STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 23, 2013

GOLDEN BUSH YAIZIMA CLOUDS MARA NNE



WAKALI wa soka jijini Dar es Salaam, Golden Bush Veterani jana ilitimiza tambo zake kwa kuifumua timu ya Clouds Fc kwa mabao 4-1 katika mechi kali iliyochezwa kwenye uwanja wa Tanganyika Packers, Kawe jijini Dar es Salaam.
Golden Bush iliahidi kutoa kipigo kwa wapinzani wao kabla ya mchezo huo uliochezwa jioni ya jana kupitia kwa mlezi wake na mmoja wa wachezaji tegemeo, Onesmo Waziri 'Ticotico'.
Tambo hizo zilihitimishwa baada ya mechi hiyo iliyochezeshwa na mwamuzi, Othman Kazi kwa mabao mawili ya Said Swedi 'Panucci', Nico Nyagawa na De Natale, huku bao la kufutia machozi la Clouds iliyokuwa ikiongozwa na Mbwiga Mbwiguke lilifungwa na Ben Kinyaiya.
Ticotico alisema ushindi huo umekiuwa faraja kwao baada ya wiki iliyopita kuchezea kichapo toka Survet, pia kuzima ngebe za wapinzani wao waliokuwa wakichonga kabla ya pambano hilo.

Aliongeza kwa sasa timu yake imevunja kambi yake iliyokuwa imewekwa hoteli ya Star Light na kufanya mazoezi ya kawaida kujiandaa na mechi za kirafiki zitakazochezwa hivi karibuni pamoja na mipambano ya kusherehekea sikukuu ya Pasaka.

No comments:

Post a Comment