STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 14, 2013

Martin Saanya kuzihukumu Simba, Yanga viingilio vyatajwa


Vijana wa Yanga watacheka kama hivi Jumamosi?
Mwamuzi Martin Saanya atakayezihukumu Simba na Yanga

Vijana wa Simba nao watakenua kama hivi J'mosi Taifa?
Na Boniface Wambura
MWAMUZI Martin Saanya wa Morogoro ndiye aliyepewa jukumu la kuzihuku Simba na Yanga zitakazoumana siku ya Jumamosi kwenye pambano la kufungia msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara wa 2012-2013 litakalofanyika kwenye katika uwanja wa Taifa Dar es salaam.

Mwamuzi huyo atasaidiwa na Samuel Mpenzu wa Arusha, na Jesse Erasmo kutoka Morogoro, huku . Mwamuzi wa akiba ni Hashim Abdallah wa Dar es Salaam.

Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Emmanuel Kavenga kutoka Mbeya wakati mtathmini wa waamuzi (referees assessor) ni Leslie Liunda.

Aidha Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeanika viingilio vya pambano hilo la Jumamosi ambapo kiingilio cha chini kwenye mechi ya VPL kitakuwa sh. 5,000. Kiingilio hicho kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648.

Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu kiingilio ni sh. 7,000, viti vya rangi ya chungwa itakuwa sh. 10,000, VIP C kiingilio ni sh. 15,000, VIP B itakuwa sh. 20,000 wakati VIP A yenye viti 748 tu tiketi moja itapatikana kwa sh. 30,000.

Tiketi zitaanza kuuzwa siku moja kabla ya mchezo huo utakaoanza saa 10 kamili jioni.

No comments:

Post a Comment