STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 22, 2013

Hatimaye ratiba Ligi Kuu yatoka, Simba, Yanga kuanza na wageni zenyewe kuumana Okt. 20

http://blog.pesatimes.com/wp-content/uploads/2013/06/kochaaa.jpg
Yanga itaendelea kubebana kama hivi katika ligi ya msimu huu itakayoanza Agosti 24?
Na Boniface Wambura
LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara msimu wa 2013/2014 inatarajiwa kuanza  kutimua vumbi rasmi Agosti 24 mwaka huu kwa timu zote 14 kuwa viwanjani katika miji saba tofauti, ambapo mabingwa watetezi Yanga wataanza kibarua dhidi ya Ashanti United, jijini Dar..

Hata hivyo, kabla ya ligi hiyo kuanza kutakuwa na mechi ya kufungua msimu (Ngao ya Jamii- Community Shield) kati ya bingwa mtetezi Yanga na Makamu bingwa Azam itakayochezwa Agosti 17 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mbali na pambano la Yanga na Ashanti litakalopigwa kwenye uwanja wa Taifa, siku hiyo ya ufunguzi wa ligi hiyo, Mtibwa Sugar na Azam zitaonyeshana kazi kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro huku JKT Oljoro na Coastal Union zitapepetana mjini Arusha kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Simba wenyewe wataanzia ugenini mjini Tabora kuumana na 'wageni' Rhino Rangers, kwenye uwanja wa Ally Hassani Mwinyi, wakati  Mgambo Shooting itaialika JKT Ruvu katika Uwanja wa Mkwakwani, mjini Tanga huku wageni wengine wa ligi hiyo Mbeya City watakuwa nyumbani mjini Mbeya kuikaribisha Kagera Sugar katika uwanja wa Soikoine na Ruvu Shooting na Tanzania Prisons zitaumana Mabatini, Mlandizi.

Pambano la watani wa jadi nchini lenyewe kwa raundi ya kwanza litachezwa Oktoba 20 ambapo Simba watakuwa wenyeji kabla ya kurudiana mwakani April 27, katika moja ya mechi za kufungia msimu Yanga wakiwa ndiyo wenyeji wa pambano hilo.

Mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo utamalizika Novemba 3 mwaka huu wakati wa pili utamalizika Aprili 27 mwakani. (Ratiba kamili ya ligi hiyo itatupiwa hapa MICHARAZO muda si mrefu)

Taifa Stars kuifuata Uganda The Cranes keshokutwa

Stars na The Craned walipoumana katika mechi ya kwanza jijini Dar es Salaam
Na Boniface Wambura
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inaondoka Mwanza keshokutwa (Julai 24 mwaka huu) kwenda Kampala, Uganda kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la CHAN itakayochezwa Jumamosi (Julai 27 mwaka huu) Uwanja wa Mandela kuanzia saa 10 kamili jioni.

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iko kambini jijini Mwanza chini ya Kocha Kim Poulsen tangu Julai 14 mwaka huu kujiandaa kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya hizo mbili itacheza Fainali za CHAN zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.

Timu hiyo itaondoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza saa 7.25 mchana kwa ndege ya PrecisionAir, na inatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe saa 10.15 jioni.

Wakati huo huo, Kocha Kim Poulsen kesho (Julai 23 mwaka huu) atakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia maandalizi ya kikosi chake. Mkutano huo utafanyika saa 5 kamili asubuhi kwenye hoteli ya La Kairo jijini Mwanza.

Pepe Reina kutimkia Napoli kumfuata kocha Rafa Benitez

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02622/pepe_reina_2622933b.jpg
  GOLIKIPA wa klabu ya Liverpool, Pepe Reina anatarajiwa kujiunga na timu ya Napoli ya Italia kwa mkopo wa muda mrefu.
Kocha wa Napoli Rafael Benitez amekuwa akimkufukuzia Mhispania mwenzake huyo ambaye alikuwa nambari moja kipindi chake Anfield, baada ya kushindwa kumnasa mlinda mlango wa QPR Julio Cesar.
Reina mwenye umri wa miaka 30, alitarajiwa kurejea mazoezini katika klabu yake jana Jumapili kwa kujiunga na wachezaji wenzake huko katika ziara ya maandalizi ya msimu.
Liverpool ilimsainisha mlinda mlango Simon Mignolet raia wa Ubelgiji kutoka katika klabu ya Sunderland kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni £9 mwezi uliopita.
Reina alijunga na Liverpool akitokea Villarreal mwaka 2005.

