STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, May 2, 2014

Sevilla, Benfica zafuzu fainali za UEFA Ueropa League

Stephen M'Bia akiifungia Sevilla bao muhimu lililowapeleka fainali za Europa League
Wachezaji wa Benfica wakifurahia kufuzu fainali za Europa kwa mara ya pili mfululizo
KLABU za Benfica ya Ureno na Sevilla zimefanikiwa kufuzu fainali za Ligi Ndogo ya Ulaya (UEFA Ueropa League) baada ya kupata matokeo ya kusisimua ugenini dhidi ya Juventus na Valencia.
Benfica imepenya hatua hiyo kwa mara ya pili mfululizo baada ya kuidindia Juventus mjini Turin na kutoka suluhu ya kutofungana na kufuzu kwa jumla ya mabao 2-1 yaliyopatikana kwenye mechi yao ya kwanza wiki iliyopita nchini Ureno.
Wareno hao ambao waliokuwa pungufu wachezaji wawili baada ya Enzo Perez  kupewa kadi ya pili ya njano na kufuatiwa na nyekundu dakika ya 67 na baadaye na Markovic kupewa nyekundu ya moja kwa moja dakika ya 89 sambamba na Vucinic wa Juventsu, hawajawahi kunyakua taji hilo licha ya kucheza fainali mbili za michuano hiyo sasa itavaana na Sevilla ya Hispania ambayo iliwaduwaza wenyeji wao Valencia kwa kufunga bao dakika za jioni wakati wenyeji wakionekana wameshatinga fainali za michuano hiyo.
Stephen M'Bia alifunga kwa kichwa bao muhimu kwa timu yake dakika chache kabla ya pambano hilo kumalizika na kuivusha Sevilla katika fainali hizo zitakazofanyika Mei 14 mjini Turin, Italia ambazo zitakuwa za tatu kwa timu hiyo baada ya kufanya hivyo mara mbili 2006 ilipotwaa ubingwa na na 2007.
Kabla ya hapo matumaini ya Sevilla yaliyeyuka baada ya wenyeji kuongoza kwa mabao matatu mpaka zikiwa zimesalia dakika 20 za mwisho.
Mabao ya Sofiane Feghouli katika dakika ya 14 na jingine la kujifunga kwa kipa wa Sevilla Beto katika dakika ya 26na lililowanyong'onyesha wageni katika dakika ya 70 kupitia kwa Jemery Flamin, liliwapa matumaini wageni kutinfa fainali hizo kabla ya M'bia kuwakata maini kwa bao hilo la jioni.
Matokeo ya mwisho yalikuwa 3-3, lakini Sevilla imefuzu kutokana na kupata ushindi wa mabao 2-0 nyumbani na hivyo bao la ugenini ilililopata limekuwa na faida kwao na sasa itavaana na Benfica.

No comments:

Post a Comment