STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, September 9, 2016

Wilshere mbona mtamu, subirini tu muone-Wenger

http://www.telegraph.co.uk/content/dam/football/2016/04/07/jack-wilshere8-large_trans++qVzuuqpFlyLIwiB6NTmJwfSVWeZ_vEN7c6bHu2jJnT8.jpgMBONA freshi tu! Kocha wa klabu ya NEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amedai kuwa Jack Wilshere anaweza kuitumikia klabu hiyo kwa kipindi kirefu mbele ya safari huku akisisitiza kuwa kiungo huyo hana chochote cha kumuonyesha zaidi ya kuwa fiti. Wilshere ameenda kwa mkopo wa msimu mzima katika klabu ya AFC Bournemouth dakika za mwisho kabla ya dirisha la usajili majira ya kiangazi halijafungwa ikiwa kama sehemu ya mikakati ya kujijenga upya kufuatia kusumbuliwa na majeruhi ya mara kwa mara katika misimu miwili iliyopita.
Akizungumza kuelekea mchezo wao wa Ligi Kuu dhidi ya Southampton, Wenger alipuuza habari kuwa amekuwa haelewani na kiungo huyo mwenye umri wa miaka 24 ambaye amekuwa akimtaja kuwa na uwezo mkubwa.
Kocha Wenger alisema alizungumza na Wilshere naye alimwambia hadhani kama ataweza kupata muda wa kutosha kucheza akibakia hapo kwa vile anataka  kucheza zaidi msimu huu baada ya kupona majeruhi yake.
Wengeraliendelea kudai kuwa alimruhusu kuondoka kwasababu alikuwa hawezi kumuahidi muda wa kutosha wa kucheza kama alivyotaka mwenyewe.

Ronaldo kamili gado kuanza mambo La Liga

http://www.ronaldo7.net/news/2014/04/824-cristiano-ronaldo-fitness-drills.jpgUSIYEMPENDA Kaja. Ndivyo ambavyo Osasuna watakuwa wanawaza sana, baada ya kuwepo kwa taarifa kwamba nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo yupo fiti na kesho huenda akashuka uwanjani kuvaana nao.
Straika huyo amebainisha kuwa atarejea uwanjani Jumamosi hii katika mchezo dhidi ya Osasuna.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 31 amekuwa akijiuguza goti lake katika majeruhi aliyopata katika mchezo wa fainali ya michuano ya Ulaya hali iliyomfanya kukosa mechi ys Super Cup ya Ulaya na zingine walizocheza Madrid katika La Liga msimu huu. Akihojiwa kuhusiana na hali yake inavyoendelea, nahodha huyo wa Ureno amesema yuko tayari kurejea uwanjani na anatarajia kucheza katika mchezo dhidi ya Osasuna.
Madrid wameshinda mechi zao zote mbili za la Liga walizocheza msimu huu, kwa kuzifunga Real Sociedad na Celta Vigo.

Buriani Kocha Mohammed Hassan Msomali

Kocha Mohammed Hassan 'Msomali' enzi za uhai wake hivi karibuni
Msomali wa kwanza kushoto waliochuchumaa enzi za uhai wake akikipiga Cosmopolitan
ALIYEKUWA Kocha mkongwe na mwenye mafanikio makubwa nchini, Mohammed Hassan 'Msomali' (74) amezikwa leo mjini Morogoro baada ya kufariki dunia jana mchana nyumbani kwake mjini humo.
Marehemu aliyewahi kuzichezea Yanga, Cosmo na Taifa Stars kwa mafanikio makubwa kabla ya kuzinoa timu za Tumbaku, Mseto, Pan Africans na Moro United sambamba na timu za Mkoa wa Morogoro na Taifa Stars, atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika soka la Tanzania.
Ukiondoa kuwa miongoni mwa walioisaidia Cosmo kubeba taji la Ligi ya Tanzania mwaka 1968 wakiipoka Simba (enzi za Sunderland) iliyokuwa ikimiliki taji kwa miaka miwili tangu kuanzishwa kwa Ligi hiyo mwaka 1965, pia ndiye kocha wa kwana kubeba taji kwa timu za mkoani.
Alifanya hivyo mwaka 1975 akiwa na Mseto ya Morogoro na kubeba tena akiiongoza Pan Africans mwaka 1982.
Kocha huyo ndiye aliyewaibua nyota mbalimbali waliowahi kutamba na kuendelea kuwa kiigizo chema kwa wanasoka wa kisasa kama Zamoyoni Mogella, Malota Soma, John Simkoko, Omar Hussein, na kikosi cha dhahabu cha Pan Africans wakiongozwa na kipa Juma Pondamali, Sunday Manara, Mohammed Mkweche, Mohammed Yahya 'Tostao' Mohammed Rishard Adolph, Jafar Abdulrahman, Ally Katolila na wengine.
Mwaka jana kocha huyo aliyekuwa kiungo mahiri na aliyeiwakilisha Tanzania kwenye michezo ya Afrika (All Africa Games) mwaka 1973 ilipofanyikia Nigeria, alienda kuhiji Makka kwa maana hiyo mautio yamekumta akiwa ni ALHAJI.
Innalillah Waina Illaiy Rajiun. Tangulia mzee wetu Mohammed Msomali, nasi tu nyuma yako. Blog hii ya Micharazo Mitupu inatoa pole kwa ndugu, jamaa, familia na rafiki wa marehemu Msomali sambamba na wadau wa soka kwa kuwakumbusha kuwa kila nafsi itaonja mauti.Tumuombee katika safari yake ya Ahera nasi tukijiandaa kwa safari hiyo kwa vile hatujui saa, siku wala mwaka.

