWALI
MAJINA YA WALICHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAADA YA KAWAIDA ELIMU YA MICHEZO
MAJINA YA WALICHAGULIWA KUJIUNGA NA STASHAADA YA KAWAIDA ELIMU YA MSINGI

Hatari! Majambazi yavamia kituo yaua Polisi wawili, waiba silaha

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjwfsRcEwCMRwNW6Uaz4brRmeREhwfGJZ7jpWieFZ-sRoZtTRriNZdo5nv6M-Jhe9Y6hqyO6Fj1immwIhHPTSpfLOQswbC4Us3OsZNJ3e4hL0-h0NqZ0X1n9BVDvRrgUeWNrABfyiJ0fF8/s640/AK+47.jpg
Mfano wa silaha ambazo hazihusiani na habari hii
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEibCw3q6Vcix9AOZSDCMq6tTz1JymOIsmtChCfomJLgxgeMYRuYVYTIbrtgaoUSoiWZL8kl2buqW-9l0iMJ8xXpb39JbuwWRpb792DNwQEOMtXG5UhBnWZahhuo8N2tEifeP_08yjVS7kw/s640/T1.jpgWATU wanaodaiwa kuwa majambazi wamevamia Kituo Kikuu cha Polisi cha Wilaya ya Bukombe kilichopo Ushirombo, mkoani Geita na kuua askari wawili na kuiba silaha za moto. 
Taarifa za awali za tukio hilo zimethibitishwa na Kamishna wa Polisi, Operesheni na Mafunzo, Paul Chagonja. 
Akizungumza na waandishi wa habari jana, alisema uvamizi huo unatajwa kufanywa majira ya saa 9 usiku katika kituo hicho mkoani Geita, ambapo inadaiwa wahalifu hao ambao idadi yao inakadiriwa kuwa zaidi ya kumi, walivamia kituo wakiwa na silaha za kivita. 
Alisema mazingira ya tukio hilo inaelezwa kuwa majambazi hao walipofika kituoni hapo, walitupa bomu la mkono katika chumba cha mashitaka na kusababisha vifo vya askari wawili wenye namba G.2615 Dunstan Kimati na WP 7106 Uria Mwandiga huku wawili wengine wakijeruhiwa. 
"Walifika katika kituo hicho wakiwa na silaha nzito za kivita, wamesababisha vifo vya askari wawili, lakini wawili wengine wanaendelea na matibabu hospitalini," alisema Chagonja. 
Alisema baada ya kuwaua na kuwajeruhi askari hao waliharibu taa na kusababisha giza kutawala kituoni hapo, ambapo walivunja chumba cha kuhifadhia silaha na kutoweka na baadhi ya silaha. 
"Majambazi hao walivunja na kuchukua baadhi ya silaha ambazo zilikuwepo kituoni hapo, ambazo mpaka sasa idadi yake haijajulikana," alisema Chagonja. 
Chagonja alisema idadi ya silaha hizo haijajulikana kutokana na operesheni mbalimbali zilizokuwa zikiendelea wilayani humo, hivyo silaha zilikuwa zikiingia na kutoka. 
Chagonja alisema, kutokana na tukio hilo Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Ernest Mangu yuko katika eneo la tukio akiwa amefuatana na  Mkurugenzi wa Upelekezi na Makosa ya Jinai (DCI) Isaya Mngulu na timu ya wataalamu wa upelelezi na operesheni ili kuhakikisha wahusika wa tukio hilo wanakamatwa. 
