STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, April 23, 2013

Game ya Golden Bush, Wahenga sasa kupigwa Kinesi


Wahenga FC
Golden Bush

PAMBANO la kukata na mudnu kati ya mahasimu wawili wa soka la maveterani jijini Dar es Salaam, Golden Bush Veterani na Wahenga FC lililokuwa limepangwa kuchezwa kwenye uwanja wa TP Afrika, Sinza, limehamishiwa uwanja wa Kinesi, Ubungo.
Sababu za kuhamishwa kwa pambano hilo litakalofanyika siku ya Ijumaa wakati watanzania wakiadhimisha miaka 49 na Muungano, ni kutokana na uwanja huo maarufu kama 'Nangwanda Sijaona' kujaa maji ya mvua zinazoendelea kunyesha na sasa utapigwa Kinesi unaofahamika zaidi kama 'St James Park Stadium'.
Msemaji wa Golden Bush, Onesmo Waziri 'Ticotico' alitoa taarifa hiyo ya kuhamishwa kwa pambajo hilo toka uwanja wa TP hadi Kinesi muda mchacxhe uliopita akisisitiza kuwa, wamepania kuwaumbua wapinzani wao ambao walipokutana nao mara ya mwisho waliwanyuka mabao 2-1 mbele ya kamanda Thobias Andengenye.
"Kwa wale wenye nia ya kuja kushuhudia pambano hilo la kukata na shoka wafike Kinesi, kutokana na uwanja wa awali tuliokuwa tupambane kujaa maji ya mvua," alisema Ticotico mmoja wa washumbuliaji wa timu hiyo.
Ticotico alisema mechi hiyo itaanza majira ya saa 10 jioni na huenda ikachezeshwa na nyota wa zamani wa Yanga na Taifa Stars, Ally Mayay Tembele.

African Lyon kujishusha daraja kesho kwa JKT Ruvu?

 
African Lyon

JKT Ruvu

Na Boniface Wambura
LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara itaendelea tena kesho (Aprili 24 mwaka huu) kwa mechi moja kati ya wenyeji African Lyon dhidi ya maafande wa JKT Ruvu.
Mechi hiyo namba 165 itachezwa Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam chini ya usimamizi wa Kamishna Hamisi Kisiwa wa Dar es Salaam. Waamuzi wa mechi hiyo itakayoanza saa 10 kamili jioni ni Hashim Abdallah, Omari Kambangwa, Abdallah Selega na Said Ndege wote wa Dar es Salaam.
Lyon inahitajika kushinda pambano hilo angalau kufufua matumaini ya kusalia msimu ujao ujao, lakini matokeo yoyote kinyume na ushindi ni kujitia muhuri wa kucheza Ligi Daraja la Kwanza msimu ujao.
Timu hiyo inayoburuza mkia wa msimamo wa ligi hiyo na pointi 19 tu ikilingana na Polisi Moro, na ushindi pekee ndiyo utawaondoa kwenye janga la kurudi 'mchangani'.
Hata hivyo JKT Ruvu wanaouguza kipigo cha mabao 3-0 toka kwa vinara wa ligi hiyo, Yanga nayo haipo katika nafasi nzuri na kupoteza mchezo wa kesho itamaanisha kwamba nao wanajiweka kuelekea kwenye FDL.
Maafande hao wana pointi 23 na wamesaliwa na mechi tatu, hivyo matokeo yoyote mabaya kwao yataweka bapaya kama ilivyo kwa Lyon na hivyo kufanya pambano hilo kuwa kama vita baada ya 'wanyonge' hao wawili waliopo maeneo ya mkiani.

Kim Poulsen amkumbuka Barthez Stars


Kocha Kim Poulsen

Ally Mustafa 'Barthez'
Na Boniface Wambura
KOCHA wa Taifa Stars, Kim Poulsen ametangaza timu ya pili ya Taifa (Young Taifa Stars) atakayoitumia kuangalia wachezaji ambao baadaye anaweza kuwajumuisha kwenye timu ya wakubwa, akimkumbuka kipa wa Yanga Ally Mustafa Barthez.

Akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo (Aprili 23 mwaka huu) kabla ya kutaja kikosi hicho, Kim amesema timu hiyo ni sehemu ya Mpango wa Maendeleo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) uliozinduliwa Aprili 4 mwaka huu ukilenga kuendeleza wachezaji.