JK kuongoza watanzania kuwaaga wanajeshi waliouwawa Darfur


 

RAIS wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dk Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwaongoza Watanzania kuiaga miili ya askari saba wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), waliouawa katika jimbo la Darfur nchini Sudan.
 
Shughuli ya kuiaga miili hiyo iliyowasili nchini juzi, itafanyika leo kwenye viwanja vya makao makuu ya jeshi hilo, Upanga jijini Dar es Salaam.

Miili ya wanajeshi hao iliwasili nchini juzi kwa ndege maalumu katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu J. K Nyerere, Terminal One na kwenda kuhifadhiwa kwenye Hospitali ya Rufaa ya Lugalo jijini Dar es Salaam.

Wanajeshi waliouawa ni Sajenti Shaibu Othuman, Koplo Oswald Chaula, Koplo Mohamed Juma, Koplo Mohamed Chikilizo, Rodney Ndunguru, Peter Werema na Fortunatus Msofe.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano, Makao Makuu ya JWTZ, ilieleza kuwa askari hao wataagwa leo na shughuli hiyo itahudhuriwa na familia, makamanda wa jeshi na viongozi wa Serikali.
 

“Shughuli ya kuaga kwa heshima za kijeshi itaanza saa tatu kamili asubuhi katika viwanja vya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Upanga na itaendelea mpaka mchana kabla ya kusafirishwa,” ilisema taarifa hiyo.
 

Wanajeshi hao ambao ni miongoni mwa askari wa kikosi cha Umoja wa Mataifa cha Kulinda Amani katika Jimbo la Darfur nchini Sudan, waliuawa kutokana na mashambulizi ya kushtukiza yaliyofanywa na waasi wanaopigana na Serikali, hivyo kuwa ni mara ya kwanza kwa idadi kubwa ya wanajeshi wa Tanzania wanaolinda amani katika nchi mbalimbali kuuawa kwa wakati mmoja.
 

Mwili wa Mr Bomba kuagwa muda huu Muhimbili rariba kamili hiko hivi

REV. John Makanyagana
Msanii John Makanyaga enzi za uhai wake
MWILI wa muigizaji mkongwe nchini, Mchungaji John Makanyaga unatarajiwa kuagwa asubuhi hii katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kabla ya saa 8 kufanyiwa misa kwenye Kanisa la Anglicana tayari kwa ajili ya kusafirishwa kwenye kuzikwa kwao Mpwapwa.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa hivi punde na Adam Malele' Swebe', mmoja wa waigizaji wenzake wa zamani wa Kaole Sanaa Group, mwili wa msanii hiyo aliyefahamika zaidi kama Mr Bomba utafanyiwa misa ya maombezi kanisa la Ilala Sharifu Shamba
Swebe alisema baada ya ibada hiyo ya mazishi kanisani hapo, mwili huo utasafirishwa kwenda Mpwapwa Dodoma kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika kesho Jumanne.
Marehemu Mr Bomba alifariki juzi hospitali ya Muhimbi kwa tatizo la uvimbe wa kansa katika ini na enzi za uhai wake alitamba na tamthilia mbalimbali kupitia kituo cha ITV kabla ya kuhamia kwenye filamu.
Pia alikuwa ni mwalimu na Mcghungaji wa kanisa la Anglakana mpaka mauti yalipomkumba, ambapo yamekuja huku watanzania wakiendelea kuuguza machungu ya vifo vya wasanii wengine wa uigizaji na muziki vilivyotokea mfululizo tangu mwaka jana.