Hata hivyo, aliwataka wananchi kuwa watulivu akisema Jeshi la Polisi litahakikisha wahusika wa tukio hilo wanakamatwa na sheria kuchukua mkondo wake, lakini pia aliwataka wananchi wenye taarifa muhimu zitakazosaidia kuwakamata wahalifu hao wazitoe ili zifanyiwe kazi. 
Kwa mwaka huu tukio kama hilo la kuvamiwa kwa Kituo cha Polisi na kuuawa kwa askari na majambazi kuchukua silaha ni la pili ambapo la kwanza lilitokea Juni, mwaka huu katika Kituo kidogo cha Polisi cha Mkamba, wilayani Mkuranga Mkoa wa Pwani ambako majambazi walimuua askari mmoja na kuwajeruhi wengine watatu  na kupora silaha tano zenye risasi ambazo ni SMG mbili na Shot gun tatu. 
Hata hivyo, wahalifu waliohusika na tukio hilo walikamatwa na kesi yao bado inaendelea. 
Ingawa taarifa ya Chagonja haikueleza idadi ya silaha zilizoibwa, taarifa za ndani ambazo gazeti hili inazo zinasema majambazi hao wameiba bunduki kumi, risasi na mabomu ya mkono, kisha kutokomea. 
Imeelezwa kuwa baada ya kufika kituoni hapo, majambazi hao walizingira kituo hicho hadi eneo la mapokezi na kuanza kuwamiminia risasi za moto askari waliokuwa zamu. 
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bukombe, Dk Honoratha Rutatinisibwa amekiri kupokea miili ya askari wawili wa kike na kiume. 
Waliojeruhiwa wamefahamika kuwa ni askari mwenye namba E.5831 David Ngupama Mwalugelwa aliyejeruhiwa kichwani na usoni na kwamba ameumizwa vibaya sehemu za mdomo wake huku meno mawili yaking'oka. 
Mwingine ni Mohammed Hassan Kilomo aliyejeruhiwa kifuani na mguu wa kulia uliovunjika mfupa kwa kupigwa risasi. 
Dk Rutatinisibwa alipoulizwa juu ya hali za majeruhi hao, alisema ni mbaya na kwamba walilazimika kuwahamishia Hospitali ya Rufaa ya Bugando, jijini Mwanza kwa matibabu zaidi. 
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Geita, Joseph Konyo awali alithibitisha kutokea kwa tukio na kuahidi kutoa taarifa zaidi mara baada ya uchunguzi kukamilika. 
Hilo ni tukio la pili kwa askari wa kituo hicho kuuawa na majambazi ambapo Juni 28, 2009 kundi la majambazi saba wenye silaha za moto aina ya SMG, yaliteka magari manne ya mizigo katika pori linalounganisha maeneo ya Lunzewe, Matabi na Buselesele lililopo Bukombe na kumuua kwa kummiminia risasi nne kifuani askari Polisi aliyejulikana kwa jina moja la Pascal wa Kituo hicho cha Polisi Bukombe. 
Tukio hilo la kinyama lilitokea majira ya saa 1:15 asubuhi, ambapo wakitumia lori lililokuwa limebeba mkaa, waliziba barabara inayokatiza katika pori hilo wakati Pascal na mwenzake wakisindikiza magari hayo ya mizigo kupita katika pori hilo.