Amesema timu hiyo inajumuisha wachezaji ambao wamepita umri wa kuchezea timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) na wakubwa ambao hawajapata fursa ya kuingia Taifa Stars, lakini atatumia Young Taifa Stars kuangalia uwezo wao.

“Timu hii ni kiungo kati ya vijana na wakubwa. Wengi wa wachezaji watakuwa vijana, lakini wakubwa wachache watapata fursa ya kuwemo ili kuangalia uwezo wao hata kama uko nyuma waliwahi kuchezea Taifa Stars. Lakini timu hii vilevile ni changamoto wa wachezaji wa Taifa Stars kuwa wapo wanaosubiri wazembee ili wachukue nafasi zao,” amesema.

Young Taifa Stars yenye wachezaji 30 itakuwa na kambi ya siku tano jijini Dar es Salaam kuanzia Mei 2 hadi 6 mwaka huu.

Wachezaji walioitwa ni Aishi Manula (Azam), Hussein Shariff (Mtibwa Sugar) na Ali Mustapha (Yanga) ambao ni makipa. Mabeki ni Kessy Hassan (Mtibwa Sugar), Kennan Ngoma (Barnsley FC, Uingereza), Himid Mao (Azam), Ismail Gambo (Azam), David Mwantika (Azam), Miraji Adam (Simba), Mohamed Hussein (Kagera Sugar), Waziri Salum (Azam), Samih Nuhu (Azam) na Emily Mgeta (Simba).

Viungo ni Haruna Chanongo (Simba), Edward Christopher (Simba), Mudathiri Yahya (Azam), William Lucian (Simba), Jonas Mkude (Simba), Hassan Dilunga (Ruvu Shooting), Jimmy Shoji (JKT Ruvu), Abdallah Seseme (Simba), Ramadhan Singano (Simba), Farid Mussa (Azam) na Vicent Barnabas (Mtibwa Sugar).

Washambuliaji ni Hussein Javu (Mtibwa Sugar), Jerome Lambele (Ashanti United), Zahoro Pazi (JKT Ruvu), Twaha Hussein (Coastal Union), Abdallah Karihe (Azam) na Juma Luizio (Mtibwa Sugar).

Robin van Persie aibebesha Man Utd taji la 20, mpiku Suarez

One hand on the trophy: Van Persie celebrates scoring his hat-trick goal after 33 minutes
Van Persie akishangilia bao lake la tatu jana usiku
Credit where it's due: Van Persie picks Wayne Rooney up after he picked the Dutchman out for his wonder goal
Wachezaji wa Manchester United wakishangilisi ushindi wao jana baada ya kuinyuka Aston Villa mabao 3-0 na kutwaa ubingwa wa 20 wa Ligi Kuu ya England

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Uholanzi, Robin van Persie jana usiku aliwezesha klabu yake ya Manchester United kutwaa taji la 20 la Ligi Kuu ya England, huku mwenyewe akiondoa 'gundu' na kumpikua Luis Suarez katika orodha ya wafungaji.
Mkali huyo alifunga mabao yote matatu yaliyoizamisha Aston Villa kwenye uwanja wa Old Trafford kwa kipigo cha mabao 3-0.
Van Persie aliyafunga mabao hayo katika dakika 33 tu ya pambano hilo na kuihakikisha Man United kuivua taji mahasimu wao Manchester City, huku akikwea kwenye kilele cha wafungaji akimzidi Suarez kwa bao moja zaidi akiwa na mabao 24.
Mholanzi huyo ambaye alikuwa na Arsenal kwa misimu kadhaa bila kuonja ladha ya kutwaa taji lolote, alianza makeke yake dakika ya pili ya mchezo huo akimalizia pasi ya Ryan Giggs.
Van Persie aliongeza bao la pili dakika ya 13 akimalizia kazi ya Wayne Rooney aliyekuwa akicheza mechi yake ya 400 akiwa na Man United kabla ya kumalizia udhia kwa kufunga bao la tatu dakiika ya 33 akiwezeshwa tena na Giggs.
Man United imetwaa taji hilo la 20 na kupikua rekodi ya Liverpool waliowakamata mwaka jana kwa kulingana nao kutwa aubingwa mara 19 wakiwa bado wamesaliwa na mechi nne mkononi.

