STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 18, 2013

Fabregas ataka fainali ya El Clasico Ulaya

Cesc Fabregas

KIUNGO nyota wa Barcelona, Cesc Fabregas amesema anatamani Fainali za Ligi ya Mabingwa ya Ulaya mwaka 2013 izikutanishe timu hasimu za Hispania.

Vigogo hao wa La Liga wanatarajiwa kuvaana na Bayern Munich na Borussia Dortmund katika mecni za Nusu Fainali zitakazochezwa wiki ijayo.
 Fabregas pamoja na kutambua ugumu wa pambano lao dhidi ya Bayern, lakini anaamini huenda mahasimu hao wa Hispania watacheza fainali zitakazofanyika Wembley, Uingereza.

"Nataka fainali kati ya Real Madrid na Barcelona. Itakuwa ni mechi muhimu na ya kihistoria katika soka," nahodha huyo wa zamani wa Arsenal alisema.
Kiungo huo aliyekuwa akihojiwa na kituo cha Radio cha RAC1, alisema; "Hata hivyo kitu cha muhimu kwa sasa ni pambano letu na nusu fainali dhidi ya Bayern. Itakuwa mechi ngumu na isiyotabirika," alisema Fabregas.
Pia kiungo huyo alizungumza kurejea kwa kocha wao, Tito Vilanova na Eric Abidal ambao wanapigana dhidi ya ugonjwa wa Saratani, na kudai itawahamasisha zaidi wachezaji dhidi ya pambano hilo dhidi ya Bayern.
"Tito na Abidal wametuongezea chachu ya kukupigana na kutinga fainali," alisema.

HUKUMU KESI YA PONDA YAAHIRISHWA MPAKA MEI 9

Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania Sheikh Ponda Issa Ponda (kulia) akiwa na mshtakiwa mwenzake Saleh Mkadamu wakielekea  kupanda basi la magereza baada ya hukumu ya kesi yao kuahirishwa hadi Mei 9. Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake 49 wanakabiriwa na makosa matano ya kula njama na kuingia kwa jinai katika uwanja namba 311/3/4 kitalu T uliopo Markaz Chang'ombe na wizi wa vifaa mbalimbali vya ujenzi vyenye thamani ya Shs milioni 59 mali ya kampuni ya Agritanza. (Picha na Habari Mseto Blog) 
 Saleh Mkadamu akipanda basi kuelekea mahabusu
 Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania Sheikh Ponda Issa Ponda akipanda basi la magereza.
 Ulinzi mkali kila kona ya mahakama
 Askari wakiimarisha ulinzi nje ya Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo.
 Msafara wa magari ya Polisi wakisindikiza gari la magereza lililomchukua Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania Sheikh Ponda Issa Ponda wakati wakielekea mahabusu baada ya hukumu ya kesi yao kuahirishwa leo hadi Mei 9.
Wafuasi wa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania Sheikh Ponda Issa Ponda wakiwa wamekusanyika nje ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo wakati hukumu ya kesi yake ilipoahirishwa leo.

HATIMAYE BI KIDUDE APUMZISHWA KABURINI VISIWANI ZENJI

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,alipohudhuria nyumbani kwa Marehemu Bi Fatma Baraka (KIDUDE) kuhani kwa Familia ya marehemu leo asubuhi Rahaleo Mjini Unguja. (Picha na Ramadhan Othman, Ikulu)
 Akina Mama mbali mbali waliofurika katika maziko ya Msanii Maarufu Marehemu Bi Fatma Baraka (KIDUDE)huko nyumbani kwake Rahaleo mjini Unguja leo.
Maelfu ya wanannchi na waislamu waliofurika katika msikiti wa Mwembr shauri katika maziko ya Marehemu bikidude leo,na kuzikwa kijini kwao Kitumba Wilaya ya Kati Unguja.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,(wa nne  kushoto) akijumuika na viongozi na waislamu katika kumswalia Marehemu Msanii maarufu Fatma Binti Baraka (kidude) katika msikiti wa Mwembeshauri Mjini Unguja leo.

