STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 2, 2014

Kiwewe, Matumaini wapona kwa Injili

WACHEKESHAJI Robert Augustino 'Kiwewe' na Tumain Martin 'Matumaini' wameamua kugeukia muziki wa Injili wakijiandaa kuachia albamu yao iitwayo 'Nimepona'.
Akizungumza na MICHARAZO hili, Kiwewe anayetamba na kipindi cha 'Ze Comedy Show' alisema kuwa albamu hiyo itakuwa na nyimbo sita na imeshakamilika ikisubiri kuachiwa mtaani.
Kiwewe alisema wameamua kumtumikia Mungu kwa kuimba kama njia ya kumshukuru kwa yote aliyowatendea tangu walipoanza kujipatia umaarufu kupitia fani ya uigizaji.
"Tumeamua kumtumia Mungu kwa njia ya huduma ya nyimbo na tunaomba mashabiki wetu watuunge mkono mara albamu hiyo itakapoingia sokoni wakati wowote kuanza sasa," alisema.
Hata hivyo Kiwewe aliweka bayana kwamba pamoja  na kuimba muziki wa Injili, yeye hajaokoka kama 'patna' wake Matumaini ambaye kwa sasa ni Mlokole akisali Mito ya Baraka.
"Sijaokoka kwa sababu siyo kila aimbaye muziki wa Injili ameokoka, ila Matumaini yeye kaokoka," alisema.
Matumaini mwenyewe alisema albam,u hiyo wameirekodia katika studuio za Levon, zilizopo Kibamba jijini Dar na kuzitaja nyimbo zilizopo katika albamu hiyo kuwa ni 'Nimepona', 'Amani ya Bwana', 'Msukule', 'Nitakutangaza Bwana', 'Mungu' na 'Anaweza Yesu' na amepanda kuiachia wiki mbili zijazo.

Mabweni Shule ya Sekondari yateketea kwa moto

MABWENI saba ya wavulana wa Shule ya Sekondari Ivumwe, mkoani hapa, inayomilikiwa na Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), yameteketea kwa moto na kuteketeza vifaa mbalimbali vya wanafunzi wa shule hiyo.

Moto huo ulizuka jana majira kati  ya saa tatu na nne asubuhi wakati wanafunzi hao wakiwa madarasani kuendelea na masomo yao.

Akitoa taarifa mbele ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi taifa, Abdallah Majura Bulembo, aliyefika mkoani hapa kujionea janga hilo, Mkuu wa shule hiyo, Emmery Muhondwa, alisema mbali na kuteketeza mabweni hayo, hakuna madhara ya kibinadamu.

Mwalimu Muhondwa alisema moto huo uliteketeza vitanda 93, magodoro 186, mashuka 372, blanketi 186, mabegi 186, matranker 186 pamoja na vitabu na madaftari, vyote vikiwa na jumla ya  thamani ya sh milioni 30.

“Katika kukabiliana na hali hiyo, tumewahamishia wanafunzi katika madarasa yaliyokuwa yanatumiwa na kidato cha sita ili walale humo, tumeazima magodoro 169 kutoka Shule ya Sekondari ya Loleza na tunawasiliana na wazazi ili wawanunulie nguo za kushindia na za shule huku tukiendelea kukarabati mabweni,’’ alisema Mwalimu Muhondwa.

Mwenyekiti wa jumuiya hiyo taifa, Bulembo, aliwapa pole wanafunzi na kuwataka wawe wavumilivu katika kipindi hiki.

Pia alitoa mchango aliouita wa dharura wa sh milioni tatu  kwa ajili ya ukarabati wa mabweni na mahitaji mengine ya haraka na kuahidi kuwashirikisha wadau wengine wa elimu ili kuwasaidia wanafunzi hao.

Mbali na mchango huo, alitoa tamko kuzitaka shule zote zinazomilikiwa na jumuiya hiyo kuwa na bima ya moto.

“Kuanzia sasa, suala la bima ya moto ni la lazima kwa shule zote za jumuiya ya wazazi wa CCM. Baraza Kuu tutakutana kwa dharura mjini Dodoma Mei 17, mwaka huu na tutakachokipata tutakileta haraka kwenu ili kusaidia janga hili la moto,’’ alisema Bulembo.

Mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo, Dk. Victoria Kanama, alimshukuru mwenyekiti huyo kwa mchango wake.

