STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 18, 2013

Yanga, maafande wa JKT Ruvu kuonyesha ubabe J'2


JKT Ruvu Stars
Yanga
Na Boniface Wambura
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga inayofukuzia kwa karibu taji la msimu huu inatarajiwa kushuka dimbanio Jumapili kwa ajili ya kuumana na maafande wa JKT Ruvu katika mechi pekee ya ligi hiyo wikiendi hii itakayofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mbali ya mechi hiyo, nyingine zitakazochezwa mwezi huu ni kati ya African Lyon na JKT Ruvu itakayofanyika Aprili 24 kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam wakati Aprili 25 ni kati ya Ruvu Shooting na Simba kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Nayo Coastal Union itaikaribisha Azam kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga katika mechi itakayochezwa Aprili 27. Uwanja wa Taifa utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya Simba na Polisi Morogoro itakayofanyika Aprili 28.

Yanga wanaoongoza msimamo wa Ligi hiyo ikiwa na pointi 53 ikifuatiwa na Azam yenye pointi 47 wakati Kagera Sugar wanashika nafasi ya tatu wakijikusanyia jumla ya pointi 40 na kufuatiwa na Simba na Mtibwa Sugar ambazo kila moja ina pointi 36 kisha wagosi wa kaya, Coastal Union wakifuatia nafasi ya sita.,
Mpaka sasa timu tano za Polisi Moro, African Lyon, Toto Africans, JKT Ruvu na Mgambo ndizo zilizopo kwenye vita ya kuepukana kushuka daraja zikipisha kwa tofauti ndogo ya pointi kati ya 19 na 25.

No comments:

Post a Comment