STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, July 10, 2015

Turan ajifunga miaka mitano Barcelona

http://static.sportskeeda.com/wp-content/uploads/2014/02/arda_turan-2116949.jpgKIUNGO wa kimataifa wa Uturuki, Arda Turan amekamilisha usajili wake katika klabu ya Barcelona baada ya kutia saini katika mkataba wa miaka mitano leo. 
Barcelona walikubali kutoa kitita cha Euro Milioni 41 kwa Atletico Madrid kw ajili ya nyota huyo wiki iliyopita. 
Hata hivyo, Turan amesisitiza hana shaka kuhusu uwezekano wa kurejea Atletico kwa muda mpaka Januari pindi Barcelona watakaporuhusiwa kumtumia. Kwa sasa Barcelona wanatumikia adhabu ya kutosajili kwa msimu miwili baada ya kukutwa na hatia ya kukiuka Sheria za Shirikisho la Soka Duniani-FIFA kwa kusajili wachezaji walio chini ya umri wa miaka 18 kinyume cha sheria, adhabu ambayo inaishia Januari mwakani. Mkali huyo ametua akitegemewa kuziba pengo lililoachwa na Xavi aliyekimbilia Umangani.

Man United yamtengea kitita Thomas Muller

http://leadership.ng/wp-content/uploads/2015/07/thomas-muller.jpgBAADA ya kuelekea kumpoteza mshambuliaji wake matata, Robin van Persie, klabu ya Manchester United imepanga kutoa kitika cha pauni Milioni 60 ili kumnasa mshambuliaji wa Kijerumani Thomas Muller.
Muller mwenye umri wa miaka 25 anaichezea klabu ya Bayern Munich na United itamsajili Mjerumani huyo kama mbadala wa RVP ambaye anatarajiwa kuuzwa klabu ya Fenerbahce ya Uturuki. Klabu hiyo ya Uturuki imekubaliana na Mashetani Wekundu kulipa dau la Pauni Milioni 4.7 kama ada ya uhamisho wa RVP ambaye atafanyiwa vipimo vya afya wikiendi hii na kusaini mkataba wa miaka minne ambao utamuwezesha kulipwa mshahara wa Pauni 200,000 kwa wiki. 
Nyota huyo alijiunga na United akitokea Arsenal kwa kitita cha Pauni Milioni 24 Agosti mwaka 2012 na alianza vyema msimu wake wa kwanza akimaliza kama Mfungaji Bora wa EPL wakati taji likienda Old Trafford. 
Lakini Van Persie sasa amepungua makali kutokana na kuwa chini ya kiwango kutokana na majeruhi yaliyomuandama chini ya kocha Louis van Gaal.

Azam yaenda Tanga kutambulisha nyota wake

https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AL92imIAABY%2FVZ%2BaswTxoL0v9NM&midoffset=2_0_0_1_4179536&partid=11&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000
Wachezaji wakijiandaa na safari kuelekea Tanga
https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AL92imIAABY%2FVZ%2BaswTxoL0v9NM&midoffset=2_0_0_1_4179536&partid=4&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000
Usiniangushe Migi
https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AL92imIAABY%2FVZ%2BaswTxoL0v9NM&midoffset=2_0_0_1_4179536&partid=5&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000
Muingereza mwenyewe huyu hapa
https://thumbp22-ne1.mail.yahoo.com/tn?sid=2126005954&mid=AL92imIAABY%2FVZ%2BaswTxoL0v9NM&midoffset=2_0_0_1_4179536&partid=7&f=1214&fid=Inbox&m=ThumbnailService&w=3000&h=3000
Migi akipasha na wenzake mapema leo

KLABU ya Azam ikiwa na nyota kadhaa wa kimataifa akiwamo Jean Baptiste Mugiraneza 'Migi'na Muingereza Ryan Burge imeondoka jijini kuelekea Tanga tayari kwa mechi mbili za kujipima nguvu kujiandaa na Kombe la Kagame litakaloanza wiki ijayo jijini Dar es Salaam.
Azam iliyofanya mazoezi mapema leo asubuhi itashuka dimba la Mkwakwani, Tanga kesho kuumana na Africans Sports kabla ya Jumapili kupepetana na Wagosi wa Kaya kwa mechi ya pili, kisha kurudi Dar kusubiri mechi zake za kundi C katika michuano hiyo ya Kagame itakayomaliza Agosti 2.
Mabingwa wa zamani wa Tanzania wanaenda kunoa makali kabla ya kuja kufanya kweli Dar katika Kagame ambayo inashirikisha timu 13 na Azam imepangwa kundi moja na KCCA ya Uganda, Al Malakia ya Sudan Kusini na Adama City ya Ethiopia.
Katika mechi hizo za wikiendi, Azam itatambulisha nyota wake wapya akiwamo Migi na Burge ambao wapo hatua ya mwisho kutua kwa Matajiri hao wa Tanzania.

Yohan Cabaye arejea England, aitosa PSG

http://e2.365dm.com/14/02/768x432/Yohan-Cabaye-Paris-St-Germain_3076500.jpg?20140201152736
Yohan Cabaye
KIUNGO fundi wa zamani wa Newcastle United, Yohan Cabaye amerejea Ligi Kuu ya England kutoka Ligue 1 ya Ufaransa.
Kiungo huyo amemwaga wino wa kukipiga klabu ya Crystal Palace akitokea PSG ya Ufaransa na kumfanya aungane tena na kocha wake, Alan Pardew. 
Klabu ya Crystal Palace imethibitisha kumsajili kiungo huyo wa kimataifa wa Ufaransa kwa mkataba wa miaka mitatu. 
Inaaminika kuwa Palace imelipa ada ya Pauni milioni 10 kwa ajili ya kumnasa kiungo huyo aliyefanya kazi na Pardew kwa miaka mitatu wakati kocha na yeye wakiwa katika klabu ya Newcastle United. Kipindi akiichezea timu hiyo, Cabaye alikuwa akihesabiwa kama mmoja wa viungo bora katika Ligi Kuu. Kiwango chake hicho ndio kilichangia kwa kiasi kikubwa kuwafanya PSG kutoa karibu pauni milioni 20 kumsajili mapema mwaka jana.

Jordan Henderson rasmi nahodha wa Liverpool, amrithi Gerrard

http://i1.liverpoolecho.co.uk/incoming/article8381445.ece/ALTERNATES/s1227b/Gerrard-Henderson.jpg
Nakukabidhi mikoba, usiniangushe!
WAKATI ikiendelea kumbembeleza nyota wake Raheem Sterling asalie klabuni, Liverpool, imethibitisha Jordan Henderson kuwa nahodha mpya wa timu hiyo akichukua nafasi ya Steven Gerrard aliyeondoka mwishoni mwa msimu uliopita. 
Henderson ambaye amesaini mkataba mpya Aprili mwaka huu, ndio aliyekuwa akipewa nafasi kubwa ya kupewa beji hiyo baada ya Gerrard kuhamia katika klabu ya Los Angeles Galaxy ya Marekani. 
Akihojiwa Henderson amesema siku zote amekuwa akitaka majukumu zaidi hususani katika kipindi hiki cha soka lake. 
Nyota huyo aliendelea kudai kuwa anajiona amekuwa kwasasa na yuko tayari kwa majukumu hayo kwani amejifunza mengi kutoka Gerrard katika kipindi chote ambacho chini yake.