Mwakyembe, Maugo kupaa kesho kwenda Russia

Mada Maugo

Benson Mwakyembe (kushoto)
MABONDIA watanzania wanaocheza ngumi za kulipwa, Mada Maugo 'King Maugo Jr' na Benson Mwakyembe wanatarajia kuondoka nchini kesho (Jumanne) kuelekea Russia kwa ajili michezo yao ya kimataifa dhidi ya wenyeji wao.
Wanamasumbwi hao wataondoka majira ya saa 10 jioni na watapanda ulingoni Jumamosi ya wiki hii katika mipambano yao ya uzito wa kati wa Kilo 75 (Super Middle).
Rais wa TPBO-Limited, Yasin Abdallah 'Ustaadh', aliiambia MICHARAZO kuwa, Maugo yeye ataenda kupigana na Movsur Yusupov  wakati Mwakyembe ataonyeshana kazi na Apti Ustarkhanov kwenye michezo itakayochezwa kwenye ukumbi wa Trade &Intertainment uliopo mjini Kasiysk, nchini Russia.
Ustaadh alisema mapambano yote hayo yatakuwa na raundi 8 kila mmoja na kwamba Watanzania hao wataungana na wakala wao kutoka Kenya, Thomas Mutua katika mji wa Dubai.
Rais huyo wa TPBO alisema mpinzani wa Maugo rekodi yake inaonyesha amecheza mapambano matatu na yote ameshindwa moja likiwa kwa KO wakati mpinzani wa Mwakyemba amecheza mechi mbili na kushinda moja na kuchapwa moja.
Hata hivyo, alisema pamoja na rekodi hizo zisizovutia kwa wapinzani wao, bado Maugo na Mwakyembe wanapaswa kwenda nchini humo na tahadhari kubwa kwani Warusi huwa hawaruhusu mabondia wa ngumi za kulipwa kucheza mpaka wawe wamepitia ngumi za ridhaa na kushiriki michezo ya Olimpiki.
Akizungumza safari hiyo, Mwakyembe aliiambia MICHARAZO asubuhi hii kwamba licha ya kutomfahamu vyema mpinzani wake, lakini anawaahidi Watanzania kwenda kuwawakilisha vyema katika mchezo huo wa kimataifa ambao ni wa pili kwake nje ya nchi.
"Naahidi sintowaangusha watanzania katika mechi hiyo ya Jumamosi, naenda nikiwa na imani ya kutaka kuweka rekodi kwa kumtwanga mwenyeji wangu na kurejea nchini kwa heshima zote, najiamini kwa mazoezi niliyofanya," alisema.
Kuhusu safari hiyo, Mwakyembe alisema kila kitu kimekaa vyema na kwamba panapo majaliwa ataondoka na mwenzake (Mada Maugo) kesho saa 10 jioni.

Suarez aitamani Arsenal, apanga kuiambia Liverpool

 http://images.dailystar-uk.co.uk/dynamic/58/photos/888000/620x/4888.jpg
MSHAMBULIAJI Luis Suarez anajiandaa kuiambia Liverpool kwamba anataka kuhamia Arsenal.
Gazeti la Sunday Mirror limesema kuwa Liverpool wanamsubiri Suarez aombe rasmi kuondoka ndiyo wamruhusu wakati mshambuliaji huyo wa Uruguay atakapowasili kutoka mapumzikoni mjini Montevideo na kujiunga na kambi ya mazoezi mjini Melbourne.
Arsenal wameongeza matumaini ya kumpata mchezaji huyo na wanatarajiwa kurejea Anfield na ofa nono zaidi baada ya ofa yao ya awali kukataliwa.
Suarez aliweka moyo wake kujiunga na Real Madrid lakini miamba hao wa Hispania hawajajitokeza tena kutaka kumsajili baada ya kuweka wazi kwamba ofa yao ya mwisho wanayoweza kutoa ni paundi milioni 25.
Kocha wa Liverpool, Brendan Rodgers, alisema kuwa thamani ya Suarez ni sawa na ya Muuruguay mwenzake, Edinson Cavani aliyeuzwa kwa paundi milioni 55 kutoka Napoli kwenda PSG. 
Arsenal wameripotiwa kuwa tayari kutoa paundi milioni 40.
Kocha Arsene Wenger anaona Suarez hana shida licha ya kuadhibiwa kwa kumfanyia vitendo vya kibaguzi Patrice Evra na kumng'ata Branislav Ivanovic kwa vile nyota huyo wa Uruguay ni mchapakazi.

