STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 26, 2014

Beki Coastal achekelea kuidungua Simba Taifa


Hamad Juma akichuana na Messi siku ya pambano la Coastal na Simba Taifa
MFUNGAJI wa bao pekee la Coastal Union ya Tanga lililoizamisha Simba kwenye uwanja wa Taifa, Hamad Juma anasema mpaka sasa haamini kama ni yeye aliyewalaza mapema vijana hao wa Msimbazi.
Hata hivyo beki huyo wa pembeni, aliyepandishwa kikosi cha kwanza toka timu ya vijana msimu huu, amesema anajisikia fahari kubwa kuwalaza mapema mashabiki wa Simba walioamini wangeshinda.
Akizungumza na MICHARAZO, Hamad alisema kila akikaa na kufikiria alichokifanya kwenye uwanja wa Taifa, hushindwa kujiamini kama ni yeye kutokana na ukweli wapinzani wao walisheheni nyota watupu.
Hamad alisema maamuzi aliyoyafanya mara baada ya beki wa Simba, Omar Salum kuzembea kuokoa mpira hakutarajia, lakini yaliweza kuwapa bao pekee lililoipa Coastal pointi tatu muhimu.
"Huwa nashindwa kuamini kama ni mimi niliyefunga bao lile na kuizamisha Simba, hata hivyo nashukuru kwa kusaidia Coastal na kuweka rekodi ya kuifunga timu kubwa kama ya Simba," alisema.
Alisema ushindi huo ulikuwa muhimu kwao ikizingatiwa kocha wao Yusuph Chipo aliwaamini vijana na kuwapanga katika pambano hilo timu yao ikitoka kufungwa mabao 4-0 na Azam.
Beki huyo alifunga bao hilo dakika ya 44 na kudumu hadi mwisho na kuifanya Simba ipoteze mechi ya nne katika ligi ya msimu huu na kuiacha ikibakia kwenye nafasi ya nne ya msimamo wa ligi hiyo.
Simba pia ilishapoteza mechi nyingine tatu mbele ya Azam, Mgambo JKT na JKT Ruvu na kutishia kukosa uwakilishi wa nchi kwa mara ya pili mfululizo kutokana kutanguliwa na Azam, Yanga na Mbeya City.

Yanga yaiua Prisons Taifa, Azam haishikiki

Yanga
Azam wanaozidi kuukomalia ubingwa unaoshikiliwa na Yanga
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga imezidi kufufua matumaini ya kutetea taji hilo baada ya jioni hii kuibugiza Prisons-Mbeya kwa mabao 5-0.
Pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa, lilishuhudia Yanga wakienda mapumziko wakiongoza kwa mabao 2-0.
Bao la kwanza la Yanga liliwekwa kimiani na Mganda Emmanuel Okwi kwa mkwaju wa faulo katika dakika ya 21 kabla ya Mrisho Ngassa kuongeza la pili dakika ya 38 akimalizia krosi ya Husseni Javu.
Kipindi cha pili Yanga ilicharuka na hasa baada ya kufanya mabadiliko ya wachezaji na kuweza kujiandikia bao la tatu lililofungwa dakika 68 na mtokea benchi, Hamis Kiiza 'Diego'.
Kiiza alifunga bao hilo akiuwahi mpira uliotemwa na kipa wa Prisons baada ya Simon Msuva kumimina krosi murua langoni mwa 'Wajelajela' na Mganda huyo kufunga kilaini.
Nahodha Nadir Haroub 'Cannavaro' aliiandikia Yanga bao la nne katika dakika ya 78 kwa mkwaju wa penati baada ya mabeki wa Prisons kumuangusha Husseni Javu, aliyeng'ara katika mchezo huo aliyoingia kipindi cha kwanza kuchukua nafasi ya Jerryson Tegete.
Dakika chache kabla ya kumalizika kwa pambano hilo, Kiiza kwa mara nyingine aliiongezea Yanga bao la tano baada ya Hussen Javu kufanya kazi nzuri kwa kufumua shuti langoni mwa wapinzani wao.
Kwa ushindi huo Yanga wamefikisha pointi 46 kutokana na kucheza mechi 21, wakiendelea kusalia nafasi ya pili nyuma ya Azam ambao jioni hii wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mgambo JKT katika pambano lililochezwa jijini Tanga.
taarifa toka Tanga zinasema kuwa Azam walipata mabao yake kupitia kwa John Bocco na Brian Umony na kuifanya timu hiyo kuendeleza rekodi yao ya kutopoteza mchezo wowote katika ligi ya msimu huu na kukaa kileleni wakiwa na pointi 51 licha ya kucheza mchezo 22.

