STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, March 25, 2014

Watatu wadakwa na 'unga', nyara za TTCL Lindi

Kamanda wa Polisi mkoa wa Lindi,Kamishna msaidizi Renatha Mzinga
Watuhumiwa wakiwa mikononi mwa polisi
Waya zilizokamatwa kwa mtuhumiwa Abdul Mahamud ambazo zimeyeyushwa zinasadikiwa kuwa za kampuni ya simu(TTCL)
..Baadhi ya madawa waliyokamatwa kwa Mtuhumiwa Salum Shaban Mapande
Na Abdulaziz Video, Lindi 
WATU watatu wanashikiliwa na Polisi Mkoani Lindi kwa tuhuma za kukutwa  na madawa ya kulevya aina ya heroin pamoja na Miundo mbinu ya Kampuni ya simu (TTCL) kinyume na Sheria.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Kamishna msaidizi Renatha Mzinga amesema leo kuwa kwa ushirikiano mkubwa waliopewa na wanajamii wamefanikiwa kumkamata Bw Salum Shaban Mapande(32)Mkazi wa Dar es sallam akiwa na madawa ya kulevya kete 42 kubwa na ndogo 104 zenye uzito wa Gram 58 na pesa taslim tsh 2,827,500 zinazosadikika kuwa za mauzo ya madawa hayo 
Watuhumiwa wengine waliokamatwa ni pamoja na mwanafunzi wa Chuo cha Utalii mjini Lindi, Masudi Mohamed(19) aliyekutwa na kete 35 za bangi huku Abdul Mahamud na Halfan Salum waliokutwa na nyaya za kampuni ya simu TTCL Zenye Uzito wa kg 5.
Kamanda Mzinga alisema mkoa wa Lindi umeanza kampeni kubwa ya kupambana na uhalifu mbalimbali ikiwemo kupambana na wimbi la uingizaji na uuzaji wa madawa ya kulevya ambalo kwa sasa kuna ongezeko kubwa la utumiaji na uuzaji wa madawa hayo ikiwemo pombe haramu ya gongo.
Aidha Kamanda Mzinga ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa huo kujidhatiti na kufichua wahalifu wakiwemo wauza madawa ya kulevya ambapo Jeshi lake litatoa ushirikiano na usiri kwa watakaotoa taarifa zinazoashiria Uvunjifu wa Amani ikiwemo za Usalama barabarani.
Matukio na Vijana

Breaking Newz: RC Mara aanguka ghafla na kufariki

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhbPVGH0kLaqzzGwCgm726E5L95gHbG_mDaef9wmO82-Q0lpd1-mOyWXZ-PTlBEmDNHjqlcBi-15RKMB5mT_SvjzOsI_90ppINqe6gajrvEnYGTbIMpHcghInX30rtWkznYVf7xkMZyr2hC/s640/Sensa%2010.jpg
RC Tupa (aliyesimama) enzi za uhai wake
HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Mkuu wa Mkoa (RC) wa Mara, John Tupa ameanguka ghafla na kutokwa na povu wakati akitoka nje ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya (DC) Tarime kuelekea kupanda gari yake tayari kuanza ziara ya Tarime.
taarifa hizo zinasema kuwa, RC huyo aliwahishwa hospitali ya Wilaya, lakini kwa bahati mbaya amepoteza uhai wake.
Tunaendelea kufuatilia na tutawafahamisha zaidi...!
MICHARAZO inawapa pole ndugu, jamaa na familia nzima ya Rc Tupa kwa msiba huo...Kwa Hakika Kila Nafsi Itaonja Mauti...BWANA Ametoa na Yeye Ametwaa Jina Lake Lihimidiwe.