Shasta ahairisha kugawa utamu wa penzi

http://thumbp4-ne1.thumb.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=ACbkimIAAAlPUdQbXwAAAJWB87w&midoffset=2_0_0_1_35347&partid=2&f=1215&fid=Inbox&w=480&h=297
Shasta akiwa katika pozi nyumbani kwake

MSANII wa filamu aliyejitosa pia katika muziki, Leah Mussa 'Shasta' amesitisha kwa muda harakati za kusambaza wimbo wake uitwao 'Utamu wa Penzi' ili kupisha mwezi mtukufu wa Ramadhani, imeelezwa.
Akizungumza mwishoni mwa wiki, Shasta alisema kuwa wimbo huo alioimba na H-Mbizo umeshakamilika na kilichobaki ni mambo madogo tu na kwamba, baada ya kumalizika kwa mfungo na sikukuu ya Idd ataendelea na kazi ya kuusambaza.
"Sasa wimbo huu utatoka baada ya Sikukuu ya Idd El Fitri," alisema Shasta ambaye amejitosa katika muziki baada ya kuvutiwa na wimbo 'Majanga' wa shoga yake na msanii mwenzake katika  filamu, Snura Mushi.
Baadhi ya filamu alizoshiriki Shasta ni 'Ong'wana', 'Julia', 'Kisasi za Mzimu', 'Siri za Majini' na 'Deception'.

Golden Bush Fc yazinduka Ligi ya Kinondoni

Vijana wa Golden Bush wakiwa mazoezini na kocha wao Shija Katina (kushoto) wakipeana mikakati ya kusaka ushindi katika Ligi daraja la Nne wanayoicheza kwa mara ya kwanza
BAADA ya wiki iliyopita kutibuiliwa rekodi yake ya ushindi mfululizo kwa kulazwa na Kijitonyama, timu ya Golden Bush Fc jana ilizinduka katika Ligi Daraja la Nne wilayani Kinondoni kwa kufanya 'mauaji' ya kutisha dhidi ya Shein Rangers kwa kuinyuka mabao 4-1.
Pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Mwananyamala, jijini Dar es Salaam lilishuhudia vijana wa Golden Bush inayonolewa na kocha Shija Katina na Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio' wakicharuka tangu mwanzo wa mchezo ili kurejesha heshima yake katiika lig hiyo.
Vijana hao walipata mabao yao yaliyotosha kuwafanya wafikishe pointi 15 katika kundi lake baada ya kucheza mechi 6 yalitumbukizwa kimiani na aliyekuwa nyota wa mchezo, Adilu aliyefunga mawili, Said na Kenan.
Timu hiyo inatarajiwa kushuka tena dimbani siku ya alhamis, ambapo uongozi wa timu hiyo umesema vijana wao watashuka wakiwa na lengo moja tu la kuendeleza vipigo ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu hatua ya pili na hatimaye kuipanda Ligi Daraja la Tatu.

Washindi shindano la kusoma Qur'an wapatikana

Msomaji wa Quran tukufu katika mashindano ya kitaifa, Abdallah Abdulkadri akisoma wakati wa fainali zake jana.

Msomaji wa Quran tukufu katika mashindano ya kitaifa, Seif Salim Said ambaye ni mremavu wa macho akisoma wakati wa fainali zake jana

Baadhi ya viongoza wa Dini wakifatilia mashindano hayo katika ukumbi wa Diamond Jubilee
Baadhi ya wanafunzi walioshiliki katika kusoma

Qur'an tukufu

Msomaji wa Quran tukufu katika mashindano ya kitaifa, Ummy Swaleh Said ambaye ni mlemavu wa macho akisoma wakati wa fainali hizo.

Baadhi ya waumini wa Dini Ya Kislam wakiongozwa na mratibu wa mashindano ya usomaji wa Qur'an Bi. Aisha Sururu wakifuatilia fainali hizo.
Bi Aisha Sururu akifuatilia mashindano hayo yaliyomalizika jana
Zawadi walizopewa washindi

Mgeni Rasmi wa Mashindano ya kuifadhi Quran tukufu kitaifa Dk, Suleiman Ally Yussuf katikati na Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni cha Ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ,Morteza Sabouri wakimkabidhi zawadi wa cherehani mshindi wa kusoma juzuu 20

Mgeni Rasmi wa Mashindano ya kuifadhi Quran tukufu kitaifa Dk Suleiman Ally Yussuf kulia na Mkurugenzi wa Kituo cha Utamaduni cha Ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ,Morteza Sabouri wakimkabidhi zawadi ya bajaj  pamoja na pesa taslmu laki tano mshindi wa kuhifadhi Quran tukufu, Suria Ally Bakari.