Tuzo za Wanamichezo Bora Juni 27

http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2013/02/kapo4.jpg
Shomari Kapombe Mwanamichezo Bora wa 2012
 TUZO za Wanamichezo Bora Tanzania zinazotolewa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) zitafanyika Juni 27, mwaka huu katika ukumbi ambao utatajwa baadaye mjini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya tuzo, Rehure Nyaulawa amesema leo kwamba baada ya kikao cha juzi cha Kamati yake juhudi za pamoja baina ya Kamati yake na Kamati ya Utendaji kuzungumza na wadhamini mbalimbali wakubwa na wadogo kwa nia ya kufanikisha tuzo hizo zimeanza.
“Kamati yetu kwanza inawaomba radhi viongozi wa vyama vyote vya michezo kutokana na tuzo kushindwa kufanyika mwaka jana na hilo kwa mujibu wa taarifa ya uongozi wa TASWA iliyowasilishwa kwenye kikao chetu, ilitokana na sababu mbalimbali lakini kubwa ni kujitoa dakika za mwisho kwa baadhi ya kampuni zilizokuwa zimethibitisha kudhamini tuzo hizo,”. Hata hivyo, Nyaulawa ameomba wendelee kutoa ushirikiano mwaka huu na kwa kuanzia watawatumia barua rasmi za kuomba majina ya wanamichezo wao waliofanya vizuri kuanzia Januari 2013 hadi Aprili mwaka huu, ambapo matarajio yao wanamichezo wasiopungua 40 watapewa tuzo. Amesema kwamba kamati pia imeamua kwamba kila mwaka tuzo hizo zijena ujumbe maalum kwa wanamichezo, ambapo kwa kuanzia tuzo za mwaka huu ujumbe wake utakuwa ni: ‘Wanamichezo Tupige Vita Ujangili’. “Tunaamini wale wote wataowania, wale watakaoshinda tuzo hizo na wanamichezo wote wakiwemo waandishi wa habari za michezo tutashirikiana na jamii kwa ujumla kwa kuwa mstari wa mbele kuhamasisha vita dhidi ya ujangili kwa namna tutakavyomudu,”amesema. Amesema pia katika kuhakikisha tuzo za mwaka huu zinakuwa bora kwa maslahi ya wanamichezo wote hapa nchini, kamati imeteua baadhi ya viongozi wa kiserikali kuwa washauri wa kamati katika masuala mbalimbali na sasa wanasubiri majibu yao ili waweze kuwatangaza rasmi.

29 waanza kambi ya Stars marekebisho Tukuyu


Na Mwandishi maalumu, Tukuyu
WACHEZAJI 29 kati ya 34 waliochaguliwa katika programu maalumu ya marekebisho ya timu ya Taifa inayoendeshwa na TFF wameshaanza mazoezi makali katika Wilaya ya Rungwe, Mbeya.

Wachezaji hao, ambao wametokea katika mikoa mabali mbali, waliingia kambini siku ya Jumamosi huku wakiongozwa na Mwalimu Salum Mayanga akisaidiwa na Patrick Mwagata, ambaye ni kocha wa makipa, Meja Joakim Mashanga ambaye ni daktari wa team na Fred Chimela ambaye ni Meneja Vifaa.