TFF yataka majina mabingwa wa mikoa kabla ya Machi 30


SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) linavikumbusha vyama vya mpira wa miguu vya mikoa kuwa vinatakiwa kuwasilisha majina ya mabingwa wao kufikia Machi 30 mwaka huu.
Majina ya mabingwa yanatakiwa kuwasilishwa pamoja na usajili wa wachezaji waliotumika kwenye ligi ya mkoa. Kila klabu inaruhusiwa kuongeza wachezaji watano kutoka ndani ya mkoa husika, ambapo unatakiwa uthibitisho wa usajili huo.
Mpaka sasa ni vyama viwili tu ndivyo vimeshawasilisha mabingwa wao. 
Vyama hivyo ni Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA) ambapo bingwa wake ni Kiluvya United, na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Lindi (LIREFA) ambapo bingwa ni Kariakoo SC.

Kalapina atoa mpya kiulayaulaya

Karama Masoud 'Kalapina' akionyesha manjonjo yake jukwaani
NYOTA wa muziki wa Hip Hip nchini, Karama Masoud 'Kalapina' amefyatua 'single' mpya  iitwayo 'Hip Hop is Alive' aliomshirikisha msanii  'Q Chilla' ambayo anatarajia kuuachia rasmi kesho.
Akizungumza na MICHARAZO, Kalapina anayetoka kundi la Kikosi cha Mizinga alisema wimbo huo umerekodiwa katika studio za Rubby Records chini ya mtayarishaji wake Jallaman.
Kalapina alisema tofauti na alivyozoeleka kuimba hip hip ngumu, safari hii amekuja kivingine akiimba hip hip laini inayoweka kuchezeka akiwa amelenga soko la kimataifa zaidi.
"Huu ni ujio mpya wa Kalapina, nimelenga soko la kimataifa kwa kuimba wimbo huo kwa staili ya Ulaya na sijaegemea Marekani au Nigeria kama ilivyo kimbilio la wasanii wengi kwa sasa, na nitaachia hadharani kuanzia kesho Jumatano," alisema.
Kalapina alisema ameamua kubadilika kidogo ili kufanya muziki wake usikilizwe na watu wa rika lote na kuweza kuwarusha wasikilizaji wake na lengo lake kubwa ni kutaka kufungua soko la muziki wake anga la kimataifa badala ya kukomalia nyumbani tu.

Timu ya Watoto wa Mitaani yaenda Brazil

  https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi-_8-_Pi8v83y40ogZfYaU-TnhwkTqBDPtblA7ofd5DJ-6KhCtG-h5Zc0BdkZlWCO-JmXfTz1vkPBXM9NxnCRxvk0HJUHPqB2MglnkrBOIcgUOXB1MlstOZxAxkEIHaQgqbOm_MsmLgE4/s1600/531480_458178010866718_1145297429_n.jpg
TIMU ya Watoto wa Mitaani ya Tanzania kutoka Kituo cha Mwanza imeondoka leo (Machi 26 mwaka huu) kwenda Brazil kushiriki mashindano ya Kombe la Dunia kwa Watoto wa Mitaani.
John Kadutu ambaye ni mjumbe wa Bodi ya kituo hicho, na pia mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) akiwakilisha klabu za Mkoa wa Mwanza ndiye kiongozi wa msafara wa timu hiyo ya Tanzania.
Michuano hiyo ya siku 10 inayoshirikisha watoto wa mitaa (wavulana na wasichana) inaanza keshokutwa (Machi 28 mwaka huu). Nchi 19 zinashiriki michuano hiyo itakayofanyika katika Jiji la Rio de Janeiro.
Mbali ya Tanzania, nchi nyingine zinazoshiriki michuano hiyo kwa upande wa wavulana ni Argentina, Burundi, India, Kenya, Liberia, Marekani, Mauritius, Misri na Pakistan. Kwa wasichana ni Afrika Kusini, Brazil, El Salvador, Indonesia, Msumbiji, Nicaragua, Philippines, Uingereza na Zimbabwe.
Mwaka 2010 mashindano hayo yalifanyika Durban, Afrika Kusini ambapo pia Tanzania ilishiriki.

