STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 23, 2013

NIYONZIMA AZIMA NGEBE ZA AZAM, AWATIA SIMANZI TAIFA



BAO pekee lililotumbukiwa kimiani na kiungo nyota wa kimataifa wa Rwanda, Haruna Niyonzima limeweza kuzima ngebe za Azam kwa kuiwezesha timu yake kuibuka na ushindi wa bao 1-0 na kuzidi kujikita kileleni mwa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Pambano hilo lililojaa upinzani na wenye kukamiana ulichezwa jioni ya leo kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kuifanya Yanga kuitambia Azam kwa kuzoa pointi zote sita za msimu huu katika ligi hiyo, baada ya duru la kwanza kuwalaza mabao 2-0.
Ushindi huo, umeifanya Yanga kufikisha jumla ya pointi 39 tatu zaidi ya Azam na ikiwa bado ina mchezo mmoja mkononi kwani vinara hao wamecheza mechi 17 wakati Azam wanaendelea kushika nafasi ya pili wamecheza mechi 18.
Mnyarwanda huyo anayefahamika kwa jina la Fabregas alifunga bao hilo la pekee lililowafanya mashabiki wa Yanga kupagawa kwa furaha na kuwazomea wale wa Azama mabo walikuwa wakiiungwa mkono na Simba, kwa shuti la nje ya 18 katika dk ya 32 baada ya kugongeana vema na Jerry Tegete kabla hya kufumua kombora kali.
Azam ilishangilia bao la kusawazisha lililofungwa kwa kichwa na John Bocco 'Adebayor' lililokataliwa na mwamuzi kwa madai alimchezea vibaya kipa Ally Mustafa kabla ya kuutumbukiza kimiani, hali iliyowakumba pia Yanga katika kipindi cha pili kwa bao la Didier Kavumbagu nalo kukataliwa na mwamuzi.
Ligi hioyo inatarajiwa kuendelea tena kesho kwa pambano litakalowakutanisha mabingwa watetezi Simba dhidi ya Mtibwa Sugar.
Pambano hilo litachezwa kwenye uwanja wa Taifa, huku Simba wakiwa na kumbukumbu ya kupoteza mechi ya awali dhidi ya Mtibwa kwa mabao 2-0.
Vikosi vya pambano la leo;
Yanga:
Ali Mustapha 'Barthez', Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Nadir Haroub, 'Cannavaro', Kelvin Yondani, Athumani Idd 'Chuji', Simon Msuva, Frank Domayo, Jerryson Tegete, Hamis Kiiza 'Diego'/ Said Bahanunzi, Haruna Niyonzima.
Azam:
Mwadini Ali, Michael Bolou, Waziri Salum, Joackins Atudo, David Mwantika, Ibrahim Mwaipopo, Salum Abubakar 'Salum Aboubakar 'Sure Boy', John Bocco 'Adebayor', Kipre Tchetche, Humphrey Mieno na Khamis Mcha 'Vialli'.

MAJANGILI MATATU YAUAWA MKOANI DODOMA

Mwili wa Mtu anayedhani wa kuwa ni Jangili ukiwa umehalibika baada ya kuuawa kuchinjwa na kuchomwa moto katika chumba cha kuhifadhia maiti mvumi Dodoma.

Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma David Misime akiwaonyesha waandishi wa Habari meno 73 ya tembo yenye thamani ya zaidi 225 mil ambayo ni sawa na tembo 36 pamoja na Gari aina ya Noah NO T 983 BZJ waliokamata juzi katika kijiji cha Miganga mvimi wilayani Chamwino Dodoma.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma David Misime akifafanua jambo mbele ya waandishi wa Habri kuhusu tukio la vifo vya watu watatu wanaodhaniwa kuwa ni majangili waliouawa na wananchi katika kiji cha miganga Mvumi Dodoma pembeni ni Gari aina ya Noah No T 983 BZJ walilokuwa wakilitumia na kuku meno 73 ya Tembo.
Na John Banda, Dodoma
MAJANGILI watatu wa nyara za serekali wameuawa kwa mishale yenye sumu na kisha miili yao kuchomwa moto na wananchi katika purukushani na polisi walipokuwa wakijaribu kukimbia ili kutorosha meno ya tembo.
Tukio hilo lilitokea jioni ya alhamis wiki hii katika kijiji cha Miganga kata ya mvumi wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma ambapo miili yao ilikutwa ikiwa imehalibika kutokana na kuchomwa moto.
Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma David Misime alisema majangili hayo yaliuawa na wanachi wenye hasira kali kwa zana mbalimbali za kijadi walipokuwa wanakimbilia polini ili kujiokoa na mkono wa polisi.
Misime alisema jeshi hilo lipokea taarifa kutoka kwa wananchi wema kuwa kulikuwa na Gali likitokea Manda likiwa na Meno ya Tembo na kisha kuweka mtego katika kijiji cha mwitikila ambapo waliona gali aina ya NOAH T 983 BZJ na kulisimamisha na Dereva wa Gali hilo alifanya kama anapunguza mwendo na kisha kuondoka kwa mwendo wa kasi.
‘’Polisi wakishirikiana na wananchi walianza kulifukuza walipofika kijiji cha Miganga Mvumi polisi walifanikiwa kupiga Risasi tairi moja ya kushoto na hivyo watu watatu waliokuwemo ndani gari hilo waliruka na kutawanyika, wananchi waliojichukulia sheria mkononi waliwashambulia kuasi cha kupoteza maisha yao’’, alisema
Aidha kamanda Misime alisema baada ya kulipekua Gari hilo walikutaMeno 73 ya Tembo yenye uzito wa kilo 255.9 yakiwa na thamani ya zaidi ya TSH 225 mil pamoja na hati ya mashitaka [CHARGE SHEET] ambayo ni kesi ya kuhujumu uchumi namba 4/2012 iliyokuwa imefunguliwa katika mahama yam panda mkoa wa katavi na Leseni ya Udereva na 4000692535 Aboubakar Peter huku wakihisi ni mmoja ya waliouawa.
Alisema walikuwa wameshitakiwa kwa kosa la kupatikana na Meno 3 ya Tembo Tarehe 17.06.2012 na maafisa wanyama poli katika eneo la Msaginya Wilaya ya Mlele mkoa wa katavi majina ya walikuwa wameshatakiwa ni Joseph Marius [NGONDO] 59 mkazi wa maili mbili Dodoma, Aboubakar Mhina 25 mkazi wa Mkuhungu Dodoma, Msafiri Milawa 36 mkazi wa Nkuhungu Dodoma na Petro Mtipula 55 mkazi wa mpanda.
Kamanda alitoa wito kwa wananchi wasijichukulie Sheria mikononi kwani kwa kufanya hivyo ni kupoteza ushahidi na inawawia vigumu polisi kupata mtandao inayohusika na matukio kama hayo. 
 
CHANZO:BOSS NGASA 

GOLDEN BUSH YAIZIMA CLOUDS MARA NNE



WAKALI wa soka jijini Dar es Salaam, Golden Bush Veterani jana ilitimiza tambo zake kwa kuifumua timu ya Clouds Fc kwa mabao 4-1 katika mechi kali iliyochezwa kwenye uwanja wa Tanganyika Packers, Kawe jijini Dar es Salaam.
Golden Bush iliahidi kutoa kipigo kwa wapinzani wao kabla ya mchezo huo uliochezwa jioni ya jana kupitia kwa mlezi wake na mmoja wa wachezaji tegemeo, Onesmo Waziri 'Ticotico'.
Tambo hizo zilihitimishwa baada ya mechi hiyo iliyochezeshwa na mwamuzi, Othman Kazi kwa mabao mawili ya Said Swedi 'Panucci', Nico Nyagawa na De Natale, huku bao la kufutia machozi la Clouds iliyokuwa ikiongozwa na Mbwiga Mbwiguke lilifungwa na Ben Kinyaiya.
Ticotico alisema ushindi huo umekiuwa faraja kwao baada ya wiki iliyopita kuchezea kichapo toka Survet, pia kuzima ngebe za wapinzani wao waliokuwa wakichonga kabla ya pambano hilo.

Aliongeza kwa sasa timu yake imevunja kambi yake iliyokuwa imewekwa hoteli ya Star Light na kufanya mazoezi ya kawaida kujiandaa na mechi za kirafiki zitakazochezwa hivi karibuni pamoja na mipambano ya kusherehekea sikukuu ya Pasaka.