Mariam Mndeme: Mwanahabari, muigizaji aliyewageukia walemavu

Mamuu akiwa na Baby Madaha
MWENYEWE anasema japo hana muda mrefu tangu ajitose kwenye fani ya uigizaji akiiweka kando taaluma yake ya uanahabari, lakini anashukuru fani hiyo imempa mafanikio makubwa ya kujivunia ambayo yanazidi kumtia nguvu ili asonge mbele zaidi.
Mariam Khamis Mndeme maarufu kama 'Mamuu', mmoja wa waigizaji wanaozidi kujua juu nchini kutokana na kipaji kikubwa alichonacho katika fani hiyo aliyoanza kuitumikia tangu akiwa kinda, anasema wala hajutii kujitosa kwenye fani hiyo aliyoipenda tangu alipokuwa kinda.
Msanii huyo aliyewahi kuwa mtangazaji wa TBC na kuyaandikia magazeti ya Global Publishers, anasema mbali na kufahamiana na kupata rafiki wengi, fani ya uigizaji imemfanya pia amudu maisha kwa kujiingizia kipato na kupanua upeo wake kiakili na kisanii.
Mariam anasema kupanuka kwake kisanii ndiko kulikomfanya afyatue filamu zake binafsi mbili za 'Pooja' na 'Tatakoa' badala ya kuendelea kuzitumikia kazi za wengine, japo anakiri kwamba safari yake kuyaendea mafanikio zaidi bado ni ndefu kwa malengo aliyojiwekea ya kujitangaza kimataifa.
"Siyo siri fani ya uigizaji imenisaidia kwa mengi kiuchumi na kimaisha kwa ujumla, kwani mbali na kuyamudu maisha pia niliwahi kumiliki Pub iliyokuwa ikiitwa Mamushka kabla ya kuachana na biashara hiyo na kujikita kwenye shughuli nyingine ninazoendelea nazo kwa sasa," anasema.
Anasema baada ya kupakua filamu yake binafsi ya kwanza iitwayo 'Pooja' kwa sasa amekamilisha kazi nyingine iitwayo 'Tatakoa' ambayo anajiandaa kuitoa hadharani hivi karibuni huku akijiandaa kuondoka nchini kwa ziara ya karibu mwezi mzima katika nchi nne tofauti za Afrika.
Ziara hiyo ataifanya mwezi ujao kwenda katika nchi za DR Congo, Zimbabwe, Angola na Msumbaji kwa ajili ya maonyesho ya muziki na filamu ambapo yeye ataenda kama mratibu, lakini pia akishirikiana na wasanii atakaoambatana nao akiwamo Baby Madaha.

Mamuu katikati nyuma akiwa na wasanii wenzake walipokuwa wakirekodi filamu ya Tatakoa

KAOLE
Mariam  aliyezaliwa mwaka 1980 akiwa  mtoto wa nne kati ya watano wa familia yao yenye asili ya kabila la Kipare, anasema sanaa ya maigizo aliipenda tangu akiwa mdogo akivutiwa zaidi na kundi la 'Mambo Hayo' kabla ya mwenyewe kuja kujitosa rasmi miaka ya katikati ya 2000.
Anasema pamoja na kuonyesha kipaji shule, lakini alikidhirisha alipojiunga na kundi la Kaole Sanaa kabla ya kujitosa jumla kwenye filamu hasa baada ya kuhitimu Stashahada yake ya Habari aliyoipata kupitia katika Chuo cha DSJ, akishiriki kazi mbalimbali zilizomtangaza vyema.
Baadhi ya filamu alizocheza kisura huyo anayependa kula chakula chochote kizuri na kunywa juisi halisi na bia kidogo, ni pamoja na 'Bestfriend',  'Fake Pastor', kabla ya kutoa filamu binafsi ya 'Pooja' aliyoitaja kama bora kwake,kisha kufuatiwa na 'Dirty Game', 'Ghost Love' na sasa 'Tatakoa'.
Shabiki huyo wa klabu za Simba na Manchester United, nanayechizishwa na rangi nyeusi, njano na nyekundu, anasema hakuna tukio la furaha kwake kama alipotengeneza filamu zake binafsi za Pooja na Tatakoa na kuhuzunishwa na vifo vya babu na baba mzazi vilivyotokea kwa nyakati tofauti.
"Siyo siri nilikuwa nampenda sana babu yangu kipenzi Mzee Msinga, kifo chake kiliniumiza na kinaniuma mpaka sasa kama kilivyokuwa cha baba yangu mzazi," anasema.