Sikia hii kutoka Chadema kuhusu jeshi la Polisi


Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Makao Makuu ya chama hicho Kinondoni Dar es Salaam leo mchana, wakati akitoa madai ya kushikiliwa kwa wafuasi wa chama hicho zaidi ya 70 wasiofahamika na wengine 10 katika vituo mbalimbali vya polisi jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za kujihusisha na masuala ya Umoja wa Kupinga Udikiteta (Ukuta), bila ya kufikishwa mahakamani. Kushoto ni Ofisa Habari wa chama hicho, Tumaini Makene.
Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Makao Makuu ya chama hicho Kinondoni Dar es Salaam leo mchana, wakati akitoa madai ya kushikiliwa kwa wafuasi wa chama hicho zaidi ya 70 wasiofahamika na wengine 10 katika vituo mbalimbali vya polisi jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za kujihusisha na masuala ya Umoja wa Kupinga Udikiteta (Ukuta). Kulia ni Mwenyekiti Baraza la Umoja wa Vijana Chadema (Bavicha), Patrobas Katambi na kushoto ni Ofisa Habari wa chama hicho, Tumaini Makene.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.

Na Dotto Mwaibale
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kinakusudia kufungua maombi katika Mahakama Kuu ya kuiomba mahakama hiyo kuiamuru Polisi kuwafikisha mahakamani watu wanaoshikiliwa katika vituo mbalimbali vya polisi jijini Dar es Salaam.
Hatua hiyo inatokana na chama hicho kudai kuwa kuna watu 10 ambao wanashikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi (Central) na Kituo cha Oysterbay vya Dar es Salaam kwa zaidi ya wiki mbili bila kupewa dhamana ya polisi au kufikishwa mahakamani.
Kauli hiyo ya Chadema imetolewa na Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, Tundu Lissu wakati akizungumza na waandishi wa habari makao makuu yake yaliyo mtaa wa Ufipa, Kinondoni jijini Dar es Salaam leo mchana.
Akifafanua kuhusu Habeas Corpus alisema, ni mamlaka iliyonayo Mahakama Kuu ya kuamuru mamlaka yoyote ya kiserikali inayomshikilia mtu kumpeleka mtu huyo mahakamani.
Lissu alisema, vijana hao walikamatwa katika mikoa mbalimbali kwa makosa aliyodai kuwa ni kujihusisha na haraka za kinachoitwa Umoja wa Kupambana na Udikteta (UKUTA) pamoja na masuala mengine ya kisiasa.
“Kama ikifika Jumanne hawajapelekwa mahakamani au hawajapewa dhamana ya polisi, tutakwenda Mahakama Kuu kufungua maombi ya habeas corpus, imuite IGP au DCI au Ma-RPC au wakuu wa vituo wanakoshikiliwa hao waeleze kwanini wanawashikilia hao watu kwa zaidi ya wiki mbili,” alisema Lissu.
Lissu alisema tayari wameshaanza maandalizi ya hati hizo ambazo zitapelekwa Mahakama Kuu ili iweze kuwaita kati ya Mkuu wa Polisi (IGP), Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Makamanda wa Polisi wa Mikoa au Wakuu wa Vituo vya Polisi wanakoshikiliwa watu hao.
Alifafanua kuwa alionana na watu hao ambao wamedai mbali na kushikiliwa lakini pia wamepigwa na kuteswa huku wakidai kuwa wamekuwa wakichukuliwa usiku na kupelekwa katika eneo lililopo Mikocheni ambako wanateshwa na kurudishwa polisi.
Alisema jeshi la polisi linakiuka sheria na haki za binadamu kwa kuwashikilia watu hao kwa muda mrefu bila kuwapa dhamana au kuwafikisha mahakamani kwa ajili ya kusomewa mashitaka.