Diamond, Lady Jaydee watisha Kili Music Awards


'Sukari ya Warembo' Diamond Platnumz
Lady Jaydee 'Comando' a.k.a Anaconda
WANAMUZIKI nyota nchini, Nassib Abdul 'Diamond Platinum' na Judith Wambura Mbibo 'Lady jaydee' a.k.a Comando au Anaconda wameteuliwa mara nyingi kuwania tuzo za muziki za Kili Music zilizotangazwa leo.
Diamond ameingia katika vipengele 6 vya kinyan’ganyiro cha tuzo za muziki nchini, maarufu kama Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2014, huku Binti Machozi akiteuliwa mara 7.
Wimbo bora wa mwaka;
1 Number one-Diamond,
2 Joto hasira-Lady Jaydee Ft Prof Jay,
3 I love u-Cassim Mganga,
4 Yahaya-Lady JayDee,
5 Kidela -Abdu Kiba Feat Ali Kiba 
6 Muziki gani-Ney ft Diamond.


Wimbo bora wenye vionjo vya asili ya Kitanzania;
1 Kwejaga nyangisha-Batarokota,
2 Nalonji-Kumpeneka,
3 Bora Mchawi-Dar Bongo massive,
4 Tumbo lamsokota-Ashimba,
5 Aliponji –Wanakijiji 
6 Agwemwana-Cocodo African music band.

Wimbo bora wa kiswahili –Bendi;
1 Ushamba mzigo-Mashujaa Band,
2 Shamba la Bibi -Victoria Sound,
3 Chuki ya nini -FM Academia,
4 Yarabi nafsi -Mapacha Watatu
5 Kiapo mara 3 -Talent Band.

Wimbo bora wa Reggae;
1 Niwe na wewe-Dabo,
2 Hakuna Matata-Lonka,
3 Tell Me-Dj Aron ft Fidempha,
4 Bado nahitaji-Chikaka ft Bless p & Lazzy B
5 Bongo Reggae-Warriors from the east.

Wimbo bora wa Afrika Mashashariki;
1 Tubonge-Jose Chamelleone,
2 Nakupenda Pia-Waire Ft Allain,
3 Badilisha-Jose Chamelleone,
4 Kipepeo-Jaguar
5 Kiboko Changu-Aman FT Weizal and Radio.

Wimbo bora wa Afro pop;
1 Number one-Diamond,
2 Joto hasira-Jay Dee,
3 Kidela-abdul kiba ft Ali Kiba,
4 I love you-Kassim,
5 Tupogo-Ommy Dimpoz Ft J Martins
6 Roho yangu-Rich Mavoko.

Wimbo bora wa Taarab;
1 Wasi wasi wako-Mzee Yusuf,
2 Asiyekujua Hakuthamini-Isha Ramadhani & Saida Ramadhani,
3 Nipe stara -Rahma Machupa,
4 Sitaki shari-Leyla Rashid,
5 Fahari ya Mwanamke-Khadija Kopa,
6 Mambo bado-Khadija Yusuf
7 Kila muomba Mungu -Mwanahawa Ali.

Wimbo bora wa Hip hop;
1 Bei ya mkaa-Weusi,
2 Nje ya box-Nick wa pili ft Joh Makini na Gnako,
3 Siri ya mchezo-Fid q ft Nature,
4 2030-Roma
5 Pesa-Mr Blue Ft Becka Title.

Wimbo bora wa R&B;
1 Listen-Belle 9,
2 Closer -Vanessa Mdee,
3 So crazy-Maua ft Fa,
4 kama huwezi-rama dee ft jay dee
5 Wa ubani-Ben Pol ft. Alice

Wimbo bora wa kushirikisha/kushirikiana;
1 Music Gani-Ney Mitego ft Diamond,
2 Joto Hasira-Lady JayDee ft. Prof Jay,
3 Kidela -Abdul Kiba ft. Ali Kiba,
4 Bila Kukunja Goti-Mwana FA na AY ft. Jay Martins
5 Tupogo-Ommy Dimpoz ft. Jay Martins.

Wimbo bora wa Ragga/Dancehall;
1 Nishai-Chibwa Ft Juru,
2 Sex girl-Dr Jahson,
3 My sweet-Jettyman Dizano,
4 Feel Alright-Lucky Stone,
5 Wine-Princess Delyla.