Shirika la HUC latangaza neema kwa vijana Tanzania katika masomo

Na Nathan Mpangala wa HUC.
SHIRIKA lisilo la kiserikali la Help for Underserved Communities Inc. (HUC), linatangaza nafasi za ufadhili wa masomo ya ufundi VETA kwa vijana wa Kitanzania. Kozi hizo ni ufundi wa magari, umeme wa magari, udereva magari/pikipiki, ufundi cherehani, hair dressing (urembo), mapambo ya ukumbi na nyinginezo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na shirika hilo, inasema, HUC, itafadhili wanafunzi 15 wa kozi mbalimbali za awali VETA kwa mwaka 2014-2015.

Walengwa ni vijana wa kike na kiume waliomaliza shule za msingi ambao wamethibitika kuwa wazazi/walezi wao wameshindwa kuwalipia ada. Imesema sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa, mwanafunzi atatakiwa kujaza kwa usahihi fomu ya maombi (imeambatanishwa hapa), akiambatanisha na barua akieleza sababu za kuomba ufadhili huu na barua ya utambulisho toka ofisi ya serikali za mitaa na mwisho wa kupokea barua za maombi ni Jumatano, Oktoba 01, 2014, saa 11 jioni.

Barua za maombi zitumwe kupitia:
Maombi ya ufadhili wa masomo,

Help for Underserved Communities Inc.
P. O. Box 7022,
Dar es Salaam,
Tanzania.
Au
Help for Underserved Communities Inc.
P.O.Box 6822,
Ellicott City, MD 21042
Au
Kupitia baruapepe:
info@myhuc.org OR kijasti@hotmail.com
fomu ya kujiunga

Taarifa hiyo imesema, majina ya watakaopata ufadhili yatatangazwa Oktoba 10, 2014 na kwamba ada italipwa moja kwa moja chuoni.
HUC ni shirika lisilo la kiserikali toka nchini Marekani lenye lengo la kuziwezesha jamii zipatazo huduma hafifu kupata maji safi na salama, vifaa vya elimu na ufadhili wa masomo ya ufundi. Mwaka jana, shirika hili lilifadhili vijana 11 VETA.

Loic Remy achekelea kuwa Chelsea, lakini...!

Delight: Remy signed for Chelsea on final week of the transfer windowMSHAMBULIAJI wa Chelsea,  Loic Remy amesema bado haelewi kwanini dili la kujiunga na Liverpool majira ya kiangazi lilivunjika.
Nyota huyo mwenye miaka 27 alitazamiwa kujiunga Anfield kwa dau la paundi milioni 8 kabla ya wekundu hao kulitupilia mbali dili hilo wakidai mchezaji huyo ameshindwa kufuzu vipimo vya afya.
Remy alishindwa kufuzu vipimo vya afya kutokana na matatizo ya moyo na goti, lakini alishangazwa na tangazo hilo.
“Binafsi sikuelewa. Tatizo wakati wa vipimo vya afya? sijui. Walitengenezea, lazima itakuwa hivyo,” aliwaambia Daily Star.
Mfaransa huyo alirejea QPR na alionekana katika mechi ya ligi kuu kabla ya kujiunga na Chelsea wiki ya mwisho ya usajili ambapo atacheza kumsaidia Diego Costa ambaye amepata majeraha ya nyama za paja katika majukumu ya kimataifa.

Remy, ambaye aliifungia Ufaransa bao la ushindi dhidi ya Hispania siku ya alhamisi, alisema; “Kichwani mwangu, nilitaka kuendelea kukaa QPR, lakini sikuogopa kwa sababu nyingi  nilizonazo: Kwa jinsi nilivyojiimarisha, kujiamini kwangu na kwa namna Chelsea walivyonihitaji, nilikubali kwasababu hii ni moja ya klabu kubwa duniani.
“Nina furaha ya kujiunga na klabu hii”

Yanga kuivaa Big Bullets bila Cannavaro, Ngassa Taifa leo

http://shaffihdauda.com/wp-content/uploads/2014/07/andrew-coutinho1.jpg
Yanga walipokuwa wakijifua ufukweni
YANGA itacheza mchezo wake wa mwisho wa kujipima ngumu kwa kuvaana na Big Bullets ya Malawi katika mechi ya kirafiki ya kimataifa itakayochezwa uwanja wa Taifa.
Hiyo ni mechi ya tano kwa Yanga chini ya Marcio Maximo ikiwa haijapoteza mchezo wowote na wa pili wa kimataifa baada ya katikati ya wiki kuilaza Thika United ya Kenya.
Katika mechi hiyo ya leo ambayo itakuwa ya mwisho kabla kujichimbia kambini kujiandaa na mechi ya kuwania Ngao ya Hisani dhidi ya Azam Jumapili ijayo kwenye uwanja huo huo.
Yanga hata hivyo itawakosa baadhi ya nyota wake katika mchezo wa leo akiwamo Nahodha Nadir Haroub Cannavaro,Kelvin Yondani, Mrisho Ngassa na Simon Msuva waliopo Burundi na kikosi cha Taifa Stars kinachocheza mechi ya kirafiki ya kimataifa leo mjini Bunjumbura.
Hata hivyo Yanga bado ina wakali wengine ambao waling'ara katika mechi yao iliyopita dhidi ya Thika akiwamo Andrey Coutinho kutoka Brazil.