Nyie vipi, Ngoma? Mambo yapo kwa Bocco baba'ake

http://www.cecafafootball.org/wp-content/uploads/2014/03/john-bocco.jpg
John Bocco akishangilia moja ya mabao yake
Na Tariq Badru

KUELEKEA raundi ya nne ya Ligi Kuu Bara, nahodha wa Azam, John Bocco 'Adebayor' amewafunika mapro wa kimataifa wa klabu za Simba na Yanga katika mbio za kuwania kiatu cha dhahabu.
Bocco ambaye yupo jijini Mbeya akiwa na kibarua cha kuiongoza tena timu yake kusaka pointi tatu ugenini dhidi ya Wagonga Nyundo wa jiji hilo, mpaka sasa ana mabao matatu akiongoza orodha ya wafungaji.
Straika huyo ngongoti amewaacha mbali kina Amissi Tambwe, Donald Ngoma wa Yanga ambao msimu uliopita walitisha kwa kutupia kambani ambao mpaka sasa hawana bao hata lile la kuotea katika msimu huu wa ligi hiyo.
Mbali na nyota hao wa Yanga, Bocco pia amemzima Laudit Mavugo aliyetabiriwa mapema kusumbua nchini kutokana na rekodi yake ya mabao nchini Burundi ambapo baada ya mechi tatu za ligi hiyo ametupia mabao mawili akiwa na Simba.
Straika mwingine wa kimataifa wa Simba aliyeachwa solemba na Bocco ni Frederick Blagnon mwenye bao moja, huku mapro wengine wa wazawa waliopo klabu tofauti 16 za ligi hiyo wakiwa hawana chao mbele ya Bocco.
Bocco ambaye hana hulka ya kujisifu wala kuzungumza sana kwenye vyombo vya habari amekuwa akisema mwanzo alioanza nao ni kudra za Mungu anayemshukuru na ameapa kupambana akishirikiana na wenzake kurejesha taji la Ligi Kuu Azam.
Azam ndiyo inayoonga msimamo wa ligi kwa sasa ikilingana kila kitu na Mbeya City watakaovaana nao kesho kwenye Uwanja wa Sokoine, zote zikiwa na pointi saba na mabao matano ya kufunga na kufungwa moja, wakifuatiwa na Simba yenye pointi kama hizo na mabao matano ya kufungwa ila imefungwa mabao mawili.
 

Orodha kamili ya wafungaji ipo hivi kwa sasa;
3- John Bocco                            (Azam)
2- Rashid Mandawa        (Mtibwa Sugar)
    Rafael Daud                   (Mbeya City)
    Laudit Mavugo                      (Simba)
1- Federick Blagnon                  (Simba)
    Shiza Kichuya                       (Simba)
    Subianka Lambert                (Prisons)
    Omar Mponda                     (Ndanda)
    Shaaban Kisiga         (Ruvu Shooting)
    Hood Mayanja              (African Lyon)
    Wazir Junior                 (Toto African)
    Mudathir Yahya                      (Azam)
    Abdallah Seseme                ( Mwadui)
    Victor Hangaya                    (Prisons)
    Frank Msese              (Ruvu Shooting)
    Shomari Ally               (Mtibwa Sugar)
    Shija Mkina                         (Ndanda)
    Deus Kaseke                          (Yanga)
    Simon Msuva                         (Yanga)
    Juma Mahadhi                       (Yanga)
    Haruna Shamte              (Mbeya City)               
    Salim Mbonde             (Mtibwa Sugar)
    Bahati Ngonyani                 (Majimaji)
    Ramadhani Chombo        (Mbeya City)
    Omar Ramadhan             (Mbeya City)
    Emmanuel Kichiba                  (Mbao )
    Ally Ramadhani           (Kagera Sugar)
    Adam Kingwande              (Stand Utd)
    Ibrahim Ajib                          (Simba)
    Abdulrahman Mussa   (Ruvu Shooting)
    Kipre Balou                             (Azam)