MWANARIADHA OSCAR PISTORIUS AACHIWA KWA DHAMANA

  Oscar Pistorius
 Oscar Pistorius akiwa na mpenzi wake Reeva Steenkamp wakati wa uhai wake.
 Reeva Steenkamp


Kesi kamili inayomkabili nyota huyo inaweza kuanza kusikilizwa miezi kadhaa ijayo, na Pistorius nyota wa Olimpiki na Paralimpiki, ambaye hana miguu yote miwili, anakabiliwa na hatari ya kifungo cha maisha kama akikutwa na hatia ya mauaji


JOHNNESBURG, South Africa

MWANARIADHA nyota wa mbio za walemavu Oscar Pistorius, hatimaye leo Ijumaa mchana ameachiwa kwa dhamana, kutokana na kesi ya mauaji ya mpenzi wake inayomkabili.

Umauzi wa Pistorius kupewa dhamana ulitolewa na Jaji Desmond Nair, na kuamsha furaha miongoni mwa wanafamilia wa Pistorius na mashabiki wake ndani na nje ya Mahakama ya jijini Pretoria, huku mwenyewe akiwa amesimama imara kama aliyenyimwa dhamana hiyo.

Kuachiwa kwa Pistorius kunafuatia wiki nzima ya usikilizaji wa maelezo ya namna mwanariadha huyo alivyompiga risasi na kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp wakiwa katika jumba lao la kifahari, asubuhi ya Siku ya Wapendao Februari 14.

Waendesha mashtaka wamesema Pistorius, 26, anakabiliwa na kesi ya kujibu kutokana na kupiga risasi nne kwenye mlango wa bafu ukiwa umefungwa, huku mpenzi wake akiwa ndani. Steenkamp, 29, alikutwa na majeraha ya risasi katika kichwa chake, mkononi na kwenye nyonga.

Upande unaomtetea Pistorius umeendelea kusisitiza kuwa mkali huyo alimuua mkewe kimakosa, wakisema alifanya hivyo kutokana na kuhisi kuwa amevamia na jambazi, wakataka apewe dhamana kuweza kujiandaa, kuikabili kesi hiyo iliyoteka hisia za wengi duniani.

Kesi kamili inayomkabili nyota huyo inaweza kuanza kusikilizwa miezi kadhaa ijayo, na Pistorius nyota wa Olimpiki na Paralimpiki, ambaye hana miguu yote miwili, anakabiliwa na hatari ya kifungo cha maisha kama akikutwa na hatia ya mauaji.

Dhamana hii imefungua milango ya matumaini miongoni mwa wanafamilia na mashabiki wake, kuwa anaweza kushinda vita ya kuepuka kifungo cha maisha.

