STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, March 26, 2014

Tuzo za Wanamichezo Bora Juni 27

http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2013/02/kapo4.jpg
Shomari Kapombe Mwanamichezo Bora wa 2012
 TUZO za Wanamichezo Bora Tanzania zinazotolewa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) zitafanyika Juni 27, mwaka huu katika ukumbi ambao utatajwa baadaye mjini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya tuzo, Rehure Nyaulawa amesema leo kwamba baada ya kikao cha juzi cha Kamati yake juhudi za pamoja baina ya Kamati yake na Kamati ya Utendaji kuzungumza na wadhamini mbalimbali wakubwa na wadogo kwa nia ya kufanikisha tuzo hizo zimeanza.
“Kamati yetu kwanza inawaomba radhi viongozi wa vyama vyote vya michezo kutokana na tuzo kushindwa kufanyika mwaka jana na hilo kwa mujibu wa taarifa ya uongozi wa TASWA iliyowasilishwa kwenye kikao chetu, ilitokana na sababu mbalimbali lakini kubwa ni kujitoa dakika za mwisho kwa baadhi ya kampuni zilizokuwa zimethibitisha kudhamini tuzo hizo,”. Hata hivyo, Nyaulawa ameomba wendelee kutoa ushirikiano mwaka huu na kwa kuanzia watawatumia barua rasmi za kuomba majina ya wanamichezo wao waliofanya vizuri kuanzia Januari 2013 hadi Aprili mwaka huu, ambapo matarajio yao wanamichezo wasiopungua 40 watapewa tuzo. Amesema kwamba kamati pia imeamua kwamba kila mwaka tuzo hizo zijena ujumbe maalum kwa wanamichezo, ambapo kwa kuanzia tuzo za mwaka huu ujumbe wake utakuwa ni: ‘Wanamichezo Tupige Vita Ujangili’. “Tunaamini wale wote wataowania, wale watakaoshinda tuzo hizo na wanamichezo wote wakiwemo waandishi wa habari za michezo tutashirikiana na jamii kwa ujumla kwa kuwa mstari wa mbele kuhamasisha vita dhidi ya ujangili kwa namna tutakavyomudu,”amesema. Amesema pia katika kuhakikisha tuzo za mwaka huu zinakuwa bora kwa maslahi ya wanamichezo wote hapa nchini, kamati imeteua baadhi ya viongozi wa kiserikali kuwa washauri wa kamati katika masuala mbalimbali na sasa wanasubiri majibu yao ili waweze kuwatangaza rasmi.

No comments:

Post a Comment