“Tutahakikisha tunakarabati mabweni haya ndani ya mwezi mmoja na kufanya jitihada za kuongeza ufanisi wa ufaulu katika shule yetu,” alisema Dk. Kanama.

Ivumwe, ni kati ya shule zenye sifa ya kufaulisha ambapo katika mtihani wa utamilifu (Mock), kidato cha sita mwaka huu, shule hiyo imeshika nafasi ya pili kati ya shule 26 zilizokuwa na watahiniwa 30 Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.
Udaku Special

Bomu lingine laua watu 10 Nigeria


mlipuko
USIKU wa kuamkia leo Maafisa nchini Nigeria wametoa taarifa kuhusu mlipuko uliotokea na kuua watu 19 katika kituo cha basi katika mji mkuu wa taifa hilo Abuja.
Kwa mujibu wa mkurugenzi wa idara ya kushughulikia mikasa na hali ya dharura- FEMA- Abbas G Idriss, watu 60 walijeruhiwa vibaya lakini 6 kati yao wametibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani pia magari sita yameharibiwa katika mlipuko huo.
Mlipuko huo umetokea katika eneo la Nyanya ambao uko karibu na kituo cha basi ambako zaidi ya watu sabini waliuwawa katika shambulizi la tarehe14 mwezi Aprili.
nyanya 
Ripoti za awali zimesema kuwa watu kadhaa wameuwawa na wengine wengi kujeruhiwa,Waandishi wanasema kuwa mlipuko huo umesababishwa na bomu lililotegwa ndani ya gari,Mmoja wa walioshuhudia kisa hicho amesema aliona miili 20 ya watu waliouwawa.
Mpaka sasa hakuna kundi lililodai kuhusika katika shambulizi hilo lakini kundi la wanamgambo wa kiislamu la Boko Haram limewahi kutekeleza mashambulizi kama hayo mjini Abuja,Mengi ya mashambulizi ya Boko Haram yamekuwa yakitokea katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Bomu la tarehe 14 Aprili lilizua hofu kwamba huenda wanamgambo hao wameanza kupanua maeneo wanayoendeleza harakati zao.