TFF yarejesha Ligi Daraja la Pili, FDL kumekucha!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgwo1n7uSdvpyJ9hXrrECTxsMgixCkxqYyRSCEx0WwOrmfUMB0KMokxfjpjhWLdp6LtrcLUQXLAap7R7s_jFFRtHtu4K9xSOXF7QX2UiAcO3aiOSI9-4ft2Q6uwAmhmsQAn5XbZR1IYCKY/s1600/tff.jpg

KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) iliyokutana hivi karibuni imekubali mapendekezo ya Kamati ya Mashindano ya kurejesha michuano ya Ligi Daraja la Pili (SDL).
Lengo la kurejesha ligi hiyo ni kuongeza wigo wa mashindano kitaifa ambapo itasaidia kushirikisha kundi kubwa zaidi la wachezaji kwenye mashindano makini yanayozingatia viwango na vigezo ili kuwapa wachezaji maendeleo ya kiuchezaji ikiwemo kuendelezwa vipaji vyao kitaalamu.
Ligi hiyo yenye timu 24 itachezwa katika hatua ya makundi manne ya timu sita sita kwa mtindo wa nyumbani na ugenini ambapo mshindi wa kila kundi atapanda kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL). Timu ya mwisho kila kundi itarudi kwenye ligi ya mkoa wake.
Hatua ya pili ni kutafuta bingwa wa SDL ambapo timu zilizoongoza makundi (nne) zitacheza kwa mtoano nyumbani na ugenini. Utakuwepo mchezo wa fainali ambapo mshindi atkuwa bingwa wa SDL msimu wa 2014/2015.
Timu zitakazocheza SDL kwa msimu huu ni zile zilizoshika nafasi ya pili hadi ya nane katika Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) katika makundi yao msimu uliopita, na tatu zilizoshuka kutoka FDL msimu uliopita.
Kundi A litakuwa na timu za Milambo FC (Tabora), Mji Mkuu FC (Dodoma), Mpanda United (Mpanda), Mvuvumwa FC (Kigoma), Singida United (Singida) na Ujenzi (Rukwa). Kundi B ni Arusha FC (Arusha), Bulyanhulu FC (Shinyanga), Eleven Stars (Kagera), Mbao FC (Mwanza), Pamba FC (Mwanza) na Rwamukoma JKT (Mara).
Timu za kundi C ni Abajalo (Dar es Salaam), Kiluvya United (Pwani), Kariakoo FC (Lindi), Mshikamano FC (Dar es Salaam), Navy FC (Dar es Salaam) na Transit Camp (Dar es Salaam). Kundi D ni Magereza FC (Iringa), Mkamba Rangers (Morogoro), Njombe Mji (Njombe), Town Small Boys (Ruvuma), Volcano FC (Morogoro) na Wenda FC (Mbeya). Ligi itachezwa kuanzia Novemba mwaka huu.
Wakati huo huo; Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu wa 2014/2015 itachezwa katika makundi mawili kwa mtindo wa nyumbani na ugenini kuanzia Oktoba 11 mwaka huu.
Kundi A lina timu za African Lyon, African Sports, Ashanti United, Friends Rangers, Kimondo SC, Kurugenzi Mafinga, Lipuli, Majimaji, Mlale JKT, Polisi Dar es Salaam, Tessema FC na Villa Squad.
Wakati kundi B lina timu za Burkina Faso, Geita Veterans SC, Green Warriors, Kanembwa JKT, Mwadui SC, Oljoro JKT, Panone FC, Polisi Dodoma, Polisi Mara, Polisi Tabora, Rhino Rangers na Toto Africans. Ratiba ya Ligi hiyo itatolewa hivi punde.

Hatma ya Emmanuel Okwi ni leo

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhyoheA_Uvou9fxK2lFEGUZbhn5TzQaXgeDX15K4eZ7FQT2g7cE9KO24lO_LVH098dn1hZ_lHvwZEzvCB_Ke7bhHVBixnOx_omri3i1GZytGeRr1DJPfh0RnPBCgj8WCSXyqSZGtQ41kBgJ/s1600/okwiiii.jpg
Kusalia katika uzi huu wa Simba au wa Yanga kama anavyoonekana chini pichani?


