STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 14, 2013

Hizi ndizo mechi za VPL zinazosubiriwa kwa hamu Jumamosi

Kikosi cha Polisi Moro kinachopigana kuepuka kuteremka daraja

African Lyon iliyokwishashuka daraja
http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2012/09/139.jpg
Kikosi cha Toto kilichovitani kuepuka kurudi 'mchangani'

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg97pj1ETW12r5ZB7z-OJ8AeGiP4rO7Ut270XLnChEjDivad0H0-rV1Af9HcJz2WAxYgIMJYzS-Rrrz-g_yDLcMerfoasb2tpWACsUj5YPZh7JzPT5nII4g5oYoBrntJnlrtmNWSdfen7Rz/s1600/Mgambo+JKT.jpg
Mgambo JKT nayo ipo kwenye mtego wa kurudi FDL

PAZIA la Ligi Kuu Tanzania bara linatarajiwa kufungwa rasmi siku ya Jumamosi kwa michezo saba tofauti, lakini ni mechi tatu tu kati ya hizo ndizo zitakazokuwa na mvuto na kufuatiliwa kwa karibu na mashabiki wa soka pengine kuliko hata pambano la watani wa jadi nchini, Simba na Yanga litakalochezwa Dar es Salaam.
Mechi hizo zitakazofuatiliwa kuliko la Simba na Yanga ambazo ni za kulinda heshima tu, ni ile ya jijini Mwanza kati ya wenyeji Toto Africans dhidi ya maafande wa Ruvu Shooting, itakayochezwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba.
Hii ni kwa sababu Toto ipo katika janga la kushuka daraja na hivyo inahitaji ushindi huku ikiziombea Polisi Moro na Mgambo JKT ziteleze ili wenyewe waponee chupuchupu kama ilivyokuwa msimu uliopita.
Timu hiyo ina pointi 22 sawa na Polisi Moro na zinatofautiana idadi ya magoli ya kufunga na kufungwa na iwapo itashinda itafikisha pointi 25 ambazo tatari zimeshafikiwa na Mgambo JKT iyakayokushuka dimbani nyumbani jijini Tanga kuumana na Africans Lyon iliyokwisha kushuka daraja.
Polisi Moro ambayo ilizinduka kwenye duru la pili ilipochukuliwa na kocha Mohammed Rishard 'Adolph' kabla ya kuzorota tena yenyewe itakuwa nyumbani kuumana na Coastal Union.
Kwa kulinganisha mechi hizo tatu za wawania kuepuka kushuka daraja unaweza kuona angalau Mgambo ipo katika nafasi nzuri ya kuokoka kuliko Toto na Polisi, hii ni kwa sababu inamaliza mechi za msimu na Lyon iliyoshuka daraja kitambo, huku ikisaka pointi moja tu kuwaokoa, ingawa kwa mechi mbili mfululizo timu hiyo iliyopanda daraja msimu huu imeshindwa kuipata mbele ya Simba na Azam.
Pazia la ligi hiyo mbali na mechi hizo na ile ya watani wa jadi, pia litafungwa na mechi nyingine tatu ambapo JKT Ruvu dhidi ya Mtibwa Sugar, Prisons na Kagera Sugar na lile la washindi wa pili na wawakilishi wa Kombe la Shirikisho kwa mara ya pili mwakani, Azam itakayokuwa ugenini mjini Arusha kuchuana na wenyeji wao JKT Oljoro.


                            P     W     D     L     F     A     D     Pts
Young Africans     25    17     6     2     45   14    31     57
Azam                    25   15     6     4     45    20   25     51   
Simba                   25    12    9     4     39     24  15     45
Kagera Sugar        25    11    8     6     27     20   7      41    
Mtibwa Sugar       25    10     9     6     29     24   5     39  
Coastal Union       25     8     11     6     25     22   3     35   
Ruvu Shooting       25     8     7     10     23     26  -3     31    
JKT Oljoro FC     25     7     8     10     22     28  -6     29    
Tanzania Prisons    25     7     8     10     16     22  -6     29   
Ruvu Stars            25     7     5     13     21     39   -18   26
JKT Mgambo       25     7     4     14     16     27   -11   25
Toto Africans        25     4     10    11     22     33  -11    22
Polisi Morogoro    25     4     10    11     13     23  -10    22   
African Lyon         25     5     4     16     16     38    -22   19
              

Mechi za kufungia pazia msimu wa 2012-2013

Mgambo JKT Vs African Lyon
JKT Ruvu Vs Mtibwa Sugar
TZ Prisons Vs Kagera Sugar
Simba SC Vs Yanga SC
JKT Oljoro Vs Azam FC
Toto African Vs Ruvu Shooting
Polisi Moro Vs Coastal Union