Wimbo bora wa Zouk /Rhumba;
1 Yahaya-Lady Jaydee,
2 Yamoto-Mkubwa na wanawe,
3 Msaliti-Christian Bella,
4 Nakuhitaji-Malaika Band
5 Narudi kazini-Beka.

Mwimbaji bora wa kike -kizazi kipya;
1 Vanessa Mdee,
2 Lady Jaydee,
3 Linah na 4 Maua

Mwimbaji bora wa kiume -kizazi kipya
1 Ben Pol,
2 Rich Mavoko,
3 Diamond,
4 Ommy Dimpoz
5 Cassim Mganga.

Mwimbaji bora wa kike –Taarab;
1 Khadija Kopa,
2 Isha Ramadhani,
3 Khadija Yusuf,
4 Mwanahawa Ali
5 Leyla Rashid,

Mwimbaji bora wa kiume –Taarab wanashindana
1 Mzee Yusuf,
2 Hashimu Saidi
3 Mohamedi Ali aka Mtoto Pori.

Mwimbaji bora wa kiume –Bendi;
1 Jose Mara,
2 Kalala Junior,
3 Charz Baba,
4 Khalid Chokoraa
5 Christian Bella,

Mwimbaji bora wa kike -Bendi
1 Luiza Mbutu,
2 Catherine (Cindy) 
3 Ciana.

Msanii bora wa -Hip hop;
1 FID Q,
2 Stamina,
3 Young killer (Msodoki),
4 Nick wa pili,
5 Gnako.

Msanii bora chipukizi anayeibukia;
1 Young Killer(Msodoki),
2 Walter Chilambo,
3 Y Tony,
4 Snura
5 Meninah,

Rapa bora wa mwaka –Bendi kuna
1 Kitokololo,
2 Chokoraa,
3 Furguson,
4 Canal Top
5 Totoo ze Bingwa.

Mtumbuizaji bora wa kike wa Muziki.
1 Khadija Kopa,
2 Vanessa Mdee,
3 Isha Ramadhani,
4 Luiza Mbutu
5 Catherine (Cindy)

Mtumbuizaji bora wa kiume wa Muziki
1 Diamond,
2 Christian Bella,
3 Rich Mavoko,
4 Ommy Dimpoz
5 Abdu Kiba.

Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka –Taarab;
1 Enrico,
2 Ababuu Mwana ZNZ
3 Bakunde

Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka -Kizazi kipya
1 Marco chali-Mj Records,
2 Man Water-Combination Sound,
3 Mazoo-Mazoo Records,
4 Sheddy Clever-Burnz Records
5 Nahreel -Home Town Record.

Mtayarishaji bora wa nyimbo wa mwaka –Bendi;
1 Allan Mapigo,
2 C9,
3 Enrico,
4 Amoroso
5 Ababuu Mwana ZNZ,

Mtunzi bora wa mwaka –Taarabu,
1 Mzee Yusuf,
2 El-Ahad Omary,
3 El-khatib Rajab,
4 Kapten Temba,
5 Sadiki Abdul
6 Nassoro Seif,

Mtunzi bora wa mwaka -kizazi kipya,
1 Belle 9,
2 Ben Pol,
3 Diamond,
4 Rama dee
5 Rich mavoko.

Mtunzi bora wa mwaka –Bendi
1 Christia Bella,
2 Jose Mara,
3 Chaz Baba,
4 Nyoshi Saadat
5 Kalala Junior

Mtunzi bora wa mwaka -Hip hop,
1 Nikki wa Pili,
2 Young Killer(Msodoki),
3 Roma,
4 FID Q
5 G- Nako.

Video bora ya muziki ya mwaka;
1 Number One-Diamond,
2 Yahaya-lady Jaydee,
3 Joto hasira-Lady Jaydee Ft Prof Jay,
4 Uswazi takeaway-Chege Ft Malaika,
5 Mama Yeyo-Gnako Ft Ben Pol.