Mgeni Rasmi wa Mashindano ya kuifadhi Quran tukufu kitaifa Dk Suleiman Ally Yussuf (kulia) akimkabidhi mshindi Abdul Hamid zawadi yake ya bajaj na pesa taslimu.


Baadhi ya washindi wa kuhifadhi Quran Tukufu wakiomba Dua baada ya kumalizika mashindano hayo

Afande Sele kuweka Dini videoni


Afande Sele akiwajibika jukwaani
MKONGWE wa muziki wa hip hop nchini, Seleman Msindi 'Afande Sele' yupo katika harakati za kufyatua video ya wimbo wake mpya unaoendelea kutamba kwenye vituo vya redio uitwao 'Dini Tumeletewa'.
Afande Sele aliiambia MICHARAZO kuwa ijapokuwa hivi sasa yupo mapumzikoni kuupisha mfungo wa mwezi wa Ramadhani, lakini bado anaendelea na mipango ya kukamilisha video ya wimbo huo ili kukata kiu ya mashabiki wake ambao wengi wamekuwa wakiiulizia mara kwa mara.
"Niko mbioni kutoa video ya wimbo Dini Tumeletewa nilioimba na Belle 9. Ikikamilika itasambazwa ili mashabiki wa muziki washuhudie kile nilichoimba,"alisema Afande.
Katika hatua nyingine, Afande Sele alisema kuwa tangu atoe wimbo huo amekuwa akipokea pongezi nyingi na kuombwa atoe video yake.
Msanii huyo amekuwa akijizolea sifa kemkem kutokana na nyimbo zake nyingi kuwa na mashairi yenye kugusa hali halisi ya maisha ya Mtanzania.

TMK Wanaume Family Sasa Tufurahie


KUNDI la muziki wa kizazi kipya la TMK Wanaume Family 'Mapanga Shaa', linatarajiwa kuuachia hewani wimbo wao mpya uitwao 'Tufurahie'.
Wimbo huo uliokamilika wiki iliyopita ni kati ya kazi mpya za kundi hilo baada ya kutamba na 'Kichwa Kinauma' na 'Tutaonekanaje'.
Akizungumza na MICHARAZO, Meneja wa TMK, Said Fella alisema wimbo huo ulirekodiwa katika studio za Tuddy Thomas wa Ngoma Records na utaachiwa leo Jumatatu.
Fella alisema katika wimbo huo, kazi kubwa imefanywa na YP, Mheshimiwa Temba na Said Chegge, na kwamba wanatumai utafanya vizuri kama ilivyokuwa kwa nyimbo zao nyingine.
"Umeandaliwa vizuri na hivyo tunaamini kwamba nao utatamba," alisema Fella.
Katika hatua nyingine, Fella alisema video ya wimbo wa msanii Is'haka Aslay 'Dogo Aslay' uitwao 'Bado Mdogo' alioimba kwa kushirikiana na Linnah wa THT imekalimika.
Wimbo huo umeelezewa na Dogo Aslay kuwa ni kisa cha kweli, akidai kwamba yupo mama mwenye umri mkubwa aliyekuwa akimghasi kwa kumtaka kimapenzi licha ya yeye kumkatalia kwa kumwambia kuwa yeye (Aslay) bado mdogo na hivyo asingependa kujihusisha na masuala hayo ya mapenzi.

Mbwana Samatta azidi kung'ara Afrika

Mbwana Samatta alipokuwa akiitumikia Stars dhidi ya Morocco

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ameendelea kung’ara katika michuano ya Afrika, baada ya mwishoni mwa wiki kuifungia timu yake ya TP Mazembe ya DR Congo bao lililoipa sare ya 1-1 ugenini dhidi ya ESS ya Algeria.
Katika pambano hilo lililochezwa Ijumaa kwenye uwanja wa Mei 8, 1945 la ufunguzi wa hatua ya Makundi Kombe la Shirikisho Afrika kwa kundi B, wenyeji walilazimika kulichomoa bao hilo la Samatta.
Samatta alifunga bao hilo katika dakika ya 81 , lakini hata hivyo dakika mbili baadaye wenyeji walichomoa kupitia kwa beki wao Mourad Delhoum.
TP ya Samatta sasa itarejea nyumbani kuisubiri FUS Rabat ya Morocco katika pambano lao litakalochezwa mjini Lubumbashi Agosti 4.