Mamuu (kushoto) akiwa na wasanii wenzake
WALEMAVU
Mariam ambaye hajaolewa japo tayari anaye mtoto wa kiume aitwaye Steve Moses, anasema pamoja na mipango ya kuliteka soko la filamu nchini na kujitangaza kimataifa, akiota ndoto za kuja  kumiliki kampuni ya kuzalisha filamu na kusaidia chipukizi wwnye vipaji, pia anatarajia kunzishaa kipindi maalum cha runinga kwa ajili ya kuwasaidia watoto walemavu wakiwamo maalbino.
Kimwana huyo, mchumba wa kijana aitwaye 'D', anasema kipindi hicho kitawamulika na kuripoti taarifa mbalimbali za watoto walemavu na maalbino wanaoishi maeneo ya vijijini ambao wamepoteza matumaini kutokana na hali walizonazo na kusahauliwa na jamii.
Anasema kusudio kubwa la kipindi hicho mbali na kufungua milango ya kuwasaidia, pia kina lengo la kuwatia nguvu na kuwapa matumaini kutokana na hali ya kukata tamaa kutokana na maisha wanayoishi na kuathiriwa na hali alizonazo  hasa maalbino ambao wamekuwa wakiuwawa.
"Natarajia kuja na kipindi maalum cha runinga kwa ajili ya kufichua maovu wanayofanyiwa walemavu na hasa wenye matatizo ya ngozi, kitakuwa maalum cha kuwatia moyo na kufungua milango ya kusaidiwa na jamii, ili wafarijike na kuishi kwa uhuru kama watu wengine," anasema.
Mariam anasema kipindi chake hicho ambacho hajajua kitarushwa katika kituo gani, kinawezeshwa kwa msaada mkubwa wa mmoja wa Mawaziri wa Serikali ya Awamu ya Nne ambaye hakupenda kumtaja jina kwa sasa, pamoja na Wema Isaac Sepetu, muigizaji anayemzimia na mmoja wa wasanii wanaojitolea kuwasaidia wenzake kwa hali na mali.

Mamuu akipozi kwa kusoma gazeti
"Ninapigwa tafu na watu hao wawili yaani Mhe Waziri na Wema Sepetu ndiyo wanaonipiga tafu, ili kufanikisha mipango ya kipindi hicho maalum cha kuwasaidia walemavu," anasema Mariam.
Mariam anawataka wasanii wenzake kupendana, kushirikiana na kuwa wabunifu ili kufanya kazi ziwe na soko la uhakika ndani na nje ya nchi, huku akiwashauri kupenda kujaribu kutoa kazi zao binafsi badala ya kuendelea kutumikishwa tu.
Msanii huyo ambaye anayeiomba serikali kuwapa sapoti wasanii ili waweze kusonga mbele na kunufaika na fani yao, anasema kama asingekuwa muigizaji au mwanahabari, angejishughulishana biashara, fani anayoifanya hata sasa wakati akiendelea na fani yake ya uigizaji.