Himid Mao aipa Azam ubingwa wa Tanzania Bara



KIUNGO mkabaji wa klabu ya Azam, Himid Mao ametangaza na kuipa ubingwa klabu yake ya Azam, licha ya kukiri kwamba Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu huu ni ngumu na isiyotabirika haraka.
Mao, mtoto wa nyota wa zamani wa Pamba, Simba, Mtibwa Sugar na Taifa Stars, alisema anaamini kwa kikosi ilichonacho Azam ni dhahiri wanastahili kuwa mabingwa wapya wa Tanzania msimu huu.
Alisema, licha ya kuwepo kwa mchuano mkali katika kuwania taji hilo klabu yake ikibanana na Yanga kileleni na ikifukuziwa kwa nyuma na mabingwa watetezi, bado haoni sababu ya Azam kunyakua taji wakayi ndiyo timu yenye kikosi bora zaidi kwa sasa nchini.
"Ni vigumu kutabiri moja kwa moja bingwa wa msimu huu, lakini kwa kuangalia ubora wa vikosi, Azam ndiyo wanaostahili kuwa Bingwa, na wachezaji tupio tayarai kutimiza ndoto hizo," alisema.
Aliongeza, mbali na kuliota taji la ligi kuu, pia karibu kila mtu ndani ya Azam analipigia hesabu pia kombe la michuano ya Shirikisho Afrika ambapo wiki ijayo Azam watarudiana na El Nasir Juba ya Sudan Kusini mjini Juba katika mechi ya marudiano huku wakiwa na hazina ya ushindi wa mabao 3-1 iliyopata nyumbani.
Mao, aliyeanzia soka la tangu darasa la nne katika Shule ya Dk Omar Juma na kucheza chandimu Kibesa Fc kisha kutua Soccer Rangers zote za Magomeni na baadaye kunyakuliwa na kituo cha Elite Academy kabla ya kusajiliwa na Azam mwaka 2008 akiichezea timu ya vijana ya U20, alisema sababu, uwezo wa Azam kuwa mabingwa wa Afrika kupitia michuano hiyo ya Kombe la Shirikisho inawezekana.
"Tunaomba Mungu atusaidie na kuwaomba Watanzania watuunge mkono, tutimize ndoto hizo za kuwa mabingwa wa Ligi Kuu na Kombe la Shirikisho," alisema.
Mao aliyetwaa mataji zaidi ya matano tangu aanze kucheza soka la ushindani akiwa na Azam U20 na ile ya wakubwa aliyoanza kuichezea katika duru la pili la msimu wa ligi wa 2008-2009 walipopanda daraja, alisema ushindani wa ligi ulivyo sasa umeondoa ule mfumo wa klabu za Simba na Yanga kuhodhi michuano hiyo.
Mbali na kutwaa Kombe la Uhai mara mbili, Mao pia amenyakua ubingwa wa Kombe la Dunia la Vijana U17 la Copa Coca Cola, Kombe la Mapinduzi mara mbili mfululizo na ile ya Hisani nchini Dr Congo.

Yanga yashtakiwa tena FIFA, uongozi wajitetea


KLABU ya soka ya Yanga, imeingia tena matatani baada ya kuburuzwa katika Shiriksho la Soka Duniani, FIFA na nyota wake wa zamani Mghana Kenneth Asamoah.
Asamoah ameiburza Yanga FIFA ikiidai Dola 5000 za Kimarekani ikiwa sehemu ya malipo yake ya kujiunga na klabu hiyo ambayo iliamua kumtema msimu huu.
FIFA limetoa taarifa ya kulipeleka rasmi madai ya mchezaji huyo kwenye chombo chake cha utatuzi wa migogoro (Dispute Resolution Chamber) baada ya klabu hiyo kutojibu chochote.
Awali FIFA ilipokea malalamiko ya Asamoah kuwa anaidai Yanga dola 5,000 za Marekani ambapo ilikuwa ni sehemu ya malipo yake (signing fee) baada ya kujiunga na klabu hiyo.
Desemba mwaka jana FIFA iliiandikia barua Yanga kupitia Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ikitaka maelezo yake kuhusu madai hayo ya Asamoah, lakini hadi sasa haijajibu madai hayo.
Kwa mujibu wa FIFA, hatua ya uchunguzi wa suala hilo umekamilika, na sasa linapelekwa rasmi katika chombo chake cha utatuzi wa migogoro (Dispute Resolution Chamber) kwa ajili ya kufanya uamuzi.
Hilo ni tukio la tatu la hivi karibuni kwa Yanga kufikishwa FIFA awali iliburuzwa na beki wao zamani John Njoroge na kocha Kostadin Papic iliyowavunjia mikataba kabla ya wakati.
Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrance Mwalusako alinukuliwa jana akidai kuwa, uongozi utamlipa fedha hizo Asamoah akisema kabla ya hapo walishapunguza deni alililokuwa akiidai klabu hiyo la karibu Sh Milioni 10.
"Hizi fedha zitalipwa sio kitu cha kukuzwa, uongozi umechelewa kummalizia kwa kuwa ilikuwa ikiendelea na uhakiki wa madeni inayodaiwa klabu, ila tunauhakikishia umma kwamba Asamoah atapewa fedha zake haraka iwezekanavyo,": alisema Mwalusako.
Alisisitiza kuwa, uongozi wao umekuwa ukionekana kama 'wababaishaji' ilihali madeni inayoangaika nayo ni ya uongozi uliopita na kuwataka wanayanga kutulia kwani kila kitu kinaenda vema na uongozi wao upo makini katika kurekebisha dosari zilizopo.