STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 22, 2013

Pepe Reina kutimkia Napoli kumfuata kocha Rafa Benitez

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02622/pepe_reina_2622933b.jpg
  GOLIKIPA wa klabu ya Liverpool, Pepe Reina anatarajiwa kujiunga na timu ya Napoli ya Italia kwa mkopo wa muda mrefu.
Kocha wa Napoli Rafael Benitez amekuwa akimkufukuzia Mhispania mwenzake huyo ambaye alikuwa nambari moja kipindi chake Anfield, baada ya kushindwa kumnasa mlinda mlango wa QPR Julio Cesar.
Reina mwenye umri wa miaka 30, alitarajiwa kurejea mazoezini katika klabu yake jana Jumapili kwa kujiunga na wachezaji wenzake huko katika ziara ya maandalizi ya msimu.
Liverpool ilimsainisha mlinda mlango Simon Mignolet raia wa Ubelgiji kutoka katika klabu ya Sunderland kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni £9 mwezi uliopita.
Reina alijunga na Liverpool akitokea Villarreal mwaka 2005.

No comments:

Post a Comment