http://www.ibn-tv.com/wp-content/uploads/2014/01/Okwi.jpg

HATMA ya Mganda Emmanuel Okwi inatarajiwa kufahamika leo wakati Kamati  ya Sheria na Hadhi ya Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania, TFF inayopongozwa na Mwanasheria Richard Sinamtwa itakapokutana kutoa maamuzi kamili dhidi ya kesi yake.
Okwi aliyekuwa akiiichezea Yanga anapingwa na klabu yake hiyo ya zamani kusajiliwa Simba kwa madai bado anao mkataba, hali iliyoleta utata kama alivyosajiliwa na Yanga msimu uliopita akitokea SC Villa.
Msimu uliopita hali kama hiyo ilijitokeza kwa mchezaji Mrisho Ngassa aliyekuwa akigombewa na Simba na Yanga na hatimaye, kufungiwa mechi sita na kulimwa faini. Je, ni Simba au Yanga watakaohalalishiwa Okwi? Tusubiri

FIFA kuendesha kozi ya Utawala Tanzania

http://www.thisissierraleone.com/wp-content/uploads/2012/08/FIFA1.jpg 
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) kwa kushirikiana na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (Fifa) wameandaa kozi ya ukufunzi wa utawala itakayofanyika Desemba mwaka huu.
Kozi hiyo itakayoendeshwa na wakufunzi kutoka Fifa itafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Desemba 1 hadi 5 mwaka huu, ambapo sifa ya chini ya elimu kwa wanaotaka kushiriki ni kidato cha nne.
Kwa wanaotaka kushiriki kozi hiyo wanatakiwa kutuma maombi yao kwa Katibu Mkuu wa TFF. Mwisho wa kupokea maombi hayo ni Septemba 12 mwaka huu ambapo wanatakiwa pia kuwasilisha nakala za vyeti vyao vya kitaaluma.

Simba wawararua Wakenya 3-0 Taifa

Mshambuliaji mpya wa Simba SC, Mkenya Paul Kiongera akishangilia moja ya mabao yake mawili katika ushindi wa 3-0 jioni ya leo kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Gor Mahia ya Kenya Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Chini ni mashabiki wa timu hiyo wakifurahia raha za Kiongera, mkali mpya wa mabao wa Msimbazi.

Vigogo wa kundi la Friends Of Simba SC, kushoto Zacharia Hans Poppe kulia Crescentius Johm Magori wakila raha Taifa leo

Mtu hatari mbele ya lango; Paul Kiongera kushoto langoni mwa Gor Mahia leo

Kocha wa Yanga SC (picha ndogo chini kushoto), Marcio Maximo kulia akiwa Msaidizi wake, Mbrazil mwenzake, Leonardo Leiva wakifuatilia mchezo wa kirafiki kati ya Simba SC na Gor Mahia ya Kenya jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Simba imeshinda 3-0. picha kubwa ni wachezaji wa Simba wakishangilia moja ya mabao yao leo

AKIWA anaijua vyema timu yake ya zamani ya Gor Mahia ya Kenya, nyota mpya wa kimataifa wa Simba ya Dar es Salaam, Raphael Muigai Kiongera 'Modo' leo ameiongoza Simba kushinda goli 3-0  katika mchezo wa kirafiki uliopigwa uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaa jioni ya leo.

Mabao ya Simba yamewekwa kimiani na nyota huyo aliyesajiliwa kutoka Gor mahia ya Kenya, Raphael Kiongera alkiingia kipindi cha pili akitokea benchi na bao moja kuwekwa wavuni na  Ramadhan Singano 'Messi'.

Simba imetoa kichapo hicho ikiongozwa na kocha wake wa mara ya tatu, Mzambia Patrick Phiri ambaye alikishusha kikosi hicho uwanja wa taifa jiji Dar es Salaam ikiwa ni takriban mwezi na siku kadhaa tangu ilipo pata kichapo cha goli 3-1 na kupelekea kutimuliwa kwa kocha Zdravko Logarusic kutoka kwa Zesco United.