Bendi bora ya mwaka;
1 FM Academia,
2 Mapacha Watatu,
3 African Stars ‘Twanga Pepeta’,
4 Akudo Impact,
5 Malaika Band,
6 Mashujaa Band,

Kikundi cha mwaka cha Taarab ni
1 Jahaz Modern Taarab,
2 Mashauzi Classic
3 Five Stars

Kikundi cha mwaka cha kizazi kipya;
1 Makomandoo
2 Navy kenzo,
3 Weusi
4 Mkubwa na wanawe

(CHANZO: www.saluti5.com).

Easy Man kuweka Mashetani wake videoni

Easy Man  katika 'kichupa' chake cha Kasoro Wewe
MSANII anayetajwa kama 'mfalme' wa mchiriku nchini kwa sasa, Is'haka Salehe 'Easy Man',  anatarajiwa kurekodi video ya wimbo wake mpya uitwao 'Mashetani'.
Easy Man alisema wimbo huo ambao ni wa pili kwake baada ya kutesa na 'Kasoro Wewe', alisema kazi ya kurekodi video hiyo inatarajiwa kuanza keshokutwa chini ya kampuni moja iliyopo maeneo ya Temeke.
"Kuanzia Alhamisi natarajia kuanza kazi ya kurekodi video ya wimbo wangu wa 'Mashetani' na baada ya hapo nitaingia tena studio kwa ajili ya kurekodi wimbo mwingine ambao nitauachia kabla ya Mei mwaka huu," alisema Easy Man.
Msanii huyo alisema ana imani video ya wimbo wake wa 'Mashetani' unafunika kama ule wa 'Kasoro Wewe', huku akikatishwa tamaa baada ya kushindwa kuingia kwenye kinyang'anyiro cha Tuzo za Muziki wa Kili Music alizokuwa akiziombea awemo safari hii.

Kamati ya Sheria TFF kukutana juu ya Katiba

Rais wa TFF, Jamal Malinzi
KAMATI ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) inatarajia kukutana mwishoni mwa wiki kupitia taarifa ya utekelezaji wa agizo la wanachama kurekebisha katiba zao. TFF ilitoa agizo kwa wanachama wetu kufanyia marekebisho katiba ikiwemo kuingiza Kamati ya Maadili. Mwisho wa utekelezaji wa agizo hilo ulikuwa Machi 20 mwaka huu. Hivyo, Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji itapokea taarifa ya utekelezaji wa agizo hilo kutoka kwa Sekretarieti, na baadaye kutoa mwongozo wa hatua inayofuata.

Japanese ataka wasanii wa kike kujifunza kupiga ala

Japanese (kulia) akiwa na wanamuziki wenzake wa Jambo Survivors
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgxe5Rtm0ti7byoMQu71Qu2RCeP9KEud2GUkrLmeGrxVLRPJp1gKactUXZTOHXJoo7jhXXQbSZTnLG8klbNhVehA7oIbPN1esGX21SAjpyExhcK1wLO_mtK85shSRI2zmvGELH-iAE88iw/s1600/FIL0.JPG
Marehemu Asia Daruwesh enzi za uhai wake akionyesha umahiri wake katika kinanda
MUIMBAJI nyota wa zamani wa African Revolution na Double M Sound, Amina Ngaluma 'Japanese' amewataka wasanii wenzake wa kike kujibidiisha kujifunza kupiga ala za muziki badala ya kuishia kuimba tu.
Japanese alisema wasanii wengi wa kike wamekuwa wakikwepa kujifunza kupiga ala au kujifunza vitu zaidi ya uuimbaji na kuwafanya waachwe nyuma na wasanii wa kiume.
Alisema imefika wakati wanawake wenzake kuacha uvivu na badala yake kukamilia ala mbalimbali ili wawe wanamuziki kamili na kuweza kusimama pamoja na wanamuziki wa kiume wanaoonekana kutawala anga la muziki nchini.
"Mimi natunga, napanga muziki, napiga gitaa na ala nyingine, kitu ambachio natamani wasanii wa kike wengine wafuate nyayo ili kuondoa dhana muziki ni wa wanaume tu na sisi kazi yetu kuimba tena wakati mwingine kuitikia tu," alisema.
Alisema pia angependa kuona idadi ya wiambaji wa kike nchini inaongezeka maradufu kama ilivyokuwa miaka ya 1980-2000 waimbaji wa kike walipokuwa wengi na wengine kama marehemu Asia Daruwesh akiwa mahiri katika kupapasa kinanda kwa ustadi mkubwa.

