STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 18, 2013

Fabregas ataka fainali ya El Clasico Ulaya

Cesc Fabregas

KIUNGO nyota wa Barcelona, Cesc Fabregas amesema anatamani Fainali za Ligi ya Mabingwa ya Ulaya mwaka 2013 izikutanishe timu hasimu za Hispania.

Vigogo hao wa La Liga wanatarajiwa kuvaana na Bayern Munich na Borussia Dortmund katika mecni za Nusu Fainali zitakazochezwa wiki ijayo.
 Fabregas pamoja na kutambua ugumu wa pambano lao dhidi ya Bayern, lakini anaamini huenda mahasimu hao wa Hispania watacheza fainali zitakazofanyika Wembley, Uingereza.

"Nataka fainali kati ya Real Madrid na Barcelona. Itakuwa ni mechi muhimu na ya kihistoria katika soka," nahodha huyo wa zamani wa Arsenal alisema.
Kiungo huo aliyekuwa akihojiwa na kituo cha Radio cha RAC1, alisema; "Hata hivyo kitu cha muhimu kwa sasa ni pambano letu na nusu fainali dhidi ya Bayern. Itakuwa mechi ngumu na isiyotabirika," alisema Fabregas.
Pia kiungo huyo alizungumza kurejea kwa kocha wao, Tito Vilanova na Eric Abidal ambao wanapigana dhidi ya ugonjwa wa Saratani, na kudai itawahamasisha zaidi wachezaji dhidi ya pambano hilo dhidi ya Bayern.
"Tito na Abidal wametuongezea chachu ya kukupigana na kutinga fainali," alisema.

No comments:

Post a Comment