Kiongera alipachika goli dakika ya 55 wakati goli la pili likifungwa dakika ya 74 na Messi na Kiongera tena kufunga hesabu katika dakika ya 78.
CRD: HABARI24

Vurugu zaibuka Kilosa, Polisi watumia mabomu kutuliza hasira wannchi

VURUGU kubwa zimezuka katika tarafa ya Magole wilayani Kilosa jana ambapo polisi ililazimika kutumia mabomu ya machozi na risasi za moto ili kuwatawanya wananchi.
Vurugu hizo zilisababishwa na wananchi wa  vijiji vitatu vya  Mabana, Mateteni na Mbigili  baada ya kuvamia eneo la Mahakama ya  Magole na kutaka kuichoma moto wakishinikiza kuachiwa kwa wenzao waliokuwa wamekamatwa.

Vurugu hizo zilitokea majira ya saa 5 asubuhi wakati wananchi hao walipokusanyika na kufanya maandamano hadi katika mahakama hiyo wakitaka wakulima wenzao 12  waliokamatwa kwa madai ya kuvamia na kulima shamba lililotengwa na serikali.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo aliyejitambulisha kwa jina moja la Rajabu, alisema kuwa chanzo cha tukio hilo ni askari polisi katika mji wa Dumila kwenda kuwakamata wakulima hao katika shamba hilo  eneo la Mkongeni ambalo zamani lilikuwa likilimwa na waliokuwa wapigania uhuru wa Afrika Kusini.

Alisema kuwa katika siku za hivi karibuni wakulima wa vijiji hivyo waliamua kuvamia na kuanza kulima bila kufanya mawasiliano na serikali wakati eneo hilo tayari lilikuwa limetengwa kwa ajili ya ujenzi wa Chuo kikuu cha Sayansi.

Alisema kuwa polisi ilifika katika eneo la shamba hilo na kukuta makundi hayo ya wakulima na ndipo likafanikiwa kuwakamata baadhi yao na kuwapeleka mahakamani kwa ajili ya kuwasomea mashtaka baada ya wengine kukimbia.

Ilidaiwa kuwa waliokimbia walienda kujikusanya katika vijiji hivyo vitatu na kufanya maandamano hadi katika mahakama hiyo na kuanza kufanya vurugu za kutaka kuchoma moto na kurushia mawe baadhi ya askari wakishinikiza kuachiwa wenzao.

Mtoa habari huyo alidai kuwa polisi walizidiwa nguvu na kulazimika kuomba msaada wa askari wengine kutoka wilaya ya Mvomero ambao walifika na kuanza kutawanya wananchi hao kwa kuwarushia mabomu ya machozi pamoja na kupiga risasi za moto hewani.

Waziri Dk Magufuli awauma sikio Wahandisi

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiKcW6NSxo6L-PGniBukjBsiqCp1veb7ms-hxdlmI9rM268bFawW1qh5L-W3bgY17po4VEAdsTUTC9L0LzIIgrQqeJ65Tz_0EH-KLAQ4sePHDJEXhCFSkwfuYzDrnI3B7h4nPd7Bkkt0QI/s1600/4-Waziri+Magufuli+akizindua+Bodi.JPG
Suleiman Msuya
WAZIRI wa Ujenzi Dk. John Magufuli amewataka wahandisi kujenga ushirikiano ili kuhakikisha kuwa wanafanikiwa katika kupata miradi mbalimbali ya ujenzi ambayo inatolewa na Serikali.
Magufuli ametoa rai wakati akifunga Mkutano wa Mwaka wa Bodi ya Wasajili ya Wahandisi (ERB)  uliofanyika jana katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.

Alisema ni vema wahandisi wote ambao wamepata usajili baada ya kula kiapo kuwa na umoja ili kuhakikisha kuwa miradi inayotolewa na serikali wanaipata kwa kutokufanya hivyo kutachangia kuikosa.

Katika mkutano huo zaidi ya wahandisi 250, wataalamu na washauri waliapa katika mkutano huo ikiwa ni baada ya kupata usajili kupitia ERB.

Waziri Magufuli alisema Serikali inaangalia uwezekano wa kuhakikisha kuwa fedha zote ambazo zinapatikana katika mfuko wa barabara zinatumika kwa kuwapatia wahandisi wa ndani ambao watapata miradi.