Yanga, Azam vitani tena kesho VPL

Yanga SC
Azam Fc
KLABU za Azam na Yanga ambazo zinachuana kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, zinashuka tena viwanjani kesho (Machi 26 mwaka huu) kuwania pointi tatu. Azam yenye pointi 47 itakuwa mgeni wa Mgambo Shooting katika mechi itakayochezwa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga. Mgambo Shooting ipo katika nafasi ya kumi na moja kwenye msimamo wa VPL ikiwa na pointi 19.
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Yanga na Tanzania Prisons kuanzia saa 10.30 jioni. Yanga ipo nyuma ya Azam kwenye msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 47. Hata hivyo, timu hiyo ina mchezo mmoja mkononi. Tanzania Prisons ambayo ipo chini ya Kocha David Mwamaja hivi sasa ina pointi 22 ikiwa katika nafasi ya kumi. Timu tatu za mwisho katika ligi hiyo itakayomalizika Aprili 19 mwaka huu zitashuka kurudi Ligi Daraja la Kwanza (FDL). Ligi itaendelea tena Jumamosi (Machi 29 mwaka huu) kwa mechi kati ya Ashanti United na Oljoro JKT itakayofanyika Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi, Dar es Salaam. Jumapili (Machi 30 mwaka huu) kutakuwa na mechi kati ya Mbeya City na Tanzania Prisons (Uwanja wa Sokoine), Kagera Sugar na Ruvu Shooting (Uwanja wa Kaitaba), Mtibwa Sugar na Coastal Union (Uwanja wa Manungu), JKT Ruvu na Rhino Rangers (Uwanja wa Azam Complex), Azam na Simba (Uwanja wa Taifa) na Mgambo Shooting na Yanga (Uwanja wa Mkwakwani).

Mahakama yaagiza Yanga ikatwe kuwalipa akina Malashi

Steven Malashi na Wisdom Ndlovu wanaoidai Yanga
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limepokea amri ya Mahakama Kuu (Kitengo cha Kazi) kukamata Sh. Milioni 106 za klabu ya Yanga kutokana na mapato ya mlangoni kwenye mechi zake ili kuwalipa waliokuwa wachezaji wake, Stephen Malashi na Wisdom Ndlovu.
Taarifa ya TFF imesema kwamba, tayari wameanza utekelezaji wa amri hiyo ambapo katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) dhidi ya Rhino Rangers iliyochezwa Machi 22 mwaka huu mjini Tabora walizuia Sh. 9,221,250 ambazo ndizo zilizokuwa mgawo wa Yanga katika mchezo huo ulioingiza jumla ya sh. 38,655,000.
Wachezaji hao walifungua kesi kortini kupinga mikataba yao na klabu hiyo kuvunjwa bila kulipwa haki zao za kimkataba. Malashi na Ndlovu walishinda kesi hiyo, hivyo korti kuwapa tuzo hiyo ya sh. milioni 106.
Tunawakumbusha wanachama wetu (klabu za Ligi Kuu, vyama vya mpira wa miguu vya mikoa na vyama shiriki) kuzingatia mikataba wanayoingia na watendaji wao wakiwemo wachezaji, makocha na maofisa wengine.
“Iwapo wanataka kuvunja mikataba ya ajira wafuate taratibu kwa vile hakuna mkataba ambao hauelezi jinsi ya kuvunjwa iwapo upande mmoja unataka kufanya hivyo,”imesema taarifa ya TFF.