Vita ya Dunia Bayern na Barca Ligi ya Mabingwas Ulaya


MUNICH, Ujerumani
KOCHA Pep Guardiola siyo peke yake anayechukuliwa kuwa ni kiunganishi kati ya Bayern Munich na Barcelona, ambazo zinakutana leo katika mechi yao ya kwanza ya nusu fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwenye Uwanja wa Allianz Arena nchini Ujerumani.
Timu zote mbili zinatawala katika ligi kuu zao, zimetwaa mataji ya Ulaya mara nne kila moja, zina ushindani mkali dhidi ya Real Madrid, na pia zote zimewahi kufundishwa na kocha mwenye majivuno, Mholanzi Louis van Gaal.
Zote pia zimewahi kufika fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya mara mbili katika miaka minne iliyopita, ingawa Barca walitwaa ubingwa katika fainali hizo na Bayern wakiambulia patupu.
Barcelona wako kileleni mwa msimamo wa La Liga, Ligi Kuu ya Hispania kwa tofauti ya pointi 13, lakini bado wanapewa nafasi ndogo ya kushinda dhidi ya 'wauaji' Bayern, ambao walishatwaa taji la Bundesliga, Ligi Kuu ya Ujerumani wiki mbili zilizopita na kupata ushindi mnono wa mabao 6-1 katika kila mchezo miongoni mwa mechi mbili zilizofuatia, tena wakitumia wachezaji wao wengi wa akiba.
"Wachezaji wanafurahia soka lao, na tuko katika hali nzuri sana. Kila mmoja amehamasika, tunacheza soka lenye pasi za kuvutia, tunaonyesha nidhamu ya hali ya juu, na tunatengeneza nafasi nyingi za kufunga magoli," alisema kocha Jupp Heynckes baada ya ushindi wao wa 6-1 dhidi ya Hanover 96 Jumamosi.
"Kwa mara nyingine tena, wachezaji wameonyesha kwamba hatuna timu ya kikosi B, tuna kikosi A tupu."
Ubabe wa Barcelona katika La Liga umeibua madai kutoka kwenye vyombo vya habari vya Madrid kwamba sasa imekuwa ni kawaida yao na kwamba hawatashangilia kwa kutwaa ubingwa msimu huu.
"Inaelekea kuna watu wanataka kuonyesha kwamba ubingwa wa ligi kuu ya Hispania si lolote, lakini hilo si la kweli, ni taji muhimu sana," alisema kiungo wa Barca, Cesc Fabregas.
Bayern wanaamini kwamba uchezaji wao na sera zao katika kuinua vipaji vya wazawa vinawafanya walingane kwa kila hali na Barcelona na hicho ndicho kilichowafanya wamtwae Guardiola, ambaye aliondoka Barca mwisho wa msimu uliopita ili aanze kuwaongoza kuanzia msimu ujao.
Rais wa Bayern, Uli Hoeness, alifichua hivi karibuni kwamba Bayern walianza mazungumzo na Guardiola kwa muda mrefu kabla hajawakubalia Januari.
"Nilihisi kitambo kwamba Bayern ni klabu ambayo inafanana sana katika masuala ya soka na Barcelona, kwahiyo haikuwa kazi kubwa kumshawishi," alisema Hoeness.
Cha kushangaza, hadi sasa kumekuwa na mechi sita tu zilizowahi kuwakutanisha Barcelona na Bayern, ambao watawakosa nyota wao Mario Mandzukic anayetumikia adhabu na majeruhi Toni Kroos.
Katika mechi yao ya mwisho iliyokuwa ya robo fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya miaka minne iliyopita, ilichezwa wakati Bayern ikiongozwa na kocha Juergen Klinsmann na katika mechi yao ya kwanza, Barca ilishinda
4-0 kwa mabao ya kipindi cha kwanza na katika marudiano, walifungana 1-1.
"Naikumbuka sana mechi ile na sitaki kuifikiria kwa sababu ilikuwa ikituumiza sana kuitazama," alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Bayern, Karl-Heinz Rummenigge.
"Hata hivyo, sasa ni fursa nzuri kwetu kuonyesha kuwa tumeimarika."
Barcelona watawakosa majeruhi Javier Mascherano na Carles Puyol, hivyo kumuacha kocha Jordi Roura akiumiza kichwa ampange mchezaji gani wa kuanza kikosini na Gerard Pique katika nafasi ya ulinzi wa kati.

Vikosi vinavyotarajiwa leo:
Bayern Munich: Manuel Neuer; Philipp Lahm, Daniel van Buyten, Dante, David Alaba; Bastian Schweinsteiger, Javi Martinez; Thomas Mueller, Franck Ribery, Arjen Robben na Mario Gomez
Barcelona: Victor Valdes; Daniel Alves, Gerard Pique, Eric Abidal, Jordi Alba; Xavi, Sergio Busquets, Andres Iniesta; Alexis Sanchez, Lionel Messi na Pedro
.
------