“Napenda kutumia nafasi hii ya kufunga mkutano huu kwa kuwaomba muungane katika baadhi ya miradi ambayo inatangazwa na serikali kama wenzenu wanaofanya kule katika daraja la Mmbutu Igunga Tabora ambao umeonyesha mafanikio makubwa”,alisema.

Dk. Magufuli alisema Wizara yake itaendelea kutoa ushirikiano wa aina yoyote ili kuhakikisha kuwa wahandisi wa Kitanzania wanafaidika na kodi zao kwa kupata zabuni ambazo watakuwa na sifa nazo.

Kwa upande wake Msajili wa (ERB) Mhandisi Stephen Mlote alisema kwa sasa jumla ya wahandisi wataalamu na washauri 13826 wamesajiliwa na makapuni 261pamoja na kula kiapo cha kazi hiyo.

Mlote alisema pia hadi kufikia sasa jumla ya wahadisi 330 wamefutiwa usajili pamoja na kampuni 32 ambazo zimeonekana kukiuka kanuni za ERB na kiapo walichoapa.

Alisema pamoja na idadi hiyo bado nchi ina kabiliwa na uchache wa wahandisi wataalamu na washauri ambapo kwa sasa ni sawa na 0.2 asilimia ya watanzania wote hali ambayo ni kinyume na nchi zilizoendelea.

Alitolea mfano nchi ya Australia ambayo ni asilimia0.4, Malaysia 0.13, Uingereza 0.8 na Japani ni asilimia 1 hivyo juhudi zinahitajika zaidi ili kuakukisha kuwa vijana wengi wanahamasishwa kusoma masomo ya sayansi.

Msajili huyo alisema ERB pia inajitahidi kuwatafutia vijana waliosoma fani ya uhandisi ajira ambapo hivi karibuni vijana 448 wameajiriwa katika taasisi mbalimbali hapa nchini.

Aidha Mlote alisema changamoto nyingine ni wahandisi kukimbia fani hiyo na kujihusisha na fani nyingine kwasababu ya kufuata maslahi mazuri ambayo yanapatikana katika sekta zingine.

Changamoto nyingine ni kuwepo kwa utamaduni wa watanzania walio wengi kutotaka kutumia wahandisi katika ujenzi jambo ambalo linawakatisha tama wahandisi kwani wajenzi hutumia mafundi wamitaani.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya ( ERB) Profesa Ninatubu Lema aliwataka wahandisi kuzingatia misingi ya kazi yao ili wawe watu wenye kuchangia uchumi wan chi kwa kazi ambazo wanazifanya.

Lema aliwataka kuzingatia mambo yafuatayo ambayo ni kuchagua, kupanga, kipaumbele, kutekeleza, kufuatilia na kutathimini wakati wanatekeleza miradi mbalimbali ya hapa nchini ili kufikia lengo la Matokeo Makubwa Sasa (BRN).

Michuano ya Walawala Cup kutimua vumbi Muheza




MASHINDANO ya kuwania Kombe la Walawala wilayani Muheza linatarajia kuanza mapema mwezi huu katika uwanja wa Jitegemee.

Mratibu wa Mashindano hayo, Omari George (OG)akizungumza mjini Dar es Salaam jana alisema maandalizi ya mashindano hayo yamekamilika ambayo ni pamoja na kuandaa vifaa vya michezo.

Alisema mashindano hayo ambayo hufanyika kila mwaka yamelenga kuibua vipaji vya wachezaji watakaochukua nafasi ya wachezaji waliowahi kuwika zamani na kujenga heshima ya wilaya Muheza kama vile Kasongo Athumani, ISsa Athumani Mgaya na James Kisaka.

OG alisema mashindano hayo ambayo hufanyika kila mwaka kutoka mwaka 2010 kila timu shiriki hupatiwa jezi na washindi hupata zawadi mbalimbali kama vile vikombe, mipira na sare za michezo.

Alisema katika mashindano ya mwaka huu kila timu imepewa jezi seti moja, sare  kwa ajili ya makocha wa timu 18 zinazoshiriki mashindano hayo, sare kwa viongozi wa Chama cha Soka Wilayani (TFF) na waamuzi watakaochezesha mashindano hayo.