Yanga yatoa ufafanuzi sakata la usajili wa akina Domayo Azam

Didier-Kavumbagu-na-Frank-Domayo-wakisaini-kuichezea-klabu-ya-Azam-FCUongozi wa klabu ya Young Africans unapenda kuwajulisha wanachama wake, wapenzi wa soka na wadau kwa ujumla kuwa taarifa za kuhama kwa wachezai wake Didier Kavumbagu na Frank Domayo kwenda kujiunga na Azam FC zisiwakatishe tamaa, ni mapenzi ya wachezaj wenyewe kwani walishakubaliana na uongozi kila kitu juu ya kuendelea kuitumikia Yanga kabla ya siku mbili hizi kuonekana wakiwa wamejiunga na wana ramba ramba.
Yanga tayari ina wachezaji watatu wenye mikataba inayoendelea na kama kanuni za VPL kwa wachezai wa kimataifa kuwa watatu zitatumika wachezaji Haruna Niyonzima, Hamisi Kizza na Emmanuel Okwi ndio watakaoendelea, hivyo uongozi uliomba mwongozo kwa TFF juu ya taratibu zitakazotumika kwa msimu ujao kabla ya kuwasainisha Kavumbagu na Twite.
Awali uongozi wa Yanga ulikuwa kwenye mazungumzo na wachezaji hao tangu mwanzoni mwa msimu wa 2013/2014 juu ya kuongezewa muda wa mikataba yao ili waweze kuendelea kuitumika Yanga kwa ajili msimu mpya ujao 2014/2015.
Didier Kavumbagu na Mbuyu Twite ambao mikataba yao ilikuwa mwishoni waliongea na uongozi tangu mapema mwaka jana mwezi wa Septemba juu ya kuweka sahihi zao na kuendelea kuitumikia Yanga na kukubaliana mambo yote ya msingi kikubwa kilichokuwa kinasubiriwa ni maamuzi ya TFF juu ya usajili wa wachezaji wa kigeni msimu mpya wa 2014/2015 kwani Azimio la Bagamoyo linapaswa kuanza kutekelezwa msimu huu
Uongozi wa Yanga uliandikia TFF barua mapema kuomba kupewa mwongozo wa kanuni zitakazotumika kwenye usajli kwa wachezaji wa kimataifa kwa msimu mpya kufuatia Azimio la Bagamoyo kuelekeza msimu huu kila timu inapasa kuwa na wachezaji watatu wa kigeni, mpaka sasa uongozi wa Yanga haujapata majibu juu ya utaratibu utakaotumika kwenye msimu wa Ligi Kuu ijayo.
Hivyo makubaliano ya wachezaji Didier Kavumbagu, Mbuyu Twite na uongozi wa Yanga SC yalikua yakisubira majibu ya TFF juu ya kanuni zipi zitakazotumika kwenye usajili msimu wa 2014/2015 kwa wachezaji wa kigeni na katika hali ya kushangaza Kavumbagu akaonekana tayari ameshasaini kuichezea timu ya Azam FC.
Kuhusu Frank Domayo aliyeripotiwa jana kujiunga na Azam FC pia alikuwa katika makubaliano ya kuongeza mkataa tangu mwezi Julai 2013, alikubaliana na uongozi juu ya mambo yote ya msingi na kilichobakia ilikuwa ni kuweka sahihi kwenye mkataba mpya, lakini Domayo alisema hawezi kusaini mpaka siku atakapokuja mjomba wake ambaye ndie wakala wake na ahadi hiyo iliendelea kwa muda wa mwaka mzima kabla ya jana kusikia ameshasaini timu nyngine.
Habari hizi zimewashitua wapenzi, wanachama na washabiki wa Young Africans lakini ukweli ni kuwa wachezaji wenyewe walishindwa kuwa wakweli kwa viongozi na mwisho wa siku walikua na mipango yao ya kuondoka, hivyo uongozi ulijtahid kadri ya uwezo wake lakini wachezaji wanaonekana hawakua tayari kuendelea kuichezea Yanga SC.
Taarifa kamili kuhusu mipango ya timu kwa msimu ujao pamoja na ripoti ya kocha mkuu Hans pamoja na benchi lake la Ufundi zitatolewa hivi karibuni baada ya benchi la ufundi na uongozi kukaa kwa pamoja na kuafikiana mipango ya msimu ujao.
Aidha uongozi wa Yanga SC unawaomba wanachama wake, wapenzi na washabiki wasiwe na wasi wasi juu ya kuondoka kwa wachezaji hao kwani Yanga bado ina nafasi wachezaji wengi wenye vipaji na itaendelea kuboresha kikosi chake kwa kuzingatia maelekezo ya kocha mkuu Hans katika usajli wa msimu ujao

Bonite Bottlers wagawa runinga kwa wateja wao

KAMPUNI ya vinywaji baridi ya Bonite Bottlers Ltd jana ilikabidhi zawadi za luninga mpya za kisasa aina ya Sony LED zenye upana wa inchi 32 kwa washindi 29 wa shindano la Jionee Mwenyewe Kombe la FIFA la Dunia.
Katika promosheni hiyo iliyozinduliwa mapema mwezi uliopita, Coca-Cola itapeleka Watanzania 14 kwenda kushuhudia mechi ya robo fainali ya Kombe la FIFA la Dunia nchini Brazil mwezi Julai. Vile vile Coca-Cola itatoa mipira 8,000 yenye nembo ya FIFA World Cup na fulana 30,000.
Waliobahatika kushinda luninga na kukabidhiwa zawadi zao jana ni Paulina Mushi, Gabriel Warance (mwanafunzi), Moun Johnson (IT Technician), Rispa Waziri, Sophia Paulo, Abela Solomon, Chediel G. Mziray, Asha Ramadhan, Godfrey Mollel na Jackson Shayo (wafanyabiashara) na Simon Mrema (mchimba madini).
Washindi wengine ni Faidha Elidaima, Costantine Urio, Magreth Mshana, Enna Mbwambo, Emmanuel Tarimo, Julius Kimaro, Amir Ali, Emmanuel Mwasha, Gerald Swai, Joseph Mushi na Martine Temu wakazi wa mji wa Moshi.
Akizungumzia ushindi wake Gabriel Warance ambaye ni mwanafunzi jijini Arusha alishukuru Mungu kwa kumuwezesha kushinda luninga. Vile vile aliishukuru kampuni ya Bonite kwa kuleta promosheni hiyo ambayo imewawezesha wale watakaobahatika kushinda kubadili maisha yao kwa namna fulani.
Washindi wengine pia hawakusita kuonyesha furaha yao na kusema kwamba wataendelea kushiriki kwa lengo la kuendelea kushinda zawadi zaidi. “Hii ni nyota njema kwangu na naamini Mungu aliyeniwezesha kushinda zawadi hii ana uwezo wa kunipa tiketi ya kwenda Brazil kushuhudia 'laivu' fainali za Kombe la FIFA la Dunia,” alisema Godfrey Mollel ambaye ni mfanyabihashara.
Akizungumza baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi, Meneja Mkuu wa Mauzo wa Bonite Bottlers, Christopher Loiruk aliwashukuru wateja wa Coca-Cola na wananchi kwa ujumla kwa kuendelea kuburudika na vinywaji vya Coca-Cola.
“Kombe la FIFA la Dunia ndiyo mchezo wenye mashabiki wengi zaidi duniani. Kwa kushirikisha wateja wetu katika promosheni hii, Coca-Cola itawawezesha mashabiki wa soka nchini Tanzania kuungana na wengine duniani kote kusherehekea kwa pamoja burudani ya Kombe la Dunia 2014,” anasema Loiruk
Washindi wamepatikana kwa kunywa vinywaji vya Coca-Cola na kupata vizibo viwili vyenye kutengeneza neno Brazil pamoja na kizibo cha ushindi. Kizibo cha ushindi kina picha ya kitu ambacho mteja ameshinda (TV, mpira au fulana) wakati kizibo cha ushindi wa zawadi ya tiketi kina nembo ya ndege kikiashiria safari ya kwenda Brazili kushuhudia moja kwa moja mechi ya Kombe la Dunia.