 Vijana waliobeba Jeneza la mwili wa Marehemu Msanii maarufu Fatma Binti Baraka (kidude) wakati wa maziko yake yaliyofanyika leo huko kijijini kwao Kitumba,Wilaya ya Katri Unguja,ambapo maziko yake yamehudhuriwa na wasanii mbali mbali ndani na nje ya nchi. 
 Baadhi ya Wananchi waliohudhuria katika maziko ya marehemu Bi Fatma Baraka (Kidude)  kijijini kwao Kitumba,Wilaya ya Katri Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein,(kutoka kulia) Rais wa  jamhuri ya Muungano Dk. Jakaya Mrisho Kikwete,Makamo wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif,na Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi,wakiitikia dua baada ya maziko ya Msanii maarufu Fatma Binti Baraka (kidude) aliyefariki jana na kuzikwa leo Kijijini kwao Kitumba,Wilaya ya Kati Unguja.

Soko la wanandinga wa Kiafrika lapanuka Ulaya, Tanzania mmmh!


Wachezaji wa Kiafrika wazidi kupata soko Barani Ulaya hivyo Watanzania wasichezee fursa ya soka la kimataifa.
*  Zaidi ya Mawakala 15 wawasiliana na Tanzania Mwandi kuwahitaji wachezaji

Zaidi ya mawakala 15 tayari wamewasiliana na Kampuni ya Tanzania Mwandi kuwahitaji wachezaji mbalimbali kwaajili ya kuwapeleka kwenye klabu za barani Ulaya, Asia na Afrika ili kucheza soka la kulipwa.

Mwitikio huo umeongezeka kutokana na vijana wa kiafrika kuwa na soko kubwa katika ulimwengu wa sasa wa mpira wa miguu kwa nchi mbalimbali kama Sweden, Uholanzi, Denmark, Ureno na nchi nyinginezo.

Arne Anderson kutoka AA Football Service ya Sweden amesema kuwa binafsi yuko tayari kuchukua wachezaji wawili kwaajili ya kuwatafutia clubs nchini humo kwani tayari mafanikio ya wachezaji watano wa kiafrika aliowapeleka yamempa maombi ya timu nyingi za Sweden.

“Niko tayari kuchukua wachezaji wawili endapo tutakubaliana kuhusu maslahi yangu pindi wachezaji hao wakianza kucheza hapa”, Arne amesema.

Kutokana na mafanikio hayo na maombi ya mawakala lukuki Kampuni ya Tanzania Mwandi inazidi kuwasisitizia wachezaji wa Kitanzania kujaza fomu zinazopatikana kupitia blog.tanzaniamwandi.co.tz ili kufanya majaribio ya kucheza soka nchini Sweden, Norway, Denmark, Uholanzi, Ureno, Uswiss, Ufaransa na Ubelgiji, barani Asia (Kuwait, China, Qatar nk) na klabu nyingine barani Afrika.

Mpaka sasa jumla ya wachezaji wa kitanzania 15 wamekwishajaza fomu za haraka kwenye tovuti ya Tanzania Mwandi huku kampuni ikiwa imepokea pia maombi ya wachezaji 25 kutoka nje ya nchi.

“Maombi yanazidi kuja ingawa tunawahimiza Watanzania wasikimbie kiingilio cha shilingi 300, 000 wakumbuke kuwa wanafanya majaribio wakiwa nyumbani na watakapopata timu Kampuni ya Tanzania Mwandi haitachukua chochote kwenye mikataba yao, ni wao na mawakala ndio watakokubaliana juu ya watakachokipata kutoka kwa klabu husika”, alisema Teonas Aswile, Mkurugenzi wa Kampuni ya Tanzania Mwandi, waandaaji wa African Youth Football Tournament.

Aswile amezialika klabu mbalimbali za ligi kuu ya soka Tanzania Bara na Visiwani kutazama wachezaji watakaofika katika michuano hiyo kwani wapo baadhi ya wachezaji kutoka nje ya nchi ambao watafika na wangependa kucheza soka la Tanzania.

“Kati ya wachezaji 25 wa nje ya nchi wengine wameomba tuwatafutie timu hapa nchini hivyo klabu zikija zinaweza kuwapata wachezaji hao wakiwa huru kwasababu watakuja kwa gharama zao kufanya majaribio nchini. Pia klabu hizo zitumie fursa hii kuuza wachezaji wake.”