Mratibu huyo alisema amekuwa akishirikiana na Kampuni ya Isere kuandaa vifaa vinabyotumika katika mashindano hayo Kutoka mashindano ya Walawala Cup yaanzishwe timu zilizowahi kutwaa ubingwa ni Polisi (2011), City Boys (2012) na Bambino (2013).

Cameroon yaua ugenini, Nigeria yafa nyumbani Afrika

http://www.africaplays.com/uploads/v7w6v6p4.jpg
Nigeria hawaamini kama walefungwa nyumbani
http://www.spotonsport.com/img/video/dr-congo-vs-cameroon-06092014.png
Cameroon wakishingailia moja ya mabao yao mjini LUbumbashi
http://static.cameroonweb.com/GHP/img/pics/48838821.295.jpg
MABAO mawili kutoka kwa wachezaji chipukizi Clinton Njie na Vincent Aboubakar walitosha kuiwezesha Cameroon kuanza kampeni zao za kuwania kwenye katika Fainali za Afrika 2015 nchini Morocco kwa kuwalaza wenyeji wa DR Congo mjini Lubumbashi katika mechi ya kundi D.
Visiting Cameroon posited a 2-0 win over DR Congo in their Group D clash on Saturday in Lubumbashi.
Mabingwa hao wa mara nne wa Afrika walipata mabao hayo katika kila kipindi na kuwapa pointi tatu muhimu ugenini katika mechi hizo za kuwania kufuzu fainali za Morocco.
Katika mechi ya kundi A Nigeria ikiwa nyumbani ilianza vibaya kampeni zake za kutetea taji lake kwa kukubali kipigo cha mabao 3-2 toka kwa Congo Brazaville na kuungaana na Sudan walionyukwa mabao 3-0 nyumbani kwao na Afrika Kusini kuburuza mkia katika kundi hilo.
Katika kundi B mechi kati ya Mali na Malawi ilishindwa kufanyika jana na kuahirishwa mpaka leo kutokana na mvua kubwa, huku Algeria ikiwa ugenini ikipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji wao Ethiopia.
Guinea ikiwa nyumbani iliishinda Togo mabao 2-1 katika mechi ya kundi E wakati Ghana ikiwa uwanja wa nyumbani ikilazimisha sare ya 1-1 na Uganda The Cranes.
Kundi C Burkina Faso iliinyoa Lesotho waliowafuata nyumbani kwaoi Ouagaoudougou na Gabon ikiilaza Angola kidude kimoja (1-0) katika mechi iliyochezwa uwanja wao wa nyumbani.
Katika mechi nyingine ya kundi D, Ivory Coast ikiwa nyumbani kwao iliisasambua majira zao Sierra Leone kwa mabao 2-1, huku katika mechi za kundi F Zambia ilitoshana nguvu na majirani zao Msumbiji kwa kutofungana na Cape Verde ikiwa ugenini iliisambaratisha Niger kwa mabao 3-1.
Mechi za kundi G, ilishuhudiwa Senegal ikiilaza Misri mabao 2-0 na  Tunisia ikiwa nyumbani ikiibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wageni wao Botswana.
Kipute cha mechi hizo za makundi zitaendelea tena siku ya Jumatano kwa kushuhudia nchi mbalimbali zikionyeshana kazi kuwania fainali hizo za mwaka 2015 zinazosubiriwa kwa hamu ni zile za Misri dhidi ya Tunisia, Cameroon na Ivory Coast na Togo na Ghana.
Ratiba kamili ya siku hiyo ni kama ifuatavyo:

Kundi A
Rwanda     v   Sudan  
Afrika Kusini vs Nigeria
Kundi B
Malawi v Ethiopia
Algeria v Mali
Kundi C
Angola v Burkina Faso
Lesotho  v Gabon
Kundi D
Cameroon v Ivory Coast
Sierra Leone v DR Congo
Kundi E
Togo v Ghana
Uganda v Guinea
Kundi F
Cape Verde v Zambia
Msumbiji v Niger
Kundi G
Misri v  Tunisia
Botswana vs Senegal

Mnyika, Makonda Polepole wawasha Moto Katiba Mpya