Sevilla, Benfica zafuzu fainali za UEFA Ueropa League

Stephen M'Bia akiifungia Sevilla bao muhimu lililowapeleka fainali za Europa League
Wachezaji wa Benfica wakifurahia kufuzu fainali za Europa kwa mara ya pili mfululizo
KLABU za Benfica ya Ureno na Sevilla zimefanikiwa kufuzu fainali za Ligi Ndogo ya Ulaya (UEFA Ueropa League) baada ya kupata matokeo ya kusisimua ugenini dhidi ya Juventus na Valencia.
Benfica imepenya hatua hiyo kwa mara ya pili mfululizo baada ya kuidindia Juventus mjini Turin na kutoka suluhu ya kutofungana na kufuzu kwa jumla ya mabao 2-1 yaliyopatikana kwenye mechi yao ya kwanza wiki iliyopita nchini Ureno.
Wareno hao ambao waliokuwa pungufu wachezaji wawili baada ya Enzo Perez  kupewa kadi ya pili ya njano na kufuatiwa na nyekundu dakika ya 67 na baadaye na Markovic kupewa nyekundu ya moja kwa moja dakika ya 89 sambamba na Vucinic wa Juventsu, hawajawahi kunyakua taji hilo licha ya kucheza fainali mbili za michuano hiyo sasa itavaana na Sevilla ya Hispania ambayo iliwaduwaza wenyeji wao Valencia kwa kufunga bao dakika za jioni wakati wenyeji wakionekana wameshatinga fainali za michuano hiyo.
Stephen M'Bia alifunga kwa kichwa bao muhimu kwa timu yake dakika chache kabla ya pambano hilo kumalizika na kuivusha Sevilla katika fainali hizo zitakazofanyika Mei 14 mjini Turin, Italia ambazo zitakuwa za tatu kwa timu hiyo baada ya kufanya hivyo mara mbili 2006 ilipotwaa ubingwa na na 2007.
Kabla ya hapo matumaini ya Sevilla yaliyeyuka baada ya wenyeji kuongoza kwa mabao matatu mpaka zikiwa zimesalia dakika 20 za mwisho.
Mabao ya Sofiane Feghouli katika dakika ya 14 na jingine la kujifunga kwa kipa wa Sevilla Beto katika dakika ya 26na lililowanyong'onyesha wageni katika dakika ya 70 kupitia kwa Jemery Flamin, liliwapa matumaini wageni kutinfa fainali hizo kabla ya M'bia kuwakata maini kwa bao hilo la jioni.
Matokeo ya mwisho yalikuwa 3-3, lakini Sevilla imefuzu kutokana na kupata ushindi wa mabao 2-0 nyumbani na hivyo bao la ugenini ilililopata limekuwa na faida kwao na sasa itavaana na Benfica.