Yanga kutetea taji lake la Kagame Ethiopia

Yanga walipokuwa wakishangilia taji lao la Kagame mwaka jana

MASHINDANO ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati maarufu Kombe la Kagame mwaka huu yanatarajiwa kufanyika Juni jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Mabingwa watetezi wa michuano hiyo ni vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga ambao watataka kuweka rekodi ya kutwaa kimoja taji hilo iwapo watafanikiwa kulitetea mwaka huu.
Yanga ilitwaa taji hilo mara mbili mfululizo michuano hiyo ikifanyika Tanzania kwa kuwalaza Simba kwa  bao 1-0 katika fainali za mwaka juzi na mwaka jana waliizima Azam kwa 2-1.
Hata hivyo, Shirikisho la Soka la Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) limesema kwamba mashindano hayo yanaweza kufanyika katika nchi nyingine itakayokuwa tayari kufuatia Ethiopia kueleza katika barua yao kwamba wanataka michuano hiyo ifanyike mwezi Septemba.
Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye, aliiambia NIPASHE kwa njia ya simu kuwa bado suala la udhamini wa michuano hiyo limekuwa tatizo na ndiyo maana wanashindwa kueleza wazi mikakati ya michuano hiyo ya mwaka huu.
Musonye alisema kwamba ili mashindano hayo yafanyike katika ubora wake wa kimataifa, CECAFA inahitaji kiasi cha Dola milioni moja za Marekani.
"Tuko katika kutafuta wadhamini na hadi kufikia mwisho wa mwezi huu tutajua ni nani hasa atakuwa mwenyeji wa michuano hii kwa kuthibitisha kwamba ataweza kuhudumia mahitaji yanayotakiwa. Uenyeji kwa sasa ni wa Ethiopia japo michuano inaweza pia kuhamishiwa katika nchi nyingine," alisema Musonye.
Aliongeza kuwa mashindano ya Kombe la Kagame ni muhimu katika ukanda huu na hayatafanyika zaidi ya mwezi Julai hivyo kama mwenyeji atashindwa kuwa tayari kwa muda huo, michuano inaweza kuhamishwa huku wakiendelea kusaka wadhamini.
Awali nchi za Sudan na Rwanda ziliandika barua ya kuomba kuwa wenyeji wa michuano hiyo ya kila mwaka lakini bado vyama vya soka vya nchi hizo havijathibitisha kama vimeshapata udhamini wa kusaidia gharama za maandalizi.
Yanga ndiyo bingwa mtetezi wa michuano hiyo ambapo pia mwaka huu Simba itashiriki kutokana na kuwa bingwa wa Tanzania Bara msimu uliopita.

CHANZO:NIPASHE


Ibrahim Mostafa wa Misri achiumba mkwara IBF Afrika



     Boxer Ibrahim Mostafa in many boxing poses
            
 
 
  
 
         Gottlieb Ndokosho (left) clubbing an opponent
EGYPTIAN  hard puncher and most feared boxer Ibrahim "Butcher" Mostafa has vowed to take the "IBF Africa, Middle East & Persian Gulf (IBF AMEPG) Title" away from the current champion, the flamboyant and stylish boxer Gottlieb Ndokosho of Namibia.

Boxer Mostafa, trained and managed by Richard Nwoba of Luoaa Boxing Promotions, a company incorporated in Cairo, Egypt goes to the forthcoming tournament with a record of 13 wins (KO 6) + lost 4 (KO 2) + drawn 2 = 19 record against 12 wins (KO 3) + lost 3 (KO 1) + drawn 0 = 16 for champion Ndokosho. This is one tournament which is been waited with keen interests by both Namibian and Egyptian boxing stakeholders.

Raised at Giza in the ouskirt of of Cairo the capital city of Egypt, Ibrahim Mostafa's name is a boxing power house in Egyptian boxing fraternity. It is only natural that many Egyptians in their thousands are expected to chart planes from Cairo and Alexandria to watch the tournament slated for June 15, 2013 in Windhoek, Namibia.

The tournament will be promoted by Kinda Boxing Promotions a company with lots of experience and synonymous with professional boxing in Namibia managed by Mr. Kinda Nangolo of Namibia who doubles as the manage/promoter of the current "IBF World Youth Jr. Lightweight Champion" Albinus Felesianu.

This will be the first defense for Ndokosho since winning the title last year by beating Tanzania slugger, Rajabu Maoja in less than one minute in their first round duel. Many boxing fans in Namibia are waiting for this D-Day in June 15, 2013 and fill the venue at SPW Country Club in Windhoek, ready to cheer  their beloved boxer Nokosho to victory.