STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 22, 2013

Suarez aitamani Arsenal, apanga kuiambia Liverpool

 http://images.dailystar-uk.co.uk/dynamic/58/photos/888000/620x/4888.jpg
MSHAMBULIAJI Luis Suarez anajiandaa kuiambia Liverpool kwamba anataka kuhamia Arsenal.
Gazeti la Sunday Mirror limesema kuwa Liverpool wanamsubiri Suarez aombe rasmi kuondoka ndiyo wamruhusu wakati mshambuliaji huyo wa Uruguay atakapowasili kutoka mapumzikoni mjini Montevideo na kujiunga na kambi ya mazoezi mjini Melbourne.
Arsenal wameongeza matumaini ya kumpata mchezaji huyo na wanatarajiwa kurejea Anfield na ofa nono zaidi baada ya ofa yao ya awali kukataliwa.
Suarez aliweka moyo wake kujiunga na Real Madrid lakini miamba hao wa Hispania hawajajitokeza tena kutaka kumsajili baada ya kuweka wazi kwamba ofa yao ya mwisho wanayoweza kutoa ni paundi milioni 25.
Kocha wa Liverpool, Brendan Rodgers, alisema kuwa thamani ya Suarez ni sawa na ya Muuruguay mwenzake, Edinson Cavani aliyeuzwa kwa paundi milioni 55 kutoka Napoli kwenda PSG. 
Arsenal wameripotiwa kuwa tayari kutoa paundi milioni 40.
Kocha Arsene Wenger anaona Suarez hana shida licha ya kuadhibiwa kwa kumfanyia vitendo vya kibaguzi Patrice Evra na kumng'ata Branislav Ivanovic kwa vile nyota huyo wa Uruguay ni mchapakazi.

No comments:

Post a Comment