STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 23, 2013

NIYONZIMA AZIMA NGEBE ZA AZAM, AWATIA SIMANZI TAIFA



BAO pekee lililotumbukiwa kimiani na kiungo nyota wa kimataifa wa Rwanda, Haruna Niyonzima limeweza kuzima ngebe za Azam kwa kuiwezesha timu yake kuibuka na ushindi wa bao 1-0 na kuzidi kujikita kileleni mwa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Pambano hilo lililojaa upinzani na wenye kukamiana ulichezwa jioni ya leo kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kuifanya Yanga kuitambia Azam kwa kuzoa pointi zote sita za msimu huu katika ligi hiyo, baada ya duru la kwanza kuwalaza mabao 2-0.
Ushindi huo, umeifanya Yanga kufikisha jumla ya pointi 39 tatu zaidi ya Azam na ikiwa bado ina mchezo mmoja mkononi kwani vinara hao wamecheza mechi 17 wakati Azam wanaendelea kushika nafasi ya pili wamecheza mechi 18.
Mnyarwanda huyo anayefahamika kwa jina la Fabregas alifunga bao hilo la pekee lililowafanya mashabiki wa Yanga kupagawa kwa furaha na kuwazomea wale wa Azama mabo walikuwa wakiiungwa mkono na Simba, kwa shuti la nje ya 18 katika dk ya 32 baada ya kugongeana vema na Jerry Tegete kabla hya kufumua kombora kali.
Azam ilishangilia bao la kusawazisha lililofungwa kwa kichwa na John Bocco 'Adebayor' lililokataliwa na mwamuzi kwa madai alimchezea vibaya kipa Ally Mustafa kabla ya kuutumbukiza kimiani, hali iliyowakumba pia Yanga katika kipindi cha pili kwa bao la Didier Kavumbagu nalo kukataliwa na mwamuzi.
Ligi hioyo inatarajiwa kuendelea tena kesho kwa pambano litakalowakutanisha mabingwa watetezi Simba dhidi ya Mtibwa Sugar.
Pambano hilo litachezwa kwenye uwanja wa Taifa, huku Simba wakiwa na kumbukumbu ya kupoteza mechi ya awali dhidi ya Mtibwa kwa mabao 2-0.
Vikosi vya pambano la leo;
Yanga:
Ali Mustapha 'Barthez', Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Nadir Haroub, 'Cannavaro', Kelvin Yondani, Athumani Idd 'Chuji', Simon Msuva, Frank Domayo, Jerryson Tegete, Hamis Kiiza 'Diego'/ Said Bahanunzi, Haruna Niyonzima.
Azam:
Mwadini Ali, Michael Bolou, Waziri Salum, Joackins Atudo, David Mwantika, Ibrahim Mwaipopo, Salum Abubakar 'Salum Aboubakar 'Sure Boy', John Bocco 'Adebayor', Kipre Tchetche, Humphrey Mieno na Khamis Mcha 'Vialli'.

No comments:

Post a Comment