Michuano ya African Youth Football Tournament inatarajia kufanyika Juni 10 hadi 14 mwaka huu katika uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam na kushirikisha vijana kati ya miaka 18 hadi 21 kutoka Tanzania na bara zima la Afrika. Taarifa zaidi kuhusu michuano hiyo zinapatikana kupitia;  blog.tanzaniamwandi.co.tz

Imetolewa na Idara ya Habari
Kampuni ya Tanzania Mwandi,
TANCOT House, Ground Floor,
S. L. P 79944,
Dar es Salaam.

Yanga, maafande wa JKT Ruvu kuonyesha ubabe J'2


JKT Ruvu Stars
Yanga
Na Boniface Wambura
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga inayofukuzia kwa karibu taji la msimu huu inatarajiwa kushuka dimbanio Jumapili kwa ajili ya kuumana na maafande wa JKT Ruvu katika mechi pekee ya ligi hiyo wikiendi hii itakayofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mbali ya mechi hiyo, nyingine zitakazochezwa mwezi huu ni kati ya African Lyon na JKT Ruvu itakayofanyika Aprili 24 kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam wakati Aprili 25 ni kati ya Ruvu Shooting na Simba kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Nayo Coastal Union itaikaribisha Azam kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga katika mechi itakayochezwa Aprili 27. Uwanja wa Taifa utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Simba na Polisi Morogoro itakayofanyika Aprili 28.

Yanga wanaoongoza msimamo wa Ligi hiyo ikiwa na pointi 53 ikifuatiwa na Azam yenye pointi 47 wakati Kagera Sugar wanashika nafasi ya tatu wakijikusanyia jumla ya pointi 40 na kufuatiwa na Simba na Mtibwa Sugar ambazo kila moja ina pointi 36 kisha wagosi wa kaya, Coastal Union wakifuatia nafasi ya sita.,
Mpaka sasa timu tano za Polisi Moro, African Lyon, Toto Africans, JKT Ruvu na Mgambo ndizo zilizopo kwenye vita ya kuepukana kushuka daraja zikipisha kwa tofauti ndogo ya pointi kati ya 19 na 25.

Yanga, Mgambo JKT wavuna Mil 24 Mkwakwani

Hamis Kiiza alipokuwa akiwania mpira na beki wa Mgambo JKT juzi kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga


Na Boniface Wambura
PAMBANO la  Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Mgambo Shooting na Yanga lililochezwa jana (Aprili 17 mwaka huu) Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga limeingiza kiasi cha sh. 24,865,000 kutokana na watazamaji 4,386.

Viingilio katika mechi hiyo namba 162 iliyomalizika kwa timu hizo kutoka sare ya bao 1-1 vilikuwa sh. 10,000 kwa jukwaa kuu na sh. 5,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 5,547,337.50 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 3,792,966.10.

Asilimia 15 ya uwanja sh. 2,820,680.08, msimamizi wa kituo sh. 120,000, kamishna wa mechi sh. 90,000, waamuzi sh. 270,000, maandalizi ya uwanja sh. 100,000 na tiketi sh. 1,587,500.

Mgawo mwingine ni gharama za mechi sh. 1,692,408.05, Kamati ya Ligi sh. 1,692,408.05, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 846,204.05 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Tanga (TRFA) sh. 658,158.69.

Makocha Azam Far Rabat kuteta kesho

Kocha wa Azam, John Stewart Hall

Na Boniface Wambura
Makocha wa timu za Azam, Stewart John Hall na AS FAR Rabat ya Morocco, Abderazzak Khairi watakutana na waandishi wa habari kesho (Aprili 19 mwaka huu) kuzungumzia mechi yao itakayofanyika Jumamosi, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mkutano huo ambao pia utawahusisha manahodha wa timu hizo mbili utafanyika saa 5 kamili asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) zilizoko Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Barabara ya Uhuru na Shaurimoyo.

Timu hizo zitakutana katika mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe la Shirikisho itakayoanza saa 10 kamili jioni. Mechi ya marudiano itachezwa nchini Morocco wiki mbili baadaye.