Wanaume wa Manchester kumalizana mchana kweupe Jumamosi


Pep Guardiola
ACHANA na kelele zote ulizosikia kuelekea kwenye pambano la kukata na shoka baina ya Manchester United dhidi ya wapinzani wao Manchester City. Mwisho wa yote ni kesho Jumamosi wakati miamba hiyo itakapokwaruzana mchana kweupee.
Itakuwa vita ya makocha Jose Mourinho wa Man United dhidi ya Pep Guardiola ambao wote wametua katika timu zao hizo hivi karibuni na tayari wameshauwasha moto wa kutosha katika mechi tatu za Ligi Kuu ya England (EPL).
Macho na masikio ya wapenzi na mashabiki wa soka duniani kote mwishoni yataelekezwa kwenye mchezo huo mkali wa kumaliza ubishi kwa mahasimu hao wa jiji la Manchester.
Mchezo huo utakaokuwa ukipigwa kwenye Uwanja wa Old Trafford, nyumbani kwa Man United una ladha nyingi za kusisimua kuanzia thamani ya pambano lenyewe na hata nyota wanaotarajiwa kuonyeshana kazi majira ya saa 8:30 mchana.
Katika mchezo huo timu hizo  zitaingia uwanjani zikiwa na rekodi nzuri ya kuanza vyema msimu mpya wa ligi wakiwa wameshinda mechi zao tatu za mwanzo. Hata hivyo pamoja matokeo hayo, United wao watakwenda katika mchezo wa kesho wakiwa na rekodi nzuri zaidi dhidi ya City katika mechi 171 walizowahi kukutana huko nyuma, ambapo wameshinda 71 dhidi ya 49 za wapinzani wao. Mchezo wa mwisho United kuitambia City ulikuwa ni ule uliofanyika Machi mwaka huu katika Uwanja wa Etihad ambapo United walishinda bao 1-0. Mchezo huo ambao unatarajiwa kuwa mgumu ni wa kwanza kukutana kwa mameneja wote wawili toka mwaka 2013 katika mchezo wa Super Cup ya Ulaya kati ya Chelsea na Bayern Munich ambapo Guardiola aliibuka kidedea kwa kushinda kwa matuta baada ya timu hizo kutoka sare ya mabao 2-2.
Mameneja hao wana historia ndefu kwani wameshawahi kukutana mara 16 wakiwa na timu tofauti katika kipindi cha miaka saba iliyopita. Kulinganisha na historia ya timu hizo, upande huu ni tofauti kidogo kwani katika mara hizo 16 walizokutana Guardiola ndio ameibuka kidedea kwa kushinda mechi saba, wakitoa sare mechi sita huku Mourinho yeye akishinda mechi tatu pekee.
Wakati Kocha Mourinho akiwa Inter Milan walikutana na Guadiola aliyekuwa Barcelona mara nne, mbili Guardiola akishinda, sare moja huku Mourinho naye akiambulia ushindi mara moja. Wakati Mourinho akiwa Real Madrid walikutana na Guardiola aliyekuwa Barcelona tena mara 11, tano kati ya hizo Guardiola akiibuka kidedea, sare nne na Mourinho akiambulia ushindi mara mbili katika kipindi chote alichokuwa Hispania. Mara ya mwisho mameneja hao kukutana ilikuwa Agosti 30 mwaka 2013, ambapo Guardiola akiwa na Bayern Munich aliibuka kidedea kwa changamoto ya mikwaju ya penati baada ya kutoka sare ya mabao 2-2 dhidi ya Chelsea ya Mourinho.
Klabu zote zitawategemea nyota wao wanaokimbiza kwenye orodha ya ufungaji, Man United ikiwa na Zlatan Ibrahimovic wakati wenzao wakitambia Raheem Starling na Duran Nolito wenye mabao mawili kila moja, kinara, Kun Aguero hatacheza pambano hilo kwa vile kafungiwa na FA kwa utovu wa nidhamu.
Kadhalika Man City itawakosa wakali wake kadhaa kwa sabau nyingine ikiwamo kuwa majeruhi akiwamo nahodha, Vincent Kompany, Bacary Sagna, Leroy Sane, Ilkay Gundogan, huku Man United ikimkosa Henrikh Mkhitaryan  aliye majeruhi na kuna uwezekano mkubwa wa Marcus Rashford kulianza pambano hilo kama Mourinho ataamua kusikiliza maombi ya mashabiki wengi wa klabu hiyo iliyopo nafasi tatu.
Katika mechi zao za mwisho, Manchester United ilipata ushindi mwembamba ugenini dhidi ya Hull City, bao likitupiwa kambani na kinda hilo, wakati wapinzani wao walishinda nyumbani kwa mabao 3-1 dhidi ya West Ham na kukaa kileleni.


Ratiba kamili ya EPL kwa wikiendi hii ipo hivi;

Kesho Jumamosi
14:30 Man United    v Manchester City
17:00 Arsenal          v Southampton
17:00 Bournemouth v West Brom
17:00 Burnley          v Hull
17:00 Middlesbroughv Crystal Palace
17:00 Stoke City      v Tottenham
17:00 West Ham      v Watford
19:30 Liverpool        v Leicester City
 

Jumapili
18:00 Swansea        v Chelsea
 

Jumatatu Septemba 12
22:00 Sunderland    v Everton