Timu ya Taifa, Taifa stars, inayodhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager kwa mwaka wa pili mfululizo sasa, inatarajiwa kupata mabadiliko makubwa sana ndani ya miezi miwili ijayo ili ipatikane timu bora itakayoshiriki katika mechi za kufuzu kupata tiketi ya kucheza Kombe la Afrika.

Mashetani Wekundu wafa tena, Arsenal yabanwa Everton yapeta

Edin Dzeko
Edin Dzeko akiwatungua Manchester United
Wilfried Bony
Hekaheka langoni mwa Arsenal

Everton's Ross Barkley
Shhhhh!
  JAHAZI la Manchester United limezidi kuzama baada ya usiku wa kuamkia leo kukandikwa mabao 3-0 kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Old Trafford na mahasimu wao wa jiji la Manchester, Manchester City.
Mabao ya Edin Dzeko aliyefunga mawili katika sekundu chache baada ya kuanza kwa mchezo huo na jingine la dakika 26 na lile la Yaya Toure dakika za 'jioni' yaliwafanya vijana wa David Moyes kushindwa kujua wamekumbwa na nini msimu huu.
Ushindi huo umeipeleka City hadi nafasi ya pili ikiiengua Liverpool itakayoshuka dimbani leo kuumana na Sunderland, kutokana na kufikisha pointi 66 baada ya kucheza mechi 29, mechi mbili pungufu na vinara wa ligi hiyo Chelsea wanaoongoza wakiwa na pointi 69.
Katika mechi nyingine, Arsenal ikiwa nyumbani ilinyang'anywa tonge mdomoni baada ya kulazimishwa sare ya 2-2 na Swansea City kwenye uwanja wa Emirates.
Wageni walitangulia kupata bao dakika ya 11 kupitia kwa Wilfried Bony kabla ya wenyeji kuja kusawazisha katika kipindi cha pili kupitia kwa Lucas Podolski katika dakika ya 73 na kuongeza jingine kupitia kwa Olivier Giroud.
Hata hivyo wakati Arsenal ikijiandaa kushangilia ushindi mchezaji wake Mathieu Flamini alijifunga katika harakati za kuokoa shambulizi langoni mwake na kuwapa sare Swansea na kugawa pointi moja moja.
Nao Everton wakiwa ugenini waliwaduwaza wenyeji wao Newcastle Utd kwa kuwakandika mabao 3-0, mabao yaliyowekwa kimiani na Barkley, Lukaku na Osman.
Kwa ushindi huo umeifanya Everton kufikisha pointi 57 na kupanda nafasi ya tano na kuishusha Tottenham Hotspur yenye pointi 56 ambayo inarudi katika nafasi ya sita.
Kivumbi cha ligi hiyo kitaendelea tena usiku wa leo kwa michezo miwili, Liverpool itakayoumana na Sunderland na West Ham Utd itaikaribisha Hull City.

Bayern Munich nouma yatetea taji Ujerumani kwa aina yake

 http://www.sportsarena.com.sg/di/library/omnisport/11/68/bayernmunich_1um7biac60yco14kixp752v0gm.jpg?t=-616441876w=570

MABINGWA watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Bayern Munich imefanikiwa kutetea taji lake la Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) usiku wa jana baada ya kuwafunga Hertha Berlin kwa mabao 3-1.
Watetezi hao wametwaa taji hilo la 23 wakiwa wameshinda mechi 10 mfululizo na pia wakiwa wamecheza mechi 52 ya mashindano yote bila kupoteza.
Mabo ya washindi katika pambano hilo lililochezwa mjini Berlin, yalifungwa na  Toni Kroos, Mario Goetze na Frank Ribery na kuifanya Bavarians kunyakua taji hilo ikiwa na mechi saba mkononi kabla ya kumaliza msimu wa Bundesliga.